-
Je, Dunia Yetu Itaharibiwa?Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
Pia, wanasayansi fulani wanaonya kwamba huenda dunia na uhai wote ulio duniani ukaharibiwa na vitu kama vile kimondo, nyota zinazolipuka, au kupungua kwa nguvu za jua.
Wanasayansi wanaamini kwamba hatua kwa hatua—labda kwa mabilioni ya miaka—dunia itapoteza uwezo wake wa kutegemeza uhai wa wanadamu. Kitabu kimoja (Encyclopædia Britannica) kinaeleza jambo hilo kuwa “mwelekeo usioweza kubadilishwa wa kuharibika.”
-
-
Je, Dunia Yetu Itaharibiwa?Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
Mapema kabla wanasayansi hawajagundua kwamba vitu vyote vya asili vina “mwelekeo usioweza kubadilishwa wa kuharibika,” mtunga-zaburi wa Biblia aliandika hivi: “Wewe [yaani, Mungu] uliiweka misingi ya dunia zamani za kale, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako. Hizo zitaangamia, lakini wewe mwenyewe utaendelea kusimama; nazo zote zitachakaa kama vazi. Utazibadili kama mavazi, nazo zitamaliza zamu yake. Lakini wewe ni yuleyule, nayo miaka yako mwenyewe haitamalizika.”—Zaburi 102:25-27.
Alipoandika maneno hayo, mtunga-zaburi hakuwa akipinga kusudi la Mungu la milele kwa dunia. Badala yake, alikuwa akitofautisha kuwepo kwa Mungu kwa milele na mwelekeo wa kuharibika wa vitu ambavyo Mungu ameumba. Pasipo nguvu za Mungu za milele za kufanyiza vitu upya, ulimwengu—kutia ndani mfumo wa jua ambao tunautegemea kwa ajili ya nuru, nishati, na kuimarisha dunia—utaharibika hatua kwa hatua na hatimaye kuangamia kabisa. Hivyo, ikiachiliwa, dunia yetu ‘itachakaa,’ au itaangamia milele.
-