-
Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
-
-
Ili kujibu swali hilo, acheni tuchunguze mkutano ambao Yesu aliongoza muda mfupi baada ya kufufuliwa.
14. (a) Ni mambo gani yaliyotukia kabla ya mkutano ambao ulipangwa na Yesu? (b) Kwa nini ni wazi kwamba mitume walifarijiwa ‘Yesu alipokaribia na kusema nao’?
14 Kwanza, angalia mambo ambayo yalitukia kabla ya mkutano huo. Kabla tu ya Yesu kuuawa, mitume ‘walimwacha na kukimbia,’ na kama ilivyotabiriwa, ‘walitawanyika na kwenda kila mmoja kwenye nyumba yake.’ (Marko 14:50; Yoh. 16:32) Kisha, baada ya Yesu kufufuliwa, aliwaalika mitume wake walioshuka moyo wahudhurie mkutano wa pekee.d Basi, “wale wanafunzi kumi na mmoja wakaingia Galilaya mpaka kwenye mlima ambako Yesu alikuwa amewafanyia mpango.” Walipofika, ‘Yesu alikaribia na kusema nao.’ (Mt. 28:10, 16, 18) Wazia jinsi mitume walivyofarijiwa wakati Yesu alipochukua hatua hiyo! Yesu alizungumzia mambo gani?
15. (a) Yesu alizungumzia mambo gani, lakini hakuzungumza kuhusu nini? (b) Mkutano huo ulikuwa na matokeo gani kwa mitume?
15 Yesu alianza kwa kutangaza hivi: “Nimepewa mamlaka yote.” Kisha, akawapa mgawo: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi.” Mwishowe, akawahakikishia hivi kwa upendo: “Mimi nipo pamoja nanyi siku zote.” (Mt. 28:18-20) Lakini je, uliona jambo ambalo Yesu hakufanya? Hakuwakemea mitume wake; wala hakutumia mkutano huo kutilia shaka nia yao au kuwafanya wahisi kwamba wana hatia zaidi kwa kutaja udhaifu wa imani ambao walionyesha kwa muda mfupi. Badala yake, Yesu aliwahakikishia tena upendo wake na wa Baba yake kwa kuwapa mgawo mzito. Njia ambayo Yesu alitumia ilikuwa na matokeo gani kwa mitume? Walijengwa, walitiwa moyo, na kufarijiwa sana hivi kwamba muda mfupi baada ya mkutano huo, walianza tena “kufundisha na kutangaza habari njema.”—Mdo. 5:42.
-
-
Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
-
-
d Huenda hiyo ndiyo pindi ambayo Paulo alitaja baadaye aliposema kwamba Yesu “aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano.”—1 Kor. 15:6.
-