-
Dhabihu Zilizompendeza MunguMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 15
-
-
11. Kuhani wa cheo cha juu wa Israeli alitoa aina gani mbili za matoleo, na kwa makusudi gani?
11 “Kila kuhani wa cheo cha juu huwekwa rasmi ili kutoa zawadi na dhabihu pia,” asema mtume Paulo. (Waebrania 8:3) Ona kwamba Paulo anatenganisha matoleo ya kuhani wa cheo cha juu wa Israeli la kale katika sehemu mbili, yaani, “zawadi” na “dhabihu” au “dhabihu kwa ajili ya dhambi.” (Waebrania 5:1) Kwa ujumla, watu hutoa zawadi ili kuonyesha upendo na shukrani, na vilevile kusitawisha urafiki, au kupata kibali. (Mwanzo 32:20; Mithali 18:16) Vivyo hivyo, matoleo mengi ambayo Sheria iliagiza yatolewe yanaweza kuonwa kuwa “zawadi” inayotolewa kwa Mungu ili kupata kibali chake.b
-
-
Dhabihu Zilizompendeza MunguMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 15
-
-
13. Fafanua matoleo yaliyotolewa kwa hiari yakiwa zawadi kwa Mungu.
13 Matoleo ya kuchomwa, matoleo ya nafaka, na matoleo ya ushirika ni kati ya matoleo yaliyotolewa kwa hiari yakiwa zawadi au njia ya kumkaribia Mungu ili kupata kibali chake. Wasomi fulani wanaonelea kwamba neno la Kiebrania linalotafsiriwa “toleo la kuchomwa” lamaanisha “toleo la kupaa” au “toleo lenye kupaa.” Hiyo ni tafsiri ifaayo kwa sababu toleo la kuchomwa lilipotolewa, mnyama aliyechinjwa alichomwa kwenye madhabahu na harufu tamu, au ya kuburudisha, ikapaa kuelekea mbinguni kwa Mungu. Jambo lililofanya toleo la kuchomwa liwe tofauti ni kwamba baada ya damu yake kunyunyizwa kuzunguka madhabahu, sehemu zote za mnyama huyu zilitolewa kwa Mungu. Makuhani ‘waliziteketeza zote juu ya madhabahu, ili ziwe sadaka ya kuteketezwa [“toleo la kuchomwa,” NW], dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza [“kuburudisha,” NW] kwa BWANA.’—Mambo ya Walawi 1:3, 4, 9; Mwanzo 8:21.
14. Toleo la nafaka lilitolewaje?
14 Toleo la nafaka linafafanuliwa kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 2. Lilikuwa toleo la hiari la unga mwembamba, ambao kwa kawaida ulitiwa mafuta yenye ubani. “[Kuhani] atatwaa konzi moja katika huo unga mwembamba, na katika mafuta yake, na huo ubani wote; kisha kuhani atauteketeza kuwa ndio ukumbusho wake juu ya madhabahu, ni kafara ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza [“kuburudisha,” NW] kwa BWANA.” (Mambo ya Walawi 2:2) Ubani ulikuwa sehemu mojawapo ya uvumba mtakatifu uliochomwa kwenye madhabahu ya uvumba katika tabenakulo na hekalu. (Kutoka 30:34-36) Mfalme Daudi alifikiria hilo aliposema: “Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.”—Zaburi 141:2.
15. Dhabihu ya ushirika ilitolewa kwa kusudi gani?
15 Toleo jingine la hiari lilikuwa dhabihu ya ushirika, ambayo yafafanuliwa katika kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 3. Dhabihu ya ushirika yaweza pia kutafsiriwa kuwa “dhabihu ya matoleo ya amani.” Katika Kiebrania, neno “amani” lamaanisha mengi zaidi ya kutokuwa na vita au machafuko. “Katika Biblia, lamaanisha hivyo, na pia lamaanisha hali au uhusiano wenye amani pamoja na Mungu, ufanisi, shangwe, na furaha,” chasema kitabu Studies in the Mosaic Institutions. Hivyo, dhabihu za ushirika zilitolewa si kwa ajili ya kupata amani pamoja na Mungu, kana kwamba kumtuliza, bali ili kushukuru au kusherehekea kwa sababu ya hali nzuri ya amani pamoja na Mungu ambayo hufurahiwa na wale wanaokubaliwa naye. Makuhani na mtoaji walikula dhabihu baada ya kumtolea Yehova damu na mafuta. (Mambo ya Walawi 3:17; 7:16-21; 19:5-8) Katika njia ya mfano na yenye kupendeza, mtoaji, makuhani, na Yehova Mungu walikuwa kana kwamba wanakula pamoja, hilo likionyesha uhusiano wenye amani uliokuwepo miongoni mwao.
-
-
Dhabihu Zilizompendeza MunguMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 15
-
-
b Neno la Kiebrania ambalo mara nyingi hutafsiriwa “toleo” ni qor·banʹ. Alipokuwa akiandika juu ya shutumu la Yesu dhidi ya mazoea fulani mabaya ya waandishi na Mafarisayo, Marko alieleza kwamba “korbani” lamaanisha “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu.”—Marko 7:11.
-