-
Je, Dunia Inakabili Hatari?Amkeni!—2008 | Agosti
-
-
Kulingana na yale tunayojua, je, tunaweza kuwatarajia wanadamu kwa ujumla wabadili mtindo wao wa maisha ili wahifadhi makao yetu yanayopendeza na kutuhifadhi pia? Isitoshe ikiwa shughuli za binadamu zinaongeza kiwango cha joto duniani, huenda tuna miaka tu wala si karne nyingi za kufanya mabadiliko. Kufanya mabadiliko hayo kunamaanisha kushughulikia haraka vyanzo vya matatizo ya dunia, yaani, pupa ya mwanadamu, ubinafsi, kukosa ujuzi, serikali zisizo na uwezo, na kutojali. Je, hilo ni jambo linalowezekana au ni ndoto tu? Ikiwa ni ndoto, je, tuna tumaini lolote? Swali hilo litazungumziwa katika makala inayofuata.
-
-
Je, Dunia Inakabili Hatari?Amkeni!—2008 | Agosti
-
-
Gazeti International Herald Tribune linasema kwamba huko Ufaransa, ambayo ni mojawapo ya nchi zinazotegemea zaidi nishati ya nyuklia, kila mwaka inahitaji lita bilioni 18,900 za maji ili kupoesha mitambo ya nyuklia. Kulipokuwa na joto kali sana mnamo 2003, maji moto ambayo hutolewa kwa ukawaida katika mitambo hiyo ya nyuklia ilitishia kuongeza kiwango cha joto katika mito hivi kwamba viumbe wote wangehatarishwa. Hivyo, mitambo fulani iliacha kutumiwa. Inatazamiwa kwamba hali hiyo itakuwa mbaya zaidi ikiwa viwango vya joto duniani vitaongezeka.
“Ni lazima tusuluhishe tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa ili tutumie nishati ya nyuklia,” mtaalamu wa mambo ya nyuklia David Lochbaum ambaye ni mwanachama wa Muungano wa Wanasayansi Wanaojali.
-
-
Wakati Ujao wa Dunia Umo Mikononi mwa Nani?Amkeni!—2008 | Agosti
-
-
Wakati Ujao wa Dunia Umo Mikononi mwa Nani?
“KUONGEZEKA kwa joto duniani kumetokeza mtihani mkubwa zaidi ambao wanadamu wamewahi kukabili,” likasema toleo la Oktoba 2007 la National Geographic. Gazeti hilo lilisema kwamba ili tutatue tatizo hilo kwa mafanikio, tunahitaji “kutenda haraka, kwa njia inayofaa, na kwa ukomavu ambao kwa kawaida sisi wanadamu hatuonyeshi.”
Je, wanadamu watatatua tatizo hilo kwa ukomavu? Kuna vipingamizi vingi: kutojali, pupa, ukosefu wa ujuzi, mapendezi ya vikundi mbalimbali, jitihada za kupata utajiri katika nchi zinazositawi, na mtazamo wa mamilioni wanaotaka kuishi maisha ya kawaida na hivyo kutumia nishati nyingi sana.
Nabii wa kale wa Mungu anachanganua uwezo wetu wa kutatua matatizo ya kimaadili, kijamii, na kiserikali. Aliandika hivi: “Njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Historia yenye kusikitisha ya mwanadamu inathibitisha ukweli wa maneno hayo. Ingawa leo kuna maendeleo mengi ya sayansi na tekinolojia, tunakabili hatari ambazo hazikuwaziwa hapo awali. Basi tunawezaje kuwa na hakika kwamba hali zitakuwa nzuri wakati ujao?
Ni kweli kwamba mengi yamesemwa kuhusu kutatua tatizo la kubadilika kwa hali ya hewa na mambo mengine yenye kudhuru, lakini ni machache ambayo yamefanywa. Kwa mfano, mataifa yalitendaje mnamo 2007 Njia ya Kaskazini-Magharibi ilipofunguka na kutumiwa kwa mara ya kwanza? Makala katika gazeti New Scientist inajibu: “Waling’ang’ania bila aibu kujipatia maeneo ambayo wangeweza kuchimba mafuta na gesi zaidi.”
-