Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Eunike na Loisi—Waelimishaji Walio Vielelezo Bora
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Mei 15
    • Hata hivyo, Eunike hakuwa peke yake katika itikadi zake. Yaonekana kwamba Timotheo alipokea maagizo katika “maandishi matakatifu” kutoka kwa mama yake na kutoka kwa nyanya yake wa upande wa mama, Loisi.a Mtume Paulo alimhimiza sana Timotheo hivi: “Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishwa kuamini, ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza hayo na kwamba tangu utoto sana umeyajua maandishi matakatifu, yawezayo kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.”—2 Timotheo 3:14, 15.

  • Eunike na Loisi—Waelimishaji Walio Vielelezo Bora
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Mei 15
    • Timotheo ‘alishawishwa kuamini’ kweli za Maandiko. Kulingana na kamusi moja ya Kigiriki, neno alilotumia Paulo hapa humaanisha “kushawishiwa kwa uthabiti; kuhakikishiwa” kitu fulani. Bila shaka, wakati na jitihada kubwa zilihitajiwa ili kukaza usadikisho huo ndani ya moyo wa Timotheo, ukimsaidia kusababu juu ya Neno la Mungu na kudhihirisha imani katika hilo. Basi, yaonekana kwamba, Eunike na Loisi pia walifanya bidii kumfundisha Timotheo Maandiko. Nao wanawake hao wenye kumhofu Mungu walivuna thawabu iliyoje! Paulo aliweza kuandika hivi juu ya Timotheo: “Nakumbuka imani iliyo katika wewe isiyo na unafiki wowote, na iliyokaa kwanza katika nyanya yako Loisi na mama yako Eunike, lakini ambayo mimi nina hakika imo pia katika wewe.”—2 Timotheo 1:5.

      Eunike na Loisi walitimiza fungu muhimu kama nini katika maisha ya Timotheo! Kuhusu jambo hilo, mwandikaji David Read asema: “Kama huyo mtume aliamini kwamba hilo halikuwa jambo la maana ila kugeuzwa imani kwa Timotheo binafsi, angemkumbusha hivyo mara moja. Lakini jambo la kwanza asemalo kuhusu imani ya Timotheo ni kwamba, tayari ‘ilikuwa hai ndani ya Loisi . . . na Eunike.’” Taarifa ya Paulo kuhusu imani ya Loisi, Eunike, na Timotheo yaonyesha kwamba mara nyingi elimu ya mapema ya Kimaandiko ifanywayo nyumbani na wazazi na hata wazakuu ni msingi wa kuamua matazamio ya wakati ujao wa kiroho wa kijana. Je, hilo halipaswi kufanya washiriki wa familia wafikirie kwa uzito kile wanachofanya ili kutimiza daraka hilo kuelekea Mungu na watoto wao?

      Labda pia Paulo alikuwa akifikiria aina ya mazingira ya nyumbani ambayo Loisi na Eunike walitokeza. Huenda mtume akawa alitembea nyumbani kwao wakati wa kukaa kwake Listra, mwaka wa 47/48 W.K. hivi. Hao wanawake wawili labda waligeuzwa imani kuwa Wakristo wakati huo. (Matendo 14:8-20) Labda mahusiano yenye uchangamfu, na furaha yaliyokuwa katika nyumba ile, yalimchochea Paulo kuchagua maneno ya kusema alipomrejezea Loisi kuwa “nyanya” ya Timotheo. Kulingana na msomi Ceslas Spicq, neno la Kigiriki alilotumia (mamʹme, tofauti na neno bora na lenye staha teʹthe) ni “neno la mtoto la upendo” kwa nyanya yake, ambalo katika muktadha huu laonyesha “tofauti zilizofichika za kujuana na shauku.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki