-
Kusafiri Mbali Zaidi ya Mediterania Nyakati za KaleMnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
-
-
Watu walioishi huko Brittany walikuwa na ujuzi wa kutengeneza meli na walikuwa mabaharia stadi waliofanya biashara na Uingereza. Eneo la Cornwall, lililo kwenye nchi iliyo kusini-magharibi ya Uingereza, lilikuwa na kiasi kikubwa cha madini ya bati, ambayo yanatumiwa kutengeneza shaba, na huko ndiko Pytheas alikoelekea. Ripoti yake ilitaja ukubwa wa nchi ya Uingereza na umbo lake linalokaribia kufanana na pembetatu, kuonyesha kwamba alizunguka kisiwa hicho.
Ingawa njia ambayo Pytheas alitumia haijulikani kikamili, huenda alisafiri katikati ya Uingereza na Ireland, na akakaa kwenye Kisiwa cha Man, ambacho kina latitudo ambayo inalingana na kipimo chake cha pili cha mwinamo wa jua. Huenda alipima kipimo chake cha tatu akiwa Lewis huko Outer Hebrides, karibu na pwani ya magharibi ya Scotland. Kutoka huko, huenda alielekea kaskazini kwenye Visiwa vya Orkney, kaskazini ya Scotland, kwa sababu simulizi lake lililonukuliwa na Plini Mkubwa, linaripoti kwamba kulikuwa na visiwa 40.
-
-
Kusafiri Mbali Zaidi ya Mediterania Nyakati za KaleMnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
-
-
Inawaziwa kwamba Pytheas alirudi Uingereza kwa njia ileile aliyofuata na hivyo akazunguka kisiwa hicho. Hatujui ikiwa aliendelea kuvumbua pwani ya kaskazini ya Ulaya kabla ya kurudi kwenye eneo la Mediterania. Kwa vyovyote vile, Plini Mkubwa anamtaja Pytheas kuwa mtu aliyejua sana maeneo yaliyokuwa na kaharabu. Maeneo ambayo zamani yalikuwa na kaharabu yalikuwa huko Jutland, sehemu ambayo sasa iko nchini Denmark, na pia kwenye ufuo wa kusini wa Bahari ya Baltiki. Bila shaka, huenda Pytheas alijua kuhusu maeneo hayo alipotembelea mojawapo ya bandari zilizo mashariki mwa Uingereza, ingawa hakuna habari zozote zinazoonyesha kwamba alisema kuwa alitembelea bandari hizo.
-