Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kupatana juu ya Mahari ya Kiasi
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 15
    • Kwa kusikitisha, katika ulimwengu wa leo wenye kufuatia vitu vya kimwili, wazazi wengi ni kama Labani. Na wengine ni wabaya zaidi. Kulingana na gazeti moja la Afrika, mapatano ya ndoa fulani hufanywa “kwa minajili tu ya akina baba wenye pupa kujifaidi.” Kisababishi kingine ni mkazo wa kiuchumi ambao huwashawishi wazazi fulani wawaone binti zao kuwa njia ya kuondolea mbali matatizo ya kifedha.a

      Wazazi fulani huwakawiza binti zao wasiolewe kwa sababu wanamngoja atakayetoa kiasi kikubwa zaidi. Hilo laweza kutokeza matatizo mazito. Ripota wa gazeti katika Afrika Mashariki aliandika hivi: “Vijana huamua kutoroka kwa siri na wapenzi wao ili kuepuka kudaiwa mahari ya juu na wakwe wagumu.” Ukosefu wa adili katika ngono ni mojawapo ya matatizo yanayosababishwa na kudaiwa kwa kiasi cha juu cha mahari. Isitoshe wanaume wengi vijana hufanikiwa kumnunua mke lakini huachwa katika deni kubwa sana. “Wazazi wapaswa kuwa wenye kiasi,” akahimiza mfanyakazi wa kijamii wa Afrika Kusini. “Hawapaswi kudai kiasi kikubwa. Wenzi waliooana karibuni wahitaji kujikimu. . . . Basi mbona kumfilisi kijana?”

      Wazazi Wakristo waweza kuwekaje kielelezo cha kuwa wenye kiasi, wenye kukubali sababu, wanapopatana juu ya malipo au upokeaji wa mahari? Jambo hili ni zito, kwa kuwa Biblia huamuru hivi: “Hali yenu ya kukubali sababu na ijulikane kwa watu wote.”—Wafilipi 4:5.

      Kanuni za Biblia Zenye Kupatana na Akili

      Iwapo wazazi Wakristo wataamua kufanya mapatano juu ya mahari au la ni uamuzi wa kibinafsi. Wakiamua kupatana, mapatano hayo yapaswa kufanywa kulingana na kanuni za Biblia. “Acheni namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa fedha,” lasema Neno la Mungu. (Waebrania 13:5) Endapo kanuni hii haidhihiriki katika mapatano kuhusu ndoa, huenda mzazi Mkristo akawa anajidhihirisha kuwa kielelezo kisichofaa. Wanaume wenye madaraka katika kutaniko la Kikristo wapaswa kuwa wenye “kukubali sababu,” si ‘wapenda-fedha’ au “wenye pupa ya pato lisilo la haki.” (1 Timotheo 3:3, 8) Mkristo atozaye kiasi kikubwa cha mahari kwa pupa bila toba aweza hata kutengwa na ushirika wa kutaniko.—1 Wakorintho 5:11, 13; 6:9, 10.

      Kwa sababu ya matatizo yanayotokezwa na pupa, serikali fulani zimetunga sheria ambazo hudhibiti mahari.

  • Kupatana juu ya Mahari ya Kiasi
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 15
    • Wakristo fulani wamepatwa na pupa ya kiasi kikubwa cha mahari na jambo hili limehuzunisha. Kwa kielelezo, fikiria ripoti hii kutoka ofisi nyingine ya tawi ya Watch Tower Society: “Kwa kawaida ni vigumu kwa ndugu waseja kuoa au dada kupata wenzi. Tokeo limekuwa ongezeko la visa vya kutenga na ushirika kwa sababu ya ukosefu wa adili katika ngono. Ndugu fulani huenda kwenye migodi wakatafute dhahabu au almasi ambazo waweza kuziuza ili wapate mali inayotosha kuoa. Hilo laweza kuwachukua mwaka mmoja au miwili au zaidi, na kwa kawaida wao hudhoofika kiroho wanapokwenda mbali na ushirika wa akina ndugu na wa kutaniko.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki