-
Kujenga Pamoja Duniani PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Karibu wakati uleule, Mashahidi kwenye kisiwa cha Guadeloupe cha Karibea walikuwa wakichora ramani ya Jumba la Kusanyiko la kutimiza mahitaji yao. Walihisi kwamba ingefaidi ikiwa wangekuwa na makusanyiko ya mzunguko katika sehemu nyingi tofauti-tofauti. Lakini miji iliyo mingi haikuwa na vifaa vilivyokuwa vikubwa vya kutosha. Kwa hiyo Mashahidi walijenga muundo uwezao kubebeka uliofanyizwa kwa vyuma na paa ya aluminiamu, kitu ambacho kingetosha kwa watu 700 na ambacho kingeweza kujengwa popote palipokuwa na ardhi iliyokuwa tambarare kidogo. Walilazimika kuongezea ukubwa wa jumba hilo tena na tena, mpaka lilipofikia kuweza kutoshea watu 5,000. Ebu fikiria kusafirisha, kujenga, na kubomoa tani 30 za vifaa kwa kila kusanyiko! Hilo Jumba la Kusanyiko lilijengwa na kubomolewa mara kadhaa kwa mwaka kwa muda wa miaka 13, mpaka ilipokuwa vigumu kupata ardhi kwa ajili ya jumba lenye kubebeka, ikawa lazima kununua ardhi na kujenga Jumba la Kusanyiko la kudumu, ambalo sasa hutumika kwa ajili ya makusanyiko ya mzunguko na mikusanyiko ya wilaya.
-
-
Kujenga Pamoja Duniani PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 329]
Mawili ya Majumba ya Kusanyiko ya kwanza
New York City
Guadeloupe
-