Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Habari Njema za Amani Zafika Kwenye Milima ya Chiapas
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Desemba 15
    • “Mimi Ni Mmoja wa Mashahidi wa Yehova”

      Adolfo, kijana mmoja ambaye hivi majuzi alipata kuwa mhubiri wa Ufalme, alikuwa akifanya kazi siku moja kwenye kituo cha redio huko Ocosingo. Kwa ghafula akasikia mlango ukibishwa kwa nguvu. Kikundi cha wanaume waliokuwa wamejifunika vichwa waliingia na kumwelekezea bunduki zao kichwani. Waliingia mbio-mbio kwenye chumba cha matangazo, wakatwaa vifaa kwa nguvu, na kutangaza kwenye redio kwamba wameanzisha vita dhidi ya serikali.

      Wanaume hao wenye silaha walimgeukia Adolfo na kumwamuru ajiunge na harakati yao. “Mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova,” akajibu Adolfo, hata ingawa hakuwa amebatizwa bado. Aliwaeleza kwamba tumaini pekee la amani ni Ufalme wa Mungu, akakataa katakata yunifomu na bunduki waliyompa. Walipoona msimamo wake imara, walimruhusu aende. Akikumbuka tukio hilo, Adolfo asema: “Tukio hilo liliimarisha imani yangu kwelikweli.”

      Hatimaye hali ilitulia, lakini eneo hilo likawa bado linasimamiwa na majeshi. Licha ya hali hiyo, Adolfo alikubali kwa furaha ombi la wazee wa kutaniko la kwao afanye kazi na kikundi cha Wakristo waliokuwa mbali na eneo hilo. Katika vituo vya ukaguzi alivyolazimika kupitia, askari-jeshi walimstahi alipojitambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Baadaye alibatizwa na amepata uradhi wa kusaidia kikundi hicho kilicho mbali kuwa kutaniko la Mashahidi wa Yehova. “Kwa kuwa sasa nimebatizwa,” akasema Adolfo, “naweza kusema kwa usadikisho kamili kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova!”

  • Habari Njema za Amani Zafika Kwenye Milima ya Chiapas
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Desemba 15
    • Wakati wa kampeni hiyo—katika sehemu iitwayo Pueblo Nuevo, Ciro—ambaye ni painia wa kawaida, alipata familia iliyoonyesha upendezi. Aliporudi siku tatu baadaye, alianzisha funzo la Biblia pamoja na familia hiyo. Lakini Ciro aliporudi akiwa na rafiki fulani ili kuendeleza funzo na familia hiyo, mwenye nyumba hakuwako. Badala yake, kulikuwa na kikundi cha wanaume waliokuwa wamejifunika vichwa wakimngojea ili wamwumize. Walimwuliza Ciro na mwandamani wake ni nini walichokuwa wakitafuta na wakatisha kuwaua. Baada ya kusali kwa Yehova kwa ukimya, Wakristo hao wawili waliwaeleza kwa ujasiri kwamba walikuwa wamekuja kufundisha familia hiyo Biblia. Baada ya kusikia mambo hayo, wanaume hao waliojifunika vichwa waliwaachilia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki