Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kutambua na Kuushinda Udhaifu Wowote wa Kiroho
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 15
    • Kumbuka kwamba miongoni mwa vipande vya silaha zetu za kiroho ni “bamba la kifuani la uadilifu,” ambalo huulinda moyo wetu, na “kofia ya chuma ya wokovu,” ambayo huilinda akili yetu. Kujifunza kuyatumia maandalizi hayo kwa matokeo kwaweza kumaanisha tofauti kati ya ushindi na ushinde.—Waefeso 6:14-17; Mithali 4:23; Waroma 12:2.

  • Jinsi ya Kutambua na Kuushinda Udhaifu Wowote wa Kiroho
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 15
    • Kuvaa “kofia ya chuma ya wokovu” huhusisha kuweka dhahiri akilini baraka za ajabu zilizo mbele, pasipo kujiruhusu tukengeushwe fikira na vitu vya ulimwengu vinavyometameta na kuvutia. (Waebrania 12:2, 3; 1 Yohana 2:16) Kuwa na mtazamo huo kutatusaidia kutanguliza mapendezi ya kiroho mbele ya manufaa za kimwili au za kibinafsi. (Mathayo 6:33) Hivyo, ili kuwa na uhakika kwamba tuna kipande hiki cha silaha kikiwa mahali panapofaa, ni lazima tujiulize kwa unyofu hivi: Ni nini ninachofuatia maishani? Je, nina miradi mahususi ya kiroho? Ninafanya nini ili kuifikia? Iwe sisi ni wa mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta au wa kundi la “umati mkubwa,” twapaswa kumwiga Paulo, aliyesema hivi: “Bado mimi sijifikirii mwenyewe kuwa nimekwisha kulishika hilo; bali kuna jambo moja juu ya hilo: Nikisahau mambo ya nyuma na kujinyoosha mbele kwenye mambo ya mbele, ninafuatilia sana kuuelekea mradi.”—Ufunuo 7:9; Wafilipi 3:13, 14.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki