Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hosea
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
    • “JICHUKULIE MKE WA UASHERATI”

      (Hosea 1:1–3:5)

      Yehova anamwambia Hosea: “Nenda, jichukulie mke wa uasherati.” (Hosea 1:2) Hosea anatii naye anazaa mwana na Gomeri. Kwa wazi, Gomeri anazaa nje ya ndoa watoto wawili wanaofuata. Maana ya majina yao, Lo-ruhama na Lo-ami, inaonyesha kwamba Yehova hatawaonyesha Waisraeli rehema na atawakataa watu wake wasio washikamanifu.

      Kwa kweli, Yehova anahisi namna gani kuhusu watu wake ambao wameasi? Anamwambia Hosea hivi: “Nenda tena, mpende mwanamke anayependwa na rafiki yako na ambaye anafanya uzinzi, kama vile Yehova alivyowapenda wana wa Israeli ingawa wanageukia miungu mingine.”—Hosea 3:1.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hosea
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
    • “YEHOVA ANA KESI”

      (Hosea 4:1–13:16)

      “Yehova ana kesi na wakaaji wa nchi.” Kwa nini? Kwa sababu “hakuna kweli wala fadhili zenye upendo wala kumjua Mungu katika nchi.” (Hosea 4:1) Waisraeli walioasi wamewapunja watu, wamemwaga damu, na kufanya uasherati wa kimwili na wa kiroho. Badala ya kumwomba Mungu awasaidie, “wameita Misri; wameenda Ashuru.”—Hosea 7:11.

      Yehova anatangaza hukumu yake, akisema: “Israeli watamezwa.” (Hosea 8:8) Ufalme wa Yuda pia una hatia. “Yehova ana kesi na Yuda,” Hosea 12:2 linasema, “kumtoza Yakobo hesabu kulingana na njia zake; atamlipa kulingana na matendo yake.” Lakini bila shaka watarudishwa, kwa kuwa Mungu anaahidi hivi: “Nitawakomboa wao kutoka katika mkono wa Kaburi; nitawaokoa wao kutoka kwenye kifo.”—Hosea 13:14.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hosea
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
    • “NJIA ZA YEHOVA ZIMENYOOKA”

      (Hosea 14:1-9)

      Hosea anasihi hivi: “Ee Israeli, rudi kwa Yehova Mungu wako, kwa maana umejikwaa katika kosa lako.” Anawahimiza watu wamwambie Yehova hivi: “Samehe kosa letu; na ukubali lililo jema, nasi tutatoa ng’ombe-dume wachanga wa midomo yetu.”—Hosea 14:1, 2.

      Mkosaji anayetubu anapaswa kumrudia Yehova, kukubali njia zake, na kumtolea dhabihu za sifa. Kwa nini? Kwa sababu “njia za Yehova zimenyooka, na waadilifu ndio watakaotembea katika hizo.” (Hosea 14:9) Tunashangilia kama nini kwamba bado wengi “watakuja kwa Yehova na kwa wema wake wakitetemeka katika siku za mwisho”!—Hosea 3:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki