Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwige Mwalimu Mkuu
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 23]

      Je, Unakumbuka Vielezi Hivi?

      Hapa pana vielezi vichache vyenye matokeo. Mbona usichunguze vichapo vinavyotajwa na kuona jinsi kielezi kilivyokazia hoja inayozungumziwa?

      • Kama vile wanaume wawili wanaopakua makatoni mazito ya bidhaa, ndoa yenye mafanikio hutegemea hasa wenzi wanaopatana.—Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 2001, ukurasa wa 16.

      • Kueleza hisia zako ni sawa na kutupa mpira. Unaweza kuurusha kwa uanana au kuuvurumisha kwa nguvu na kuumiza mtu.—Amkeni!,

      Januari 8, 2001, ukurasa wa 10.

      • Kujifunza kuonyesha upendo ni kama vile kujifunza lugha mpya.—Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1999, ukurasa wa 18, 22-23.

      • Dhambi tuliyorithi inaweza kulinganishwa

      na kile kinachotukia wakati faili za kompyuta zinapovurugwa na kasoro fulani.—Je, Kuna Muumba Anayekujali?, ukurasa wa 156.

      • Uwasiliani-roho husaidia roho waovu kama vile chambo husaidia wawindaji. Huvutia windo.—Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, ukurasa wa 111.

      • Yesu anayeokoa wazao wa Adamu anaweza kulinganishwa na mfadhili tajiri anayelipa deni la kampuni (lililosababishwa na meneja asiye mnyoofu) na kufungua upya kiwanda hicho, na hivyo kunufaisha wafanyakazi wengi.—Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1991, ukurasa wa 13.

      • Kama vile watu wanaopenda sanaa hujitahidi sana ili kurudisha upya mchoro ulioharibiwa, Yehova anaweza kutusamehe kasoro zetu, kuona wema wetu, na hatimaye kuturudisha katika hali ya ukamilifu iliyopotezwa na Adamu.—Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1990,

      ukurasa wa 22.

  • Mwige Mwalimu Mkuu
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
    • 18. Tunawezaje kupata vielezi vinavyofaa?

      18 Tunawezaje kupata vielezi vinavyofaa? Si lazima tufikirie hadithi ndefu zenye mambo mengi. Vielezi vifupi vinaweza kuwa na matokeo sana. Jaribu kufikiria mifano inayohusu jambo linalozungumziwa. Kwa mfano, tuseme tunazungumzia msamaha wa Mungu, na tunataka kutoa kielezi kwa hoja inayotajwa katika andiko la Matendo 3:19, ambalo linasema kwamba Yehova ‘hufuta’ makosa yetu. Taarifa hiyo yenyewe inatumia lugha ya mfano, lakini tunaweza kutumia mfano gani halisi kueleza jambo hilo—kifuto? sponji? Huenda tukasema: ‘Yehova anapotusamehe dhambi zetu, ni kana kwamba anachukua sponji (au kifuto) na kuzifuta kabisa.’ Si vigumu kuelewa jambo linalokaziwa na kielezi hicho rahisi.

      19, 20. (a) Tunaweza kupata wapi vielezi vinavyofaa? (b) Ni baadhi ya vielezi gani vyenye matokeo ambavyo vimechapishwa katika vichapo vyetu? (Ona pia sanduku.)

      19 Unaweza kupata wapi vielezi vinavyofaa, kutia ndani mifano inayohusu maisha halisi? Vitafute maishani mwako au katika mazingira mbalimbali na mambo yaliyoonwa na waabudu wenzako. Vielezi vinaweza kuchaguliwa kutokana na vitu vingi, kutia ndani vitu vilivyo hai na visivyo hai, vifaa vya nyumbani, au tukio la karibuni linalojulikana na watu katika jumuiya. Njia moja yenye matokeo ya kupata vielezi vinavyofaa ni kuwa macho, “kutazama kwa uangalifu” hali za kila siku zinazotuzunguka. (Matendo 17:22, 23) Kitabu kimoja cha kitaalamu kinasema hivi kuhusu kutoa hotuba hadharani: ‘Msemaji ambaye ni makini kuona watu na kazi mbalimbali wanazofanya, huzungumza na watu wa aina zote, huchunguza mambo kwa makini na kujiuliza maswali hadi aelewe, hukusanya habari nyingi itakayomsaidia sana kwa vielezi.’

      20 Pia tunaweza kupata vielezi vingi sana vyenye matokeo kutoka kwa Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, na vichapo vingine vinavyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza kujifunza mengi kwa kuchunguza jinsi vichapo hivyo vinavyotumia vielezi.c Kwa mfano, fikiria kielezi kilichotumiwa katika kitabu Ujuzi sura ya 17 fungu la 11. Kinalinganisha nyutu mbalimbali kutanikoni na magari mbalimbali yanayosafiri yakielekea upande mmoja. Kwa nini ni chenye matokeo? Ona kwamba kinahusu hali za kawaida maishani, kinalingana na jambo linalotajwa, na matumizi yake ni wazi. Huenda tukatumia vielezi vinavyopatikana katika vichapo vyetu tunapofundisha, labda kwa kuvitumia vifae mahitaji ya mwanafunzi wa Biblia au kuvitumia kwenye hotuba.

  • Mwige Mwalimu Mkuu
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
    • c Ili kupata mifano, ona Watch Tower Publications Index 1986-2000, chini ya kichwa “Illustrations (Vielezi).”—Kimechapishwa katika lugha kadhaa na Mashahidi wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki