Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Hamwijui Ile Siku Wala Saa”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
    • WATIWA-MAFUTA WATHIBITISHA KWAMBA WAKO TAYARI

      11. Baada ya mwaka wa 1914, kwa nini watiwa-mafuta fulani walifikiri kwamba Bwana amekawia?

      11 Kumbuka mifano ya Yesu kuhusu wale mabikira na talanta. Ikiwa mabikira au watumwa katika mifano hiyo wangejua wakati ambapo bwana-arusi au bwana mkubwa angekuja, hawangehitaji kuendelea kukesha. Lakini hawakujua, kwa hiyo, walihitaji kuendelea kuwa tayari. Ingawa kwa miongo mingi watiwa-mafuta waliuona mwaka wa 1914 kuwa mwaka wa pekee, hawakuelewa waziwazi ni nini ambacho kingetukia. Mambo yalipokosa kutukia kama walivyotarajia, huenda baadhi yao walidhani kwamba Bwana-arusi amekawia. Baadaye, ndugu mmoja alikumbuka hivi: “Wachache kati yetu walifikiri kwa hakika kwamba tungeenda mbinguni katika juma la kwanza la Oktoba [mwaka wa 1914].”

      12. Watiwa-mafuta walionyeshaje kwamba ni waaminifu na wenye busara?

      12 Hebu fikiria jinsi ilivyovunja moyo kutarajia mwisho uje lakini haukuja! Isitoshe, akina ndugu walikabiliana na upinzani wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu! Kisha kukawa na kipindi cha kutotenda, kama cha usingizi. Lakini mwaka wa 1919, kulikuwa na mwito wa kuamka! Yesu alikuja katika hekalu la kiroho la Mungu, na wakati wa ukaguzi ulikuwa umefika. Hata hivyo, baadhi ya Wakristo hawakufaulu kupita ukaguzi huo na hivyo wakapoteza pendeleo lao la kuendelea kufanya “biashara” ya Mfalme. (Mt. 25:16) Kama wale mabikira wapumbavu, ni kana kwamba hawakuwa na bidii ya kuongeza mafuta yao ya kiroho.

  • “Hamwijui Ile Siku Wala Saa”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
    • KUTHIBITISHA KWAMBA TUKO TAYARI

      14. Tutalindwa jinsi gani tukishikamana na jamii inayotumiwa na Mungu kuandaa chakula cha kiroho?

      14 Kama Wakristo watiwa-mafuta, washiriki wa umati mkubwa ambao wako macho wanashikamana kabisa na jamii hiyo iliyowekwa rasmi na Mungu ili kuandaa chakula cha kiroho. Kwa njia hiyo, ni kana kwamba wao pia wanaongeza mafuta yao ya kiroho kutoka katika Neno la Mungu na roho yake. (Soma Zaburi 119:130; Yohana 16:13.) Wakiwa wameimarishwa hivyo, wao pia wanaonyesha kwamba wako tayari kwa ajili ya kurudi kwa Kristo, wakiendelea kuonyesha bidii hata chini ya majaribu makali. Kwa mfano, katika kambi moja ya Wanazi, mwanzoni akina ndugu walikuwa na Biblia moja tu. Basi, wakasali ili wapate chakula zaidi cha kiroho. Muda mfupi baadaye walipata habari kwamba ndugu aliyeletwa kambini humo alifaulu kuficha magazeti machache mapya ya Mnara wa Mlinzi ndani ya mguu wake bandia wa mbao na kuyaleta kambini. Ndugu Ernst Wauer, ndugu mtiwa-mafuta aliyekuwa miongoni mwa watu waliookoka kutoka katika kambi hiyo, alikumbuka hivi baadaye: “Yehova alitusaidia kwa njia ya ajabu kukumbuka mawazo yenye kuimarisha yaliyokuwa katika makala hizo.” Kisha akasema: “Siku hizi, ni rahisi sana kupata chakula cha kiroho, lakini je, sikuzote tunakithamini? Nina hakika kwamba Yehova atawabariki sana wale wanaomtegemea, wanaobaki washikamanifu, na kula kwenye meza yake.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki