Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwa Wahudumu Wenye Ubunifu, Wanaobadilika Kulingana na Hali
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • 10, 11. Paulo alibadilishaje mifano yake iwafae wasikilizaji? (Ona pia maelezo ya chini.)

      10 Paulo alifanya nini alipotaka kuwaeleza wasikilizaji wake kweli nzito za Biblia? Mtume huyo alikuwa na ustadi wa kutumia mifano ya kawaida iliyo rahisi kueleweka ili kueleza mambo magumu ya kiroho. Kwa mfano, Paulo alijua kwamba watu huko Roma walijua sana mfumo wa utumwa uliokuwepo kotekote katika Milki ya Roma. Isitoshe, watu wengi kati ya wale ambao Paulo aliwaandikia walikuwa watumwa. Hivyo, Paulo alitumia mfano wa utumwa kutetea hoja yake nzito, iliyoonyesha kwamba mtu anaweza kuchagua kuwa mtumwa wa dhambi au wa uadilifu.—Waroma 6:16-20.

      11 Kitabu kimoja kinasema hivi: “Miongoni mwa Waroma, bwana mkubwa angeweza kumweka huru mtumwa wake bila masharti, au mtumwa angeweza kununua uhuru wake kwa kumlipa bwana wake. Pia, mtu angeweza kuwekwa huru ikiwa angefanywa kuwa mtumwa wa mungu fulani.” Mtumwa aliyewekwa huru angeweza kuendelea kumfanyia kazi bwana wake kwa malipo. Inaonekana Paulo alikuwa akirejelea zoea hilo alipoandika kwamba mtu anaweza kuchagua ni bwana yupi ambaye atatii—dhambi au uadilifu. Wakristo huko Roma walikuwa wamewekwa huru kutokana na dhambi na kuwa mali ya Mungu. Walikuwa huru kumtumikia Mungu, lakini ikiwa wangependa bado wangeweza kuchagua kutumikia dhambi, bwana wao wa zamani. Mfano huo rahisi na wenye kueleweka ungewachochea Wakristo huko Roma kujiuliza, ‘Ninamtumikia bwana yupi?’b

  • Kuwa Wahudumu Wenye Ubunifu, Wanaobadilika Kulingana na Hali
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • b Vivyo hivyo, ili kueleza uhusiano mpya kati ya Mungu na “wana” wake waliotiwa mafuta kwa roho, Paulo alitumia wazo la kisheria lililojulikana sana na wasomaji wake katika Milki ya Roma. (Waroma 8:14-17) Kulingana na kitabu kimoja (St. Paul at Rome), “Waroma walikuwa na desturi ya kuwachukua watu wazima au watoto wa watu wengine na kuwafanya kuwa wana wao, nayo ilipatana sana na maoni yao kuhusu familia.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki