-
Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya KweliBiblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
3. (a) Biblia inasema nini kuhusu kutumia sanamu, na kwa nini huenda ikawa vigumu kwa wengine kukubali maoni ya Mungu? (b) Unapaswa kufanya nini ikiwa una vitu vinavyohusiana na ibada ya uwongo?
3 Watu fulani wamekuwa na sanamu au vihekalu katika nyumba zao kwa miaka mingi. Je, wewe ni mmoja wao? Ikiwa ndivyo, huenda ukaona kwamba ni vigumu au ni vibaya kusali kwa Mungu bila kutumia vitu vinavyoonekana. Huenda hata unavipenda sana baadhi ya vitu hivyo. Lakini Mungu ndiye anayesema jinsi anavyotaka aabudiwe, na Biblia inafundisha kwamba hataki tutumie sanamu. (Kutoka 20:4, 5; Zaburi 115:4-8; Isaya 42:8; 1 Yohana 5:21) Kwa hiyo, unaweza kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli kwa kuharibu vitu vyovyote ulivyo navyo ambavyo vinahusiana na ibada ya uwongo. Kwa vyovyote vile, vione vitu hivyo jinsi Yehova anavyoviona, yaani, ni ‘vitu vinavyochukiza.’—Kumbukumbu la Torati 27:15.
-
-
Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya KweliBiblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
5. Unaweza kufanya nini ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu au kuabudu mababu?
5 Ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu au kuabudu mababu, unaweza kufanya nini? Soma na utafakari maandiko ya Biblia yanayoonyesha maoni ya Mungu. Sali kwa Yehova kila siku kuhusu tamaa yako ya kuchukua msimamo upande wa kweli, na umwombe akusaidie uwe na maoni kama yake.—Isaya 55:9.
-