Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Kuna Uhai Baada ya Kifo?
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Je! Kuna Uhai Baada ya Kifo?

      “Maana kuna matumaini ya muti; ya kuwa ukikatwa, utachipuka tena . . . Kama mutu akikufa, ataishi tena?”—MUSA, NABII WA ZAMANI.

      1-3. Namna gani watu wengi hutafuta kitulizo wanapopoteza mpendwa katika kifo?

      KATIKA jumba la kulinda maiti kwa ajili ya mazishi katika mji wa New York, marafiki na watu wa familia waandamana polepole karibu ya sanduku lenye kufunuliwa. Watazama kwa mshangao mwili wa kijana mwenye umri wa miaka 17. Marafiki zake wa shuleni wamtambua kwa shida. Utunzaji wa kutumia dawa za kemikali umemuondoa nywele zake; ugonjwa wa kansa umemfanya apoteze uzito wake. Je! huyu ndiye kweli waliyemjua kuwa rafiki yao? Miezi michache tu kabla ya hapo alikuwa mwenye kujaa mawazo, maulizo, nguvu—yaani uhai! Mama wa kijana mwenye kuvunjika moyo ajaribu kupata tumaini na kujituliza na wazo la kwamba kwa vyovyote mwana wake bado ni mwenye kuishi. Kwa machozi arudilia tena na tena yale amefundishwa: “Tommy ni mwenye furaha zaidi sasa. Mungu alipenda kuwa pamoja na Tommy mbinguni.”

      2 Mbali kadiri ya kilomita 11,000, katika Jamnagar, India, wale wana watatu wa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka 58 wasaidia kuulaza mwili wa baba yao juu ya chungu ya kuni ya kuchomea maiti. Wakati wenye kungaa wa jua la mchana-kati, mwana aliye mkubwa zaidi aanza kuunguza maiti kwa kuwasha moto magogo ya kuni na kuumwangia mwili wa baba yake usiokuwa na uhai mchanganyiko wenye kunukia vizuri wa marashi-vikolezo na uvumba. Mlio wenye kutatarika wa moto unapitwa na misemwa ya sala ya dini ya Kihindu yenye kurudiliwa ya Brahman inayomaanisha: “Acha nafsi hiyo isiyokufa kamwe iendelee katika nguvu yayo kuwa mwishowe jambo halisi.”

      3 Ndugu hao watatu wanapoendelea kutazama kuunguzwa kwa mwili, kila mmoja kwa kimya hujiuliza, ‘Je! mimi naamini kuwako kwa uhai baada ya kifo?’ Wakiwa wameelimishwa kutoka sehemu mbalimbali za dunia, wanatoa majibu yenye kutofautiana. Aliye mdogo zaidi anajisikia kuwa hakika kwamba baba yao mpendwa atazaliwa upya katika mwili mwingine wa hali ya juu zaidi. Ndugu yake wa kati anaamini kwamba wafu ni wenye kulala, hawajui lolote. Aliye mkubwa wao ajaribu tu kukubali kifo kuwa jambo la kawaida, sababu yeye hufikiri kwamba hakuna mtu anayeweza kujua hakika jambo linalotufikia tunapokufa.

      Ulizo Moja Lenye Majibu Mengi

      4. Ni ulizo gani limekuwa likisumbua wanadamu kwa miaka mingi?

      4 Je! kuna uhai baada ya kifo? Hilo ni ulizo ambalo limehangaisha wanadamu muda wa maelfu ya miaka. “Hata wanateolojia wanatatanishwa wanapopambana na ulizo hilo,” asema Hans Küng, msomi Mkatoliki. Miaka mingi imepita watu katika kila jamii wamekuwa wakifikiri sana juu ya jambo hilo, na majibu yanayotolewa ni mengi.

      5-8. Dini nyingi hufundisha nini kuhusu uhai baada ya kifo?

      5 Wakristo wengi wa jina tu wanaamini katika mbingu na helo. Kwa upande mwingine, Wahindu wanaamini kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Akieleza kuhusu maoni ya Waislamu, Amir Muawiyah, msaidizi kwenye makao makuu ya dini ya Kislamu, asema: “Tunaamini kutakuwa siku ya hukumu kisha kufa, wakati uendapo mbele ya Mungu, Allah, ambayo itakuwa tu namna mambo yanavyoendeshwa kwenye korti [mahakama].” Kulingana na imani ya Kiislamu, ndipo Allah atakapokadiria mwendo wa maisha wa kila mmoja na kumpeleka kwenye paradiso au helo ya moto.

      6 Katika Sri Lanka, Wabuddha na Wakatoliki huiacha milango na madirisha wazi kabisa wakati kifo kinapotokea katika jamaa yao. Taa yenye mafuta huashwa, na sanduku linalazwa hivi kwamba miguu ya mtu aliyekufa inaangalia kwenye mlango. Wanaamini kwamba kufanya hivyo kutawezesha roho au nafsi ya mtu aliyekufa kuondoka nyumbani kwa urahisi.

      7 Ronald M. Berndt kutoka Chuo Kikuu cha Australia ya Magharibi asema kwamba Waborijeni wa Australia wanaamini kwamba “viumbe vya kibinadamu wanayo roho isiyoweza kuharibiwa.” Makabila mengine ya Kiafrika yanaamini kwamba kisha kufa watu wa kawaida hugeuka kuwa mizuka, wakati uohuo watu kabaila hugeuka roho za mababu, ambao wataheshimiwa na kutolewa maombi wakiwa viongozi wasiyoonekana wa jamii ya watu.

      8 Katika inchi nyingine, zile imani kuhusiana na vinavyowaziwa kuwa nafsi za watu waliokufa ni mchanganyiko wa mapokeo ya kienyeji na Ukristo wa jina tu. Kwa mfano, katika Afrika ya mashariki, kati ya Wakatoliki na Waprotestanti wengi, ni jambo la kawaida kufunika kioo mtu anapokufa ili kwamba yeyote asije akatazama ndani na hivyo kuiona roho ya mtu aliyekufa. Ndipo, baada ya siku 40 tangu kufa kwa mpendwa, familia na marafiki husherehekea kupanda kwa nafsi mbinguni.

      Jambo Linaloenea Pote

      9, 10. Ni juu ya imani gani ya msingi dini mbalimbali hukubaliana?

      9 Majibu kwa ulizo kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa yanatolewa kwa kutofautiana kulingana na desturi pia imani za watu wanaoyatoa. Lakini, dini nyingi hukubaliana juu ya wazo moja la msingi: Kwamba kitu fulani ndani ya mtu—nafsi, roho, muzimu—ni kisichoweza kufa na hivyo huendelea kuishi baada ya kifo.

      10 Imani ya kutoweza kufa kwa nafsi inaenea karibu pote katika maelfu ya dini na mifarakano ya Jumuiya ya Wakristo. Hilo ni fundisho la kawaida katika dini ya Kiyahudi pia. Katika dini ya Wahindu imani hii ndiyo msingi wenyewe wa fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Waislamu huamini kwamba nafsi huja kwenye uhai pamoja na mwili lakini huendelea kuishi mwili ufapo. Imani nyingine—fundisho la Afrika la kuwako kwa roho ziwezazo kutenganishwa na mwili, dini ya Shinto, na hata ya Buddha—hufundisha mambo tofauti juu ya jambo hili.

      11. Wataalamu wengine wana maoni gani kuhusu wazo la kwamba nafsi ni isiyoweza kufa?

      11 Wengine huchukua msimamo tofauti, kwamba uhai wenye ufahamu unamalizika mtu afapo. Kwao, jambo la kwamba uhai wenye hisia na akili huendelea katika kitu kisicho na utu, nafsi yenye kivuli inayoachana na mwili ni wazo lisilo la akili. Miguel de Unamuno, mwandikaji na pia msomi Mhispania wa karne ya 20 aandika: “Kuamini katika kutoweza kufa kwa nafsi ni kutaka kwamba ile nafsi iwe isiyokufa, lakini kutaka hilo kwa nguvu kama hiyo ya kuazimia kutamfanya mtu akose kufikiria sababu vizuri na kuwa hivyo mpumbavu.” Miongoni mwa wale waliokataa kuamini kutoweza kufa kwa nafsi wamo wanafalsafa wenye kujulikana sana wa kale Aristote na Epicure, mwanafizikia Hippocrates, mwanafalsafa Mskoti David Hume, Msomi Muarabu Averroës, na waziri-mkuu wa kwanza wa India baada ya uhuru, Jawaharlal Nehru.

      12, 13. Ni maulizo gani ya lazima yanayotokea kuhusu fundisho la kutokufa kwa nafsi?

      12 Ulizo ni, je! kweli tunayo nafsi isiyoweza kufa? Ikiwa hakika nafsi si isiyoweza kufa, basi fundisho kama hili la uongo lingewezaje kuwa sehemu ya maana zaidi ya dini nyingi leo? Chanzo cha wazo hili ni gani? Na ikiwa kweli nafsi yakoma kuwapo kisha kufa, kuna tumaini gani kwa wafu?

      13 Je! tunaweza kupata majibu yenye ukweli na yenye kutosheleza kwa maulizo hayo? Ndiyo! Maulizo hayo na mengine yatajibiwa katika kurasa zinazofuata. Kwanza, acheni tuchunguze namna fundisho la kutokufa kwa nafsi lilivyoanza.

  • Kutoweza Kufa kwa Nafsi—Chanzo cha Fundisho Hilo
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Kutoweza Kufa kwa Nafsi—Chanzo cha Fundisho Hilo

      “Hakuna kichwa cha mazungumzo ambacho, kwa kulinganisha na uhai wake wenye chanzo cha kiroho, kimevuta akili ya mwanadamu sana kama kile cha hali yake ya baada ya kifo.”—“ENCYCLOPÆDIA OF RELIGION AND ETHICS.”

      1-3. Namna gani Socrates na Plato waliendeleza wazo la kwamba nafsi ni isiyoweza kufa?

      MTAALAMU na mwalimu mwenye umri wa miaka 70 alishtakiwa ukosefu wa heshima kwa Mungu na uharibifu wa mawazo ya vijana kwa fundisho lake. Ingawa alijitetea kwa akili sana wakati wa kusambishwa, baraza la waamzi wenye upendeleo lilimpata na kosa na hivyo akahukumiwa kifo. Saa chache kabla ya kuuawa, mwalimu huyu mzee atolea wanafunzi waliokusanyika kumzunguka mfululizo wa sababu ili kuhakikisha kwamba nafsi ni isiyoweza kufa na kwamba kifo si jambo la kuogopa.

      2 Mwanaume huyu aliyehukumiwa kifo ni Socrates, mwanafalsafa Mgiriki mwenye sifa sana wa karne ya tano K.W.K.a Mwanafunzi wake Plato aliandika matukio haya katika vitabu Apologie na Phaedo. Socrates na Plato ni wenye kusifiwa kuwa kati ya watu wa kwanza walioendeleza mbele wazo la kwamba nafsi ni isiyoweza kufa. Lakini si wao walio vyanzo vya fundisho hilo.

      3 Kama tutakavyoona, vyanzo vya wazo hilo la kutoweza kufa kwa nafsi ya binadamu ni tangu nyakati za mapema zaidi. Lakini Socrates na Plato, ndio waliolikuza sana wazo hili na kulifanya kuwa fundisho la kifalsafa, hivyo kulifanya livutie zaidi jamii za watu wenye elimu wa siku zao na kuendelea.

      Kutoka Pythagoras mpaka Mapiramidi

      4. Kabla ya Socrates, maoni ya Wagiriki yalikuwa nini kuhusu maisha ya baadaye?

      4 Wagiriki walioishi kabla ya Socrates na Plato pia waliamini kwamba nafsi inaendelea kuishi baada ya kifo. Pythagoras, Mgiriki mwenye elimu ya hesabu ajulikanaye sana wa karne ya sita K.W.K., alishikilia kwamba nafsi ni isiyoweza kufa na hivyo yapaswa kugeuka na kuingia mwili mwingine. Kabla yake, Thales wa Miletus, aliyefikiriwa kuwa mwanafalsafa Mgiriki aliyejulikana mapema zaidi, alifikiri kwamba nafsi isiyoweza kufa inapatikana si tu katika watu, wanyama na mimea lakini pia imo katika vitu kama smaku, kwa kuwa inaweza kusogeza chuma. Wagiriki wa kale walidai kwamba nafsi za wafu zilikuwa zikichukuliwa kwa mashua ndogo kuvuka mto Styx mpaka kwenye nchi kubwa chini ya ardhi iitwayo Ulimwengu wa chini. Huko, waamuzi wahukumia zile nafsi kuingia ama kwenye mateso katika gereza lenye kuzungukwa na kuta ndefu sana, ama kwenye raha kamili katika makao ya waliobarikiwa baada ya kifo.

      5, 6. Waajemi waliiona nafsi namna gani?

      5 Katika Irani, au Uajemi, kuelekea mashariki, nabii aitwaye Zoroastre alitokea katika karne ya saba K.W.K. Yeye aliingiza namna ya ibada iliyojulikana baadaye kuwa Kizoroastriani. Hiyo ilikuwa dini ya Milki ya Uajemi, iliyoutawala ulimwengu kabla ya Ugiriki kuwa nguvu kubwa ya ulimwengu. Maandishi ya Kizoroastriani yasema: “Nafsi ya Mwadilifu itakuwa milele katika shangwe ikiwa isiyoweza kufa, lakini nafsi ya Mwongo hakika itakuwa yenye kuteswa. Na hizi amri Ahura Mazda [maana yake mungu mwenye hekima] ameziamuru kupitia enzi Yake yenye mamlaka.”

      6 Lile fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi lilikuwa pia sehemu ya dini ya Kiirani ya kabla ya Kizoroatriani. Kwa mfano, makabila ya zamani ya Irani yalishugulikia nafsi za waliokufa kwa kuwatolea chakula na mavazi ili kuwafaidi hao walio katika ulimwengu wa chini.

      7, 8. Wamisri wa kale waliamini nini kuhusu kuokoka kifo cha mwili kwa nafsi?

      7 Imani katika uhai baada ya kifo ilikuwa fundisho la maana sana katika dini ya Misri. Wamisri walishikilia kwamba ile nafsi ya mtu aliyekufa ingeweza kuhukumiwa na Osiris, mungu mkuu katika ulimwengu wa chini. Kwa mfano, maandishi ya funjo (papyrus) yanayodaiwa kuwa ya kutoka karne ya 14 K.W.K. yaonyesha Anubis, mungu wa wafu, akiongoza nafsi ya yule mwandishi Hunefer mbele ya Osiris. Moyo wa mwandishi ukiwakilishwa na dhamiri yake, unapimwa juu ya mizani dhidi ya nyoya ambayo mungu mke wa ukweli na haki huvaa kwenye kichwa chake. Thoth, mungu mwingine, hurekodi matokeo. Kwa kuwa moyo wa Hunefer si mzito kwa kulemewa na kosa, wapima uzito ulio chini ya lile nyoya, naye Hunefer aruhusiwa kuingia nchi ya Osiris na kupata kutoweza kufa. Funjo hilo huonyesha pia dubwana wa kike akisimama pembeni ya mizani, tayari kumla mtu aliyekufa ikiwa moyo wake unashindwa jaribio. Wamisri pia walikuwa wakimumiani wafu wao ili wasioze na kulinda miili ya mafarao katika mapiramidi yenye kustaajabisha kwa kuwa walifikiri kwamba kuokoka kwa nafsi kulitegemea kulindwa kwa mwili.

      8 Kwa hiyo, ustaarabu mbalimbali wa kale ulishikilia kwa umoja fundisho moja—kule kutoweza kufa kwa nafsi. Je! walipata fundisho hili kutoka chanzo kilekile kimoja?

      Chanzo-Asili

      9. Ni dini gani iliyokuwa na uvutano juu ya ulimwengu wa kale wa Misri, Uajemi na Ugiriki?

      9 Kitabu The Religion of Babylonia and Assyria chasema: “Katika ulimwengu wa zamani, Misri, Uajemi, na Ugiriki zilihisi uvutano wa dini ya Kibabuloni.” Kitabu hiki kinaendelea kufasiria: “Katika mwono wa muungano wa mapema kati ya Misri na Babuloni, kama ilivyofunuliwa na vibao vya kuandikia vya El-Amarna, bila shaka kulikuwa uwezekano mwingi wa kuingia kwa maoni na desturi za Kibabuloni katika ibada za Misri. Katika Uajemi, ibada ya Mithra hufunua uvutano ulio wazi wa mawazo ya Kibabuloni . . . Mchanganyiko wenye nguvu wa sehemu ya Kisemiti katika hadithi za kwanza za Kigiriki na pia katika madhehebu ya kwanza ya Kigiriki sasa unakubaliwa kwa ujumla na wanachuo kuwa hauhitaji maelezo zaidi. Sehemu hizo za Kisemiti kwa kadiri kubwa ni za Kibabuloni hasa.”b

      10, 11. Maoni ya Wababuloni kuhusu uhai baada ya kifo yalikuwa nini?

      10 Lakini, je! maoni ya Kibabuloni kuhusu jambo linalotukia baada ya kifo hayatofautiani kabisa na yale ya Kimisri, Kiajemi na Kigiriki? Kwa mfano, fikiria Utungo wa Kishairi wa Gilgamesh. Mwanamume shujaa mzee, Gilgamesh, akisumbuliwa mara kwa mara na kuwapo kwa kifo, ashika njia akitafuta kutoweza kufa lakini ashindwa kukupata. Katika safari akutana na kijana mwanamke mchuuza-mvinyo ambaye pia humsadikisha apate faida yote ya maisha aliyo nayo sasa, kwa kuwa hatapata uhai usiokuwa na mwisho autafutao. Ujumbe wa utungo mzima wa shairi ni kwamba kifo hakiepukiki na tumaini la kutoweza kufa ni ndoto tu. Je! hili laonyesha sasa kwamba Wababuloni hawakuamini katika maisha ya kisha kufa?

      11 Profesa Morris Jastrow, Jr., wa Chuo Kikuu cha Pennsylvania, Shirikisho la Amerika, aliandika: “Wala watu wala viongozi wa kidini [wa Babuloni] hawakufikiria kamwe uwezekano wa kutoweka kabisa kwa kile ambacho wakati moja kilikuja kwenye uhai. Kifo [katika maoni yao] kilikuwa mpito wa kuingia katika aina nyingine ya uhai, na kukana kutokufa kwa mtu ni kutilia tu mkazo kwamba mtu hawezi kuepuka kifo ambacho, kulingana na imani yao, humpeleka mtu kwenye aina nyingine ya uhai.” Ndiyo, Wababuloni waliamini pia kwamba uhai wa aina nyingine, katika umbo lingine, uliendelea kuwako baada ya kifo. Walionyesha wazo hilo kwa kuzika vitu fulani pamoja na mfu ili aendelee kuvitumia baadaye.

      12-14. (a) Kisha Garika, chanzo cha fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi kilikuwa wapi? (b) Namna gani fundisho hili lilisambaa juu ya dunia?

      12 Bila shaka, lile fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi larudi nyuma huko Babuloni wa kale. Kulingana na Biblia, kitabu chenye kutia alama historia sahihi, jiji la Babeli au Babuloni liliwekewa msingi na Nimrodi, mjukuu mkubwa wa Noa.c Kisha Garika ya ulimwenguni pote katika siku za Noa, kulikuwako lugha moja na dini moja tu. Kwa kuanzisha jiji na kuujenga mnara wake hapo, Nimrodi alianzisha dini nyingine. Maandishi ya Biblia huonyesha kwamba kisha mvurugo wa lugha huko Babeli, wajenzi wa mnara ambao hawakufanikiwa walisambaa na kufanyiza mianzo mipya, wakichukua pamoja nao dini yao. (Mwanzo 10:6-10; 11:4-9) Hivyo mafundisho ya kidini ya Kibabuloni yalisambaa juu ya uso wa dunia.

      13 Kulingana na mapokeo, Nimrodi alikufa kifo chenye jeuri. Kisha kifo chake Wababuloni kwa sababu zenye kusikika wangelikuwa na mwelekeo wa kumheshimu sana kama mwanzilishi, mjenzi na mfalme wa kwanza wa jiji lao. Kwa kuwa mungu Marduku (Merodak) alifikiriwa kuwa mwanzilishi wa Babuloni, wasomi wengine wamependekeza kwamba Marduku awakilisha Nimrodi aliyefanywa kuwa mungu. Ikiwa ni hivyo, basi lile wazo la kwamba mtu anayo nafsi ambayo huendelea kuishi baada ya kufa lilikubaliwa na wengi haikosi wakati wa kifo cha Nimrodi. Kwa vyovyote, kurasa zenye kuandikwa za historia hufunua kwamba kufuatia Garika, chanzo cha fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi kilikuwa ni Babuloni.

      14 Basi, namna gani fundisho hilo lilikuja kuwa la lazima sana katika dini nyingi za wakati wetu? Sehemu ifuatayo itachunguza kuingia kwa fundisho hili katika dini za Mashariki.

      [Maelezo ya Chini]

      a K.W.K. humaanisha “Kabla ya Wakati wa Kawaida.” W.K. huonyesha “Wakati wa Kawaida,” ambao mara nyingi huitwa A.D., kwa Anno Domini, ikimaanisha “katika mwaka wa Bwana wetu.”

      b El-Amarna ni uwanja wenye magofu wa mji Akhetaton wa Misri, unaodaiwa kuwa ulijengwa katika karne ya 14 K.W.K.

      c Tazama Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, kurusa 37-54, kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      [Picha katika ukurasa wa 6]

      Maoni ya Wamisri juu ya nafsi zilizo katika ulimwengu wa chini

      [Picha katika ukurasa wa 7]

      Socrates alijadili kwamba nafsi ni isiyokufa

  • Wazo Hilo Laingia Dini za Mashariki
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Wazo Hilo Laingia Dini za Mashariki

      “Sikuzote nilifikiri kwamba kutoweza kufa kwa nafsi ilikuwa kweli yenye kuenea pote ambayo kila mtu alikubali. Kwa hiyo hakika nilishangazwa kusikia kwamba watu fulani wenye akili sana wa Mashariki na Magharibi walijadiliana kwa nguvu juu ya imani hii. Sasa ninajiuliza namna gani wazo la kutoweza kufa lilikuja kuingia katika akili ya Wahindu.”—MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU ALIYELELEWA KATIKA IMANI YA WAHINDU.

      1. Kwa nini ujuzi juu ya kukua na kuchipuka kwa fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi ya mwanadamu katika dini mbalimbali ni wenye faida kwetu?

      NAMNA gani wazo la kwamba mtu anayo nafsi isiyoweza kufa liliingia katika dini ya Wahindu na zile dini nyingine za Mashariki? Ulizo hili ni lenye kupendeza hata kwa wale walio Magharibi ambao huenda hawafahamiani na dini hizi, kwa kuwa imani hiyo hubadili maoni ya kila mtu kuhusu wakati ujao. Kwa sababu fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi ya mwanadamu ni lilelile katika dini nyingi leo, kujua namna wazo hilo lilivyokua bila shaka kunaweza kufanyiza kuwe na mapatano na upashanaji habari bora.

      2. Kwa nini India imekuwa chanzo chenye kustahili kuangaliwa cha uvutano wa kidini katika Asia?

      2 Ninian Smart, profesa wa mafunzo ya kidini kwenye chuo kikuu cha Lancaster katika Uingereza asema: “Kitovu cha maana zaidi chenye uvutano wa kidini katika Asia kimekuwa ni India. Hili si tu kwa sababu India yenyewe imekuwa chanzo cha imani nyingi—Uhindu, dini ya Buddha, Jaini, Sikh, n.k. bali kwa sababu mojapo wa dini hizi, yaani dini ya Buddha, imekuja kuingiza uvutano wa maana sana katika utamaduni wa karibu Asia ya Magharibi yote.” Tamaduni nyingi zilizovutiwa katika njia hii “bado zaendelea kuitazama India kuwa makao yao ya kiroho,” asema mwanaelimu Mhindu, Nikhilananda. Basi, namna gani fundisho hili la kutoweza kufa kwa nafsi lilingia katika India na sehemu nyingine za Asia?

      Fundisho la Kihindu la Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine

      3. Kulingana na mwanahistoria mmoja, yawezekana wazo lile la uhamaji wa nafsi liliingizwa na nani katika India?

      3 Katika karne ya sita K.W.K., wakati Pythagoras na wafuasi wake katika Ugiriki walipokuwa wakitetea kisio la uhamaji wa nafsi, wanahekima Wahindu waliokuwa wakiishi kando ya kingo za mito India na Ganges katika India walikuwa wakikuza wazo ilihili. Kutokea kwa imani hii katika wakati uleule “katika ulimwengu wa Kigiriki na India hakungeweza kuwa kwa urahisi jambo la bahati tu,” asema mwanahistoria Arnold Toynbee. “Chanzo kilekile kimoja kinachowezekana [cha uvutano],” Toynbee atokeza, “ni jamii ya Waerasia wenye kuhamahama, ambao, katika karne za 8 na 7 K.W.K., walishuka India, Asia ya Kusini-Magharibi, inchi yenye nyika karibu na pwani la Bahari Nyeusi, na Balkani na peninsula za Anatolia.” Kabila za Waerasia wahamaji bila shaka zilichukua pamoja nao mpaka India lile wazo la uhamaji wa nafsi.

      4. Kwa nini wazo la uhamaji wa nafsi lilivutia Wahindu wenye hekima?

      4 Uhindu ulikuwa umeanza mapema sana katika India, karibu na mwaka wa 1500 K.W.K., Waariani walipofika. Kutoka mwanzoni sana, Uhindu ulishikilia imani ya kwamba nafsi ilikuwa tofauti na mwili na kwamba nafsi huokoka kifo. Kwa hiyo Wahindu walizoea ibada ya mababu na kuandalia chakula nafsi za wafu wao ili wale. Karne nyingi baadaye wakati wazo la uhamaji wa nafsi lilipofika India, lapaswa kuwa lilivuta wanahekima Wahindu waliopambana sana na matatizo yenye kuenea kuhusu uovu na mateso kati ya wanadamu. Kuchanganya fundisho hili na kile walichokiita sheria ya Karma, ile sheria inayosema kwamba kila jambo na sababu yake, wanahekima Wahindu walikuza kisio la fundisho la kuhama kwa nafsi ambalo kupitia kwalo kustahili ao kutostahili katika uhai wa mtu kunathawabishwa au kuadhibiwa katika uhai wa baadaye.

      5. Kulingana na Dini ya Kihindu, mradi wa upeo wa nafsi ni nini?

      5 Lakini kulikuwa wazo lingine lililovutia fundisho la Kihindu kuhusu nafsi. “Inaonekana kuwa kweli kwamba wakati uleule ambapo kisio la uhamaji wa nafsi na karma liliundwa, au hata mapema zaidi,” yasema Encyclopædia of Religion and Ethics, “wazo lingine . . . lilikuwa likikomaa katika kikundi kidogo cha wenye akili katika India ya Kaskazini—wazo la kifalsafa la Brahman-Ātman [Brahman mkuu zaidi na wa milele, Nafsi ya upeo].” Wazo hili lilichanganywa na kisio la kuzaliwa upya katika mwili mwingine ili kufasiria mradi wa mwisho wa Wahindu—kukombolewa kutoka mzunguko unaojirudia wa uhamaji wa nafsi katika kusudi la kuwa mtu afikiaye mwisho halisi. Imani hii ya Kihindu inafikiwa kwa kufanya jitihada kutokana na mwenendo wa kijamii wenye kukubaliwa na ujuzi wa kipekee wa Kihindu.

      6, 7. Ni nini iliyo imani ya Dini ya Kihindu ya kisasa kuhusu uhai baada ya kifo?

      6 Hivyo wanaume wenye hekima walifanyiza wazo la uhamaji wa nafsi kuwa fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine kwa kulichanganya na ile sheria ya Karma na wazo la Brahman. Octavio Paz, mwanashairi aliyepata Tuzo la Nobel na balozi Mmeksiko wa kale katika India aandika: “Kadiri Uhindu ulivyotawanyika, ndivyo ilivyokuwa na wazo moja . . . lililo kiini kwa dini ya Kibrahmani, Kibuddha, na dini nyingine za Asia: nafsi kutoka mwili wakati wa kifo na kuingia mwili mwingine kupitia uhai wenye kufaulu.”

      7 Fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine ndiyo nguzo ya Uhindu wa siku za leo. Mwanafalsafa Mhindu Nikhilananda asema: “Kupata kutoweza kufa si pendeleo la hesabu ya wachaguliwa wachache pekee, bali ni haki ya urithi ya kila mtu, ni sadikisho la kila Mhindu mwema.”

      Mrudio wa Kuzaliwa Upya Katika Dini ya Buddha

      8-10. (a) Dini ya Buddha inafasiriaje uhai? (b) Msomi wa Dini ya Buddha alifasiriaje fundisho la kuzaliwa tena?

      8 Dini ya Buddha ilianzishwa katika India karibu na mwaka 500 K.W.K. Kulingana na pokeo la Kibuddha, mwana-mfalme Mhindi mwenye jina la Siddhārtha Gautama, aliyekuja kujulikana baadaye kwa jina la Buddha baada ya kupata mnurisho, alianzisha Dini ya Buddha. Kwa kuwa inachipuka kutokana na Uhindu, mafundisho yayo yanafanana katika njia fulani na yale ya Uhindu. Kulingana na Dini ya Buddha, maisha ni kuendelea kwa mzunguko unaojirudia wa kuzaliwa upya na kifo, na kama vile katika Uhindu, hali ya kila mtu katika maisha yake ya sasa inaamuliwa na matendo ya maisha yake yaliyotangulia.

      9 Lakini Dini ya Buddha haifasirie uhai katika maneno ya nafsi yenye utu ambayo huokoka kifo. Arnold Toynbee alisema: “[Buddha] aliona katika nafsi ya mwanadamu mifuatano yenye kupita upesi ya hali za kiroho, ambayo huunganishwa pamoja kwa tamaa tu.” Ijapokuwa hivyo, Buddha aliamini kwamba kitu fulani—hali fulani au kani—inaendelea kupita kutoka uhai moja hadi mwingine. Dr. Walpola Rahula, msomi Mbuddha afasiria:

      10 “Mtu si kitu ila mchanganyiko wa kani na nishati za kimwili na kiakili. Kile tunachokiita kifo ni kutotenda kwa ujumla kwa mwili wenye nyama. Je! kani na nishati hizo zote hukoma kabisa mwili uachapo kutenda? Dini ya Buddha husema ‘La.’ Kupenda, uchaguzi, tamaa, kiu cha kuishi, kuendelea, kupata kuzaliwa upya tena na tena, ni kani ya ajabu inayosukuma uhai wote, maisha zote, inayosukuma hata ulimwengu mzima. Hiyo ndiyo kani kubwa zaidi, nishati kubwa zaidi kuliko zote katika ulimwengu. Kulingana na Dini ya Buddha, kani hii haikomi mwili unapoacha kutenda, yaani kifo; bali huendelea kujidhihirisha yenyewe katika umbo lingine, ikitokeza maisha mengine yanayoitwa kuzaliwa tena.”

      11. Maoni ya Wabuddha ni gani kuhusu uhai baada ya kifo?

      11 Maoni ya Wabuddha juu ya uhai baada ya kifo ni haya: Kuishi kwa kudumu milele isipokuwa mtu afikie lengo la mwisho la Nirvana, kukombolewa kutoka mzunguko unaojirudia wa kuzaliwa mara ya pili. Nirvana ni hali isiyo wala ya baraka ya milele wala ya mtu kuwa na nafsi ya upeo. Ni hali tu ya kutokuwako kwa mtu—“mahali pasipo na kifo” kupita kuwako kwa mtu. Webster’s Ninth New Collegiate Dictionary hufasiria “Nirvana” kuwa “mahali au hali ya kutokumbuka juto, teso, au uhalisi wa nje ya mtu.” Badala ya kutafuta kutoweza kufa, Wabuddha wanatiwa moyo kupita kutoweza kufa na kufikia Nirvana.

      12-14. Namna gani vikundi mbalimbali vya dini ya Buddha hufasiria wazo la kutoweza kufa kwa nafsi?

      12 Kadiri Dini ya Buddha ilivyosambaa mahali mbalimbali katika Asia, ilibadilisha mafundisho yayo kuyaambatanisha na imani za mahali. Kwa mfano, aina ya Dini ya Kibuddha iitwayo Mahayana ambayo inatawala katika China na Japani yashikilia imani ya mabodhisattva (Mabuddha walionurishwa) wa kimbinguni, au Mabuddha wa wakati ujao. Bodhisattva huahirisha kuingia Nirvana yao na kupata maisha mengi katika kusudi la kutumikia wengine na kuwasaidia wafikie Nirvana. Hivyo mtu aweza kuchagua kuendelea katika mzunguko unaojirudia wa kuzaliwa upya hata baada ya kufikia Nirvana.

      13 Badiliko lingine ambalo lilikuwa lenye uvutano wa pekee katika China na Japan ni fundisho la Bara Lenye Utakato la Magharibi, lililoumbwa na Buddha Amitabha, au Amida. Wale wanaoliitia jina la Buddha katika imani wazaliwa tena katika Bara Lenye Utakato, au Paradiso, mahali ambapo hali zafaa zaidi ili kufikia mnurisho wa mwisho. Ni jambo gani lilikomazwa kutokana na fundisho hilo? Profesa Smart, aliyetajwa mapema, afasiria: “Kama ilivyotazamiwa, fahari za paradiso, zilizosimuliwa kwa udhahiri katika maandishi fulani ya Mahayana, zilikuja kuchukua mahali pa nirvana katika mawazo ya watu wengi kama lengo lenye upeo mkubwa.”

      14 Dini ya Buddha ya Tibet yaingiza imani nyingine ya mahali. Kwa mfano, kitabu cha wafu cha Tibet chasimulia ajali ya mtu katika hali ya kati kabla ya kuzaliwa tena. Yasemekana kwamba wafu huwekwa kwenye nuru nyangavu ya nafsi ya upeo, na wale wote wasioweza kuvumilia nuru hiyo hawapati ukombozi bali wanazaliwa tena. Bila shaka, Dini ya Buddha katika aina mbalimali yatoa wazo la kutoweza kufa.

      Ibada ya Mababu Waliokufa Katika Shinto ya Japan

      15-17. (a) Namna gani ibada ya roho za mababu waliokufa ilikomaa katika Dini ya Shinto? (b) Namna gani imani ya kutoweza kufa kwa nafsi ni fundisho la msingi katika Dini ya Shinto?

      15 Dini iliyokuwako katika Japan kabla ya kufika kwa Ubuddha katika karne ya Sita W.K. ilikuwa ni dini isiyo na jina, na ilifanyizwa na imani zilizoshirikishwa na adili na desturi za watu. Walakini, pamoja na kuingizwa kwa Ubuddha, uhitaji uliamshwa ili kutofautisha dini ya Kijapani na ile ya kigeni. Ndivyo dini ya “Shinto,” maana yake “njia ya vijimungu,” ilivyotokea.

      16 Ni imani gani dini ya Shinto ya asili iliyoshikilia kuhusu maisha baada ya kifo? Ukulima wa mchele kwenye ardhi yenye maji ulipofika, ‘kilimo cha udongo wa majimaji kilitaka jumuiya zilizopangwa vizuri na zenye kuimarika kitengenezo,’ chaeleza Kodansha Encyclopedia of Japan, ‘na sherehe za kilimo—ambazo baadaye zilitimiza fungu la maana sana katika dini ya Shinto—zilisitawishwa.’ Woga wa nafsi zilizoondoka uliongoza watu hawa wa kale kutunga sherehe za ibada za kuzituliza. Hilo likatokeza ibada ya roho za mababu wa kale waliokufa.

      17 Kulingana na imani ya dini ya Shinto, nafsi “iliyoondoka” bado ina utu wayo lakini hutiwa uchafu kwa sababu ya kifo. Waliofiwa wanapofanya sherehe za ukumbusho, nafsi inatakaswa kufikia kiwango cha kuondolewa uovu wote, na kutwaa tabia ya amani na ya wema. Baada ya muda, roho hiyo ya babu aliyekufa hupanda ngazi ya kuwa kiabudiwa, au mlinzi. Kwa kuwako pamoja na dini ya Buddha, dini ya Shinto iliingiza mafundisho fulani ya Wabuddha, kutia ndani fundisho la paradiso. Hivyo, tunaona kwamba imani ya kutoweza kufa kwa nafsi ni fundisho la msingi kwa dini ya Shinto.

      Kutoweza Kufa kwa Nafsi Katika Dini ya Tao, Ibada ya Roho za Mababu Katika Dini ya Confucius

      18. Dini ya Tao inalo wazo gani kuhusu kutoweza kufa kwa nafsi?

      18 Dini ya Tao ilianzishwa na Lao-tzu, asemekanaye kuwa aliishi katika karne ya Sita K.W.K. katika China. Kulingana na dini ya Tao, kusudi katika maisha ni kupatanisha utendaji wa mtu na Tao—njia ya maumbile. Wazo la Dini ya Tao kuhusu kutoweza kufa kwa nafsi laweza kujumlishwa kama ifuatavyo: Tao ndiyo kanuni inayoongoza ya ulimwengu wote. Tao hana mwanzo wala mwisho. Kwa kuishi kulingana na Tao, mtu huishiriki na huwa wa milele.

      19-21. Kukisia-kisia kwa Wafuasi wa Dini ya Tao kumeongoza kwenye jitihada gani?

      19 Katika kujaribu kwao kufanya umoja na maumbile, Wafuasi wa Dini ya Tao kwa muda wakawa wenye kupendezwa hasa na uwezo wa mwili wa kutozeeka na uwezo wa kujiponya. Walikisia-kisia kwamba labda kwa kuishi kwa kupatana na Tao, au njia ya asili, mtu aweza kwa njia fulani kujua siri za asili na apate kingo kutokana na hasara ya kimwili, magonjwa, na hata kifo.

      20 Wafuasi wa Dini ya Tao walianza kufanya jaribio la kutafakari, mazoezi ya kupumua, na kula vyakula fulani tu, mambo yaliyofikiriwa yangeweza kuahirisha kuchakaa kwa mwili na kifo. Upesi hadithi za kimapokeo zikaanza kusambaa kuhusu watu wasioweza kufa ambao wangeweza kuruka kwenye mawingu na kutokea na kutoweka wapendapo na ambao waliishi juu ya milima mitakatifu au visiwa vya mbali kwa miaka isiyohesabika, wakila umande au matunda ya kimiujiza. Historia ya China huripoti kwamba katika 219 K.W.K., maliki Ch’in Shih Huang Ti aliongoza msafara wa meli mkiwamo vijana wanaume na wanawake 3,000 wakatafute kisiwa cha kihadisi cha P’eng-lai, kilichokuwa makao ya wasioweza kufa, ili wakalete dawa ya mti-shamba ya hali ya kutoweza kufa. Kwa wazi, hawakurudi na dawa hiyo ya kurefusha maisha.

      21 Utafutaji wa uzima wa milele uliongoza Wafuasi wa Dini ya Tao kujaribu mchanganyo wa vidonge vya dawa ya kutoweza kufa kupitia alkemia. Kwa maoni ya Dini ya Tao, uhai watokea wakati zile kani zenye kupingana za yin na yang (kike na kiume) zinapoungana. Kwa hiyo, kwa kuunganisha risasi (aina ya madini ya rangi nyeusi, au yin) na zebaki (mercure yenye kung’aa, au yang), wataalamu hao wa alkemia walikuwa wakiiga utaratibu wa asili, na walifikiri kwamba dawa hiyo ingelitokeza kidonge cha kupatia hali ya kutoweza kufa.

      22. Matokeo yalikuwa nini kutokana na uvutano wa Dini ya Buddha juu ya maisha ya kidini ya watu wa China?

      22 Kufikia karne ya saba W.K., Dini ya Buddha ilikuwa ikijipenyeza katika maisha ya kidini ya watu wa China. Matokeo yakawa ni muchanganyiko wa sehemu za Dini ya Buddha, uasiliano-roho, na ibada ya mababu waliokufa. Profesa Smart asema: “Dini ya Buddha na Dini ya Tao, zilitolea umbo na msingi wa imani kuhusu uhai baada ya kifo, mafundisho yaliyokuwa ya msingi katika ibada ya kale ya mababu waliokufa katika China.”

      23. Msimamo wa Confucius ulikuwa nini kuhusiana na ibada ya mababu waliokufa?

      23 Confucius, Mchina mwenye hekima ajulikanaye sana wa karne ya sita K.W.K., ambaye falsafa yake ilikuja kuwa msingi wa Dini ya Confucius, hakutoa maelezo marefu juu ya uhai baada ya kifo. Badala yake, alitilia mkazo ulazima wa wema wa kiadili na tabia zenye kukubalika kijamii. Lakini alikuwa na mwelekeo wenye kufaa kuelekea ibada ya mababu waliokufa na alitia mkazo sana juu ya ufuatiaji wa desturi na sherehe zinazohusiana na roho za mababu wa kale waliokufa.

      Dini Zingine za Mashariki

      24. Dini ya Jaini yafundisha nini kuhusu nafsi?

      24 Dini ya Jaini ilianzishwa katika India katika karne ya sita K.W.K. Mahāvīra, mwanzishi wayo, alifundisha kwamba vitu vyote vyenye uhai vinayo nafsi ya milele na kwamba wokovu wa nafsi kutoka kifungo cha Karma waweza kupatikana tu kupitia kujikana mno na kujitia adabu na kufuatia sana kutofanyia viumbe vyote jeuri. Mpaka leo wafuasi wa Dini ya Jaini hushikilia imani hizi.

      25, 26. Imani gani za Dini ya Kihindu zapatikana pia katika Dini ya Sikh?

      25 India pia ndipo palipozaliwa Dini ya Sikh, inayofuatwa na watu milioni 19. Dini hii ilianza katika karne ya 16 wakati Guru Nānak alipoamua kuchanganya mafundisho yaliyo bora ya Dini ya Kihindu na Uislamu na kufanya dini yenye muungano. Dini ya Sikh ilichukua imani za Kihindu za nafsi isiyoweza kufa, kuzaliwa upya katika mwili mwingine, na Karma.

      26 Bila shaka, imani ya kwamba uhai huendelea baada ya mwili kufa ni sehemu ya maana ya nyingi za dini za Mashariki. Ingawaje, vipi Dini ya Jumuiya ya Wakristo, Dini ya Kiyahudi, na Uislamu?

      [Ramani katika ukurasa wa 10]

      (Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa.)

      ASIA YA KATI

      KASHMIR

      TIBETI

      CHINA

      KOREA

      JAPAN

      Banaras

      INDIA

      Buddh Gaya

      MYANMAR

      THAILAND

      SRI LANKA

      KAMBODIA

      JAVA

      KARNE YA 3 K.W.K.

      KARNE YA 1 K.W.K.

      KARNE YA 1 W.K.

      KARNE YA 4 W.K.

      KARNE YA 6 W.K.

      KARNE YA 7 W.K.

      Dini ya Buddha ilikuwa na uvutano juu ya dini zote za Asia ya Mashariki

      [Picha katika ukurasa wa 9]

      Kuzaliwa upya katika mwili mwingine ndio nguzo ya Uhindu

      [Picha katika ukurasa wa 11]

      Kwa kuishi kwa kupatana na maumbile, Mfuasi wa dini ya Tao hujaribu kuwa wa milele

      [Picha katika ukurasa wa 12]

      Confucius alikuwa na maoni yafaayo juu ya ibada ya mababu waliokufa

  • Wazo Hilo Laingia Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo, na Uislamu
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Wazo Hilo Laingia Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo, na Uislamu

      “Kati ya mambo mengine, dini pia ni njia inayopatanisha watu kutokana na jambo la kwamba siku fulani wanapaswa kufa, ama kwa ahadi ya uzima bora upande ule mwingine wa kaburi, kuzaliwa upya, ama yote mawili.”—GERHARD HERM, MBUNI-VITABU MJERUMANI.

      1. Juu ya imani gani ya msingi dini nyingi hutegemeza ahadi yazo ya uhai baada ya kifo?

      KATIKA kutoa ahadi ya uhai baada ya kufa, kila dini yategemea imani ya kwamba mwanadamu anayo nafsi isiyoweza kufa na ambayo wakati wa kifo husafiri hadi kwenye makao mengine au huhamia katika kiumbe kingine. Kama ilivyoonyeshwa katika sehemu iliyotangulia, imani katika kutoweza kufa kwa nafsi ya kibinadamu imekuwa sehemu ya maana ya dini za Mashariki tangu mianzo yazo. Lakini, namna gani Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo na Uislamu? Namna gani lile fundisho lilikuja kuwa la maana kwa imani hizi?

      Dini ya Kiyahudi Yameza Mawazo ya Kigiriki

      2, 3. Kupatana na Encyclopaedia Judaica, je! maandishi matakatifu ya Kiebrania yalifundisha kutoweza kufa kwa nafsi?

      2 Mizizi ya Dini ya Kiyahudi hurudi nyuma hadi Abrahamu, karibu miaka 4,000 iliyopita. Maandishi matakatifu ya Kiebrania yalianza kuandikwa katika karne ya 16 K.W.K., na yalikamilishwa wakati Socrates na Plato walipounda kisio la kutoweza kufa kwa nafsi. Je! Maandiko hayo yalifundisha kutoweza kufa kwa nafsi?

      3 Encyclopaedia Judaica yajibu: “Ni katika kipindi cha baadaye cha kibiblia tu kwamba imani iliyo wazi na thabiti katika kutoweza kufa kwa nafsi ilishikiliwa imara . . . na ikaja kuwa mojawapo wa mawe ya pembeni ya imani za Dini ya Kiyahudi na Kikristo.” Hiyo hueleza pia: “Katika kipindi cha kibiblia mtu alionwa kuwa jumla. Hivyo nafsi haikutenganishwa na mwili waziwazi.” Wayahudi wa mapema waliamini katika ufufuo wa wafu, na jambo hilo “ni la kutenganisha na imani katika . . . kule kutoweza kufa kwa nafsi,” yaonyesha wazi hiyo encyclopedia.

      4-6. Namna gani fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi lilikuja kuwa “mojawapo wa mawe ya pembeni” ya Dini ya Kiyahudi?

      4 Hivyo basi, namna gani ile imani ilikuja kuwa “mojawapo wa mawe ya pembeni” ya Dini ya Kiyahudi? Historia inatoa jibu. Katika 332 K.W.K., Aleksanda Mkuu alishinda sehemu kubwa ya Mashariki ya Kati kwa kasi kama ya umeme. Alipofika Yerusalemu, Wayahudi walimkaribisha kwa shauku. Kulingana na mwanahistoria Myahudi wa karne ya kwanza Flavio Yosefo, wao walimwonyesha hata unabii kutoka kitabu cha Danieli, ulioandikwa mapema zaidi ya miaka 200, ambao ulieleza waziwazi ushindi mbalimbali wa Aleksanda akiwa “mfalme wa Ugiriki.” (Danieli 8:5-8, 21) Waliochukua mahali pa Aleksanda waliendeleza mpango wake wa kufanya mambo Kiyunani, kujaza sehemu zote za milki kwa lugha, utamaduni, na falsafa vya Kigiriki. Mchanganyiko wa zile tamadumi mbili—ya Kigiriki na ya Kiyahudi—ulikuwa usioepukika.

      5 Mapema katika karne ya tatu K.W.K., tafsiri ya kwanza ya Maandiko ya Kiebrania katika Kigiriki, iliyoitwa La Septante ilikuwa imeanzishwa. Kupitia kwayo watu wengi wa mataifa wakaja kuwa na heshima na maarifa ya Dini ya Kiyahudi, wengine wakawa hata waongofu. Kwa upande mwingine, Wayahudi wakawa wenye kufahamiana na wazo la Kigiriki, na wengine wakawa wanafalsafa, jambo la kigeni kabisa kwao. Philo wa Aleksandria, wa karne ya kwanza W.K., alikuwa mwanafalsafa Myahudi wa namna hiyo.

      6 Philo alimheshimu Plato na alijitahidi kueleza Dini ya Kiyahudi katika misemo ya falsafa ya Kigiriki. “Kwa kufanya falsafa ya Plato na pokeo la kibiblia kuwa kitu kimoja,” chasema kitabu Heaven—A History, “Philo alitayarisha njia kwa wenye kufikiri wa Ukristo [kama vile Wayahudi] wa baadaye.” Nayo imani ya Philo kuhusu nafsi ilikuwa nini? Kitabu kinaendelea kueleza: “Kwa maoni yake, kifo kinarudisha nafsi kwenye hali yayo ya asili, hali ya kabla ya kuzaliwa. Kwa kuwa nafsi ni ya ulimwengu wa kiroho, uhai katika mwili huwa wa muda mfupi, mara nyingi ukiwa wenye taabu,” jambo moja katika mfululizo wa mambo mengine. Wayahudi wengine wenye kufikiri walioamini katika kutoweza kufa kwa nafsi ni kutia ndani Isaac Israeli, mfikizikia Myahudi mwenye kujulikana sana wa karne ya 10, na pia Moses Mendelssohn, mwanafalsafa Myahudi wa Ujerumani wa karne ya 18.

      7, 8. (a) Namna gani Talmud inafafanua nafsi? (b) Baadaye vitabu vya kifumbo vimesema nini kuhusu nafsi?

      7 Kitabu ambacho kilivutia sana pia wazo la Kiyahudi na uhai ni Talmud—inayoitwa muhtasari ulioandikwa wa sheria ya mdomo, pamoja na maelezo na mafasirio ya baadaye ya ile sheria, iliyokusanywa na marabi tokea karne ya pili W.K. katika Enzi za Kati. “Marabi wa Talmud,” yasema Encyclopaedia Judaica, “waliamini katika kuendelea kuishi kwa nafsi baada ya kifo.” Talmud inasema hata kuhusu wafu wakiathiri walio hai. “Huenda kwa habari ya uvutano wa wazo la Plato,” yasema Encyclopædia of Religion and Ethics, “[marabi] waliamini katika kuwako kwa nafsi kabla ya kuishi.”

      8 Baadaye kitabu cha kifumbo cha Kiyahudi, yaani Cabala, chaenda hata mbali hadi kufundisha fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Kuhusu imani hii, The New Standard Jewish Encyclopedia inaeleza: “Wazo laonekana kuwa limetokea India. . . . Katika Kabbalah, kuonekana kwalo mara ya kwanza ni katika kitabu Bahir, na ndipo, tokea Zohar na kuendelea, lilikubaliwa kwa kawaida na watu wenye kutafakari, likifanyiza sehemu ya maana katika imani na vitabu vya uhasidimu.” Katika Israeli leo, fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine linakubalika sana kuwa fundisho la Kiyahudi.

      9. Ni nini msimamo wa vikundi vingi vya Dini ya Kiyahudi vya leo kuhusu kutoweza kufa kwa nafsi?

      9 Kwa hiyo, wazo la kutoweza kufa kwa nafsi likaingia Dini ya Kiyahudi kupitia uvutano wa falsafa ya Kigiriki, na wazo hilo lakubaliwa leo na vikundi vingi vya dini hiyo. Isemweje kuhusu kuingia kwa fundisho hilo katika Jumuiya ya Wakristo?

      Jumuiya ya Wakristo Yakubali Mawazo ya Plato

      10. Msomi Mhispania mwenye kujulikana sana alikata kauli gani kuhusu imani ya Yesu katika kutoweza kufa kwa nafsi?

      10 Ukristo wa kweli ulianza na Kristo Yesu. Kuhusu Yesu, Miguel de Unamuno, msomi Mhispania mwenye kujulikana sana wa karne ya 20 aliandika: “Badala yake yeye aliamini ufufuo wa mnofu, kulingana na namna ya Kiyahudi, si katika kutoweza kufa kwa nafsi, kulingana na namna ya Kiplato [ya Kigiriki]. . . . Vithibitisho vya hilo vyaweza kuonwa katika kitabu chochote chenye haki ya kufasiri.” Yeye alikata maneno hivi: “Kutoweza kufa kwa nafsi . . . ni fundisho la kifalsafa la kipagani.”

      11. Wakati gani falsafa ya Kigiriki ilianza kupenya katika Ukristo?

      11 Wakati gani na namna gani hili “fundisho la kifalsafa la kipagani” lilipenya katika Ukristo? The New Encyclopædia Britannica inatokeza wazi: “Tokea katikati ya karne ya 2 W.K., Wakristo ambao walikuwa wamepata mazoezi fulani katika falsafa ya Kigiriki walianza kuhisi ulazima wa kuelezea imani yao katika misemo ya falsafa ya Kigiriki, ili kutosheleza tamaa yao ya kiakili na katika kusudi la kubadili wapagani walioelimishwa. Falsafa iliyowafaa zaidi ilikuwa ni lile wazo la Plato.”

      12-14. Origen na Augustino walitimiza fungu gani katika kuchanganya falsafa ya Plato na Ukristo?

      12 Wanafalsafa wawili wa mapema kama hao walifanyiza uvutano mkubwa sana juu ya mafundisho ya Jumuiya ya Wakristo. Mmoja alikuwa ni Origen wa Aleksandria (185-254 W.K.), na mwingine ni Augustino wa Hippo (354-430 W.K.). Kuwahusu, New Catholic Encyclopedia inasema: “Pamoja na Origen tu katika Mashariki na Mt. Augustino katika Magharibi nafsi ilithibitishwa kuwa kitu cha kiroho na wazo la kifalsafa lililofanyizwa kutoka asili yake.” Origen na Augustino waliunda mawazo yao kuhusu nafsi juu ya msingi gani?

      13 Origen alikuwa mwanafunzi wa Clement wa Aleksandria aliyekuwa “wa kwanza wa Mababa kupokea kwa wazi kutokana na pokeo la Kigiriki kuhusu nafsi,” yasema New Catholic Encyclopedia. Mawazo ya Plato kuhusu nafsi yanapaswa kuwa yalimvutia sana Origen. “[Origen] alijenga katika fundisho la Ukristo namna yenye kupanuka ya mafundisho kuhusu nafsi, ambayo alichukua kutoka kwa Plato,” akaandika mwanateolojia Werner Jaeger katika The Harvard Theological Review.

      14 Augustino huonwa na wengi katika Jumuiya ya Wakristo kuwa mfikiri mkubwa wa zamani. Kabla ya kuongoka kuwa “Mkristo” akiwa na umri wa miaka 33, Augustino alikuwa na upendezi mkubwa katika falsafa na alikuja kuwa mfuasi wa mawazo mapya ya Plato.a Hata baada ya kuongoka kwake, alibaki na mawazo mapya ya Plato katika fikira zake. “Akili yake ilikuwa mahali ambapo dini ya Agano Jipya ilikuwa kabisa kabisa yenye kuchanganyika na pokeo la Plato la falsafa ya Kigiriki,” yasema The New Encyclopædia Britannica. New Catholic Encyclopedia yakubali kwamba ‘fundisho la Augustino [kuhusu nafsi], ambalo limekuwa kawaida katika Mashariki kufikia karne ya 12 baadaye, lilitokana na mawazo mapya ya Plato.’

      15, 16. Je! upendezi katika mafundisho ya Aristote katika karne ya 13 ulibadili msimamo wa kanisa kuhusu fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi?

      15 Katika karne ya 13, mafundisho ya Aristote yalikuwa yakipata ushindi katika kupendeza watu wengi katika Ulaya, zaidi kwa sababu ya kupatikana katika Kilatini kwa kazi za wasomi wa Kiarabu, ambao walikuwa wametoa maelezo kwa wingi kuhusu maandishi ya Aristote. Msomi Mkatoliki aitwaye Thomas Aquinas aliingiwa sana na wazo la Aristote. Kwa sababu ya maandishi ya Aquinas, maoni ya Aristote yalikuwa na uvutano mwingi zaidi juu ya mafundisho ya kanisa kushinda yale ya Plato. Hata hivyo, mwelekeo huu, haukuathiri fundisho kuhusu kutoweza kufa kwa nafsi.

      16 Aristote alifundisha kwamba nafsi iliunganishwa kwa namna isivyoweza kutenganishwa na mwili na haiendelei kuishi kipekee baada ya kifo na kwamba ikiwa kitu fulani cha umilele huishi katika mtu, kilikuwa kitu cha kuwazika tu, akili isiyo na utu. Namna hiyo ya kuona nafsi haikuwa yenye upatano na imani ya kanisa kuhusu nafsi zenye utu zinazookoka kifo. Kwa hiyo, Aquinas alibadili maoni ya Aristote kuhusu nafsi, akidai kwamba kutoweza kufa kwa nafsi kunaweza kuthibitishwa kwa kutoa sababu. Hivyo, imani ya kanisa katika kutoweza kufa kwa nafsi ikabaki isiyotikisika.

      17, 18. (a) Je! Mapinduzi Makubwa ya kidini ya karne ya 16 yaliingiza mapinduzi katika fundisho kuhusu nafsi? (b)  Ni nini msimamo wa madhehebu mengi ya Jumuiya ya Wakristo kuhusu kutoweza kufa kwa nafsi?

      17 Mnamo karne ya 14 na 15, sehemu ya mapema ya Mfufuko wa harakati, kulikuwa na uamsho mpya wa kupendezwa na Plato. Jamii yenye sifa ya Medici katika Italia hata ikasaidia kuanzisha chuo kikuu katika Florence ili kuendeleza funzo la falsafa ya Plato. Mnamo karne ya 16 na 17, kupendezwa katika Aristote kukafifia. Na Mapinduzi Makubwa ya kidini ya karne ya 16 hayakuingiza mapinduzi katika mafundisho kuhusu nafsi. Ingawa Wapinduzi wa Kiprotestenti walibishana kuhusu fundisho la pirigatori, walikubali wazo la mateso ya milele au kuthawabishwa milele.

      18 Hivyo fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi likapata nguvu katika madhehebu mengi ya Jumuiya ya Wakristo. Akifahamu hili, msomi mmoja Mwamerika aliandika: “Kwa kweli, dini, kwa watu wengi wa rangi yetu wenyewe, yamaanisha kutoweza kufa, na si jambo lingine. Mungu ndiye mtokezaji wa kutoweza kufa.”

      Kutoweza Kufa na Uislamu

      19. Uislamu ulianzishwa wakati gani, na ulianzishwa na nani?

      19 Uisalamu ulianza na kuitwa kwa Muḥammad kuwa nabii alipokuwa na umri wa karibu miaka 40. Kwa kawaida inaaminiwa na Waislamu kwamba ufunuo mbalimbali ulimjia kwa muda wa kipindi cha miaka kama 20 au 23, tokea karibu 610 W.K. mpaka kifo chake mnamo 632 W.K. Ufunuo huo mbalimbali ni wenye kunakiliwa katika Qurani, kitabu kitakatifu cha Kiislamu. Wakati Uislamu ulipokuja kuwapo, Dini ya Kiyahudi na Jumuiya ya Wakristo zilikuwa zimeingiwa na wazo la Plato juu ya nafsi.

      20, 21. Waislamu huamini nini kuhusu maisha ya baada ya kifo?

      20 Waislamu huamini kwamba imani yao ni upeo wa ufunuo mbalimbali uliotolewa kwa Waebrania na Wakristo waaminifu wa zamani. Qurani yataja Maandiko ya Kiebrania na ya Kigiriki. Lakini juu ya fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi, Qurani yaachana na maandishi haya. Qurani inafundisha kwamba mtu anayo nafsi ambayo huendelea kuishi baada ya kifo. Pia inasimulia juu ya ufufuo wa wafu, siku ya hukumu, na kile kinachotukia kwa nafsi mwishowe—ama uzima katika bustani ya paradiso ya kimbinguni au adhabu katika helo yenye kuunguza.

      21 Waislamu hushikilia kwamba nafsi ya mtu anayekufa huenda kwenye Barzakh, au “Kiambaza,” “mahali au hali ambayo watu watakuwamo baada ya kifo na kabla ya Hukumu.” (Sura 23:99, 100, Qurani Tukufu, kielezi-chini) Nafsi ina fahamu humo, ikipatwa na kinachoitwa “Kurudiwa kwa Kaburi” ikiwa mtu huyo alikuwa mwovu au akiona furaha ikiwa alikuwa mwaminifu. Lakini waaminifu pia lazima wapatwe na mateso fulani kwa sababu ya zambi zao chache walizotenda walipokuwa wangali hai. Siku ya hukumu, kila mtu hukabili tokeo lake la milele, ambalo hukomesha hali hiyo ya katikati.

      22. Wanafalsafa wa Kiarabu walitoa makisio gani tofauti kuhusu tokeo la nafsi?

      22 Wazo la kutoweza kufa kwa nafsi katika Dini ya Kiyahudi na katika Jumuiya ya Wakristo lilitokea kwa sababu ya uvutano wa mawazo ya Plato, lakini wazo hilo lilijengwa katika Uislamu tangu mwanzo wa dini hiyo. Hilo halimaanishi kwamba wasomi wa Kiarabu hawakujaribu kuchanganya mafundisho ya Kiislamu na falsafa ya Kigiriki. Kwa kweli, ulimwengu wa Kiarabu ulivutwa sana na kazi ya Aristote. Na wasomi wa Kiarabu wenye kujulikana, kama vile Avicenna na Averroës, walieleza na kujenga juu ya mawazo ya Aristote. Hata hivyo, katika majaribio yao ya kupatanisha mawazo ya Kigiriki na mafundisho ya Kiislamu kuhusu nafsi, walisitawisha makisio yenye kutofautiana. Kwa mfano, Avicenna alitangaza kwamba nafsi ya mtu ni isiyoweza kufa. Averroës, kwa upande mwingine, alibishana juu ya maoni hayo. Ingawa maoni hayo tofauti, fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi labaki imani ya Waislamu.

      23. Ni nini msimamo wa Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo na Uislamu kuhusu swala la kutoweza kufa kwa nafsi?

      23 Basi, ni wazi kwamba Dini ya Kiyahudi, Jumuiya ya Wakristo na Uislamu zote hufundisha fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi.

      [Maelezo ya Chini]

      a Mfuasi wa mawazo mapya ya Plato, tafsiri mpya ya falsafa ya Plato iliyositawishwa na Plotinus katika Roma ya karne ya tatu.

      [Picha katika ukurasa wa 14]

      Ushindi wa Aleksanda Mkuu uliongoza kwenye mchanganyiko wa tamaduni za Kigiriki na za Kiyahudi

      [Picha katika ukurasa wa 15]

      Origen, kwanza, na Augustino walijaribu kuchanganya falsafa ya Plato na Ukristo

      [Picha katika ukurasa wa 16]

      Avicenna, kwanza, alisema kwamba nafsi ya mtu ni isiyoweza kufa. Averroës alibishana dhidi ya maoni hayo

  • Mahali pa Kwenda Ili Kupata Majibu
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Mahali pa Kwenda Ili Kupata Majibu

      “Kisio la kuteswa milele halipatani na imani katika upendo wa Mungu kuelekea vitu vilivyoumbwa. . . . Kuamini katika adhabu ya milele ya nafsi kwa sababu ya makosa ya miaka michache, bila kuipatia hiyo nafasi ya kujikosoa, ni kwenda kinyume cha kanuni zenye akili nzuri.”—NIKHILANANDA, MWANAFALSAFA MHINDU.

      1, 2. Tufikiriapo imani mbalimbali kuhusu uhai baada ya kifo, ni maulizo gani hutokea?

      KAMA mwanafalsafa huyu Mhindu, watu wengi leo husumbuliwa na fundisho la mateso ya milele. Wengine, wakionyesha dalili ileile, wanayo magumu ya kusikia mawazo kama yale ya kufikia Nirvana ao kufanya umoja na Tao.

      2 Lakini, kwa sababu ya wazo la kwamba nafsi ni isiyoweza kufa, dini za Mashariki na Magharibi zimesitawisha mfululizo wenye kubadilika-badilika unaotia wasiwasi wa imani kuhusu uhai baada ya kufa. Je! inawezekana kujua kweli kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa? Je! kweli nafsi ni isiyoweza kufa? Tunaweza kwenda wapi ili kupata jibu?

      Sayansi na Falsafa

      3. Je! sayansi au njia za kisayansi za uchunguzi zatoa majibu kwa maulizo yanayohusu uhai baada ya kufa?

      3 Je! sayansi au njia za kisayansi za uchunguzi zatoa majibu kwa maulizo yanayohusiana na uhai baada ya kifo? Kwa msingi wa habari za karibuni kuhusu mkaribio-kifo au hisi za ‘nje ya mwili,’ watafiti fulani wamejaribu kusimulia kuhusu uhai baada ya kifo. Akirudilia upya baadhi ya madai yao katika hotuba yake “Kifo Kama Vile Kiingilio katika Nuru?,” mteolojia Mkatoliki Hans Küng alimalizia: “Hisi za aina hii hazionyeshi kitu chochote kuhusu uwezekano wa uhai baada ya kifo: hapa ni jambo la dakika tano za mwisho kabla ya kifo na si la uhai wa milele baada ya kifo.” Akaongeza: “Swala la uwezekano wa uhai baada ya kifo ni lenye umaana mkubwa kwa ajili ya uhai kabla ya kifo. Hilo lataka jibu ambalo laweza kutafutwa mahali pengine ikiwa haliwezi kutolewa na wataalamu wa kiganga.”

      4. Je! falsafa yaweza kutusaidia kupata majibu kutoka katika uwezekano mwingi unaotolewa na dini mbalimbali kuhusu uhai wa baadaye?

      4 Vipi kuhusu falsafa? Je! yaweza kutusaidia kupata majibu kutoka katika uwezekano mwingi unaotolewa na dini mbalimbali kuhusu uhai wa baadaye? Uvumbuzi wa kifalsafa hutia ndani “utendaji wa kukisiakisia,” asema Bertrand Russell, mwanafalsafa Muingereza wa karne ya 20. Kulingana na The World Book Encyclopedia, falsafa ni “aina ya utafiti—njia ya mchanganuo, upekuzi, fasirio, kisiokisio.” Kuhusu kichwa cha habari cha uhai baada ya kifo, makisiokisio ya kifalsafa yamebadilika kutoka kuita kutoweza kufa kuwa wazo tamanifu tu mpaka kutangaza hilo kuwa haki ya kuzaliwa ya kila mwanadamu.

      Chanzo Pekee cha Majibu

      5. Ni kipi kilicho kitabu cha zamani zaidi kilichopata kuandikwa?

      5 Hata hivyo, kuna kitabu ambacho ndani yake mnapatikana majibu ya kweli kwa maulizo ya maana kuhusu uhai na kifo. Hicho ndicho kitabu cha zamani zaidi kilichopata kuandikwa, sehemu zacho zikiwa zimeandikwa yapata miaka 3,500 iliyopita. Sehemu ya kwanza ya kitabu hiki iliandikwa karne chache kabla ya kutungwa kwa mashairi ya mapema zaidi ya Uhindu, yaani Veda, na karibu miaka elfu moja kabla ya Buddha, Mahāvīra, na Confucius kuishi duniani. Kitabu hiki kilikamilishwa katika 98 W.K., zaidi ya miaka 500 kabla ya Muḥammad kuanzisha Uislamu. Chanzo hiki cha pekee cha hekima ya juu ni Biblia.a

      6. Kwa nini twaweza kutazamia Biblia itueleze nafsi ni nini?

      6 Katika Biblia mna historia ya zamani iliyo sahihi zaidi sana kuliko kitabu kingine chochote kilichopo. Historia iliyorekodiwa katika Biblia yarudi nyuma mpaka kwenye mwanzo wa familia ya kibinadamu na inafasiria namna tulivyokuja kuwa hapa duniani. Hiyo huturudisha nyuma hadi kwenye wakati wa kabla wanadamu kuumbwa. Bila shaka kitabu kama hicho kinaweza kutupatia ufahamu wa kujua namna mtu alivyofanywa na nini iliyo nafsi.

      7, 8. Kwa nini twaweza kuiendea Biblia kwa matumaini ili kupata majibu ya kweli na yenye kutosheleza kuhusu kile kinachotufikia tunapokufa?

      7 Zaidi ya hilo, Biblia ni kitabu cha unabii ambao umekuwa na utimizo usiodanganyika. Kwa mfano, ilitabiri moja kwa moja kuinuka na kuanguka kwa milki za Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Maneno haya yalikuwa sahihi sana kiasi cha kwamba wapekuzi wamejaribu, lakini bila kufanikiwa, kuthibitisha kwamba yaliandikwa baada ya mambo hayo kutukia. (Danieli 8:1-7, 20-22) Unabii mwingine mbalimbali ulioandikwa katika Biblia unaendelea kutimizwa moja kwa moja katika wakati wetu.b—Mathayo, sura 24; Marko, sura 13; Luka, sura 21; 2 Timotheo 3:1-5, 13.

      8 Hakuna mwanadamu, hata awe mwenye akili kama nini, angeweza kutabiri kwa usahihi hivyo matukio ya wakati ujao. Mwenye uweza wote na Muumbaji mwenye hekima yote peke yake aweza kufanya hivyo. (2 Timotheo 3:16, 17; 2 Petro 1:20, 21) Hakika, Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu. Bila shaka, kitabu kama hicho kinaweza kututolea majibu ya kweli na yenye kutosheleza kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa. Kwanza, acheni tuone kile inachosema kuhusu nafsi.

      [Maelezo ya Chini]

      a Tazama broshua Kitabu Kwa Ajili ya Watu Wote, iliyotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      b Tazama Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      [Picha katika ukurasa wa 18]

      Kitabu cha zamani zaidi kilichopata kuandikwa

      [Picha katika ukurasa wa 18]

      Kitabu kinachotoa majibu yenye kutumainika na yenye kutosheleza

  • Nafsi Kulingana na Biblia
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Nafsi Kulingana na Biblia

      “Na mutu alikuwa nafsi ya uhai.”—MWANZO 2:7.

      1. Ni jambo gani tunalohitaji kuchunguza ili kuamua kile ambacho Biblia hufundisha juu ya nafsi?

      KAMA tulivyoona, imani kuhusu nafsi ni nyingi na zenye umbalimbali. Hata kati ya wale wanaojidai kutegemeza imani zao juu ya Biblia, kunayo mawazo tofauti kuhusu nafsi na jambo linaloipata wakati tunapokufa. Lakini, kwa kweli Biblia inafundisha nini kuhusu nafsi? Ili kupata jibu, tunahitaji kuchunguza maana ya maneno ya Kiebrania na ya Kigiriki ambayo hutafsiriwa “nafsi” katika Biblia.

      “Nafsi” Kama Kiumbe Hai

      2, 3. (a) Ni neno gani hutafsiriwa kuwa “nafsi” katika Maandiko ya Kiebrania, nayo maana ya msingi ya neno hili ni gani? (b) Namna gani Mwanzo 2:7 huhakikisha kwamba neno “nafsi” laweza kumaanisha mtu mzima?

      2 Neno la Kiebrania linalotafsiriwa kuwa “nafsi” ni neʹphesh, nalo laonekana mara 754 katika Maandiko ya Kiebrania (yaitwayo kwa kawaida Agano la Kale). Neʹphesh lamaanisha nini? Kulingana na The Dictionary of Bible and Religion, hilo “kwa kawaida huelekeza kwa kiumbe kizima chenye uhai, mtu mzima.”

      3 Kwa mfano, Mwanzo 2:7 hueleza: “BWANA [Yehova, NW] Mungu akafanya mutu wa mavumbi ya inchi, akapuliza pumuzi ya uzima ndani ya pua yake; na mutu alikuwa nafsi ya uhai.” Angalia kwamba Adamu hakupata nafsi; yeye alikuwa nafsi—kama vile mtu anayekuwa daktari ni daktari. Kwa hiyo, neno “nafsi” laweza kueleza mtu mzima.

      4, 5. (a) Toa mifano inayoonyesha kwamba neno “nafsi” huelekeza kwa mtu mzima. (b) Namna gani The Dictionary of Bible and Religion hutegemeza uelewevu wa kwamba mtu ni nafsi?

      4 Kuelewa huku kunategemezwa popote katika Maandiko ya Kiebrania, ambamo tunakuta misemwa kama vile “na mutu [nafsi, NW] ye yote akifanya zambi” (Walawi 5:1), “na mutu [nafsi, NW] ye yote anayefanya kazi ya namna yo yote” (Walawi 23:30), “mutu akionekana mwenye kuiba mumoja [nafsi, NW] wa ndugu zake” (Kumbukumbu la Torati 24:7), “roho [nafsi, NW] yake ikachokozwa hata kufa” (Waamuzi 16:16), “hata wakati gani mutatesa nafsi yangu?” (Yobu 19:2), na “nafsi yangu inayeyuka kwa uzito.”—Zaburi 119:28.

      5 Katika maandiko haya hakuna jambo lolote linaloonyesha kwamba nafsi ni kitu fulani chenye kivuli kinachoendelea kuishi baada ya kifo. Usemi wa kwamba ‘nafsi’ ya mpendwa imeondoka kwenda kuwa pamoja na Bwana au kusimulia juu ya ‘nafsi isiyoweza kufa,’ kungekuwa kusikoeleweka katika utamaduni wa AK [Agano la Kale],” yasema The Dictionary of Bible and Religion.

      6, 7. Ni neno gani hutafsiriwa kuwa “nafsi” katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, nayo maana ya msingi ya neno hili ni gani?

      6 Neno linalotafsiriwa kuwa “nafsi” zaidi ya mara mia moja katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (yaitwayo kwa kawaida Agano Jipya) ni psy·kheʹ. Kama vile neʹphesh, neno hili mara nyingi huelekeza kwa mtu mzima. Kwa mfano, fikiria misemwa inayofuata: “Nafsi yangu yataabika.” (Yohana 12:27) “Hofu ikaanza kuwa juu ya kila nafsi.” (Matendo 2:43) “Acheni kila nafsi iwe katika ujitiisho kwa mamlaka zilizo kubwa.” (Waroma 13:1) “Semeni kwa kuliwaza nafsi zilizoshuka moyo.” (1 Wathesalonike 5:14) “Watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.”—1 Petro 3:20.

      7 Psy·kheʹ, kama vile neʹphesh, kwa wazi yaelekeza kwa mtu mzima. Kulingana na msomi Nigel Turner, neno hili “lamaanisha kilicho cha namna ya kibinadamu, mwenyewe, mwili wenye nyama ukiwa na rûaḥ [roho] ya Mungu iliyopulizwa ndani yake. . . . Mkazo watiwa juu ya mtu mzima.”

      8. Je! wanyama ni nafsi? Fasiria.

      8 Katika Biblia neno “nafsi” latumiwa si tu juu ya wanadamu lakini pia juu ya wanyama. Kwa mfano, katika kuelezea uumbaji wa viumbe vya majini, Mwanzo 1:20 lasema kwamba Mungu aliamuru hivi: “Maji yajae kwa wingi na viumbe [nafsi, NW] vilivyo hai.” Na kwenye siku iliyofuata ya uumbaji, Mungu alisema: “Inchi itoe kila kiumbe [nafsi, NW] kilicho hai kwa namna yake, ngombe na mutambazi, na nyama ya inchi kwa namna yake.” (Mwanzo 1:24; linganisha na Hesabu 31:28.) Kwa hiyo, “nafsi” yaweza kuelekeza kwa kiumbe hai, iwe mwanadamu au mnyama.

      “Nafsi” Kama Uhai wa Kiumbe

      9. (a) Maana gani pana yaweza kutolewa kwa neno “nafsi”? (b) Je! hilo linapingana na wazo la kwamba nafsi ni mtu mwenyewe?

      9 Mara nyingine, neno “nafsi” huelekeza kwa maisha ambayo mtu au mnyama hufurahia. Jambo hilo halibadili ufasirio wa Biblia juu ya nafsi kuwa mtu au mnyama. Tutumie kielezi: Tunasema kwamba mtu fulani yuko hai, kumaanisha kwamba yeye ni mtu anayeishi. Tungeweza pia kusema kwamba yeye anao uhai. Katika njia ileile, mtu anayeishi ni nafsi. Lakini, wakati yeye ni hai, “nafsi” yaweza kusemwa kama vile kitu fulani ambacho yeye anacho.

      10. Toa mifano kuonyesha kwamba neno “nafsi” laweza kuelekeza kwa uhai ambao mtu au mnyama hufurahia.

      10 Kwa mfano, Mungu alimwambia Musa: “Watu wote waliotafuta uzima [nafsi, NW] wako wamekufa.” (Kutoka 4:19) Kwa kweli, maadui wa Musa walikuwa wakitafuta kuondoa uhai wake. Utumizi wenye kufanana na huo wa neno “nafsi” waonekana katika misemwa inayofuata: “Tuliogopa sana kwa uzima [nafsi, NW] wetu” (Yosua 9:24) “Wakakimbia wapate kujiponyesha nafsi zao.” (2 Wafalme 7:7) “Mwenye haki anafikili uzima [nafsi, NW] wa nyama yake.” (Mezali 12:10) “Mwana wa binadamu alikuja . . . kutoa nafsi yake kuwa fidia katika kubadilishana kwa ajili ya wengi.” (Mathayo 20:28) “Alikaribia sana kifo, akihatarisha nafsi yake.” (Wafilipi 2:30) Katika kila kisa, neno “nafsi” lamaanisha “uhai.”a

      11. Tuseme nini kuhusu matumizi ya Biblia ya neno “nafsi”?

      11 Basi, neno “nafsi” kama linavyotumiwa katika Biblia laelekeza kwa mtu au mnyama au uhai ambao mtu au mnyama hufurahia. Ufasirio wa Biblia juu ya nafsi, ni mwepesi, wenye kupatana, na usiosongwa na falsafa zenye kutatanisha na ushirikina mwingi wa watu. Lakini, jambo gani huifikia nafsi wakati wa kifo? Ili kujibu ulizo hilo, lazima kwanza tuelewe kwa nini tunakufa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Mathayo 10:28 pia hutumia neno “nafsi” kumaanisha “uhai.”

      [Picha katika ukurasa wa 20]

      Wote ni nafsi

  • Kwa Nini Tunakufa?
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Kwa Nini Tunakufa?

      “Juu ya vichwa vya milima ni kimya sasa, katika vichwa vya miti hausikii sauti hata kidogo; ndege wanalala katika miti: ngoja; karibuni kama hawa utapumzika.”—JOHANN WOLFGANG VON GOETHE, MSHAIRI MJERUMANI.

      1, 2. (a) Watu waliumbwa wakiwa na tamaa gani? (b) Watu wawili wa kwanza walifurahia maisha ya namna gani?

      MUNGU aliumba wanadamu wakiwa na tamaa ya kuishi milele. Kwa kweli, Biblia husema kwamba ameweka “milele vilevile ndani ya mioyo yao.” (Muhubiri 3:11) Lakini Mungu alifanya zaidi kuliko kuwapa tu wanadamu tamaa ya kuishi milele. Yeye pia aliwatolea uwezekano wa kuishi milele.

      2 Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, waliumbwa wakamilifu, bila kasoro akilini au mwilini. (Kumbukumbu 32:4) Fikiri—hakukuwa maumivu yenye kuendelea wala uchungu, hakukuwa hofu yenye kutisha wala mahangaiko! Zaidi tena, Mungu aliwaweka katika makao-paradiso yenye kupendeza. Mungu alikusudia kwamba mtu aweze kuishi milele na halafu dunia ingejaa na uzao wake mkamilifu. (Mwanzo 1:31; 2:15) Basi, kwa nini tunakufa?

      Kutotii Kwaleta Kifo

      3. Uzima wa milele wa Adamu na Hawa ulitegemea nini?

      3 Mungu alimuamuru Adamu hivi: “Wa kila muti wa shamba unaweza kula; lakini wa muti wa kujua uzuri na ubaya usile kwa maana siku unapokula, hakika utakufa.” (Mwanzo 2:16, 17) Kwa hiyo, uzima wa milele wa Adamu na Hawa ulitiliwa sharti; ulitegemea utii wao kwa Mungu.

      4. Adamu na Hawa walipofanya dhambi, kwa nini walipoteza tazamio la kuishi milele katika Paradiso?

      4 Lakini, kwa huzuni Adamu na Hawa hawakutii sheria ya Mungu. (Mwanzo 3:1-6) Kwa kufanya hivyo, wakawa wafanya dhambi, kwa kuwa “dhambi ni uasi-sheria.” (1 Yohana 3:4) Matokeo ni kwamba Adamu na Hawa hawakuwa tena kamwe na tazamio la uzima wa milele. Kwa nini? Kwa sababu “mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo.” (Waroma 6:23) Hivyo, alipotamka hukumu juu ya Adamu na Hawa, Mungu alisema: “Mavumbi wewe, na utarudi kwa mavumbi.” Ndipo wazazi wetu wa kwanza wakafukuzwa katika makao yao ya kiparadiso. Siku hiyo walipotenda dhambi, Adamu na Hawa wakaanza polepole lakini kwa uthabiti hatua ya kifo.—Mwanzo 3:19, 23, 24.

      “Kifo Kikasambaa kwa Watu Wote”

      5. Namna gani kifo kilisambaa kwa jamii yote ya kibinadamu?

      5 Sasa Adamu na Hawa wakawa na dhambi iliyoingia sana katika jeni zao. Kwa hiyo, hawangeliweza kutokeza uzao wenye kukamilika, kama vile chombo cha kupikia mkate chenye kasoro hakiwezi kutokeza kitu chenye kukamilika. (Yobu 14:4) Kweli, kila kuzaliwa kwa mtu kwahakikisha kwamba wazazi wetu wa kwanza walipoteza afya kamilifu na uzima wa milele kwao wenyewe na kwa uzao wao. Mtume Mkristo Paulo aliandika: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikasambaa kwa watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.”—Waroma 5:12; linganisha Zaburi 51:5.

      6. Kwa nini tunakufa?

      6 Leo wanasayansi hawajui hakika kwa nini watu huzeeka na kufa. Lakini, Biblia hufasiria kwamba tunakufa kwa sababu tunazaliwa tukiwa wenye dhambi, tukiwa tumerithi hali hii kutoka wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu. Lakini, jambo gani hutufikia tunapokufa?

  • Jambo Gani Huifikia Nafsi Wakati wa Kifo?
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Jambo Gani Huifikia Nafsi Wakati wa Kifo?

      “Fundisho la kwamba nafsi ya mwanadamu ni isiyoweza kufa na kwamba itaendelea kuwako baada ya kufa kwa mtu na kuharibika kwa mwili wake ni mojapo wa fundisho la msingi la falsafa na teolojia ya Ukristo.”—“NEW CATHOLIC ENCYCLOPEDIA.”

      1. New Catholic Encyclopedia chakubali nini kuhusu kuokoka kifo kwa nafsi?

      LAKINI, rejezeo hilo hilo lakubali kwamba “wazo la kuendelea kuishi kwa nafsi baada ya kifo halitambulikani kabisa katika Biblia.” Hivyo, basi, Biblia kwa kweli hufundisha nini kuhusu jambo ambalo huifikia nafsi wakati wa kifo?

      Wafu Hawajui Lolote

      2, 3. Wafu wanayo hali gani, na ni maandiko gani yanayofunua hilo?

      2 Hali ya wafu yaonyeshwa wazi kwenye Muhubiri 9:5, 10, ambapo twasoma hivi: “Wafu hawajui kitu . . . hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima ndani ya kaburi.” Kwa hiyo, kifo ni hali ya kutokuwako. Mtunga-Zaburi aliandika kwamba wakati mtu anapokufa, “anarudia udongo wake; siku ileile mafikili yake yanapotea.”—Zaburi 146:4.

      3 Basi, wafu hawajui lolote, ni wasiotenda. Alipotamka hukumu juu ya Adamu, Mungu alisema: “Mavumbi wewe, na utarudi kwa mavumbi.” (Mwanzo 3:19) Kabla ya Mungu kumfanya kutoka katika mavumbi ya ardhi na kumpa uhai, Adamu hakuwako. Adamu alipokufa, alirudi katika hali ileile. Adhabu yake ilikuwa kifo—na si kuhama kwenda makao mengine.

      Nafsi Yaweza Kufa

      4, 5. Toa mifano kutoka Biblia, inayoonyesha kwamba nafsi yaweza kufa.

      4 Adamu alipokufa, jambo gani liliifikia nafsi yake? Kumbuka kwamba katika Biblia neno “nafsi” kwa kawaida huelekeza kwa mtu. Basi, tunaposema kwamba Adamu alikufa, tunamaanisha kwamba nafsi iliyoitwa Adamu ilikufa. Kwa mtu ambaye huamini katika kutoweza kufa kwa nafsi hilo linaweza kuonekana kuwa jambo geni. Hata hivyo, Biblia yaeleza hivi: “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.” (Ezekieli 18:4) Walawi 21:1 husimulia juu ya “nafsi iliyokufa” (“wafu,” Zaïre Swahili Bible). Na wanaziri waliambiwa kwamba wasikaribie “nafsi yoyote iliyokufa” (“maiti,” ZSB).—Hesabu 6:6.

      5 Rejezeo linalofanana na hilo kuhusu nafsi lapatikana kwenye 1 Wafalme 19:4. Eliya mwenye kutaabishwa vikali sana ‘alianza kuomba kwamba nafsi yake iweze kufa.’ Vivyo hivyo, Yona aliendelea kuomba kwamba nafsi yake iweze kufa, naye alirudilia kusema hivi: “Ni vema kwangu kufa kuliko kuishi.” (Yona 4:8) Na Yesu alitumia usemi “kuua nafsi,” ambao Zaïre Swahili Bible huutafsiri “kuua.” (Marko 3:4) Basi, kifo cha nafsi chamaanisha tu kifo cha mtu.

      ‘Kutoka’ na ‘Kurudi’

      6. Biblia inamaanisha nini isemapo kwamba nafsi ya Raheli ilikuwa “ikitoka“?

      6 Lakini namna gani kuhusu kifo chenye kutia huzuni cha Raheli, kilichotukia alipokuwa akizaa mwana wake wa pili? Tunasoma kwenye Mwanzo 35:18 hivi: “Na ilikuwa wakati alipokuwa akikata roho [nafsi yake ilikuwa ikimtoka, NW] (kwa sababu alikufa) akaita jina lake Benoni; lakini baba yake alimwita Benyamina.” Je! andiko hili lamaanisha kwamba Raheli alikuwa na kiumbe kingine cha ndani ambacho kiliondoka wakati wa kufa kwake? La, Hasha! Kumbuka, neno “nafsi” laweza kuelekeza kwa uhai alio nao mtu. Basi, katika kisa hiki “nafsi” ya Raheli ilimaanisha tu “uhai” wake. Ndiyo sababu Biblia zingine hutafsiri usemi huu ‘nafsi yake ilikuwa ikimtoka’ kuwa ‘uhai wake ulikuwa ukitoka’ (Knox), “alivuta pumzi yake ya mwisho” (Jerusalem Bible), na ‘uhai wake ulimtoka’ (Bible in Basic English). Hakuna jambo fulani linaloonyesha kwamba sehemu ya kifumbo ya Raheli iliendelea kuishi baada ya kifo chake.

      7. Katika njia gani yasemwa kwamba nafsi ya mwana aliyefufuliwa wa mjane “ilimurudia”?

      7 Jambo lenye kufanana na hilo ni ufufuo wa mwana wa mjane, unaorekodiwa kwenye 1 Wafalme sura ya 17. Katika mstari wa 22, twasoma kwamba kadiri Eliya alivyosali kwa ajili ya kijana, “BWANA [Yehova, NW] alisikiliza sauti ya Eliya; roho [nafsi, NW] ya mutoto ilimurudia, akafufuka.” Mara nyingine tena, neno “nafsi” lamaanisha “uhai.” Hivyo, New American Standard Bible husomwa: “Uhai wa mtoto ukamrudia naye akaishi tena.” Ndiyo, ulikuwa uhai, wala si kitu chenye kivuli, uliomrudia tena kijana huyo. Hilo lapatana na yale Eliya alimwambia mama ya mtoto huyo: “Tazama, mwana wako [mtu kamili] anaishi.”—1 Wafalme 17:23.

      Shaka la Wazo la “Hali ya Katikati”

      8. Watu wengi wanaojidai kuwa Wakristo wanaamini jambo gani litatokea wakati wa ufufuo?

      8 Wengi wanaokiri kuwa Wakristo wanaamini kwamba kutakuwa na ufufuo wakati ujao ambapo mwili utaungana na nafsi zisizoweza kufa. Ndipo, wafufuliwa watakuwa mbele ya tokeo lao la mwisho—ama thawabu kwa wale waliyoongoza uhai wao vizuri au kisasi kwa waovu.

      9. Usemi “hali ya katikati” wamaanisha nini, nao wengine husema jambo gani huifikia nafsi katika kipindi hicho?

      9 Wazo hili laonekana kuwa jepesi. Lakini wale wanaoshikamana na imani ya kutoweza kufa kwa nafsi wanayo matatizo ya kufasiria jambo linaloifikia nafsi kati ya wakati wa kufa na wakati wa ufufuo. Kwa kweli, hii “hali ya katikati,” kama itwavyo kwa kawaida, imechochea kufikiri-fikiri kwa karne nyingi. Wengine husema kwamba katika kipindi hicho nafsi huenda kwenye pirigatori, ambapo yaweza kutakaswa na dhambi ndogo na hivyo kuwa yenye kustahili kuingia mbinguni.a

      10. Kwa nini haipatani na maandiko kuamini kwamba nafsi zinaendelea kukaa kwa muda katika pirigatori baada ya kifo, na namna gani jambo lililompata Lazaro lahakikisha hilo?

      10 Walakini, kama tulivyoona, nafsi ni mtu mwenyewe. Mtu anapokufa, nafsi inakufa. Kwa hiyo, hakuna maisha yenye ufahamu baada ya kifo. Kwa kweli, Lazaro alipokufa, Yesu Kristo hakusema kwamba alikuwa katika pirigatori, katika Limbo, au katika “hali ya katikati” nyingine yoyote. Badala yake, Yesu alisema tu: “Lazaro analala usingizi.” (Yohana 11:11, ZSB) Bila shaka, Yesu, aliyejua kweli kuhusu jambo linaloipata nafsi wakati wa kifo, aliamini kwamba Lazaro hakuwa na ufahamu, hakuwako.

      Roho Ni Nini?

      11. Kwa nini neno “roho” halingeweza kuelekeza kwa sehemu ya mtu isiyo na mwili inayookoka kifo?

      11 Biblia yasema kwamba wakati mtu anapokufa, “pumuzi [roho, NW] yake inatoka, anarudia udongo wake.” (Zaburi 146:4) Je! hilo lamaanisha kwamba roho isiyo na mwili huondoka kihalisi na kuendelea kuishi baada ya kifo cha mtu? Haiwezekani iwe hivyo, kwa kuwa mtunga-zaburi asema tena: “Siku ile ile mafikili yake yanapotea” (“fikira zake hukoma,” New English Bible). Basi, roho ni nini, na namna gani ‘inamtoka’ mtu wakati wa kufa kwake?

      12. Katika Biblia, maneno ya Kiebrania na Kigiriki yanayotafsiriwa “roho” yamaanisha nini?

      12 Katika Biblia, maneno yaliyotafsiriwa “roho” (Kiebrania, ruʹach; Kigiriki, pneuʹma) kwa msingi yamaanisha “pumzi.” Hivyo, badala ya ‘roho yake inatoka,’ tafsiri ya R. A. Knox yatumia usemi “pumzi yauacha mwili wake.” (Zaburi 145:4, Knox) Lakini, neno “roho” lamaanisha mengi zaidi kuliko tendo la kupumua. Kwa mfano, katika kuelezea uharibifu wa uhai wa binadamu na mnyama wakati wa Garika la ulimwenguni pote, Mwanzo 7:22 husema: “Wote waliokuwa na pumuzi ya roho [kani, NW] [au, roho; Kiebrania: ruʹach] ya uzima kwa pua yao, wa wote waliokuwa katika inchi kavu, wakakufa.” Basi, “roho” yaweza kuelekeza kwa kani ya uhai ambayo hutenda katika viumbe vyote vinavyoishi, wanadamu na wanyama, na ambayo hutegemezwa na kupumua.

      13. Katika njia gani roho yaweza kulinganishwa na mkondo wa umeme?

      13 Tutoe kielezo: Mkondo wa umeme hutoa nguvu kwa vifaa mbalimbali. Mkondo ukisimama, vifaa vinaacha kufanya kazi. Mkondo hauwi chombo kingine kinachoachana na vifaa. Jambo lenye kufanana, mtu anapokufa, roho yake inaacha kuzitia nguvu chembe za mwili. Roho haiuachi mwili na kuendelea mpaka makao mengine.—Zaburi 104:29.

      14, 15. Namna gani roho hurudi kwa Mungu wakati wa kifo?

      14 Basi, kwa nini Muhubiri 12:7 hueleza kwamba mtu anapokufa, “roho inarudi kwa Mungu aliyeitoa”? Je! hilo lamaanisha kwamba roho yasafiri kihalisi kupitia anga kwenda mpaka aliko Mungu? Haimaanishi hivyo. Kumbuka, roho ni kani ya uhai. Mara tu hiyo kani ya uhai kuondoka, Mungu pekee ndiye anao uwezo wa kuirudisha tena. Basi, roho “inarudi kwa Mungu” katika maana ya kwamba tumaini lolote la uhai kwa wakati ujao kumhusu mtu huyo sasa linabaki kabisa kwa Mungu.

      15 Mungu pekee ndiye awezaye kuirudisha roho, au kani ya uhai, kusababisha mtu arudi tena kwenye uhai. (Zaburi 104:30) Lakini, je! Mungu ana kusudi la kufanya hivyo?

      [Maelezo ya Chini]

      a Kulingana na New Catholic Encyclopedia, “Kwa ujumla Mababa wa [Kanisa] huwa wazi katika uthibitisho wao wa kuwako kwa pirigatori.” Lakini, kitabu hiki cha marejezo pia chakubali kwamba “fundisho la Kikatoliki kuhusu pirigatori lategemea juu ya pokeo, na si juu ya Andiko Takatifu.”

      [Sanduku katika ukurasa wa 23]

      KUMBUKUMBU ZA UHAI ULIOTANGULIA

      IKIWA hakuna kitu kinachoendelea kuishi kisha kufa kwa mwili, basi namna gani kuhusu kumbukumbu za uhai uliotangulia ambazo wengine hudai kuwa nazo?

      Msomi mhindu Nikhilananda asema kwamba ‘mambo yanayoonwa baada ya kifo hayawezi kuonyeshwa kwa kutoa sababu.’ Katika hotuba “Vielelezo vya Imani katika Umilele katika Dini,” mwanateolojia Hans Küng aonyesha wazi: “Hakuna hata moja ya habari—zinazotoka kwa kawaida kwa watoto au kutoka nchi ambako watu huamini katika kuzaliwa upya katika mwili mwingine—za kumbukumbu la uhai uliotangulia zinazoweza kuthibitishwa.” Yeye aongeza: “Wengi wa [watafiti wanaotumika kwa bidii na kisayansi kuhusu jambo hilo hukubali kwamba uchunguzi uliofanywa nao hautoi msingi wa uthibitisho wa kweli wenye kusadikisha kweli kweli wa kurudia-rudia kwa uhai wa kidunia.”

      Lakini namna gani ikiwa unahisi kwamba wewe unazo kumbukumbuku za kipekee za uhai uliotangulia? Kuhisi huko kwaweza kutokana na mambo mengi. Nyingi za habari tunazopokea zinalindwa akiba mbali katika ncha zenye kufichama za ufahamu wa akili zetu kwa sababu matumizi yazo si ya moja kwa moja au ya papo hapo. Wakati kumbukumbu zilizosahauliwa zinaporudi tena, watu wengine hueleza hayo kuwa uhakika wa uhai wa zamani. Hata hivyo, jambo hakika ni kwamba hatuna uchunguzi wenye kuthibitishwa wa uhai kuliko huu ambao tunaishi sasa. Watu walio wengi wanaoishi duniani hawana kumbukumbu juu ya jambo la kwamba waliishi mapema, wala hawafikiri kwamba huenda walikuwa na uhai uliotangulia.

  • Tumaini Hakika
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Tumaini Hakika

      “Tangu wakati wa kuzaliwa kuna ule uwezekano usiobadilika kwamba mwanadamu huenda akafa wakati wowote ule; na kwa njia isiyoepukika uwezekano huo unakuja kuwa jambo lenye kutimia.”—ARNOLD TOYNBEE, MWANAHISTORIA MUINGEREZA.

      1. Wanadamu wamelazimika kukubali uhakika gani, na huo ukitokeza maulizo gani?

      NANI awezaye kubishana na kweli ya kihistoria isiyotiliwa shaka inayotajwa hapo juu? Sikuzote wanadamu wamelazimika kukubali uhakika wenye kutia hofu wa kifo. Na wakati mtu fulani tumpendaye anapokufa tunajisikia kuwa wasioweza kufanya lolote ili kusaidia! Kupoteza huko kunaonekana kusikobadilishwa kabisa. Je! yawezekana kuungana tena na wapendwa wetu waliokufa? Biblia hutoa tumaini gani kwa wafu? Tazama habari inayofuata.

      ‘Rafiki Yetu Amekufa’

      2-5. (a) Rafiki yake Lazaro alipokufa, namna gani Yesu alionyesha kutaka kwake na uwezo wa kumfufua? (b) Zaidi ya kumrudisha Lazaro kwenye uhai, muujiza wa ufufuo ulitimiza nini?

      2 Ulikuwa ni mwaka 32 W.K. Katika mji mdogo wa Bethania, kilomita 3 nje ya Yerusalemu, waliishi Lazaro pamoja na dada zake Martha na Maria. Walikuwa marafiki wa karibu wa Yesu. Siku moja, Lazaro akawa mgonjwa sana. Bila kukawia, dada zake wenye kusikitishwa wakatuma habari hiyo kwa Yesu, akiwa ngambo ya Mto Yordani. Yesu alikuwa na shauku kuelekea Lazaro na dada zake, hivyo baadaye akaondoka kuelekea Bethania. Wakiwa njiani, Yesu akawambia wanafunzi wake: “Lazaro rafiki yetu ameenda kupumzika, lakini ninafunga safari huko ili kumwamsha kutoka usingizini.” Kwa kuwa wanafunzi hawakufahamu mara moja maana ya habari hiyo, Yesu akawaambia waziwazi: “Lazaro amekufa.”—Yohana 11:1-15.

      3 Waliposikia kwamba Yesu alikuwa akija Bethania, Martha alienda mbio nje kukutana naye. Akiguswa na sikitiko lake, Yesu akamhakikishia: “Ndugu yako atainuka.” Martha akamjibu: “Najua atafufuliwa katika ufufuo siku ya mwisho.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi ndio ufufuo na uhai. Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, hata ingawa afa, atakuja kwenye uhai.”—Yohana 11:20-25.

      4 Ndipo Yesu akaenda kwenye kaburi na akaagiza kwamba jiwe lililofunga kiingilio liondolewe mbali. Kisha kusali kwa sauti kubwa, akaamuru: “Lazaro, njoo huku nje!” Na macho ya wote yakiwa yamekaziwa kwenye kaburi, Lazaro kwa kweli akaja nje. Yesu alimfufua Lazaro—akirudisha uhai kwa mwanamume aliyekuwa amekuwa mfu kwa siku nne!—Yohana 11:38-44.

      5 Tayari Martha alikuwa na imani katika ahadi ya ufufuo. (Yohana 5:28, 29; 11:23, 24) Muujiza wa kurudishwa kwa Lazaro kwenye uhai ulisaidia kutia nguvu imani yake na kuingiza imani katika wengine. (Yohana 11:45) Lakini, kwa usahihi neno “ufufuo” lamaanisha nini?

      “Atainuka”

      6. Neno “ufufuo” lamaanisha nini?

      6 Neno “ufufuo” latafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki a·naʹsta·sis, ambalo kwa njia halisi lamaanisha “kusimama wima tena.” Watafsiri Waebrania wa Kigiriki walitafsiri a·naʹsta·sis wakitumia maneno ya Kiebrania techi·yathʹ ham·me·thimʹ, yanayomaanisha “kuamka kwa wafu.”a Hivyo, ufufuo hutia ndani kuinua mtu kutoka katika hali isiyo ya uhai ya kifo—kurudisha tena kigezo cha uhai cha mtu.

      7. Kwa nini ufufuo wa watu hautatokeza tatizo hata moja kwa Yehova Mungu na Yesu Kristo?

      7 Akiwa mwenye hekima isiyo na mwisho na mkamilifu katika kumbukumbu, Yehova Mungu aweza kwa urahisi kumfufua mtu. Kukumbuka kigezo cha uhai wa watu waliokufa—tabia za nyutu zao, historia ya maisha yao, na mambo yote yanayowatambulisha—si tatizo kwake. (Yobu 12:13; linganisha Isaya 40:26.) Yehova pia ndiye Chanzo cha uhai. Kwa hiyo, yeye aweza kwa urahisi kurudisha kwenye uhai mtu yuleyule, akimpa utu uleule katika mwili wenye muundo mpya. Tena, kama inavyoonyeshwa na jambo lililompata Lazaro, Yesu Kristo ni mwenye kutaka na mwenye uwezo wa kufufua wafu.—Linganisha Luka 7:11-17; 8:40-56.

      8, 9. (a) Kwa nini ufufuo haupatani na wazo la kutoweza kufa kwa nafsi? (b) Ni nini dawa ya kifo?

      8 Hata hivyo, fundisho la Kimaandiko kuhusu ufufuo ni lisilopatana na fundisho la kutoweza kufa kwa nafsi. Ikiwa nafsi isiyoweza kufa inaokoka kifo, hakuna yeyote angehitaji kufufuliwa au kurudishwa kwenye uhai. Kwa kweli, Martha hakuonyesha wazo lolote kuhusu nafsi isiyoweza kufa ambayo ilikuwa ikiendelea kuishi mahali fulani baada ya kifo. Yeye hakuamini kwamba Lazaro alikuwa tayari amekwenda kwenye makao fulani ya kiroho na kuendelea kuishi huko. Tofauti na hilo, alionyesha imani yake katika kusudi la Mungu la kupindua matokeo ya kifo. Yeye alisema: “Najua atafufuliwa katika ufufuo siku ya mwisho.” (Yohana 11:23, 24) Vivyo hivyo, Lazaro mwenyewe hakueleza kuwa amewahi kuona jambo lolote katika maisha ya baada ya kifo. Hakukuwa jambo lolote la kuripoti.

      9 Hakuna shaka, kulingana na Biblia, nafsi hufa na dawa kwa kifo ni ufufuo. Lakini maelfu ya mamilioni ya watu wamekuwa wakikufa tangu kuwako duniani kwa mtu wa kwanza, Adamu. Basi, ni nani atakayefufuliwa na wapi?

      ‘Wote Waliomo Ndani ya Makaburi ya Ukumbusho’

      10. Ni ahadi gani Yesu alitoa kuhusiana na wale walio katika makaburi ya ukumbusho?

      10 Yesu Kristo alisema: “Saa inakuja ambayo katika hiyo wote wale waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake [Yesu] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29) Ndiyo, Yesu Kristo aliahidi kwamba wote wale walio katika kumbukumbu la Yehova watafufuliwa. Maelfu ya mamilioni ya watu wameishi na kufa. Nani kati yao aliye katika kumbukumbu la Mungu, akingojea ufufuo?

      11. Nani watakaofufuliwa?

      11 Wale ambao wamefuatilia mwendo wa uadilifu kama watumishi wa Yehova watafufuliwa. Lakini mamilioni ya watu wengine wamekufa bila kuonyesha ikiwa wangeweza kukubali viwango vya uadilifu vya Mungu. Walikuwa ama wasiojua matakwa ya Yehova, ama walikosa wakati wa kutosha kufanya mabadiliko yaliyohitajiwa. Hawa pia wamo katika kumbukumbu la Mungu na kwa hiyo watafufuliwa, kwa kuwa Biblia yaahidi: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.

      12. (a) Ni mwono gani mtume Yohana alipata kuhusu ufufuo? (b) Nini “huvurumishwa katika ziwa la moto,” na usemi huo unamaanisha nini?

      12 Mtume Yohana alipata ono lenye kusisimua la waliofufuliwa wakisimama mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu. Akieleza jambo hilo, yeye aliandika: “Nayo bahari ikawatoa hao wafu waliokuwa ndani yayo, na kifo na Hadesi vikawatoa wafu ndani yavyo, nao walihukumiwa mmoja-mmoja kulingana na vitendo vyao. Na kifo na Hadesi vikavurumishwa ndani ya ziwa la moto. Hili humaanisha kifo cha pili, ziwa la moto.” (Ufunuo 20:12-14) Fikiria kile ambacho jambo hilo humaanisha! Wafu wote walio katika kumbukumbu la Mungu watafunguliwa kutoka katika Hadesi, au Sheoli, kaburi la kawaida la wanadamu. (Zaburi 16:10; Matendo 2:31) Ndipo “kifo na Hadesi” vitavurumishwa ndani ya kile kinachoitwa “ziwa la moto,” likimaanisha uharibifu kamili. Kaburi la kawaida la wanadamu litakoma kuwapo.

      Kufufuliwa Wapi?

      13. Kwa nini Mungu alipangia wengine kwamba wafufuliwe kwenda mbinguni, na Yehova atawapatia mwili wa aina gani?

      13 Hesabu ndogo ya wanaume na wanawake watafuliwa kwenye uzima mbinguni. Hao watatawala pamoja na Kristo wakiwa wafalme na makuhani na watashiriki katika kuangamiza matokeo yote ya kifo ambacho wanadamu walirithi kutoka mtu wa kwanza, Adamu. (Waroma 5:12; Ufunuo 5:9, 10) Kulingana na Biblia, wahesabiwa kuwa 144,000 tu na wamechaguliwa kutoka miongoni mwa wafuasi wa Kristo, kuanzia mitume waaminifu. (Luka 22:28-30; Yohana 14:2, 3; Ufunuo 7:4; 14:1, 3) Yehova atapatia kila mmoja wa hao watakaofufuliwa mwili wa kiroho hivi kwamba waweze kuishi mbinguni.—1 Wakorintho 15:35, 38, 42-45; 1 Petro 3:18.

      14, 15. (a) Walio wengi zaidi kati ya hao waliokufa watafufuliwa kwenye uhai wa aina gani? (b) Wanadamu watiifu wataziona baraka gani?

      14 Lakini, walio wengi zaidi ya wale waliokufa watafufuliwa kwenye uhai duniani. (Zaburi 37:29; Mathayo 6:10) Dunia ya aina gani? Leo dunia inajaa ugomvi, umwagaji-damu, uharibifu wa mazingira, na jeuri. Ikiwa wafu wangepaswa kurudi kwenye uhai katika dunia kama hiyo, hakika furaha yoyote ingekuwa ya muda mfupi tu. Lakini Muumba ameahidi kwamba karibuni ataleta kwenye mwisho jamii ya ulimwengu ya sasa ambayo ni chini ya uongozi wa Shetani. (Mezali 2:21, 22; Danieli 2:44) Jamii mpya ya watu yenye uadilifu—“dunia mpya”— itakuwa hivyo jambo halisi. (2 Petro 3:13) Wakati huo “hapana mwenyeji atakayesema, mimi ni mugonjwa.” (Isaya 33:24) Hata uchungu wa kifo utaondolewa, kwa sababu Mungu “atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:4.

      15 Katika ulimwengu mpya ulioahidiwa na Mungu, wapole “watajifurahisha katika wingi wa salama.” (Zaburi 37:11) Serikali ya kimbinguni ya Kristo Yesu na washiriki wenzake 144,000 watarudisha polepole wanadamu watiifu kwenye ukamilifu ambao wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walipoteza. Kati ya wakaaji wa dunia mtakuwamo pia wale watakaofufuliwa.—Luka 23:42, 43.

      16-18. Ufufuo utaletea familia shangwe gani?

      16 Biblia yatoa mwono mdogo wa furaha ambayo ufufuo utaletea familia. Fikiria furaha aliyohisi yule mjane wa Naini wakati Yesu aliposimamisha andamano la mazishi na kumfufua mwana wake pekee! (Luka 7:11-17) Baadaye, karibu na Ziwa la Galilaya, wakati Yesu alipomrudisha binti mwenye umri wa miaka 12 kwenye uhai, wazazi wake “wakapigwa na bumbuazi ya upeo wa shangwe kubwa.”—Marko 5:21-24, 35-42; tazama pia 1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:32-37.

      17 Kuhusu mamilioni wanaolala sasa katika kifo, ufufuo utamaanisha uhai katika ulimwengu mpya wenye amani. Fikiri kidogo juu ya tazamio lenye kusisimua ambalo jambo hilo hufungulia Tommy na mfanyabiashara, waliotajwa katika sehemu ya kwanza ya broshua hii! Tommy aamkapo kwenye uhai katika Paradiso duniani, atakuwa ni Tommy yuleyule ambaye mamaye alijua—lakini pasipo magonjwa. Atakuwa na uwezekano wa kumgusa, kumshika katika mikono yake, na kumpenda. Vilevile, pahali pa kunaswa katika karibu duara isiyo na mwisho ya kuzaliwa upya tena na tena, yule mfanyabiashara kutoka India analo tazamio la ajabu la kufungua macho yake akiwa katika ulimwengu mpya wa Mungu na kuwatazama wana wake.

      18 Kujua kweli kuhusu nafsi, kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa, na kuhusu tumaini la ufufuo kunaweza pia kuwa na matokeo yenye kina juu ya wale wanaoishi sasa. Acheni tuone namna hilo linavyokuwa na matokeo hayo.

      [Maelezo ya Chini]

      a Huku neno “ufufuo” likiwa halipatikani katika Maandiko ya Kiebrania, tumaini la ufufuo linaonyeshwa wazi kwenye Yobu 14:13, Danieli 12:13, na Hosea 13:14.

      [Picha katika ukurasa wa 26]

      Ufufuo utaleta shangwe yenye kudumu

  • Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
    • Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana

      “Nanyi mtajua kweli, na kweli itawaweka nyinyi huru.”—YOHANA 8:32.

      1. Kwa nini ni jambo la maana kuzichunguza imani zetu kuhusu nafsi na kifo?

      IMANI kuhusu kifo na uhai baada ya kifo ni matokeo hasa ya elimu ya kidini na ya kitamaduni ya mtu. Kama tulivyoona, hizo hujipanga kutoka sadikisho la kwamba nafsi hutimiza lengo layo la mwisho kisha tu kuzaliwa upya mara nyingi mpaka kwenye wazo la kwamba kipindi kimoja cha maisha kinaamua tokeo la mwisho la mtu. Kama tokeo, mtu mmoja anaweza kujihisi kuwa hakika kuhusu kuungana mwishowe na nafsi ya upeo baada ya kufa, mtu mwingine anaweza kujisikia kuwa hakika kufikia Nirvana, na bado mwingine kufikia kuvuna dhawabu ya kimbingu. Basi, kweli ni gani? Kwa kuwa imani zetu huwa na uvutano juu ya maelekeo yetu, matendo yetu na maamuzi yetu, je! hatungepaswa kuhangaikia kupata jibu kwa ulizo hilo?

      2, 3. (a) Kwa nini tunaweza kuweka tumaini katika kile ambacho Biblia husema kuhusu nafsi? (b) Kama inavyoelezwa katika Biblia, ni nini kweli kuhusu nafsi?

      2 Biblia, kitabu cha zamani zaidi sana katika ulimwengu, huiandika historia ya mwanadamu tangu kuumbwa kwa nafsi ya kwanza ya kibinadamu. Kwa wazi, Biblia hueleza kweli kuhusu nafsi: Nafsi yako ni wewe, wafu ni wasioishi kabisa; na wale walio katika kumbukumbu la Mungu watafufuliwa katika wakati wake unaofaa. Kujua mambo hayo kunaweza kumaanisha nini kwako?

      3 “Nanyi mtajua kweli, na kweli itawaweka nyinyi huru,” akasema Yesu Kristo kwa wafuasi wake. (Yohana 8:32) Ndiyo, kweli inaweka mtu huru. Lakini, ni kutoka nini kweli kuhusu nafsi itatuweka huru?

      Uhuru Kutoka Woga na Kukosa Tumaini

      4, 5. (a) Kweli kuhusu nafsi inaondoa woga gani? (b) Namna gani tumaini la ufufuo lilimpa moyo binti aliyefikia mwisho wa ugonjwa wake?

      4 “Watu wengi huogopa kifo na wanajaribu kuepuka kufikiri juu yacho,” yasema The World Book Encyclopedia. Mwanahistoria mmoja aonyesha kwamba “katika Mashariki neno ‘kifo’ lenyewe limekuwa karibu lisilotajwa.” Na katika tamaduni nyingine, maneno ya badala kama vile “kufariki” na “kupita” hutumiwa kwa kawaida ili kusimulia juu ya mtu anayekufa. Woga huo wa kifo leo ni woga hasa wa kisichojulikana, kwa kuwa kwa watu wengi kifo ni fumbo. Ujuzi wa kweli kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa watuliza woga huo.

      5 Tazama, kwa mfano, hali ya akilini ya binti Michaelyn mwenye umri wa miaka 15. Alikuwa na ugonjwa wa leukemia na alipambana na kifo chenye kusikitisha. Mamaye, Paula, akumbuka: “Michaelyn alisema hakuwa mwenye kusumbuliwa na wazo la kufa kwa kuwa alijua kwamba kifo ni jambo la muda tu. Tulizungumza sana kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu na kuhusu wale wote watakaofufuliwa humo. Michaelyn alikuwa na imani ya ajabu katika Yehova Mungu na ufufuo—bila shaka yoyote.” Tumaini la ufufuo lilimweka huru binti kijana huyu kutoka woga wenye kulemea wa kifo.

      6, 7. Kweli kuhusu nafsi hutuweka huru kutoka ukosefu gani wa tumani? Eleza.

      6 Namna gani kweli iliathiri wazazi wa Michaelyn? “Kifo cha binti wetu mdogo kilikuwa jambo lenye kuumiza sana ambalo halijawahi kutufikia kamwe,” asema Jeff, babaye. “Lakini tunatumaini kabisa katika ahadi ya Yehova ya ufufuo, na tunatazama mbele siku moja kumshika mpendwa wetu Michaelyn katika mikono mara nyingine. Huko kutakuwa kukutana kama nini!”

      7 Ndiyo, kweli kuhusu nafsi humweka mtu huru kutoka ule ukosefu wa tumaini uwezao kuletwa na kifo cha mpendwa. Hakika, hakuna kitu kiwezacho kuondoa kabisa umizo na sikitiko vinavyompata mtu wakati mpendwa anapokufa. Lakini, tumaini la ufufuo latuliza ombolezo na kufanya iwe rahisi zaidi kuvumilia umizo hilo.

      8, 9. Kweli kuhusu hali ya wafu hutuweka huru kutoka woga gani?

      8 Kweli ya Kimaandiko kuhusu hali ya wafu pia hutuweka huru kutoka woga wa wafu. Tangu kujifunza kweli hiyo, wengi waliokuwa hapo mwanzo wamefungwa kama kwa pingu na desturi za ushirikina kuhusu wafu hawahangaishwi tena na mambo ya kulaani, ishara mbaya, hirizi, na uchawi, wala hawatoi dhabihu zenye bei ili kutuliza roho za mababu wao waliokufa na kuwazuia kurudi ili kuwadhuru walio hai. Kwa kweli, kwa kuwa wafu “hawajui jambo lolote” mazoea kama hayo ni ya bure.—Mhubiri 9:5.

      9 Kweli kuhusu nafsi, ipatikanayo katika Biblia, ni yenye kukomboa na yenye kutumainika kabisa. Lakini tazama pia tazamio la pekee ambalo Biblia yakutolea.

      [Blabu katika ukurasa wa 29]

      Kweli kuhusu nafsi hukuweka huru kutoka woga wa kifo, woga wa wafu, kukosa tumaini juu ya kifo cha mpedwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki