-
Unaweza Kukabiliana na Ukosefu wa Haki!Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 15
-
-
Hata hivyo, matukio hayo hayawezi kamwe kulinganishwa na ukosefu wa haki ambao Kristo Yesu alitendewa. Alihukumiwa kifo kwa mashtaka ya uwongo na kesi isiyo halali. Gavana Mroma aliyekuwa akimhukumu hakuwa imara kutetea mambo aliyoona kuwa sawa. (Yohana 18:38-40) Ndiyo, Shetani alimtendea Kristo Yesu matendo makubwa zaidi yasiyo ya haki kuliko yale ambayo mtu mwingine yeyote amewahi kutendewa!
-
-
Unaweza Kukabiliana na Ukosefu wa Haki!Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 15
-
-
Yesu alikufa. Hata hivyo, Mungu alimfufua na kumpa cheo cha juu “zaidi kuliko kila serikali na mamlaka na nguvu na utawala na kila jina linalotajwa.” (Waefeso 1:20, 21) Ukosefu wa haki ambao Shetani alimtendea Kristo Yesu haungeweza kumzuia Yehova asimthawabishe Mwana wake. Yesu alikuwa na hakika kwamba Yehova angeweza kuzuia mara moja hatua isiyo ya haki ya kumkamata kinyume cha sheria, kama yangekuwa mapenzi ya Yehova kufanya hivyo. Lakini, Kristo alijua pia kwamba Yehova ana wakati wa kutimiza Maandiko na kuondoa ukosefu wowote wa haki.
-