-
Unaweza Kukabiliana na Ukosefu wa Haki!Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 15
-
-
Mfikirie Yosefu, ambaye aliuzwa utumwani huko Misri na ndugu zake wenye wivu. Huko Misri, mke wa bwana wake alijaribu kumtongoza Yosefu, na alipokataa, mke huyo alimshtaki kwa uwongo kwamba alitaka kulala naye. Kwa sababu hiyo, Yosefu alitiwa gerezani. Hata hivyo, imani yake ilikuwa na nguvu kuliko pingu za chuma ambazo alifungwa. Hakuruhusu ukosefu huo wa haki uharibu hali yake ya kiroho au udhoofishe tumaini lake katika Yehova.—Mwanzo 37:18-28; 39:4-20; Zaburi 105:17-19.
-
-
Unaweza Kukabiliana na Ukosefu wa Haki!Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 15
-
-
Kwa kuwa Yosefu aliuzwa utumwani, aliweza kuokoa familia yake. Alikuja kuwa msimamizi wa chakula nchini Misri kabla ya njaa kubwa ambayo iliikumba familia yake. Hebu fikiria, ikiwa Yehova angezuia Yosefu asitendewe isivyo haki, Yosefu hangekuwa gerezani. Aliweza kutafsiri ndoto za wale wafungwa wawili humo gerezani, na ni mfungwa mmoja kati yao ndiye aliyemwambia Farao baadaye kumhusu Yosefu, na hivyo Yosefu akawekwa kuwa msimamizi wa chakula.—Mwanzo 40:1; 41:9-14; 45:4-8.
-