-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
Tofauti na wale walionakili ujumbe mbalimbali wa kiimla kutoka kwa Mungu, waandikaji wa Biblia waliopokea maono au ndoto au walioona njozi, mara nyingi walikuwa na uhuru wa kufafanua katika maneno yao wenyewe yale waliyoona. Habakuki aliambiwa hivi: “Iandike njozi [“ono,” NW] ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji.”—Habakuki 2:2.
Je, hilo lamaanisha kwamba sehemu hizo za Biblia hazikupuliziwa kabisa kama zile zilizoto-lewa kiimla? La hasha. Kupitia roho yake, Yehova alikazia imara ujumbe wake katika akili ya kila mwandikaji, ili mawazo ya Mungu na si ya mwanadamu yawasilishwe. Ingawa Yehova aliruhusu mwandikaji ateue maneno yafaayo, yeye aliongoza akili na moyo wa mwandikaji ili kwamba asiache habari muhimu na mwishowe hayo maneno yalionekana kwa kufaa kuwa ya Mungu.—1 Wathesalonike 2:13.
-
-
Mungu Aliipuliziaje Biblia?Mnara wa Mlinzi—1997 | Juni 15
-
-
Ingawa waandikaji wa Biblia ‘walichukuliwa na roho takatifu,’ hata hivyo kufikiri kwa uangalifu kulihitajika upande wao. Kwa kielelezo, Solomoni ‘alitafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi. Akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyoofu, yaani maneno ya kweli.’—Mhubiri 12:9, 10.
-