Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Biblia Ni Neno la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
    • “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.”—2 TIMOTHEO 3:16, 17.

      MTUME Paulo alisema maneno yenye nguvu kama nini kuhusu thamani kubwa ya Biblia! Bila shaka, alikuwa akizungumzia hasa sehemu ya Biblia ambayo alikuwa nayo wakati huo, yaani, maandishi ambayo nyakati nyingine wengine wanayaita Agano la Kale. Lakini maneno yake yanahusu pia vitabu vyote 66 vya Biblia, kutia ndani vile vilivyoandikwa na wanafunzi waaminifu wa Yesu katika karne ya kwanza W.K.

      Je, unaiheshimu sana Biblia kama Paulo alivyoiheshimu? Je, unafikiri kwamba kwa kweli waandikaji wa Biblia waliongozwa na roho ya Mungu? Wakristo wa karne ya kwanza waliamini hivyo. Sikuzote Wakristo wa kweli wameamini hivyo. Kwa mfano, kasisi Mwingereza wa karne ya 14, John Wycliffe, aliiona Biblia kuwa “sheria isiyokosea ya kweli.” Kikieleza kuhusu maneno ya Paulo yaliyo hapo juu, kitabu kimoja (The New Bible Dictionary) kinasema kwamba ‘kwa kuwa Biblia imeongozwa na roho ya Mungu basi ni hakika kwamba mambo yote ambayo inasema ni ya kweli.’

  • Kwa Kweli Biblia Ni Neno la Mungu Lililoongozwa na Roho Yake
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 1
    • MTUME Paulo alimaanisha nini hasa aliposema kwamba Biblia ‘iliongozwa na roho ya Mungu’? (2 Timotheo 3:16) Akiandika katika lugha ya Kigiriki, Paulo alitumia neno ambalo kihalisi linamaanisha “lenye pumzi ya Mungu.” Paulo aliposema hivyo alimaanisha kwamba Mungu kupitia roho yake takatifu aliwaongoza waandikaji wa Biblia waandike tu mambo ambayo Alitaka waandike.

      Mtume Petro alisema kwamba waandikaji hao wa Biblia “walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” (2 Petro 1:21) Mtume Paulo alisema pia kwamba vitabu vya Biblia ni “maandishi matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.”—2 Timotheo 3:15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki