Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nabii wa Mungu Awaletea Wanadamu Nuru
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura ya 1

      Nabii wa Mungu Awaletea Wanadamu Nuru

      1, 2. Ni hali zipi leo zinazotia watu wengi wasiwasi?

      TUNAISHI muda ambao yaonekana mwanadamu aweza kupata chochote akitakacho. Usafiri wa angani, ufundi wa kompyuta, ujuzi wa kurekebisha utendaji wa chembe za urithi, na mavumbuzi mengine ya kisayansi yamewezesha binadamu kufanya mambo mapya, yakileta tumaini la maisha mazuri zaidi —labda hata marefu zaidi.

      2 Je, maendeleo hayo yamekuletea usalama wa kuondoa kufuli milangoni? Je, yamekomesha tisho la vita? Je, yameponya magonjwa au kumaliza huzuni ya kufiwa na mpendwa? Wapi! Maendeleo ya binadamu ni machache, ingawa ni ya ajabu. “Tumejua jinsi ya kwenda kwenye mwezi, kutengeneza vidude bora vya kutunza habari kwa elektroni, na kupandikiza chembe za urithi za kibinadamu,” yasema ripoti moja ya Shirika la Worldwatch. “Lakini hatujaweza kuwapa watu bilioni moja maji safi, kupunguza maangamizi ya maelfu ya aina mbalimbali za viumbe, wala kutimiza mahitaji yetu ya nishati bila kuharibu hali ya anga.” Ndiyo sababu watu wengi wana wasiwasi wa wakati ujao, maana hawana uhakika watapata wapi faraja na tumaini.

      3. Ni hali gani iliyokuwako katika Yuda karne ya nane K.W.K.?

      3 Hali yetu leo ni kama ile ya watu wa Mungu karne ya nane K.W.K. Wakati huo, Mungu alimwagiza Isaya mtumishi wake apelekee wakaaji wa Yuda ujumbe wa faraja, kwani faraja ilihitajika sana. Taifa lilikuwa na misukosuko. Karibuni Milki katili ya Ashuru ingetisha nchi hiyo, ijaze watu wengi hofu. Watu wa Mungu wangeweza kutafuta wapi wokovu? Walidai kwamba Yehova ni Mungu wao, lakini wakaona ni bora kutumaini wanadamu.—2 Wafalme 16:7; 18:21.

      Nuru Inang’aa Gizani

      4. Isaya aliagizwa atangaze ujumbe gani wenye sehemu mbili?

      4 Kwa sababu ya mwendo wa kuasi wa Yuda, Yerusalemu lingeharibiwa, na wakaaji wa Yuda wangetekwa wapelekwe Babiloni. Ndiyo, siku za giza zilikuwa njiani. Yehova alimwagiza Isaya nabii wake atabiri kipindi hiki chenye msiba, lakini pia atangaze habari njema. Kumbe, Wayahudi wangekombolewa Babiloni baada ya miaka 70 ya uhamisho! Mabaki wenye shangwe wangerudi Sayuni wapate pendeleo la kurudisha ibada ya kweli huko. Yehova aliangaza nuru gizani kwa kumtumia nabii wake kutoa ujumbe huo wa furaha.

      5. Kwa nini Yehova alifunua makusudi yake yakiwa mbali sana kutimizwa?

      5 Yuda ilifanywa ukiwa zaidi ya karne moja baada ya Isaya kuandika unabii wake mbalimbali. Kwa nini, basi, Yehova alifunua makusudi yake yakiwa mbali sana kutimizwa? Je, wale waliokuwa wameyasikia binafsi matangazo ya Isaya hawangekuwa wamekufa muda mrefu kabla ya unabii huo kutimizwa? Ni kweli. Hata hivyo, mafunuo ya Yehova kwa Isaya yaliwapa wale walioishi wakati wa kuharibiwa kwa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K. kumbukumbu iliyoandikwa ya ujumbe mbalimbali wa unabii wa Isaya. Hiyo ingetoa uhakikisho usioweza kukanushwa kwamba Yehova ndiye ‘atangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado.’—Isaya 46:10; 55:10, 11.

      6. Ni zipi baadhi ya njia ambazo Yehova anawapita watabiri wote wa kibinadamu?

      6 Yehova pekee ndiye mwenye haki ya kudai hivyo. Huenda mwanadamu akaweza kutabiri yatakayofanyika karibuni kwa sababu anajua hali ya kisiasa na ya kijamii ya siku zake. Lakini Yehova tu ndiye anayeweza kutangulia kuona matukio ya wakati wowote ule, hata ya wakati ujao ulio mbali, akiwa na uhakika kamili. Pia ana nguvu za kuwawezesha watumishi wake watabiri matukio muda mrefu sana kabla hayajatukia. Biblia husema hivi: “Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.”—Amosi 3:7.

      Kulikuwa na “Isaya” Wangapi?

      7. Wasomi wengi wameutiliaje shaka uandikaji wa Isaya, na kwa nini?

      7 Unabii ni jambo moja ambalo limefanya wasomi wengi watilie shaka uandikaji wa Isaya. Hao wakosoaji hushikilia kwamba sehemu ya mwisho ya kitabu hicho bila shaka iliandikwa na mtu wa karne ya sita K.W.K., ama wakati wa uhamisho Babiloni ama baadaye. Maoni yao ni kwamba unabii mbalimbali wa ukiwa wa Yuda uliandikwa baada ya kutimizwa, na basi haukuwa utabiri kamwe. Wao husema pia kwamba baada ya sura ya 40, kitabu cha Isaya huongea kana kwamba serikali kuu wakati huo ilikuwa Babiloni na Waisraeli walikuwa watekwa huko. Kwa hiyo wanasababu kwamba hakuna shaka kuwa yeyote yule aliyeandika sehemu ya mwisho ya Isaya aliiandika wakati huo—karne ya sita K.W.K. Je, kusababu huko kuna msingi mzuri? Hata kidogo!

      8. Kutilia shaka uandikaji wa Isaya kulianza lini, na kulieneaje?

      8 Karne ya 12 W.K. ilipofika, hapo ndipo uandikaji wa Isaya ulipoanza kutiliwa shaka. Ulitiliwa shaka na mwelezaji Myahudi Abraham Ibn Ezra. Kichapo Encyclopaedia Judaica husema kwamba “katika maelezo yake juu ya Isaya, [Abraham Ibn Ezra] anasema kwamba ile nusu ya pili, kuanzia sura ya 40, ni maandishi ya nabii aliyeishi wakati wa Uhamisho wa Babiloni na mapema baada ya Kurudi Sayuni.” Katika karne ya 18 na ya 19, maoni ya Ibn Ezra yalifuatwa na wasomi kadhaa, mmoja wao akiwa Johann Christoph Doederlein, mtaalamu wa dini Mjerumani aliyechapisha kitabu cha kufafanua Isaya mwaka wa 1775, kukiwa na chapa ya pili mwaka wa 1789. Kichapo New Century Bible Commentary husema hivi: “Sasa wasomi wote, isipokuwa wale wanaoshikilia maoni yao, wanakubaliana na fikira ya Doederlein . . . kwamba unabii mbalimbali unaopatikana katika sura ya 40 mpaka ya 66 katika kitabu cha Isaya si maneno ya nabii Isaya wa karne ya nane, bali ulitokea baadaye.”

      9. (a) Kitabu cha Isaya kimegawanywaje? (b) Mwelezaji mmoja wa Biblia anatoaje muhtasari wa ubishi unaohusu uandikaji wa Isaya?

      9 Hata hivyo, maswali kuhusu uandikaji wa kitabu cha Isaya hayakuishia hapo. Fikira ya kwamba kulikuwa na Isaya wa pili ilianzisha wazo la kwamba huenda ikawa kulikuwa na mwandishi wa tatu.a Kisha kitabu cha Isaya kikazidi kugawanywa, hivi kwamba msomi mmoja anasema sura ya 15 na ya 16 ziliandikwa na nabii asiyejulikana, huku mwingine akitilia shaka uandishi wa sura ya 23 mpaka ya 27. Bado mwingine anasema haiwezi kuwa ni Isaya aliyeandika maneno yaliyo katika sura ya 34 na ya 35. Kwa nini? Kwa sababu habari zilizomo zinafanana sana na zile za sura ya 40 mpaka ya 66, zilizokuwa tayari zimetajwa kuwa ziliandikwa na mtu mwingine wala si Isaya wa karne ya nane! Mwelezaji wa Biblia Charles C. Torrey anataja kwa ufupi matokeo ya kusababu hivyo. Anasema kwamba “Yule ‘Nabii wa Uhamishoni’ aliyekuwa mashuhuri amepoteza umashuhuri wake kabisa, na maandishi yake yamegawanywa ovyo kuwa vipande vipande.” Hata hivyo, si wasomi wote wanaokubaliana na ugawanyaji huo wa kitabu cha Isaya.

      Ushuhuda Kwamba Mwandishi Ni Mmoja

      10. Toa mfano mmoja kuonyesha kwamba kupatana kwa maneno ni ushuhuda wa kuwa kitabu cha Isaya kiliandikwa na mtu mmoja.

      10 Kuna sababu yenye nguvu ya kushikilia kwamba kitabu cha Isaya kimeandikwa na mwandishi mmoja tu. Ushuhuda mmoja unahusu upatano wa maneno. Kwa mfano, kifungu hiki “Mtakatifu wa Israeli” hupatikana mara 12 katika Isaya sura ya 1 mpaka ya 39, na mara 13 katika Isaya sura ya 40 mpaka ya 66, lakini maelezo hayo kuhusu Yehova yanaonekana mara 6 tu kwingineko kote katika Maandiko ya Kiebrania. Kurudiwa-rudiwa kwa maneno hayo yasiyotumika kikawaida hutetea kwamba kitabu chote kiliandikwa na Isaya mmoja.

      11. Kuna mifanano gani kati ya sura ya 1 mpaka ya 39, na sura ya 40 mpaka ya 66 ya Isaya?

      11 Kuna mifanano mingine kati ya Isaya sura ya 1 mpaka ya 39, na sura ya 40 mpaka ya 66. Sehemu zote mbili zinatumia sana semi za mfano za kipekee kwa njia ileile, kama vile mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, na “njia” au “njia kuu.”b Pia “Sayuni” inatajwa-tajwa, na neno hilo linatumiwa mara 29 katika sura ya 1 mpaka ya 39, kisha mara 18 katika sura ya 40 mpaka ya 66. Kwa kweli, Sayuni inatajwa mara nyingi katika Isaya kuliko katika kitabu kinginecho cha Biblia! Kichapo The International Standard Bible Encyclopedia kinasema kwamba shuhuda kama hizo “zinaonyesha kitabu hicho kina hali ya pekee ambayo ni ngumu kuelezeka” iwapo itasemwa kwamba kiliandikwa na waandishi wawili, watatu, au zaidi.

      12, 13. Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanaonyeshaje kwamba kitabu cha Isaya kiliandikwa na mwandishi mmoja?

      12 Ushuhuda wenye nguvu zaidi kwamba kitabu cha Isaya kiliandikwa na mtu mmoja tu unapatikana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yaliyopuliziwa. Hayo huonyesha wazi kwamba Wakristo wa karne ya kwanza waliamini kwamba kitabu cha Isaya kiliandikwa na mtu mmoja. Kwa mfano, Luka anasimulia juu ya ofisa Mwethiopia aliyekuwa akisoma habari ambazo sasa zinapatikana katika Isaya sura ya 53, sehemu ile ile ambayo wakosoaji siku hizi husema iliandikwa na Isaya wa Pili. Hata hivyo, Luka husema kwamba Mwethiopia huyo alikuwa “akimsoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.”—Matendo 8:26-28.

      13 Halafu fikiria mwandishi wa Gospeli, Mathayo, anayeeleza jinsi huduma ya Yohana Mbatizaji ilivyotimiza maneno ya unabii ambayo sasa tunayapata kwenye Isaya 40:3. Mathayo anasema unabii huo uliandikwa na nani? Je, ni Isaya wa Pili asiyejulikana? Sivyo, bali anamtambulisha mwandishi kuwa tu ni “Isaya nabii.”c (Mathayo 3:1-3) Wakati mwingine, Yesu alisoma katika kitabu cha kukunjwa maneno ambayo sasa tunayapata kwenye Isaya 61:1, 2. Akisimulia habari hiyo, Luka anasema hivi: “Akapewa hati-kunjo ya nabii Isaya.” (Luka 4:17) Katika barua yake kwa Waroma, Paulo anataja sehemu zote mbili za Isaya, ile ya mapema na ya baadaye, lakini hataji hata kidogo kwamba kulikuwa na mwandishi mwingine tofauti na Isaya yule mmoja tu. (Waroma 10:16, 20; 15:12) Ni wazi Wakristo wa karne ya kwanza hawakuamini kwamba kitabu cha Isaya kiliandikwa na waandishi wawili, watatu, au zaidi.

      14. Makunjo ya Bahari ya Chumvi yanatusaidiaje kuelewa uandishi wa Isaya?

      14 Fikiria, pia, ushuhuda wa Makunjo ya Bahari ya Chumvi, yaani, maandishi ya kale ambayo mengi kati ya hayo ni ya kabla ya wakati wa Yesu. Hati moja ya Isaya, iitwayo Kunjo la Isaya, ni ya kuanzia karne ya pili K.W.K., na inakanusha madai ya wakosoaji kwamba Isaya fulani wa pili aliendeleza uandishi kuanzia sura ya 40. Jinsi gani? Katika maandiko hayo ya kale, ile ambayo sasa tunaijua kuwa sura ya 40 inaanza kwenye mstari wa mwisho wa safu, na sentensi ya kwanza imemaliziwa katika safu inayofuata. Ni wazi kwamba kufikia hapo mnakili hakuwa na habari za badiliko lolote linalodhaniwa kuwa lilifanyika kuhusu mwandishi au mgawanyo wa kitabu hicho.

      15. Flavius Josephus, mwanahistoria Myahudi wa karne ya kwanza anasema nini juu ya unabii mbalimbali wa Isaya kumhusu Koreshi?

      15 Mwisho, fikiria ushuhuda wa Flavius Josephus, mwanahistoria Myahudi wa karne ya kwanza. Zaidi ya kuonyesha kwamba unabii mbalimbali ulio katika Isaya kuhusu Koreshi uliandikwa karne ya nane K.W.K., anasema pia kwamba Koreshi alikuwa na habari juu ya unabii huo. Josephus anaandika kwamba “Koreshi aliyajua mambo haya kwa kusoma kitabu cha unabii ambacho Isaya aliacha miaka mia mbili na kumi mapema.” Kulingana na Josephus, kwa kuwa Koreshi aliujua unabii huo mbalimbali, huenda ikawa hiyo hata ilimfanya akubali kuamuru Wayahudi warudie nchi yao, kwa maana Josephus anaandika kwamba Koreshi “alishikwa na tamaa kubwa na bidii ya kufanya yale yaliyokuwa yameandikwa.”—Jewish Antiquities, Kitabu cha 11, sura ya 1, fungu la 2.

      16. Ni nini linaloweza kusemwa juu ya dai la wakosoaji kwamba Babiloni inaelezwa katika sehemu ya mwisho ya Isaya kuwa ndiyo serikali kubwa ya wakati huo?

      16 Kama ilivyotajwa mapema, wakosoaji wengi huonyesha kwamba kuanzia Isaya sura ya 40 na kuendelea, Babiloni inaelezwa kuwa ndiyo serikali kubwa ya wakati huo, na Waisraeli wanatajwa kuwa uhamishoni tayari. Je, hiyo haingeonyesha kwamba mwandishi aliishi karne ya sita K.W.K.? Si lazima. Ukweli ni kwamba nyakati fulani Babiloni huelezwa kuwa serikali kubwa ya ulimwengu iliyokuwako hata kabla ya sura ya 40 ya Isaya kuandikwa. Kwa mfano, kwenye Isaya 13:19, Babiloni huitwa “huo utukufu wa falme,” au “ufalme mzuri wa falme zote,” kulingana na fasiri ya Today’s English Version. Ni wazi maneno hayo ni ya unabii, kwani zaidi ya karne moja ilipita ndipo Babiloni ikawa serikali kubwa ya ulimwengu. Mkosoaji mmoja “hutatua” hilo linalosemwa kuwa tatizo kwa kupuuza Isaya 13 akisema iliandikwa na mwandishi mwingine! Lakini, ni kawaida ya unabii wa Biblia kuyataja matukio ya wakati ujao kana kwamba tayari yametukia. Njia hiyo ya uandishi hukazia vizuri uhakika wa kutimizwa kwa unabii. (Ufunuo 21:5, 6) Kwa kweli, Mungu wa unabii wa kweli pekee ndiye anayeweza kusema hivi: “Nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapasheni habari zake.”—Isaya 42:9.

      Kitabu cha Unabii Unaotegemeka

      17. Badiliko la namna ya uandikaji kuanzia Isaya sura ya 40 na kuendelea linaweza kuelezwaje?

      17 Basi, ushuhuda unaelekeza kwenye uamuzi gani? Kwamba kitabu cha Isaya kiliandikwa na mtu mmoja aliyepuliziwa. Kitabu chote hiki kimepitishwa muda wa karne nyingi kikiwa kitabu kimoja tu, wala si vitabu viwili au zaidi. Ni kweli huenda wengine wakasema kwamba namna ya uandikaji wa kitabu cha Isaya hubadilika kidogo kuanzia sura ya 40 na kuendelea. Hata hivyo, kumbuka kwamba Isaya alitumikia akiwa nabii wa Mungu kwa miaka isiyopungua 46. Si ajabu kwamba katika muda huo habari za ujumbe wake na njia yake ya kueleza ujumbe huo zingebadilika. Kwa kweli, Isaya hakuagizwa na Mungu atoe tu maonyo makali ya hukumu. Alipaswa pia kutangaza maneno haya ya Yehova: “Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu.” (Isaya 40:1) Watu wa agano la Mungu wangefarijiwa kikweli na ahadi yake kuwa Wayahudi wangerudishwa nchi yao baada ya miaka 70 ya uhamisho.

      18. Ni kichwa gani katika kitabu cha Isaya kitakachozungumziwa katika kichapo hiki?

      18 Kichwa cha sura nyingi za Isaya zinazozungumzwa katika kitabu hiki ni kuachiliwa kwa Wayahudi kutoka utekwa wa Babiloni.d Kiasi fulani cha unabii huo kinatimizwa siku hizi, kama tutakavyoona. Tena, katika kitabu cha Isaya tunapata unabii mbalimbali wa kusisimua uliotimizwa wakati wa kuishi na wa kufa kwa Mwana mzaliwa pekee wa Mungu. Hakika watumishi wa Mungu na watu wengine duniani pote watafaidika kwa kujifunza unabii mbalimbali muhimu ulio katika kitabu cha Isaya. Kweli unabii huo ni nuru kwa wanadamu wote.

  • Wenye Kufariji Unaokuhusu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura ya 2

      Wenye Kufariji Unaokuhusu

      Isaya 41:1-29

      1. Kwa nini tupendezwe na unabii wa Isaya?

      ISAYA aliandika kitabu chenye jina lake karibu miaka 3,000 iliyopita, lakini kina thamani kubwa kwetu leo. Tunaweza kujifunza kanuni zilizo muhimu katika matukio ya historia aliyoyaandika. Tena tunaweza kujenga imani yetu kwa kujifunza unabii mbalimbali alioandika kwa jina la Yehova. Ndiyo, Isaya alikuwa nabii wa Mungu aliye hai. Yehova alimpulizia kuandika historia mapema—kueleza matukio kabla hayajatendeka. Hivyo Yehova alionyesha kwamba anaweza kutabiri wakati ujao na pia kuuelekeza. Baada ya kujifunza kitabu cha Isaya, Wakristo wa kweli husadiki kwamba Yehova atatimiza ahadi zake zote.

      2. Hali ya Yerusalemu ilikuwaje Isaya alipoandika kitabu chake cha unabii, na ni badiliko gani lingetokea?

      2 Isaya alipomaliza kuandika unabii wake, tayari Yerusalemu lilikuwa limeokoka tisho la Waashuri. Bado hekalu lilikuwako, na watu waliendelea na shughuli za kila siku kama ilivyokuwa imekuwa kwa mamia ya miaka. Hata hivyo, mambo yangebadilika. Utajiri wa wafalme Wayahudi ungepelekwa Babiloni, na vijana Wayahudi wangekuwa maofisa wa baraza katika jiji hilo.a (Isaya 39:6-7) Hilo lingetukia miaka zaidi ya 100 baadaye.—2 Wafalme 24:12-17; Danieli 1:19.

      3. Isaya sura ya 41 ina ujumbe gani?

      3 Hata hivyo, ujumbe wa Mungu kupitia Isaya si ujumbe wa maangamizi tu. Sura ya 40 ya kitabu chake huanza kwa neno “Faraja,” NW.b Wayahudi wangefarijiwa na uhakikisho wa kwamba wao ama watoto wao wangeweza kurudi kwao. Sura ya 41 inaendeleza ujumbe huo wa faraja na kutabiri kwamba Yehova angetokeza mfalme mwenye nguvu atimize mapenzi ya kimungu. Sura hiyo ina uhakikisho mwingi na inatia moyo kumtumaini Mungu. Pia inafichua kwamba miungu ya uwongo inayotumainiwa na watu wa mataifa haina nguvu. Hayo yote yanaimarisha sana imani, siku za Isaya na zetu pia.

      Yehova Atolea Mataifa Mwito wa Ushindani

      4. Yehova anatumia maneno gani kuwatolea mataifa mwito wa ushindani?

      4 Yehova anatumia nabii wake kusema hivi: “Nyamazeni mbele zangu, enyi visiwa, na mataifa wajipatie nguvu mpya; na waje karibu wakanene; na tukaribiane pamoja kwa hukumu.” (Isaya 41:1) Yehova anasema hayo kuyatolea mwito wa ushindani mataifa yanayopinga watu wake. Na yasimame mbele zake yajitayarishe kusema! Kama itakavyoonwa baadaye, Yehova anatenda kana kwamba yeye ni hakimu mahakamani kwa kudai kwamba mataifa haya yatoe uthibitisho kuwa sanamu zao ni miungu kikweli. Je, miungu hiyo inaweza kutabiria waabudu wake matendo ya wokovu au hukumu za adui zao? Ikiwa ndivyo, je, inaweza kutimiza unabii huo? Sivyo. Ni Yehova tu anayeweza hayo.

      5. Eleza jinsi unabii mbalimbali wa Isaya ulivyo na utimizo zaidi ya mmoja.

      5 Tunapofikiria unabii wa Isaya, na tukumbuke kwamba maneno yake yana utimizo zaidi ya mmoja, kama ulivyo unabii mwingi wa Biblia. Mwaka wa 607 K.W.K., Yuda wataenda uhamishoni Babiloni. Hata hivyo, unabii wa Isaya unafunua kwamba Yehova atawakomboa Waisraeli waliotekwa huko. Hiyo inatukia mwaka wa 537 K.W.K. Kisa hiki cha kufunguliwa kilikuwa na ulinganifu mapema katika karne ya 20. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, watumishi wa Yehova watiwa-mafuta duniani walipitia kipindi cha dhiki. Mwaka wa 1918, Jumuiya ya Wakristo, ile sehemu kuu ya Babiloni Mkubwa, ilichochea ulimwengu wa Shetani hata ukakaribia kuikomesha kabisa kazi iliyopangwa ya kuhubiri habari njema. (Ufunuo 11:5-10) Maofisa fulani wenye kuongoza Watch Tower Society walifungwa gerezani kwa mashtaka ya kutungwa. Ikaonekana ni kama ulimwengu umeshinda pigano lake juu ya watumishi wa Mungu. Halafu, kama ilivyokuwa kule nyuma mwaka wa 537 K.W.K., Yehova akawakomboa bila kutazamiwa. Mwaka wa 1919, maofisa waliokuwa gerezani walifunguliwa, na mashtaka waliyofanyiwa yakaondolewa baadaye. Mkusanyiko mmoja wa Cedar Point, Ohio, Septemba 1919 uliwatia nguvu tena watumishi wa Yehova ili waanze tena kazi ya kuhubiri habari njema za Ufalme. (Ufunuo 11:11, 12) Tangu hapo, kazi ya kuhubiri imeongezeka ajabu. Tena, mengi ya maneno ya Isaya yatatimizwa vizuri ajabu katika dunia-Paradiso itakayokuja. Hivyo basi, maneno ya kale ya Isaya yanahusu mataifa yote na jamii zote leo.

      Mkombozi Aitwa

      6. Nabii anamfafanuaje mshindi wa wakati ujao?

      6 Kupitia Isaya, Yehova anatabiri mshindi atakayeokoa watu wa Mungu kutoka Babiloni na pia ahukumu adui zao. Yehova anauliza hivi : “Ni nani aliyemwinua mmoja atokaye mashariki, ambaye katika haki amemwita mguuni pake? ampa mataifa mbele yake, na kumtawaza juu ya wafalme [“kumfanya aende akitiisha hata wafalme,” “NW”]; awatoa wawe kama mavumbi kwa upanga wake, kama makapi yaliyopeperushwa kwa upinde wake. Awafuatia, apita salama hata kwa njia asiyoikanyaga kamwe kwa miguu yake. Ni nani aliyetenda na kufanya jambo hilo, aviitaye vizazi tangu mwanzo? Mimi, BWANA, wa kwanza na wa mwisho, mimi ndiye.”—Isaya 41:2-4.

      7. Ni nani mshindi anayekuja, naye anatimiza nini?

      7 Ni nani aliyeinuliwa kutoka sehemu za mashariki? Nchi za Umedi-Uajemi na Elamu ziko mashariki ya Babiloni. Koreshi Mwajemi apiga miguu kutoka huko pamoja na majeshi yake hodari. (Isaya 41:25; 44:28; 45:1-4, 13; 46:11) Ingawa Koreshi si mwabudu wa Yehova, yeye anatenda kupatana na mapenzi ya Yehova, yule Mungu mwenye haki. Koreshi anatiisha wafalme, nao wanatawanywa kama vumbi mbele yake. Anafuatia ushindi kwa kupita “salama” katika njia zisizopitiwa kwa kawaida, akishinda vipingamizi vyote. Kufikia mwaka wa 539 K.W.K., Koreshi afikia jiji hodari la Babiloni na kulipindua. Basi watu wa Mungu wanafunguliwa ili warudi Yerusalemu kuanzisha upya ibada safi.—Ezra 1:1-7.c

      8. Ni Yehova tu anayeweza kufanya nini?

      8 Hivyo, Yehova anamtumia Isaya kutabiri kuinuka kwa Koreshi, zamani kabla mfalme huyo hajazaliwa. Ni Mungu wa kweli tu anayeweza kutoa unabii kama huo kwa usahihi. Hakuna aliye sawa na Yehova kati ya miungu ya uwongo ya mataifa. Basi Yehova ana sababu nzuri ya kusema hivi: “Utukufu wangu sitampa mwingine.” Yehova tu ndiye mwenye haki ya kusema hivi: “Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu.”—Isaya 42:8; 44:6, 7.

      Jamii Zenye Hofu Zinatumaini Sanamu

      9-11. Mataifa yanatendaje Koreshi anaposonga mbele?

      9 Isaya sasa anaeleza jinsi mataifa yanavyotenda kuhusu mshindi huyo wa wakati ujao: “Visiwa vimeona, vikaogopa; ncha za dunia zilitetemeka; walikaribia, walikuja. Wakasaidiana, kila mtu na mwenzake, kila mtu akamwambia ndugu yake; Uwe na moyo mkuu. Seremala [“fundi,” “NW”], akamtia moyo mfua dhahabu [“mfanyakazi wa metali,” “NW”] na yeye alainishaye kwa nyundo akamhimiza yule apigaye fuawe, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, Ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike.”—Isaya 41:5-7.

      10 Yehova anachunguza tamasha ya ulimwengu kwa kutazama miaka 200 hivi inayokuja. Majeshi hodari yanayoongozwa na Koreshi yanaenda kasi, yakishinda wapinzani wote. Jamii za watu—hata wakaaji wa visiwa, walio mbali kabisa—wanatetemeka anapokaribia. Wanaungana kwa hofu kupinga yule ambaye Yehova ameita kutoka mashariki atekeleze hukumu. Wanajaribu kutiana moyo, wakisema: “Uwe na moyo mkuu.”

      11 Mafundi wanashirikiana kutengeneza miungu-sanamu iwakomboe watu. Mbao inatengenezwa na seremala, naye anamtia moyo mfua dhahabu aifunike kwa metali, labda kwa dhahabu. Mhunzi anatwanga-twanga ile metali kuilainisha, kisha anaukubali myeyusho uliofanyiwa metali hiyo. Labda ni dhihaka inayotumiwa wakati inapotajwa kwamba sanamu inakazwa kwa misumari ili isitikisike au kulegea, kama vile sanamu ya Dagoni ilivyotikisika na kubwagika chini mbele ya sanduku la Yehova.—1 Samweli 5:4.

      Msihofu!

      12. Yehova anaipa Israeli uhakikisho gani?

      12 Sasa Yehova anawafikiria watu wake. Wale wanaomtumaini Mungu wa kweli hawahitaji kuwa na woga kamwe kama yale mataifa yanayotumaini sanamu zao zisizo na uhai. Uhakikisho wa Yehova unaanza kwa kikumbusha cha kwamba Israeli ni uzao wa Abrahamu rafiki yake. Kwa maneno mororo sana, Isaya anaripoti asemavyo Yehova: “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu; wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.”—Isaya 41:8-10.

      13. Kwa nini maneno ya Yehova yatawafariji Wayahudi watekwa?

      13 Maneno haya yatawafariji kama nini Wayahudi waaminifu walioshikwa mateka katika nchi ya kigeni! Watatiwa moyo kama nini kumsikia Yehova akiwaita “mtumishi wangu” wakiwa wahamishwa, watumishi wa mfalme wa Babiloni! (2 Mambo ya Nyakati 36:20) Ingawa Yehova atawatia nidhamu kwa kukosa uaminifu, hatawakataa. Israeli ni mali ya Yehova, si ya Babiloni. Watumishi wa Mungu hawatahitaji kutetemeka eti Koreshi mshindi anakuja. Yehova atakuwa pamoja na watu wake ili kuwasaidia.

      14. Watumishi wa Mungu wanafarijiwaje leo na maneno ambayo Yehova aliambia Israeli?

      14 Maneno hayo yamewapa watumishi wa Mungu uhakikisho na nguvu mpaka siku zetu. Kule nyuma mwaka wa 1918, wao walitaka sana kujua mapenzi ya Yehova kwao. Walitamani kukombolewa kutoka utekwa wao wa kiroho. Leo sisi tunatamani kupata kitulizo tutoke kwenye mikazo tunayotwikwa na Shetani, ulimwengu, na kutokamilika kwetu wenyewe. Lakini tunafahamu kwamba Yehova anajua wakati na jinsi hasa ya kusaidia watu wake. Kama watoto wadogo, sisi tunaendelea kushika mkono wake hodari, tukiwa na hakika atatusaidia kukabiliana na hali. (Zaburi 63:7, 8) Yehova huwathamini wanaomtumikia. Yeye hututegemeza sisi leo sawa na vile alivyowategemeza watu wake kupita katika kile kipindi kigumu cha mwaka wa 1918 mpaka wa 1919, na sawa na vile alivyowategemeza Waisraeli waaminifu zamani za kale.

      15, 16. (a) Adui za Israeli watapatwa na nini, na Israeli anafanana na mdudu kwa njia zipi? (b) Maneno ya Yehova yanatia moyo hasa leo kwa sababu ya shambulio gani linalokaribia?

      15 Fikiria yale ambayo Yehova anasema sasa kupitia Isaya: “Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika [“wataona aibu,” “NW”] na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia. Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema BWANA na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.”—Isaya 41:11-14.

      16 Adui za Israeli hawatashinda. Wale wanaoona hasira juu ya Israeli wataona aibu. Wale wanaopigana juu yake wataangamia. Ingawa Waisraeli walio mateka wanaonekana walegevu na bila ulinzi kama mdudu anayejipinda-pinda vumbini, Yehova atawasaidia. Lo, hiki kimekuwa kitia-moyo kizuri kama nini muda wote wa “siku za mwisho” wakati Wakristo wa kweli wamekabili uadui wa watu wengi sana ulimwenguni! (2 Timotheo 3:1) Tena ahadi ya Yehova ni yenye kutia nguvu kama nini wakati shambulio la Shetani, anayetajwa katika unabii kuwa “Gogu wa Magogu,” linapokaribia! Wakati Gogu atakapofanya shambulio kali juu ya watu wa Yehova, wataonekana kana kwamba hawana ulinzi sawasawa na mdudu—watu ‘wanaokaa pasipo kuta,’ pasipo hata “makomeo wala malango.” Hata hivyo, wanaomtumainia Yehova hawatahitaji kutetema kwa hofu. Mweza yote mwenyewe atapigana ili kuwakomboa.—Ezekieli 38:2, 11, 14-16, 21-23; 2 Wakorintho 1:3.

      Faraja kwa Israeli

      17, 18. Isaya anaelezaje juu ya kutiwa nguvu kwa Israeli, nasi tuwe na uhakikisho wa utimizo gani?

      17 Yehova anaendelea kufariji watu wake: “Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno [“kuwili,” “NW”]; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi. Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia BWANA, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.”—Isaya 41:15, 16.

      18 Israeli atapewa nguvu ashambulie ili kujitetea, na kuwatiisha kiroho adui zake walio kama milima. Israeli arudipo kutoka uhamishoni, atawashinda maadui wanaojaribu kuzuia hekalu na kuta za Yerusalemu zisijengwe upya. (Ezra 6:12; Nehemia 6:16) Hata hivyo, maneno ya Yehova yatatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Yesu anawaahidi Wakristo watiwa-mafuta hivi: “Yeye ashindaye na kushika vitendo vyangu hadi mwisho hakika nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye hakika atachunga watu kwa fimbo ya chuma hivi kwamba watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo wa mfinyanzi, sawa na vile mimi nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufunuo 2:26, 27) Hakika wakati utafika ambapo ndugu za Kristo waliofufuliwa kwenye utukufu wa kimbingu watashiriki kuwaangamiza adui za Yehova Mungu.—2 Wathesalonike 1:7, 8; Ufunuo 20:4, 6.

      19, 20. Isaya anaandika nini juu ya kurudishwa kwa Israeli mahali penye uzuri, na hilo linatimizwaje?

      19 Kwa usemi wa mfano, sasa Yehova anaimarisha ahadi yake ya kusaidia watu wake. Isaya anaandika hivi: “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, wala hapana; ndimi zao zimekauka kwa kiu; mimi, BWANA, nitawasikia, mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha. Nitafunua vijito vya maji juu ya vilima, na chemchemi katikati ya mabonde; nitageuza jangwa kuwa ziwa la maji, na mahali pakavu kuwa vijito vya maji. Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja; ili waone, na kujua, wakafikiri, na kufahamu pamoja, ya kuwa mkono wa BWANA ndio uliofanya jambo hilo. Mtakatifu wa Israeli ndiye aliyeliumba.”—Isaya 41:17-20.

      20 Ingawa Waisraeli wahamishwa wanakaa jiji kuu la serikali kubwa ya ulimwengu yenye utajiri, kwao jiji hilo ni kama jangwa lisilo na maji. Wanahisi kama Daudi, alipokuwa akijificha Mfalme Sauli. Mwaka wa 537 K.W.K., Yehova anawafungulia njia ya kurudi Yuda wakajenge upya hekalu lake Yerusalemu, na hivyo warudishe ibada safi. Naye Yehova anawabariki. Katika unabii wa baadaye, Isaya anatabiri hivi: “BWANA ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama bustani ya Edeni, na nyika yake kama bustani ya BWANA.” (Isaya 51:3) Hilo linatukia kikweli Wayahudi wanaporudi kwao.

      21. Ni kisa gani cha kurudishwa kilichotokea nyakati za kisasa, na itakuwaje wakati ujao?

      21 Jambo kama hilo lilitukia nyakati za kisasa, Koreshi Mkuu Zaidi, Kristo Yesu, alipokomboa wafuasi wake watiwa-mafuta kutoka utekwa wa kiroho ili waweze kufanya kazi ya kurudisha ibada safi. Waaminifu hao walibarikiwa kwa paradiso ya kiroho yenye utele, bustani ya Edeni ya mfano. (Isaya 11:6-9; 35:1-7) Karibuni, Mungu atakapoharibu adui zake, dunia nzima itageuzwa iwe paradiso halisi, sawa na vile Yesu alivyomwahidi mtenda-maovu juu ya ule mti.—Luka 23:43.

      Mwito wa Ushindani kwa Adui za Israeli

      22. Kwa mara nyingine, Yehova anayatolea mataifa mwito wa ushindani kwa kutumia maneno gani?

      22 Sasa Yehova anarudia ubishi wake na mataifa na miungu yao iliyo sanamu: “Haya, leteni maneno yenu, asema BWANA; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo. Wayatangaze na kutujulisha yatakayokuwa; watuonyeshe mambo ya zamani, ni mambo gani, tukapate kuyatia moyoni, tukajue mwisho wake; au wamdhihirishie yatakayotokea baadaye. Tujulisheni yatakayokuwa baadaye, nasi tutakiri ya kuwa ninyi ni miungu; naam, tendeni mema au tendeni mabaya, ili tujipime, tukaone pamoja. Tazameni, ninyi si kitu, tena kazi yenu si kitu; awachaguaye ninyi ni chukizo.” (Isaya 41:21-24) Je, miungu ya mataifa inaweza kutoa unabii kwa usahihi na hivyo ithibitishe kwamba ina ujuzi unaopita ule wa kawaida? Ikiwa inaweza, basi kwapaswa kuwe na matokeo fulani, mema ama mabaya, ya kuunga mkono madai yao. Ingawa hivyo, ukweli ni kwamba miungu-sanamu haina uwezo wa kutimiza lolote, nayo ni kama kazi bure.

      23. Ni kwa nini Yehova, kupitia manabii wake, aliendelea sana kulaumu sanamu vikali?

      23 Siku zetu, huenda wengine wakajiuliza ni kwa nini Yehova, kupitia Isaya na manabii wenzake, alitumia muda wote huo kulaumu vikali upumbavu wa kuabudu sanamu. Huenda wengi leo wakaonekana wanatambua wazi kwamba sanamu zilizotengenezwa na wanadamu ni bure. Hata hivyo, mfumo wa imani za uwongo ukiisha kuanzishwa na kukubaliwa mahali pengi, ni vigumu kuung’oa akilini mwa wale wanaouamini. Imani nyingi za wakati wetu ni upumbavu kama tu upumbavu wa kuamini kwamba mifano isiyo na uhai ni miungu kikweli. Na bado watu hushikilia imani hizo hata kama kuna hoja za kusadikisha kwamba imani hizo si kweli. Ni baada tu ya kusikia ukweli tena na tena kwamba wengine huguswa moyo kuiona hekima ya kumtumaini Yehova.

      24, 25. Yehova anamtaja tena Koreshi kwa njia gani, na hiyo inatukumbusha unabii gani mwingine?

      24 Yehova anamtaja tena Koreshi: “Nimemwinua mtu toka kaskazini, naye amekuja; toka maawio ya jua amekuja anitajaye jina langu; naye atawajilia maliwali kama akanyagaye matope, na kama mfinyanzi afinyangaye udongo.” (Isaya 41:25)d Tofauti na miungu ya mataifa, Yehova anaweza kutimiza mambo. Atakapomleta Koreshi kutoka mashariki, kutoka “maawio ya jua,” Mungu ataonyesha uwezo wake wa kutabiri kisha kuelekeza wakati ujao ili utimize utabiri wake.

      25 Maneno haya yanatukumbusha maelezo ya kiunabii ya mtume Yohana juu ya wafalme ambao wangeinuliwa kuchukua hatua wakati wetu. Kwenye Ufunuo 16:12, tunasoma kwamba njia itatayarishwa “kwa ajili ya wafalme watokao macheo ya jua.” Wafalme hawa si wengine ila Yehova Mungu na Yesu Kristo. Sawa na vile Koreshi alivyowakomboa watu wa Mungu zamani za kale, wafalme hao walio hodari mno kumzidi wataangamiza adui za Yehova na kuwachunga watu wake waipite dhiki kubwa waingie ulimwengu mpya wa uadilifu.—Zaburi 2:8, 9; 2 Petro 3:13; Ufunuo 7:14-17.

      Yehova Ndiye Mkuu Zaidi!

      26. Sasa Yehova anatokeza swali gani, na je, linajibiwa?

      26 Tena, Yehova anatangaza ukweli wa kwamba yeye tu ndiye Mungu wa kweli. Anauliza hivi: “Ni nani aliyeihubiri habari tokea mwanzo, tupate kuijua? na tokea zamani, tupate kusema, Yeye ni mwenye haki? Naam, hapana hata mmoja aliyetujulisha; naam, hapana hata mmoja aliyetuonyesha; naam, hapana hata mmoja aliyesikia maneno yenu.” (Isaya 41:26) Hakuna mungu-sanamu aliyewatangazia wenye kumtumaini kwamba kuna mshindi anayekuja kuwakomboa. Miungu yote hiyo haina uhai, tena ni bubu. Si miungu kamwe.

      27, 28. Ni kweli gani muhimu inayokaziwa katika mistari ya kumalizia ya Isaya 41, na ni nani tu wanaoitangaza?

      27 Baada ya kueleza maneno hayo ya unabii wa Yehova wenye kuchochea, Isaya anakazia ukweli mmoja muhimu: “Mimi kwanza nitauambia Sayuni, Tazama; hawa ndio; nami nitampa Yerusalemu mletaji wa habari njema. Na nitazamapo, hapana mtu, hata katika watu hao hapana mshauri mmoja, ambaye, nikimwuliza, aweza kunijibu neno. Tazama, hao wote ni ubatili; kazi zao si kitu; sanamu zao ni upepo na fujo.”—Isaya 41:27-29.

      28 Yehova ndiye namba moja. Yeye ndiye mkuu zaidi! Ndiye Mungu wa kweli, anayetangaza kukombolewa kwa watu wake, akiwaletea habari njema. Na ni Mashahidi wake tu wanaoyatangazia mataifa ukuu wake. Yehova anawashutumu wale wanaotumaini ibada ya sanamu, akipuuza sanamu zao kuwa “upepo na fujo.” Hiyo ni sababu yenye nguvu kama nini ya kufanya mtu ajishikilie sana kwa Mungu wa kweli! Yehova pekee ndiye anayestahili tumaini letu hakika.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona sura ya 29 ya Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I.

      b Ona sura ya 30 ya Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I.

      c Koreshi Mkuu Zaidi, ambaye mwaka wa 1919 aliwakomboa “Israeli wa Mungu” kutoka utekwa wa kiroho, si mwingine ila Yesu Kristo, aliyeketi akiwa Mfalme mtawazwa wa Ufalme wa kimbingu wa Mungu, tangu mwaka wa 1914.—Wagalatia 6:16.

      d Ingawa nchi ya nyumbani kwa Koreshi ilikuwa mashariki ya Babiloni, aliposhambulia jiji hilo mara ya mwisho, alishuka kutoka kaskazini, kutoka Asia Ndogo.

      [Picha katika ukurasa wa 19]

      Ingawa Koreshi ni mpagani, anachaguliwa afanye kazi ya Mungu

      [Picha katika ukurasa wa 21]

      Mataifa hutumaini sanamu zisizo na uhai

      [Picha katika ukurasa wa 27]

      Israeli ‘atasaga milima’ akiwa kama ‘chombo cha kupuria’

  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Tatu

      “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!

      Isaya 42:1-25

      1, 2. Kwa nini sura ya 42 ya Isaya inawapendeza Wakristo leo?

      “NINYI ni mashahidi wangu, asema BWANA, na mtumishi niliyemchagua.” (Isaya 43:10) Tangazo hili lililotolewa na Yehova, na kuandikwa na nabii Isaya katika karne ya nane K.W.K., linaonyesha kwamba watu wa kale wa agano la Yehova walikuwa taifa la mashahidi. Walikuwa mtumishi mteule wa Mungu. Miaka kama 2,600 baadaye, mwaka wa 1931, Wakristo watiwa-mafuta walitangaza peupe kwamba maneno hayo yaliwahusu. Walichukua jina Mashahidi wa Yehova, wakakubali kwa moyo wote madaraka ya kuwa mtumishi wa Mungu duniani.

      2 Mashahidi wa Yehova hutaka sana kumpendeza Mungu. Kwa hiyo, sura ya 42 ya kitabu cha Isaya inampendeza mno kila mmoja wao, maana inaonyesha hali ya mtumishi mmoja ambaye Yehova anamkubali, na ya mtumishi mwingine ambaye anamkataa. Kuufikiria unabii huo na utimizo wake hutufahamisha kinacholeta kibali cha Mungu na kinachofanya tusimpendeze.

      “Nimetia Roho Yangu Juu Yake”

      3. Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii gani juu ya “mtumishi wangu”?

      3 Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii wa kuja kwa mtumishi atakayemchagua mwenyewe: “Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu [“haki,” “NW”]. Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu. Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi utokao moshi hatauzima; atatokeza hukumu kwa kweli. Hatazimia, wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani; na visiwa vitaingojea sheria yake.”—Isaya 42:1-4.

      4. “Mteule” aliyetabiriwa ni nani, na tunajuaje hivyo?

      4 Mtumishi anayetajwa hapa ni nani? Hatuachwi na shaka. Tunaupata mtajo wa maneno hayo katika Gospeli ya Mathayo, nao umetumiwa kumhusu Yesu Kristo. (Mathayo 12:15-21) Yesu ndiye Mtumishi mpendwa, “mteule.” Yehova aliweka roho yake juu ya Yesu lini? Mwaka wa 29 W.K., wakati wa ubatizo wa Yesu. Maandishi yaliyopuliziwa hueleza kuhusu ubatizo huo, ya kwamba Yesu akiisha kutoka katika maji, “mbingu ilifunguliwa na roho takatifu katika umbo la kiwiliwili kama njiwa ikateremka juu yake, na sauti ikaja kutoka mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mpendwa; nimekukubali wewe.’” Yehova mwenyewe alimtambulisha hivyo Mtumishi wake mpendwa. Huduma ya Yesu iliyofuata na miujiza aliyoifanya, zilithibitisha kwamba kweli roho ya Yehova ilikuwa juu yake.—Luka 3:21, 22; 4:14-21; Mathayo 3:16, 17.

      ‘Atawatolea Mataifa Haki’

      5. Kwa nini maana ya haki ya kweli ilihitajika kueleweshwa wazi katika karne ya kwanza W.K.?

      5 Mteule wa Yehova ‘angetoa,’ au angetokeza wazi haki ya kweli. “Lililo haki atafanya kuwa wazi kwa mataifa.” (Mathayo 12:18) Hakika hilo lilihitajika sana karne ya kwanza W.K.! Viongozi wa kidini Wayahudi walifunza maoni kombo juu ya haki na uadilifu. Walitafuta kupata uadilifu kwa kufuata sheria ngumu-ngumu—nyingi zikiwa zao wenyewe. Haki yao ya kufuatilia sana sheria ilikosa rehema na huruma.

      6. Yesu alijulisha haki ya kweli kwa njia zipi?

      6 Lakini, Yesu alifunua maoni ya Mungu kuhusu haki. Yesu alionyesha kwa mafundisho na maisha yake kwamba haki ya kweli ina huruma na rehema. Ebu fikiria Mahubiri yake yenye sifa ya Mlimani. (Mathayo, sura ya 5-7) Hayo ni maelezo stadi kama nini kuhusu jinsi ya kufuata haki na uadilifu! Tusomapo masimulizi ya Gospeli, je, hatuguswi moyo na huruma ya Yesu kwa maskini na wanaoonewa? (Mathayo 20:34; Marko 1:41; 6:34; Luka 7:13) Alipeleka ujumbe wake wa faraja kwa wengi waliokuwa kama mianzi iliyopondeka, iliyoinama na kupigwa huku na huku. Walikuwa kama utambi unaotoa moshi ukitaka kuzimika, uhai wao ukikaribia kufifia kabisa. Yesu hakuvunja “mwanzi uliopondeka” wala hakuzima “utambi utokao moshi.” Bali, maneno na matendo yake ya upendo na huruma yaliinua mioyo ya wapole.—Mathayo 11:28-30.

      7. Kwa nini unabii ungeweza kusema kwamba Yesu ‘hangepaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu’?

      7 Lakini ni kwa nini unabii unasema kwamba Yesu “hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu”? Kwa sababu hakujipeleka kwa majivuno, kama walivyofanya watu wengi wa siku zake. (Mathayo 6:5) Akiponya mwanamume mkoma, Yesu alimwambia hivi mtu huyo aliyeponywa: “Angalia kwamba huambii mtu yeyote hata jambo moja.” (Marko 1:40-44) Yesu hakujitangaza na kuwafanya watu wakate kauli kutokana na uvumi, bali alitaka wao wenyewe watambue mambo kwa msingi wa ushuhuda imara ulioonyesha kwamba ndiye Kristo, Mtumishi mtiwa-mafuta wa Yehova.

      8. (a) Yesu aliyatolea ‘mataifa haki’ jinsi gani? (b) Kielezi cha Yesu juu ya Msamaria mwenye ujirani kinatufundisha nini juu ya haki?

      8 Huyo Mtumishi Mteule angetolea ‘mataifa haki.’ Ndivyo Yesu alivyofanya. Pamoja na kukazia kwamba haki ya kimungu ina huruma, Yesu alifundisha kuwa haki hiyo inapasa kuhusisha watu wote. Wakati mmoja, Yesu alikumbusha mwanamume mjuzi wa Sheria kwamba anapaswa kumpenda Mungu na jirani yake. Mwanamume huyo akamwuliza Yesu: “Ni nani kwa kweli aliye jirani yangu?” Labda alitazamia Yesu ajibu hivi: “Ni Myahudi mwenzako.” Lakini Yesu alisimulia mfano wa yule Msamaria mwenye ujirani. Mfano huo unasema Msamaria alimsaidia mwanamume aliyeshambuliwa na wanyang’anyi, lakini Mlawi na kuhani walikataa. Hapo mwenye swali akalazimika kukubali kwamba jirani wakati huo hakuwa Mlawi wala kuhani, bali yule Msamaria aliyedharauliwa. Yesu alimalizia kielezi kwa kushauri hivi: “Uwe ukifanya hilohilo wewe mwenyewe.”—Luka 10:25-37; Mambo ya Walawi 19:18.

      “Hatazimia, Wala Hatakata Tamaa”

      9. Hali yetu itakuwaje tukiifahamu haki ya kweli?

      9 Kwa kuwa Yesu alijulisha wazi kiini cha haki ya kweli, wanafunzi wake walijifunza kuonyesha sifa hiyo. Sisi pia ni lazima tujifunze. Kwanza, tunahitaji kukubali viwango vya Mungu vya mema na mabaya, maana ndiye mwenye haki ya kuamua la haki na la uadilifu. Tunapojitahidi kufanya mambo kwa njia ya Yehova, mwenendo wetu mnyoofu utaonyesha wazi haki ya kweli ni nini.—1 Petro 2:12.

      10. Kwa nini kuonyesha haki kunahusu pia kushiriki kazi ya kuhubiri na kufundisha?

      10 Pia sisi huonyesha haki ya kweli tunapohubiri na kufundisha. Yehova ameandaa kwa wingi ujuzi wenye kuokoa uhai unaohusu yeye mwenyewe, Mwana wake, na makusudi yake. (Yohana 17:3) Haingekuwa sawa au haki tukiwanyima wengine ujuzi huo. “Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda,” anasema Solomoni. (Mithali 3:27) Acheni tuwaambie watu wote, kwa moyo wote, mambo tunayojua juu ya Mungu, hata wawe ni wa rangi, kabila, au taifa gani.—Matendo 10:34, 35.

      11. Tunapaswa kuwatendeaje wengine kwa kumwiga Yesu?

      11 Tena, Mkristo wa kweli hutendea wengine kama Yesu alivyofanya. Watu wengi leo wana matatizo ya kuvunja moyo, nao wanahitaji huruma na kitia-moyo. Hata Wakristo fulani waliojiweka wakfu huenda wakatwangwa na hali za maisha hata wafanane na mianzi iliyopondeka au tambi zinazotoka moshi zikikaribia kuzimika. Wanahitaji tegemezo letu, sivyo? (Luka 22:32; Matendo 11:23) Lo, inaburudisha kama nini kuwa sehemu ya ushirika wa Wakristo wa kweli, wanaojaribu kumwiga Yesu kwa kufuata haki!

      12. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba karibuni watu wote watatendewa haki?

      12 Je, siku moja watu wote watatendewa haki? Bila shaka, ndiyo. Mteule wa Yehova ‘hatazimia, wala hatakata tamaa, hata atakapoweka haki duniani.’ Karibuni sana Mfalme aliyetawazwa, Kristo Yesu aliyefufuliwa, ‘ataleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu.’ (2 Wathesalonike 1:6-9; Ufunuo 16:14-16) Ufalme wa Mungu utachukua mahali pa utawala wa kibinadamu. Haki na uadilifu zitakuwa tele. (Mithali 2:21, 22; Isaya 11:3-5; Danieli 2:44; 2 Petro 3:13) Watumishi wa Yehova kotekote—hata wale wa sehemu za mbali, au “visiwa”—wanaingoja kwa hamu siku hiyo.

      ‘Nitamtoa Awe Nuru ya Mataifa’

      13. Yehova anatoa unabii gani juu ya Mtumishi wake Mteule?

      13 Isaya anaendelea kusema hivi: “Mungu BWANA anena, yeye aliyeziumba mbingu, na kuzitanda; yeye aliyeitandaza nchi na mazao yake; yeye awapaye pumzi watu walio juu yake; yeye awapaye roho wao waendao ndani yake.” (Isaya 42:5) Lo, hayo ni maelezo yenye mkazo kama nini juu ya Yehova, Muumba! Kikumbusha hicho juu ya uweza wa Yehova kinakazia maneno yake. Yehova anasema hivi: “Mimi, BWANA, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.”—Isaya 42:6, 7.

      14. (a) Inaposemwa kwamba Yehova anashika mkono wa Mtumishi wake aliyekubaliwa, hiyo ina maana gani? (b) Huyo Mtumishi Mteule ana kazi gani?

      14 Muumba Mtukufu wa ulimwengu mzima, Mpaji na Mwendelezaji wa uhai, anashika mkono wa Mtumishi wake Mteule na kuahidi kumsaidia kabisa wakati wote. Ni uhakikishio mzuri, wee! Tena, Yehova anamlinda salama ili amtoe awe “agano la watu.” Agano ni mkataba, mapatano, ahadi nzito. Ni amri hakika. Ndiyo, Yehova amemfanya Mtumishi wake “rehani kwa hao watu.”—An American Translation.

      15, 16. Yesu alitumikiaje akiwa “nuru ya mataifa”?

      15 Akiwa “nuru ya mataifa,” Mtumishi aliyeahidiwa ‘atafunua macho ya vipofu’ na kuwakomboa “wale walioketi gizani.” Ndivyo Yesu alivyofanya. Yesu alitukuza jina la Baba yake wa kimbingu kwa kuishuhudia kweli. (Yohana 17:4, 6) Alifunua wazi uwongo mwingi wa kidini, akahubiri habari njema za Ufalme, akawafungulia mlango wa uhuru wa kiroho wale waliokuwa katika utumwa wa kidini. (Mathayo 15:3-9; Luka 4:43; Yohana 18:37) Alitoa onyo la kutofanya kazi za giza na kumfichua Shetani kuwa “baba ya uwongo” na “mtawala wa ulimwengu huu.”—Yohana 3:19-21; 8:44; 16:11.

      16 Yesu alisema hivi: “Mimi ni nuru ya ulimwengu.” (Yohana 8:12) Alipata kuwa nuru hiyo kwa njia ya wazi sana alipotoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa fidia. Hivyo aliwafungulia njia wale wenye kudhihirisha imani ili wapate msamaha wa dhambi, uhusiano unaokubalika pamoja na Mungu, na tazamio la uhai wa milele. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Kwa kuendeleza ujitoaji mkamilifu wa kimungu maisha yake yote, Yesu aliiunga mkono enzi kuu ya Yehova, akathibitisha Ibilisi ni mwongo. Kweli Yesu alikuwa mfunguaji wa macho ya vipofu, na mkombozi wa wale waliotiwa katika gereza la giza la kiroho.

      17. Sisi tunatumikia tukiwa wachukua-nuru kwa njia zipi?

      17 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nyinyi ndio nuru ya ulimwengu.” (Mathayo 5:14) Je, sisi pia si wachukua-nuru? Kwa njia yetu ya maisha na kazi yetu ya kuhubiri, tuna pendeleo la kuelekeza wengine kwa Yehova, Chanzo cha nuru ya kweli. Kwa kumwiga Yesu, tunajulisha jina la Yehova, tunaiunga mkono enzi Yake kuu, na kutangaza kwamba Ufalme Wake ndio tumaini pekee kwa wanadamu. Pia, sisi tulio wachukua-nuru tunafunua uwongo mwingi wa kidini, tunatoa onyo juu ya kazi chafu za giza, na kumfichua Shetani, yule mwovu.—Matendo 1:8; 1 Yohana 5:19.

      ‘Mwimbieni Yehova Wimbo Mpya’

      18. Yehova hujulisha watu wake nini?

      18 Sasa Yehova anawageukia watu wake, akisema: “Mimi ni BWANA [“Yehova,” “NW”]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. Tazama, mambo ya kwanza yamekuwa, nami nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapasheni habari zake.” (Isaya 42:8, 9) Unabii kuhusu “mtumishi wangu” ulinenwa, si na mmoja wa miungu isiyofaa kitu, bali na yule Mungu mmoja tu aliye hai na wa kweli. Ilikuwa lazima utimie, na ulitimia. Kweli Yehova Mungu ndiye Mwanzilishi wa mambo mapya, naye hufanya watu wake wayajue kabla hayajatukia. Sisi tunapaswa kuitikiaje?

      19, 20. (a) Ni lazima wimbo gani uimbwe? (b) Ni nani leo wanaomwimbia Yehova wimbo wa sifa?

      19 Isaya anaandika hivi: “Mwimbieni BWANA wimbo mpya, na sifa zake tokea mwisho wa dunia; ninyi mshukao baharini, na vyote vilivyomo, na visiwa, nao wakaao humo. Jangwa na miji yake na ipaze sauti zao, vijiji vinavyokaliwa na Kedari; na waimbe wenyeji wa Sela, wapige kelele toka vilele vya milima. Na wamtukuze BWANA, na kutangaza sifa zake visiwani.”—Isaya 42:10-12.

      20 Wakaaji wa miji, wa vijiji jangwani, wa visiwa, hata wa “Kedari,” au kambi zilizopigwa katika majangwa—watu kila mahali—wanahimizwa wamwimbie Yehova wimbo wa sifa. Inasisimua kama nini kwamba katika siku zetu mamilioni ya watu wameitikia mwito huo wa unabii! Wameikubali kweli ya Neno la Mungu kwa moyo, wakamkubali Yehova awe Mungu wao. Watu wa Yehova wanaimba wimbo huo mpya—wakisema Yehova anastahili utukufu—katika nchi zaidi ya 230. Inasisimua kama nini kuimba katika kwaya hiyo ya tamaduni, lugha, na rangi nyingi sana!

      21. Kwa nini adui za watu wa Mungu hawawezi kunyamazisha wimbo wa kumsifu Yehova?

      21 Je, wapinzani wanaweza kusimama wampinge Mungu na kunyamazisha wimbo huo wa sifa? Haiwezekani! “BWANA atatokea kama shujaa; ataamsha wivu kama mtu wa vita; atalia, naam, atapiga kelele; atawatenda adui zake mambo makuu.” (Isaya 42:13) Ni nguvu gani inayoweza kumzuia Yehova? Miaka kama 3,500 iliyopita, nabii Musa na wana wa Israeli waliimba hivi kwa sauti: “BWANA ni mtu wa vita, BWANA [“Yehova,” NW] ndilo jina lake. Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.” (Kutoka 15:3, 4) Yehova alishinda jeshi lenye nguvu kupita yote ya wakati huo. Yehova anapojitokeza akiwa shujaa wa vita, hakuna adui yeyote wa watu wa Mungu anayeweza kitu.

      “Siku Nyingi Nimenyamaza Kimya”

      22, 23. Kwa nini Yehova ‘ananyamaza kimya siku nyingi’?

      22 Yehova hutenda kwa haki na bila kuonea, hata anapohukumu adui zake. Anasema hivi: “Siku nyingi nimenyamaza kimya; nimenyamaza, nikajizuia; sasa nitapiga kelele [“nitapiga kite,” “NW”] kama mwanamke aliye katika kuzaa; nitaugua na kutweta pamoja. Nitaharibu milima na vilima, nitavikausha vyote vimeavyo; nitaifanya mito ya maji kuwa visiwa, na kuyakausha maziwa ya maji.”—Isaya 42:14, 15.

      23 Yehova huacha wakati upite kabla ya kuhukumu, ili awape wakosaji nafasi ya kugeuka waache njia zao mbaya. (Yeremia 18:7-10; 2 Petro 3:9) Kwa mfano, wafikirie Wababiloni ambao, wakiwa ndio serikali kubwa ya ulimwengu wakati huo, wanafanya Yerusalemu ukiwa mwaka wa 607 K.W.K. Yehova anaruhusu hilo kuwatia nidhamu Waisraeli kwa kukosa uaminifu. Hata hivyo, Wababiloni hawatambui fungu wanalotimiza. Wanakuwa wakali kwa watu wa Mungu kwa kuzidi kiasi kinachotakiwa na hukumu ya Mungu. (Isaya 47:6, 7; Zekaria 1:15) Mungu wa kweli anaumia kama nini kuona watu wake wakiteseka! Lakini anajizuia kuchukua hatua mpaka wakati wake unaofaa. Halafu, anajikakamua—kama mwanamke anayezaa—ili kuwakomboa watu wa agano lake, na kuwatokeza wakiwa taifa huru. Ili atimize jambo hilo, katika mwaka wa 539 K.W.K., anakausha na kuharibu Babiloni na kinga zake.

      24. Ni tazamio gani ambalo Yehova anawafungulia watu wake Israeli?

      24 Baada ya kukaa uhamishoni miaka mingi sana, watu wa Mungu wanasisimuka kama nini wakati njia ya kurudi kwao inapowafungukia! (2 Mambo ya Nyakati 36:22, 23) Bila shaka wanafurahi sana kujionea utimizo wa ahadi hii ya Yehova: “Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.”—Isaya 42:16.

      25. (a) Watu wa Yehova wanaweza kuwa na uhakika gani leo? (b) Tuazimie kufanya nini?

      25 Maneno haya yanahusikaje leo? Kwa muda mrefu—ndiyo, kwa karne kadhaa—Yehova ameacha mataifa yafanye yatakavyo. Hata hivyo, wakati wake uliowekwa wa kumaliza maneno unakaribia. Nyakati za kisasa ametokeza jamii fulani ya watu ishuhudie jina lake. Kwa kubomoa upinzani wowote unaowakabili, amelainisha njia ili wamwabudu “kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24) Aliahidi: “Sitawaacha,” na kweli ametimiza ahadi yake. Namna gani wale wanaoendelea kuabudu miungu ya uwongo? Yehova anasema hivi: “Watarudishwa nyuma, wataaibishwa sana, hao wanaotumainia sanamu za mawe, na kuziambia sanamu za madini, Ninyi ndinyi miungu yetu.” (Isaya 42:17) Ni muhimu kama nini tubaki waaminifu kwa Yehova kama alivyofanya Mteule Wake!

      ‘Mtumishi Aliye Kiziwi na Kipofu’

      26, 27. Israeli wanakuwaje ‘mtumishi kiziwi na kipofu,’ na matokeo ni nini?

      26 Mtumishi Mteule wa Mungu, Yesu Kristo, alibaki mwaminifu mpaka kifo. Ingawa hivyo Israeli, watu wa Yehova, wanakuwa mtumishi asiye mwaminifu, kiziwi tena kipofu kiroho. Akiwahutubia, Yehova anasema hivi: “Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona. Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? naam, kipofu kama mtumishi wa BWANA? Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii. BWANA akapendezwa, kwa ajili ya haki yake, kuitukuza sheria, na kuiadhimisha.”—Isaya 42:18-21.

      27 Lo, Israeli ameshindwa kwa njia ya kusikitisha kama nini! Kila mara watu wake wanaangukia ibada ya miungu-mashetani ya mataifa. Tena na tena, Yehova anaendelea kuwatuma wajumbe wake, lakini watu wake hawasikii. (2 Mambo ya Nyakati 36:14-16) Isaya anatabiri matokeo: “Watu hawa ni watu walioibiwa [“walioporwa,” “NW”] na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha. Ni nani miongoni mwenu atakayetega sikio lake kuyasikia hayo? atakayesikiliza na kusikia kwa wakati ujao? Ni nani aliyemtoa Yakobo awe mateka, aliyemtia Israeli katika mikono ya wanyang’anyi? Si yeye, BWANA? yeye tuliyemkosa, ambaye hawakutaka kwenda katika njia zake, wala hawakuitii sheria yake. Kwa sababu hiyo alimwaga ukali wa hasira yake juu yake, na nguvu za vita; ukawasha moto wa kumzunguka pande zote, wala hakujua; ukamteketeza, wala hakuyatia hayo moyoni mwake.”—Isaya 42:22-25.

      28. (a) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa wakaaji wa Yuda? (b) Tunaweza kutafuta kibali cha Yehova jinsi gani?

      28 Kwa sababu wakaaji wake si waaminifu, Yehova anaruhusu nchi ya Yuda iporwe na kutekwa nyara mwaka wa 607 K.W.K. Wababiloni wanachoma hekalu la Yehova, wanafanya Yerusalemu ukiwa, na kupeleka Wayahudi mateka. (2 Mambo ya Nyakati 36:17-21) Na tuweke moyoni mfano huo wa kuonya, wala tusijitie uziwi wa kutosikia maagizo ya Yehova, wala tusijitie upofu wa kutoliona Neno lake lililoandikwa. Bali, na tutafute kibali cha Yehova kwa kumwiga Kristo Yesu, yule Mtumishi ambaye Yehova mwenyewe alikubali. Kama Yesu, na tujulishe haki ya kweli kwa yale tusemayo na kutenda. Kwa njia hiyo, tutabaki kati ya watu wa Yehova, tukitumikia tukiwa wachukua-nuru wanaomsifu Mungu wa kweli na kumpa utukufu.

      [Picha katika ukurasa wa 33]

      Haki ya kweli ina huruma na rehema

      [Picha katika ukurasa wa 34]

      Katika mfano wa yule Msamaria mwenye ujirani, Yesu alionyesha kwamba haki ya kweli inahusisha watu wote

      [Picha katika ukurasa wa 36]

      Kwa kuwatia wengine moyo na kuwafadhili, tunatenda haki ya kimungu

      [Picha katika ukurasa wa 39]

      Kupitia mahubiri yetu, tunaonyesha haki ya kimungu

      [Picha katika ukurasa wa 40]

      Mtumishi aliyekubaliwa alitolewa awe “nuru ya mataifa”

  • “Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Nne

      “Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!

      Isaya 43:1-28

      1. Yehova anatumiaje unabii, na watu wake wanapaswa kuitikiaje unabii uliotimizwa?

      UWEZO wa kutabiri wakati ujao ni jambo moja linalotofautisha Mungu wa kweli na miungu yote ya uwongo. Lakini Yehova anapotoa unabii, lengo lake si kuthibitisha Uungu wake tu. Kama inavyoonyeshwa katika Isaya sura ya 43, Yehova anatumia unabii kuthibitisha Uungu wake na pia kuthibitisha anawapenda watu wa agano lake. Nao watu wake hawapaswi kukaa kimya wakiisha kuutambua unabii uliotimizwa; wanapaswa kushuhudia mambo ambayo wameona. Ndiyo, wanapaswa kuwa mashahidi wa Yehova!

      2. (a) Israeli wana hali gani ya kiroho wakati wa Isaya? (b) Yehova anafunguaje macho ya watu wake?

      2 Kwa kuhuzunisha, kufikia wakati wa Isaya, hali ya Israeli inasikitisha sana hivi kwamba Yehova anaona watu hao kuwa wasiojiweza kiroho. “Walete vipofu walio na macho, na viziwi walio na masikio.” (Isaya 43:8) Vipofu na viziwi wa kiroho wanawezaje kumtumikia Yehova wakiwa mashahidi wake walio hai? Wanaweza kwa njia moja tu. Ni lazima macho na masikio yao yafunguliwe kimwujiza. Haya basi, Yehova anayafungua! Jinsi gani? Kwanza, Yehova anatoa nidhamu kali—wakaaji wa ufalme wa kaskazini wa Israeli wanaenda uhamishoni mwaka wa 740 K.W.K., kisha wale wa Yuda, mwaka wa 607 K.W.K. Halafu, Yehova anafanya tendo hodari kutetea watu wake kwa kuwakomboa na kuwarudisha mabaki waliotubu, waliotiwa upya nguvu za kiroho, kwenye nchi yao mwaka wa 537 K.W.K. Kwa kweli, Yehova ana uhakika sana kuwa hilo kusudi lake haliwezi kuzuiwa, hata anataja kukombolewa kwa Israeli miaka 200 hivi mapema kana kwamba kumekwisha kutukia.

      3. Yehova anawapa kitia-moyo gani wahamishwa hao wa wakati ujao?

      3 “BWANA aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza. Maana mimi ni BWANA, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako.”—Isaya 43:1-3a.

      4. Inakuwaje kwamba Yehova ni Muumba wa Israeli, naye anawapa watu wake uhakikisho gani kuhusu kuirudia nchi yao?

      4 Yehova anapendezwa kipekee na Israeli kwa sababu taifa hilo ni lake. Ni yeye mwenyewe ameliumba ili kutimiza agano la Kiabrahamu. (Mwanzo 12:1-3) Hivyo, Zaburi 100:3 inasema hivi: “Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu; ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.” Akiwa Muumba na Mkombozi wa Israeli, Yehova atawarudisha watu wake kwenye nchi yao wakiwa salama. Vizuizi kama maji mengi, mito yenye kufurika, na majangwa yenye moto, havitapunguza mwendo wao kama vile babu zao wa zamani hawakuzuiwa na vitu kama hivyo wakiwa njiani kwenda Nchi ya Ahadi miaka elfu moja mapema.

      5. (a) Maneno ya Yehova yanafariji Israeli wa kiroho jinsi gani? (b) Ni nani waandamani wa Israeli wa kiroho, nao walifananishwa na nani kimbele?

      5 Maneno ya Yehova yanawafariji pia mabaki wa kisasa wa Israeli wa kiroho, ambao washiriki wake ni “kiumbe kipya” kilichozaliwa kwa roho. (2 Wakorintho 5:17) Wakiisha kujitokeza watembee kwa ujasiri mbele ya “maji mengi,” yaani wanadamu, wamefurahia ulinzi wa Mungu wenye upendo wakapita gharika za mfano. Moto kutoka kwa adui zao haujawaumiza, bali umesaidia kuwatakasa. (Zekaria 13:9; Ufunuo 12:15-17) Ulinzi wa Yehova umeufikia pia “umati mkubwa” wa “kondoo wengine,” ambao wamejiunga na taifa la kiroho la Mungu. (Ufunuo 7:9; Yohana 10:16) Hawa walifananishwa kimbele na “kundi kubwa la watu waliochangamana mno,” walioondoka Misri pamoja na Waisraeli katika lile tukio la Kutoka; na pia walifananishwa kimbele na watu wasio Wayahudi waliorudi kutoka Babiloni pamoja na wahamishwa waliowekwa huru.—Kutoka 12:38; Ezra 2:1, 43, 55, 58.

      6. Yehova anajionyeshaje kuwa Mungu wa haki kwa kuwafidi (a) Israeli wa kimwili? (b) Israeli wa kiroho?

      6 Yehova anaahidi kuwakomboa watu wake kutoka Babiloni kwa kutumia majeshi ya Umedi na Uajemi. (Isaya 13:17-19; 21:2, 9; 44:28; Danieli 5:28) Kwa kuwa Yehova ni Mungu wa haki, atawalipa “wafanyakazi” wake Wamedi na Waajemi fidia inayofaa kwa kubadilishana na Israeli. “Nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.” (Isaya 43:3b, 4) Historia inathibitisha kwamba Milki ya Uajemi ilishinda Misri, Kushi (Ethiopia), na Seba iliyo karibu, sawa na vile Mungu alivyotabiri. (Mithali 21:18) Vivyo hivyo, mwaka wa 1919 Yehova alimtumia Yesu Kristo kuwafungua mabaki ya Israeli wa kiroho katika utekwa. Hata hivyo, Yesu hakuhitaji thawabu yoyote kwa huduma zake. Yeye hakuwa mtawala mpagani. Tena alikuwa akikomboa ndugu zake mwenyewe wa kiroho. Tena, Yehova alikuwa amekwisha kumpa “mataifa kuwa urithi [wake], na miisho ya dunia kuwa milki [yake]” katika mwaka wa 1914.—Zaburi 2:8.

      7. Yehova anahisije juu ya watu wake, nyakati za kale na za kisasa pia?

      7 Angalia jinsi Yehova anavyoonyesha wazi hisia zake nyororo kwa wahamishwa hao waliokombolewa. Anawaambia kwamba anawaona kuwa “wa thamani” na ‘wenye kuheshimiwa,’ na kwamba ‘anawapenda.’ (Yeremia 31:3) Anahisi hivyo hivyo—hata zaidi ya hivyo—kuelekea watumishi wake waaminifu-washikamanifu leo. Wakristo watiwa-mafuta wameletwa katika uhusiano pamoja na Mungu, si kwa kuzaliwa, bali kwa utendaji wa roho takatifu ya Mungu baada ya wakfu wao kwa Muumba wao. Yehova amewavuta waje kwa Mwanawe na kwake mwenyewe, akaandika sheria na kanuni zake juu ya mioyo yao yenye usikivu.—Yeremia 31:31-34; Yohana 6:44.

      8. Yehova anawapa wahamishwa uhakikisho gani, nao watahisi namna gani kuhusu ukombozi wao?

      8 Akiwapa wahamishwa hao uhakikisho zaidi, Yehova anaongezea hivi: “Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi; nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia. Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemwumba kwa ajili ya utukufu wangu; mimi nimemwumba, naam, mimi nimemfanya.” (Isaya 43:5-7) Hata miisho ya dunia haitakuwa mbali mno kwa Yehova wakati wake ufikapo wa kuwaweka huru wana wake na binti zake, na kuwarudisha kwenye nchi yao kipenzi. (Yeremia 30:10, 11) Bila shaka, wao wanaona kwamba ukombozi huu wa sasa utaupita kwa mbali ule ukombozi wa mapema wa taifa hilo kutoka Misri.—Yeremia 16:14, 15.

      9. Yehova anahusianisha matendo yake ya ukombozi na jina lake kwa njia zipi mbili?

      9 Kwa kuwakumbusha Israeli kwamba wanaitwa kwa jina lake, Yehova anahakikisha ahadi yake ya kuwakomboa. (Isaya 54:5, 6) Isitoshe, Yehova anahusianisha jina lake na ahadi zake za ukombozi. Kwa kufanya hivyo, anahakikisha kwamba ndiye atakayepokea utukufu neno lake litakapotimizwa. Hata mwenye kuishinda Babiloni hatastahili heshima iliyo haki ya Mungu mmoja tu aliye hai.

      Miungu Yafanyiwa Kesi

      10. Ni mwito gani wa ushindani ambao Yehova anaweka mbele ya mataifa na miungu yao?

      10 Sasa Yehova anafanya ile ahadi yake ya kuwaweka huru Israeli iwe msingi wa kuifanyia miungu ya mataifa kesi katika mahakama ya ulimwengu mzima. Tunasoma hivi: “Na wakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni [mwa miungu wao] awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonyesha mambo ya zamani? [Hao miungu wao] na walete mashahidi wao, wapate kuhesabiwa kuwa na haki; au na wasikie, wakaseme, Ni kweli.” (Isaya 43:9) Yehova anaweka mwito wa ushindani wa kuogopesha mbele ya mataifa ya ulimwengu. Ni kama anasema hivi: ‘Miungu yenu na ithibitishe kuwa ni miungu kwa kutabiri wakati ujao kwa usahihi.’ Kwa kuwa ni Mungu wa kweli tu anayeweza kutoa unabii bila kukosea, jaribu hili litafichua walaghai wote. (Isaya 48:5) Lakini Mweza Yote anaongeza takwa jingine la kisheria: Wote wanaodai kuwa miungu ya kweli lazima walete mashahidi wa kutetea matabiri yao na pia utimizo wake. Ni wazi kuwa Yehova hajiondoi katika takwa hilo la kisheria.

      11. Ni agizo gani ambalo Yehova anampa mtumishi wake, na Yehova anafunua nini juu ya Uungu wake?

      11 Miungu ya uwongo haiwezi kutokeza mashahidi maana haiwezi kitu. Basi aibu ndiyo hiyo, kizimba cha ushahidi kinabaki tupu. Lakini sasa ni wakati wa Yehova kuthibitisha Uungu wake. Akiwatazama watu wake, anasema hivi: “Ninyi ni mashahidi wangu, . . . na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni BWANA [“Yehova,” “NW”], zaidi yangu mimi hapana mwokozi. Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, . . . nami ni Mungu. Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye [kuuzuia mkono wangu]?”—Isaya 43:10-13.

      12, 13. (a) Watu wa Yehova wana ushuhuda gani mwingi wa kutoa? (b) Jina la Yehova limetokeaje waziwazi nyakati za kisasa?

      12 Kwa kuyaitikia maneno ya Yehova, umati wa mashahidi wenye shangwe unajaa upesi kizimbani. Ushuhuda wao ni wazi na hauwezi kukanushwa. Wao, kama vile Yoshua, wanashuhudia kwamba ‘yote aliyonena Yehova yametimia. Hapana neno lo lote limepungua.’ (Yoshua 23:14) Bado watu wa Yehova wanayakumbuka maneno ya Isaya, Yeremia, Ezekieli, na manabii wengine waliotabiri, kana kwamba ni kwa sauti moja, kuhamishwa kwa Yuda kisha kukombolewa kwao kimwujiza. (Yeremia 25:11, 12) Koreshi, mkombozi wa Yuda, alitajwa jina mapema sana hata kabla hajazaliwa!—Isaya 44:26–45:1.

      13 Ushuhuda chungu nzima umetolewa, basi nani atakataa kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli? Ni Yehova tu asiyeumbwa, tofauti na miungu ya kipagani; ni yeye tu Mungu wa kweli.a Basi, watu wanaoitwa kwa jina la Yehova wana pendeleo la kipekee, tena la kusisimua, kusimulia maajabu yake kwa vizazi vya wakati ujao, na kwa wengine wanaoulizia habari zake. (Zaburi 78:5-7) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wa kisasa wana pendeleo la kutangaza jina la Yehova duniani pote. Miaka ya 1920, Wanafunzi wa Biblia walizidi kufahamu umaana mkubwa wa jina la Mungu, Yehova. Kisha, Julai 26, 1931, kwenye mkusanyiko kule Columbus, Ohio, msimamizi wa Sosaiti, Joseph F. Rutherford, akatokeza azimio lenye kichwa “Jina Jipya.” Yale maneno, “Nasi twataka tujulikane na kuitwa kwa jina hili, yaani, mashahidi wa Yehova,” yalisisimua wahudhuriaji, sauti zao zikavuma “Ndiyo!” kwa kukubali azimio hilo. Tangu hapo, jina la Yehova limesifika ulimwenguni pote.—Zaburi 83:18.

      14. Yehova anawakumbusha nini Waisraeli, na kwa nini kikumbusha hicho ni cha wakati unaofaa?

      14 Yehova anawajali wale wanaoitwa kwa jina lake huku wakililetea heshima, na anawaona “kama mboni ya jicho” lake. Anawakumbusha Waisraeli hivyo kwa kuwaeleza jinsi alivyowakomboa kutoka Misri, akawaongoza salama kuvuka jangwa. (Kumbukumbu la Torati 32:10, 12) Wakati huo hakukuwa na mungu wa kigeni kati yao, maana walijionea miungu ya Misri ikiaibishwa kabisa. Ndiyo, miungu yote ya Misri haikuweza kulinda Misri wala kuzuia Israeli wasiondoke. (Kutoka 12:12) Vivyo hivyo, Babiloni hodari, ambayo ina mji wenye angalau mahekalu 50 ya miungu ya uwongo, haitaweza kuzuia mkono wa Mweza Yote anapowaweka huru watu wake. Ni wazi “hapana mwokozi” zaidi ya Yehova.

      Farasi wa Vita Waanguka, Magereza Yafunguka

      15. Yehova anatoa unabii gani kuhusu Babiloni?

      15 “BWANA, Mkombozi wenu, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Kwa ajili yenu nimetuma ujumbe Babeli nami nitawashusha wote mfano wa wakimbizi [“nitafanya mapingo ya magereza yaanguke chini,” “NW”], naam, Wakaldayo, katika merikebu zao walizozifurahia [“katika meli zao wakilia vilio virefu vikali vya kuomboleza,” “NW”]. Mimi ni BWANA, Mtakatifu wenu, Muumba wa Israeli, mfalme wenu. BWANA asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari; na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu; atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi.”—Isaya 43:14-17.

      16. Ni nini kitakachopata wafanyabiashara Wakaldayo, na watu wowote wanaotaka kulinda Babiloni?

      16 Babiloni ni kama gereza la wahamishwa hao kwa kuwa inawazuia kurudi Yerusalemu. Lakini vizuizi vya Babiloni si pingamizi kwa Mweza Yote, Yule ambaye zamani alifanya “njia katika bahari [Nyekundu]; na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu”—ambayo inaelekea kuwa ni yale ya Yordani. (Kutoka 14:16; Yoshua 3:13) Vivyo hivyo, Koreshi, mwakilishi wa Yehova, ataufanya Eufrati wenye nguvu upungue na kuruhusu mashujaa wake wa vita waingie jijini. Wafanyabiashara Wakaldayo wanaopita-pita katika mifereji ya Babiloni—yale mapito ya maji yanayotumiwa na maelfu ya merikebu za kibiashara na mashua zinazobeba miungu ya Babiloni—watalia kilio kirefu kikali cha kuomboleza wakati jiji lao kuu lenye nguvu liangukapo. Magari ya vita ya Babiloni yenye mbio yatakuwa bure, kama magari ya Farao katika Bahari Nyekundu. Hayataokoa jiji hilo. Kama vile ilivyo rahisi kuzima taa ya kibatari, mvamizi atauzima fyu uhai wa watu wowote wanaotaka kulinda jiji hilo.

      Yehova Awaongoza Watu Wake Salama Kwenda Nyumbani

      17, 18. (a) Yehova anatoa unabii wa jambo gani “jipya”? (b) Ni kwa njia gani watu hao hawapaswi kuyakumbuka mambo ya kwanza, na kwa nini?

      17 Yehova analinganisha matendo yake ya mapema ya ukombozi na tendo lile analokaribia kufanya, akisema: “Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu; watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.”—Isaya 43:18-21.

      18 Anaposema, “msiyakumbuke mambo ya kwanza,” Yehova hadokezi kwamba watumishi wake wafute akilini matendo yake yaliyopita ya wokovu. Mengi ya hayo ni sehemu ya historia ya Israeli iliyopuliziwa kimungu, na Yehova aliamuru kwamba lile tukio la kutoroka Misri likumbukwe kila mwaka kwenye mwadhimisho wa Kupitwa. (Mambo ya Walawi 23:5; Kumbukumbu la Torati 16:1-4) Hata hivyo, sasa Yehova anataka watu wake wamtukuze kwa sababu ya “neno jipya”—jambo watakalojionea wenyewe. Linatia ndani si ukombozi wao kutoka Babiloni tu, bali pia safari yao ya kurudi kwao kimwujiza, labda kwa kufuata ile njia ya moja kwa moja ya jangwani. Katika nchi hiyo tasa, Yehova atawafanyia “njia,” awafanyie maajabu yatakayowakumbusha yale aliyowafanyia Waisraeli siku za Musa—ndiyo, awalishe jangwani hao wenye kurudi, azime kiu yao kwa mito ya hakika. Yehova atawapa vitu vingi hivi kwamba hata wanyama wa mwituni watamtukuza Mungu waepuke kuwashambulia.

      19. Mabaki ya Israeli wa kiroho na waandamani wao wanatembeaje katika “Njia ya utakatifu”?

      19 Vivyo hivyo, mwaka wa 1919 mabaki ya Israeli wa kiroho waliwekwa huru kutoka utekwa wa Kibabiloni, wakaanza safari kufuata njia waliyotayarishiwa na Yehova, “Njia ya utakatifu.” (Isaya 35:8) Haikuwa lazima wapitie jangwa lenye joto kali kama Waisraeli, kutoka hapa kwenda hapa, wala safari yao haikwisha baada ya miezi michache ya kufika mahali fulani Yerusalemu. Hata hivyo, “Njia ya utakatifu” iliwaongoza mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta kuingia katika paradiso ya kiroho. Nao hubaki katika “Njia ya utakatifu,” maana ni lazima bado waendelee na safari kuuvuka mfumo huu wa mambo. Mradi wanabaki katika ile njia kuu—mradi wanashika viwango vya Mungu vya usafi na utakatifu—wanabaki katika paradiso ya kiroho. Na wanapata shangwe iliyoje wakati umati mkubwa wa waandamani wao ‘wasio Waisraeli’ wanapojiunga nao! Mabaki na pia waandamani wao wanaendelea kufurahia mlo mnono wa kiroho mkononi mwa Yehova, tofauti kabisa na watu wanaotegemea mfumo wa Shetani. (Isaya 25:6; 65:13, 14) Watu wengi wenye tabia za kinyama wamebadili njia zao na kumtukuza Mungu wa kweli baada ya kuona baraka ya Yehova juu ya watu wake.—Isaya 11:6-9.

      Yehova Afunua Maumivu Yake

      20. Ni jinsi gani Israeli wa siku za Isaya hakutimiza takwa la Yehova?

      20 Nyakati za kale mabaki waliorudishwa wa Israeli wanaonekana kuwa watu waliobadilika wanapolinganishwa na kizazi kiovu cha Isaya. Kuhusu kizazi hicho kiovu, Yehova anasema hivi: “Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli. Hukuniletea wana-kondoo kuwa kafara zako, wala hukuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukutumikisha kwa matoleo, wala sikukuchosha kwa ubani. Hukuninunulia manukato [“kikonyo kitamu,” “NW”] kwa fedha, wala hukunishibisha kwa mafuta ya sadaka zako; bali umenitumikisha kwa dhambi zako, umenichosha kwa maovu yako.”—Isaya 43:22-24.

      21, 22. (a) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba matakwa ya Yehova si mzigo? (b) Ni kwa njia gani watu hao ni kama wanamlazimisha Yehova awatumikie?

      21 Anaposema, “Sikukutumikisha kwa matoleo, wala sikukuchosha kwa ubani,” Yehova hatoi wazo la kwamba dhabihu na ubani (sehemu mojawapo ya uvumba mtakatifu) hazihitajiwi. Kwa kweli, hizo ni sehemu muhimu ya ibada ya kweli chini ya agano la Sheria. Ndivyo na “kikonyo,” kishina chenye manukato, kimojawapo cha vichanganyo vya kutayarisha mafuta matakatifu ya kupaka watu. Waisraeli wamekuwa wakipuuza vitu hivyo kwa kutovitumia katika utumishi wa hekalu. Lakini je, matakwa hayo ni mzigo wa kulemea? Sivyo kamwe! Matakwa ya Yehova ni mepesi kwa kulinganishwa na ya miungu ya uwongo. Kwa mfano, yule mungu wa uwongo Moleki alidai watoto watolewe dhabihu kwake—jambo ambalo Yehova hajawahi kulitaka kamwe!—Kumbukumbu la Torati 30:11; Mika 6:3, 4, 8.

      22 Laiti Waisraeli wangekuwa na utambuzi wa kiroho, kwani ‘hawangechoshwa na Yehova’ kamwe. Kwa kuichunguza Sheria yake, wangeona kwamba anawapenda sana kisha wamtolee “mafuta,” yaani sehemu bora zaidi ya dhabihu zao. Badala ya hivyo, wanajiwekea kwa pupa mafuta hayo. (Mambo ya Walawi 3:9-11, 16) Kweli taifa hilo ovu linamsumbua Yehova kwa mzigo wa dhambi zao—ni kama kumlazimisha yeye awatumikie!—Nehemia 9:28-30.

      Nidhamu Yatokeza Matunda

      23. (a) Kwa nini nidhamu ya Yehova inastahiliwa sana? (b) Ni nini kinachohusika katika tendo la Mungu la kutia Israeli nidhamu?

      23 Ingawa nidhamu ya Yehova ni kali, na inastahili kuwa hivyo, inatimiza matokeo yaliyotakiwa, kufanya rehema iwezekane. “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako. Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako. Baba yako wa kwanza alifanya dhambi, na wakalimani wako wameniasi. Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa patakatifu, nami nitamfanya Yakobo kuwalaani [“kama mtu wa kuharibiwa,” “NW”], na Israeli kuwa tukano.” (Isaya 43:25-28) Kama mataifa yote ya ulimwengu, Israeli ametokana na Adamu, yule “wa kwanza.” Kwa hiyo, hakuna Mwisraeli anayeweza kujithibitisha kuwa yeye ni mwenye “haki.” Hata “wakalimani” wa Israeli—walimu au wafafanuzi wake wa Sheria—wamemtenda Yehova dhambi na kufundisha uwongo mwingi. Basi Yehova naye atalitoa taifa lake zima liingie katika ‘uharibifu’ na “tukano.” Pia atawatia unajisi wote wanaofanya kazi rasmi kwenye “patakatifu” pake.

      24. Ni kwa msingi gani Yehova atasamehe watu wake—wa kale na wa kisasa—lakini yeye ana hisia zipi kuwaelekea?

      24 Ingawa hivyo, ona kwamba rehema ya kimungu haitapatikana kwa sababu ya kusikitika kwa Israeli tu; itakuwa kwa ajili ya Yehova mwenyewe. Ndiyo, jina lake linahusika. Kama angeacha Israeli kwenye uhamisho wa kudumu, jina lake mwenyewe lingesutwa na watazamaji. (Zaburi 79:9; Ezekieli 20:8-10) Leo vilevile, umuhimu wa wokovu wa wanadamu ni mdogo kuliko umuhimu wa kutakaswa kwa jina la Yehova na kutetewa kwa enzi yake kuu. Hata hivyo, Yehova huwapenda wale wanaokubali nidhamu yake bila moyo nusunusu, na kumwabudu kwa roho na kweli. Wawe ni watiwa-mafuta au kondoo wengine, yeye huwaonyesha upendo wake kwa kufuta makosa yao kwa msingi wa dhabihu ya Yesu Kristo.—Yohana 3:16; 4:23, 24.

      25. Ni mambo gani ya kuogopesha ambayo Yehova atafanya karibuni, nasi tunaweza kuonyeshaje uthamini wetu sasa?

      25 Tena, karibuni Yehova ataonyesha anapenda umati mkubwa wa waabudu wake waaminifu-washikamanifu atakapotenda jambo jipya kwa ajili yao kwa kuwakomboa wapite “dhiki kubwa” waingie “dunia mpya” iliyosafishwa. (Ufunuo 7:14; 2 Petro 3:13) Watashuhudia wonyesho wa kuogopesha wa uwezo wa Yehova ambao haujapata kuonwa na wanadamu. Tazamio hakika la tukio hilo hufanya mabaki watiwa-mafuta na wote watakaojumlika kuwa umati mkubwa washangilie na kuishi kila siku kulingana na lile agizo tukufu: “Ninyi ni mashahidi wangu”!—Isaya 43:10.

      [Maelezo ya Chini]

      a Katika hadithi za mataifa, miungu mingi “huzaliwa” na huzaa “watoto.”

      [Picha katika ukurasa wa 48, 49]

      Yehova atategemeza Wayahudi wakiwa njiani kurudi kwao Yerusalemu

      [Picha katika ukurasa wa 52]

      Yehova hutolea mataifa mwito wa ushindani watokeze mashahidi wa kutetea miungu yao

      1. Sanamu ya Baali ya shaba nyeusi 2. Visanamu vya udongo vya Ashtorethi  3. Utatu wa Kimisri wa Horusi, Osirisi, na Isisi  4. Miungu ya Kigiriki Athena (kushoto) na Afrodaiti

      [Picha katika ukurasa wa 58]

      “Ninyi ni mashahidi wangu.”—Isaya 43:10

  • Mungu wa Kweli Anatabiri Ukombozi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Tano

      Mungu wa Kweli Anatabiri Ukombozi

      Isaya 44:1-28

      1, 2. (a) Yehova anatokeza maswali gani? (b) Yehova atathibitishaje kuwa ni yeye tu aliye Mungu wa kweli?

      ‘MUNGU wa kweli ni nani?’ Swali hilo limeulizwa karne zote. Basi, inashangaza kwamba Yehova mwenyewe anatokeza swali hilo katika kitabu cha Isaya! Anakaribisha wanadamu kufikiria jambo hili: ‘Je, Yehova tu ndiye Mungu wa kweli? Au kuna mwingine wa kushindana na cheo chake?’ Baada ya kuanzisha mazungumzo, Yehova anaweka vipimo vizuri vya kutatua suala la Uungu. Kusababu kunakotokezwa huwaongoza wanyofu kufikia uamuzi mmoja tu usiokanushika.

      2 Siku za Isaya, mifano inaabudiwa mahali pengi. Katika mazungumzo ya wazi kabisa yaliyoandikwa katika sura ya 44 ya kitabu cha unabii cha Isaya, ibada ya mifano inaonyeshwa kuwa ni ya bure kabisa! Hata hivyo, watu wa Mungu mwenyewe wametumbukia katika mtego wa kuabudu sanamu. Kwa hiyo, kama ilivyoonwa katika sura zilizotangulia za Isaya, Waisraeli wanaelekea kutiwa nidhamu kali. Ingawa hivyo, Yehova anahakikishia taifa hilo kwa upendo kwamba, ingawa ataruhusu Wababiloni wawapeleke watu wake utekwani, atawakomboa kwa wakati wake mwenyewe. Utimizo wa unabii mbalimbali unaohusu kukombolewa kutoka utekwani na kurudishwa kwa ibada safi utathibitisha pasipo shaka kwamba Yehova tu ndiye Mungu wa kweli, kisha iwe aibu kwa wote wanaoabudu miungu ya mataifa isiyo na uhai.

      3. Maneno ya kiunabii ya Isaya yanawasaidiaje Wakristo leo?

      3 Unabii mbalimbali katika sehemu hii ya Isaya na utimizo wake nyakati za kale unatia nguvu imani ya Wakristo leo. Zaidi ya hilo, maneno ya kiunabii ya Isaya yana utimizo siku zetu na hata wakati ujao. Na matukio hayo yanahusisha mkombozi na ukombozi mkubwa kuliko ule uliotabiriwa kwa ajili ya watu wa Mungu wa kale.

      Tumaini kwa Wale Walio wa Yehova

      4. Yehova anamtiaje moyo Israeli?

      4 Sura ya 44 inaanza kwa mwelekeo mzuri ikiwa na kikumbusha cha kwamba Israeli amechaguliwa na Mungu, akatenganishwa na mataifa yanayomzunguka ili awe mtumishi wake. Unabii huo unasema hivi: “Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua; BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.” (Isaya 44:1, 2) Yehova amemtunza Israeli tangu alipoanza kuwa taifa baada ya kutoka Misri, ikawa ni kana kwamba anamtunza kuanzia tumbo la uzazi la mama yake. Anawaita watu wake kwa ujumla “Yeshuruni,” maana yake “Aliye Mnyofu,” mtajo unaoonyesha upendo na wororo. Pia jina hilo ni kikumbusha cha kwamba lazima Waisraeli wabaki wanyoofu, kwani wameshindwa kufanya hivyo mara nyingi.

      5, 6. Yehova anampa Israeli viburudisho gani, na tokeo ni nini?

      5 Maneno ya Yehova yanayofuata yanaburudisha kama nini! Anasema hivi: “Nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.” (Isaya 44:3, 4) Hata katika nchi kavu yenye joto, miti inaweza kusitawi pamoja kwa mfuatano kando ya chemchemi za maji. Yehova atakapoandaa maji yake mengi ya ukweli yanayowapa watu uhai, akimimina pia roho yake takatifu, Israeli atasitawi sana, kama miti kandokando ya mitaro ya maji ya kulimia. (Zaburi 1:3; Yeremia 17:7, 8) Yehova atawatia nguvu watu wake wamalize kazi yao ya kuwa mashahidi wa Uungu wake.

      6 Tokeo moja la huku kumiminwa kwa roho takatifu ni kwamba watu fulani mmoja-mmoja watathamini upya uhusiano wa Israeli pamoja na Yehova. Hivyo, tunasoma hivi: “Mmoja atasema, Mimi ni wa BWANA [“Yehova,” “NW”]; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa BWANA [“Yehova,” “NW”], na kujiita kwa jina la Israeli.” (Isaya 44:5) Ndiyo, itakuwa heshima kubeba jina la Yehova, kwani ataonwa kuwa ni yeye tu aliye Mungu wa kweli.

      Mwito wa Ushindani kwa Miungu

      7, 8. Yehova anaitoleaje miungu ya mataifa mwito wa ushindani?

      7 Chini ya Sheria ya Kimusa, mkombozi—kwa kawaida mwanamume aliye jamaa wa karibu—angeweza kumnunua mtu wake kutoka utumwani. (Mambo ya Walawi 25:47-54; Ruthu 2:20) Sasa Yehova anajitambulisha kuwa Mkombozi wa Israeli—ambaye atalikomboa taifa, hata Babiloni na miungu yake yote ione aibu. (Yeremia 50:34) Yehova anaikabili miungu ya uwongo na waabudu wake, akisema: “BWANA, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, BWANA wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu. Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze. Msiogope wala msifanye hofu; je! sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? na ninyi ni mashahidi wangu. Je! yuko Mungu zaidi yangu mimi? hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.”—Isaya 44:6-8.

      8 Yehova anatokeza ushindani kwamba miungu ijitetee. Je, wanaweza kutaja mambo yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako, kuyatabiri yajayo kwa usahihi hata ionekane ni kama tayari yanatendeka? Anayeweza kufanya hivyo ni yule tu ‘wa kwanza na wa mwisho,’ aliyekuwako kabla ya miungu yote ya uwongo kuwaziwa, na ambaye bado atakuwako muda mrefu baada ya miungu hiyo kutokomea. Watu wake hawahitaji kuogopa kutoa ushahidi kuhusu kweli hiyo kwa kuwa wanategemezwa na Yehova, aliye imara na thabiti kama mwamba mkubwa sana!—Kumbukumbu la Torati 32:4; 2 Samweli 22:31, 32.

      Ubatili wa Kuabudu Mifano

      9. Je, lilikuwa kosa kwa Waisraeli kufanya aina yoyote ya kiwakilishi cha kitu kilicho hai? Eleza.

      9 Mwito wa ushindani wa Yehova kwa miungu ya uwongo unakumbusha mtu ile amri ya pili kati ya zile Amri Kumi. Amri hiyo ilisema hivi: “Usijifanyie sanamu ya [“mfano wa,” NW] kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia.” (Kutoka 20:4, 5) Bila shaka, katazo hilo halikumaanisha kwamba Waisraeli hawakupaswa kufanya viwakilishi vya mapambo. Yehova mwenyewe alielekeza kwamba viwakilishi vya mimea na makerubi viwekwe katika tabenakulo. (Kutoka 25:18, 33; 26:31) Lakini, havikupasa kuheshimiwa kwa kicho wala kuabudiwa. Hakuna aliyepaswa kuvitolea sala au dhabihu viwakilisho hivyo. Amri iliyopuliziwa na Mungu ilikataza kufanyiza aina yoyote ya mfano kwa matumizi ya ibada. Kuabudu mifano au kuiinamia kwa heshima yenye kicho ni kuabudu sanamu.—1 Yohana 5:21.

      10, 11. Kwa nini Yehova anaiona mifano kuwa aibu?

      10 Sasa Isaya anaeleza ubatili wa mifano isiyo hai na aibu inayowangoja wale wanaoifanyiza: “Wachongao sanamu [“mifano,” “NW”], wote ni ubatili; wala mambo yao yawapendezayo hayatafaa kitu; wala mashahidi wao wenyewe hawaoni, wala hawajui; ili watahayarike. Ni nani aliyejichongea mungu mmoja, au aliyesubu sanamu isiyofaa kitu [“mfano duni wa kuyeyushwa,” “NW”]? Tazama, wenziwe wote watatahayari; na mafundi, hao ni wanadamu; na wakusanyike pamoja, wakasimame; wataogopa na kutahayari pamoja.”—Isaya 44:9-11.

      11 Kwa nini Mungu anaiona mifano hiyo kuwa ya aibu sana? Kwanza, haiwezekani kumwakilisha Mweza Yote kwa kutumia vitu halisi vinavyoonekana. (Matendo 17:29) Tena, kuabudu kiumbe badala ya Muumba ni kukaidi Uungu wa Yehova. Na je, kufanya hivyo si kushusha heshima ya mwanadamu, aliyeumbwa “kwa mfano wa Mungu”?—Mwanzo 1:27; Waroma 1:23, 25.

      12, 13. Kwa nini mwanadamu hawezi kuunda mfano wowote unaostahili kuabudiwa?

      12 Je, kitu halisi kinaweza kupata utakatifu kwa njia fulani eti kwa sababu kimeundwa ili kiabudiwe? Isaya anatukumbusha kwamba kutengeneza mfano ni kazi ya binadamu tu. Vyombo na maarifa yanayotumiwa na mtengeneza-mifano ni sawa na vile vya fundi mwingine yeyote: “Mfua chuma hufanza shoka, hufanya kazi kwa makaa, huitengeneza sanamu kwa nyundo, huifanyiza kwa nguvu za mkono wake; naam, huona njaa, nguvu zake zikampungukia; asipokunywa maji huzimia. Seremala hunyosha uzi; huiandika kwa kalamu ya mate; huitengeneza kwa randa, huiandika kwa bikari, huifanza kwa mfano wa mwanadamu, sawasawa na uzuri wa mwanadamu, ili ikae nyumbani.”—Isaya 44:12, 13.

      13 Mungu wa kweli aliumba vitu vyote vilivyo hai juu ya dunia hii, kutia na mwanadamu. Viumbe vyenye fahamu vinashuhudia vizuri sana Uungu wa Yehova, lakini ni wazi kuwa viumbe vyote vya Yehova vina cheo kidogo kuliko yeye. Je, inawezekana mwanadamu afanye makubwa zaidi ya hayo? Je, anaweza kutengeneza kitu kilicho na cheo kikubwa kuliko yeye mwenyewe—kiwe na cheo kikubwa sana hata kistahili ujitoaji wake? Mwanadamu anapotengeneza mfano, yeye huchoka, huona njaa, na kiu. Hayo ni mapungufu ya kibinadamu, lakini angalau yanaonyesha kwamba mwanadamu huyo yuko hai. Ule mfano anaotengeneza huenda ukafanana na mwanadamu. Huenda hata ukawa maridadi. Lakini hauna uhai. Mifano si miungu kamwe. Isitoshe, hakuna mfano wowote wa kuchongwa ambao umewahi ‘kuanguka kutoka mbinguni,’ kana kwamba aliyeutengeneza si mwanadamu anayekufa.—Matendo 19:35.

      14. Watengeneza-mifano wanamtegemea Yehova kabisa kwa jinsi gani?

      14 Isaya anaendelea kuonyesha kwamba watengeneza-mifano hutegemea kabisa taratibu za kiasili na vitu vilivyoumbwa na Yehova: “Yeye hujikatia mierezi, hutwaa mtiriza, na mwaloni, hujichagulia mti mmoja katika miti ya msituni; hupanda mvinje, mvua ikausitawisha. Kisha utamfaa mwanadamu kwa kuni; hutwaa kipande, akaoka mkate; naam, huufanya mungu, akauabudu; huifanya sanamu ya [“mfano wa,” “NW”] kuchonga, akaisujudia. Sehemu moja huiteketeza; kwa sehemu nyingine hula nyama; huoka chakula kiokwacho, akashiba; naam, huota moto, akasema, Aha, nimeota moto, nimeona moto; na kwa sehemu iliyobakia hufanya mungu, yaani, sanamu yake ya [“mfano wa,” “NW”] kuchonga; husujudu mbele yake akaiabudu, akaiomba, akasema, Uniokoe; maana wewe u mungu wangu.”—Isaya 44:14-17.

      15. Mtengeneza-mifano huonyesha hafahamu nini hata kidogo?

      15 Je, ukuni ambao haujachomeka unaweza kukomboa mtu yeyote? Wapi. Mungu wa kweli tu ndiye anayeweza kukomboa. Watu wanawezaje kuabudu sanamu zisizo hai? Isaya anaonyesha kwamba tatizo halisi limo moyoni mwa mtu: “Hawajui wala hawafikiri; maana amewafumba macho, wasione, na mioyo yao, wasiweze kufahamu. Wala hapana atiaye moyoni, wala hapana maarifa, wala fahamu kusema, Nimeteketeza sehemu motoni, naam, pia nimeoka mkate juu ya makaa yake; nimeoka nyama nikaila; nami, je! kilichobaki nikifanye kuwa chukizo? Je! nisujudie shina la mti? Hula majivu; moyo uliodanganyika umempotosha, asiweze kuiokoa nafsi yake, wala kusema, Je! sio uongo mkononi mwangu?” (Isaya 44:18-20) Ndiyo, kufikiri kwamba ibada ya sanamu ina mafaa yoyote ya kiroho ni kama kula majivu badala ya chakula chenye lishe.

      16. Ibada ya sanamu ilianzaje, nayo huwezekana kwa nini?

      16 Kwa kweli ibada ya sanamu ilianza katika mbingu wakati kiumbe-roho hodari, aliyekuja kuwa Shetani, alipotamani ibada iliyo haki ya Yehova tu. Tamaa ya Shetani ilikuwa kali sana hata ikamtenga na Mungu. Huo ukawa hasa ndio mwanzo wa ibada ya sanamu, kwa kuwa mtume Paulo alisema kutamani ni sawa na ibada ya sanamu. (Isaya 14:12-14; Ezekieli 28:13-15, 17; Wakolosai 3:5) Shetani aliwashawishi wanadamu wawili wa kwanza wafikirie-fikirie mawazo ya ubinafsi. Hawa alitamani toleo la Shetani: “Mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” Yesu alisema kwamba kutamani hutoka ndani ya moyo. (Mwanzo 3:5; Marko 7:20-23) Ibada ya sanamu huwezekana wakati mioyo inapotiwa ufisadi. Basi, ni muhimu sana sote ‘tulinde mioyo yetu,’ tusiruhusu kamwe mtu yeyote au kitu chochote kichukue nafasi iliyo haki ya Yehova!—Mithali 4:23; Yakobo 1:14.

      Yehova Huvutia Mioyo

      17. Israeli anapaswa kukumbuka nini sana?

      17 Kisha Yehova anawasihi Waisraeli wakumbuke kwamba wamo katika cheo chenye pendeleo na daraka. Wao ni mashahidi wake! Anasema hivi: “Kumbuka haya, Ee Yakobo; nawe Israeli, maana wewe u mtumishi wangu; nimekuumba; u mtumishi wangu; Ee Israeli, hutasahauliwa na mimi. Nimeyafuta makosa yako kama wingu zito, na dhambi zako kama wingu; unirudie; maana nimekukomboa. Imbeni, enyi mbingu, maana BWANA ametenda hayo; pigeni kelele, enyi mabonde ya nchi; pazeni nyimbo, enyi milima; nawe, msitu, na kila mti ndani yake. Maana BWANA amemkomboa Yakobo, naye atajitukuza katika Israeli.”—Isaya 44:21-23.

      18. (a) Kwa nini Israeli ana sababu ya kushangilia? (b) Watumishi wa Yehova wanaweza kuigaje kielelezo chake cha rehema leo?

      18 Si Israeli aliyemfanyiza Yehova. Yeye si mungu wa kutengenezwa na mwanadamu. Bali, Yehova ndiye aliyemfanyiza Israeli kuwa mtumishi wake mteule. Naye atathibitisha Uungu wake tena atakapolikomboa taifa hilo. Anasema na watu wake kwa wororo, akiwahakikishia atafunika dhambi zao kabisa wakitubu, afiche makosa yao kana kwamba anayaficha nyuma ya mawingu yasiyopenyeka. He, kweli Israeli wana sababu nzuri sana ya kushangilia! Kielelezo cha Yehova husukuma watumishi wake wa kisasa waige rehema yake. Wanaweza kufanya hivyo kwa kujitahidi kuwasaidia wakosaji—kujaribu kuwaimarisha upya kiroho, ikiwezekana.—Wagalatia 6:1, 2.

      Upeo wa Kutahini Uungu

      19, 20. (a) Yehova anafikisha kesi yake kwenye upeo kwa njia gani? (b) Yehova anawatolea watu wake unabii wa mambo gani yenye kuchangamsha, na ni nani atakuwa mwakilishi wake wa kuyatimiza?

      19 Yehova sasa analeta hoja yake ya kisheria kwenye upeo mpevu. Yeye mwenyewe anakaribia kuujibu mtihani mkali kupita wote wa Uungu wake, yaani, kama kweli anaweza kutabiri wakati ujao kwa usahihi. Msomi mmoja wa Biblia aliiita mistari mitano inayofuata ya Isaya sura ya 44, “shairi lisilo na kifani la Mungu wa Israeli,” yule Muumba mmoja, tena mmoja tu, aliye Mfunuaji pekee wa wakati ujao na tumaini la ukombozi wa Israeli. Maelezo ya kifungu hicho yanafikia upeo wenye kuvutia sana hatua kwa hatua kwa kutangaza jina la mwanamume atakayekomboa taifa hilo kutoka Babiloni.

      20 “BWANA, mkombozi wako, yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi; Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote; nizitandaye mbingu peke yangu; niienezaye nchi; ni nani aliye pamoja nami? nizitanguaye ishara za waongo, na kuwatia waganga wazimu; niwarudishaye nyuma wenye hekima, na kuyageuza maarifa yao kuwa ujinga; nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka; niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako; nimwambiaye Koreshi, Mchungaji wangu, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa.”—Isaya 44:24-28.

      21. Maneno ya Yehova yanaandaa uhakikisho gani?

      21 Ndiyo, si kwamba Yehova ana uwezo wa kutabiri matukio ya wakati ujao tu, bali pia ana uwezo wa kutimiza kusudi lake lote lililofunuliwa. Tangazo hili litawapa Israeli tumaini. Huo ni uhakikisho kamili kwamba majeshi ya Babiloni yajapoiacha nchi ukiwa, Yerusalemu na majiji yanayoitegemea itainuka tena, na ibada ya kweli itasimamishwa upya huko. Lakini jinsi gani?

      22. Eleza Mto Eufrati unakauka jinsi gani.

      22 Kwa kawaida waaguzi wasiopuliziwa hawathubutu kutabiri mambo hususa, kwa kuhofu kwamba watathibitishwa kuwa waongo baada ya muda. Lakini Yehova ni tofauti kwa sababu anafunua kupitia Isaya jina hususa la mwanamume ambaye Yeye atamtumia kuwaweka huru watu wake watoke utekwani, waweze kwenda nyumbani wakajenge upya Yerusalemu na hekalu. Jina lake ni Koreshi, na anajulikana kuwa Koreshi Mkuu wa Uajemi. Yehova anatoa hata maelezo madogo-madogo kuhusu maarifa ambayo Koreshi atatumia kuupenya mfumo mkubwa sana wa Babiloni ulio na kinga nyingi. Babiloni italindwa na kuta ndefu na mapito ya maji yanayotiririka ndani ya jiji na vizingo vyake. Koreshi atageuza sehemu kubwa ya mfumo huo—ule Mto Eufrati—itimize lengo lake. Kulingana na wanahistoria wa kale Herodotus na Xenophon, katika upande fulani wa juu wa Babiloni, Koreshi aliyaelekeza kando maji mengi ya Mto Eufrati maji yakapungua kiasi cha askari zake kupita kwa miguu. Eufrati unakauka kwa maana ya kwamba hauwezi kulinda Babiloni.

      23. Kuna maandishi gani ya kuonyesha utimizo wa ule unabii wa kwamba Koreshi angekomboa Israeli?

      23 Namna gani ile ahadi ya kwamba Koreshi atawafungua watu wa Mungu na kwamba atahakikisha Yerusalemu na hekalu vitajengwa upya? Koreshi mwenyewe, katika tangazo rasmi lililohifadhiwa katika Biblia, anatangaza hivi: “Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; BWANA, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, BWANA, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya BWANA, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.” (Ezra 1:2, 3) Ahaa! Neno la Yehova kupitia Isaya limetimizwa kabisa.

      Isaya, Koreshi, na Wakristo Leo

      24. Kutokezwa kwa amri ya Artashasta ya “kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu” kuna uhusiano gani na kuja kwa Mesiya?

      24 Sura ya 44 ya Isaya humtukuza Yehova kuwa Mungu mmoja tu wa kweli na Mkombozi wa watu wake wa kale. Tena, leo unabii huo una maana ya ndani sana kwetu. Amri ya Koreshi ya kujenga upya hekalu la Yerusalemu, iliyotolewa mwaka wa 538/537 K.W.K., ilianzisha matukio yaliyofikia upeo katika utimizo wa unabii mwingine wa ajabu. Amri ya Koreshi ilifuatwa na ile amri ya mtawala wa baadaye, Artashasta, aliyeamuru jiji la Yerusalemu lijengwe upya. Kitabu cha Danieli kilifunua kwamba “tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu [mwaka wa 455 K.W.K.] hata zamani zake masihi aliye mkuu,” kungekuwa na “majuma” 69, kila juma likiwa miaka 7. (Danieli 9:24, 25) Unabii huo pia ulitimia. Bila kuchelewa hata kidogo, mwaka wa 29 W.K., miaka 483 baada ya amri ya Artashasta kutimia katika Nchi ya Ahadi, Yesu alibatizwa akaanza huduma yake ya kidunia.a

      25. Anguko la Babiloni mikononi mwa Koreshi linaelekeza kwenye nini nyakati za kisasa?

      25 Kufunguliwa kwa Wayahudi waaminifu-washikamanifu uhamishoni, ambako kuliwezekana Babiloni ilipoanguka, kulikuwa kivuli cha kufunguliwa kwa Wakristo watiwa-mafuta kutoka uhamisho wa kiroho mwaka wa 1919. Kufunguliwa huko kulithibitisha kwamba Babiloni mwingine, anayefafanuliwa kuwa kahaba, Babiloni Mkubwa—anayefananisha dini za uwongo za ulimwengu zikiwa zote pamoja kwa ujumla—alikuwa ameanguka. Mtume Yohana aliona mapema anguko la mwanamke huyo, kama lilivyoandikwa katika kitabu cha Ufunuo. (Ufunuo 14:8) Pia aliuona mapema uharibifu wake wa ghafula. Maelezo ya Yohana kuhusu uharibifu wa milki hiyo ya ulimwengu iliyojaa sanamu kochokocho yanafanana kwa njia fulani-fulani na maelezo ya Isaya kuhusu ushindi wa Koreshi juu ya jiji la kale la Babiloni. Sawa na vile mapito ya maji yenye kulinda Babiloni yalivyoshindwa kuokoa jiji hilo kutoka kwa Koreshi, hivyo ndivyo ‘maji,’ yaani wanadamu wanaotegemeza na kulinda Babiloni Mkubwa, ‘yatakavyokaushwa’ kabla mwanamke huyo hajaharibiwa impasavyo.—Ufunuo 16:12.b

      26. Unabii wa Isaya na utimizo wake unaitiaje nguvu imani yetu?

      26 Hapo tulipo, milenia zaidi ya mbili na nusu baada ya Isaya kutoa unabii wake, tunaweza kuona kwamba kweli Mungu ‘huyafikiliza mashauri ya wajumbe wake.’ (Isaya 44:26) Basi, utimizo wa unabii wa Isaya ni mfano wa kutokeza unaoonyesha kutumainika kwa unabii wote wa Maandiko Matakatifu.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona sura ya 11 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      b Ona sura ya 35 na ya 36 katika kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      [Picha katika ukurasa wa 63]

      Je, ukuni ambao haujachomeka unaweza kukomboa mtu yeyote?

      [Picha katika ukurasa wa 73]

      Kichwa cha marimari cha mfalme fulani wa Iran, ambaye yawezekana ni Koreshi

      [Picha katika ukurasa wa 75]

      Koreshi atimiza unabii kwa kuyaelekeza kando maji mengi ya Mto Eufrati

  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Sita

      Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”

      Isaya 45:1-25

      1, 2. Ni mahakikisho gani yanayotolewa katika Isaya sura ya 45, na ni maswali gani yatakayochunguzwa?

      AHADI za Yehova zinategemeka. Yeye ndiye Mungu wa ufunuo, na tena ndiye Mungu wa uumbaji. Tena na tena amekuwa Mungu mwenye haki na mwokozi wa watu wa mataifa yote. Hayo ndiyo baadhi ya uhakikisho wa kuchangamsha moyo unaopatikana katika Isaya sura ya 45.

      2 Zaidi ya hayo, Isaya sura ya 45 ina mfano mzuri ajabu unaoonyesha kwamba Yehova ana uwezo wa kutoa unabii. Roho ya Mungu inamwezesha Isaya kukazia macho nchi za mbali na kukagua matukio ya karne zitakazokuja, kisha roho hiyo inamsukuma kusimulia tukio ambalo ni Yehova tu, yule Mungu wa unabii wa kweli, angeweza kutabiri kwa usahihi sana hivyo. Hilo ni tukio gani? Nalo lina matokeo gani juu ya watu wa Mungu katika siku za Isaya? Tena lina umaana gani kwetu leo? Acheni tuyachunguze maneno ya nabii huyo.

      Tangazo Rasmi la Yehova Kupinga Babiloni

      3. Isaya 45:1-3a inasimulia ushindi wa Koreshi kwa maneno gani dhahiri?

      3 “Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kuume, ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza viuno vya wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa. Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma; nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri.”—Isaya 45:1-3a.

      4. (a) Kwa nini Yehova anamwita Koreshi “masihi” wake? (b) Yehova atamhakikishiaje Koreshi ushindi?

      4 Yehova anamtumia Isaya kumtaja Koreshi kana kwamba yuko hai, ingawa Koreshi bado hajazaliwa siku za Isaya. (Waroma 4:17) Kwa kuwa Yehova anamweka rasmi Koreshi mapema ili atimize kazi fulani hususa, Koreshi anaweza kusemwa kuwa ni “masihi” wa Mungu. Koreshi ataongozwa na Mungu kutiisha mataifa, awadhoofishe wafalme na kuwamaliza nguvu za ukinzani. Kisha, Koreshi ashambuliapo Babiloni, Yehova atahakikisha kwamba milango ya jiji imeachwa wazi, aifanye iwe ovyo kama malango ambayo yamekwisha kuvunjwa-vunjwa. Ataenda mbele ya Koreshi, akitandaza vipingamizi vyote. Mwishowe, vikosi vya Koreshi vitalishinda jiji na kutwaa “mali zilizofichwa” humo, utajiri wake uliowekwa katika ghala za gizani. Isaya anatabiri hivyo. Je, maneno yake yanatimia?

      5, 6. Unabii wa anguko la Babiloni unatimia wakati gani na jinsi gani?

      5 Mwaka wa 539 K.W.K.—kama miaka 200 baada ya Isaya kuandika unabii huu—kwa kweli Koreshi anawasili kwenye kuta za Babiloni kushambulia jiji hilo. (Yeremia 51:11, 12) Hata hivyo, Wababiloni hawajali. Wanaona kwamba jiji lao halishindiki. Kuta zake ndefu zimeinuka sana juu ya mahandaki ya kina kirefu yaliyojaa maji ya Mto Eufrati, ambao ni sehemu ya mfumo wa kinga za jiji. Miaka zaidi ya mia moja ndiyo hiyo, na hakuna adui amefaulu kuipiga Babiloni dafrao! Kwa kweli, Belshaza, aliye mtawala mkazi wa Babiloni, anajiona salama salimini, hata anakula karamu na washiriki wa baraza lake. (Danieli 5:1) Usiku huo—huo usiku wa Oktoba 5/6—Koreshi akamilisha mbinu murua ya ushambulizi wa kijeshi.

      6 Kwenye maji ya upande wa juu kutoka Babiloni, wahandisi wa Koreshi wamepasua njia kuupita ukingo wa Mto Eufrati, wakabadili mkondo wa maji yake mengi, na sasa hayatiririki tena kusini kuelekea jijini. Muda si muda, maji ya mto yaliyo ndani ya Babiloni na vizingo vyake yamepunguka sana hivi kwamba vikosi vya Koreshi vyaweza kupita chubwichubwi katika sakafu ya mto, kuelekea kitovu cha jiji hilo. (Isaya 44:27; Yeremia 50:38) Jamani, malango kando ya mto yako wazi, sawasawa na utabiri wa Isaya. Majeshi ya Koreshi yamiminika Babiloni kama siafu, yanaiteka kasri, yanamwua Mfalme Belshaza. (Danieli 5:30) Kwa usiku mmoja, ushindi wakamilika. Babiloni kaanguka, unabii katimizwa neno kwa neno.

      7. Wakristo wanatiwaje nguvu na utimizo mzuri ajabu wa unabii wa Isaya kuhusu Koreshi?

      7 Utimizo hususa wa unabii huu unaimarisha imani ya Wakristo leo. Hiyo ni sababu thabiti ya kuwafanya wao waamini kwamba unabii wa Biblia ambao bado haujatimizwa unategemeka kabisa. (2 Petro 1:20, 21) Waabudu wa Yehova wanajua kwamba anguko la “Babiloni Mkubwa,” lililotangulia kufananishwa na anguko la Babiloni mwaka wa 539 K.W.K., lilikwisha kutukia kule nyuma mwaka wa 1919. Na bado, wanatazamia tengenezo hilo la kisasa la kidini liharibiwe, na vilevile mfumo wa kisiasa ulio chini ya udhibiti wa Shetani uondolewe kama ilivyoahidiwa, naye Shetani afungwe ndani ya abiso, kisha kuwe na mbingu mpya na dunia mpya. (Ufunuo 18:2, 21; 19:19-21; 20:1-3, 12, 13; 21:1-4) Wanajua kwamba unabii mbalimbali wa Yehova si ahadi tupu, bali ni masimulizi ya matukio mahususi ya wakati ujao. Uhakika wa Wakristo wa kweli unatiwa nguvu wanapoukumbuka utimizo wa mambo yote madogo-madogo ya unabii wa Isaya yanayohusiana na anguko la Babiloni. Wao wanajua kwamba Yehova hutimiza neno lake daima.

      Sababu Itakayofanya Yehova Ampendelee Koreshi

      8. Ni sababu gani mojawapo inayofanya Yehova ampe Koreshi ushindi juu ya Babiloni?

      8 Baada ya kutaja ni nani atakayeshinda Babiloni na atashinda jinsi gani, Yehova anaendelea kueleza sababu moja itakayofanya Koreshi apewe ushindi huo. Yehova anaongea na Koreshi kwa njia ya unabii na kusema kwamba sababu ni ili “upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA [“Yehova,” “NW”], nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.” (Isaya 45:3b) Inafaa mtawala huyo wa serikali kubwa ya nne ya ulimwengu katika historia ya Biblia atambue kwamba ushindi wake mkubwa zaidi umetokea kwa kuungwa mkono na mtu mkubwa kuliko yeye—Yehova, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Mzima. Inampasa Koreshi akiri kwamba yule anayemwita, au kumpa utume, ni Yehova, Mungu wa Israeli. Maandishi ya Biblia yanaonyesha kwamba kwa kweli Koreshi alikiri kuwa ushindi wake mkubwa ulitoka kwa Yehova.—Ezra 1:2, 3.

      9. Ni sababu gani ya pili inayofanya Yehova amlete Koreshi kushinda Babiloni?

      9 Yehova anaeleza sababu ya pili inayofanya amlete Koreshi kushinda Babiloni: “Kwa ajili ya Yakobo, mtumishi wangu, na Israeli, mteule wangu, nimekuita kwa jina lako; nimekupa jina la sifa; ijapokuwa hukunijua.” (Isaya 45:4) Ushindi wa Koreshi juu ya Babiloni unatetemesha nchi. Unaangusha serikali moja kubwa ya ulimwengu na kutawaza nyingine, kisha unaweka kumbukumbu ya daima katika historia ya vizazi vingi vinavyokuja. Hata hivyo, inaelekea kwamba mataifa ya huku na huku, wanaotazama kwa matazamio, wangegutuka kujua kwamba yote hayo yanatendeka kwa faida ya wahamishwa ‘duni’ walioko Babiloni, ambao idadi yao ni elfu chache tu—wale Wayahudi ambao ni wazao wa Yakobo. Lakini, machoni pa Yehova, waokokaji hao wa taifa la kale la Israeli si duni kamwe. Wao ni “mtumishi” wake. Kati ya mataifa yote ya dunia, wao ndio ‘mteule wake.’ Hata ingawa Koreshi hakumjua Yehova hapo kwanza, Yehova anamtumia akiwa mtiwa-mafuta Wake kulipindua jiji hilo lililokataa kuwaachilia mateka waliomo. Mungu hakusudii wateule wake waendelee kunyong’onyea katika nchi ya kigeni milele.

      10. Ni sababu gani muhimu kupita zote inayofanya Yehova amtumie Koreshi kuikomesha Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Babiloni?

      10 Kuna sababu ya tatu, iliyo ya maana zaidi, inayofanya Yehova amtumie Koreshi kupindua Babiloni. Yehova anasema hivi: “Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine; zaidi yangu mimi hapana Mungu; nitakufunga mshipi ijapokuwa hukunijua; ili wapate kujua toka maawio ya jua, na toka magharibi, ya kuwa hapana mwingine zaidi ya mimi; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.” (Isaya 45:5, 6) Naam, kuanguka kwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Babiloni kunaonyesha Uungu wa Yehova, na kuthibitishia watu wote kwamba yeye pekee ndiye anayestahili ibada. Kwa sababu watu wa Mungu wanafunguliwa, hiyo itafanya watu mmoja-mmoja wa mataifa mengi—kutoka mashariki hadi magharibi—waje kukiri kwamba ni Yehova pekee aliye Mungu wa kweli.—Malaki 1:11.

      11. Yehova anaonyeshaje kwamba ana uwezo wa kutimiza kusudi lake kuhusu Babiloni?

      11 Kumbuka kwamba unabii huu wa Isaya uliandikwa miaka 200 hivi kabla ya tukio hilo. Huenda ikawa wengine walijiuliza hivi walipousikia, ‘Je, kweli Yehova ana uwezo wa kuutimiza?’ Ndiyo anao, kulingana na ushuhuda wa historia. Yehova anaeleza kwa nini inafaa itazamiwe kwamba yeye anaweza kutimiza maneno yake: “Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu [“amani,” “NW”], na kuhuluku ubaya; Mimi ni BWANA, niyatendaye hayo yote.” (Isaya 45:7) Kila kitu katika uumbaji—kuanzia nuru mpaka giza—na kila kitu katika historia—kuanzia amani mpaka ubaya—kinaweza kudhibitiwa na Yehova. Yeye atafanyia Israeli amani, na Babiloni ubaya, sawa na vile yeye aumbavyo nuru ya mchana na giza la usiku. Yehova ana uwezo wa kuumba ulimwengu mzima, tena ana uwezo wa kutimiza unabii wake mbalimbali. Huo ni uhakikisho wenye faraja kwa Wakristo leo, wanaojifunza neno lake la unabii kwa makini.

      12. (a) Yehova anafanya mbingu na dunia za mfano zizae nini? (b) Maneno ya Isaya 45:8 yana ahadi gani ya kuwafariji Wakristo leo?

      12 Kwa kufaa, Yehova anatumia matukio ya kawaida ya uumbaji kutoa mfano wa mambo yanayowangoja Wayahudi mateka: “Dondokeni, enyi mbingu, toka juu, mawingu na yamwage haki; nchi [“dunia,” “NW”] na ifunuke, ili kutoa wokovu, nayo itoe haki ikamee pamoja; Mimi, BWANA, nimeiumba.” (Isaya 45:8) Sawa na vile mbingu halisi zinavyonyesha mvua iletayo uhai, ndivyo Yehova atakavyofanya miongozo ya haki iwanyeshee watu wake kutoka kwenye mbingu za mfano. Na sawa na vile dunia halisi ifungukavyo kuzaa mavuno kemkemu, ndivyo Yehova atakavyoitolea dunia ya mfano mwito wa kutokeza matukio yanayopatana na kusudi lake la haki—hasa wokovu kwa watu wake walio mateka Babiloni. Mwaka wa 1919, Yehova alifanya matukio ya jinsi hiyo hiyo yatoke ‘mbinguni’ na ‘duniani’, ili kuwakomboa watu wake. Wakristo leo hushangilia kwa kuyaona mambo hayo. Kwa nini? Kwa sababu matukio hayo huimarisha imani yao wanapoutazamia wakati ambao mbingu za mfano, yaani Ufalme wa Mungu, zitaleta baraka kwenye dunia ya haki. Wakati huo haki na wokovu ambazo zitatoka kwenye mbingu na dunia za mfano zitakuwa nyingi sana kuliko wakati Babiloni la kale lilipopinduliwa. Utimizo huo wa mwisho wa maneno ya Isaya utakuwa mtukufu wee!— 2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1.

      Baraka za Kuitambua Enzi Kuu ya Yehova

      13. Kwa nini ni upuzi wanadamu kuthubutu kushindana na makusudi ya Yehova?

      13 Baada ya kuelezea baraka hizo zenye shangwe za wakati ujao, unabii unageuka ghafula kuelekea upande mwingine, na Isaya anatangaza ole maradufu: “Ole wake ashindanaye na Muumba wake! kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? au kazi yako, Hana mikono? Ole wake amwambiaye baba yake, Wazaa nini? au mwanamke, Una utungu wa nini?” (Isaya 45:9, 10) Inaonekana kwamba wana wa Israeli wanaukataa utabiri wa Yehova. Labda hawaamini kwamba Yehova ataruhusu watu wake waende uhamishoni. Au labda wanaona ni makosa Israeli kukombolewa utumwani na mfalme wa taifa la kipagani badala ya kukombolewa na mfalme wa nyumba ya Daudi. Kuonyesha upuzi wa kukataa kwao, Isaya anawalinganisha wenye kukataa na mafungu ya udongo na vigae vilivyotupwa ambavyo eti vingethubutu kuitilia shaka hekima ya mwenye kuvitengeneza. Kitu kile kile kilichofanyizwa na mfinyanzi eti sasa kinasema mfinyanzi hana mikono wala uwezo wa kufanyiza vitu. Upumbavu gani huo! Wenye kukataa ni kama watoto wadogo wanaothubutu kuchambua mamlaka ya wazazi wao.

      14, 15. Maneno “Mtakatifu” na “Muumba” yanafunua nini juu ya Yehova?

      14 Isaya anatoa jibu la Yehova kwa hao wenye kukataa: “BWANA, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! niagizeni. Mimi nimeiumba dunia, nimemhuluku mwanadamu juu yake; Mimi, naam, mikono yangu mimi, imezitanda mbingu, na jeshi lake lote nimeliamuru. Mimi nimemwinua katika haki, nami nitazinyosha njia zake zote; ataujenga mji wangu, naye atawaacha huru watu wangu waliohamishwa, si kwa kulipwa fedha, wala kwa kupewa zawadi, asema BWANA wa majeshi.”—Isaya 45:11-13.

      15 Yehova anapojitaja kuwa “Mtakatifu,” anakazia utakato wake. Kumwita “Muumba” kunatia mkazo kwamba yeye ndiye Muumba aliye na haki ya kuamua jinsi mambo yatakavyokuwa. Yehova anaweza kuwaarifu wana wa Israeli mambo yatakayokuja na kuutunza ufundi wa mikono yake, yaani, watu wake. Hapa tena, kanuni za uumbaji na za ufunuo zinaonyeshwa kuwa zinahusiana. Kwa kuwa Yehova ndiye Muumba wa ulimwengu mzima, ana haki ya kuongoza matukio kulingana na uamuzi wake. (1 Mambo ya Nyakati 29:11, 12) Katika kisa kinachozungumziwa, Mtawala Mwenye Enzi Kuu ameamua kumwinua Koreshi, mpagani, awe mkombozi wa Israeli. Ingawa bado Koreshi hajaja, ni hakika kwamba atakuja sawa na vile ilivyo hakika kwamba kuna mbingu na dunia. Basi, ni mwana yupi wa Israeli angethubutu kumchambua Baba, “BWANA wa majeshi”?

      16. Kwa nini watumishi wa Yehova wanapaswa kujitiisha chini yake?

      16 Mistari hii hii ya Isaya ina sababu nyingine ya kuwafanya watumishi wa Mungu wajitiishe kwake. Maamuzi yake ni ya kunufaisha watumishi wake daima. (Ayubu 36:3) Alitunga sheria za kuwasaidia watu wake wajinufaishe. (Isaya 48:17) Wayahudi wa siku za Koreshi wanaoikubali enzi kuu ya Yehova wanauona ukweli huo. Koreshi anatenda kupatana na haki ya Yehova na kuwaagiza watoke Babiloni wakalijenge hekalu upya. (Ezra 6:3-5) Vivyo hivyo leo, baraka hupatikana na wale wanaotumia sheria za Mungu katika maisha yao ya kila siku na kujinyenyekeza chini ya enzi kuu yake.—Zaburi 1:1-3; 19:7; 119:105; Yohana 8:31, 32.

      Baraka kwa Mataifa Mengine

      17. Zaidi ya Israeli, ni nani watakaonufaika na matendo ya Yehova ya kuokoa, na jinsi gani?

      17 Israeli silo taifa pekee litakalonufaika na kuanguka kwa Babiloni. Isaya anasema hivi: “BWANA asema hivi, Kazi ya Misri [“vibarua wasiolipwa wa Misri,” “NW”], na bidhaa ya Kushi [“wafanyabiashara wa Ethiopia,” “NW”], na Waseba, watu walio warefu, [“wao wenyewe,” “NW”] watakujilia, nao watakuwa wako; watakufuata; watakuja katika minyororo; wataanguka chini mbele yako, watakuomba, wakisema, Hakika Mungu yu ndani yako [“yumo katika muungano na wewe,” “NW”]; wala hapana mwingine, hapana Mungu tena.” (Isaya 45:14) Siku za Musa, “kundi kubwa la watu [wasio Waisraeli] waliochangamana” na Waisraeli liliandamana pamoja nao katika lile tukio la Kutoka Misri. (Kutoka 12:37, 38) Vivyo hivyo, wageni wataandamana na wahamishwa Wayahudi wanaorudi kutoka Babiloni. Watu hao wasio Wayahudi hawatalazimishwa kwenda, bali ‘wao wenyewe watakuja.’ Yehova anaposema, “wataanguka chini mbele yako” na “watakuomba,” anamaanisha ujitiisho na ushikamano wa hiari ambao wageni hao waliwaonyesha Israeli. Wakivaa minyororo, itakuwa kwa moyo wa kupenda, kuonyesha nia yao ya kuwatumikia watu wa agano la Mungu, wawaambie hivi: ‘Mungu yumo katika muungano na wewe.’ Watamwabudu Yehova wakiwa wageuzwa-imani, chini ya maandalizi ya agano lake pamoja na Israeli.—Isaya 56:6.

      18. Ni nani leo wamenufaika na hatua ya Yehova ya kukomboa “Israeli wa Mungu,” na kwa njia zipi?

      18 Tangu mwaka wa 1919, “Israeli wa Mungu” alipokombolewa kutoka utekwa wa kiroho, maneno ya Isaya yametimizwa kwa njia kubwa zaidi kuliko katika siku za Koreshi. Mamilioni ya watu duniani pote wanaonyesha moyo wa kupenda kumtumikia Yehova. (Wagalatia 6:16; Zekaria 8:23) Wao hujitolea kutumia nguvu zao za kimwili na fedha zao kwa uchangamfu ili kuunga mkono ibada ya kweli, kama wale “vibarua” na “wafanyabiashara” wanaotajwa na Isaya. (Mathayo 25:34-40; Marko 12:30) Wao hujiweka wakfu kwa Mungu na hutembea katika mapito yake, wakifurahia kuwa watumwa wake. (Luka 9:23) Wao humwabudu Yehova peke yake, wakifurahia manufaa za kushirikiana na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” ambao wamo katika uhusiano wa pekee wa agano pamoja na Mungu. (Mathayo 24:45-47; 26:28; Waebrania 8:8-13) Ingawa “vibarua” na “wafanyabiashara” hao si washiriki katika agano hilo, wananufaika kutokana nalo na wanatii sheria zinazoshirikishwa nalo, wakitangaza hivi kwa ujasiri: “Hakuna Mungu mwingine.” Inasisimua kama nini leo kujionea ongezeko kubwa sana la watu wanaounga mkono ibada ya kweli kwa moyo wa kupenda jinsi hiyo!—Isaya 60:22.

      19. Ni nini kitakachowapata wale wanaoendelea kuabudu sanamu?

      19 Akiisha kufunua kwamba watu wa mataifa watajiunga kumwabudu Yehova, nabii anapaza sauti ya mshangao hivi: “Hakika wewe u Mungu ujifichaye nafsi yako, Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi”! (Isaya 45:15) Ingawa Yehova anajizuia asionyeshe uwezo wake sasa, wakati ujao hatajificha tena. Ataonyesha kuwa yeye ni Mungu wa Israeli, Mwokozi wa watu wake. Hata hivyo, Yehova hatakuwa Mwokozi wa wale wanaozitumaini sanamu. Kuhusu hao, Isaya anasema hivi: “Watatahayarika, naam, watafadhaika, wote pia; wale wafanyao sanamu wataingia fadhaa pamoja.” (Isaya 45:16) Fadhaa yao haitakuwa fedheha na aibu ya muda tu. Bali, itamaanisha kifo—kinyume cha ahadi ambayo sasa Yehova anampa Israeli.

      20. Taifa la Israeli litapataje “wokovu wa milele”?

      20 “Bali Israeli wataokolewa na BWANA [“katika muungano na Yehova,” “NW”] kwa wokovu wa milele; ninyi hamtatahayarika, wala kufadhaika, milele na milele.” (Isaya 45:17) Yehova anawaahidi Israeli wokovu wa milele, lakini kuna masharti. Ni lazima Israeli wabaki “katika muungano na Yehova.” Israeli watakapovunja muungano huo kwa kumkataa Yesu wakisema siye Mesiya, taifa hilo litapoteza taraja lake la kupata “wokovu wa milele.” Hata hivyo, wengine katika Israeli watadhihirisha kuwa wana imani katika Yesu, nao watakuwa kiini cha taifa la Israeli wa Mungu, ambalo litachukua mahali pa Israeli wa kimwili. (Mathayo 21:43; Wagalatia 3:28, 29; 1 Petro 2:9) Taifa la Israeli wa kiroho halitaaibishwa kamwe. Litaingizwa katika “agano lidumulo milele.”—Waebrania 13:20.

      Yehova Anategemeka Katika Uumbaji na Katika Ufunuo

      21. Yehova anaonyeshaje kuwa yeye ni mwenye kutegemeka kabisa katika kuumba na katika kufunua mambo?

      21 Je, Wayahudi wanaweza kuitegemea ahadi ya Yehova ya kuwapa Israeli wokovu wa milele? Isaya anajibu hivi: “Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa [“bure,” “NW”], aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine. Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, BWANA, nasema haki; nanena mambo ya adili.” (Isaya 45:18, 19) Kwa mara ya nne na ya mwisho kabisa katika sura hii, Isaya anafungua kifungu cha maneno mazito ya unabii kwa usemi huu: ‘BWANA asema hivi.’ (Isaya 45:1, 11, 14) Yehova anasema nini? Kwamba yeye ni mwenye kutegemeka, katika kuumba na katika kufunua mambo. Hakuiumba dunia “bure.” Vivyo hivyo, yeye hawaombi watu wake, Israeli, wamtafute “bure.” Sawa na vile kusudi la Mungu kwa dunia litakavyotimizwa, ndivyo kusudi la Mungu kwa wateule wake litakavyotimizwa. Maneno ya Yehova husemwa waziwazi, tofauti na matamko yasiyo wazi ya wale wanaotumikia miungu ya uwongo. Maneno yake ni ya haki, nayo yatatimia. Wale wanaomtumikia hawatamtumikia bure tu.

      22. (a) Wayahudi waliopelekwa uhamishoni Babiloni wanaweza kuwa na uhakika wa jambo gani? (b) Wakristo leo wana uhakikisho gani?

      22 Maneno hayo yanawahakikishia watu wa Mungu waliopelekwa uhamishoni Babiloni kwamba Nchi ya Ahadi haitabaki ukiwa. Itakaliwa upya. Na ahadi za Yehova kuwahusu zinatimia. Kwa maana pana, maneno ya Isaya yanawahakikishia watu wa Mungu leo kwamba dunia haitakuwa magofu yenye ukiwa—ichomwe na moto iwe makaa, kama vile wengine wanavyoamini, wala iharibiwe na makombora ya nyukilia, kama vile wengine wanavyohofu. Mungu anakusudia dunia ibaki milele, ikiwa imepambwa uzuri wa kiparadiso na kukaliwa na wakaaji wenye haki. (Zaburi 37:11, 29; 115:16; Mathayo 6:9, 10; Ufunuo 21:3, 4) Ndiyo, maneno ya Yehova yatategemeka kama vile yalivyotegemeka kuhusu Israeli.

      Yehova Hukunjua Rehema Yake

      23. Kuna matokeo gani kwa wale wanaoabudu sanamu, na wale wanaomwabudu Yehova wanakuwa na hali gani?

      23 Wokovu wa Israeli unakaziwa katika maneno ya Yehova yanayofuata: “Jikusanyeni mje; na kukaribia pamoja, ninyi wa mataifa mliookoka; hawana maarifa wale wachukuao mti wa sanamu yao ya kuchonga; wamwombao mungu asiyeweza kuokoa. Hubirini, toeni habari; naam, na wafanye mashauri pamoja; ni nani aliyeonyesha haya tangu zamani za kale? ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, BWANA? wala hapana Mungu zaidi ya mimi; Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi.” (Isaya 45:20, 21) Yehova anawaagiza ‘waliookoka’ waulinganishe wokovu wao na kile kinachowapata wanaoabudu sanamu. (Kumbukumbu la Torati 30:3; Yeremia 29:14; 50:28) Kwa sababu waabudu-sanamu husali na kutumikia miungu hoi isiyoweza kuwaokoa, “hawana maarifa.” Ibada yao ni ya bure—bure bilashi. Hata hivyo, wale wanaomwabudu Yehova wanapata kwamba ana uwezo wa kutimiza matukio aliyotabiri “zamani za kale,” mojawapo likiwa ni wokovu wa watu wake walioko uhamishoni Babiloni. Uwezo huo na nguvu hizo za kuona mbele humtofautisha Yehova na miungu mingine yote. Kwa kweli, yeye ni “Mungu mwenye haki, mwokozi.”

      “Sisi Tunawiwa Wokovu na Mungu Wetu”

      24, 25. (a) Yehova anatoa mwaliko gani, na kwa nini ni hakika kwamba ahadi yake itatimizwa? (b) Yehova anataka apewe nini kilicho haki yake?

      24 Rehema ya Yehova humsukuma kutoa mwaliko huu: “Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa. Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki [“kamili,” “NW”] na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika. Katika BWANA wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka [“kujisifu juu yao wenyewe,” “NW”].”—Isaya 45:22-25.

      25 Yehova anawaahidi Israeli kwamba atawaokoa wale walioko Babiloni ambao wanamgeukia. Haiwezekani unabii wake ushindwe kutimia kwa sababu Yehova ana tamaa na pia uwezo wa kuwaokoa watu wake. (Isaya 55:11) Maneno ya Mungu yenyewe yanategemeka, lakini yanategemeka hata zaidi Yehova anapoyaongezea kiapo chake kuyathibitisha. (Waebrania 6:13) Kwa haki, yeye hutaka wale wanaotamani upendeleo wake wamwonyeshe unyenyekeo (“kila goti litapigwa”) na kuwajibika mbele zake (“kila ulimi utaapa”). Waisraeli wanaovumilia katika kumwabudu Yehova wataokolewa. Wataweza kujisifia yale ambayo Yehova anawafanyia.—2 Wakorintho 10:17.

      26. “Umati mkubwa” kutoka kwenye mataifa yote unaitikiaje mwaliko wa Yehova kwamba wamgeukie?

      26 Hata hivyo, si wahamishwa walioko Babiloni peke yao wanaopewa mwaliko wa Mungu wamgeukie. (Matendo 14:14, 15; 15:19; 1 Timotheo 2:3, 4) Mwaliko huo ungali ukitolewa, na “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote” unaitikia na kutangaza hivi: ‘Sisi tunawiwa wokovu na Mungu wetu na Mwana-Kondoo,’ Yesu. (Ufunuo 7:9, 10; 15:4) Kila mwaka, mamia ya maelfu ya wapya huipanua idadi ya umati mkubwa kwa kumgeukia Mungu, wakitambua kikamili enzi yake kuu na kutangaza peupe ushikamanifu wao kwake. Zaidi ya hilo, wao huwaunga mkono Israeli wa kiroho, “mbegu ya Abrahamu.” (Wagalatia 3:29) Wao huonyesha wanaupenda utawala mwadilifu wa Yehova kwa kutangaza ulimwenguni pote hivi: ‘Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu kamili.’a Katika barua yake kwa Waroma, mtume Paulo alinukuu tafsiri ya Septuagint ya Isaya 45:23 kuonyesha kwamba hatimaye kila mtu aliye hai atakiri enzi kuu ya Mungu na kusifu jina lake kwa uendelevu.—Waroma 14:11; Wafilipi 2:9-11; Ufunuo 21:22-27.

      27. Kwa nini Wakristo leo wanaweza kuzitumaini kabisa ahadi za Yehova?

      27 Kwa nini washiriki wa umati mkubwa wanaweza kutumaini kwamba kumgeukia Mungu humaanisha wokovu? Ni kwa sababu ahadi za Yehova zinategemeka, kama vile maneno ya unabii yaliyomo katika Isaya sura ya 45 yanavyoonyesha wazi. Sawa na vile Yehova alivyokuwa na uwezo na hekima ya kuziumba mbingu na dunia, ndivyo alivyo na uwezo na hekima ya kutimiza unabii wake mbalimbali. Na sawa na vile alivyohakikisha kwamba unabii uliomhusu Koreshi ulitimizwa, ndivyo atakavyotimiza unabii mwingine wowote wa Biblia ambao bado unangoja kutimizwa. Kwa hiyo, waabudu wa Yehova wanaweza kuwa na uhakika kwamba karibuni Yehova atathibitika tena kuwa “Mungu mwenye haki, mwokozi.”

      [Maelezo ya Chini]

      a Biblia ya New World Translation hutumia usemi “uadilifu kamili” kwa sababu maandishi ya Kiebrania yanaonyesha neno “uadilifu” kwa namna ya wingi. Hapa wingi umetumiwa kuonyesha utele wa uadilifu wa Yehova.

      [Picha katika ukurasa wa 80, 81]

      Yehova, anayefanyiza nuru na kuumba giza, anaweza kufanyiza amani na kuumba ubaya

      [Picha katika ukurasa wa 83]

      Yehova atafanya “mbingu” zinyeshe baraka na “dunia” itokeze wokovu

      [Picha katika ukurasa wa 84]

      Je, vigae vilivyotupwa vitilie shaka hekima ya mwenye kuvitengeneza?

      [Picha katika ukurasa wa 89]

      Yehova hakuiumba dunia bure

  • Kuirudia Ibada ya Yehova
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Saba

      Kuirudia Ibada ya Yehova

      Isaya 46:1-13

      1. Miungu miwili kati ya miungu mikuu ya Babiloni inaitwaje, na ni nini kinachotabiriwa kuihusu?

      ISRAELI watakapopelekwa uhamishoni Babiloni, watazungukwa na ibada ya uwongo. Wakati wa Isaya, watu wa Yehova bado wamo katika nchi yao wenyewe, na wana hekalu na ukuhani. Hata hivyo, wengi katika taifa lililo wakfu wamejiacha washindwe na ibada ya sanamu. Basi ni muhimu kuwatayarisha mapema wasiihofu mno miungu ya uwongo ya Babiloni wala kushawishika kuitumikia. Hivyo basi, Isaya anatoa unabii kuhusu miwili kati ya miungu mikuu ya Babiloni, akisema hivi: “Beli anaanguka chini, Nebo anainama; sanamu zao ziko juu ya wanyama, na juu ya ng’ombe; vitu vile mlivyokuwa mkivichukua huku na huku vimekuwa mzigo, mzigo wa kumlemea mnyama aliyechoka.” (Isaya 46:1) Beli ndiye mungu-sanamu aliye mkuu miongoni mwa Wakaldayo. Naye Nebo anaheshimiwa sana kuwa mungu wa hekima na masomo. Watu wengi wanaiheshimu miungu hiyo miwili, na hiyo inaonekana wazi kwa kuwa majina ya miungu hiyo yanahusishwa katika majina kadhaa ya Wababiloni binafsi—Belshaza, Nabopolasa, Nebukadreza, na Nebuzaradani, kutaja machache tu.

      2. Kutojiweza kwa miungu ya Babiloni kunatiliwaje mkazo?

      2 Isaya anasema kwamba Beli ‘ameanguka chini,’ na Nebo “anainama.” Miungu hiyo ya uwongo itabwagwa chini. Haitaweza kuwasaidia waabudu wake Yehova aletapo hukumu zake juu ya Babiloni. Hata haitaweza kujiokoa yenyewe, ng’o! Beli na Nebo hawatabebwa tena katika mahali pa heshima wakati wa maandamano, kama yale ya kuadhimisha sherehe za Siku ya Mwaka Mpya wa Babiloni. Bali, waabudu wao watawakokota kama mizigo ya kawaida. Badala ya kusifiwa na kutukuzwa, miungu hiyo itazomewa na kudharauliwa.

      3. (a) Wababiloni watagutushwa na nini? (b) Kilichoipata miungu ya Babiloni kinaweza kuwa na somo gani leo?

      3 He, acha Wababiloni wagutuke wanapotambua kwamba kumbe sanamu zao vipenzi ni mizigo tu inayobebwa na wanyama wachovu! Vivyo hivyo, leo miungu ya ulimwengu—vitu vile ambavyo watu huvitumainia na kuvitolea jasho na hata uhai wao—ni madanganyo matupu. Vitu kama utajiri, silaha, raha, watawala, uzalendo na mifano yake ya uzalendo, na vinginevyo kadha wa kadha vimeabudiwa na watu. Miungu hiyo itaonyeshwa wazi kuwa bure kabisa wakati wa Yehova uwadiapo.—Danieli 11:38; Mathayo 6:24; Matendo 12:22; Wafilipi 3:19; Wakolosai 3:5; Ufunuo 13:14, 15.

      4. Miungu ya Babiloni ‘inajiinamisha’ na ‘kuinama’ katika maana gani?

      4 Unabii unazidi kukazia kushindwa kabisa kwa miungu ya Babiloni, unaposema hivi: “Wanajiinamisha, wanainama pamoja; hawakuweza kuutua mzigo [“kuupatia mzigo njia ya kuokoka,” “NW”], bali wao wenyewe wamekwenda kufungwa.” (Isaya 46:2) Inaonekana miungu ya Babiloni ‘inajiinamisha’ na ‘kuinama’ kana kwamba imejeruhiwa vitani au ikawa vizee vinyonge. Hata haiwezi kuupunguza mzigo wa wanyama duni wanaoibeba, wala kuwapa njia ya kuokokea. Mambo yakiwa hivyo, je, watu wa agano la Yehova wanapaswa kweli kuiheshimu miungu hiyo kwa vyovyote, hata ingawa wao ni mateka Babiloni? La! Hali kadhalika, hata wakati watumishi wa Yehova waliotiwa mafuta walipokuwa katika utekwa wa kiroho hawakuiheshimu miungu ya uwongo ya “Babiloni Mkubwa,” iliyoshindwa kumzuia asianguke mwaka wa 1919 na tena itashindwa kumwokoa na mabaya yatakayomwangukia wakati wa “dhiki kubwa.”—Ufunuo 18:2, 21; Mathayo 24:21.

      5. Leo Wakristo huepukaje kuyarudia makosa yaliyofanywa na Wababiloni waabudu-sanamu?

      5 Leo Wakristo wa kweli hawainamii sanamu za aina yoyote. (1 Yohana 5:21) Misalaba, tasbihi, na mifano ya watakatifu haifanyi iwezekane kumfikia Muumba kwa urahisi zaidi. Vitu hivyo haviwezi kutuombea. Katika karne ya kwanza, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake njia iliyo sawa ya kumwabudu Mungu aliposema hivi: “Mimi ndiyo njia na kweli na uhai. Hakuna ajaye kwa Baba ila kupitia mimi. Mkiomba jambo lolote katika jina langu, hakika nitalifanya.”—Yohana 14:6, 14.

      ‘Waliinuliwa Tangu Mimbani’

      6. Yehova anatofautianaje na miungu ya mataifa?

      6 Baada ya kuonyesha wazi ubatili wa kuabudu miungu-sanamu ya Babiloni, Yehova anawaambia watu wake hivi: “Nisikilizeni, enyi wa nyumba ya Yakobo, ninyi mlio mabaki ya nyumba ya Israeli, mliochukuliwa nami tangu tumboni, mlioinuliwa tangu mimbani.” (Isaya 46:3) Lo, Yehova ni tofauti kama nini na mifano ya kuchongwa ya Babiloni! Miungu ya Babiloni haina faida kwa waabudu wake. Miungu hiyo ikitaka kwenda, ni lazima ibebwe na mnyama mbeba-mizigo. Kinyume cha hilo, Yehova amekuwa akiwabeba watu wake. Amewaruzuku “tangu mimbani,” tangu taifa hilo liundwe. Wayahudi hao wakikumbuka kwa shauku jinsi Yehova alivyowabeba, watatiwa moyo waepuke kuabudu sanamu, wamtumainie Baba yao aliye Rafiki pia.

      7. Ni jinsi gani utunzaji mwororo ambao Yehova huwapa waabudu wake ulivyo mkubwa kuliko utunzaji ambao wazazi wa kibinadamu huwapa watoto wao?

      7 Yehova anawaongezea watu wake maneno haya mororo: “Na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua [“nitabeba,” “NW”]; naam, nitachukua na kuokoa.” (Isaya 46:4) Njia ya Yehova ya kuwatunza watu wake inaupita kwa mbali utunzaji wa mzazi wa kibinadamu aliye makini mno. Huenda wazazi wakahisi kwamba daraka lao la kuwatunza watoto wao linaendelea kupungua zaidi na zaidi kadiri watoto hao wanavyoendelea kukua. Wazazi hao wanapozeeka, mara nyingi wao hutunzwa na watoto wao. Yehova hawi hivyo kamwe. Yeye haachi kamwe kuwatunza watoto wake wa kibinadamu—hata wakiwa wazee. Leo waabudu wa Mungu wanamtumainia na kumpenda Muumba wao, nao hufarijiwa sana na maneno hayo ya unabii wa Isaya. Wao hawana haja ya kuhangaikia siku au miaka ya maisha yao yaliyobaki katika mfumo huu wa mambo. Yehova anaahidi kwamba ataendelea ‘kuwachukua’ wale waliozeeka, awape nguvu wanazohitaji ili wavumilie na kudumu wakiwa waaminifu. Atawabeba, awatie nguvu, awaokoe.—Waebrania 6:10.

      Jihadhari na Sanamu za Kisasa

      8. Baadhi ya wananchi wenzi wa Isaya wametenda dhambi gani isiyoweza kutetewa?

      8 Ebu wazia jinsi Wababiloni wanaozitumaini sanamu watakavyokata tamaa itakapoonekana hakika kwamba sanamu hizo ni ovyo tu! Je, Israeli wanapaswa kuamini kwamba miungu hiyo inaweza kulinganishwa na Yehova? Hata kidogo. Kwa haki, Yehova anauliza hivi: “Mtanifananisha na nani, na kunisawazisha naye, na kunilinganisha naye, ili tuwe sawasawa?” (Isaya 46:5) Hivyo basi, wananchi wenzi wa Isaya hawawezi kujitetea kwa kugeukia ibada ya sanamu bubu, bure, hoi! Ni upumbavu wa mwisho, eti taifa linalomjua Yehova litegemee mifano isiyo na uhai, tena isiyoweza kujikinga, iliyotengenezwa kwa mikono ya binadamu.

      9. Eleza ni jinsi gani waabudu fulani wa sanamu huwazawaza kwa ukichwamaji.

      9 Ebu ona jinsi waabudu-sanamu walivyo na mawazowazo ya ukichwamaji. Unabii unaendelea kusema hivi: “Watu wamwagao dhahabu kutoka mfukoni, na kupima fedha katika mizani, huajiri mfua dhahabu, akaifanya mungu; huanguka, naam, huabudu.” (Isaya 46:6) Waabudu wanajikung’uta senti yao ya mwisho eti wajitengenezee mungu, kana kwamba sanamu ya bei ghali ndiyo yenye nguvu za kuokoa kuliko sanamu ya mbao. Lakini, hata kama watajitahidi juu chini, na hata kama watatumia vifaa vya pesa na mapesa, sanamu isiyo na uhai ni sanamu tu, kwisha.

      10. Ubatili mtupu wa kuabudu sanamu unafafanuliwaje?

      10 Unabii unazidi kukazia upumbavu wa kuabudu sanamu unaposema hivi: “Humchukua begani, humchukua, wakamsimamisha mahali pake, akasimama; hataondoka katika mahali pake, naam, mmoja atamwita, lakini hawezi kujibu, wala kumwokoa na taabu yake.” (Isaya 46:7) Kuelekeza sala kwenye mfano usiosikia wala kutenda ni upuzi kama nini! Mtunga-zaburi anaeleza vizuri kwamba vitu hivyo vya ibada ni bure kabisa kwa kusema hivi: “Sanamu zao ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu. Zina vinywa lakini hazisemi, zina macho lakini hazioni, zina masikio lakini hazisikii, zina pua lakini hazisikii harufu, mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, wala hazitoi sauti kwa koo zake. Wazifanyao watafanana nazo, kila mmoja anayezitumainia.”—Zaburi 115:4-8.

      “Mjipe Moyo”

      11. Ni nini kitakachowasaidia wale wanaoyumbayumba ‘wajipe moyo’?

      11 Baada ya kuonyesha ubatili wa kuabudu sanamu, sasa Yehova anawapa watu wake sababu ambazo inawapasa wamtumikie yeye: “Kumbukeni haya, mkajionyeshe kuwa waume [“mjipe moyo,” “NW”]; jifahamisheni haya, ninyi mkosao; kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi.” (Isaya 46:8, 9) Wale wanaoyumbayumba kati ya ibada ya kweli na ibada ya sanamu wanapaswa waikumbuke historia. Wanapaswa kuzingatia mambo ambayo Yehova amefanya. Hiyo itawasaidia wajipe moyo kutenda lililo haki. Itawasaidia warudie kumwabudu Yehova.

      12, 13. Wakristo wamekabwa katika mapambano gani, na wanaweza kushinda jinsi gani?

      12 Kitia-moyo hicho kingali kinahitajiwa leo. Hali moja na Waisraeli, Wakristo wanyofu hulazimika kupigana na vishawishi na hali zao wenyewe za kutokamilika. (Waroma 7:21-24) Isitoshe, wamekabana na adui asiyeonekana mwenye nguvu sana katika vita vya kiroho. Mtume Paulo anasema hivi: “Tuna kushindana mwereka, si dhidi ya damu na mwili, bali dhidi ya serikali, dhidi ya mamlaka, dhidi ya watawala wa ulimwengu wa giza hili, dhidi ya majeshi ya roho waovu katika mahali pa kimbingu.”—Waefeso 6:12.

      13 Shetani na roho wake waovu watajitahidi kufa na kupona kujaribu kuwaondoa Wakristo katika ibada ya kweli. Ili Wakristo wafanikishe pigano lao, wanahitaji kufuata shauri la Yehova na kujipa moyo. Jinsi gani? Mtume Paulo anaeleza hivi: “Vaeni suti kamili ya silaha kutoka kwa Mungu ili mpate kuweza kusimama imara dhidi ya mbinu za Ibilisi.” Yehova hawapeleki watumishi wake piganoni wakiwa na vifaa ovyo. Silaha zao za kiroho zinahusisha ‘ngao kubwa ya imani, ambayo kwayo wataweza kuzima vishale vyote vinavyowaka moto vya yule mwovu.’ (Waefeso 6:11, 16) Waisraeli walikuwa wakosaji kwa sababu waliyapuuza maandalizi ya kiroho ambayo Yehova alikuwa amewafanyia. Kama wangaliyafikiria maajabu ambayo Yehova aliwafanyia tena na tena, wasingaligeuka kamwe kuziabudu sanamu zenye kuchukiza. Na tujifunze kutokana na mfano wao, tupige moyo konde kwamba hatutayumbayumba kamwe katika pigano la kutenda haki.—1 Wakorintho 10:11.

      14. Yehova anaelekeza kwenye uwezo gani kuonyesha kwamba yeye pekee ndiye Mungu wa kweli?

      14 Yehova ndiye ‘atangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; akisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.’ (Isaya 46:10) Ni mungu yupi mwingine awezaye kulingana na Yehova katika jambo hilo? Uwezo wa kuutabiri wakati ujao unathibitisha Uungu wa Muumba kwa njia ya kutokeza. Hata hivyo, uhakika wa kutimizwa kwa matabiri hautokani na uwezo wa kuona mbele tu. Lile tangazo rasmi la kwamba “shauri langu litasimama” linakazia kutobadilika kwa kusudi la Mungu lililotajwa hususa. Kwa kuwa uwezo wa Yehova si haba, ulimwengu mzima hauna chochote cha kumzuia asitimize mapenzi yake. (Danieli 4:35) Kwa hiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba unabii wowote ambao haujatimizwa mpaka sasa utatimizwa kabisa wakati wa Mungu ukiwadia.—Isaya 55:11.

      15. Fikira zetu zinaelekezwa kwenye mfano gani wa ajabu unaoonyesha kwamba Yehova anaweza kuutabiri wakati ujao?

      15 Halafu sasa unabii wa Isaya unatuonyesha mfano mzuri ajabu wa kwamba Yehova ana uwezo wa kutabiri matukio ya wakati ujao kisha kuyatimiza maneno yake: “Nikiita ndege mkali kutoka mashariki, mtu wa shauri langu toka nchi iliyo mbali; naam, nimenena, nami nitatekeleza; nimekusudia, nami nitafanya.” (Isaya 46:11) Yehova Mungu ndiye ‘atangazaye mwisho tangu mwanzo,’ kwa hiyo ataelekeza hali za mambo ya kibinadamu ili atimize shauri lake. Atamwita Koreshi “kutoka mashariki,” au kutoka kule maawio ya jua Uajemi, ambako kutakuwa na mji mkuu wa Pasargadae, ulio kipenzi cha Koreshi. Naye Koreshi atafanana na “ndege mkali,” airukie Babiloni vu!

      16. Yehova anathibitishaje kwamba utabiri wake kuhusu Babiloni ni hakika?

      16 Maneno haya, “Nimenena, nami nitatekeleza,” yanauthibitisha uhakika wa utabiri wa Yehova kuhusu Babiloni. Ingawa mwanadamu asiye mkamilifu ana maelekeo ya kutoa ahadi za msisimuko tu, Muumba hashindwi kamwe kutimiza neno lake. Kwa kuwa Yehova ndiye Mungu “asiyeweza kusema uwongo,” tunaweza kuwa na uhakika kwamba iwapo ‘amekusudia,’ ‘atafanya.’—Tito 1:2.

      Mioyo Isiyo na Imani

      17, 18. Ni nani wanaoweza kufafanuliwa kuwa ‘wenye mioyo mishupavu’ (a) nyakati za kale? (b) leo?

      17 Kwa njia ya unabii, Yehova anaelekeza fikira zake tena kwa Wababiloni, akisema: “Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mshupavu, mlio mbali na haki.” (Isaya 46:12) Maneno “ninyi mlio na moyo mshupavu” hufafanua wale wenye shingo ngumu, wapinzani sugu wa mapenzi ya Mungu. Pasipo shaka, Wababiloni wako mbali sana na Mungu. Chuki yao kwa Yehova na watu wake inawaongoza kuharibu Yerusalemu na hekalu lake na kuwapeleka wakaaji wake uhamishoni.

      18 Leo wale walio na mioyo ya kutia shaka, isiyoamini, hukataa kwa ushupavu kusikiliza ujumbe wa Ufalme unaohubiriwa katika dunia yote inayokaliwa. (Mathayo 24:14) Hawataki kukiri kuwa Yehova ndiye Mwenye Enzi Kuu anayestahili. (Zaburi 83:18; Ufunuo 4:11) Wanakinza na kupinga mapenzi yake kwa mioyo ‘iliyo mbali na haki.’ (2 Timotheo 3:1-5) Wanakuwa kama Wababiloni kwa kukataa kumsikiliza Yehova.

      Wokovu wa Mungu Hautakawia

      19. Yehova atawafanyiaje Israeli tendo la haki?

      19 Maneno ya kumalizia ya Isaya sura ya 46 yanakazia pande mbalimbali za utu wa Yehova: “Mimi ninaleta karibu haki yangu, haitakuwa mbali, na wokovu wangu hautakawia; nami nitaweka wokovu katika Sayuni kwa ajili ya Israeli, utukufu wangu.” (Isaya 46:13) Mungu atakapowakomboa Israeli, hilo litakuwa tendo la haki. Yeye hataruhusu watu wake waendelee kukawia sana uhamishoni. Wokovu wa Sayuni utakuja wakati ufaao, “hautakawia.” Baada ya kufunguliwa utekwani, Waisraeli watakuwa tamasha kwa mataifa yanayowazunguka. Yehova atakapolikomboa taifa lake, hiyo itashuhudia kwamba yeye ana uwezo wa kuokoa. Miungu ya Babiloni, Beli na Nebo, itafunuliwa wazi ili watu wote waione kuwa ni miungu ya bure, isiyoweza kitu.—1 Wafalme 18:39, 40.

      20. Wakristo wanawezaje kuwa na hakika kwamba ‘wokovu wa Yehova hautakawia’?

      20 Mwaka wa 1919, Yehova alisababisha ukombozi wa watu wake kutoka kwenye utekwa wa kiroho. Hakuchelewa. Sisi leo tunatiwa moyo na tukio hilo, vilevile na yale matukio ya nyakati za kale ambapo Babiloni lilianguka mikononi mwa Koreshi. Yehova ameahidi kuukomesha mfumo huu mwovu wa mambo, pamoja na ibada yake ya uwongo. (Ufunuo 19:1, 2, 17-21) Kwa kuchukua mambo kwa maoni ya kibinadamu, huenda Wakristo fulani wakahisi kwamba wokovu wao umekawizwa. Hata hivyo, subira ambayo Yehova anaendelea kuonyesha mpaka wakati wake mwenyewe ufaao ufike ni kitendo cha haki kwelikweli. Isitoshe, “[Yehova] hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Petro 3:9) Basi, uwe na hakika kwamba, sawa na siku za Israeli wa kale, ‘wokovu hautakawia.’ Kwa kweli, siku ya wokovu inapozidi kukaribia, Yehova anaendelea kutoa mwaliko huu kwa upendo: “Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu; mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie BWANA, naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.”—Isaya 55:6, 7.

      [Picha katika ukurasa wa 94]

      Miungu ya Babiloni inashindwa kumlinda na uharibifu

      [Picha katika ukurasa wa 98]

      Ni lazima Wakristo leo wajihadhari na sanamu za kisasa

      [Picha katika ukurasa wa 101]

      Jipe moyo wa kutenda lililo haki

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Nane

      Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele

      Isaya 47:1-15

      1, 2. (a) Kwa nini watu fulani wanaona haielekei kuwa mabadiliko makubwa yatazipata dini za ulimwengu hivi karibuni? (b) Tunajuaje kwamba maneno ya Isaya sura ya 47 yana matumizi ya wakati ujao? (c) Kwa nini mtajo “Babiloni Mkubwa” unazifaa dini zote za uwongo?

      “DINI Yarudia Hali Yake.” Ujumbe huo ulitangazwa na makala moja katika The New York Times Magazine. Ilionyesha kwamba bado dini inaonekana kuwa imara katika mioyo na akili za mamilioni ya watu. Basi huenda ikawa vigumu kuamini kwamba badiliko kubwa linakaribia kuzipata dini za ulimwengu. Lakini badiliko la jinsi hiyo limeonyeshwa katika sura ya 47 ya Isaya.

      2 Maneno ya Isaya yalitimizwa miaka 2,500 iliyopita. Hata hivyo, maneno yaliyoandikwa kwenye Isaya 47:8 yamenukuliwa katika kitabu cha Ufunuo yakionyeshwa kuwa yana matumizi ya wakati ujao. Hapo Biblia inautabiri mwisho wa tengenezo lililo kama kahaba, liitwalo “Babiloni Mkubwa”—milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo. (Ufunuo 16:19) Mtajo “Babiloni” unafaa unapotumiwa kuhusiana na dini za uwongo za ulimwengu, kwa kuwa dini ya uwongo ilianzia Babiloni ya kale. Kutoka huko dini hiyo ilisambaa hadi pembe nne za dunia. (Mwanzo 11:1-9) Karibu dini zote, kutia ndani Jumuiya ya Wakristo, zinafuata mafundisho ya kidini yaliyoanzia Babiloni, kama vile kutokufa kwa nafsi, moto wa helo, na kuabudu miungu ya utatu.a Je, unabii wa Isaya unaangaza nuru yoyote kuhusu wakati ujao wa dini?

      Babiloni Yashushwa Chini Kwenye Vumbi

      3. Fafanua ukuu wa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Babiloni.

      3 Ebu lisikilize tangazo hili rasmi la kimungu linalosisimua: “Haya, shuka, keti mavumbini, ewe bikira, binti Babeli; keti chini pasipo kiti cha enzi, ewe binti wa Wakaldayo; maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.” (Isaya 47:1) Kwa miaka mingi, Babiloni amekalia kiti cha ufalme akiwa serikali kubwa ya ulimwengu yenye mamlaka. Amekuwa “utukufu wa falme”—kitovu chenye usitawi wa kidini, wa kibiashara na wa kijeshi. (Isaya 13:19) Babiloni anapofikia upeo, milki yake imetandaa hadi mbali kusini kwenye mpaka wa Misri. Kisha, anapomshinda Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., inaonekana ni kama Mungu mwenyewe hawezi kumzuia kupata-pata ushindi! Basi, Babiloni anajiona kuwa ‘binti bikira,’ ambaye hataingiliwa kamwe na mvamizi wa kigeni.b

      4. Babiloni atapatwa na nini?

      4 Hata hivyo, “bikira” huyo kichwa kikubwa atadondoshwa kutoka kwenye kiti chake cha kifalme asiwe tena serikali kubwa ya ulimwengu isiyoweza kubishaniwa, ‘aketishwe mavumbini’ kwa kutiwa aibu. (Isaya 26:5) Hataonwa tena kuwa “mwororo, mpenda anasa,” mfano wa malkia wa kubembelezwa-bembelezwa. Hivyo basi, Yehova anaamuru hivi: “Twaa mawe ya kusagia, usage unga; vua utaji wako, ondoa mavazi yako [“rinda lako refu,” “NW”], funua mguu wako, pita katika mito ya maji.” (Isaya 47:2) Baada ya Babiloni kulitia utumwani taifa zima la Yuda, sasa yeye mwenyewe atatendwa kama mtumwa! Wamedi na Waajemi, wanaomwondoa katika kiti chake cha mamlaka, watamfanyisha kazi ngumu ya kumwaibisha.

      5. (a) Babiloni atavuliwaje ‘utaji na rinda lake refu’? (b) Amri inayotolewa kwamba Babiloni ‘apite katika mito ya maji’ huenda ikawa inaonyesha nini?

      5 Hivyo Babiloni atavuliwa ‘utaji na rinda lake refu,’ hata masazo ya ukuu na fahari yake ya zamani yakung’utwe fyuu. “Pita katika mito ya maji,” mabwana wake wa kazi watamwamuru. Labda Wababiloni fulani wataagizwa hasa kufanya kazi ngumu ya mtumwa kule nje. Au pengine unabii unamaanisha kwamba watu fulani wataburutwa wavuke mito wanapopelekwa uhamishoni. Vyovyote vile, Babiloni hatasafiri tena kwa madaha ya malkia anayesafirishwa na kuvushwa kijito akiwa amekalia kiti au akiwa katika kigari. Bali atakuwa kama mtumwa anayelazimika kuachilia mbali uungwana kwa kuinua rinda lake juu na kufichua miguu yake ili aweze kuvuka mto. Ni aibu iliyoje!

      6. (a) Uchi wa Babiloni utafunuliwa katika maana gani? (b) Ni jinsi gani Mungu ‘hamkubali mtu ye yote’? (Ona kielezi-chini.)

      6 Yehova anaendeleza shutuma yake: “Uchi wako utafunuliwa, naam, aibu yako itaonekana. Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.” (Isaya 47:3)c Naam, Babiloni ataaibishwa na kuvunjiwa heshima. Uovu na ukatili anaowafanyia watu wa Mungu utafichuliwa peupe. Hakuna binadamu anayeweza kuzuia kisasi cha Mungu!

      7. (a) Wahamishwa Wayahudi wataitikiaje habari za anguko la Babiloni? (b) Yehova atawakomboa watu wake kwa njia gani?

      7 Baada ya watu wa Mungu kuwa wameshikwa mateka muda wa miaka 70 katika Babiloni lililo hodari, watashangilia sana anguko lake. Watapaza sauti kusema: “Mkombozi wetu, BWANA wa majeshi ndilo jina lake, Mtakatifu wa Israeli.” (Isaya 47:4) Chini ya Sheria ya Kimusa, iwapo Mwisraeli alijiuza utumwani kulipia madeni yake, mkombozi (mtu wa damu yake) angeweza kumnunua, au kumkomboa, kutoka utumwani. (Mambo ya Walawi 25:47-54) Kwa kuwa Wayahudi watakuwa wameuzwa utumwani Babiloni, watahitaji kukombolewa, au kuwekwa huru. Nchi moja inaposhindwa na nyingine, watumwa hawafaidiki sana ila huhamishwa tu kutoka kwa bwana-mkubwa mmoja kupelekwa kwa mwingine. Lakini Yehova atamwongoza Mfalme Koreshi mshindi awafungue Wayahudi kutoka utumwani. Koreshi atapewa Misri, Kushi (Ethiopia), na Seba ziwe “ukombozi,” ili naye awaachilie Wayahudi. (Isaya 43:3) Basi ni vizuri kwamba Mwokozi wa Israeli anaitwa “BWANA wa majeshi.” Jeshi la Babiloni linaloonekana kuwa hodari sana si kitu mbele ya vikosi vya Yehova vya malaika wasioonekana.

      Malipo ya Ukatili

      8. Babiloni ‘ataingia gizani’ kwa maana gani?

      8 Yehova anairudia shutuma yake ya kiunabii kuhusu Babiloni: “Kaa kimya, ingia gizani, Ee binti wa Wakaldayo; maana hutaitwa tena Malkia [“Bi-Mkubwa,” “NW”] wa falme.” (Isaya 47:5) Babiloni ataona giza tupu, giza tititi. Hatatawala tena falme nyinginezo akiwa bi-mkubwa mkatili.—Isaya 14:4.

      9. Kwa nini Yehova anawakasirikia Wayahudi kwa haki?

      9 Kwanza hata imekuwaje Babiloni akaruhusiwa kuwadhuru watu wa Mungu? Yehova anaeleza hivi: “Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako.” (Isaya 47:6a) Yehova ana sababu nzuri ya kuwakasirikia Wayahudi. Zamani zile, aliwaonya kwamba wasipoitii Sheria yake wangefukuzwa nchini. (Kumbukumbu la Torati 28:64) Walipotumbukia katika ibada ya sanamu na ukosefu wa adili kingono, Yehova alionyesha upendo kwa kutuma manabii wakawasaidie kuirudia ibada safi. “Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.” (2 Mambo ya Nyakati 36:16) Basi, wakati Babiloni anapovamia Yuda na kuchafua hekalu Lake takatifu, Mungu anaruhusu nchi hiyo, iliyo urithi wake, itiwe unajisi.—Zaburi 79:1; Ezekieli 24:21.

      10, 11. Kwa nini Yehova anakasirikia Babiloni, hata ingawa ni mapenzi yake kwamba Babiloni awashinde watu wake?

      10 Basi, je, Babiloni anapowatumikisha Wayahudi, hafanyi hivyo ili kutimiza mapenzi ya Mungu tu? Sivyo, kwani Mungu anasema hivi: “Wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana. Ukasema, Mimi nitakuwa bibi [“Bi-Mkubwa,” “NW”] milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.” (Isaya 47:6b, 7) Mungu hajampa Babiloni amri ya kuwa mkatili mno, hivi kwamba hata hawawaonyeshi “wazee” hisani. (Maombolezo 4:16; 5:12) Wala hajawahimiza wajifurahishe kinyama kwa kuwadhihaki mateka Wayahudi.—Zaburi 137:3.

      11 Babiloni hatambui kwamba amewashika Wayahudi kwa muda tu. Ameyapuuza maonyo ya Isaya yasemayo kuwa wakati utawadia Yehova awaweke huru watu wake. Babiloni anatenda kana kwamba ni haki yake kuwatawala Wayahudi daima na kubakia milele akiwa bi-mkubwa anayesimamia mataifa yaliyo vibaraka vyake. Anakataa kuusikiza ujumbe wa kwamba utawala wake mwonevu utafika “mwisho”!

      Anguko la Babiloni Latabiriwa

      12. Kwa nini Babiloni anaitwa ‘mwanamke apendaye anasa’?

      12 Yehova anatangaza rasmi hivi: “Sasa, basi, sikia haya, wewe [“mwanamke,” “NW”] upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto.” (Isaya 47:8) Babiloni amevuma sana kwa kutafuta anasa. Mwanahistoria Herodotus wa karne ya tano K.W.K. anaelezea “desturi ya aibu sana” ya Wababiloni, ya kwamba wanawake wote walitakiwa kufanya umalaya ili kuonyesha kwamba wanamheshimu sana mungu wao wa kike wa mapenzi. Naye Curtius, mwanahistoria wa kale, alisema hivi: “Uchafu wa jiji hilo hauna kifani; hakuna zoea la ufisadi liwezalo kuwachochea watu na kuamsha tamaa zao za uasherati kwa kiwango kile.”

      13. Mwelekeo wa Babiloni wa kutafuta anasa utaharakishaje anguko lake?

      13 Mwelekeo wa Babiloni wa kutafuta anasa utaharakisha anguko lake. Muda mfupi kabla ya anguko lake, mfalme wa Babiloni na watu wenye vyeo watakula karamu, wanywe walewe chakari. Hivyo, hawatayajali hata kidogo majeshi ya Umedi-Uajemi yanayolivamia jiji. (Danieli 5:1-4) ‘Akiwa amekaa kwa kujiona salama,’ Babiloni atawaza kwamba hawezi kuvamiwa kwani kuta zake na handaki lake lenye maji zinampa himaya inayoonekana kuwa isiyopenyeka. Anajiambia kwamba “hapana mwingine” kamwe wa kutwaa cheo chake cha ukuu. Hafikiri kwamba angeweza kuwa “mjane,” afiwe na maliki wake, na vilevile “watoto” au wananchi wake. Vyovyote vile, hakuna ukuta uwezao kumhami kutokana na mkono wa Yehova Mungu wa kulipiza kisasi! Yehova atasema hivi baadaye: “Babeli ujapopanda mbinguni, na ujapopafanya mahali pa juu penye nguvu zake kuwa ngome, hata hivyo toka kwangu wenye kuangamiza watamwendea.”—Yeremia 51:53.

      14. Babiloni ‘atafiwa na watoto na kuwa mjane’ kwa njia zipi?

      14 Ni matokeo gani yatakayompata Babiloni? Yehova anaendelea kusema hivi: “Lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.” (Isaya 47:9) Naam, ukuu wa Babiloni akiwa serikali kubwa ya ulimwengu utakoma ghafula. Katika nchi za kale za Mashariki, kuwa mjane na kufiwa na watoto ndiyo maafa makubwa zaidi ambayo yangeweza kumpata mwanamke. Hatujui Babiloni anafiwa na “watoto” wangapi usiku wa anguko lake.d Ingawa hivyo, wakati utawadia jiji hilo liwe mahame kabisa. (Yeremia 51:29) Pia, ujane utamfika Babiloni kwa kuwa wafalme wake watang’olewa.

      15. Licha ya Babiloni kuwatenda Wayahudi ukatili, ni sababu gani zaidi inayomfanya Yehova amghadhibikie?

      15 Hata hivyo, hasira kali ya Yehova haiji kwa sababu tu ya dhuluma ambazo Babiloni anawatenda Wayahudi. Pia ‘uchawi wake mwingi’ unaichochea hasira ya Yehova. Sheria ya Mungu kwa Israeli hushutumu zoea la kuwasiliana na roho waovu; ingawa hivyo, Babiloni huyafuatia sana mafumbo ya roho. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Ezekieli 21:21) Kitabu Social Life Among the Assyrians and Babylonians kinasema kwamba Wababiloni waliishi ‘wakiwahofu daima roho wengi sana waovu ambao waliamini kuwa wamewazunguka.’

      Kutumaini Ubaya

      16, 17. (a) Babiloni ‘anautumainia ubaya wake’ jinsi gani? (b) Kwa nini mwisho wa Babiloni hauwezi kuepukwa?

      16 Je, wabashiri wa Babiloni watamwokoa? Yehova anajibu hivi: “Umeutumainia ubaya wako; umesema, Hapana anionaye; hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha, nawe umesema moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi.” (Isaya 47:10) Babiloni anafikiri kwamba kupitia hekima yake ya kilimwengu na ya kidini, pamoja na uhodari wake wa kijeshi na ukatili wake wenye ujanja, anaweza kudumisha cheo chake akiwa serikali kubwa ya ulimwengu. Anahisi kwamba hakuna awezaye ‘kumwona,’ yaani kumtoza hesabu kwa maovu anayoyatenda. Haoni mtu atakayeweza kupimana nguvu naye hivi karibuni. “Mimi ndiye, wala hapana mwingine,” anajiambia.

      17 Lakini Yehova anaonya hivi kupitia mwingine wa manabii wake: “Je, mtu ye yote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone?” (Yeremia 23:24; Waebrania 4:13) Basi Yehova anatangaza hivi: “Ubaya utakupata; wala hutajua kutopoa kwake; na msiba utakuangukia; hutaweza kuuondoa; na ukiwa utakupata kwa ghafula, usioujua.” (Isaya 47:11) Miungu ya Babiloni wala ‘utopozi’ wa waganga wake wanaowasiliana na roho waovu haiwezi kuepusha maafa yanayokuja—maafa ambayo Babiloni hajawahi kuona kifani chake!

      Washauri wa Babiloni Washindwa

      18, 19. Babiloni atapatwaje na msiba kwa kuwategemea washauri wake?

      18 Yehova anaamuru hivi kwa kejeli kali: “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.” (Isaya 47:12) Babiloni anaambiwa ajitokeze ‘asimame,’ au aendelee kutegemea uganga bila kujirekebisha. Basi na asimame, kwani si muda wote tangu “ujana” wake akiwa taifa amekazana kuendeleza sanaa za mafumbo ya roho.

      19 Lakini Yehova anamdhihaki, akisema: “Umechoka kwa wingi wa mashauri yako [“washauri wako,” “NW”]; basi, na wasimame hao wajuao falaki [“waabudu wa mbingu,” “NW”], wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata.” (Isaya 47:13)e Babiloni ataona wazi washauri wake wakishindwa vibaya sana. Ni kweli kwamba uchunguzi mwingi wa nyota utakuwa umefanywa kwa muda wa karne nyingi ili kusitawisha unajimu wa Babiloni. Lakini katika ule usiku wa anguko lake, wanajimu wake watakuwa hoi, ionekane wazi kwamba uaguzi ni kitu cha bure.—Danieli 5:7, 8.

      20. Washauri wa Babiloni watapatwa na msiba gani?

      20 Yehova anamalizia sehemu hii ya unabii kwa kusema hivi: “Tazama, watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza; hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao. Ndivyo yatakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale waliofanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.” (Isaya 47:14, 15) Naam, hivi karibuni washauri hao waongo wataona mambo motomoto. Moto wenyewe si moto mtamu wa kuotwa na watu, bali utakuwa moto wa uharibifu na uteketezaji, utakaowafichua washauri hao waongo kuwa mabua ovyo. Basi si ajabu kwamba washauri wa Babiloni watatimua mbio za hofu ya kubabaika! Tegemeo la mwisho la Babiloni likiisha kutokomea, atakosa wa kumwokoa. Ataupata msiba ule ule atakaokuwa ameiletea Yerusalemu.—Yeremia 11:12.

      21. Maneno ya unabii wa Isaya yanatimia jinsi gani na wakati gani?

      21 Mwaka wa 539 K.W.K., maneno haya yaliyopuliziwa yanaanza kutimizwa. Majeshi ya Wamedi na Waajemi yanaongozwa na Koreshi kuliteka jiji na kumwua mfalme mkazi, Belshaza. (Danieli 5:1-4, 30) Kwa usiku mmoja, Babiloni kapinduliwa kutoka cheo chake cha kuutawala ulimwengu. Hivyo zinakoma karne nyingi za ukuu wa Washemu, na sasa ulimwengu unadhibitiwa na Waarya. Babiloni yenyewe inaanza kipindi cha karne nyingi za kuzorota. Kufikia karne ya nne W.K., Babiloni ni rundo la “magofu.” (Yeremia 51:37) Hivyo unabii wa Isaya umetimizwa kabisa.

      Babiloni wa Kisasa

      22. Anguko la Babiloni linatufundisha somo gani juu ya kiburi?

      22 Unabii wa Isaya una mengi ya kufikiriwa sana. Kwanza, unakazia hatari za kiburi na kichwa kikubwa. Anguko la Babiloni yenye kiburi ni mfano unaoonyesha ukweli wa mithali hii ya Biblia: “Kiburi hutangulia uangamivu; na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.” (Mithali 16:18) Nyakati nyingine kiburi hutawala hali zetu za kutokamilika, lakini ‘kututumuka kwa kiburi’ kunaweza kuongoza mtu “ndani ya shutumu na mtego wa Ibilisi.” (1 Timotheo 3:6, 7) Basi, inafaa tutii shauri hili la Yakobo: “Jinyenyekezeni wenyewe machoni pa Yehova, naye atawakweza.”—Yakobo 4:10.

      23. Unabii wa Isaya unatusaidia tuwe na uhakika gani?

      23 Maneno haya ya kiunabii yanatusaidia pia tuwe na uhakika katika Yehova, aliye na nguvu nyingi kuliko wapinzani wake wote. (Zaburi 24:8; 34:7; 50:15; 91:14, 15) Hicho ni kikumbusha chenye faraja katika siku hizi ngumu. Uhakika katika Yehova unalitia nguvu azimio letu la kubaki bila lawama machoni pake, tukijua kwamba ‘wakati ujao wa mtu asiye na lawama utakuwa wenye amani.’ (Zaburi 37:37, 38, NW) Ni jambo la hekima nyakati zote kumtegemea Yehova wala si maarifa na nguvu zetu wenyewe tunapokabiliana na “vitendo vyenye hila za kiufundi” vya Shetani.—Waefeso 6:10-13, kielezi-chini.

      24, 25. (a) Kwa nini unajimu haupatani na kufikiri kuzuri, na bado watu wengi wanaugeukia kwa sababu gani? (b) Ni zipi baadhi ya sababu zinazowafanya Wakristo waepuke ushirikina?

      24 Sana-sana tunaonywa juu ya mazoea ya uwasiliani-roho, hasa unajimu. (Wagalatia 5:20, 21) Babiloni ilipoanguka, unajimu haukuacha kutawala watu. Jambo la kushangaza ni kwamba kitabu Great Cities of the Ancient World kinasema kuwa mipangilio ya nyota iliyochorwa na Wababiloni ‘imehama’ mahali mbalimbali ambapo zilikuwa zamani za kale, “kuonyesha kwamba shughuli yote hiyo [yaani, unajimu] ni upuuzi.” Na bado, unajimu unaendelea kusitawi, na magazeti mengi yana safu za utabiri wa nyota ambazo ni rahisi kupatikana na wasomaji wa magazeti hayo.

      25 Ni nini huwafanya watu—wengi wao wakiwa na elimu ya kutosha—watafute ushauri wa nyota au waingilie mazoea mengine ya kishirikina yasiyopatana na kufikiri kuzuri? Kichapo The World Book Encyclopedia kinasema hivi: “Labda ushirikina utakuwapo maishani mradi watu wanaogopana na kuwa na shaka juu ya wakati ujao.” Hofu na shaka huenda zikasukuma watu wawe na ushirikina. Hata hivyo, Wakristo huepuka ushirikina. Hawamhofu mwanadamu—Yehova ndiye tegemezo lao. (Zaburi 6:4-10) Nao hawana shaka juu ya wakati ujao; wanayajua makusudi ya Yehova yaliyofunuliwa na hawana shaka kwamba “shauri la BWANA lasimama milele.” (Zaburi 33:11) Kupatanisha maisha yetu na shauri la Yehova kunatuhakikishia wakati ujao wa kudumu, ulio na furaha.

      26. “Mawazowazo ya watu wenye hekima” yamekuwaje “ubatili”?

      26 Miaka ya hivi majuzi, watu fulani wamejaribu kutambua mambo ya wakati ujao kwa njia zilizo “za kisayansi” zaidi. Hata kuna somo linaloitwa taaluma ya wakati ujao, linalofafanuliwa kuwa “uchunguzi unaohusu mambo yanayowezekana kufanyika wakati ujao kwa kutegemea mielekeo ya sasa.” Kwa mfano, kule nyuma mwaka wa 1972 kikundi cha wasomi na wafanyabiashara kijulikanacho kama Chama cha Roma kilitabiri kwamba kufikia mwaka wa 1992 akiba zote za dhahabu, zebaki, zinki, na mafuta ya kuchimbwa zingemalizika. Ni kweli kwamba ulimwengu umekabiliwa na matatizo ya kuogofya tangu mwaka wa 1972, lakini utabiri huo ulikosea katika mambo yote. Dunia ingali ina akiba za dhahabu, zebaki, zinki, na mafuta ya kuchimbwa. Ni hakika kwamba mwanadamu amejichosha sana akijaribu kuutabiri wakati ujao, lakini matazamio anayokisia hukosa kutegemeka nyakati zote. Kweli, “mawazowazo ya watu wenye hekima ni ya ubatili”!—1 Wakorintho 3:20.

      Mwisho Unaokuja wa Babiloni Mkubwa

      27. Ni wakati gani na jinsi gani Babiloni Mkubwa ilianguka kama vile Babiloni ilivyoanguka mwaka wa 539 K.W.K.?

      27 Dini za kisasa zimeendeleza mengi ya mafundisho ya Babiloni ya kale. Hivyo basi, milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo imeitwa kwa kufaa Babiloni Mkubwa. (Ufunuo 17:5) Tayari muungano huo wa dini za kimataifa umeanguka kama Babiloni ya kale ilivyoanguka mwaka wa 539 K.W.K. (Ufunuo 14:8; 18:2) Mwaka wa 1919 mabaki ya ndugu za Kristo walitoka katika utekwa wa kiroho na kuyakung’utia mbali mavutano ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo, iliyo sehemu kuu ya Babiloni Mkubwa. Tangu wakati huo Jumuiya ya Wakristo imepoteza sana mavutano yake katika nchi nyingi ambako ilikuwa na nguvu zamani.

      28. Babiloni Mkubwa anajisifu kwa kusema nini, lakini ni nini kinachomngojea?

      28 Hata hivyo, anguko hilo lilikuwa kitangulizi tu cha uharibifu utakaopata dini ya uwongo hatimaye. Kwa kupendeza, unabii wa Ufunuo juu ya uharibifu wa Babiloni Mkubwa unatukumbusha maneno ya kiunabii yaliyoandikwa kwenye Isaya 47:8, 9. Kama Babiloni wa kale, Babiloni Mkubwa wa kisasa anasema hivi: “Naketi nikiwa malkia, nami si mjane, nami sitaona maombolezo kamwe.” Lakini “katika siku moja tauni zake zitakuja, kifo na kuomboleza na njaa kali, naye atachomwa kabisa kwa moto, kwa sababu Yehova Mungu, aliyemhukumu, ni mwenye nguvu.” Kwa hiyo, maneno ya kiunabii yaliyoandikwa katika Isaya sura ya 47 yangali ni onyo kwa wale ambao wangali wakishirikiana na dini ya uwongo. Ili waepuke kuharibiwa pamoja na dini hiyo, basi na waisikize amri hii iliyopuliziwa: “Tokeni kwake”!—Ufunuo 18:4, 7, 8.

      [Maelezo ya Chini]

      a Ili upate habari zaidi kuhusu usitawi wa mafundisho ya dini za uwongo, ona kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      b Kwa Kiebrania, “bikira, binti Babeli” ni msemo unaomaanisha Babiloni au wakaaji wa Babiloni. Yeye ni “bikira” kwa sababu hakuna mshindi amewahi kumteka nyara tangu awe serikali kubwa ya ulimwengu.

      c Usemi wa Kiebrania uliotafsiriwa “simkubali mtu ye yote” umefafanuliwa na wasomi kuwa “kifungu kigumu mno” kutafsiriwa. Biblia ya New World Translation huingiza neno “kwa fadhili” kutoa wazo la kwamba hakuna watu wowote wa nje ambao wangeruhusiwa kuja kumwokoa Babiloni. Tafsiri ya Jewish Publication Society hutafsiri hivi maneno hayo: ‘Sitaruhusu mwanadamu yeyote afanye upatanisho.’

      d Kitabu Nabonidus and Belshazzar, kilichoandikwa na Raymond Philip Dougherty, kinasema kwamba, ingawa Tarihi za Nabonidus hudai kwamba waliovamia Babiloni waliingia “bila kupigana,” mwanahistoria Mgiriki Xenophon huonyesha kuwa huenda ikawa damu nyingi ilimwagika.

      e Wengine wanafasiri usemi wa Kiebrania uliotafsiriwa “waabudu wa mbingu” kuwa “wagawanyaji wa mbingu.” Usemi huo ungerejezea lile zoea la kuzigawanya mbingu sehemu sehemu ili kupiga falaki.

      [Picha katika ukurasa wa 111]

      Babiloni mtafuta-anasa atashushwa chini kwenye vumbi

      [Picha katika ukurasa wa 114]

      Wanajimu wa Babiloni watashindwa kutabiri anguko lake

      [Picha katika ukurasa wa 116]

      Kalenda ya Kibabiloni inayohusu unajimu, milenia ya kwanza K.W.K.

      [Picha katika ukurasa wa 119]

      Hivi karibuni Babiloni wa kisasa atatokomea

  • Yehova Hutufundisha kwa Faida Yetu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Tisa

      Yehova Hutufundisha kwa Faida Yetu

      Isaya 48:1-22

      1. Wenye hekima huyaitikiaje maneno ya Yehova?

      YEHOVA anaposema, wenye hekima husikiliza kwa heshima nyingi na kuyaitikia maneno yake. Kila neno lisemwalo na Yehova lina manufaa kwetu, naye hupendezwa sana na masilahi yetu. Kwa mfano, moyo unajawa na uchangamfu ulioje tunapofikiria jinsi Yehova alivyowahutubia watu wa kale wa agano lake: “Laiti ungalisikiliza amri zangu!” (Isaya 48:18) Kwa kuwa mafundisho ya Mungu yamethibitishwa kuwa yenye thamani, hilo lapasa kutuvuta tumsikilize na kuufuata mwongozo wake. Maandishi ya unabii uliotimizwa yanaondoa shaka yoyote kuhusu azimio la Yehova la kuzitimiza ahadi zake.

      2. Maneno ya Isaya 48 yaliandikiwa nani, na ni nani wengine wanaoweza kunufaika nayo?

      2 Ushuhuda unaonyesha kwamba maneno ya sura ya 48 ya kitabu cha Isaya yaliandikiwa Wayahudi ambao wangekuwa wahamishwa Babiloni. Isitoshe, maneno hayo yana ujumbe ambao Wakristo leo hawawezi kuupuuza. Katika Isaya sura ya 47, Biblia ilitabiri anguko la Babiloni. Sasa Yehova anaeleza jambo analokusudia kuwafanyia wahamishwa Wayahudi waliomo katika jiji hilo. Yehova anahuzunika sana kwa kuwa wateule wake ni wanafiki na wanakataa kwa shingo ngumu kuziamini ahadi zake. Na bado anataka kuwafundisha kwa faida yao. Anaona mapema kwamba kutakuwako kipindi cha kusafishwa sana ambacho mwishowe kitafanya mabaki waaminifu warudishwe kwenye nchi yao.

      3. Ibada ya Yuda ilikuwa na kasoro gani?

      3 Lo, watu wa Yehova wamekengeuka mbali kama nini kutoka kwenye ibada safi! Maneno ya utangulizi ya Isaya yanahitaji kufikiriwa kwa makini: “Sikieni haya, enyi watu wa nyumba ya Yakobo, mnaoitwa kwa jina la Israeli, mliotoka katika maji ya Yuda; mnaoapa kwa jina la BWANA [“Yehova,” “NW”], na kumtaja Mungu wa Israeli, lakini si kwa kweli, wala si kwa haki. Maana hujiita wenyeji wa mji mtakatifu, hujitegemeza juu ya Mungu wa Israeli; BWANA wa majeshi ni jina lake.” (Isaya 48:1, 2) Unafiki kama nini! Ni wazi kwamba ‘kuapa kwa jina la Yehova’ ni kutumia jina la Mungu kidesturi tu. (Sefania 1:5) Kabla ya kuhamishiwa Babiloni, Wayahudi walimwabudu Yehova kwenye “mji mtakatifu,” Yerusalemu. Lakini ibada yao haikuwa ya moyo mweupe. Mioyo yao ilikuwa mbali sana na Mungu, na vitendo vyao vya ibada vilikuwa ‘si vya kweli, wala si vya haki.’ Hawakuwa na imani kama ile ya wazee wa ukoo.—Malaki 3:7.

      4. Ni ibada ya aina gani inayompendeza Yehova?

      4 Maneno ya Yehova yanatukumbusha kwamba ibada haipaswi kuwa desturi ya kijuujuu tu. Ni lazima ifanywe kwa hisia za moyoni. Utumishi wa kuonyesha tu—labda unaofanywa ili kuwafurahisha au kuwavutia wengine tu—si “vitendo vya ujitoaji-kimungu.” (2 Petro 3:11) Ibada ya mtu haikubaliki kwa Mungu eti kwa sababu tu mtu anajiita Mkristo. (2 Timotheo 3:5) Ni muhimu kutambua kwamba Yehova yuko, lakini huo ni mwanzo tu. Yehova anataka ibada ya nafsi yote, inayoongozwa na upendo wa kina kirefu na uthamini.—Wakolosai 3:23.

      Kutabiri Mambo Mapya

      5. Ni nini baadhi ya “mambo ya kale” yaliyotabiriwa na Yehova?

      5 Labda Wayahudi waliomo Babiloni wanahitaji kukumbushwa mambo. Kwa hiyo, Yehova anawakumbusha tena kwamba yeye ndiye Mungu wa unabii wa kweli: “Mimi nimehubiri mambo ya kale tangu zamani; naam, yalitoka katika kinywa changu, nikayadhihirisha; naliyatenda kwa ghafula, yakatokea.” (Isaya 48:3) “Mambo ya kale” ni mambo yale ambayo tayari Mungu ameyatimiza, kama vile kuwakomboa Waisraeli kutoka Misri na kuwapa Nchi ya Ahadi iwe urithi. (Mwanzo 13:14, 15; 15:13, 14) Matabiri ya jinsi hiyo hutoka katika kinywa cha Mungu; chanzo chake ni cha kimungu. Mungu hufanya wanadamu wasikie maagizo yake, nao wanapaswa kusukumwa na maagizo hayo wawe watiifu. (Kumbukumbu la Torati 28:15) Yeye huchukua hatua ya ghafula kuyatimiza matabiri yake. Kwa kuwa Yehova ndiye Mweza-Yote, hiyo inahakikisha kwamba kusudi lake linatimizwa.—Yoshua 21:45; 23:14.

      6. Wayahudi wamekuwa ‘wakaidi na waasi’ kwa kadiri gani?

      6 Watu wa Yehova wamekuwa ‘wakaidi na waasi.’ (Zaburi 78:8) Yeye anawaambia wazi hivi: “Wewe u mkaidi . . . shingo yako ni shingo ya chuma, na kipaji cha uso wako ni shaba.” (Isaya 48:4) Kama vile metali, Wayahudi ni wagumu kukunjwa—hawaambiliki. Hiyo ni sababu moja inayomfanya Yehova afunue mambo kabla hayajatukia. Asipoyafunua, watu wake watasema hivi kuhusu mambo ambayo Yehova amefanya: “Sanamu yangu imetenda haya; sanamu yangu ya kuchonga, na sanamu yangu ya kuyeyusha, imeyaamuru.” (Isaya 48:5) Je, yale ambayo Yehova anasema sasa yataleta angalau badiliko fulani juu ya Wayahudi wasio waaminifu? Mungu anawaambia hivi: “Umesikia haya; tazama haya yote; nanyi, je! hamtayahubiri? Nimekuonyesha mambo mapya tangu wakati huu, naam, mambo yaliyofichwa, usiyoyajua. Yameumbwa sasa, wala si tokea zamani; na kabla ya siku hii ya leo hukusikia habari yake; usije ukasema, Tazama, naliyajua.”—Isaya 48:6, 7.

      7. Wayahudi wahamishwa watalazimika kukiri nini, na wanaweza kutazamia nini?

      7 Isaya aliandika utabiri wa anguko la Babiloni kitambo kirefu kabla halijatukia. Sasa Wayahudi wakiwa wahamishwa Babiloni, wanaamrishwa kiunabii wafikirie sana utimizo wa utabiri huo. Je, sasa wanaweza kukana kwamba Yehova siye Mungu wa unabii uliotimizwa? Na kwa kuwa wakaaji wa Yuda wameona na kusikia kwamba Yehova ni Mungu wa kweli, je, hawana budi kuwatangazia wengine pia kweli hiyo? Neno la Yehova lililofunuliwa linatabiri mapya ambayo bado hayajatokea, kwa mfano ushindi wa Koreshi juu ya Babiloni na kufunguliwa kwa Wayahudi. (Isaya 48:14-16) Matukio hayo ya kugutusha yanaonekana ni kama yanatokea kwa kishindo cha kushangaza. Hakuna mtu angaliweza kuyaona mapema kwa kuzitazama tu hali za ulimwengu. Yanatokea kama mwujiza. Nani kayasababisha? Jibu ni wazi, kwani Yehova ndiye anayeyatabiri miaka 200 hivi mapema.

      8. Ni mambo gani mapya ambayo leo Wakristo wanatumainia kuyaona, na kwa nini wanaliamini kabisa neno la Yehova la kiunabii?

      8 Tena, Yehova anatekeleza neno lake kulingana na ratiba yake. Unabii mbalimbali uliotimizwa unathibitisha Uungu wake kwa Wayahudi wa nyakati za kale na hali kadhalika kwa Wakristo wa leo. Maandishi yaliyopo kuhusu unabii mwingi sana uliotimizwa wakati uliopita, ambao ndio “mambo ya kale,” yanahakikisha kwamba yale mambo mapya yaliyoahidiwa na Yehova, yaani “dhiki kubwa” inayokuja, kuokoka kwa “umati mkubwa” kwa kuipita dhiki hiyo, “dunia mpya,” na mengine kadha wa kadha, yatatimizwa pia. (Ufunuo 7:9, 14, 15; 21:4, 5; 2 Petro 3:13) Uhakikisho huo huwasukuma wale walio na mioyo ya kupenda haki leo wanene habari zake kwa bidii. Wao wanajihisi kama mtunga-zaburi, aliyesema hivi: “Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. Sikuizuia midomo yangu.”—Zaburi 40:9.

      Yehova Huonyesha Kujidhibiti

      9. Taifa la Israeli limekuwaje “mkosaji tangu kuzaliwa”?

      9 Wayahudi hawakuuamini unabii wa Yehova, na hiyo imewazuia kuyatii maonyo yake. Ndiyo sababu anaendelea kuwaambia hivi: “Naam, hukusikia; naam, hukujua; naam, tokea zamani sikio lako halikuzibuka; maana nalijua ya kuwa wewe watenda kwa hila nyingi, nawe umeitwa mkosaji tangu kuzaliwa kwako.” (Isaya 48:8) Yuda ameziba sikio asisikie habari za Yehova za mteremo. (Isaya 29:10) Tabia ya watu wa agano la Mungu inaonyesha kwamba taifa hilo ni “mkosaji tangu kuzaliwa.” Tangu kuzaliwa na hata muda wote wa historia yake, taifa la Israeli limekuwa na kawaida ya kuasi. Ukosaji na hila ni kasoro zilizowakolea watu hao, wala si dhambi za mara moja-moja tu.—Zaburi 95:10; Malaki 2:11.

      10. Kwa nini Yehova atajizuia?

      10 Je, hakuna tumaini? Liko. Ingawa Yuda amekuwa mwasi na mwenye hila, Yehova ni wa kweli na mwaminifu daima. Kwa kuliheshimu jina lake mwenyewe lililo kuu, ataangalia asiruke mipaka anapomimina hasira yake. Anasema hivi: “Kwa ajili ya jina langu nitaahirisha [“nitadhibiti,” “NW”] hasira yangu, na kwa ajili yako nitajizuia, ili nisifiwe, wala nisikukatilie mbali.” (Isaya 48:9) Ebu ona tofauti hiyo! Watu wa Yehova, Israeli na hata Yuda, wamekosa uaminifu kwake. Lakini Yehova atalitakasa jina lake, atende kwa njia itakayoliletea jina hilo sifa na heshima. Kwa sababu hiyo, yeye hatawakatilia mbali wateule wake.—Yoeli 2:13, 14.

      11. Kwa nini Mungu hataruhusu watu wake waangamizwe kabisa?

      11 Watu mmoja-mmoja wenye mioyo ya kupenda haki miongoni mwa Wayahudi wahamishwa wanaamshwa na kemeo la Mungu, kisha wanapiga moyo konde kuyasikiza mafundisho yake. Watu hao wanafarijiwa sana na tangazo hili rasmi: “Tazama, nimekusafisha, lakini si kama fedha; nimekuchagua katika tanuru ya mateso. Kwa ajili ya nafsi yangu, kwa ajili ya nafsi yangu, nitatenda haya; je! litiwe unajisi jina langu? Wala sitampa mwingine utukufu wangu.” (Isaya 48:10, 11) Majaribu makali—kama vile kuwa katika “tanuru ya mateso”—ambayo Yehova ameruhusu yawapate watu wake yamewatahini na kuwasafisha, yakafunua yaliyomo mioyoni mwao. Jambo kama hilo lilitendeka karne nyingi mapema Musa alipowaambia hivi babu zao wa kale: ‘BWANA Mungu wako alikuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako.’ (Kumbukumbu la Torati 8:2) Wajapokuwa na mtazamo wa uasi, Yehova hakuliangamiza taifa hilo wakati huo, wala sasa hataliangamiza litokomee. Kwa njia hiyo jina lake na heshima yake zitatukuzwa. Kama watu wake wangeangamizwa na Wababiloni, yeye hangetimiza agano lake, na hapo jina lake lingetiwa unajisi. Ingeonekana kana kwamba Mungu wa Israeli amekuwa hoi asiweze kuwaokoa watu wake.—Ezekieli 20:9.

      12. Wakristo wa kweli walisafishwaje wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza?

      12 Nyakati za kisasa pia, watu wa Yehova wamehitaji kusafishwa. Kule nyuma, mapema katika karne ya 20, wengi katika kile kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia walimtumikia Mungu wakitamani kwa moyo mweupe kumpendeza, lakini wengine walikuwa na makusudio mabaya, kama vile kujitafutia umashuhuri. Kikundi hicho kidogo kingehitaji kusafishwa kwanza kabla hakijaweza kushika usukani wa kuielekeza kazi ya kuhubiri habari njema ulimwenguni pote, ambayo unabii ulisema ingefanywa wakati wa mwisho. (Mathayo 24:14) Nabii Malaki alitabiri kwamba usafishaji huo hususa ungetimizwa kuhusiana na kuja kwa Yehova kwenye hekalu lake. (Malaki 3:1-4) Maneno yake yalitimizwa mwaka wa 1918. Wakristo wa kweli walikuwa wamepitia kipindi cha majaribu motomoto huku vita ya ulimwengu ya kwanza ikiwa imechacha, na majaribu hayo yalifikia upeo wakati Joseph F. Rutherford, aliyekuwa msimamizi wa Watch Tower Society wakati huo, alipofungwa gerezani pamoja na baadhi ya maofisa wenye kuongoza wa shirika hilo. Wakristo hao wenye moyo mweupe walinufaika kutokana na zile hatua za kusafishwa sana. Baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza walipiga moyo konde kuliko wakati mwingine wowote kumtumikia Mungu wao mkuu kwa njia yoyote ile atakayowaonyesha.

      13. Watu wa Yehova wameuitikiaje mnyanyaso katika ile miaka ya tangu vita ya ulimwengu ya kwanza?

      13 Tangu siku hizo, Mashahidi wa Yehova wamekabiliwa mara nyingi na minyanyaso yenye ukatili wa kupindukia. Lakini hiyo haijawafanya walitilie shaka neno la Muumba wao. Bali, wameyakumbuka maneno ya mtume Petro kwa Wakristo walionyanyaswa siku zake: ‘Mmetiwa kihoro kwa namna mbalimbali za majaribu, ili ubora wa imani yenu uliojaribiwa upatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo wa Yesu Kristo.’ (1 Petro 1:6, 7) Mnyanyaso motomoto hauangamizi uaminifu-maadili wa Wakristo wa kweli. Bali, hufunua kwamba wana makusudio safi kabisa. Huiongezea imani yao ubora uliojaribiwa na kuonyesha kina cha ujitoaji na upendo wao.—Mithali 17:3.

      ‘Mimi Ni wa Kwanza, Mimi Ni wa Mwisho’

      14. (a) Ni jinsi gani Yehova alivyo “wa kwanza” na “wa mwisho”? (b) Yehova alitimiza kazi zipi zenye nguvu kwa “mkono” wake?

      14 Sasa Yehova anawasihi watu wa agano lake kwa hisia changamfu: “Nisikilize mimi, Ee Yakobo; na Israeli, niliyekuita; mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho pia. Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja.” (Isaya 48:12, 13) Mungu si kama mwanadamu, kwani Yeye ni wa milele na hana kigeugeu. (Malaki 3:6) Yehova anatangaza rasmi hivi katika Ufunuo: “Mimi ndiye Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho.” (Ufunuo 22:13) Hakukuwako Mungu yeyote mweza yote kabla ya Yehova, wala hakutakuwako na yeyote baada yake. Yeye ndiye Mkuu Zaidi, Wa Milele, na Muumba. “Mkono” wake, yaani nguvu zake zikiwa katika hali ya kutumika, ndio ulioikaza dunia na kuzitandaza mbingu zenye nyota. (Ayubu 38:4; Zaburi 102:25) Anapoviita vitu alivyoviumba, vitu hivyo husimama chonjo, tayari kumtumikia.—Zaburi 147:4.

      15. Yehova “amempenda” Koreshi jinsi gani na kwa kusudi gani?

      15 Mwaliko mzito unaelekezwa kwa Wayahudi na hata kwa watu wasio Wayahudi: “Kusanyikeni, ninyi nyote, mkasikie; ni nani miongoni mwao aliyehubiri haya? BWANA amempenda; atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, na mkono wake utakuwa juu ya Wakaldayo. Mimi, naam, mimi, nimenena; naam, nimemwita; nimemleta, naye ataifanikisha njia yake.” (Isaya 48:14, 15) Yehova peke yake ndiye mwenye nguvu zote na anaweza kutabiri matukio kwa usahihi. Hakuna sanamu yoyote miongoni “mwao,” yaani miongoni mwa sanamu hizo ovyo, inayoweza kueleza mambo hayo. Ni Yehova, wala si sanamu hizo, ambaye “amempenda” Koreshi—yaani, Yehova amemchagua kwa kusudi fulani hususa. (Isaya 41:2; 44:28; 45:1, 13; 46:11) Yeye ametangulia kumwona Koreshi akitokea katika mandhari ya ulimwengu, akamtaja wazi kuwa ndiye mshindi atakayeteka Babiloni wakati ujao.

      16, 17. (a) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba Mungu hajatoa matabiri yake kwa siri? (b) Leo Yehova ameyajulishaje makusudi yake peupe?

      16 Yehova anaendelea kusema hivi kwa sauti nzuri ya mwaliko: “Nikaribieni, sikieni haya; tokea mwanzo sikunena kwa siri; tangu yalipokuwapo, mimi nipo.” (Isaya 48:16a) Matabiri kutoka kwa Yehova hayajatolewa kwa siri wala kujulishwa kwa washiriki wachache tu wa kikundi maalumu. Manabii wa Yehova walikuwa wasemaji waliosema mambo waziwazi kwa niaba ya Mungu. (Isaya 61:1) Walitangaza mapenzi ya Mungu peupe. Kwa mfano, matukio yaliyomhusu Koreshi hayakuwa mapya kwa Mungu wala hayakutukia bila yeye kuyaona kimbele. Miaka 200 hivi mapema, Mungu aliyatabiri matukio hayo waziwazi kupitia Isaya.

      17 Vivyo hivyo leo, Yehova haweki makusudi yake kuwa siri. Mamilioni ya watu katika mamia ya nchi na visiwa vya bahari hutangaza nyumba kwa nyumba, barabarani, na popote pale wawezapo juu ya onyo linalohusu mwisho unaokuja wa mfumo huu wa mambo, na pia juu ya habari njema za baraka zitakazokuja chini ya Ufalme wa Mungu. Kweli Yehova ni Mungu wa mawasiliano kuhusu makusudi yake.

      ‘Sikiliza Amri Zangu!’

      18. Yehova anatamani nini kuhusu watu wake?

      18 Akiwa ametiwa nguvu na roho ya Yehova, nabii anatangaza rasmi hivi: “Bwana MUNGU amenituma, na roho yake. BWANA, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.” (Isaya 48:16b, 17) Wonyesho huu wenye upendo wa kujali kwa Yehova unapasa kulihakikishia upya taifa la Israeli kwamba Mungu atawakomboa kutoka Babiloni. Yeye ndiye Mkombozi wao. (Isaya 54:5) Yehova anatamani kwa hisia za moyoni kwamba Waisraeli warudishe uhusiano wao naye na kuzisikiliza amri zake. Kutii maagizo ya kimungu ndio msingi wa ibada ya kweli. Waisraeli hawawezi kutembea katika njia ifaayo wasipofundishwa ‘njia iwapasayo kuifuata.’

      19. Yehova anasihi namna gani kwa hisia za kutoka moyoni?

      19 Tamaa ya Yehova kwamba watu wake wayaepuke maafa na kufurahia maisha inaelezwa kwa usemi wa kuvutia: “Laiti ungalisikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari.” (Isaya 48:18) Hapo, Muumba mweza-yote anawasihi kwa hisia nzuri kama nini za kutoka moyoni! (Kumbukumbu la Torati 5:29; Zaburi 81:13) Badala ya kwenda utekwani, Waisraeli wanaweza kufurahia amani maridhawa kama maji yanayotiririka mtoni. (Zaburi 119:165) Matendo yao ya haki yanaweza kuwa yasiyohesabika kama mawimbi ya bahari. (Amosi 5:24) Yehova ndiye anayependezwa kweli kweli na Waisraeli, naye anawasihi akiwaonyesha kwa upendo njia iwapasayo kuipitia. Jamani, laiti wangesikiliza!

      20. (a) Tamaa ya Mungu ni nini kuhusu Israeli wajapokuwa waasi? (b) Tunajifunza nini juu ya Yehova kutokana na njia zake za kushughulika na watu wake? (Ona sanduku katika ukurasa wa 133.)

      20 Ni baraka gani zingekuja ikiwa Israeli angetubu? Yehova anasema hivi: “Wazao wako wangalikuwa kama mchanga, na hao waliotoka katika tumbo lako kama chembe zake; jina lake lisingalikatika, wala kufutwa mbele zangu.” (Isaya 48:19) Yehova anawakumbusha watu wa ahadi yake kwamba mbegu ya Abrahamu ingekuwa nyingi, “kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani.” (Mwanzo 22:17; 32:12) Hata hivyo, wazao hawa wa Abrahamu wamekuwa waasi, na hawana haki ya kutimiziwa ahadi hiyo. Kwa kweli, matendo yao yamekuwa mabaya sana hivi kwamba kulingana na Sheria ya Yehova mwenyewe, jina la taifa lao linapasa kukatiliwa mbali. (Kumbukumbu la Torati 28:45) Na bado, Yehova hatamani watu wake wafutiliwe mbali wala hataki kuwatupa.

      21. Ni baraka gani tunazoweza kuzipata leo tukiyatafuta mafundisho ya Yehova?

      21 Kanuni zilizomo katika kifungu hicho chenye mkazo zinatumika kuwahusu waabudu wa Yehova leo. Yehova ndiye Chanzo cha uhai, na ndiye anayejua zaidi ya mtu mwingine yeyote jinsi itupasavyo kutumia maisha yetu. (Zaburi 36:9) Lengo la miongozo ambayo ametupa si kutunyang’anya furaha, bali ni kutunufaisha. Wakristo wa kweli huitikia kwa kutafuta kufundishwa na Yehova. (Mika 4:2) Maelekezo yake huilinda hali yetu ya kiroho na uhusiano wetu pamoja naye, tena hutukinga na mavutano ya Shetani yenye kufisidi. Tunapozithamini kanuni zilizo msingi wa sheria za Mungu, tunaona kwamba Yehova hutufundisha kwa faida yetu. Tunatambua kwamba “amri zake si zenye kulemea.” Na hatutakatiliwa mbali.—1 Yohana 2:17; 5:3.

      ‘Haya, Tokeni Katika Babeli!’

      22. Wayahudi waaminifu wanahimizwa kufanya nini, na wanahakikishiwa mambo gani?

      22 Babiloni atakapoanguka, je, Wayahudi wowote wataonyesha hali ifaayo ya moyoni? Je, watajifaidi na ukombozi wa Mungu, warudie nchi yao, na kuirudisha ibada safi? Ndiyo. Maneno ya Yehova yanayofuata yanaonyesha kwamba ana hakika itakuwa hivyo. “Haya, tokeni katika Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo; hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya, yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni, BWANA amemkomboa mtumishi wake, Yakobo. Wala hawakuona kiu alipowaongoza jangwani; alitoa maji katika mwamba kwa ajili yao; pia akaupasua mwamba, maji yakatoka kwa nguvu.” (Isaya 48:20, 21) Watu wa Yehova wanahimizwa kiunabii waondoke Babiloni bila kukawia. (Yeremia 50:8) Ukombozi wao ni lazima ujulishwe hadi miisho ya dunia. (Yeremia 31:10) Baada ya lile tukio la Kutoka Misri, Yehova aliwaruzuku watu wake walipokuwa wakipita katika nchi zenye jangwa. Na atawaruzuku watu wake hali kadhalika washikapo njia ya kurudi nyumbani kutoka Babiloni.—Kumbukumbu la Torati 8:15, 16.

      23. Ni nani ambao hawatafurahia amani itolewayo na Mungu?

      23 Ni lazima Wayahudi wazingatie kanuni nyingine muhimu kuhusu matendo ya Yehova ya kuokoa. Huenda wale walio na mwelekeo wa kufuata haki wakataabika kwa sababu ya dhambi zao, lakini hawataangamizwa. Hata hivyo, mambo ni tofauti kwa wasio haki. “Hapana amani kwa wabaya, asema BWANA.” (Isaya 48:22) Watenda-dhambi wasiotubu hawataipokea amani ambayo Mungu amewawekea wanaompenda. Matendo ya wokovu hayafanywi kwa manufaa ya waovu wenye shingo ngumu au wale wasioamini. Yanafanywa kwa manufaa ya wale tu walio na imani. (Tito 1:15, 16; Ufunuo 22:14, 15) Waovu hawana ile amani itokayo kwa Mungu.

      24. Ni nini kilichofanya watu wa Mungu washangilie nyakati za kisasa?

      24 Mwaka wa 537 K.W.K., Waisraeli waaminifu walikuwa na shangwe kubwa walipopata fursa ya kuondoka Babiloni. Mwaka wa 1919 watu wa Mungu walishangilia walipofunguliwa kutoka utekwa wa Kibabiloni. (Ufunuo 11:11, 12) Walijawa na tumaini, wakaishika fursa hiyo kuupanua utendaji wao. Ni kweli, moyo mkuu ulihitajika ili kikosi hicho kidogo cha Wakristo kiweze kutumia vizuri nafasi mpya zilizotokea za kuhubiri katika ulimwengu wenye uhasama. Lakini kwa msaada wa Yehova, walianza kuzihubiri habari njema kwa makini. Historia inashuhudia kwamba Yehova aliwabariki.

      25. Kwa nini ni muhimu kuyafuata maagizo ya Mungu ya haki kwa makini?

      25 Sehemu hii ya unabii wa Isaya inakazia kwamba Yehova hutufundisha kwa faida yetu. Ni muhimu sana tuyafuate maagizo ya Mungu ya haki kwa makini. (Ufunuo 15:2-4) Tukijikumbusha hekima na upendo wa Mungu, hiyo itatusaidia tujipatanishe na mambo yale ambayo Yehova anasema yanafaa. Amri zake zote ni za kutuletea faida.—Isaya 48:17, 18.

      [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 133]

      Mungu Mweza-Yote Ajizuia

      “Nitaahirisha [“nitadhibiti,” “NW”] hasira yangu . . . nitajizuia,” Yehova akawaambia Waisraeli waasi-imani. (Isaya 48:9) Taarifa kama hizo hutusaidia kuelewa kwamba Mungu huweka mfano bora kabisa wa kutotumia mamlaka vibaya. Ni kweli kwamba hakuna aliye na nguvu nyingi kuliko Mungu. Hiyo ndiyo sababu tunamtaja kuwa Mwenye nguvu zote, Mwenye uwezo wote. Wakati anapotumia cheo “Mwenyezi” kujitaja, anafanya hivyo kwa haki. (Mwanzo 17:1) Si kwamba tu nguvu zake hazina mipaka, bali pia mamlaka yake ni kamili kwa sababu ya cheo chake akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu mzima aliouumba. Ndiyo sababu hakuna awezaye kuthubutu kuuzuia mkono wa Yehova wala kumwambia, “Unafanya nini wewe?”—Danieli 4:35.

      Hata hivyo, Mungu si mwepesi wa hasira, hata wakati anapohitajika kuonyesha nguvu zake juu ya adui zake. (Nahumu 1:3) Yehova anaweza ‘kudhibiti hasira yake,’ ndiposa yeye hufafanuliwa kwa usahihi kuwa “si mwepesi wa hasira” kwa sababu upendo—wala si hasira—ndiyo sifa yake kuu. Hasira yake, wakati inapoonyeshwa, huwa ya uadilifu daima, ya haki daima, yenye kudhibitiwa daima.—Kutoka 34:6; 1 Yohana 4:8.

      Kwa nini Yehova hutenda kwa njia hiyo? Ni kwa sababu yeye husawazisha nguvu zake za kuweza mambo yote na zile sifa zake nyingine tatu zilizo kuu—hekima, haki, na upendo. Yeye hutumia nguvu zake kwa kupatana daima na sifa zile nyingine.

      [Picha katika ukurasa wa 122]

      Ujumbe wa Isaya wa kurudishwa unaandaa dalili ya tumaini kwa ajili ya Wayahudi waaminifu walio uhamishoni

      [Picha katika ukurasa wa 124]

      Wayahudi walikuwa na mwelekeo wa kuzisifu sanamu kwa matendo yaliyofanywa na Yehova

      1. Ishtari 2. Sehemu ya ukuta wa matofali iliyopambwa na kutiwa nakshi kwenye Njia ya Maandamano kule Babiloni 3. Alama ya joka la kumfananisha Marduki

      [Picha katika ukurasa wa 127]

      “Tanuru ya mateso” inaweza kufunua kama makusudio yetu ya kumtumikia Yehova ni safi au si safi

      [Picha katika ukurasa wa 128]

      Wakristo wa kweli wamekabiliwa na minyanyaso yenye ukatili wa kupindukia

  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi

      “Wakati wa Nia Njema”

      Isaya 49:1-26

      1, 2. (a) Isaya alifurahia baraka gani? (b) Ni nani wanaohusika katika maneno ya kiunabii yaliyoandikwa katika nusu ya kwanza ya Isaya sura ya 49?

      WANADAMU wote waaminifu wamefurahia kibali cha Mungu na ulinzi wake kwa muda mrefu. Lakini Yehova haonyeshi nia yake njema hivi hivi tu. Ni lazima mtu aistahili baraka hiyo isiyo na kifani. Isaya ni mmoja wa wale walioistahili. Alifurahia upendeleo wa Mungu, akatumiwa na Yehova kama chombo cha kujulisha wengine mapenzi Yake. Mfano wa jambo hilo umeandikwa katika nusu ya kwanza ya sura ya 49 ya unabii wa Isaya.

      2 Maneno hayo yanaelekezwa kiunabii kwa mbegu ya Abrahamu. Katika utimizo wa kwanza, mbegu hiyo ni taifa la Israeli lililotokana na Abrahamu. Hata hivyo, sehemu kubwa ya lugha inayotumiwa hapo inahusu ile Mbegu ya Abrahamu iliyotumainiwa kwa muda mrefu, Mesiya aliyeahidiwa. Maneno hayo yaliyopuliziwa yanatumika pia kuwahusu ndugu za kiroho za Mesiya, wanaokuwa sehemu ya mbegu ya kiroho ya Abrahamu na ya “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 3:7, 16, 29; 6:16) Hasa, sehemu hii ya unabii wa Isaya inafafanua uhusiano uliopo kati ya Yehova na Mwanawe mpendwa, Yesu Kristo.—Isaya 49:26.

      Awekwa Rasmi na Kulindwa na Yehova

      3, 4. (a) Mesiya anategemezwa na nani? (b) Mesiya anasema na nani?

      3 Mesiya anafurahia nia njema au kibali cha Mungu. Yehova anampa mamlaka na sifa za kumtambulisha kuwa anastahili kutimiza utume wake. Basi, kwa kufaa, Mesiya huyo wa wakati ujao anasema hivi: “Nisikilizeni, enyi visiwa; tegeni masikio yenu, enyi kabila za watu mlio mbali sana; BWANA ameniita tangu tumboni; toka tumbo la mama yangu amenitaja jina langu.”—Isaya 49:1.

      4 Hapa Mesiya anaelekeza maneno yake kwa jamii za watu wa “mbali sana.” Ingawa ni Wayahudi ambao wameahidiwa Mesiya, huduma yake itatumika kubariki mataifa yote. (Mathayo 25:31-33) Ingawa “visiwa” na “kabila za watu” hazimo katika agano pamoja na Yehova, zinapaswa kumsikiza Mesiya wa Israeli kwa sababu anatumwa kuwaletea wanadamu wote wokovu.

      5. Mesiya anatajwaje jina hata kabla hajazaliwa akiwa binadamu?

      5 Unabii unasema kwamba Yehova atamtaja Mesiya kwa jina kabla hajazaliwa akiwa mwanadamu. (Mathayo 1:21; Luka 1:31) Muda mrefu kabla Yesu hajazaliwa, anaitwa “Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.” (Isaya 9:6) Imanueli, jina ambalo linaelekea kuwa ni la mwana wa Isaya, linakuja kuwa jina la kiunabii la Mesiya pia. (Isaya 7:14; Mathayo 1:21-23) Hata lile jina la kwanza ambalo Mesiya ataitwa, yaani Yesu, linatabiriwa kabla ya kuzaliwa kwake. (Luka 1:30, 31) Jina hilo limetokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Yehova Ni Wokovu.” Ni wazi kuwa Yesu hakujiweka mwenyewe kuwa Kristo.

      6. Kinywa cha Mesiya ni kama upanga mkali kwa njia gani, naye amefichwa na kusitiriwa jinsi gani?

      6 Maneno ya Mesiya ya kiunabii yanaendelea kusema: “Naye anifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali; katika kivuli cha mkono wake amenisitiri; naye amenifanya kuwa mshale uliosuguliwa; katika podo lake amenificha.” (Isaya 49:2) Wakati ufikapo ili Mesiya wa Yehova aanze huduma yake ya kidunia mwaka wa 29 W.K., kweli maneno na matendo ya Yesu yanakuwa kama silaha kali zilizosuguliwa, zinazoweza kuipenya mioyo ya wasikilizaji. (Luka 4:31, 32) Maneno na matendo yake yanaichokora ghadhabu ya adui mkuu wa Yehova, Shetani, na wawakilishi wake. Kuanzia wakati Yesu anapozaliwa, Shetani anajaribu kumwua, lakini Yesu ni kama mshale uliofichwa katika podo la Yehova mwenyewe.a Anaweza kuutegemea ulinzi wa Baba yake akiwa na uhakika. (Zaburi 91:1; Luka 1:35) Yesu anatoa uhai wake kwa ajili ya wanadamu katika wakati uliowekwa. Lakini wakati utafika ajitokeze akiwa shujaa hodari wa kimbingu mwenye silaha tofauti, upanga mkali unaotoka katika kinywa chake. Safari hii, upanga huo mkali unawakilisha mamlaka ya Yesu ya kutamka hukumu na kuzifikiliza juu ya adui za Yehova.—Ufunuo 1:16.

      Kazi za Mtumishi wa Mungu Si za Bure

      7. Maneno ya Yehova kwenye Isaya 49:3 yanatumiwa kuhusu nani, na kwa nini?

      7 Sasa Yehova anasema maneno haya ya kiunabii: “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika wewe nitatukuzwa [“nitaonyesha urembo wangu,” “NW”].” (Isaya 49:3) Yehova analitaja taifa la Israeli kuwa mtumishi wake. (Isaya 41:8) Lakini Yesu Kristo ndiye Mtumishi namba moja wa Mungu. (Matendo 3:13) Hakuna kiumbe chochote cha Mungu kinachoweza kuonyesha “urembo” wa Yehova kuliko Yesu. Kwa hiyo, ingawa kwa halisi maneno hayo yanaelekezwa kwa Israeli, yanatumika kumhusu Yesu hasa.—Yohana 14:9; Wakolosai 1:15.

      8. Watu wa Mesiya mwenyewe wanamwitikiaje, lakini Mesiya anategemea nani kuhukumu mafanikio yake?

      8 Lakini je, si kweli kwamba Yesu anadharauliwa na kukataliwa na wengi wa watu wake mwenyewe? Ndiyo. Kwa ujumla, taifa la Israeli halimkubali Yesu kuwa Mtumishi mtiwa-mafuta wa Mungu. (Yohana 1:11) Huenda marika wa Yesu wakayaona yote anayoyatimiza akiwa duniani kama yasiyo na thamani kubwa, hata yasiyofaa kitu. Ndipo sasa Mesiya anapogusia hali hiyo ya kuonekana kana kwamba ameshindwa kuitimiza huduma yake: “Nimejitaabisha bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida.” (Isaya 49:4a) Maneno hayo hayasemwi eti kwa sababu Mesiya amevunjika moyo. Yafikirie yale anayosema sasa: “Hakika hukumu yangu ina BWANA, na thawabu yangu ina [“mshahara wangu una,” “NW”] Mungu wangu.” (Isaya 49:4b) Mafanikio ya Mesiya hayaamuliwi na wanadamu, bali na Mungu.

      9, 10. (a) Ni utume gani ambao Mesiya amepewa na Yehova, na anapata matokeo gani? (b) Wakristo leo wanaweza kutiwaje moyo na yaliyompata Mesiya?

      9 Yesu anahangaikia kupata kibali au nia njema ya Mungu hasa. Katika unabii, Mesiya anasema hivi: “Sasa BWANA asema hivi, yeye aliyeniumba tangu tumboni niwe mtumishi wake, ili nimletee Yakobo tena, na Israeli wakusanyike mbele zake tena;(maana mimi nimepata heshima mbele ya macho ya BWANA, na Mungu wangu amekuwa nguvu zangu).” (Isaya 49:5) Mesiya anakuja kugeuza mioyo ya wana wa Israeli imrudie Baba yao wa kimbingu. Walio wengi hawaitikii, lakini wengine wanaitikia. Hata hivyo, mshahara wake halisi una Yehova Mungu. Mafanikio yake hayapimwi kwa viwango vya wanadamu, bali kwa viwango vya Yehova mwenyewe.

      10 Leo, nyakati fulani huenda wafuasi wa Yesu wakahisi kana kwamba wanatoa jasho la bure. Mahali fulani fulani, huenda matokeo ya huduma yao yakaonekana kuwa si kitu yakilinganishwa na kiasi cha kazi na jitihada wanazofanya. Hata hivyo, wao huvumilia kwa kutiwa moyo na mfano wa Yesu. Wanatiwa nguvu pia na maneno ya mtume Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa sababu hiyo, ndugu zangu wapendwa, iweni imara, wasioondoleka, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu ya jasho si bure kuhusiana na Bwana.”—1 Wakorintho 15:58.

      “Nuru ya Mataifa”

      11, 12. Mesiya amekuwaje “nuru ya mataifa”?

      11 Katika unabii wa Isaya, Yehova anamtia moyo Mesiya kwa kumkumbusha kwamba kuwa Mtumishi wa Mungu si “neno dogo.” Yesu anapaswa “kuziinua kabila za Yakobo, na kuwarejeza watu wa Israeli waliohifadhiwa.” Tena Yehova anaeleza hivi: “Zaidi ya hayo nitakutoa uwe nuru ya mataifa, upate kuwa wokovu wangu hata miisho ya dunia.” (Isaya 49:6) Kwa kuwa huduma ya Yesu ya kidunia imewekewa mipaka ifanyike katika Israeli peke yake, itakuwaje kwamba anayatolea mataifa nuru “hata miisho ya dunia”?

      12 Maandishi ya Biblia yanaonyesha kwamba “nuru ya mataifa” itokayo kwa Mungu haikuzimika Yesu alipoondoka duniani. Karibu miaka 15 baada ya kufa kwa Yesu, mishonari Paulo na Barnaba walinukuu unabii wa Isaya 49:6 na kuutumia kuhusu wanafunzi wa Yesu, ndugu zake wa kiroho. Walieleza hivi: “Yehova ameweka amri juu yetu kwa maneno haya, ‘Nimewaweka nyinyi rasmi kuwa nuru ya mataifa, ili nyinyi muwe wokovu hadi ncha ya dunia.’” (Matendo 13:47) Kabla ya kifo chake mwenyewe, Paulo aliziona habari njema za wokovu zikienezwa si kwa Wayahudi peke yao bali pia kwa “viumbe vyote chini ya mbingu.” (Wakolosai 1:6, 23) Leo, mabaki ya ndugu watiwa-mafuta wa Kristo wanaiendeleza kazi hiyo. Wanatumikia wakiwa “nuru ya mataifa” katika nchi zaidi ya 230 ulimwenguni kote kwa kuungwa mkono na “umati mkubwa” wenye mamilioni ya watu.—Ufunuo 7:9.

      13, 14. (a) Mesiya na wafuasi wake wametendewaje kwa kufanya kazi ya kuhubiri? (b) Ni hali gani ambazo zimebadilika?

      13 Hakika Yehova amekuwa ndiye nguvu inayotegemeza Mesiya Mtumishi wake, ndugu watiwa-mafuta wa Mesiya, na wale wote wa umati mkubwa wanaoshirikiana nao kuiendeleza kazi ya kuzihubiri habari njema. Ni kweli kwamba wanafunzi wa Yesu wamedharauliwa na kupingwa kama yeye. (Yohana 15:20) Lakini Yehova hufanya hali zibadilike kwa wakati wake mwenyewe, ili awaokoe na kuwathawabisha watumishi wake waaminifu-washikamanifu. Kwa habari ya Mesiya, “anayedharauliwa” na ‘kuchukiwa na taifa hili,’ Yehova anaahidi hivi: “Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya BWANA aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua.”—Isaya 49:7.

      14 Baadaye mtume Paulo aliwaandikia Wakristo katika Filipi juu ya hali hizo zilizotabiriwa kuwa zingebadilika. Alieleza habari za Yesu kuwa ni mtu aliyekuwa ameaibishwa juu ya mti wa mateso lakini akakwezwa na Mungu baada ya hapo. Yehova alimpa Mtumishi wake “cheo cha juu zaidi akampa kwa fadhili jina lililo juu ya kila jina jingine, ili katika jina la Yesu kila goti likunjwe.” (Wafilipi 2:8-11) Wafuasi waaminifu wa Kristo wameonywa kwamba wao pia watanyanyaswa. Lakini wao, kama Mesiya wanahakikishiwa kwamba watapata nia njema ya Yehova.—Mathayo 5:10-12; 24:9-13; Marko 10:29, 30.

      “Wakati Wenye Kukubalika Hasa”

      15. Ni “wakati” gani maalumu unaotajwa katika unabii wa Isaya, na hiyo inatoa wazo gani?

      15 Unabii wa Isaya unaendelea kwa kutoa taarifa yenye umaana mkubwa. Yehova anamwambia Mesiya hivi: “Wakati uliokubalika [“wakati wa nia njema,” “NW”] nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa.” (Isaya 49:8a) Unabii unaofanana na huo umeandikwa kwenye Zaburi 69:13-18. Mtunga-zaburi anarejezea “wakati wa nia njema,” akitumia usemi ‘wakati upendezao.’ Maneno haya yanatokeza wazo la kwamba nia njema ya Yehova na ulinzi wake hutolewa kwa njia maalumu lakini kwa kipindi hususa cha muda mfupi tu.

      16. Wakati wa Yehova wa nia njema kwa Israeli wa kale ulikuwa lini?

      16 Wakati huo wa nia njema ulikuwa lini? Maneno hayo yaliposemwa mara ya kwanza yalikuwa sehemu ya unabii wa kurudishwa na yalitabiri kurudi kwa Wayahudi kutoka uhamishoni. Taifa la Israeli lilipata wakati wa nia njema lilipoweza “kuiinua nchi” na kumiliki tena “urithi uliokuwa ukiwa.” (Isaya 49:8b) Hawakuwa ‘wafungwa’ tena Babiloni. Wakati wa safari yao ya kurudi nyumbani, Yehova alihakikisha kwamba ‘hawakuona njaa’ wala ‘hawakuona kiu,’ wala ‘hari haikuwapiga’ kwa vyovyote. Waisraeli waliotawanyika walimiminika kama kundi kuirudia nchi yao “kutoka mbali . . . , kutoka kaskazini, na kutoka magharibi.” (Isaya 49:9-12) Ijapokuwa utimizo huo wa kwanza wa kutazamisha ulitukia, Biblia inaonyesha kwamba unabii huu unatumika kwa njia nyinginezo zilizo pana.

      17, 18. Yehova aliweka wakati gani wa nia njema katika karne ya kwanza?

      17 Kwanza, wakati wa kuzaliwa kwa Yesu, malaika walitangaza amani na nia njema ya Mungu, au upendeleo wake, kuelekea wanadamu. (Luka 2:13, 14) Nia njema hiyo ilitolewa iweze kupatikana, si na wanadamu wote kwa ujumla, bali na wale tu waliodhihirisha imani katika Yesu. Baadaye Yesu aliusoma peupe unabii wa Isaya 61:1, 2 na kuutumia umhusu yeye mwenyewe akiwa mtangazaji wa “mwaka wa Yehova wenye kukubalika.” (Luka 4:17-21) Mtume Paulo alitaja kwamba Kristo alipokea ulinzi maalumu wa Yehova katika siku za mwili wake. (Waebrania 5:7-9) Kwa hiyo wakati huu wa nia njema unatumika kuhusu upendeleo ambao Mungu alimwonyesha Yesu wakati wa maisha yake akiwa binadamu.

      18 Hata hivyo, unabii huu una matumizi zaidi. Baada ya kuyanukuu maneno ya Isaya kuhusu wakati wa nia njema, Paulo aliendelea kusema hivi: “Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2) Paulo aliyaandika maneno haya miaka 22 baada ya kifo cha Yesu. Ushuhuda unaonyesha kuwa kutaniko la Kikristo lilipozaliwa Pentekoste ya 33 W.K., Yehova aliurefusha mwaka wake wa nia njema ili uwahusishe pia wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo.

      19. Wakristo leo wanaweza kunufaikaje na wakati wa Yehova wa nia njema?

      19 Namna gani wafuasi wa Yesu leo wasiotiwa mafuta kuwa warithi wa ufalme wa kimbingu wa Mungu? Je, wale walio na tumaini la kidunia wanaweza kunufaika na wakati huu uliokubalika? Ndiyo. Kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinaonyesha kwamba huu ni wakati wa nia njema kwa upande wa Yehova kuelekea umati mkubwa ‘utakaotoka katika dhiki kubwa’ ili kufurahia maisha katika dunia-paradiso. (Ufunuo 7:13-17) Kwa hiyo, Wakristo wote wana fursa ya kukitumia vizuri kipindi hiki kifupi ambacho Yehova huwatolea nia yake njema wanadamu wasio wakamilifu.

      20. Wakristo wanaweza kuepukaje kulikosa kusudi la fadhili isiyostahiliwa ya Yehova?

      20 Mtume Paulo alitoa onyo kabla ya kuutangaza wakati wa Yehova unaokubalika. Aliwasihi Wakristo ‘wasiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi lake.’ (2 Wakorintho 6:1) Kwa hiyo, Wakristo hutumia kila fursa wampendeze Mungu na kufanya mapenzi yake. (Waefeso 5:15, 16) Inafaa wafuate onyo la upole la Paulo: “Jihadharini, akina ndugu, kwa kuhofu kusije kamwe kukasitawi katika yeyote kati yenu moyo mwovu unaokosa imani kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai; lakini fulizeni kuhimizana kwa bidii mtu na mwenzake kila siku, maadamu yaweza kuitwa ‘Leo,’ kwa kuhofu yeyote kati yenu asije akafanywa kuwa mgumu kwa nguvu ya udanganyifu ya dhambi.”—Waebrania 3:12, 13.

      21. Ni taarifa gani yenye shangwe inayomalizia sehemu ya kwanza ya Isaya sura ya 49?

      21 Huku maongezi ya kiunabii kati ya Yehova na Mesiya wake yakifikia mwisho, Isaya anatamka taarifa yenye shangwe: “Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, naye atawahurumia watu wake walioteswa.” (Isaya 49:13) Lo, maneno hayo murua ni faraja iliyoje leo kwa Waisraeli wa zamani na kwa Mtumishi mkuu wa Yehova, Yesu Kristo, na pia kwa watumishi watiwa-mafuta wa Yehova na waandamani wao ambao ni “kondoo wengine”!—Yohana 10:16.

      Yehova Hawasahau Watu Wake

      22. Yehova anakaziaje kwamba hatawasahau watu wake kamwe?

      22 Sasa Isaya anaendelea kuripoti matamko rasmi ya Yehova. Anatabiri kwamba Waisraeli wahamishwa wataelekea kuchoka kabisa na kupoteza tumaini. Isaya anasema hivi: “Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.” (Isaya 49:14) Je, hii ni kweli? Je, Yehova amewaacha watu wake na kuwasahau? Akitenda kama msemaji wa Yehova, Isaya anaendelea kusema hivi: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” (Isaya 49:15) Hilo ni itikio lenye upendo kama nini kutoka kwa Yehova! Upendo wa Mungu kwa watu wake ni mkubwa kuliko ule wa mama kwa mtoto wake. Yeye anawafikiria daima waaminifu-washikamanifu wake. Anawakumbuka kana kwamba majina yao yamechorwa katika mikono yake: “Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.”—Isaya 49:16.

      23. Paulo aliwatiaje moyo Wakristo watumainie kuwa Yehova hatawasahau?

      23 Katika barua yake kwa Wagalatia, mtume Paulo aliwahimiza Wakristo hivi: “Acheni tusife moyo katika kufanya lililo bora, kwa maana katika majira yapasayo tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.” (Wagalatia 6:9) Aliwaandikia Waebrania maneno haya ya kuwatia moyo: “Mungu si asiye mwadilifu ili asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake.” (Waebrania 6:10) Hatupaswi kamwe kuhisi kwamba Yehova amewasahau watu wake. Kama Sayuni wa kale, Wakristo wana sababu nzuri ya kushangilia na kumngoja Yehova kwa subira. Yeye huyashika imara masharti ya agano lake na ahadi zake.

      24. Sayuni atarudishwa jinsi gani, na atauliza maswali gani?

      24 Yehova anatoa faraja ya ziada kupitia Isaya. Wale ‘waharibuo Sayuni,’ wawe ni Wababiloni au ni Wayahudi waasi-imani, wameacha kuwa tisho. “Watoto” wa Sayuni, yaani Wayahudi wahamishwa wanaobaki wakiwa waaminifu-washikamanifu kwa Yehova, ‘wamefanya haraka.’ ‘Watajikusanya.’ Wakiisha kurudi Yerusalemu upesi, Wayahudi waliorejezwa kwao watakuwa mapambo kwa jiji lao kuu, sawa na vile “bibi arusi” huvikwa “kwa uzuri.” (Isaya 49:17, 18) Mahali pa Sayuni pamefanywa ‘ukiwa.’ Basi wazia mshangao wa Sayuni anapokaliwa na wakazi wengi sana kwa ghafla hivi kwamba makao yake yanaonekana kuwa membamba, yasiyomtosha. (Soma Isaya 49:19, 20.) Si ajabu kwamba anauliza ni wapi walikotoka watoto hawa wote: “Utasema moyoni mwako, Ni nani aliyenizalia watoto hawa, na mimi nimefiwa na watoto wangu [“nami ni tasa,” “NW”], nami ni peke yangu, nimehamishwa, ninatanga-tanga huko na huku? Tena ni nani aliyewalea hawa? Tazama, naliachwa peke yangu; hawa je! walikuwa wapi?” (Isaya 49:21) Hiyo ni furaha iliyoje kwa Sayuni ambaye hapo kwanza alikuwa tasa!

      25. Nyakati za kisasa, Israeli wa kiroho alirudishwa katika hali gani?

      25 Maneno haya yana utimizo wa kisasa. Katika ile miaka migumu ya vita ya ulimwengu ya kwanza, Israeli wa kiroho alipatwa na kipindi cha ukiwa na utekwa. Lakini alirudishwa akaja kuwa katika paradiso ya kiroho. (Isaya 35:1-10) Inaweza kusemwa kwamba alifurahi sana, kama jiji lile ambalo Isaya alielezea habari zake, kwa kujikuta akimiminikwa na waabudu wengi wa Yehova wenye shangwe na utendaji mwingi.

      “Ishara kwa Kabila za Watu”

      26. Yehova anawapa watu wake waliokombolewa mwelekezo gani?

      26 Kwa njia ya unabii, sasa Yehova anampeleka Isaya kwenye wakati ambao watu Wake watafunguliwa kutoka Babiloni. Je, watapokea mwelekezo wowote wa kimungu? Yehova anajibu hivi: “Tazama, nitawainulia mataifa mkono wangu [“ishara,” “NW”], na kuwatwekea kabila za watu bendera [“ishara,” “NW”] yangu; nao wataleta wana wako vifuani mwao, na binti zako watachukuliwa mabegani mwao.” (Isaya 49:22) Katika utimizo wa kwanza, jiji la Yerusalemu, ambalo hapo kwanza lilikuwa makao makuu ya serikali na mahali pa hekalu la Yehova, linakuwa “ishara” ya Yehova. Hata watu mashuhuri na wenye uweza mwingi kutoka mataifa mengine, kama vile “wafalme” na “mabinti-wafalme,” wanawasaidia Waisraeli katika safari yao ya kurudi huko. (Isaya 49:23a, “NW”) Wafalme Waajemi, Koreshi na Artashasta Longimano, pamoja na watu wa nyumba zao wanakuwa miongoni mwa wasaidizi hao. (Ezra 5:13; 7:11-26) Halafu maneno ya Isaya yanatumika kwa njia nyingine tena.

      27. (a) Katika utimizo ulio mkubwa zaidi, ni “ishara” gani ambayo watu wataiendea makundi makundi? (b) Matokeo yatakuwa nini mataifa yote yalazimikapo kuuinamia utawala wa Mesiya?

      27 Isaya 11:10 hutaja “ishara kwa kabila za watu.” Mtume Paulo aliyatumia maneno hayo kumhusu Kristo Yesu. (Waroma 15:8-12) Hivyo, katika utimizo ulio mkubwa zaidi, Yesu na watawala wenzake waliotiwa mafuta kwa roho ni “ishara” ya Yehova ambayo kabila za watu zinaiendea makundi makundi. (Ufunuo 14:1) Katika wakati ufaao, kabila zote za dunia—hata jamii za watawala wa leo—zitalazimika kuuinamia utawala wa Mesiya. (Zaburi 2:10, 11; Danieli 2:44) Matokeo yatakuwa nini? Yehova anasema hivi: “Nawe utajua ya kuwa mimi ni BWANA, tena waningojeao hawatatahayarika.”—Isaya 49:23b.

      “Sasa Wokovu Wetu Uko Karibu Zaidi”

      28. (a) Yehova anatumia maneno gani kuwahakikishia watu wake tena kwamba watafunguliwa? (b) Ni wajibu gani ambao Yehova angali nao kuhusu watu wake?

      28 Baadhi ya wale walio uhamishoni Babiloni huenda wakajiuliza hivi, ‘Je, kweli itawezekana Israeli wafunguliwe?’ Yehova analitia maanani swali hilo kwa kuuliza hivi: “Je! aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?” (Isaya 49:24) Ndiyo. Yehova anawahakikishia hivi: “Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye jabari wataokoka.” (Isaya 49:25a) Uhakikisho huo unafariji kama nini! Zaidi ya hilo, Yehova huwaonyesha watu wake nia njema kwa kujiwajibisha sana kuwalinda. Yeye anasema waziwazi hivi: “Nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu.” (Isaya 49:25b) Wajibu huo ungali upo. Kama ilivyoandikwa kwenye Zekaria 2:8, Yehova anawaambia watu wake hivi: ‘Yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho langu.’ Ni kweli kwamba sasa tunafurahia kipindi cha nia njema, wakati ambao makundi-makundi ya watu kotekote duniani yana fursa ya kumiminika yakienda kwenye Sayuni wa kiroho. Hata hivyo, kipindi hicho cha nia njema kitafikia mwisho.

      29. Ni tazamio gani la kuogofya linalowangoja wale wanaokataa kumtii Yehova?

      29 Ni jambo gani litakalowapata wale wanaokataa kwa shingo ngumu kumtii Yehova na hata wanawanyanyasa waabudu wake? Yeye anasema hivi: “Hao wanaokuonea nitawalisha nyama yao wenyewe, nao watalewa kwa kuinywa damu yao wenyewe, kama kwa mvinyo mpya.” (Isaya 49:26a) Loo, ni tazamio la kuogofya kama nini! Wapinzani hao wenye shingo ngumu hawana maisha marefu ya wakati ujao. Wataangamizwa. Hivyo, kwa kuwaokoa watu wake na hata kuwaangamiza adui zao, Yehova ataonwa kuwa Mwokozi. “Wote wenye mwili watajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako, na Mkombozi wako ni Mwenye enzi wa Yakobo.”—Isaya 49:26b.

      30. Yehova amewafanyia watu wake maokozi gani, na bado atafanya nini?

      30 Maneno hayo yalitumika kwanza Yehova alipomtumia Koreshi kuwaweka watu Wake huru kutoka katika utumwa wa Babiloni. Yalitumika jinsi hiyo hiyo mwaka wa 1919 Yehova alipomtumia Mwana wake mtawazwa, Yesu Kristo, kuwafungua watu Wake kutoka utumwa wa kiroho. Hivyo, Biblia huwataja wote wawili, Yehova na Yesu, kuwa waokozi. (Tito 2:11-13; 3:4-6) Yehova ni Mwokozi wetu, na Yesu, aliye Mesiya, ni ‘Wakili wake Mkuu.’ (Matendo 5:31) Kweli Mungu amefanya maokozi mazuri ajabu kupitia Yesu Kristo. Yehova huzitumia habari njema kuwaweka huru watu walio na mioyo ya kupenda haki kutoka katika utumwa wa dini ya uwongo. Yeye huwakomboa kutoka katika utumwa wa dhambi na kifo kupitia ile dhabihu ya fidia. Mwaka wa 1919 aliwatoa ndugu za Yesu katika utumwa wa kiroho. Kisha ataokoa umati mkubwa wa wanadamu waaminifu kutoka kwenye uharibifu utakaowapata watenda-dhambi katika vita ya Har-Magedoni inayokaribia kasi.

      31. Wakristo wanapaswa kuitikiaje kwa sababu wao ni wapokezi wa nia njema ya Mungu?

      31 Basi, ni pendeleo kama nini kuwa wapokezi wa nia njema ya Mungu! Acheni sisi sote tutumie kwa hekima wakati huu unaokubalika. Kisha na tutende kupatana na uharaka wa nyakati zetu, huku tukiyatii maneno ya Paulo kwa Waroma: “Nyinyi watu mwayajua majira, kwamba tayari ni saa ya nyinyi kuamka kutoka katika usingizi, kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko tulipopata kuwa waamini. Usiku umesonga sana; mchana umekaribia. Kwa hiyo acheni tuondoe kazi za giza na acheni tuvae silaha za nuru. Kama katika wakati wa mchana acheni tujiendeshe kwa adabu, si katika sherehe zenye makelele ya ulevi na vipindi vya kulewa, si katika ngono isiyo halali na mwenendo mlegevu, si katika zogo na wivu. Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, na msiwe mkipanga kimbele kwa ajili ya tamaa za mwili.”—Waroma 13:11-14.

      32. Watu wa Mungu wamehakikishiwa mambo gani?

      32 Yehova ataendelea kuwapendelea wale wanaotii shauri lake. Atawaandalia nguvu na uwezo mbalimbali unaohitajiwa ili kutimiza kazi ya kuhubiri habari njema. (2 Wakorintho 4:7) Yehova atawatumia watumishi wake kama vile anavyomtumia Kiongozi wao, Yesu. Atafanya kinywa chao kiwe “kama upanga mkali” ili waifikie mioyo ya wasikivu kwa ujumbe wa habari njema. (Mathayo 28:19, 20)  Atawalinda watu wake “katika kivuli cha mkono wake.” Watafichwa “katika podo lake” kama “mshale uliosuguliwa.” Kwa kweli, Yehova hatawaacha watu wake!—Zaburi 94:14; Isaya 49:2, 15.

      [Maelezo ya Chini]

      a “Hakuna shaka kwamba Shetani alitambua kuwa Yesu ndiye Mwana wa Mungu na kwamba ndiye aliyetajwa na unabii kuwa atamponda kichwa (Mwa 3:15), na kwa hiyo alijaribu juu chini kumwangamiza Yesu. Lakini, malaika Gabrieli alipokuwa akimtangazia Maria kuhusu kutungwa mimba ya uhai wa Yesu, alimwambia hivi: ‘Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Zaidi Sana itakufunika kivuli. Kwa sababu hiyo pia kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.’ (Lu 1:35) Yehova alimlinda Mwana wake. Jitihada za kumwangamiza Yesu akiwa kitoto kichanga hazikufaulu.”—Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 868, lililochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      [Picha katika ukurasa wa 139]

      Mesiya ni kama “mshale uliosuguliwa” katika podo la Yehova

      [Picha katika ukurasa wa 141]

      Mesiya amekuwa “nuru ya mataifa”

      [Picha katika ukurasa wa 147]

      Upendo wa Mungu kwa watu wake ni mkubwa kuliko ule wa mama kwa mtoto wake

  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Moja

      “Msiwatumainie Wakuu”

      Isaya 50:1-11

      1, 2. (a) Wayahudi hawasikizi shauri gani lililopuliziwa, na matokeo ni nini? (b) Kwa nini Yehova anauliza hivi: “Iko wapi hati ya talaka”?

      “MSIWATUMAINIE wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. . . . Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake, aliyezifanya mbingu na nchi.” (Zaburi 146:3-6) Laiti Wayahudi wanaoishi siku za Isaya wangefuata shauri la mtunga-zaburi! Laiti wangemtumainia “Mungu wa Yakobo” kuliko kuitumainia Misri au taifa jingine lolote la kipagani! Ndipo, wakati ambapo adui za Yuda wangemvamia, Yehova angechukua hatua kumlinda. Hata hivyo, Yuda amekataa kumwomba Yehova msaada. Matokeo ni kwamba, Yehova ataruhusu jiji la Yerusalemu liharibiwe, na wakaaji wa Yuda wapelekwe utekwani Babiloni.

      2 Yuda atajilaumu mwenyewe. Hana haki ya kudai kwamba uangamivu wake umetokea kwa sababu Yehova ametenda hila au amepuuza agano lake na taifa hilo. Muumba si mvunja-maagano. (Yeremia 31:32; Danieli 9:27; Ufunuo 15:4) Yehova anakazia uhakika huo kwa kuwauliza Wayahudi hivi: “Iko wapi hati ya talaka ya mama yenu, ambayo kwa hiyo naliachana naye?” (Isaya 50:1a) Chini ya Sheria ya Kimusa, mwanamume anayemtaliki mke wake ni lazima ampe hati ya talaka. Kisha mwanamke huyo anakuwa huru kuwa wa mwanamume mwingine. (Kumbukumbu la Torati 24:1, 2) Katika maana ya mfano, Yehova amempa Israeli, ule ufalme ulio dada ya Yuda, hati ya jinsi hiyo, lakini Yuda hakupewa.a Bado Yehova ndiye ‘mume na mmilikaji’ wa Yuda. (Yeremia 3:8, 14, NW) Yuda hayuko huru kamwe kuwa mwenzi wa mataifa ya kipagani. Uhusiano wa Yehova pamoja na Yuda utaendelea “mpaka Shilo [Mesiya] aje.”—Mwanzo 49:10, NW.

      3. Kwa nini Yehova ‘anawauza’ watu wake?

      3 Vilevile, Yehova anauliza Yuda hivi: “Nimewauza ninyi kwa nani katika watu wanaoniwia?” (Isaya 50:1b) Wayahudi hawatapelekwa katika utekwa Babiloni kulipia deni fulani ambalo Yehova amejiletea. Yehova si kama Mwisraeli maskini anayelazimika kumaliza madeni yake kwa kuwauza watoto wake kwa mkopeshaji. (Kutoka 21:7) Bali, Yehova anaonyesha sababu halisi itakayofanya watu wake wafanywe watumwa: “Ninyi mliuzwa kwa sababu ya maovu yenu; tena mama yenu ameachwa kwa sababu ya makosa yenu.” (Isaya 50:1c) Wayahudi ndio wamemwacha Yehova; siye amewaacha.

      4, 5. Yehova anawaonyeshaje watu wake upendo, lakini Yuda anaitikiaje?

      4 Swali la Yehova linalofuata linaonyesha wazi kwamba anawapenda watu wake: “Basi, nilipokuja, mbona hapakuwa na mtu? nilipoita, mbona hapakuwa na mtu aliyenijibu?” (Isaya 50:2a) Ni kana kwamba Yehova ameingia nyumbani mwa watu wake kwa kutumia watumishi wake manabii kuwasihi wamrudie kwa mioyo yao yote. Lakini wao wamekaa kimya. Wayahudi hao wanaona ni afadhali wapate msaada kwa kumtegemea mwanadamu wa ardhini, na nyakati nyingine hata wanageukia Misri.—Isaya 30:2; 31:1-3; Yeremia 37:5-7.

      5 Je, Misri ni mwokozi wa kutegemeka kuliko Yehova? Inaonekana kwamba Wayahudi hao wasio waaminifu wameyasahau matukio yaliyoongoza kwenye kuzaliwa kwa taifa lao karne nyingi mapema. Yehova anawauliza hivi: “Je! mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? au je! mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu. Mimi nazivika mbingu weusi, nami nafanya nguo ya magunia kuwa kifuniko chao.”—Isaya 50:2b, 3.

      6, 7. Yehova alionyeshaje nguvu zake za kuokoa wakati Misri ilipotokeza tisho?

      6 Mwaka wa 1513 K.W.K., Misri ilikuwa mkandamizi—si mkombozi aliyetumainiwa—wa watu wa Mungu. Waisraeli walikuwa watumwa katika nchi hiyo ya kipagani. Lakini Yehova akawakomboa, nao ulikuwa ukombozi wa kusisimua kama nini! Kwanza alileta Mapigo Kumi juu ya nchi hiyo. Baada ya pigo la kumi lenye maangamizi makubwa zaidi, Farao wa Misri aliwahimiza Waisraeli waondoke nchini. (Kutoka 7:14–12:31) Lakini, punde tu baada ya hapo, Farao akabadili nia. Akavikusanya vikosi vyake, akashika njia kwenda kuwashurutisha Waisraeli warudi Misri. (Kutoka 14:5-9) Jeshi la askari Wamisri likiwa nyuma ya Waisraeli, na Bahari Nyekundu ikiwa mbele yao, Waisraeli wakawa mtegoni! Lakini Yehova alikuwapo kuwapigania.

      7 Yehova akawazima Wamisri kwa kuweka nguzo ya wingu kati yao na Waisraeli. Upande wa Wamisri wa wingu hilo kubwa kulikuwako giza, lakini katika upande wa Waisraeli kukawa na nuru. (Kutoka 14:20) Hapo basi, huku majeshi ya Misri yakiwa yamebanwa, Yehova “akaifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wa nguvu utokao mashariki, usiku kucha, akaifanya bahari kuwa nchi kavu.” (Kutoka 14:21) Maji yakiisha kutenganishwa, watu wote—wanaume, wanawake, na watoto—wakaweza kuivuka salama Bahari Nyekundu. Watu wa Yehova walipofika mbali kuikaribia ng’ambo ya pili ya ufuo, Yehova akaliinua wingu. Wamisri wakatifua vumbi wakiwafuata na kujivurumisha baharini. Watu wa Yehova waliposalimika ufuoni, Yehova akayafungulia maji, yakazamisha Farao na majeshi yake. Hivyo ndivyo Yehova alivyowapigania watu wake. Lo, ni kitia-moyo kilichoje kwa Wakristo leo!—Kutoka 14:23-28.

      8. Mwishowe wakaaji wa Yuda wanaenda uhamishoni kwa kupuuza maonyo gani?

      8 Kufikia wakati wa Isaya, miaka mia saba imepita tangu kuwe na ushindi huo wa kimungu. Yuda sasa ni taifa kamili. Nyakati nyingine, linafanya mapatano ya kibalozi na serikali za kigeni, kama vile Ashuru na Misri. Lakini viongozi wa mataifa hayo ya kipagani hawatumainiki. Kila wakati, wao huweka masilahi yao wenyewe mbele ya maagano yoyote wanayoyafanya pamoja na Yuda. Manabii wanaongea kwa jina la Yehova na kuwaonya watu wasiwatumainie wanadamu hao, lakini wapi, wanaziba masikio. Mwishowe, Wayahudi watahamishiwa Babiloni wakae huko miaka 70 ya kutumikishwa. (Yeremia 25:11) Hata hivyo, Yehova hatawasahau watu wake, wala hatawatupilia mbali kwa wakati usio dhahiri. Wakati uliowekwa ukifika, atawakumbuka, awafungulie njia ya kurejea kwenye nchi yao wakarudishe ibada safi. Kwa kusudi gani? Ili wajitayarishe kwa ajili ya kuja kwa Shilo, yule atakayetiiwa na watu wote!

      Shilo Aja

      9. Shilo ni nani, naye ni mwalimu wa aina gani?

      9 Karne zinapita. “Kikomo kamili cha wakati” kinawasili, kisha yule aitwaye Shilo, yaani Bwana Yesu Kristo, anatokea duniani. (Wagalatia 4:4; Waebrania 1:1, 2) Kwa kuwa Yehova amemteua mwandamani wake wa karibu zaidi kuwa Msemaji wake kwa Wayahudi, hiyo inaonyesha kwamba Yehova anawapenda sana watu wake. Yesu anakuwa msemaji wa aina gani? Wa hali ya juu kabisa! Licha ya Yesu kuwa msemaji, yeye ni mwalimu pia—Mwalimu Stadi. Hiyo haishangazi, kwa maana anafunzwa na Mfunzi wa ajabu—Yehova Mungu mwenyewe. (Yohana 5:30; 6:45; 7:15, 16, 46; 8:26) Jambo hilo linahakikishwa na yale ambayo Yesu anasema kiunabii kupitia Isaya: “Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno [“neno,” “NW”] yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.”—Isaya 50:4.b

      10. Yesu anaigaje upendo wa Yehova kwa watu Wake, na anaitikiwa jinsi gani?

      10 Kabla Yesu hajaja duniani, alifanya kazi akiwa karibu na Baba yake mbinguni. Uhusiano mchangamfu ulio kati ya Baba na Mwana unaelezwa kishairi kwenye Mithali 8:30: “Ndipo nilipokuwa pamoja naye [Yehova], kama stadi wa kazi; . . . nikifurahi daima mbele zake.” Yesu alipata shangwe kubwa kwa kumsikiliza Baba yake. Aliwapenda “wanadamu” jinsi Baba yake alivyowapenda. (Mithali 8:31) Yesu anapokuja duniani, anamjibu ‘kwa neno yeye aliyechoka.’ Anaanza huduma yake kwa kusoma kifungu chenye faraja kutoka unabii wa Isaya: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kutangaza habari njema kwa walio maskini, . . . kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa.” (Luka 4:18; Isaya 61:1) Lo, habari njema kwa maskini! Burudisho kwa waliochoka sana! Tangazo hilo linapaswa kuwaletea watu shangwe iliyoje! Wengine wanashangilia—lakini si wote. Mwishowe, wengi wanazikataa sifa zinazotambulisha kwamba Yesu alifundishwa na Yehova.

      11. Ni nani wanaokuja chini ya nira pamoja na Yesu, nao wanapata nini?

      11 Hata hivyo, wengine wanataka kusikia mengi zaidi. Wanaterema kupata mwaliko huu wa Yesu unaochangamsha moyo: “Njoni kwangu, nyinyi nyote mnaomenyeka na kulemezwa mizigo, nami hakika nitawaburudisha nyinyi. Chukueni nira yangu juu yenu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na wa hali ya chini moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu.” (Mathayo 11:28, 29) Kati ya watu wanaomkaribia Yesu, kuna wale wanaume ambao baadaye wanakuwa mitume wake. Wanajua kwamba ili waje wawe na Yesu chini ya nira moja, ni lazima watie bidii. Mojawapo la mambo yanayohusika katika bidii hiyo ni kuzihubiri habari njema za Ufalme hadi miisho ya dunia. (Mathayo 24:14) Mitume na wanafunzi wengine wanapojihusisha na kazi hiyo, wanakuta kwamba kwa kweli inaburudisha nafsi zao. Kazi hiyo hiyo inatimizwa na Wakristo waaminifu leo, nao wanapata shangwe za namna ile ile kwa kuishiriki.

      Yeye Si Mkaidi

      12. Yesu anaonyesha kwamba anamtii Baba yake wa kimbingu kwa njia zipi?

      12 Yesu hasahau kamwe kusudi lake la kuja duniani—kufanya mapenzi ya Mungu. Maoni yake yametabiriwa hivi: “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma.” (Isaya 50:5) Yesu anamtii Mungu daima. Hata anafikia kusema hivi: “Mwana hawezi kufanya hata kitu kimoja kwa uanzisho wake mwenyewe, ila tu kile atazamacho Baba akifanya.” (Yohana 5:19) Katika maisha yake kabla hajawa mwanadamu, Yesu alifanya kazi akiwa karibu na Baba yake kwa mamilioni, hata mabilioni, ya miaka. Na anaendelea kufuata maagizo ya Yehova baada ya kuja duniani. Basi sembuse sisi wafuasi wa Kristo wasio wakamilifu kujichunga sana ili tufuate mwelekezo wa Yehova!

      13. Ni mambo gani yanayomngoja Yesu kule mbele, lakini anaonyeshaje kuwa ana moyo mkuu?

      13 Mwana mzaliwa pekee wa Yehova ananyanyaswa na baadhi ya wale wanaomkataa, na jambo hilo pia limetabiriwa: “Naliwatolea wapigao mgongo wangu, na wang’oao ndevu mashavu yangu; sikuficha uso wangu usipate fedheha na kutemewa mate.” (Isaya 50:6) Kulingana na unabii, Mesiya atateswa na kuaibishwa na wapinzani wake. Yesu anajua ataaibishwa. Na anajua atanyanyaswa hivyo kwa kadiri gani. Hata hivyo, wakati wake duniani unapokaribia kumalizika, haonyeshi hofu. Anapiga moyo konde akiwa mgumu kama gumegume na kwenda Yerusalemu, ambako uhai wake wa kibinadamu utakoma. Huko njiani, Yesu anawaambia wanafunzi wake hivi: “Sisi hapa, tunasonga mbele kupanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu, na waandishi, nao watamhukumu adhabu ya kifo na watamkabidhi kwa watu wa mataifa, nao watamfanyia ucheshi na watamtemea mate na kumpiga mijeledi na kumuua, lakini siku tatu baadaye atafufuliwa.” (Marko 10:33, 34) Dhuluma yote hiyo itachochewa na makuhani wakuu na waandishi, wanaume ambao kulingana na kiwango cha ujuzi wao wanapaswa kutambua kwamba haifai kutenda hivyo.

      14, 15. Maneno ya Isaya kwamba Yesu angepigwa na kuaibishwa yanatimizwaje?

      14 Usiku wa Nisani 14, 33 W.K., Yesu yumo katika bustani ya Gethsemane pamoja na baadhi ya wafuasi wake. Anasali. Ghafula, kundi la wafanya-ghasia linatokea na kumpeleka kizuizini. Lakini yeye haogopi. Anajua Yehova yu pamoja naye. Yesu anawahakikishia mitume wake waliojawa na hofu kuwa kama angalitaka angaliweza kumsihi Baba yake apeleke malejioni zaidi ya 12 ya malaika ili kumwokoa, lakini anaongezea hivi: “Katika kisa hicho, Maandiko yangetimizwaje?”—Mathayo 26:36, 47, 53, 54.

      15 Kila jambo lililotabiriwa kuhusu majaribu na kifo cha Mesiya linatimia. Baada ya kesi iliyoundwa kilaghai kufanyika mbele ya Sanhedrini, Yesu anahojiwa na Pontio Pilato, naye anaagiza Yesu apigwe viboko. Askari Waroma ‘wanampiga kichwani kwa tete na kumtemea mate.’ Hivyo maneno ya Isaya yanatimizwa. (Marko 14:65; 15:19; Mathayo 26:67, 68) Ingawa Biblia haitaji kwamba baadhi ya ndevu za Yesu zinang’olewa—hiyo ikiwa ni ishara ya madharau mengi—hakuna shaka kwamba inatukia hivyo, sawa na vile Isaya alivyotabiri.c—Nehemia 13:25.

      16. Yesu anaonyesha mwenendo wa namna gani anapopatwa na mikazo mikali mno, na kwa nini haoni aibu?

      16 Yesu anaposimama mbele ya Pilato, haombiombi kwamba uhai wake usikomeshwe, bali anadumisha heshima yake kwa utulivu, akijua kwamba ni lazima afe ili Maandiko yatimizwe. Gavana huyo Mroma anapoonyesha wazi kwamba ana mamlaka ya kumhukumu Yesu auawe au afunguliwe, Yesu anajibu hivi bila woga: “Wewe hungekuwa na mamlaka hata kidogo dhidi yangu isipokuwa uwe ulikuwa umepewa hiyo kutoka juu.” (Yohana 19:11) Askari wa Pilato wanamtenda Yesu mambo yasiyo ya ubinadamu, lakini wanashindwa kumtia aibu. Mbona aone aibu? Yeye haadhibiwi kwa haki kwa sababu ya kukiuka sheria fulani. Bali, ananyanyaswa kwa ajili ya uadilifu. Kwa habari hiyo, unabii zaidi wa Isaya unatimizwa: “Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama gumegume, nami najua ya kuwa sitaona haya.”—Isaya 50:7.

      17. Yehova amemtegemeza Yesu kwa njia zipi muda wote wa huduma yake?

      17 Yesu anafaulu kuwa na moyo mkuu kwa sababu anamtumaini Yehova kabisa. Jinsi anavyojichukua inaonyesha kwamba anayafuata maneno haya ya Isaya kwa ukamili: “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye hasimu yangu? Na anikaribie basi. Tazama, Bwana MUNGU atanisaidia; ni nani atakayenihukumu kuwa mkosa? tazama hao wote watachakaa kama vazi; nondo atawala.” (Isaya 50:8, 9) Siku ya ubatizo wa Yesu, Yehova anamtangaza kuwa mwenye haki akiwa mwana wa kiroho wa Mungu. Kwa kweli, sauti ya Mungu mwenyewe inasikiwa pindi hiyo ikisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” (Mathayo 3:17) Maisha ya Yesu ya kidunia yanapokaribia kumalizika, anaposali akiwa amepiga magoti katika bustani ya Gethsemane, ‘malaika kutoka mbinguni anamtokea na kumtia nguvu.’ (Luka 22:41-43) Kwa hiyo Yesu anajua kwamba Baba yake anaukubali mwendo wa maisha yake. Mwana huyu mkamilifu wa Mungu hajatenda dhambi. (1 Petro 2:22) Adui zake wanamshtaki kwa uwongo kuwa mvunja-Sabato, mlevi, na mtu mwenye roho waovu, lakini Yesu havunjiwi heshima na mashtaka yao ya uwongo. Mungu yuko pamoja naye, basi ni nani awezaye kumpinga?—Luka 7:34; Yohana 5:18; 7:20; Waroma 8:31; Waebrania 12:3.

      18, 19. Wakristo watiwa-mafuta wamepatwa na mambo gani yaliyompata Yesu pia?

      18 Yesu anawaonya wanafunzi wake hivi: “Ikiwa wameninyanyasa mimi, watawanyanyasa nyinyi pia.” (Yohana 15:20) Muda si muda, mambo yanayotukia yanathibitisha ukweli wa maneno hayo. Kwenye Pentekoste ya 33 W.K., roho takatifu inawajilia wanafunzi waaminifu wa Yesu, na hapo kutaniko la Kikristo linazaliwa. Haujapita muda, viongozi wa kidini wanajaribu kuikandamiza kazi ya kuhubiri ya wanaume na wanawake hao waaminifu ambao sasa wanashirikiana na Yesu wakiwa sehemu ya “mbegu ya Abrahamu” na kufanywa wana wa kiroho wa Mungu. (Wagalatia 3:26, 29; 4:5, 6) Ingawa Wakristo watiwa-mafuta wanasimama imara upande wa uadilifu, tangu karne ya kwanza mpaka sasa wamelazimika kushindana na propaganda za uwongo na mnyanyaso mkatili sana kutoka kwa adui za Yesu.

      19 Na bado wanayakumbuka maneno ya Yesu yenye kutia moyo: “Wenye furaha ni nyinyi watu wawashutumupo na kuwanyanyasa nyinyi na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo ovu dhidi yenu kwa ajili yangu. Shangilieni na kuruka kwa shangwe, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa katika mbingu.” (Mathayo 5:11, 12) Hivyo basi, Wakristo watiwa-mafuta wanaona fahari hata chini ya shambulio kali kupita yote. Hata wapinzani wao wasemeje, Mungu amekwisha kuwatangaza rasmi kuwa waadilifu. Machoni pake, wao ‘hawana waa na lawama yoyote.’—Wakolosai 1:21, 22.

      20. (a) Ni akina nani wanaowaunga mkono Wakristo watiwa-mafuta, nao wamejionea nini? (b) Ni jinsi gani Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine” wanavyokuja kuwa na ulimi wa wale waliofundishwa?

      20 Nyakati za kisasa, Wakristo watiwa-mafuta wanaungwa mkono na “umati mkubwa” wa “kondoo wengine.” Wao pia wanasimama upande wa uadilifu. Kwa hiyo, wameteseka pamoja na ndugu zao watiwa-mafuta na “wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Yehova amewatangaza rasmi kuwa waadilifu wakiwa na tazamio la kuiokoka “dhiki kubwa.” (Ufunuo 7:9, 14, 15; Yohana 10:16; Yakobo 2:23) Hata ikiwa wapinzani wao wanaonekana kuwa wenye nguvu sasa hivi, unabii wa Isaya unasema kwamba wakati wa Mungu ukiwadia, wapinzani hao watakuwa kama vazi lililoliwa na nondo, linalofaa kutupiliwa mbali tu. Kwa sasa, Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine” pia wanaendelea kuwa na nguvu kwa kusali kwa ukawaida, kujifunza Neno la Mungu, na kuhudhuria mikutano ya ibada. Hivyo wanafundishwa na Yehova na kujifunza kusema wakitumia ulimi wa wale waliofundishwa.

      Litumainie Jina la Yehova

      21. (a) Ni nani wale wanaotembea katika nuru, na kuna matokeo gani kwao? (b) Ni nini kinachowapata wale wanaotembea gizani?

      21 Sasa angalia utofautiano wa kushangaza: “Nani kati yenu amchaye Mwenyezi-Mungu? Nani anayetii maneno ya mtumishi wake? Kama yupo atembeaye gizani bila taa, amtumainie Mwenyezi-Mungu, na kumtegemea Mungu wake.” (Isaya 50:10, “Biblia Habari Njema”) Wale wanaoisikiliza sauti ya Yesu Kristo, Mtumishi wa Mungu, hutembea katika nuru. (Yohana 3:21) Si kwamba tu wanalitumia jina la Mungu, Yehova, bali pia wanamtumainia mwenye jina hilo. Hata ikiwa wakati mmoja walitembea gizani, sasa hawawaogopi wanadamu. Wanamwegemea Mungu. Lakini, wale wanaoendelea kutembea gizani wanashikwa na hali ya kumwogopa mwanadamu. Ndivyo ilivyo kuhusu Pontio Pilato. Ingawa anajua kwamba Yesu hana hatia ya mambo ya uwongo ambayo ameshtakiwa, woga unamzuia ofisa huyo Mroma kumfungua Yesu. Askari Waroma wanamwua Mwana wa Mungu, lakini Yehova anamfufua na kumvika taji la utukufu na heshima. Namna gani Pilato? Kulingana na mwanahistoria Myahudi Flavius Josephus, miaka minne tu baada ya kifo cha Yesu, mtu mwingine alipewa cheo cha Pilato cha kuwa gavana Mroma, kisha Pilato akaagizwa arudi Roma kujibu mashtaka ya kosa zito. Namna gani wale Wayahudi waliosababisha kifo cha Yesu? Muda unaopungua miongo minne baadaye, majeshi ya Roma yaliharibu Yerusalemu na kusababisha wakaaji wake wauawe au wapelekwe utumwani. Hakuna matazamio maangavu kwa wale wanaopendelea giza!—Yohana 3:19.

      22. Kwa nini kuwategemea wanadamu ili kupata wokovu ni upumbavu wa mwisho?

      22 Kuwategemea wanadamu ili kupata wokovu ni upumbavu wa mwisho. Unabii wa Isaya unaeleza sababu: “Tazama, ninyi nyote mwashao moto, mjifungiao hiyo mienge; endeni ninyi katika mwali wa moto wenu, na katikati ya mienge [“cheche,” “NW”] mliyoiwasha. Mtayapata haya kwa mkono wangu; mtalala kwa huzuni.” (Isaya 50:11) Viongozi wa kibinadamu hutokea na kutokomea. Mtu mwenye karama ya kipekee huenda akanasa fikira za watu kwa muda. Lakini hata mwanadamu aliye na moyo mweupe pepepe ana mipaka ya mambo awezayo kutimiza. Badala ya mtu huyo kuwasha moto unaowaka kwa fujo, kama vile wafuasi wake wanavyotazamia, huenda akawasha “cheche” chache tu, zenye kiasi kidogo cha mwanga na joto kisha zinafifia upesi. Kwa upande mwingine, wale wanaomtumainia Shilo, yule Mesiya wa Mungu aliyeahidiwa, hawatakata tamaa kamwe.

      [Maelezo ya Chini]

      a Katika mistari mitatu ya kwanza ya Isaya sura ya 50, Yehova anaeleza kwamba taifa la Yuda kwa ujumla ni mke wake, na wakaaji wake mmoja-mmoja ni watoto wake.

      b Kuanzia mstari wa 4 hadi mwisho wa sura hiyo, inaonekana mwandishi anaongea kuhusu yeye mwenyewe. Huenda ikawa Isaya alipatwa na baadhi ya majaribu anayoyataja katika mistari hiyo. Lakini, katika maana kamili, unabii huo unatimizwa kuhusiana na Yesu Kristo.

      c Inafaa kuangalia kwamba, katika Septuagint, Isaya 50:6 inasema hivi: “Niliutoa mgongo wangu upigwe mijeledi, na mashavu yangu yapate mapigo.”

      [Picha katika ukurasa wa 155]

      Wayahudi wanawategemea watawala wa kibinadamu badala ya Yehova

      [Picha katika ukurasa wa 156, 157]

      Kwenye Bahari Nyekundu, Yehova aliwalinda watu wake kwa kuweka nguzo ya wingu kati yao na Wamisri

  • Faraja kwa Watu wa Mungu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Mbili

      Faraja kwa Watu wa Mungu

      Isaya 51:1-23

      1. Ni matazamio gani ya kuhuzunisha yanayongoja Yerusalemu na wakaaji wake, lakini kuna tumaini gani?

      TAIFA la Yuda litatekwa Babiloni miaka 70, muda unaolingana na urefu wa kawaida wa maisha ya mwanadamu. (Zaburi 90:10; Yeremia 25:11; 29:10) Waisraeli wengi sana waliochukuliwa mateka watazeekea Babiloni na kufia huko. Ebu wazia jinsi shutuma kali na dhihaka za adui zao zitakavyowashushia heshima. Vilevile fikiria malawama makubwa yatakayowekwa juu ya Mungu wao, Yehova, wakati jiji hilo ambalo ameliita kwa jina lake litakapokaa ukiwa muda mrefu sana. (Nehemia 1:9; Zaburi 132:13; 137:1-3) Lile hekalu kipenzi, lililojazwa utukufu wa Mungu lilipowekwa wakfu na Solomoni, halitakuwapo tena. (2 Mambo ya Nyakati 7:1-3) Lo, ni matazamio ya kuhuzunisha kama nini! Lakini Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii unaohusu kurudishwa kwa hali za kwanza. (Isaya 43:14; 44:26-28) Tunapata mambo mengine ya unabii unaohusu kichwa hiki chenye kufariji katika sura ya 51 ya kitabu cha Isaya.

      2. (a) Yehova anamtumia Isaya kuelekeza ujumbe wake wa faraja kwa nani? (b) Wayahudi waaminifu ‘wanafuatiaje uadilifu’?

      2 Yehova anawaambia hivi wale walio katika Yuda wanaoelekeza mioyo yao kwake: “Nisikilizeni, ninyi mnaoifuatia haki [“uadilifu,” “NW”]; ninyi mnaomtafuta BWANA.” (Isaya 51:1a) ‘Kufuatia uadilifu’ kunamaanisha kuchukua hatua. Wale ‘wanaofuatia uadilifu’ hawatadai kwa maneno tu kwamba wao ni watu wa Mungu. Watajitahidi sana kuwa waadilifu na kuishi kupatana na mapenzi ya Mungu. (Zaburi 34:15; Mithali 21:21) Watamtegemea Yehova kuwa Chanzo pekee cha uadilifu, na ‘watamtafuta BWANA.’ (Zaburi 11:7; 145:17) Hiyo haimaanishi kuwa wanafanya hivyo kwa sababu hawajamjua Yehova au hawajui jinsi ya kumkaribia katika sala. Inamaanisha kuwa watajitahidi kumkaribia zaidi, kumwabudu, kumpelekea sala, na kutafuta mwelekezo wake katika yote wayafanyayo.

      3, 4. (a) Ni nani “mwamba” ambao Wayahudi walichongwa kutokana nao, na ni nani “tundu la shimo” ambamo walichimbuliwa? (b) Kwa nini Wayahudi watafarijika kwa kuikumbuka asili ya uzawa wao?

      3 Hata hivyo, wenye kufuatia uadilifu kweli kweli ni wachache katika Yuda kwa kulinganishwa na idadi iliyoko, na hiyo huenda ikawatia woga na hali ya kukata tamaa. Kwa hiyo Yehova anatumia kielezi cha machimbo ya mawe kuwatia moyo: “Uangalieni mwamba ule ambao mlitolewa kwa kuchongwa, na tundu la shimo ambalo mlitolewa kwa kuchimbuliwa. Mwangalieni Ibrahimu, baba yenu, na Sara, aliyewazaa [“kwa utungu wa kuzaa,” “NW”]; kwa maana alipokuwa mmoja tu nalimwita, nikambariki, nikamfanya kuwa wengi.” (Isaya 51:1b, 2) “Mwamba” ambao Wayahudi walichongwa kutokana nao ni Abrahamu, mtu maarufu kihistoria ambaye taifa la Israeli hujivunia. (Mathayo 3:9; Yohana 8:33, 39) Yeye ndiye mzazi, yaani mwanadamu aliye chanzo cha taifa hilo. Sara ndiye “tundu la shimo,” alimotoka Isaka babu wa kale wa Israeli.

      4 Abrahamu na Sara walikuwa wamepita umri wa kuzaa na wakawa hawana mtoto. Hata hivyo, Yehova aliahidi kumbariki Abrahamu na ‘kumfanya kuwa wengi.’ (Mwanzo 17:1-6, 15-17) Mungu aliwarudishia Abrahamu na Sara nguvu zao za uzazi wakapata mtoto katika uzee wao, na kutokana na mtoto huyo likazuka lile taifa la agano la Mungu. Kwa njia hiyo, Yehova alimfanya mwanamume huyo mmoja awe baba wa taifa kuu, ambalo liliongezeka likawa na watu wasiohesabika kama nyota za mbinguni. (Mwanzo 15:5; Matendo 7:5) Ikiwa Yehova angeweza kumtoa Abrahamu nchi ya mbali na kumfanya awe taifa hodari, hakika anaweza kutimiza ahadi yake ya kuwaweka huru mabaki walio waaminifu watoke utumwani Babiloni, awarudishe kwenye nchi yao, awafanye wawe taifa kuu tena. Ahadi ya Mungu kwa Abrahamu ilitimizwa; ahadi yake kwa Wayahudi hao watekwa itatimizwa pia.

      5. (a) Abrahamu na Sara wanafananisha nani? Eleza. (b) Katika utimizo wa mwisho, ni nani wanaofuatilia asili yao hadi kuufikia “mwamba”?

      5 Inaelekea kuwa uchimbaji wa mfano unaotajwa katika Isaya 51:1, 2 una matumizi zaidi. Kumbukumbu la Torati 32:18, NW, humwita Yehova “Mwamba” aliyezaa Israeli na “yule Mwenye kumtokeza [Israeli] kwa utungu wa kuzaa.” Katika usemi huo wa mwisho, kitenzi cha Kiebrania kilichotumiwa hapo ni kama kile kinachoonekana kwenye Isaya 51:2 kuhusu Sara akizaa Israeli. Hivyo basi, Abrahamu ni mfano wa unabii wa kumfananisha Yehova, yule Abrahamu Mkubwa Zaidi. Sara, mke wa Abrahamu, anafananisha vema tengenezo la Yehova la kimbingu la ulimwengu mzima wa viumbe-roho, wanaoonyeshwa katika Maandiko Matakatifu kuwa mke, au mwanamke, wa Mungu. (Mwanzo 3:15; Ufunuo 12:1, 5) Katika utimizo wa mwisho wa maneno haya ya unabii wa Isaya, taifa linalozuka kutokana na ule “mwamba” ni “Israeli wa Mungu,” lile kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, lililozaliwa Pentekoste 33 W.K. Kama vile ilivyozungumziwa katika sura zilizotangulia za kitabu hiki, taifa hilo liliingia katika utekwa wa Kibabiloni mwaka wa 1918 lakini likarudishwa kwenye hali ya ufanisi wa kiroho mwaka wa 1919.—Wagalatia 3:26-29; 4:28; 6:16.

      6. (a) Ni nini kinachoingoja nchi ya Yuda, na ni hali gani itakayohitaji kurudishwa? (b) Isaya 51:3 hutukumbusha juu ya hali gani ya kisasa ya kurudishwa?

      6 Yehova anafariji Sayuni, au Yerusalemu, kwa mambo mengine mengi licha ya ile ahadi ya kutokeza taifa lenye watu wengi sana. Tunasoma hivi: “BWANA ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama bustani ya Edeni, na nyika yake kama bustani ya BWANA; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba.” (Isaya 51:3) Wakati wa ile miaka 70 ya ukiwa, nchi ya Yuda itarudi kuwa jangwa lililofunikwa na vichaka vya miiba, mikwamba, na majani-mwitu mengineyo. (Isaya 64:10, NW; Yeremia 4:26; 9:10-12) Kwa hiyo, licha ya kuwapa Yuda makao mapya, ni lazima nchi pia irudishwe kwenye hali yake ya zamani, igeuzwe iwe bustani ya Kiedeni yenye mashamba yaliyo na mazao na maji ya kutosha, pamoja na viunga vyenye matunda mengi. Ardhi itaonekana ni kama inashangilia. Nchi hiyo ikilinganishwa na jinsi ilivyokuwa wakati wa uhamisho, sasa itakuwa ya kiparadiso. Mabaki watiwa-mafuta wa Israeli wa Mungu waliingia katika paradiso ya jinsi hiyo hasa kwa maana ya kiroho katika mwaka wa 1919.—Isaya 11:6-9; 35:1-7.

      Sababu za Kumtumaini Yehova

      7, 8. (a) Yehova ana maana gani anapotoa mwito watu watege sikio kumsikiliza? (b) Kwa nini ni muhimu Yuda wamsikize Yehova?

      7 Yehova anaomba tena watu wake wamsikilize, akisema hivi: “Nisikilizeni mimi, enyi watu wangu; nisikieni, taifa langu; maana sheria itatoka kwangu, nami nitaistarehesha hukumu yangu iwe nuru ya mataifa. Haki yangu i karibu, wokovu wangu umekuwa wazi, na mikono yangu itawahukumu kabila za watu; visiwa vitaningoja, navyo vitautumainia mkono wangu.”—Isaya 51:4, 5.

      8 Yehova anapotoa mwito watu watege sikio kumsikiliza, kinachohitajiwa si kuusikia ujumbe wake tu. Inamaanisha kutega sikio kwa lengo la kuyatenda yale yanayosikiwa. (Zaburi 49:1; 78:1) Ni lazima taifa lifahamu kwamba Yehova ndiye Chanzo cha maagizo, haki, na wokovu. Yeye peke yake ndiye Chanzo cha nuru ya kiroho. (2 Wakorintho 4:6) Yeye ndiye Hakimu anayekata kauli ya mwisho kuhusu wanadamu. Sheria na maamuzi ya hukumu zitokazo kwa Yehova ni nuru kwa wale wanaojiruhusu waongozwe nazo.—Zaburi 43:3; 119:105; Mithali 6:23.

      9. Licha ya watu wa agano la Mungu, ni nani watakaonufaika na vitendo vya Yehova vya kuokoa?

      9 Yote hayo yatawahusu watu wenye mwelekeo ufaao kila mahali, wala si watu wa agano la Mungu peke yao. Yatawahusu hata wale walio katika visiwa vya mbali kabisa baharini. Tumaini lao katika Mungu na uwezo wake wa kuwatetea na kuwaokoa watumishi wake waaminifu halitakatishwa tamaa. Uhodari au uwezo wake unaofananishwa na mkono wake ni hakika; hauwezi kuzimwa na mtu yeyote. (Isaya 40:10; Luka 1:51, 52) Vivyo hivyo leo, kazi ya kuhubiri kwa bidii inayofanywa na washiriki waliobaki wa Israeli wa Mungu imeongoza mamilioni ya watu kumgeukia Yehova na kumwamini, wengi wao wakiwa wa visiwa vya mbali baharini.

      10. (a) Mfalme Nebukadreza atalazimika kujifunza kweli gani? (b) Ni “mbingu” zipi na “dunia” ipi zitakazokomeshwa?

      10 Ndiposa Yehova anarejezea kweli moja ambayo Mfalme Nebukadreza wa Babiloni atalazimika kujifunza. Hakuna chochote mbinguni wala duniani cha kumzuia Yehova asitimize mapenzi yake. (Danieli 4:34, 35) Tunasoma hivi: “Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi [“dunia,” “NW”] chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi [“dunia,” “NW”] itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika [“kama wadudu,” “BHN”]; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na haki yangu haitatanguka.” (Isaya 51:6) Ingawa kuruhusu mateka warudi kwao ni kinyume cha sera ya watawala Wababiloni, tendo la Yehova la kuwaokoa watu wake halitazuiwa. (Isaya 14:16, 17) “Mbingu” za Kibabiloni, au mamlaka zake zinazotawala, zitavunjwa-vunjwa katika ushinde. Nayo “dunia” ya Kibabiloni, ambayo ni raia wa mamlaka hizo zinazotawala, itafikia mwisho hatua kwa hatua. Naam, hata ile mamlaka kubwa zaidi ya siku hizo haiwezi kuupinga uhodari wa Yehova wala kuvizuia vitendo vyake vya wokovu.

      11. Kwa nini kutimizwa kabisa kwa unabii wa kukomeshwa kwa “mbingu” za Kibabiloni na “dunia” yake kunawatia moyo Wakristo leo?

      11 Lo, Wakristo leo wanatiwa moyo kweli kweli kujua kwamba maneno haya ya kiunabii yalitimizwa kabisa! Kwa nini? Kwa sababu mtume Petro alitumia maneno kama hayo kuhusu tukio jingine la wakati ujao. Aliongea juu ya siku ya Yehova inayokaribia kasi, “ambayo kupitia kwayo mbingu zikiwa zimewaka moto zitafumuliwa na elementi zikiwa zimewaka moto sana zitayeyuka!” Halafu akasema hivi: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:12, 13; Isaya 34:4; Ufunuo 6:12-14) Ingawa yale mataifa hodari na watawala wao waliotukuka wakiwa kama nyota huenda wakasimama kwa kumkaidi Yehova, wakati wake ukiwadia, watamalizwa—wapondwe kwa urahisi kama kumponda mdudu. (Zaburi 2:1-9) Serikali adilifu ya Mungu peke yake ndiyo itakayotawala milele juu ya jamii adilifu ya kibinadamu.—Danieli 2:44; Ufunuo 21:1-4.

      12. Kwa nini watumishi wa Mungu hawapaswi kuogopa wanapoharibiwa jina na wapinzani wa kibinadamu?

      12 Sasa Yehova anaongea na watu wale ‘wanaofuatia uadilifu,’ akisema hivi: “Nisikilizeni, ninyi mjuao haki, watu ambao mioyoni mwenu mna sheria yangu; msiogope matukano ya watu, wala msifadhaike kwa sababu ya dhihaka zao. Maana nondo itawala kama vazi, na funza atawala kama sufu; bali haki yangu itakuwa ya milele, na wokovu wangu hata vizazi vyote.” (Isaya 51:7, 8) Wale wanaomtumainia Yehova wataharibiwa jina na kusutwa kwa sababu ya msimamo wao wa ushujaa, lakini hilo si jambo la kuogopwa. Wasutaji ni wanadamu tu wenye kufa, ambao ‘wataliwa,’ sawa na vile vazi la sufu huliwa na nondo.a Kama vile Wayahudi waaminifu wa kale, Wakristo wa kweli leo hawana sababu ya kuwaogopa wapinzani wowote. Yehova, Mungu wa milele, ndiye wokovu wao. (Zaburi 37:1, 2) Suto kutoka kwa adui za Mungu ni ushuhuda wa kwamba watu wa Yehova wana roho yake.—Mathayo 5:11, 12; 10:24-31.

      13, 14. Maneno “Rahabu” na ‘yule joka wa baharini’ yanafananisha nini, naye ‘atakatwa-katwa’ na ‘kuchomwa’ kwa njia gani?

      13 Isaya anasema hivi kana kwamba anamwita Yehova achukue hatua kuwatetea watu Wake walio mateka: “Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; amka kama katika siku zile za kale, katika vizazi vile vya zamani. Si wewe uliyemkata-kata Rahabu? Uliyemchoma yule joka [“wa baharini,” “NW”]? Si wewe uliyeikausha bahari, na maji ya vilindi vikuu; uliyevifanya vilindi kuwa njia, ili wapite watu waliokombolewa?”—Isaya 51:9, 10.

      14 Mifano hiyo ya kihistoria inayotajwa na Isaya imechaguliwa vizuri sana. Kila Mwisraeli anajua taifa hilo lilikombolewa kutoka Misri kisha likavuka Bahari Nyekundu. (Kutoka 12:24-27; 14:26-31) Maneno “Rahabu” na ‘yule joka wa baharini’ yanarejezea Misri ikiwa chini ya Farao wake aliyepinga lile tukio la Kutoka kwa Israeli nchini Misri. (Zaburi 74:13; 87:4; Isaya 30:7) Misri ilifanana na joka kubwa ajabu, kichwa chake kikiwa kwenye Delta ya Mto Naili, na kiwiliwili chake kirefu kikiinuka juu mamia ya kilometa katika bonde la Mto Naili lenye rutuba. (Ezekieli 29:3) Lakini joka hilo kubwa lilikatwa vipande vipande Yehova alipomimina Mapigo Kumi juu yake. Lilidungwa, likajeruhiwa vibaya, likadhoofishwa jeshi lake lilipoangamizwa katika maji mengi ya Bahari Nyekundu. Naam, Yehova alizionyesha nguvu za mkono wake katika shughuli zake na Misri. Sembuse yeye kuwa tayari kuwapigania watu wake waliopelekwa uhamishoni Babiloni!

      15. (a) Hali ya kuhuzunika na kuugua kwa Sayuni itakimbiaje? (b) Kuhuzunika na kuugua kuliwakimbiaje Israeli wa Mungu nyakati za kisasa?

      15 Sasa unabii unaelekeza mbele kwenye ukombozi wa Israeli kutoka Babiloni na kusema hivi: “Nao waliokombolewa na BWANA watarejea, watafika Sayuni, wakiimba; furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; watapata shangwe na furaha; huzuni na kuugua zitakimbia.” (Isaya 51:11) Wale wanaotafuta uadilifu wa Yehova wana matazamio mazuri ajabu, hata kama wana masikitiko makubwa kule Babiloni. Wakati utafika waache kabisa kuhuzunika na kuugua. Midomo ya hao waliokombolewa, au waliofidiwa, itaimba kwa shangwe, furaha na mchachawo. Katika utimizo wa kisasa wa maneno hayo ya kiunabii, Israeli wa Mungu walifunguliwa wakatoka katika utekwa wa Kibabiloni mwaka wa 1919. Walirudishwa kwenye makao yao ya kiroho wakiwa na shangwe kubwa—shangwe ambayo imeendelea hadi leo.

      16. Ni bei gani inayolipwa ili kuwakomboa Wayahudi?

      16 Wayahudi watakombolewa kwa bei gani? Tayari unabii wa Isaya umefunua kwamba Yehova anatoa ‘Misri kuwa ukombozi wake; ametoa Kushi na Seba kwa ajili yake.’ (Isaya 43:1-4) Hilo litatukia baadaye. Baada ya kushinda Babiloni na kuwafungua mateka Wayahudi, Milki ya Uajemi itashinda Misri, Kushi (Ethiopia), na Seba. Nchi hizo zitatolewa kwa kubadilishana na nafsi za Waisraeli. Hiyo inapatana na kanuni inayotajwa kwenye Mithali 21:18: “Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.”

      Uhakikisho Zaidi

      17. Kwa nini Wayahudi hawahitaji kuiogopa hasira kali ya Babiloni?

      17 Kisha Yehova anazidi kuwahakikishia watu wake hivi: “Mimi, naam, mimi, ndimi niwafarijiye; wewe u nani hata ukamwogopa mtu atakayekufa, na mwanadamu atakayefanywa kuwa kama majani? Ukamsahau BWANA, Muumba wako, yeye aliyezitanda mbingu, na kuiweka misingi ya dunia; nawe unaogopa daima mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu yake yeye aoneaye, hapo afanyapo tayari kuharibu; nayo i wapi ghadhabu yake aoneaye [“yule anayekusonga,” “NW”]?” (Isaya 51:12, 13) Miaka mingi ya kukaa uhamishoni inakuja. Hata hivyo, hakuna sababu ya kuiogopa hasira kali ya Babiloni. Ingawa taifa hilo, lililo serikali kubwa ya tatu ya ulimwengu kulingana na maandishi ya Biblia, litawashinda watu wa Mungu na kutaka ‘kuwasonga,’ au kuwazuia wasiponyoke, Wayahudi waaminifu wanajua Yehova ametabiri kwamba Babiloni itaanguka mikononi mwa Koreshi. (Isaya 44:8, 24-28) Kwa kutofautiana na Muumba, yule Mungu wa milele, Yehova—wakaaji wa Babiloni watatoweka kama vile nyasi zinavyonyauka chini ya jua kali la kiangazi. Vitisho vyao na hasira yao kali vitakuwa wapi wakati huo? Hivyo basi, kumwogopa mwanadamu na kumsahau Yehova, aliyezifanya mbingu na dunia, ni ukosefu wa hekima kama nini!

      18. Ingawa watu wa Yehova watakuwa wafungwa kwa muda fulani, yeye anawahakikishia mambo gani?

      18 Ingawa watu wa Yehova watakuwa mateka kwa muda, kana kwamba ‘wameinama chini kwa kufungwa minyororo,’ watafunguliwa ghafula. Hawatafutiliwa mbali huko Babiloni wala kufa njaa wakiwa wafungwa—kuwa wafu katika Sheoli, lile shimo. (Zaburi 30:3; 88:3-5) Yehova anawahakikishia hivi: “Yeye aliyehamishwa na kufungwa [“anayeinama chini kwa kufungwa minyororo,” “NW”] atafunguliwa kwa haraka; wala hatakufa na kushuka shimoni, wala chakula chake hakitapunguka.”—Isaya 51:14.

      19. Kwa nini Wayahudi waaminifu wanaweza kuwa na uhakika kamili na maneno ya Yehova?

      19 Yehova anaendelea kusema hivi, bado akiifariji Sayuni: “Maana mimi ni BWANA, Mungu wako, niichafuaye bahari, mawimbi yake yakavuma. BWANA wa majeshi ndilo jina lake. Nami nimetia maneno yangu kinywani mwako, nami nimekusitiri katika kivuli cha mkono wangu, ili nizipande mbingu, na kuiweka misingi ya dunia, na kuuambia Sayuni, Ninyi ni watu wangu.” (Isaya 51:15, 16) Biblia hutaja mara nyingi kwamba Mungu anaweza kunyosha nguvu zake juu ya bahari na kuidhibiti. (Ayubu 26:12; Zaburi 89:9; Yeremia 31:35) Anadhibiti kabisa nguvu za asili, kama alivyoonyesha alipowakomboa watu wake kutoka Misri. Ni nani anayeweza kulinganishwa na ‘Yehova wa majeshi,’ hata kwa njia ndogo sana?—Zaburi 24:10.

      20. Yehova anaporudisha Sayuni katika hali ya kwanza, ni “mbingu” zipi na “dunia” ipi zitakazotokea, naye atatamka maneno gani yenye kufariji?

      20 Bado Wayahudi ni watu wa agano la Mungu, na Yehova anawahakikishia kwamba watairudia nchi yao, ili wakaishi tena chini ya Sheria. Wakiwa huko, watajenga upya Yerusalemu na hekalu lake, warudie madaraka yao wakiwa chini ya agano aliloagana nao kupitia Musa. Nchi ianzapo kukaliwa upya na Waisraeli waliorudishwa pamoja na mifugo yao, “dunia mpya” itatokea. “Mbingu mpya,” ambazo ni mfumo mpya wa kiserikali, zitawekwa juu ya hiyo “dunia mpya.” (Isaya 65:17-19, NW; Hagai 1:1, 14) Yehova ataiambia tena Sayuni: “Ninyi ni watu wangu.”

      Mwito wa Kuchukua Hatua

      21. Yehova anatoa mwito gani wa kuchukua hatua?

      21 Baada ya kuipa Sayuni uhakikisho zaidi, Yehova anatoa mwito wa kuchukua hatua. Akiongea kana kwamba Sayuni imekwisha fikia kikomo cha mateso yake, anasema hivi: “Amka, amka, simama, Ee Yerusalemu, wewe uliyenywea, mkononi mwa BWANA, kikombe cha hasira yake; bakuli la kikombe cha kulevya-levya umelinywea na kulimaliza.” (Isaya 51:17) Naam, lazima Yerusalemu ainuke kutoka kwenye misiba yake, arudie cheo na fahari yake ya zamani. Utafika wakati atakapokuwa amekunywa kinywaji chote fyu katika kikombe cha mfano, chenye malipizo ya kimungu. Hapo ndipo hasira ya Mungu itakapokamilika kumwelekea.

      22, 23. Yerusalemu atapatwa na nini atakapokunywa kikombe cha hasira ya Yehova?

      22 Hata hivyo, Yerusalemu anapoadhibiwa hakuna yeyote wa wakaaji wake, “wana” wake, atakayeweza kuzuia adhabu hiyo. (Isaya 43:5-7; Yeremia 3:14) Unabii unasema hivi: “Hapana hata mmoja wa kumwongoza miongoni mwa wana wote aliowazaa, wala hapana hata mmoja wa kumshika mkono miongoni mwa wana wote aliowalea.” (Isaya 51:18) Atateswa na Wababiloni weee! “Mambo haya mawili yamekupata; ni nani awezaye kukusikitikia? Ukiwa na uharibifu, na njaa na upanga; niwezeje kukutuliza? Wana wako wamezimia, wamelala penye pembe za njia kuu zote kama kulungu [“kondoo-mwitu,” “NW”] wavuni; wamejaa hasira ya BWANA, lawama ya Mungu wako.”—Isaya 51:19, 20.

      23 Maskini Yerusalemu! Atalazimika kuvumilia “ukiwa na uharibifu,” na vilevile “njaa na upanga.” “Wana” wake watasimama wakiwa hoi kwa kushindwa kumwongoza na kumshikilia asianguke, wakiwa wamekonda sana, na kuwa wanyonge kiasi cha kutokuweza kuwakinza wavamizi Wababiloni. Watalala peupe kwenye makutano au pembe ya barabara, wakiwa wamezimia, wamedhoofika, na kuishiwa na nguvu. (Maombolezo 2:19; 4:1, 2) Watakuwa wamekunywa kikombe cha hasira kali ya Mungu, wawe hoi kama wanyama walionaswa wavuni.

      24, 25. (a) Yerusalemu hatatendewa nini tena? (b) Ni nani atakayemfuata Yerusalemu kunywa kikombe cha hasira ya Yehova?

      24 Lakini sikitisho hilo litakoma. Isaya anatoa faraja akisema hivi: “Basi, kwa sababu ya hayo, ulisikilize neno hili, ewe uliyeteswa, na kulewa, lakini si kwa mvinyo; BWANA, Bwana wako na Mungu wako, awateteaye watu wake, asema hivi, Tazama, nimeondoa mkononi mwako kikombe cha kulevya-levya, hilo bakuli la kikombe cha hasira yangu; hutakinywea tena; nami nitakitia mikononi mwao wakutesao; waliokuambia nafsi yako, Inama, tupate kupita; nawe uliufanya mgongo wako kuwa kama nchi, na kama njia, kwa hao wapitao juu yake.” (Isaya 51:21-23) Baada ya kumtia Yerusalemu nidhamu, Yehova yu tayari kumwonyesha rehema na roho ya kusamehe.

      25 Sasa Yehova atageuza hasira yake mbali na Yerusalemu amwelekezee Babiloni. Babiloni atakuwa amekwisha kubomoa Yerusalemu kabisa na kumwaibisha. (Zaburi 137:7-9) Lakini Yerusalemu hatalazimika kunywa kutokana na kikombe hicho tena mikononi mwa Babiloni wala mwa washirika wake. Bali, Yerusalemu atapokonywa kikombe hicho wapewe wale walioishangilia aibu yake. (Maombolezo 4:21, 22) Babiloni atadondoka chini, yu mlevi wa kupindukia. (Yeremia 51:6-8) Huku Babiloni yuadondoka chini, na huku Sayuni yuainuka! Lo, badiliko la ajabu kama nini! Kweli Sayuni anaweza kufarijiwa na tazamio hilo. Na watumishi wa Yehova wanaweza kuwa na uhakikisho wa kwamba jina lake litatakaswa kupitia matendo yake ya kuokoa.

      [Maelezo ya Chini]

      a Kulingana na ushuhuda, nondo anayetajwa hapa ni yule nondo mtengeneza-utando katika nguo, akiwa hasa katika ile hatua ya kuwa buu lenye uharibifu.

      [Picha katika ukurasa wa 167]

      Yehova, yule Abrahamu Mkubwa Zaidi, ndiye “mwamba” ambao watu wake ‘walichongwa’ kutokana nao

      [Picha katika ukurasa wa 170]

      Wapinzani wa watu wa Mungu watatoweka, kama vazi lililoliwa na nondo

      [Picha katika ukurasa wa 176, 177]

      Yehova ameonyesha kuwa ana uwezo wa kudhibiti nguvu za asili

      [Picha katika ukurasa wa 178]

      Babiloni na washirika wake watapokezwa kikombe ambacho Yerusalemu atakuwa amekinywa

  • ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Tatu

      ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!

      Isaya 52:1-12

      1. Kwa nini unabii wa Isaya sura ya 52 ni chanzo cha shangwe, na una matimizo gani mawili?

      UKOMBOZI! Hakuna kitu kinachowapa mateka shangwe kubwa kuliko tazamio lao la kukombolewa! Kwa kuwa kichwa kikuu katika kitabu cha Isaya ni ukombozi na urudisho, si ajabu kwamba licha ya Zaburi, kitabu hiki cha Biblia ndicho chenye semi nyingi zaidi za shangwe kuliko kitabu kingine chochote. Isaya sura ya 52 hasa huwapa watu wa Mungu sababu ya kushangilia. Unabii wake unatimizwa juu ya Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. Na una utimizo mkubwa zaidi unaohusisha “Yerusalemu la juu,” tengenezo la Yehova la kimbingu la viumbe-roho, ambalo nyakati nyingine hufafanuliwa kuwa mama na mke.—Wagalatia 4:26; Ufunuo 12:1.

      “Jivike Nguvu Zako, Ee Sayuni”!

      2. Sayuni anaamka lini, na hilo linatukiaje?

      2 Yehova anamtumia Isaya kupaza sauti akitoa mwito ufuatao kwa Sayuni, jiji Lake kipenzi: “Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, mji mtakatifu; kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako asiyetahiriwa, wala aliye najisi. Jikung’ute mavumbi; uondoke, uketi, Ee Yerusalemu; jifungulie vifungo vya shingo yako, Ee binti Sayuni uliyefungwa.” (Isaya 52:1, 2) Yerusalemu amelala ukiwa muda wa miaka 70 kwa sababu wakaaji wake wameichochea hasira ya Yehova. (2 Wafalme 24:4; 2 Mambo ya Nyakati 36:15-21; Yeremia 25:8-11; Danieli 9:2) Sasa wakati umefika aamke kutoka kwenye kipindi chake kirefu cha kutokutenda, ajivike mavazi mazuri ya ukombozi. Yehova ameugusa moyo wa Koreshi kumweka huru ‘binti Sayuni aliyefungwa’ ili wakaaji wa zamani wa Yerusalemu na wazao wao waweze kuondoka Babiloni, warudi Yerusalemu, warudishe ibada ya kweli. Watu wowote wasiotahiriwa na walio najisi hawapaswi kamwe kuwako Yerusalemu.—Ezra 1:1-4.

      3. Kwa nini kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kuitwa “binti Sayuni,” nao wanakombolewa katika maana gani?

      3 Maneno hayo ya Isaya yana utimizo unaohusu kutaniko la Kikristo pia. Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kufafanuliwa kuwa “binti Sayuni” wa kisasa, kwa kuwa “Yerusalemu la juu” ndiye mama yao.a Kwa kuwa watiwa-mafuta wamewekwa huru kutokana na mafundisho ya kipagani na ya uasi-imani, ni lazima wadumishe msimamo safi mbele za Yehova, si kwa kutahiriwa mwili, hapana, bali kwa kutahiriwa katika mioyo yao. (Yeremia 31:33; Waroma 2:25-29) Hiyo inahusisha kudumisha usafi wa kiroho, wa kiakili, na wa kiadili mbele za Yehova.—1 Wakorintho 7:19; Waefeso 2:3.

      4. Ingawa “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova, ni mambo gani yaliyowapata wawakilishi wake duniani yanayofanana na yale ya wakaaji wa kale wa Yerusalemu?

      4 Ni kweli kwamba “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova. Hata hivyo, wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, wawakilishi wake duniani—Wakristo watiwa-mafuta—walivunja sheria ya Yehova bila kujua kwa sababu hawakuuelewa vizuri msimamo wa kweli wa kutokuwamo kwa Kikristo. Walipoteza upendeleo wa kimungu, wakaingia katika utekwa wa kiroho wa “Babiloni Mkubwa,” ile milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo. (Ufunuo 17:5) Upeo wa utumwa wao ulifika Juni 1918 wakati washirika wanane kati ya wafanyakazi wa Watch Tower Society walipofungwa gerezani kwa mashtaka ya uwongo, mojawapo likiwa ni kufanya uhaini. Hapo basi kazi ya kuhubiri habari njema kwa mpangilio mzuri ikawa ni kama imekoma. Lakini, mwaka wa 1919 mbiu ikapigwa kuwaita waamke kiroho. Wakristo watiwa-mafuta walianza kujitenga kwa ukamili zaidi na uchafu wa kiadili na wa kiroho wa Babiloni Mkubwa. Waliinuka kutoka kwenye mavumbi ya utekwa, nalo “Yerusalemu la juu” likapata fahari ya kuwa “mji mtakatifu” ambapo uchafu wa kiroho hauruhusiwi.

      5. Kwa nini Yehova ana haki kamili ya kuwakomboa watu wake bila kuwapa watekaji wao malipo?

      5 Mwaka wa 537 K.W.K. na pia mwaka wa 1919 W.K., Yehova alikuwa na haki kamili ya kuwakomboa watu wake. Isaya anaeleza hivi: “BWANA asema hivi, Mliuzwa bure; nanyi mtakombolewa bila fedha.” (Isaya 52:3) Babiloni wa kale wala Babiloni Mkubwa hakulipa chochote alipowatwaa watu wa agano la Mungu ili kuwamiliki wakiwa watumwa wao. Kwa kuwa mapatano ya kifedha hayakufanywa, bado Yehova ndiye aliyekuwa Mmiliki halali wa watu wake. Je, Yehova angalipaswa kuhisi kuwa ana deni la mtu yeyote? Hata kidogo. Katika visa vyote viwili, Yehova angeweza kuwa na haki ya kuwakomboa waabudu wake bila kuwapa watekaji wao malipo yoyote.—Isaya 45:13.

      6. Adui za Yehova hawakutii masomo gani ya kihistoria?

      6 Adui za Yehova hawakuwa wamejifunza masomo yoyote kutokana na historia. Tunasoma hivi: “Bwana MUNGU asema hivi, Watu wangu hapo kwanza walishuka Misri ili wakae huko hali ya ugeni; na Mwashuri akawaonea bila sababu.” (Isaya 52:4) Ingawahapo kwanza Waisraeli walikuwa wamealikwa kukaa Misri wakiwa wageni, Farao wa nchi hiyo aliwaweka utumwani. Lakini Yehova alimzamisha Farao na jeshi lake katika Bahari Nyekundu. (Kutoka 1:11-14; 14:27, 28) Naye Mfalme Senakeribu wa Ashuru alipotisha Yerusalemu, malaika wa Yehova aliua askari 185,000 wa mfalme huyo. (Isaya 37:33-37) Hivyo hivyo, wala Babiloni wa kale wala Babiloni Mkubwa hawezi kuyahepa matokeo ya kuwakandamiza watu wa Mungu.

      “Watu Wangu Watalijua Jina Langu”

      7. Utekwa wa watu wa Yehova umekuwa na matokeo gani juu ya jina lake?

      7 Utekwa wa watu wa Yehova unaathiri jina lake, kama vile unabii unavyoonyesha: “Basi sasa, nafanya nini hapa [“ninapata faida gani hapa,” “NW”], asema BWANA, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema BWANA, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa. Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu kwa hiyo watajua siku ile ya kuwa mimi ndimi ninenaye; tazama ni mimi.” (Isaya 52:5, 6) Yehova anapata faida gani katika hali hiyo? Mbona ahangaike kwamba Israeli wamewekwa utumwani Babiloni? Ni lazima Yehova achukue hatua kwa sababu Babiloni amewateka watu wake na kuwapigia yowe la shangwe ya ushindi. Kujigamba huko kumefanya Babiloni alidharau jina la Yehova. (Ezekieli 36:20, 21) Babiloni ameshindwa kutambua kwamba Yerusalemu limekuwa ukiwa kwa sababu Yehova amechukizwa na watu wake. Badala yake, Babiloni ameuona utumwa wa Wayahudi kuwa ni ushahidi wa kuonyesha kwamba Mungu wao ni dhaifu. Belshaza, mtawala-msaidizi wa Babiloni, hata anamdhihaki Yehova kwa kutumia vyombo kutoka kwenye hekalu Lake wakati wa karamu ya kuheshimu miungu ya Babiloni.—Danieli 5:1-4.

      8. Jina la Yehova limetendewaje tangu mitume walipokufa?

      8 Hayo yote yanahusuje “Yerusalemu la juu”? Tangu uasi-imani utie mizizi miongoni mwa wale wanaojiita Wakristo, ingeweza kusemwa kwamba “jina la Mungu linafanyiwa kufuru miongoni mwa mataifa kwa sababu ya [hao] watu.” (Waroma 2:24; Matendo 20:29, 30) Hivyo basi, hatimaye Wayahudi walianza kuepuka kutumia jina la Mungu kwa hofu ya kishirikina. Upesi baada ya kifo cha mitume, Wakristo waasi-imani walifuata mkondo huo huo wakaacha kulitumia jina la kibinafsi la Mungu. Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni sehemu kubwa ya Babiloni Mkubwa, ilisitawi kutokana na uasi-imani huo. (2 Wathesalonike 2:3, 7; Ufunuo 17:5) Jina la Yehova limepata sifa mbaya kwa sababu ya ukosefu wa adili ulioenea sana katika Jumuiya ya Wakristo na hatia yake ya kumwaga damu kwa macho makavu.—2 Petro 2:1, 2.

      9, 10. Watu wa agano la Mungu wa nyakati za kisasa wamepata uelewevu gani wa kina kirefu zaidi kuhusu viwango vya Yehova na jina lake?

      9 Koreshi Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, alipowaweka huru watu wa agano la Mungu kutoka utekwa wa Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919, waliyaelewa matakwa ya Yehova vizuri zaidi. Tayari walikuwa wamejisafisha kwa kuondoa mafundisho mengi ya Jumuiya ya Wakristo yaliyo na mizizi katika upagani wa nyakati zilizoutangulia Ukristo, kama vile Utatu, kutokufa kwa nafsi, na mateso ya milele katika helo yenye moto. Sasa walianza kujiondolea kabisa dalili zote za mavutano ya Kibabiloni. Pia wakaja kuutambua umuhimu wa kudumisha msimamo wa kutokuwamo kabisa katika mambo ya uzalendo wa ulimwengu huu. Hata walitaka kujitakasa kwa kuondoa hatia yoyote ya damu ambayo huenda ikawa baadhi yao walijiletea.

      10 Pia watumishi wa kisasa wa Mungu walipata uelewevu wa kina kirefu zaidi juu ya umuhimu wa jina la Yehova. Mwaka wa 1931 walikubali kulitwaa jina Mashahidi wa Yehova, na hivyo wakatangaza peupe kwamba wanaunga mkono Yehova na jina lake. Zaidi ya hilo, kwa kuchapisha Biblia ya New World Translation tangu mwaka wa 1950, Mashahidi wa Yehova wamelirudisha jina la Mungu mahali pake katika Biblia. Naam, wao wamekuja kuthamini jina la Yehova na wanalijulisha mpaka miisho ya dunia.

      “Aletaye Habari Njema”

      11. Kwa nini inafaa kwamba sauti inapaazwa kusema “Mungu wako anamiliki!” kuhusiana na matukio ya mwaka wa 537 K.W.K.?

      11 Sasa uangalifu wetu unageuzwa kumwelekea tena Sayuni akiwa bado katika ukiwa wake. Mjumbe anakaribia akiwa na habari njema: “Jinsi ilivyo mizuri [“yenye kupendeza,” “NW”] juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!” (Isaya 52:7) Mwaka wa 537 K.W.K., inawezaje kusemwa eti Mungu wa Sayuni amemiliki? Je, kwani Yehova hakuwa Mfalme nyakati zote? Kweli kabisa, yeye ndiye “Mfalme wa umilele”! (Ufunuo 15:3) Lakini kupaaza sauti kwamba “Mungu wako anamiliki!” kunafaa kwa kuwa utawala wa ufalme wa Yehova unaonekana wazi kwa njia mpya baada ya anguko la Babiloni na mbiu ya kifalme kupigwa ikisema hekalu likajengwe upya Yerusalemu, na kwamba ibada safi irudishwe huko.—Zaburi 97:1.

      12. Ni nani aliyeongoza katika ‘kuleta habari njema,’ na jinsi gani?

      12 Siku za Isaya, hakuna mtu mmoja au kikundi cha watu kilichotambulishwa kuwa ndicho mtu huyo “aletaye habari njema.” Ingawa hivyo, leo mletaji huyo wa habari njema anajulikana. Yesu Kristo ndiye mjumbe mkubwa zaidi wa amani wa Yehova. Alipokuwa duniani, alizihubiri habari njema kwamba watu wangefunguliwa kabisa wasiwe na madhara ya dhambi iliyorithiwa kutoka kwa Adamu, baadhi yake yakiwa ni magonjwa na kifo. (Mathayo 9:35) Yesu aliweka mfano kwa kutia bidii kuzitangaza habari njema hizo za kitu kizuri zaidi, akatumia kila nafasi aliyopata kuwafundisha watu Ufalme wa Mungu. (Mathayo 5:1, 2; Marko 6:34; Luka 19:1-10; Yohana 4:5-26) Nao wanafunzi wake waliufuata mfano wake.

      13. (a) Mtume Paulo anaelezaje kwa upana maana ya usemi ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza juu ya milima miguu yake aletaye habari njema’? (b) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba miguu ya wajumbe hao ni “yenye kupendeza”?

      13 Katika barua yake kwa Waroma, mtume Paulo ananukuu Isaya 52:7 kukazia umuhimu wa kazi ya kuzihubiri habari njema. Anatokeza mfululizo wa maswali yanayoamsha fikira, mojawapo likiwa ni ‘Watu watasikiaje bila mtu fulani kuhubiri?’ Halafu anasema hivi: “Kama vile imeandikwa: ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale watangazao habari njema ya mambo mema!’” (Waroma 10:14, 15) Hivyo Paulo anapanua matumizi ya Isaya 52:7, akitumia neno “wale” kwa wingi, badala ya neno “yule” kwa umoja, linalopatikana katika maandishi-awali ya Isaya. Wakristo wote ni wajumbe wa habari njema za amani kwa kumwiga Yesu Kristo. Miguu yao ‘inapendeza’ jinsi gani? Isaya anaongea kana kwamba mpiga-mbiu anakaribia Yerusalemu kutoka kwenye milima ya Yuda iliyo karibu. Haiwezekani kuiona miguu ya mjumbe huyo kwa mbali. Hivyo basi, uangalifu hapa unaelekezwa kwenye mjumbe mwenyewe, kwani ile miguu inawakilisha mjumbe mwenyewe. Sawa na vile Yesu na wanafunzi wake walivyokuwa na sura maridadi kwa watu wasikivu karne ya kwanza, Mashahidi wa kisasa ni wenye kupendeza machoni pa watu wanyenyekevu wanaousikiza ujumbe wa habari njema unaookoa uhai.

      14. Yehova amekuwaje Mfalme nyakati za kisasa, na ni tangu lini wanadamu wametangaziwa jambo hilo?

      14 Ni tangu lini katika nyakati za kisasa sauti imesikika ikipaazwa kusema “Mungu wako anamiliki!”? Ni tangu mwaka wa 1919. Mwaka huo, kwenye mkusanyiko fulani Cedar Point, Ohio, J. F. Rutherford, msimamizi wa Watch Tower Society wakati huo, aliwachochea wasikilizaji wake kwa hotuba yenye kichwa “Hotuba kwa Wafanyakazi Wenzi.” Hotuba hiyo, ambayo msingi wake ulikuwa Isaya 52:7 na Ufunuo 15:2, iliwatia moyo wahudhuriaji wote waanze kazi ya kuhubiri. Hivyo, ‘miguu yenye kupendeza’ ilianza kuonekana ‘milimani.’ Kwanza Wakristo watiwa-mafuta, na baadaye waandamani wao wa “kondoo wengine,” walijitokeza kwenda kuzihubiri habari njema kwamba Yehova amekuwa Mfalme. (Yohana 10:16) Yehova akawa Mfalme jinsi gani? Alionyesha kwamba amekuwa mfalme kwa njia mpya mwaka wa 1914 alipomtawaza Mwanawe, Yesu Kristo, awe Mfalme katika Ufalme wa kimbingu uliokuwa umeanzishwa karibuni. Kisha Yehova akafanya wonyesho mwingine wa utawala wake wa kifalme mwaka wa 1919 alipokomboa “Israeli wa Mungu” kutoka Babiloni Mkubwa.—Wagalatia 6:16; Zaburi 47:8; Ufunuo 11:15, 17; 19:6.

      ‘Walinzi Wako Wanapaza Sauti Zao’

      15. “Walinzi” wanaopaza sauti yao mwaka wa 537 K.W.K. ni akina nani?

      15 Je, kule kupaza sauti kwamba “Mungu wako anamiliki!” kunatokeza itikio fulani? Ndiyo. Isaya anaandika hivi: “Sauti ya walinzi wako! Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja; maana wataona jicho kwa jicho, jinsi BWANA arejeavyo Sayuni.” (Isaya 52:8) Hakuna walinzi halisi wanaoenda kushika zamu kule Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. ili kuwakaribisha wahamishwa wa kwanza wanaorudi. Jiji limelala ukiwa miaka 70. (Yeremia 25:11, 12) Kwa hiyo, “walinzi” wanaopaza sauti yao bila shaka ni Waisraeli wale wanaozipata mapema habari za kurudishwa kwa Sayuni, ambao wanakuwa na daraka la kueneza habari hizo kwa watoto wale wengine wa Sayuni. Walinzi hao wanapomwona Yehova akiitia Babiloni mikononi mwa Koreshi mwaka wa 539 K.W.K., hawana shaka katika akili zao kwamba Yehova anawakomboa watu wake. Walinzi hao wanaendelea kupaaza sauti zao kwa shangwe pamoja na wale wanaoitikia mwito wao, ili wengine wazisikie habari njema.

      16. “Walinzi” wanaonana na nani “jicho kwa jicho,” na katika maana gani?

      16 Walinzi hao walio chonjo wanaimarisha uhusiano wa karibu na wa kibinafsi pamoja na Yehova, kana kwamba wanamwona “jicho kwa jicho,” au uso kwa uso. (Hesabu 14:14) Ukaribiano wao pamoja na Yehova na pamoja na mtu na mwenzake unakazia kwamba wana umoja na kwamba ujumbe wao ni wa shangwe.—1 Wakorintho 1:10.

      17, 18. (a) Jamii ya kisasa ya mlinzi imepazaje sauti yake? (b) Ni katika maana gani jamii ya mlinzi imetoa mwito kwa kupaaza sauti pamoja?

      17 Katika utimizo wa kisasa, jamii ya mlinzi, yaani yule “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” inapaza sauti yake, si kuwaelekea wale tu ambao tayari wamo katika tengenezo la Mungu linaloonekana, bali pia kuwaelekea watu wa nje. (Mathayo 24:45-47) Mwaka wa 1919 mwito ulitokezwa kuwakusanya watiwa-mafuta waliobakia, kisha mwito huo ukakaziwa mwaka wa 1922 kwenye mkusanyiko wa Cedar Point, Ohio, kwa ombi lililosema “tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Tangu mwaka wa 1935, fikira zimeelekezwa hasa kwenye kazi ya kukusanya umati mkubwa wa watu walio kama kondoo. (Ufunuo 7:9, 10) Miaka ya hivi majuzi tangazo linalohusu utawala wa ufalme wa Yehova limetiliwa nguvu zaidi. Jinsi gani? Mwaka wa 2000, watu wapatao milioni sita walikuwa wakishiriki kutangaza utawala wa Ufalme wa Yehova katika nchi na maeneo zaidi ya 230. Isitoshe, Mnara wa Mlinzi, chombo kikuu kinachotumiwa na jamii ya mlinzi, kinapaaza sauti ya ujumbe huo wenye shangwe katika lugha zaidi ya 130.

      18 Unyenyekevu na upendo wa kidugu unahitajiwa ili kushiriki katika kazi hiyo ya kuleta umoja. Ili mwito uwe na matokeo mazuri, ni lazima wahusika wote wauhubiri ujumbe ule ule mmoja, wakikazia jina la Yehova, uandalizi wake wa fidia, hekima yake, upendo wake, na Ufalme wake. Wakristo wote ulimwenguni kote wanapofanya kazi bega kwa bega, kifungo cha uhusiano wao binafsi na Yehova kinaimarishwa ili kuvumisha pamoja habari za mteremo.

      19. (a) “Mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa” panakuwaje na kelele za furaha? (b) Yehova ‘ameuweka wazi mkono wake mtakatifu’ katika maana gani?

      19 Huku watu wa Mungu wakiwa wanapaaza sauti kwa shangwe, hata makao yao yenyewe yanaonekana yakipiga kelele kwa furaha. Unabii unaendelea kusema hivi: “Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja [“kwa shangwe,” “NW”], enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalemu. BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu machoni pa mataifa yote; na ncha zote za dunia zitauona wokovu wa Mungu wetu.” (Isaya 52:9, 10) Wale wanaorudi kutoka Babiloni wanapofika, sehemu za ukiwa wa Yerusalemu zenye sura ya maombolezo zinaonekana kama zinapiga kelele kwa furaha kwa sababu sasa ibada safi ya Yehova inaweza kurudishwa. (Isaya 35:1, 2) Ni wazi kuwa mkono wa Yehova unahusika katika jambo hili. “Ameweka wazi mkono wake mtakatifu,” kana kwamba anakunja mikono ya shati lake kuwaokoa watu wake.—Ezra 1:2, 3.

      20. Kumekuwako na bado kutakuwako matokeo gani kwa sababu Yehova ameuweka mkono wake ukiwa wazi nyakati za kisasa?

      20 Katika hizi “siku za mwisho,” Yehova ameuweka wazi mkono wake mtakatifu ili kuwahuisha mabaki watiwa-mafuta, wale ‘mashahidi wawili’ wa kitabu cha Ufunuo. (2 Timotheo 3:1; Ufunuo 11:3, 7-13) Tangu mwaka wa 1919, wameingizwa katika paradiso ya kiroho, makao ya kiroho wanayoyashiriki sasa pamoja na mamilioni ya washirika wao, wale kondoo wengine. Mwishowe, Yehova atauweka wazi mkono wake mtakatifu awaletee watu wake wokovu kwenye “Har-Magedoni.” (Ufunuo 16:14, 16) Hapo ndipo “ncha zote za dunia zitauona wokovu wa Mungu wetu.”

      Takwa la Haraka

      21. (a) Wale ‘wanaochukua vyombo vya Yehova’ wanatakiwa wafanye nini? (b) Kwa nini Wayahudi wanaoondoka Babiloni hawana sababu ya kubabaika kwa hofu?

      21 Wale wanaotoka Babiloni kurudi Yerusalemu wana takwa fulani la kutimiza. Isaya anaandika hivi: “Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA. Maana hamtatoka kwa haraka [“kubabaika kwa hofu,” “NW”], wala hamtakwenda kwa kukimbia, kwa sababu BWANA atawatangulia; na Mungu wa Israeli atawafuata nyuma; awalinde.” (Isaya 52:11, 12) Ni lazima Waisraeli wanaoondoka waache huko Babiloni kitu chochote kilicho na doa la ibada ya uwongo ya Babiloni. Kwa kuwa wanachukua vyombo vya Yehova vilivyotoka hekaluni Yerusalemu, ni lazima wawe safi moyoni hasa, wala si kwa nje tu, kwa kufuata desturi fulani rasmi. (2 Wafalme 24:11-13; Ezra 1:7) Isitoshe, Yehova anawatangulia, kwa hiyo si lazima wababaike kwa hofu, wala si lazima wapige mbio kwa bumbuazi, kana kwamba watu wenye hamu ya kumwaga damu wanatifua vumbi wakiwafuata hima-hima. Mungu wa Israeli yuko kama mlinzi nyuma yao.—Ezra 8:21-23.

      22. Paulo anakaziaje uhitaji wa usafi miongoni mwa Wakristo watiwa-mafuta?

      22 Maneno ya Isaya kuhusu kuendelea kuwa safi yanatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya wazao wa “Yerusalemu la juu.” Paulo alipowaonya kwa upole Wakristo Wakorintho wasifungwe nira pamoja na wasio waamini kwa njia isiyosawazika, aliyanukuu maneno ya Isaya 52:11: “‘Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, na jitengeni wenyewe,’ asema Yehova, ‘na komeni kugusa kitu kisicho safi.’” (2 Wakorintho 6:14-17) Sawa na vile ilivyokuwa kwa Waisraeli wakielekea nyumbani kutoka Babiloni, ni lazima Wakristo waepuke kabisa ibada ya uwongo ya Kibabiloni.

      23. Watumishi wa Yehova leo hujitahidi kujidumisha wakiwa safi kwa njia zipi?

      23 Ndivyo hasa ilivyokuwa kwa habari ya wale wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu Kristo waliokimbia kutoka Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919. Walijisafisha hatua kwa hatua wakajiondolea dalili zote zilizobaki za ibada ya uwongo. (Isaya 8:19, 20; Waroma 15:4) Pia walipata ufahamu zaidi kuhusu umuhimu wa usafi wa kiadili. Ingawa nyakati zote Mashahidi wa Yehova wametetea viwango vya juu vya kiadili, mwaka wa 1952 gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa na makala zilizokazia uhitaji wa kuwatia nidhamu wakosefu wa adili ili kudumisha usafi wa kutaniko. Hatua hiyo ya nidhamu humsaidia mkosaji mwenyewe atambue uhitaji wa kutubu kwa moyo mweupe.—1 Wakorintho 5:6, 7, 9-13; 2 Wakorintho 7:8-10; 2 Yohana 10, 11.

      24. (a) ‘Vyombo vya Yehova’ ni nini nyakati za kisasa? (b) Kwa nini Wakristo leo wana uhakika kwamba Yehova ataendelea kutangulia mbele yao na pia awe mlinzi nyuma yao?

      24 Wakristo watiwa-mafuta pamoja na ule umati mkubwa wa kondoo wengine wamepiga moyo konde kutogusa kitu chochote chenye uchafu wa kiroho. Hali yao iliyotiwa utakato na usafi huwastahilisha wawe wachukuaji wa ‘vyombo vya Yehova.’ Vyombo hivyo ni yale maandalizi ya thamani kubwa ambayo Mungu hufanya ili yatumiwe katika utumishi mtakatifu wa huduma ya nyumba kwa nyumba na ya funzo la Biblia na namna nyingine za utendaji wa Kikristo. Kwa kudumisha msimamo safi, watu wa Mungu leo wanaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova ataendelea kutangulia mbele yao na vilevile awe mlinzi nyuma yao. Kwa kuwa wao ni watu safi wa Mungu, wana sababu tele za ‘kuimba pamoja kwa shangwe’!

      [Maelezo ya Chini]

      a Ona Sura ya 15 ya kitabu hiki ili upate mazungumzo marefu zaidi juu ya uhusiano uliopo kati ya “Yerusalemu la juu” na watoto wake wa kidunia, walio watiwa-mafuta.

      [Picha katika ukurasa wa 183]

      Sayuni atawekwa huru kutoka utekwani

      [Picha katika ukurasa wa 186]

      Kuanzia mwaka wa 1919, ‘miguu yenye kupendeza’ imeonekana tena ‘milimani’

      [Picha katika ukurasa wa 189]

      Mashahidi wa Yehova huongea kwa sauti ya umoja

      [Picha katika ukurasa wa 192]

      Wale ‘wanaovichukua vyombo vya Yehova’ ni lazima wawe safi kiadili na kiroho

  • Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa Kimesiya
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Nne

      Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa Kimesiya

      Isaya 52:13–53:12

      1, 2. (a) Toa mfano wa hali iliyokabiliwa na Wayahudi wengi mapema katika karne ya kwanza W.K. (b) Yehova alikuwa amefanya uandalizi gani wa kuwasaidia Wayahudi waaminifu wamtambue Mesiya?

      WAZIA kwamba utakutana na mheshimiwa fulani. Wakati na mahali pamekwisha pangwa. Lakini kuna tatizo: Hujui sura yake, na atasafiri kwa utulivu, bila vigelegele vya kujionyesha. Utamtambuaje? Ingefaa uwe na maelezo kamili kumhusu.

      2 Mapema katika karne ya kwanza W.K., Wayahudi wengi walikabili hali kama hiyo. Walikuwa wakimtazamia Mesiya—mwanamume ambaye angekuwa mashuhuri kupita wote waliopata kuishi. (Danieli 9:24-27; Luka 3:15) Lakini Wayahudi waaminifu wangepaswa kumtambuaje? Yehova alikuwa amewatumia manabii Waebrania kuandika maelezo kamili ya matukio yaliyohusiana na Mesiya ili watu wenye ufahamu waweze kumtambua bila kukosea.

      3. Ni maelezo gani kuhusu Mesiya yameandaliwa kwenye Isaya 52:13–53:12?

      3 Labda ule unabii ulioandikwa kwenye Isaya 52:13–53:12 ndio unaoeleza wazi zaidi juu ya Mesiya kuliko unabii mwingine wote wa Kiebrania ulioandikwa kumhusu. Zaidi ya miaka 700 mapema, Isaya alifafanua, si sura ya kimwili ya Mesiya, bali mambo yale yaliyokuwa ya maana zaidi. Yaani, alifafanua kusudi la mateso yake na jinsi ambavyo yangempata, na pia habari hususa za kifo chake, mazishi yake, na kukwezwa kwake. Sisi tutachangamshwa mioyo na kuimarishwa imani kwa kuufikiria unabii huu na utimizo wake.

      “Mtumishi Wangu”—Yeye Ni Nani?

      4. Baadhi ya wasomi Wayahudi wametoa maoni gani kuhusu utambulisho wa “mtumishi,” lakini kwa nini maoni hayo hayapatani na unabii wa Isaya?

      4 Muda mfupi uliopita Isaya amekuwa akisimulia habari za kufunguliwa kwa Wayahudi kutoka uhamishoni Babiloni. Sasa anatazama mbele kwenye tukio kubwa hata zaidi anapoandika maneno ya Yehova: “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara [“ufahamu wenye kina,” “NW”], atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu [“atakwezwa,” “NW”] sana.” (Isaya 52:13) “Mtumishi” huyu ni nani hasa? Muda wa karne zilizopita, wasomi Wayahudi walitoa maoni mbalimbali. Wengine wao walidai kwamba aliwakilisha taifa zima la Israeli likiwa uhamishoni Babiloni. Lakini maelezo hayo hayapatani na unabii wenyewe. Mtumishi wa Mungu anateseka kwa hiari yake. Ingawa hana hatia, anateseka kwa ajili ya dhambi za wengine. Hakika maelezo hayo hayapatani na hali ya taifa la Kiyahudi, lililoingia uhamishoni kwa sababu ya njia zake zenye dhambi. (2 Wafalme 21:11-15; Yeremia 25:8-11) Wengine walidai kwamba Mtumishi huyo aliwakilisha watu wa vyeo vya juu ambao walijiona kuwa wenye haki katika Israeli, na kwamba watu hao walipatwa na mateso kwa ajili ya Waisraeli wenye dhambi. Hata hivyo, nyakati za kuteseka katika Israeli, hakuna kikundi fulani cha watu hususa kilichotaabika kwa ajili ya kingine.

      5. (a) Wasomi fulani Wayahudi wameonyesha matumizi gani kuhusu unabii wa Isaya? (Ona kielezi-chini.) (b) Yule Mtumishi anatambulishwa wazi kuwa nani katika kitabu cha Biblia cha Matendo?

      5 Kabla ya kufika kwa Ukristo, na kwa kadiri fulani wakati wa zile karne za mapema za Wakati wa Kawaida, wasomi wachache Wayahudi walitumia unabii huu kumhusu Mesiya. Usahihi wa kutumia unabii huo kwa njia hiyo unaonekana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kitabu cha Matendo kinaripoti kwamba yule towashi Mwethiopia aliposema kuwa hajui ni nani anayetambuliwa kuwa Mtumishi wa unabii wa Isaya, Filipo ‘alimtangazia habari njema juu ya Yesu.’ (Matendo 8:26-40; Isaya 53:7, 8) Vivyo hivyo, vitabu vingine vya Biblia humtambulisha Yesu Kristo kuwa ndiye Mtumishi wa Kimesiya wa unabii wa Isaya.a Tunapozungumzia unabii huu, tutaona ulinganifu mbalimbali usioweza kukanushwa uliopo kati ya yule ambaye Yehova anamwita “mtumishi wangu” na Yesu wa Nazareti.

      6. Unabii wa Isaya unaonyeshaje kwamba Mesiya atafanikiwa kuyatimiza mapenzi ya kimungu?

      6 Unabii unaanza kwa kueleza mafanikio ya mwisho ya Mesiya katika kuyatimiza mapenzi ya kimungu. Neno “mtumishi” linaonyesha kwamba yeye atakubali kufuata mapenzi ya Mungu, kama vile mtumishi anavyokubali kufuata mapenzi ya mkubwa wake. Kwa kufanya hivyo, “atatenda kwa [“ufahamu wenye kina,” NW].” Ufahamu ni uwezo wa kuona hali fulani kindani. Kutenda kwa ufahamu wenye kina ni kutenda kwa akili. Kitabu kimoja cha marejezo husema hivi kuhusu kitenzi cha Kiebrania kilichotumiwa hapa: “Wazo kuu la neno hilo ni kushughulikia mambo kwa uangalifu na kwa hekima. Yeye anayeshughulikia mambo kwa hekima atapata mafanikio.” Uhakika wa kwamba Mesiya atafanikiwa unaonekana kutokana na vile unabii unavyosema ‘atainuliwa juu na kukwezwa sana.’

      7. Yesu Kristo ‘alitendaje kwa ufahamu wenye kina,’ na ‘ameinuliwa juu na kukwezwa sana’ jinsi gani?

      7 Kweli Yesu ‘alitenda kwa ufahamu wenye kina,’ akaonyesha kuwa anaelewa unabii mbalimbali wa Biblia uliotumika kumhusu, akaongozwa na unabii huo kuyafanya mapenzi ya Baba yake. (Yohana 17:4; 19:30) Matokeo yakawa nini? Baada ya Yesu kufufuliwa na kupaa mbinguni, “Mungu alimkweza kwenye cheo cha juu zaidi akampa kwa fadhili jina lililo juu ya kila jina jingine.” (Wafilipi 2:9; Matendo 2:34-36) Halafu, mwaka wa 1914 Yesu aliyetukuzwa akainuliwa juu hata zaidi. Yehova alimkweza kwenye kiti cha Ufalme wa Kimesiya. (Ufunuo 12:1-5) Naam, ‘aliinuliwa juu na kukwezwa sana.’

      ‘Kumkodolea Macho kwa Kustaajabu’

      8, 9. Wakati Yesu aliyekwezwa atakapokuja kufikiliza hukumu, watawala wa kidunia watatendaje, na kwa nini?

      8 Mataifa na watawala wao watatendaje kuhusu Mesiya aliyekwezwa? Tukiyaruka kwa muda yale maelezo yaliyo katika mabano katika sehemu ya pili ya mstari wa 14, unabii unasema hivi: “Kama vile wengi walivyokustaajabia . . . ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu.” (Isaya 52:14a, 15) Kwa maneno hayo, Isaya anaeleza, si juu ya kutokea kwa Mesiya mara ya kwanza, bali juu ya kukabiliana kwake na watawala wa kidunia mara ya mwisho.

      9 Yesu aliyekwezwa atakapokuja kufikiliza hukumu juu ya mfumo huu wa mambo usiomhofu Mungu, watawala wa kidunia ‘watamstaajabia.’ Ni kweli kuwa watawala wa kibinadamu hawatamwona kihalisi Yesu aliyetukuzwa. Lakini wataona dalili za waziwazi za kuthibitisha nguvu zake akiwa Mpiganaji wa kimbingu mwenye kumtetea Yehova. (Mathayo 24:30) Watalazimika kulifahamu jambo ambalo hawajawahi kusikia likisimuliwa na viongozi wa kidini—kwamba Yesu ndiye Mfikilizaji wa hukumu za Mungu! Mtumishi aliyekwezwa watakayekutana naye atatenda kwa njia ambayo hawaitazamii.

      10, 11. Inaweza kusemwaje kwamba Yesu aliharibiwa sura katika karne ya kwanza, na sura yake imeharibiwaje leo?

      10 Kulingana na maelezo yaliyo katika mabano katika mstari wa 14, Isaya anasema hivi: “Uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu ye yote, na umbo lake [“lenye fahari,” “NW”] zaidi ya wanadamu.” (Isaya 52:14b) Je, Yesu aliharibiwa sura kwa njia fulani? Sivyo. Ingawa Biblia haitoi maelezo kamili juu ya sura ya Yesu, hakuna shaka kwamba huyo Mwana mkamilifu wa Mungu alikuwa na sura na uso wa kupendeza. Ushuhuda unaonyesha kwamba maneno ya Isaya yanataja aibu ambayo Yesu alitendwa. Yeye aliwafichua kwa ujasiri viongozi wa kidini wa siku zake kuwa wanafiki, waongo, na wauaji; nao wakajibu kwa kumtukana. (1 Petro 2:22, 23) Walimshtaki kuwa ni mvunja-sheria, mkufuru, mdanganyi, mchochezi juu ya serikali ya Roma. Hivyo, washtaki hawa wa uwongo waliharibu uso wa Yesu kwa kumharibia sifa kabisa.

      11 Leo sifa ya Yesu inaendelea kuharibiwa. Watu walio wengi hufikiri kwamba Yesu ni kitoto kichanga katika hori ya ng’ombe au ni jamaa mwenye uso wa msiba akiwa amepigiliwa misumari msalabani, akiwa na taji la miiba kichwani na huku uso wake ukiwa umekunjamana vibaya kwa maumivu makali. Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo ndio wamehimiza maoni hayo. Wameshindwa kuonyesha kwamba Yesu ni Mfalme wa kimbingu aliye hodari, ambaye mataifa watatoa hesabu mbele yake. Hivi karibuni, watawala wa kibinadamu watakapokabiliana na Yesu aliyekwezwa, watalazimika kushughulika na Mesiya mwenye “mamlaka yote mbinguni na juu ya dunia”!—Mathayo 28:18.

      Nani Atazisadiki Habari Njema Hizi?

      12. Maneno yaliyo kwenye Isaya 53:1 yanatokeza maswali gani ya kuvutia?

      12 Baada ya kueleza jinsi ambavyo Mesiya amebadilika sura kwa njia ya kustaajabisha, yaani akaacha ‘kuharibika uso’ akawa mwenye ‘kukwezwa sana,’ Isaya anauliza hivi: “Ni nani aliyesadiki habari mliyoileta [“jambo lililosikiwa nasi,” “NW”]? Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?” (Isaya 53:1) Maneno haya ya Isaya yanatokeza maswali ya kuvutia: Je, unabii huu utatimizwa? Je, ‘mkono wa BWANA,’ unaowakilisha uwezo wa Yehova wa kutokeza nguvu nyingi, utajifunua na kuyatimiza maneno hayo?

      13. Paulo alionyeshaje kwamba unabii wa Isaya ulitimizwa katika Yesu, na kulikuwako itikio gani?

      13 Bila shaka jibu ni ndiyo! Katika barua yake kwa Waroma, Paulo ananukuu maneno ya Isaya kuonyesha kwamba unabii uliosikiwa na kuandikwa na Isaya ulitimia katika Yesu. Kutukuzwa kwa Yesu baada ya mateso yaliyompata duniani kulikuwa habari njema. “Hata hivyo,” anasema Paulo akiwataja Wayahudi wasioamini, “si wote waliotii habari njema. Kwa maana Isaya asema: ‘Yehova, ni nani aliyeweka imani katika jambo lililosikiwa kutoka kwetu?’ Kwa hiyo imani hufuata jambo lisikiwalo. Nalo jambo lisikiwalo ni kupitia neno juu ya Kristo.” (Waroma 10:16, 17) Ingawa hivyo, inasikitisha kwamba ni wachache katika siku za Paulo walioziamini habari njema juu ya Mtumishi wa Mungu. Kwa nini?

      14, 15. Mesiya anapaswa kuingia duniani akiwa na hali gani?

      14 Kisha unabii unawaeleza Waisraeli sababu za maswali yaliyoandikwa katika mstari wa 1 na, unapofanya hivyo, unaonyesha ni kwa nini wengi hawatamkubali Mesiya: “Alikua mbele zake [mtazamaji] kama mche mwororo, na kama mzizi katika nchi kavu; yeye hana umbo [“lenye fahari,” “NW”] wala uzuri; na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.” (Isaya 53:2) Hapa tunaiona hali ambayo Mesiya atapaswa kuingia nayo duniani. Atapaswa kuanza kwa hali ya chini, aonekane na watazamaji kama asiyeweza kuwa mtu wa maana. Zaidi ya hilo, atapaswa kuwa kama mche tu, kikonyo chororo, kinachokua juu ya shina au tawi la mti. Pia atapaswa kuwa kama mzizi unaotegemea maji katika udongo mkavu, usioweza kuzaa. Na hatapaswa kuja kwa sherehe na fahari—atakuja bila majoho ya kifalme, bila mataji yoyote yanayometameta. Bali, atapaswa kuanza kwa hali ya chini, bila kujionyesha.

      15 Huo ni ufafanuzi mzuri kama nini kuhusu mwanzo wa Yesu wa hali ya chini akiwa binadamu! Maria, yule Myahudi bikira, alimzaa katika chaa cha ng’ombe, katika mji mdogo uitwao Bethlehemu.b (Luka 2:7; Yohana 7:42) Maria na mume wake, Yosefu, walikuwa maskini. Siku 40 hivi baada ya Yesu kuzaliwa, walileta toleo la dhambi lililoruhusiwa iwapo watu walikuwa maskini, yaani “njiwa-tetere au hua wachanga wawili.” (Luka 2:24; Mambo ya Walawi 12:6-8) Baadaye, Maria na Yosefu wakakaa Nazareti, Yesu akakulia huko katika familia kubwa, ambayo inaelekea ilikuwa na riziki ya kiasi tu.—Mathayo 13:55, 56.

      16. Ni kweli kwamba Yesu hakuwa na ‘umbo lenye fahari’ wala ‘uzuri’ jinsi gani?

      16 Alipokuwa binadamu, ilionekana ni kama Yesu hakutia mizizi yake katika udongo unaofaa. (Yohana 1:46; 7:41, 52) Ingawa alikuwa mwanadamu mkamilifu aliye mzao wa Mfalme Daudi, hali zake za chini hazikumpa kamwe ‘umbo lenye fahari’ wala ‘uzuri’—angalau machoni pa wale waliokuwa wakimtazamia Mesiya atoke katika asili yenye kuvutia zaidi. Kwa kuchochewa na viongozi wa kidini Wayahudi, watu wengi waliongozwa kumpuuza na hata kumdharau. Mwishowe halaiki za watu hazikuona kitu cha kupendeza katika huyo Mwana mkamilifu wa Mungu.—Mathayo 27:11-26.

      “Alidharauliwa na Kukataliwa na Watu”

      17. (a) Isaya anaanza kueleza nini, na kwa nini anaandika kwa kutumia usemi wa wakati uliopita? (b) Ni nani ‘waliomdharau’ na ‘kumkataa’ Yesu, na jinsi gani?

      17 Sasa Isaya anaanza kueleza kirefu jinsi Mesiya atakavyoonwa na kutendewa: “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; mtu wa huzuni nyingi [“aliyekusudiwa maumivu,” “NW”], ajuaye sikitiko [“ugonjwa,” “NW”]; na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa wala hamkumhesabu kuwa kitu.” (Isaya 53:3) Kwa kuwa Isaya ana uhakika kwamba maneno yake yatatimizwa, anaandika kwa kutumia wakati uliopita, kana kwamba yamekwisha timizwa. Je, kweli Yesu Kristo alidharauliwa na kukataliwa na watu? Ndivyo hasa! Viongozi wa kidini waliojiona kuwa waadilifu, na pia wafuasi wao, walimwona kuwa mtu wa kuchukiza kuliko wanadamu wote. Walimwita rafiki ya wakusanya-kodi na makahaba. (Luka 7:34, 37-39) Walimtemea mate usoni. Walimpiga ngumi na kumtukana. Walimchekacheka kwa dhihaka. (Mathayo 26:67) ‘Watu wa Yesu mwenyewe hawakumkaribisha,’ kwani walishawishiwa na adui hawa wa ukweli.—Yohana 1:10, 11.

      18. Kwa kuwa Yesu hakupata kuwa mgonjwa kamwe, alikuwaje ‘mtu aliyekusudiwa maumivu, ajuaye ugonjwa’?

      18 Akiwa mwanadamu mkamilifu, Yesu hakuwahi kuwa mgonjwa. Na bado yeye alikuwa ‘mtu aliyekusudiwa maumivu, ajuaye ugonjwa.’ Maumivu na magonjwa hayo hayakuwa yake mwenyewe. Yesu alitoka mbinguni akaingia katika ulimwengu mgonjwa. Aliishi miongoni mwa wenye kuteseka na kuumia, lakini hakuwaepuka wale waliokuwa wagonjwa, ama kimwili ama kiroho. Akiwa kama tabibu mwenye kujali, alifahamu sana mateso ya watu waliokuwa karibu naye. Isitoshe, aliyaweza mambo yasiyowezwa na tabibu aliye binadamu wa kawaida.—Luka 5:27-32.

      19. Ni uso wa nani ‘uliofichwa,’ na adui za Yesu walionyeshaje kwamba ‘walimhesabu kuwa si kitu’?

      19 Hata hivyo, adui za Yesu walikuwa na maoni ya kwamba yeye ndiye mgonjwa, wakawa hawamtaki. Uso wake ‘ulifichwa’ usionekane, lakini si kwa sababu ya yeye kuficha uso asionwe na wengine. Wakati The New English Bible inapotafsiri Isaya 53:3, inatumia kifungu cha maneno “kitu ambacho watu wanageuza macho kwingineko ili waache kukiona.” Wapinzani wa Yesu walimwona kuwa chukizo kubwa, hata wakageuka kumwepuka kana kwamba yeye ni maudhi yasiyostahili kutazamwa. Walimwona kuwa mwenye thamani isiyozidi bei ya mtumwa. (Kutoka 21:32; Mathayo 26:14-16) Walimpa heshima ndogo kuliko ile waliyompa yule mwuaji Baraba. (Luka 23:18-25) Lo! kweli walimwonyesha Yesu upeo wa madharau.

      20. Maneno ya Isaya yanawatolea watu wa Yehova faraja gani leo?

      20 Watumishi wa Yehova leo wanaweza kupata faraja nyingi kutokana na maneno ya Isaya. Nyakati nyingine, huenda wapinzani wakawafanyia waabudu waaminifu wa Yehova madharau au kuwatendea kana kwamba wao si kitu. Hata hivyo, kama ilivyokuwa kuhusu Yesu, jambo la maana ni jinsi ambavyo Yehova Mungu anatuona kuwa watu wenye thamani. Ingawa wanadamu ‘walimwona Yesu kuwa si kitu,’ hiyo haikugeuza thamani yake kubwa machoni pa Mungu!

      ‘Alidungwa kwa Makosa Yetu’

      21, 22. (a) Mesiya alichukua na kujitwika nini kwa ajili ya wengine? (b) Wengi walimwonaje Mesiya, na kuteseka kwake kulifikia upeo gani?

      21 Kwa nini Mesiya alilazimika kuteseka na kufa? Isaya anaeleza hivi: “Hakika ameyachukua masikitiko [“magonjwa,” “NW”] yetu, amejitwika huzuni zetu [“maumivu yetu,” “NW”]; lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa [“kwa tauni,” “NW”], amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa [“alikuwa akidungwa,” “NW”] kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu; adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Sisi sote kama kondoo tumepotea [“tumetanga-tanga,” “NW”]; kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; na BWANA ameweka juu yake maovu yetu sisi sote.”—Isaya 53:4-6.

      22 Mesiya alichukua magonjwa ya wengine na kujitwika maumivu yao. Ni kana kwamba aliinua mizigo yao, akaiweka juu ya mabega yake mwenyewe na kuichukua. Na kwa kuwa ugonjwa na maumivu ni matokeo ya hali yenye dhambi ya wanadamu, Mesiya alizichukua dhambi za wengine. Wengi hawakuelewa sababu ya mateso yake na waliamini kwamba Mungu alikuwa akimwadhibu, akimpiga kwa tauni ya ugonjwa wa kuchukiza sana.c Kuteseka kwa Mesiya kulifikia upeo alipodungwa, akachubuliwa, na kujeruhiwa. Maneno hayo yanakazia sana kifo chenye jeuri na maumivu. Lakini kifo chake kina nguvu za kufunika dhambi; kinaandaa msingi wa kuwarudishia hali njema wale wanaotanga-tanga katika makosa na dhambi, kuwasaidia waweze kupata amani pamoja na Mungu.

      23. Yesu alijitwikaje mateso ya wengine?

      23 Yesu alijitwikaje mateso ya wengine? Gospeli ya Mathayo inanukuu Isaya 53:4 ikisema hivi: “Watu walimletea watu wengi waliopagawa na roho waovu; naye akafukuza hao roho kwa kusema neno, naye akaponya wote waliokuwa na hali mbaya; ili kupate kutimizwa lile lililosemwa kupitia Isaya nabii, akisema: ‘Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na kuchukua maradhi yetu.’” (Mathayo 8:16, 17) Kwa kuwaponya wale waliomjia wakiwa na maradhi mbalimbali, Yesu alijitwika mateso yao. Na maponyo hayo yalitumia nguvu zake. (Luka 8:43-48) Uwezo wake wa kuponya magonjwa ya aina zote—ya kimwili na ya kiroho—ulithibitisha kwamba alitiwa nguvu za kusafisha watu dhambi.—Mathayo 9:2-8.

      24. (a) Kwa nini ilionekana machoni pa watu wengi ni kama Yesu ‘alipigwa kwa tauni’ na Mungu? (b) Kwa nini Yesu aliteseka na kufa?

      24 Na bado, watu wengi waliona ni kama Yesu ‘alipigwa kwa tauni’ na Mungu. Kwani je, yeye hakuteseka kwa uchochezi wa viongozi waheshimiwa wa kidini? Hata hivyo, kumbuka kwamba hakuteseka kwa sababu ya dhambi zozote alizozitenda mwenyewe. “Kristo aliteseka kwa ajili yenu,” anasema Petro, “akiwaachia kigezo ili nyinyi mfuate hatua zake kwa ukaribu. Yeye hakufanya dhambi, wala udanganyo haukupatikana kinywani mwake. Yeye mwenyewe alichukua dhambi zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti, ili tupate kuachana kabisa na dhambi na kuishi kuelekea uadilifu. Na ‘kwa mapigo yake mliponywa.’” (1 Petro 2:21, 22, 24) Wakati mmoja sisi sote tulipotea katika dhambi, ‘kama kondoo, tukipotea njia.’ (1 Petro 2:25) Hata hivyo, Yehova alimtumia Yesu kuandaa ukombozi kututoa katika hali yetu yenye dhambi. Aliweka maovu yetu ‘juu yake Yesu.’ Yesu asiye na dhambi aliteseka kwa hiari ili alipie adhabu ya dhambi zetu. Kwa kuteseka isivyostahili katika kifo cha aibu juu ya mti, alifanya iwezekane sisi tupatanishwe na Mungu.

      ‘Alijiacha Aumizwe’

      25. Tunajuaje kwamba Mesiya aliteseka na kufa kwa hiari?

      25 Je, Mesiya alikuwa na hiari ya kuteseka na kufa? Isaya anasema hivi: “Alionewa, lakini alinyenyekea [“alikuwa akijiacha aumizwe,” “NW”], wala hakufunua kinywa chake; kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, na kama vile kondoo anyamazavyo mbele yao wakatao manyoya yake; naam, hakufunua kinywa chake.” (Isaya 53:7) Katika usiku wa mwisho wa maisha yake, Yesu angaliweza kuagiza “malejioni zaidi ya kumi na mawili ya malaika” yaje kumsaidia. Lakini yeye alisema hivi: “Katika kisa hicho, Maandiko yangetimizwaje kwamba lazima itendeke kwa njia hii?” (Mathayo 26:53, 54) “Mwana-Kondoo wa Mungu” hakutokeza upinzani wowote. (Yohana 1:29) Makuhani wakuu na wanaume wazee walipomshtaki kwa uwongo mbele ya Pilato, Yesu “hakutoa jibu.” (Mathayo 27:11-14) Hakutaka kusema lolote ambalo lingaliweza kumvuruga asitimize mapenzi ya Mungu kumhusu. Yesu alikuwa na hiari ya kufa akiwa Mwana-Kondoo wa dhabihu, akijua vema kabisa kwamba kifo chake kingekomboa wanadamu watiifu kutoka kwenye dhambi, ugonjwa, na kifo.

      26. “Kizuizi” kilitumiwaje na wapinzani wa Yesu?

      26 Sasa Isaya anaeleza kirefu juu ya kuteseka na kuaibishwa kwa Mesiya. Nabii huyo anaandika hivi: “Kwa kuonewa na kuhukumiwa [“kwa sababu ya kizuizi na hukumu,” “NW”] aliondolewa; na maisha yake ni nani atakayeisimulia? [“na ni nani atakayejihangaisha kujua hata mambo madogo madogo kuhusu kizazi chake?” “NW”] Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.” (Isaya 53:8) Yesu alipochukuliwa na adui zake mwishowe, wapinzani hao wa kidini waliweka “kizuizi” kwa jinsi ambavyo walishughulika naye. Haimaanishi kwamba walisitasita kuonyesha chuki yao, bali kwamba walimzuia au kumnyima kutendewa haki. Katika tafsiri yake ya Isaya 53:8, Septuagint ya Kigiriki inasema “kuaibishwa” badala ya “kizuizi.” Adui za Yesu walimwaibisha kwa kumnyima haki ya kutendewa bila kuonewa, haki ambayo hata mhalifu wa kawaida anaistahili. Kesi ya Yesu ilisikizwa kwa njia ya kupuuza haki kabisa. Jinsi gani hivyo?

      27. Viongozi wa kidini Wayahudi walipokuwa wakisikiza kesi ya kushtakiwa kwa Yesu, walipuuza sheria zipi, na walivunja Sheria ya Mungu kwa njia zipi?

      27 Kwa kupiga moyo konde wammalize Yesu, viongozi wa kidini Wayahudi walivunja sheria zao wenyewe. Kulingana na mapokeo, Sanhedrini haingeweza kusikiza kesi ya kifo mahali penginepo, isipokuwa katika ukumbi wa mawe yaliyochongwa, ndani ya eneo la hekalu peke yake, wala si katika nyumba ya kuhani wa cheo cha juu. Kesi kama hiyo ilipasa kufanywa mchana, wala si baada ya jua kushuka. Na katika kesi ya kifo, uamuzi wa kuhukumu mtu kuwa mwenye hatia ulipasa kutangazwa siku ile iliyofuata kumalizika kwa kesi. Hivyo basi, hakuna kesi ambazo zingeweza kusikizwa usiku wa kuamkia Sabato au sikukuu. Sheria zote hizo zilipuuzwa katika kesi ya kusikiza mashtaka ambayo Yesu alifanyiwa. (Mathayo 26:57-68) Kwa ubaya zaidi, viongozi hao wa kidini waliivunja Sheria ya Mungu kimachomacho wakati wa kushughulikia kesi hiyo. Kwa mfano, waliona ni afadhali watoe rushwa ili kumnasa Yesu. (Kumbukumbu la Torati 16:19; Luka 22:2-6) Waliwasikiza mashahidi wa uwongo. (Kutoka 20:16; Marko 14:55, 56) Tena walitunga hila ili wafungue mwuaji, na kwa njia hiyo wakajiletea hatia ya damu, wao wenyewe na nchi yao. (Hesabu 35:31-34; Kumbukumbu la Torati 19:11-13; Luka 23:16-25) Hivyo basi, hakukuwa na “hukumu,” wala kesi haikusikizwa kwa haki ili iamuliwe kwa usahihi na bila upendeleo.

      28. Ni nini ambacho adui za Yesu hawakufikiria katika uamuzi wao?

      28 Je, adui za Yesu walichunguza waone mwanamume huyo aliyekuwa akifanyiwa kesi mbele yao alikuwa nani hasa? Isaya anauliza swali kama hilo: “Ni nani atakayejihangaisha kujua hata mambo madogo madogo kuhusu kizazi chake?” Huenda neno “kizazi” likamaanisha ukoo wa mtu, au mambo yanayohusiana na asili yake. Yesu alipofanyiwa kesi mbele ya Sanhedrini, washiriki wa baraza hilo hawakufikiria mambo yaliyohusiana na asili yake—kwamba aliyatimiza matakwa ya Mesiya aliyeahidiwa. Badala yake, walimshtakia kukufuru, wakakata kesi kwamba anastahili kufa. (Marko 14:64) Baadaye, gavana Mroma Pontio Pilato alikazwa mpaka akakubali kufanya vile alivyoambiwa, akamhukumu Yesu kutundikwa mtini. (Luka 23:13-25) Hivyo ndivyo Yesu ‘alivyokatiliwa mbali’ katikati ya maisha yake, akiwa na umri wa miaka 33 1/2 tu.

      29. Yesu alifanyiwaje kaburi “pamoja na wabaya” na “pamoja na matajiri”?

      29 Kwa habari ya kifo na mazishi ya Mesiya, sasa Isaya anaandika hivi: “Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; na pamoja na matajiri katika kufa kwake; ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.” (Isaya 53:9) Yesu alikuwaje pamoja na waovu na matajiri pia alipokufa na kuzikwa? Siku ya Nisani 14, 33 W.K., alikufa juu ya mti wa kufikiliza hukumu ya kifo, nje ya kuta za Yerusalemu. Kwa kuwa alitundikwa mtini kati ya watenda maovu wawili, kwa kadiri fulani alifanyiwa kaburi pamoja na wabaya katika maana hiyo. (Luka 23:33) Hata hivyo, baada ya Yesu kufa, Yosefu, mwanamume tajiri wa kutoka Arimathea, alipiga moyo konde akamwomba Pilato ruhusa ya kuushusha mwili wa Yesu auzike. Yosefu, akiwa pamoja na Nikodemo, aliutayarisha mwili ili uzikwe, akauweka katika kaburi lake lililochimbwa karibuni. (Mathayo 27:57-60; Yohana 19:38-42) Kwa hiyo Yesu alifanyiwa kaburi pamoja na matajiri pia.

      “Bwana Aliridhika Kumchubua”

      30. Yehova aliridhika kumchubua Yesu katika maana gani?

      30 Kisha Isaya anasema jambo la kugutusha: “BWANA aliridhika kumchubua; amemhuzunisha; utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi [“toleo la hatia,” “NW”], ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, na mapenzi ya BWANA yatafanikiwa mkononi mwake; ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki atawafanya wengi kuwa wenye haki [“ataletea wengi msimamo wenye uadilifu,” “NW”]; naye atayachukua maovu yao.” (Isaya 53:10, 11) Kwa kweli ingewezekanaje Yehova aridhike kumwona mtumishi huyu mwaminifu akiwa amechubuka? Ni wazi kwamba si Yehova binafsi aliyemtesa Mwana wake mpendwa. Adui za Yesu walikuwa na lawama kamili kwa yale waliyomtenda. Lakini Yehova aliwaruhusu watende ukatili. (Yohana 19:11) Kwa sababu gani? Hakika huyo Mungu wa hisia-mwenzi na huruma nyororo aliumia kumwona Mwanawe asiye na hatia akiteseka. (Isaya 63:9; Luka 1:77, 78) Hakika Yehova hakuchukizwa na Yesu kwa vyovyote. Hata hivyo, Yehova aliridhishwa na hiari ya Mwanawe kuteseka kwa ajili ya baraka zote ambazo zingetokana na mateso yake.

      31. (a) Yehova aliitoaje nafsi ya Yesu iwe “toleo la hatia”? (b) Baada ya taabu zote zilizompata Yesu akiwa mwanadamu, ni hakika kwamba yeye anaridhishwa na jambo gani hasa?

      31 Kwanza, Yehova aliitoa nafsi ya Yesu iwe “toleo la hatia.” Hivyo basi, Yesu alipopaa kurudi mbinguni, aliingia mbele za Yehova, akiwa na ubora wa uhai wake wa kibinadamu uliotolewa dhabihu uwe toleo la hatia, na Yehova alifurahi kuukubali kwa niaba ya wanadamu wote. (Waebrania 9:24; 10:5-14) Yesu alijipatia “uzao” kupitia toleo lake la hatia. Akiwa “Baba wa milele,” anaweza kuwapa uhai—uhai wa milele—wale wanaodhihirisha imani katika damu yake iliyomwagwa. (Isaya 9:6) Baada ya taabu zote zilizompata Yesu akiwa nafsi ya kibinadamu, yeye anaridhika kama nini kuwa na tazamio la kuwakomboa wanadamu kutoka katika dhambi na kifo! Na bila shaka anaridhika hata zaidi kujua kwamba uaminifu wake wa maadili ulimwandalia Baba yake wa kimbingu jibu kwa ajili ya dhihaka kali za Adui Yake, Shetani Ibilisi.—Mithali 27:11.

      32. Yesu anatumia “maarifa” gani ‘kuletea wengi msimamo wenye uadilifu,’ na ni nani wanaopata msimamo huo?

      32 Baraka nyingine inayotokana na kifo cha Yesu ni kwamba analetea “wengi msimamo wenye uadilifu,” hata sasa. Isaya anasema kwamba anafanya hivyo “kwa maarifa yake.” Ushuhuda unaonyesha kwamba hayo ni maarifa ambayo Yesu alijipatia kwa kuwa mwanadamu na kuteseka isivyo haki kwa kumtii Mungu. (Waebrania 4:15) Baada ya kuteseka hadi kifo, Yesu aliweza kuandaa dhabihu iliyohitajiwa ili kuwasaidia wengine wapate msimamo wenye uadilifu. Ni nani wanaopata msimamo huo wenye uadilifu? Kwanza, ni wafuasi wake watiwa-mafuta. Kwa sababu wanadhihirisha imani katika dhabihu ya Yesu, Yehova anawatangaza kuwa waadilifu kwa tazamio la kuwafanya wawe wanawe, na kuwafanya warithi-washirika na Yesu. (Waroma 5:19; 8:16, 17) Halafu “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” unadhihirisha imani katika damu ya Yesu iliyomwagwa na kufurahia msimamo wenye uadilifu wakiwa na tazamio la kuwa rafiki za Mungu na kuwa waokokaji wa Har-Magedoni.—Ufunuo 7:9; 16:14, 16; Yohana 10:16; Yakobo 2:23, 25.

      33, 34. (a) Ni jambo gani la kuchangamsha mioyo yetu tunalojifunza kuhusu Yehova? (b) “Walio wengi” ambao Mtumishi wa Kimesiya anapokea “sehemu” akiwa miongoni mwao ni akina nani?

      33 Mwisho, Isaya anaeleza juu ya ushindi mbalimbali wa Mesiya: “Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu [“walio wengi,” “NW”], naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, na kuwaombea wakosaji.”—Isaya 53:12.

      34 Maneno ya kumalizia ya sehemu hii ya unabii wa Isaya yanafundisha jambo fulani la kuchangamsha moyo kuhusu Yehova: Yeye anawathamini wale wanaobaki wakiwa waaminifu-washikamanifu kwake. Hiyo inaonyeshwa na ahadi ya kwamba ‘atamgawia’ Mtumishi wa Kimesiya ‘sehemu pamoja na walio wengi.’ Inaonekana kwamba maneno haya yametokana na ile desturi ya kugawana nyara za vita. Yehova anauthamini uaminifu-mshikamanifu wa waaminifu “wengi” wa nyakati za kale, miongoni mwao wakiwamo Noa, Abrahamu, na Yobu, na amewawekea “sehemu” katika ulimwengu wake mpya unaokuja. (Waebrania 11:13-16) Na atamgawia Mtumishi wake wa Kimesiya sehemu jinsi hiyo hiyo. Hakika Yehova hatamwacha Mtumishi huyo akose thawabu kwa uaminifu wake wa maadili. Sisi pia tunaweza kukaa na uhakikisho wa kwamba Yehova ‘hatasahau kazi yetu na upendo tunaoonyesha kwa ajili ya jina lake.’—Waebrania 6:10.

      35. Ni akina nani “walio hodari” ambao Yesu anagawana nyara nao, na nyara hizo ni nini?

      35 Mtumishi wa Mungu atapata nyara za vita pia kwa kuwashinda adui zake. Atagawana nyara hizo na “walio hodari.” Hao “walio hodari” ni akina nani katika utimizo wa jambo hilo? Ni wanafunzi wa Yesu walio wa kwanza kuushinda ulimwengu kama alivyofanya—wale raia 144,000 wa “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16; Yohana 16:33; Ufunuo 3:21; 14:1) Basi, nyara hizo ni nini? Ushuhuda unaonyesha kwamba zinahusisha “zawadi zikiwa wanadamu,” ambazo kwa njia ya mfano inaweza kusemwa kwamba Yesu anampokonya Shetani zawadi hizo na kulipatia kutaniko la Kikristo. (Waefeso 4:8-12) Wale 144,000 “walio hodari” wanapewa pia sehemu ya nyara nyingine. Kwa sababu ya kuushinda ulimwengu, wanamnyang’anya Shetani msingi wowote wa kumdhihaki Mungu vikali. Wanamkweza Yehova kwa kumwonyesha ujitoaji usiovunjika, wakiufanya moyo wake ushangilie.

      36. Je, Yesu alijua kwamba alikuwa akiutimiza unabii kuhusu Mtumishi wa Mungu? Eleza.

      36 Yesu alijua kwamba alikuwa akiutimiza unabii kuhusu Mtumishi wa Mungu. Katika usiku aliokamatwa, aliyanukuu maneno yaliyoandikwa kwenye Isaya 53:12 akayatumia yamhusu yeye mwenyewe: “Nawaambia nyinyi kwamba lazima hili ambalo limeandikwa litimizwe katika mimi, yaani, ‘Naye alihesabiwa pamoja na waasi-sheria.’ Kwa maana kile kinihusucho mimi kinakuwa na utimizo.” (Luka 22:36, 37) Inasikitisha kwamba Yesu alitendwa kama mwasi-sheria. Aliuawa kama mvunja-sheria, akiwa ametundikwa kati ya wanyang’anyi wawili. (Marko 15:27) Hata hivyo, alivumilia suto hilo kwa hiari, akijua vema kabisa kwamba alikuwa akitufanyia upatanisho. Kwa njia hiyo alisimama kati ya watenda dhambi na pigo la adhabu ya kifo, naye mwenyewe akalipokea pigo hilo.

      37. (a) Maandishi ya kihistoria kuhusu maisha ya Yesu na kifo chake hutuwezesha kutambua nini? (b) Kwa nini tunapaswa kumshukuru Yehova Mungu na Mtumishi wake aliyekwezwa, Yesu Kristo?

      37 Maandishi ya kihistoria kuhusu maisha ya Yesu na kifo chake hutuwezesha kumtambua bila kukosea: Yesu Kristo ndiye Mtumishi wa Kimesiya wa unabii wa Isaya. Inatupasa tushukuru kama nini kwamba Yehova alionyesha hiari ya kumwacha Mwanawe mpendwa atimize fungu la kiunabii la Mtumishi, akiteseka na kufa ili sisi tuweze kukombolewa kutoka katika dhambi na kifo! Hivyo Yehova alituonyesha upendo mkubwa sana. Waroma 5:8 husema hivi: “Mungu apendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.” Vilevile inatupasa tumshukuru kama nini Yesu Kristo, yule Mtumishi aliyekwezwa, kwa kumwaga nafsi yake kwa hiari hadi kifo chenyewe!

      [Maelezo ya Chini]

      a Targumi ya Jonathan ben Uzziel (karne ya kwanza W.K.), iliyotafsiriwa na J. F. Stenning, inasema hivi inapofasiri Isaya 52:13: “Tazama, mtumishi wangu, Yule Mtiwa-Mafuta (au, yule Mesiya), atapata ufanisi.” Hivyo hivyo, Talmudi ya Kibabiloni (karibu karne ya tatu W.K.) inasema hivi: “Yule Mesiya—jina lake nani? . . . [; wale] wa nyumba ya Rabi [husema, Yule mgonjwa], kwa kuwa inasemwa, ‘Hakika yeye amebeba magonjwa yetu.’”—Sanhedrin 98b; Isaya 53:4.

      b Nabii Mika alitaja kwamba Bethlehemu ni “mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda.” (Mika 5:2) Na bado, Bethlehemu huyo mdogo aliipata heshima isiyo na kifani ya kuwa mji ambamo Mesiya alizaliwa.

      c Neno la Kiebrania lililotafsiriwa ‘kupigwa kwa tauni’ linatumiwa pia kuhusu ukoma. (2 Wafalme 15:5) Wasomi fulani wanasema kwamba, wazo ambalo Wayahudi fulani walipata kutokana na Isaya 53:4 ni kwamba Mesiya angekuwa mwenye ukoma. Talmudi ya Kibabiloni hutumia mstari huu kuhusu Mesiya, ikimwita “yule msomi mwenye ukoma.” Tafsiri ya Kikatoliki iitwayo Douay Version, inatoa wazo moja na Vulgate ya Kilatini kwa kuufasiri mstari huo hivi: “Tumemfikiria kana kwamba ni mwenye ukoma.”

      [Chati katika ukurasa wa 212]

      MTUMISHI WA YEHOVA

      Jinsi Yesu Alivyotimiza Fungu la Kuwa

      UNABII

      TUKIO

      UTIMIZO

      Isa. 52:13

      Atukuzwa na kukwezwa

      Mdo. 2:34-36; Flp. 2:8-11; 1 Pet. 3:22

      Isa. 52:14

      Alisingiziwa na kuharibiwa sifa

      Mt. 11:19; 27:39-44, 63, 64; Yn 8:48; 10:20

      Isa. 52:15

      Alishtua mataifa mengi

      Mt. 24:30; 2 The. 1:6-10; Ufu. 1:7

      Isa. 53:1

      Hakusadikiwa

      Yn. 12:37, 38; Rom. 10:11, 16, 17

      Isa. 53:2

      Mwanzo wa kibinadamu wa hali ya chini na usio wa kujionyesha

      Luka 2:7; Yn 1:46

      Isa. 53:3

      Alidharauliwa na alikataliwa

      Mt. 26:67; Luka 23:18-25; Yn 1:10, 11

      Isa. 53:4

      Alichukua mago njwa yetu

      Mt. 8:16, 17; Luka 8:43-48

      Isa. 53:5

      Alidungwa

      Yn 19:34

      Isa. 53:6

      Aliteseka kwa ajili ya makosa ya wengine

      1 Pet. 2:21-25

      Isa. 53:7

      Mnyamavu na asiyelalamika mbele ya washitaki

      Mt. 27:11-14; Mar 14:60, 61; Mdo 8:32, 35

      Isa. 53:8

      Alifanyiwa kesi bila haki na akahukumiwa hatia

      Mt. 26:57-68; 27:1, 2, 11-26; Yn 18:12-14, 19-24, 28-40

      Isa. 53:9

      Alizikwa pamoja na matajiri

      Mt 27:57-60; Yn 19:38-42

      Isa. 53:10

      Nafsi iliwekwa kuwa toleo la hatia

      Ebr. 9:24; 10:5-14

      Isa. 53:11

      Alifungua njia ya wengi kujipatia msimamo wenye uadilifu

      Rom. 5:18, 19; 1 Pet. 2:24; Ufu. 7:14

      Isa. 53:12

      Alihesabiwa kuwa pamoja na watenda dhambi

      Mt. 26:55, 56; 27:38; Luka 22:36, 37

      [Picha katika ukurasa wa 203]

      ‘Alidharauliwa na watu’

      [Picha katika ukurasa wa 206]

      “Hakufunua kinywa chake”

      [Hisani]

      Picha imetolewa katika “Ecce Homo” ya Antonio Ciseri

      [Picha katika ukurasa wa 211]

      “Alimwaga nafsi yake hata kufa”

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Tano

      Yule Mwanamke Tasa Ashangilia

      Isaya 54:1-17

      1. Kwa nini Sara alitamani sana kuzaa watoto, na alipatwa na nini?

      SARA alitamani sana kuzaa watoto. Lakini jambo la kusikitisha lilikuwa kwamba yeye alikuwa tasa, na hilo lilimwuma sana. Siku zake, utasa ulionwa kuwa suto, lakini Sara hakuumwa na hilo tu. Alitamani sana kuona utimizo wa ahadi ya Mungu kwa mumewe. Abrahamu alipaswa kuwa baba wa mbegu ambayo ingekuwa baraka kwa familia zote za dunia. (Mwanzo 12:1-3) Hata hivyo, miongo mingi baada ya Mungu kutoa ahadi hiyo, bado mtoto hakutokea. Sara alizeeka angali hajapata mtoto. Huenda ikawa nyakati nyingine alijiuliza-uliza kama alikuwa amejiwekea matumaini ya bure. Lakini, siku moja kutamauka kwake kukageuka kuwa shangwe!

      2. Kwa nini unabii ulioandikwa katika Isaya sura ya 54 utupendeze?

      2 Shida ya Sara hutusaidia kuuelewa unabii ulioandikwa katika Isaya sura ya 54. Humo Yerusalemu anaambiwa mambo kana kwamba ni mwanamke tasa anayepata shangwe kubwa ya kuwa na watoto wengi. Yehova anawaonyesha watu wake wa kale hisia nyororo kwa kuwataja wote kwa ujumla kuwa mke wake wa mfano. Zaidi ya hilo, sura hii ya Isaya inatusaidia kufumbua sehemu muhimu inayohusiana na kile ambacho Biblia hukiita “siri takatifu.” (Waroma 16:25, 26) Nuru muhimu inaangazwa juu ya ibada safi leo kupitia kutambulishwa kwa “mwanamke” huyo na mambo yaliyotabiriwa katika unabii huo kuwa yatampata.

      Yule “Mwanamke” Atambuliwa

      3. Kwa nini “mwanamke” huyo tasa atakuwa na sababu ya kushangilia?

      3 Sura ya 54 inaanza kwa hali ya furaha: “Imba, wewe [“mwanamke,” “NW”] uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto [“wana,” “NW”] wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema BWANA.” (Isaya 54:1) Isaya anasisimuka kama nini kusema maneno hayo! Na utimizo wake utawaletea faraja iliyoje Wayahudi walioko uhamishoni Babiloni! Wakati huo Yerusalemu bado atakuwa ukiwa. Kwa maoni ya kibinadamu, itaonekana ni kama hakuna kamwe tumaini la jiji hilo kukaliwa na watu tena, sawa na vile isivyo kawaida mwanamke tasa kutumainia kuzaa watoto siku za uzeeni. Lakini “mwanamke” huyu ana baraka kubwa wakati wake ujao—atapata nguvu za uzazi. Yerusalemu atachachawa kwa shangwe ya ajabu. Atamiminikwa tena na “wana,” au wakaaji.

      4. (a) Mtume Paulo anatusaidiaje kuona kwamba bila shaka Isaya sura ya 54 ina utimizo mkubwa kuliko ule wa mwaka wa 537 K.W.K.? (b) “Yerusalemu la juu” ni nini?

      4 Huenda ikawa Isaya hajui jambo hili, lakini unabii wake utakuwa na utimizo zaidi ya mmoja. Mtume Paulo ananukuu kutoka Isaya sura ya 54 na kueleza kwamba “mwanamke” huyo anamaanisha kitu muhimu sana kuliko jiji la kidunia la Yerusalemu. Anaandika hivi: “Yerusalemu la juu ni huru, nalo ni mama yetu.” (Wagalatia 4:26) Hilo “Yerusalemu la juu” ni nini? Kwa wazi si lile jiji la Yerusalemu lililo katika Nchi ya Ahadi. Jiji hilo ni la kidunia, wala haliko “juu” katika makao ya kimbingu. “Yerusalemu la juu” ni “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu, tengenezo lake la viumbe-roho walio hodari.

      5. Katika drama ya mfano iliyoonyeshwa kwenye Wagalatia 4:22-31, ni nani wanaofananishwa na (a) Abrahamu? (b) Sara? (c) Isaka? (d) Hagari? (e) Ishmaeli?

      5 Ingawa hivyo, Yehova anawezaje kuwa na wanawake wawili wa mfano—mmoja wa kimbingu na yule mwingine wa kidunia? Je, hali hii inakosa upatano? Hata kidogo. Mtume Paulo anaonyesha kwamba jibu limo katika mfano wa kiunabii uliowekwa na familia ya Abrahamu. (Wagalatia 4:22-31; ona “Familia ya Abrahamu—Mfano wa Kiunabii,” katika ukurasa wa 218.) Sara, yule “mwanamke huru” aliyekuwa mke wa Abrahamu, anafananisha tengenezo la Yehova la viumbe-roho lililo kama mke. Naye Hagari, mjakazi aliyekuwa mke wa pili, au suria, wa Abrahamu anafananisha Yerusalemu la kidunia.

      6. Tengenezo la Mungu la kimbingu lilipitia kipindi kirefu cha utasa katika maana gani?

      6 Tukiwa na habari hizo za msingi, tunaanza kuona maana yenye kina kirefu ya Isaya 54:1. Baada ya miongo ya utasa, Sara alimzaa Isaka akiwa na umri wa miaka 90. Vivyo hivyo, tengenezo la Yehova la kimbingu lilipitia kipindi kirefu cha utasa. Kule nyuma katika Edeni, Yehova aliahidi kwamba “mwanamke” wake angetokeza ile “mbegu.” (Mwanzo 3:15, NW) Miaka zaidi ya 2,000 baadaye, Yehova alifanya agano lake pamoja na Abrahamu kuhusu ile Mbegu ya ahadi. Lakini “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alilazimika kungoja karne nyingi sana kabla ya kutokeza Mbegu hiyo. Hata hivyo, wakati ulifika watoto wa huyo aliyekuwa ‘mwanamke tasa’ wakawa wengi sana kuliko wale wa Israeli wa asili. Mfano unaohusu huyo mwanamke tasa unatusaidia kuona ni kwa nini malaika walikuwa na hamu nyingi sana ya kushuhudia ile Mbegu iliyotabiriwa ikiwasili. (1 Petro 1:12) Hilo lilitukia lini hatimaye?

      7. “Yerusalemu la juu” lilipata pindi ya kushangilia wakati gani, kama vile ilivyotabiriwa kwenye Isaya 54:1, na kwa nini unajibu hivyo?

      7 Kuzaliwa kwa Yesu akiwa mtoto wa kibinadamu hakika kulikuwa pindi ya kushangilia miongoni mwa malaika. (Luka 2:9-14) Lakini hilo silo tukio lililotabiriwa kwenye Isaya 54:1. Yesu alipozaliwa kwa roho takatifu mwaka wa 29 W.K., hapo ndipo alipopata kuwa mwana wa kiroho wa “Yerusalemu la juu,” akikubaliwa na Mungu mwenyewe peupe kuwa yeye ni ‘Mwana wake, mpendwa.’ (Marko 1:10, 11; Waebrania 1:5; 5:4, 5) Hapo ndipo yule “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alipopata sababu ya kushangilia, kwa kutimiza Isaya 54:1. Sasa hatimaye mwanamke huyo akawa ametokeza ile Mbegu iliyoahidiwa, yule Mesiya! Karne zake za utasa zikawa zimekwisha. Hata hivyo, huo haukuwa mwisho wa kushangilia kwake.

      Huyo Mwanamke Tasa Apata Wana Wengi Sana

      8. Kwa nini “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alikuwa na sababu ya kushangilia baada ya kutokeza ile Mbegu iliyoahidiwa?

      8 Baada ya Yesu kufa na kufufuliwa baadaye, “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alishangilia kupokea Mwana huyo mwenye upendeleo akiwa “mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu.” (Wakolosai 1:18) Kisha mwanamke huyo akaanza kutokeza wana zaidi wa kiroho. Kwenye Pentekoste ya 33 W.K., karibu wafuasi 120 wa Yesu walitiwa mafuta kwa roho takatifu, na kwa njia hiyo wakafanywa kuwa warithi-washirika pamoja na Kristo. Baadaye siku hiyo, wengine 3,000 waliongezwa. (Yohana 1:12; Matendo 1:13-15; 2:1-4, 41; Waroma 8:14-16) Jamii hiyo ya wana iliendelea kukua. Wakati wa karne za mapema za uasi-imani wa Jumuiya ya Wakristo, ukuzi huo ulipungua ukawa haba sana. Lakini, mambo yangebadilika katika karne ya 20.

      9, 10. Maagizo ‘kupanua mahali pa hema’ yangemaanisha nini kwa mwanamke aliyeishi hemani nyakati za kale, na kwa nini huo ni wakati wa shangwe kwa mwanamke huyo?

      9 Isaya anaendelea kutoa unabii juu ya kipindi fulani cha ukuzi wa kustaajabisha: “Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu. Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena.”—Isaya 54:2-4.

      10 Hapa Yerusalemu anaambiwa mambo kana kwamba ni mke na mama anayekaa katika mahema, sawa na Sara. Anapobarikiwa kwa kupata familia inayoongezeka, umefika wakati wa mama huyo kuhakikisha kwamba nyumba yake inapanuliwa. Anahitaji kuongeza urefu wa mapazia yake na kamba zake na kuvipigilia imara vigingi vya hema mahali pake papya. Hiyo ni kazi inayomfurahisha, na kwa kuwa huo ni wakati wa shughuli nyingi, anaweza kusahau kwa urahisi miaka mingi aliyoitumia akihangaika bila kujua kama siku moja angezaa watoto wa kuendeleza ukoo wa familia.

      11. (a) “Mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alibarikiwaje mwaka wa 1914? (Ona kielezi-chini.) (b) Kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, watiwa-mafuta walio duniani wamepata baraka gani?

      11 Yerusalemu la kidunia lilibarikiwa kwa kupata wakati wa kujengwa upya jinsi hiyo baada ya ule uhamisho wa Kibabiloni. “Yerusalemu la juu” limebarikiwa hata zaidi.a Hasa tangu mwaka wa 1919, “wazao” wake watiwa-mafuta wamechanuka katika hali yao ya kiroho iliyorudishwa. (Isaya 61:4; 66:8) ‘Waliwamiliki mataifa’ katika maana ya kwamba walienea wakaingia nchi nyingi kuwatafuta wale ambao wangetaka kujiunga na familia yao ya kiroho. Matokeo ni kwamba, ukuzi mkubwa ulivuvumka kwa kukusanya wale wana watiwa-mafuta. Idadi yao ya mwisho ya 144,000 ilionekana kuwa imejazwa wakati fulani katikati ya ile miaka ya 1930. (Ufunuo 14:3) Wakati huo, kukusanywa kwa watiwa-mafuta kuliacha kuwa lengo kuu la kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, mpanuko haukukoma eti kwa sababu mkusanyo wa watiwa-mafuta ulikoma.

      12. Ni nani zaidi ya watiwa-mafuta ambao wamekusanywa wakaingizwa katika kutaniko la Kikristo tangu miaka ya 1930?

      12 Yesu mwenyewe alitabiri kwamba licha ya yeye kuwa na “kundi dogo” la ndugu watiwa-mafuta, angekuwa pia na “kondoo wengine” ambao ni lazima waletwe ndani ya zizi la kondoo la Wakristo wa kweli. (Luka 12:32; Yohana 10:16) Ingawa waandamani hao waaminifu wa watiwa-mafuta hawamo miongoni mwa wana watiwa-mafuta wa “Yerusalemu la juu,” wanatimiza sehemu muhimu iliyotajwa na unabii zamani. (Zekaria 8:23) Kuanzia miaka ya 1930 hadi leo, “umati mkubwa” wa waandamani hao umekusanywa, matokeo yakawa ni mpanuko usio na kifani wa kutaniko la Kikristo. (Ufunuo 7:9, 10) Leo huo umati mkubwa una mamilioni ya watu. Mpanuko wote huo umetokeza uharaka wa kuongeza Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na ofisi za tawi. Maneno ya Isaya yanaonekana yamezidi kufaa sana. Ni pendeleo kama nini kuwa sehemu ya mpanuko huo uliotabiriwa!

      Mama Anayewajali Wazao Wake

      13, 14. (a) Inaonekana ni kama kuna ugumu gani wa kuelewa baadhi ya semi zinazoelekezwa kwa “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu? (b) Ni ufahamu gani wa kina kirefu tunaoweza kupata kutokana na jinsi Mungu anavyotumia mifano ya uhusiano wa kifamilia?

      13 Tumeona kwamba katika utimizo mkubwa zaidi, yule “mwanamke” wa unabii anawakilisha tengenezo la Yehova la kimbingu. Lakini baada ya kusoma Isaya 54:4, huenda tukashangaa ni jinsi gani tengenezo hilo la viumbe-roho limewahi kupata aibu au suto. Mistari inayofuata inasema kwamba “mwanamke” wa Mungu atakataliwa, ateswe, na kushambuliwa. Hata ataichochea ghadhabu ya Mungu. Maneno kama hayo yanawezaje kutumiwa kuhusu tengenezo la viumbe-roho walio wakamilifu ambao hawajawahi kamwe kutenda dhambi? Jibu linahusiana na hali ya familia.

      14 Yehova anatumia uhusiano wa kifamilia—mume na mke, mama na watoto—kupasha watu kweli za kiroho zenye kina kirefu kwa sababu mifano hiyo ina maana sana kwa wanadamu. Iwe tumeona mengi au machache, mema au mabaya katika familia yetu wenyewe, inaelekea kwamba kwa kiasi fulani tunafahamu jinsi ndoa nzuri au uhusiano mzuri unavyopaswa kuwa kati ya mzazi na mtoto. Basi Yehova anatufundisha waziwazi kama nini kwamba yeye ana uhusiano mchangamfu, wa kindani na wa kuaminiana sana na halaiki kubwa za watumishi wake! Tena anatufundisha kwa njia yenye kuvutia kama nini kwamba tengenezo lake la kimbingu linawajali wazao wake watiwa-mafuta walio duniani! Wakati watumishi wa kibinadamu wanapoteseka, hata watumishi waaminifu wa kimbingu, yaani “Yerusalemu la juu,” wanateseka. Vivyo hivyo, Yesu alisema hivi: “Kwa kadiri ambayo mlimfanyia hilo mmoja wa wadogo zaidi sana wa ndugu zangu hawa [watiwa-mafuta], mlinifanyia mimi hilo.”—Mathayo 25:40.

      15, 16. Utimizo wa kwanza wa Isaya 54:5, 6 ni gani, na utimizo wake ulio mkubwa zaidi ni gani?

      15 Basi, haishangazi kwamba mengi ya maneno anayoambiwa “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova yanaonyesha mambo ambayo huwapata watoto wake duniani. Yafikirie maneno haya: “Muumba wako ni mume wako; BWANA wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote. Maana BWANA amekuita kama mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni, kama mke wakati wa ujana, atupwapo, asema Mungu wako.”—Isaya 54:5, 6.

      16 Mke anayezungumziwa hapa ni nani? Katika utimizo wa kwanza ni Yerusalemu, akiwakilisha watu wa Mungu. Wakati wa uhamisho wao wa miaka 70 katika Babiloni, watahisi kana kwamba Yehova amewakataa na kuwaacha kabisa. Katika utimizo ulio mkubwa zaidi, maneno hayo yanarejezea “Yerusalemu la juu” na tukio lake la kutokeza ile “mbegu” hatimaye kwa kutimiza Mwanzo 3:15, NW.

      Nidhamu ya Muda, Baraka za Milele

      17. (a) Yerusalemu la kidunia litapatwaje na “furiko” la ghadhabu ya kimungu? (b) Ni ‘furiko’ gani lililowapata wana wa “Yerusalemu la juu”?

      17 Unabii unaendelea kusema hivi: “Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya. Kwa ghadhabu ifurikayo nalikuficha uso wangu dakika moja; lakini kwa fadhili za milele nitakurehemu, asema BWANA, Mkombozi wako.” (Isaya 54:7, 8) Yerusalemu la kidunia linagharikishwa kwa ‘furiko’ la ghadhabu ya Mungu wakati majeshi ya Babiloni yatakapofanya shambulio mwaka wa 607 K.W.K. Huenda miaka yake 70 ya kukaa uhamishoni ikaonekana kuwa muda mrefu. Hata hivyo, majaribu hayo yanaendelea kwa “dakika moja” yakilinganishwa na baraka za milele zinazowangoja wenye kuitikia vema nidhamu wanayopewa. Hivyo hivyo, wana watiwa-mafuta wa “Yerusalemu la juu” walihisi kana kwamba walikuwa wamezidiwa na furiko la hasira kali ya kimungu, wakati Yehova alipowaruhusu washambuliwe na wanasiasa kwa kuchochewa na Babiloni Mkubwa. Lakini, kwa kutofautishwa na kipindi cha baraka za kiroho kilichofuata tangu mwaka wa 1919, baadaye nidhamu hiyo ilionekana kuwa ya muda mfupi kama nini!

      18. Ni kanuni gani muhimu inayoweza kutambuliwa kuhusu hasira kali ya Yehova juu ya watu wake, na hiyo ingeweza kuwa na matokeo gani kwetu binafsi?

      18 Mistari hii inaonyesha ukweli mwingine mkubwa—hasira kali ya Mungu inapita mbio, lakini rehema yake inadumu milele. Hasira yake huwaka juu ya ukosaji, lakini hudhibitiwa nyakati zote, huwa na kusudi fulani nyakati zote. Nasi tukiikubali nidhamu ya Yehova, hasira yake inakuwa ya “dakika moja,” kisha inapoa. Badala ya hasira hiyo kunakuwako “rehema nyingi”—msamaha wake na fadhili zake za upendo. Fadhili hizo zinadumu ‘milele.’ Basi, tunapotenda dhambi hatupaswi kusita-sita kutubu kisha kujaribu kurekebisha makosa tuliyomtenda Mungu. Ikiwa dhambi ni nzito, tunapaswa kuwafikia wazee wa kutaniko bila kukawia. (Yakobo 5:14) Ni kweli kwamba huenda nidhamu ikahitajika, na inaweza kuwa vigumu kuikubali. (Waebrania 12:11) Lakini itakuwa ya muda mfupi ikilinganishwa na baraka za milele zinazotiririka kwa kupokea msamaha wa Yehova Mungu!

      19, 20. (a) Agano la upinde wa mvua ni nini, na linawahusuje wahamishwa walioko Babiloni? (b) ‘Agano la amani’ huwapa Wakristo watiwa-mafuta uhakikisho gani leo?

      19 Sasa Yehova anawatolea watu wake uhakikisho wenye faraja: “Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa: wakati ule niliapa kwamba sitaifunika tena ardhi kwa gharika. Basi sasa naapa kwamba sitakukasirikia tena wala sitakukemea tena. Milima yaweza kutoweka, vilima vyaweza kuondolewa, lakini fadhili zangu hazitakuondoka, agano langu la amani halitaondolewa. Mimi Mwenyezi-Mungu nikuhurumiaye nimesema.” (Isaya 54:9, 10, “BHN”) Baada ya Gharika, Mungu alifanya agano—ambalo nyakati nyingine huitwa agano la upinde wa mvua—pamoja na Noa na kila nafsi nyingine iliyo hai. Yehova aliahidi kutoleta uharibifu tena juu ya dunia kwa kutumia furiko la duniani pote. (Mwanzo 9:8-17) Hiyo inamaanisha nini kwa Isaya na watu wake?

      20 Inafariji kujua kwamba adhabu ambayo ni lazima iwapate—ule uhamisho wa miaka 70 katika Babiloni—itatukia mara moja tu. Ikimalizika, haitatukia tena. Baada ya hapo, ‘agano la Mungu la amani’ litaanza kutumika. Neno la Kiebrania la “amani” halimaanishi kutokuwako kwa vita tu bali pia “hali njema ya kila aina.” Kwa upande wa Mungu, agano hilo ni la kudumu. Vilima na milima inaweza kutoweka kwa urahisi kuliko fadhili za upendo wa Mungu kuelekea watu wake waaminifu. Lakini inasikitisha kwamba hatimaye taifa lake la kidunia litashindwa kutimiza upande wao wa agano hilo, livunje-vunje amani yake lenyewe kwa kumkataa Mesiya. Hata hivyo, wana wa “Yerusalemu la juu” walifanya vema zaidi. Kipindi chao kigumu cha nidhamu kilipomalizika, walikuwa na uhakikisho wa kulindwa na Mungu.

      Usalama wa Kiroho wa Watu wa Mungu

      21, 22. (a) Kwa nini “Yerusalemu la juu” linasemwa kwamba linateswa na kurushwa na tufani? (b) Hali yenye baraka ya “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu ingemaanisha nini kuhusu “wazao” wake duniani?

      21 Yehova anaendelea kutabiri kwamba watu wake waaminifu watapata usalama: “Ewe uliyeteswa, uliyerushwa na tufani, usiyetulizwa, tazama, nitaweka mawe yako kwa rangi nzuri [“chokaa ngumu,” “NW”], nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi. Nami nitaifanya minara yako ya akiki nyekundu, na malango yako ya almasi, na mipaka yako yote ya mawe yapendezayo. Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi. Utathibitika katika haki; utakuwa mbali na kuonewa, kwa maana hutaogopa; na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia. Tazama, yamkini watakusanyana; lakini si kwa shauri langu. Watu wo wote watakaokusanyana juu yako wataanguka kwa ajili yako.”—Isaya 54:11-15.

      22 Ni wazi kuwa “mwanamke” wa Yehova katika makao ya roho hajawahi kuteswa moja kwa moja wala kurushwa-rushwa na tufani. Lakini aliteseka wakati “wazao” wake watiwa-mafuta duniani walipoteseka, hasa walipokuwa katika utekwa wa kiroho katika kile kipindi cha mwaka wa 1918 mpaka mwaka wa 1919. Hata hivyo, wakati yule “mwanamke” wa kimbingu anapokwezwa, hiyo inaonyesha kwamba wazao wake pia wanakwezwa. Basi, yafikirie maelezo ya kuvutia sana yanayotolewa kuhusu “Yerusalemu la juu.” Wazo linalotokezwa na mawe yake ya thamani juu ya malango, “chokaa ngumu” ya bei ghali, misingi yake, na hata mipaka yake ni kwamba yeye ana “uzuri, fahari, utakato, nguvu, na uimara,” kama vile kichapo kimoja cha marejezo kinavyosema. Ni nini kingewafanya Wakristo watiwa-mafuta wawe na hali ya usalama na baraka jinsi hiyo?

      23. (a) ‘Kufundishwa na Yehova’ kumekuwa na matokeo gani juu ya Wakristo watiwa-mafuta katika siku za mwisho? (b) Watu wa Mungu wamebarikiwa kwa ‘mipaka ya mawe yapendezayo’ katika maana gani?

      23 Mstari wa 13 wa Isaya sura ya 54 unaandaa jibu—wote ‘watafundishwa na Yehova.’ Yesu mwenyewe aliyatumia maneno ya mstari huo kuhusu wafuasi wake watiwa-mafuta. (Yohana 6:45) Nabii Danieli alitabiri kwamba katika huu “wakati wa mwisho,” watiwa-mafuta wangebarikiwa kwa ujuzi mwingi wa kweli na ufahamu wa kiroho wenye kina kirefu. (Danieli 12:3, 4) Ufahamu huo wenye kina kirefu umewawezesha wawe katika mstari wa mbele kuongoza kazi ya uelimishaji iliyo kubwa kupita zote katika historia, wakieneza ufundishaji wa kimungu katika dunia yote. (Mathayo 24:14) Wakati huo huo, ufahamu huo wenye kina kirefu umewasaidia waone tofauti kati ya dini ya kweli na ya uwongo. Isaya 54:12 inataja ‘mipaka ya mawe yapendezayo.’ Tangu mwaka wa 1919, Yehova amewapa watiwa-mafuta ufahamu unaozidi kuwa wazi daima juu ya mipaka—mistari ya kiroho isiyopasa kurukwa—akiwaweka kando wawe tofauti na dini ya uwongo na mambo ya ulimwengu yasiyo ya kimungu. (Ezekieli 44:23; Yohana 17:14; Yakobo 1:27) Kwa njia hiyo wanawekwa kando wawe watu wa Mungu mwenyewe.—1 Petro 2:9.

      24. Tunaweza kuhakikishaje kwamba tunafundishwa na Yehova?

      24 Hivyo, inafaa kila mmoja wetu ajiulize, ‘Je, mimi ninafundishwa na Yehova?’ Hatupokei ufundishaji huo kwa kuketi tu. Ni lazima tutie bidii. Tukilisoma Neno la Mungu kwa ukawaida na kulitafakari, na tukitwaa maagizo kwa kusoma vichapo vyenye msingi wa Biblia vinavyochapishwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” na kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya Kikristo na kuihudhuria, kweli tutafundishwa na Yehova. (Mathayo 24:45-47) Tukijitahidi kutumia yale tunayojifunza na kubaki tukiwa macho na wenye kulinda kiroho, ufundishaji wa kimungu utatutofautisha na wale walio katika ulimwengu huu usiomhofu Mungu. (1 Petro 5:8, 9) Isitoshe, ufundishaji huo utatusaidia ‘kumkaribia Mungu.’—Yakobo 1:22-25; 4:8.

      25. Ahadi ya Mungu ya amani inamaanisha nini kwa watu wake nyakati za kisasa?

      25 Pia unabii wa Isaya unaonyesha kwamba watiwa-mafuta wanabarikiwa kwa amani nyingi. Je, hiyo inamaanisha kwamba hawashambuliwi kamwe? Haimaanishi hivyo, bali Mungu huwapa uhakikisho kwamba hataagiza mashambulio hayo yafanyike wala hatayaruhusu yafanikiwe. Tunasoma hivi: “Tazama, nimemwumba mhunzi avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu. Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.”—Isaya 54:16, 17.

      26. Kwa nini tunafarijika kujua kwamba Yehova ndiye Muumba wa wanadamu wote?

      26 Kwa mara ya pili katika sura hii ya Isaya, Yehova anawakumbusha watumishi wake kwamba yeye ndiye Muumba. Mapema kidogo, anamwambia mke wake wa mfano kwamba yeye ndiye ‘Muumba’ wake. Sasa anasema kwamba yeye ndiye Muumba wa wanadamu wote. Mstari wa 16 unaeleza juu ya mhunzi anayepulizia hewa kwenye makaa ya kuvipasha moto vyombo vyake vya uhunzi, huku akiunda silaha zake za uharibifu, na pia unaonyesha shujaa wa vita, aliye “mharibu ili aharibu.” Watu kama hao wanaweza kuwaogopesha wanadamu wenzao, lakini watawezaje kutumainia kumzidi nguvu Muumba wao mwenyewe? Kwa hiyo leo, hata kama majeshi yaliyo na nguvu zaidi ulimwenguni yatawashambulia watu wa Yehova, hayataweza kupata mafanikio kamili. Kwa nini hayataweza?

      27, 28. Tunaweza kuwa na uhakika wa jambo gani katika nyakati hizi zenye msukosuko, na ni kwa nini tunajua kwamba mashambulio ya Shetani juu yetu hayatafanikiwa?

      27 Wakati wa kufanya shambulio la uharibifu juu ya watu wa Mungu na ibada yao ya roho na kweli umekwisha. (Yohana 4:23, 24) Yehova alimruhusu Babiloni Mkubwa afanye shambulio moja lililofanikiwa kwa muda. Kwa muda mfupi, “Yerusalemu la juu” liliona wazao wake wakikaribia kunyamazishwa wakati kazi ya kuhubiri duniani ilipokaribia kukomeshwa kabisa. Hilo halitatukia tena ng’o! Sasa jiji hilo linawashangilia wana wake, kwani hawawezi kushindwa kiroho. (Yohana 16:33; 1 Yohana 5:4) Ni kweli kwamba silaha za ushambulizi zimeundwa kuwapinga, na bado zitaundwa. (Ufunuo 12:17) Lakini silaha hizo hazijafaulu na hazitafaulu. Shetani hana silaha yoyote ya kuizima imani na bidii motomoto ya watiwa-mafuta na waandamani wao. Amani hii ya kiroho ndio ‘urithi wa watumishi wa Yehova,’ kwa hiyo hakuna mtu anayeweza kuwapokonya amani hiyo.—Zaburi 118:6; Waroma 8:38, 39.

      28 Ndiyo, ulimwengu wa Shetani hauna kamwe kitu kitakachoweza kuikomesha kazi na ibada safi ya daima ambayo Mungu anapewa na watumishi wake waliojiweka wakfu. Wazao watiwa-mafuta wa “Yerusalemu la juu” wamefarijiwa sana na uhakikisho huo. Na umewafariji pia washiriki wa ule umati mkubwa. Tunapozidi kujua mengi juu ya tengenezo la Yehova la kimbingu na jinsi linavyoshughulika na waabudu wa Yehova duniani, imani yetu itazidi kuwa yenye nguvu. Maadamu imani yetu ina nguvu, silaha za Shetani zitakuwa za bure kabisa zinapotumiwa kupigana nasi!

      [Maelezo ya Chini]

      a Kulingana na Ufunuo 12:1-17, “mwanamke” wa Mungu alibarikiwa sana kwa kuzaa ‘mzao’ wa maana sana—si mwana-roho mmoja tu, bali ni Ufalme wa Kimesiya ulio mbinguni. Uzawa huo ulitukia mwaka wa 1914. (Ona Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, ukurasa wa 177-186.) Unabii wa Isaya unakaza fikira juu ya shangwe ambayo mwanamke huyo anahisi kwa sababu ya baraka ambayo Mungu anawapa wana wake watiwa-mafuta walio duniani.

      [Sanduku katika ukurasa wa 218, 219]

      Familia ya Abrahamu —Mfano wa Kiunabii

      Mtume Paulo alieleza kwamba familia ya Abrahamu inatumika kuwa drama ya mfano, mfano wa kiunabii unaoonyesha uhusiano wa Yehova pamoja na tengenezo lake la kimbingu na pamoja na taifa la kidunia la Israeli chini ya agano la Sheria ya Kimusa.—Wagalatia 4:22-31.

      Abrahamu, akiwa kichwa cha familia, anawakilisha Yehova Mungu. Hiari ya Abrahamu ya kumtoa Isaka mwanawe mpendwa awe dhabihu inatangulia kuwa kivuli cha hiari ya Yehova ya kumtoa Mwanawe mwenyewe aliye mpendwa sana awe dhabihu ya dhambi za wanadamu.—Mwanzo 22:1-13; Yohana 3:16.

      Sara anafananisha “mke” wa kimbingu wa Mungu, yaani tengenezo lake la viumbe-roho. Tengenezo hilo la kimbingu linaelezwa kwa kufaa kuwa mke wa Yehova, kwa sababu linashirikiana na Yehova kindani, linanyenyekea ukichwa wake, na linaonyesha ushirikiano kamili katika utimizaji wa makusudi yake. Mke huyo anaitwa pia “Yerusalemu la juu.” (Wagalatia 4:26) “Mwanamke” huyo huyo anatajwa kwenye Mwanzo 3:15, na ameonyeshwa katika njozi kwenye Ufunuo 12:1-6, 13-17.

      Isaka ni ufananisho wa Mbegu ya kiroho ya mwanamke wa Mungu. Kwa msingi, mbegu hiyo ni Yesu Kristo. Hata hivyo, ilikuja pia kuhusisha ndugu watiwa-mafuta wa Kristo, wanaofanywa kuwa wana wa kiroho na kuwa warithi-washirika pamoja na Kristo.—Waroma 8:15-17; Wagalatia 3:16, 29.

      Hagari, mke wa pili, au suria, wa Abrahamu alikuwa mtumwa. Kwa kufaa anafananisha Yerusalemu la kidunia, ambapo mfumo wa Sheria ya Kimusa ulitawala, ukiwafunua wote wanaoifuata kuwa watumwa wa dhambi na kifo. Paulo alisema kwamba ‘Hagari anamaanisha Sinai, mlima ulio Arabuni,’ kwa sababu agano la Sheria lilianzishwa huko.—Wagalatia 3:10, 13; 4:25.

      Ishmaeli, mwana wa Hagari, anafananisha Wayahudi wa karne ya kwanza, wale wana wa Yerusalemu ambao walikuwa wangali watumwa wa Sheria ya Kimusa. Kama vile Ishmaeli alivyomnyanyasa Isaka, ndivyo Wayahudi hao walivyowanyanyasa Wakristo, waliokuwa wana watiwa-mafuta wa Sara wa mfano, yaani “Yerusalemu la juu.” Na sawa na vile Abrahamu alivyowafukuza Hagari na Ishmaeli, hatimaye Yehova alitupa Yerusalemu na wana wake waasi.—Mathayo 23:37, 38.

      [Picha katika ukurasa wa 220]

      Baada ya ubatizo wake, Yesu alitiwa mafuta kwa roho takatifu, na andiko la Isaya 54:1 likaanza kupata utimizo wake ulio wa maana zaidi

      [Picha katika ukurasa wa 225]

      Yehova aliuficha uso wake kwa “dakika moja” ili usionwe na Yerusalemu

      [Picha katika ukurasa wa 231]

      Je, shujaa wa vita na mhunzi wanaweza kumzidi nguvu Muumba wao?

  • Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Sita

      Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo

      Isaya 55:1-13

      1. Eleza jinsi hali ya wahamishwa Wayahudi ilivyokuwa huko Babiloni.

      GIZA la huzuni lilikuwa limeingia katika historia ya Yuda. Watu wa agano la Mungu walikuwa wameng’olewa katika nchi yao na sasa walikuwa wakiteseka utekwani Babiloni. Ni kweli kwamba walipewa uhuru wa kiasi fulani ili kuendeleza shughuli zao za kila siku. (Yeremia 29:4-7) Wengine walijifunza ufundi wa mambo mbalimbali na wengine wakafanya biashara.a (Nehemia 3:8, 31, 32) Hata hivyo, maisha ya mateka Wayahudi hayakuwa rahisi. Walikuwa utumwani kimwili na kiroho. Acheni tuone ilikuwaje.

      2, 3. Uhamisho ulikuwa na matokeo gani juu ya ibada ambayo Wayahudi walimtolea Yehova?

      2 Wakati majeshi ya Babiloni yalipoangamiza Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., yaliipiga ibada ya kweli pigo kali, licha ya kufanya taifa hilo ukiwa. Yalisomba vyombo vyote vya hekalu la Yehova na kuliangamiza, yakauharibu kabisa mpangilio wa ukuhani kwa kuteka baadhi ya watu wa kabila la Lawi na kuua wengine. Bila nyumba ya ibada, bila madhabahu, na bila mpangilio mzuri wa ukuhani, haikuwezekana Wayahudi wamtolee Mungu wa kweli dhabihu kwa njia iliyoagizwa na Sheria.

      3 Bado Wayahudi waaminifu wangeweza kudumisha utambulisho wao wa kidini kwa kufuata tohara na kufuata Sheria kwa kadiri ilivyowezekana. Kwa mfano, wangeweza kuepuka vyakula vilivyokatazwa na pia kuishika Sabato. Lakini kwa kufanya hivyo, wangeweza kudhihakiwa na watekaji wao kwa maana Wababiloni waliziona desturi za kidini za Wayahudi kuwa upumbavu. Kuonyesha kwamba wahamishwa hao walishuka moyo, maneno ya mtunga-zaburi yanasema hivi: “Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, tukalia tulipoikumbuka Sayuni. Katika miti iliyo katikati yake tulivitundika vinubi vyetu. Maana huko waliotuchukua mateka walitaka tuwaimbie; na waliotuonea walitaka furaha; tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.”—Zaburi 137:1-3.

      4. Kwa nini ingekuwa kazi bure ikiwa Wayahudi wangetegemea mataifa mengine ili kupata ukombozi, lakini wangeweza kugeukia nani awasaidie?

      4 Basi, mateka Wayahudi wangeweza kupata faraja kwa kugeukia nani? Wokovu wao ungetoka wapi? Ni wazi haungetoka kwa mataifa yaliyowazunguka! Mataifa hayo yote yalikuwa hoi mbele ya majeshi ya Babiloni, na mengi yaliwachukia Wayahudi. Hata hivyo kulikuwa na tumaini. Yehova, ambaye walikuwa wamemwasi wakiwa watu huru, aliwakaribisha kwa uchangamfu ingawa walikuwa uhamishoni.

      “Njoni Majini”

      5. Maneno “njoni majini” yana maana gani?

      5 Yehova anamtumia Isaya kutoa unabii ili kuwaambia hivi mateka Wayahudi walioko Babiloni: “Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; naam, njoni, nunueni divai na maziwa, bila fedha na bila thamani.” (Isaya 55:1) Maneno hayo yana semi nyingi za ufananisho. Kwa mfano, fikiria mwaliko huu: “Njoni majini.” Bila maji, haiwezekani kuwa hai. Sisi wanadamu tukikosa maji, tunaweza kuishi juma moja hivi tu. Hivyo, inafaa kwamba Yehova anatumia maji kama mfano ili kuonyesha maneno yake yatakuwa na matokeo gani juu ya mateka Wayahudi. Ujumbe wake utawaburudisha, kama kinywaji baridi wakati wa joto kali la mchana. Utawafanya waache kushuka moyo na kuzima kiu yao ya kutamani ukweli na uadilifu. Tena utawajaza tumaini la kuja kuwekwa huru kutoka utekwani. Hata hivyo, ili hao wahamishwa Wayahudi wapate faida, ni lazima wanywe ujumbe wa Mungu kama maji, wausikilize, na kutenda vile unavyosema.

      6. Wayahudi watapataje faida wakinunua “divai na maziwa”?

      6 Vilevile, Yehova anawatolea “divai na maziwa.” Maziwa hufanya watoto wapate nguvu na kukua. Vivyo hivyo, maneno ya Yehova yatawatia watu wake nguvu za kiroho na kuwawezesha kuimarisha uhusiano wao naye. Namna gani divai? Mara nyingi divai hutumiwa nyakati za sherehe. Katika Biblia, inahusianishwa na ufanisi na shangwe. (Zaburi 104:15) Kwa kuwaambia watu wake ‘wanunue divai,’ Yehova anawapa uhakikisho kwamba ‘watafurahi kabisa,’ wakiirudia ibada ya kweli kwa moyo wote.—Kumbukumbu la Torati 16:15; Zaburi 19:8; Mithali 10:22.

      7. Kwa nini huruma ya Yehova kuwaelekea wahamishwa inastahili kusifiwa, nayo inatufundisha nini juu yake?

      7 Lo, Yehova ni mwenye rehema kama nini kwa kuwatolea Wayahudi wahamishwa burudiko hilo la kiroho! Huruma yake inastahili kusifiwa hata zaidi tunapokumbuka kwamba Wayahudi wamekuwa wapotovu na waasi. Si kwamba wanastahili kibali cha Yehova, hapana. Hata hivyo, mtunga-zaburi Daudi aliandika hivi karne nyingi mapema: “BWANA amejaa huruma na neema, haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili. Yeye hatateta sikuzote, wala hatashika hasira yake milele.” (Zaburi 103:8, 9) Yehova havunji kamwe uhusiano na watu wake, bali ndiye anayechukua hatua ya kwanza ya upatanisho. Kwa kweli, yeye ni Mungu ambaye “hufurahia rehema.”—Mika 7:18.

      Tumaini Lisilofaa

      8. Wayahudi wengi wameweka tumaini lao wapi, ijapokuwa wamepewa onyo gani?

      8 Kufikia sasa, Wayahudi wengi hawajamtumainia Yehova kabisa ili wapate wokovu. Kwa mfano, kabla ya Yerusalemu kuanguka, watawala wake walitegemea mataifa yenye nguvu yawaunge mkono, wakawa ni kama wanafanya ukahaba na Misri na Babiloni. (Ezekieli 16:26-29; 23:14) Yeremia alikuwa na sababu nzuri ya kuwaonya hivi: “Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake na moyoni mwake amemwacha BWANA.” (Yeremia 17:5) Lakini watu wa Mungu walifanya vivyo hivyo!

      9. Huenda ikawa Wayahudi wengi ‘wanatoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula’ jinsi gani?

      9 Sasa wamekuwa watumwa wa mojawapo la mataifa waliyokuwa wameyatumainia. Je, wamepata somo? Huenda ikawa wengi hawajapata, kwa maana Yehova anauliza hivi: “Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha?” (Isaya 55:2a) Ikiwa Wayahudi mateka wanatumainia mtu mwingine yeyote tofauti na Yehova, ‘wanatoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula.’ Hakika hawatafunguliwa watoke Babiloni kwa sababu desturi ya huko hairuhusu mateka warudi nyumbani kwao. Kwa kweli, Babiloni haiwezi kamwe kuwafaidi Wayahudi wahamishwa kupitia utawala wake wa mabavu, biashara, na ibada ya uongo.

      10. (a) Ikiwa Wayahudi wahamishwa watamsikiliza Yehova, yeye atawathawabishaje? (b) Ni agano gani ambalo Yehova alikuwa amefanya pamoja na Daudi?

      10 Yehova anawasihi sana watu wake hivi: “Nisikilizeni mimi kwa makini, nanyi mtakula vilivyo bora, na kufurahia vinono. ‘Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu; nisikilizeni, ili mpate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawapeni fadhili nilizomwaminisha Daudi.’” (Isaya 55:2b, 3, “BHN”) Tumaini pekee kwa watu hawa wasiolishwa vizuri kiroho ni Yehova, ambaye sasa anamtumia Isaya kuongea nao kupitia unabii. Uhai wao wenyewe unategemea kusikiliza ujumbe wa Mungu, kwani anasema kwamba wakifanya hivyo, ‘wataishi.’ Ingawa hivyo, “agano la milele” ambalo Yehova atafanya na wale wanaomtii ni nini? Agano hilo linahusu “fadhili” za upendo alizomtendea Daudi. Karne kadhaa mapema, Yehova alimwahidi Daudi kwamba kiti chake cha ufalme ‘kingethibitishwa milele.’ (2 Samweli 7:16) Kwa hiyo, “agano la milele” linalotajwa hapa linahusu utawala.

      Mrithi wa Kudumu wa Ufalme wa Milele

      11. Kwa nini huenda wahamishwa walioko Babiloni wakaona kwamba ile ahadi ambayo Mungu alimpa Daudi ni kama dhana tupu?

      11 Ni kweli kwamba huenda hao wahamishwa Wayahudi wakaona ni vigumu sana utawala upite katika ukoo wa Daudi. Ala, si wamepoteza nchi yao na hata wakaacha kuwa taifa! Lakini ni kwa muda tu. Yehova hajasahau agano lake na Daudi. Kusudi la Mungu kuhusu Ufalme wa milele katika ukoo wa Daudi litafanikiwa, hata kama linaonekana kuwa jambo gumu sana machoni pa wanadamu. Lakini vipi na lini? Mwaka wa 537 K.W.K., Yehova anawafungua watu wake kutoka utekwani Babiloni na kuwarudisha kwenye nchi yao. Je, hiyo inafanya ufalme wa kudumu milele uanzishwe? Sivyo, bali wanaendelea kutiishwa chini ya milki nyingine ya kipagani, Umedi-Uajemi. “Nyakati zilizowekwa rasmi” ili mataifa yatawale hazijakwisha bado. (Luka 21:24) Kwa kuwa hakuna mfalme katika Israeli, ahadi ambayo Yehova alimtolea Daudi itakaa bila kutimizwa muda wa karne kadhaa zinazokuja.

      12. Yehova alichukua hatua gani kuelekea kutimiza agano la Ufalme alilofanya na Daudi?

      12 Zaidi ya miaka 500 baada ya Israeli kuachiliwa kutoka utekwani Babiloni, Yehova alichukua hatua kubwa kuelekea kulitimiza agano la Ufalme. Alifanya hivyo alipohamisha uhai wa Mwana wake mzaliwa wa kwanza, ambaye ndiye mwanzo wa uumbaji wake, akautoa katika utukufu wa kimbingu, akauingiza katika tumbo la uzazi la Maria, bikira Myahudi. (Wakolosai 1:15-17) Akitangaza tukio hilo, malaika wa Yehova alimwambia Maria hivi: “Huyu atakuwa mkubwa na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi Sana; na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na hakutakuwa na mwisho wa ufalme wake.” (Luka 1:32, 33) Kwa hiyo Yesu alizaliwa katika ukoo wa kifalme wa Daudi, akarithi haki ya kuwa mfalme. Akiisha kutawazwa kuwa mfalme, Yesu angetawala “hata milele.” (Isaya 9:7; Danieli 7:14) Hivyo, sasa ikawa inawezekana kutimiza ahadi ya Yehova iliyosemwa karne nyingi zilizotangulia kwamba angempa Mfalme Daudi mrithi wa kudumu.

      “Jemadari kwa Kabila za Watu”

      13. Yesu alikuwaje “shahidi kwa kabila za watu” wakati wa huduma yake na pia baada ya kupaa kwake?

      13 Mfalme huyu wa wakati ujao atafanya nini? Yehova anasema hivi: “Angalieni, nimemweka kuwa shahidi kwa kabila za watu; kuwa kiongozi na jemadari kwa kabila za watu.” (Isaya 55:4) Yesu alipokuwa mtu mzima, alikuwa mwakilishi wa Yehova duniani, shahidi wa Mungu kwa mataifa. Wakati wa maisha yake ya kibinadamu, huduma yake ilielekezwa kwa “kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” Lakini, muda mfupi kabla Yesu hajapaa mbinguni, aliwaambia wafuasi wake hivi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote . . . Tazameni! mimi nipo pamoja nanyi siku zote hadi umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 10:5, 6; 15:24; 28:19, 20) Hivyo, baada ya muda, ujumbe wa Ufalme ulipelekwa kwa watu wasio Wayahudi, na wengine wao walishiriki katika utimizo wa agano lililofanywa pamoja na Daudi. (Matendo 13:46) Kwa njia hiyo, hata baada ya Yesu kufa, kufufuliwa, na kupaa mbinguni, aliendelea kuwa ‘shahidi wa Yehova kwa kabila za watu.’

      14, 15. (a) Yesu alijithibitisha jinsi gani kwamba yeye ni “kiongozi na jemadari”? (b) Wafuasi wa Yesu wa karne ya kwanza walikuwa na tazamio gani?

      14 Pia Yesu alipaswa kuwa “kiongozi na jemadari.” Kulingana na maelezo hayo ya kiunabii, Yesu alikubali kabisa madaraka ya ukichwa wake alipokuwa duniani, akawapa watu mwongozo kwa kuwawekea mfano ufaao katika kila jambo. Alivutia vikundi vikubwa vya watu, akawafundisha maneno ya kweli, na kuwaonyesha faida zinazowajia wale wanaofuata uongozi wake. (Mathayo 4:24; 7:28, 29; 11:5) Aliwazoeza wanafunzi wake kwa njia yenye mafaa, akawatayarisha kufanya kazi kubwa ya kuhubiri iliyokuwa mbele yao. (Luka 10:1-12; Matendo 1:8; Wakolosai 1:23) Katika muda wa miaka mitatu na nusu tu, Yesu aliweka msingi wa kutaniko la kimataifa lenye umoja, lenye maelfu ya washirika waliotolewa kutoka makabila mengi! Ni “kiongozi na jemadari” wa kweli peke yake ambaye angaliweza kutimiza kazi kubwa hivyo.b

      15 Wale waliokusanywa kwenye kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza walitiwa mafuta kwa roho takatifu ya Mungu, na walikuwa na tazamio la kuwa watawala-washirika pamoja na Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu. (Ufunuo 14:1) Hata hivyo, unabii wa Isaya unahusu hata nyakati za baada ya Ukristo wa mapema. Ushuhuda unaonyesha kwamba Yesu Kristo alianza kutawala akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu mwaka wa 1914, si kabla ya hapo. Muda mfupi baada ya mwaka huo, hali fulani yenye ulinganifu mwingi na ile ya Wayahudi wahamishwa katika karne ya sita K.W.K. ilisitawi miongoni mwa Wakristo watiwa-mafuta duniani. Kwa kweli, yaliyowapata Wakristo hao yanatimiza unabii wa Isaya kwa kadiri kubwa zaidi.

      Kutekwa na Kufunguliwa Wakati wa Kisasa

      16. Baada ya Yesu kutawazwa mwaka wa 1914, kulitokea msononeko gani?

      16 Yesu alipotawazwa kuwa Mfalme mwaka wa 1914, ulimwengu ulipatwa na msononeko usio na kifani. Kwa nini? Kwa sababu, Yesu alipokwisha kuwa Mfalme, aliwafukuza Shetani na viumbe-roho wengine walio waovu kule mbinguni. Baada ya kuzuiliwa duniani, Shetani alianza kuwapiga vita watakatifu waliosalia, wale mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta. (Ufunuo 12:7-12, 17) Kilele cha vita hiyo kilifika mwaka wa 1918, wakati kazi ya kuhubiri peupe ilipokuwa ni kama imekoma, na maofisa wenye madaraka wa Watch Tower Society wakatiwa gerezani kwa mashtaka bandia ya kufanya uchochezi wa kuipinga serikali. Kwa njia hiyo, watumishi wa kisasa wa Yehova waliingia katika utekwa wa kiroho, hicho kikawa kikumbusha cha utekwa halisi wa Wayahudi wa kale. Walishushiwa sana heshima.

      17. Hali ya watiwa-mafuta iligeuzwaje mwaka wa 1919, nao waliimarishwaje wakati huo?

      17 Lakini, utekwa wa watumishi watiwa-mafuta wa Mungu haukuendelea kwa muda mrefu. Siku ya Machi 26, 1919, wale maofisa waliotiwa gerezani walifunguliwa, na baadaye mashtaka yote waliyofanyiwa yakaondolewa. Yehova alimimina roho takatifu juu ya watu wake waliokombolewa, akawatia nguvu kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele. Walipoalikwa ‘kuchukua maji ya uhai bure,’ waliitikia kwa shangwe. (Ufunuo 22:17) Walinunua “divai na maziwa, bila fedha na bila thamani,” wakaimarishwa kiroho kwa ajili ya mpanuko wa ajabu uliokuwa mbele yao, mpanuko ambao mabaki watiwa-mafuta hawakuwa wametazamia.

      Umati Mkubwa Wawakimbilia Watiwa-Mafuta wa Mungu

      18. Kati ya wanafunzi wa Yesu Kristo kuna vikundi vingapi viwili, na leo vinajumlika kuwa nini?

      18 Wanafunzi wa Yesu huwa na mojawapo la matumaini mawili. Kwanza, “kundi dogo” ambalo idadi yake ni watu 144,000 limekusanywa, nao ni Wakristo watiwa-mafuta waliokuwa na malezi ya Kiyahudi na yasiyo ya Kiyahudi. Hao ndio “Israeli wa Mungu” walio na tumaini la kutawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu. (Luka 12:32; Wagalatia 6:16; Ufunuo 14:1) Pili, katika siku za mwisho, “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wamejitokeza waziwazi. Wana tumaini la kuishi milele katika dunia-paradiso. Kabla ya dhiki kubwa kutokea ghafula, umati huo—ambao idadi yao haikuamuliwa kimbele—wanatumikia pamoja na kundi dogo, kisha vikundi vyote viwili vinajumlika kuwa “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.”—Ufunuo 7:9, 10; Yohana 10:16.

      19. “Taifa” fulani ambalo hapo kwanza halikujulikana na Israeli wa Mungu limeitikiaje mwito wa taifa hilo la kiroho?

      19 Maneno yafuatayo ya unabii wa Isaya yanaonyesha kwamba huo umati mkubwa ungekusanywa: “Tazama, utaita taifa usilolijua, na taifa lisilokujua wewe litakukimbilia, kwa sababu ya BWANA, Mungu wako, na kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli; maana amekutukuza [“atakuwa amekurembesha,” “NW”].” (Isaya 55:5) Katika ile miaka iliyofuata kufunguliwa kwao kutoka katika utekwa wa kiroho, pale mwanzoni-mwanzoni mabaki watiwa-mafuta hawakuelewa kwamba kabla ya Har-Magedoni wangetumiwa kuita “taifa” kubwa lije kwenye ibada ya Yehova. Lakini, wakati ulipozidi kupita, wengi wenye moyo wa haki lakini wasio na tumaini la kimbingu walianza kushirikiana na watiwa-mafuta na kumtumikia Yehova kwa bidii ile ile kama ya watiwa-mafuta. Wageni hawa waliuona urembo ambao watu wa Mungu walipewa, wakatambua kwamba Yehova alikuwa miongoni mwao. (Zekaria 8:23) Katika miaka ya 1930, watiwa-mafuta walielewa utambulisho halisi wa kikundi hicho kilichoendelea kuongezeka miongoni mwao. Walitambua kwamba kazi kubwa ya ukusanyaji ilikuwa ingali mbele. Umati mkubwa ulikuwa ukifanya haraka kushirikiana na watu wa agano la Mungu, na walikuwa na sababu nzuri ya kufanya hivyo.

      20. (a)  Kwa nini ni muhimu ‘kumtafuta Yehova’ siku zetu, naye anatafutwaje? (b) Yehova atatendaje kuelekea wale wanaomtafuta?

      20 Siku za Isaya, mwito huu ulitokezwa: “Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu.” (Isaya 55:6) Siku zetu, maneno haya yanawafaa wale wanaojumlika kuwa Israeli wa Mungu na pia wale wa umati mkubwa unaoongezeka. Yehova hatoi baraka yake bila masharti, wala hawapi watu mwaliko wake milele. Huu ndio wakati wa kutafuta kibali cha Mungu. Wakati uliowekwa rasmi wa hukumu ya Yehova utakapofika, itakuwa kuchelewa mno. Basi, Isaya anasema hivi: “Mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie BWANA, naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.”—Isaya 55:7.

      21. Taifa la Israeli limekosaje uaminifu kuhusiana na tangazo la baba zao wa zamani?

      21 Maneno haya ‘na amrudie Yehova’ yanadokeza kwamba wale wanaohitaji kutubu walikuwa na uhusiano fulani na Mungu hapo kwanza. Usemi huo unatukumbusha kwamba mambo mengi ya sehemu hii ya unabii wa Isaya yanatumika kwanza kuwahusu mateka Wayahudi katika Babiloni. Karne kadhaa kabla ya hapo, kina baba wa zamani wa mateka hao walitangaza azimio lao la kumtii Yehova, waliposema hivi: “Hasha! Tusimwache BWANA [“Haiwaziki sisi kumwacha Yehova,” NW], ili kuitumikia miungu mingine.” (Yoshua 24:16) Historia inaonyesha kwamba ‘lisilowazika’ lilitukia—tena na tena! Ukosefu wa imani ndio umefanya watu wa Mungu wawe wahamishwa huko Babiloni.

      22. Ni kwa nini Yehova anasema kwamba mawazo yake na njia zake ziko juu kuliko za wanadamu?

      22 Itakuwaje wakitubu? Yehova anamtumia Isaya kuahidi kwamba ‘atawasamehe kabisa.’ Na anaongezea hivi: “Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.” (Isaya 55:8, 9) Yehova ni mkamilifu, na mawazo na njia zake ziko juu sana kwa kiwango kisichoweza kufikiwa. Hata rehema yake ni ya kiwango ambacho sisi wanadamu hatuwezi kamwe kutumainia kukifikia. Fikiria hivi: Tunaposamehe mwanadamu mwenzetu, hapo ni mtenda dhambi anayemsamehe mtenda dhambi mwenzake. Tunatambua kwamba wakati fulani utafika hata sisi wenyewe tuhitaji kusamehewa na binadamu mwenzetu. (Mathayo 6:12) Lakini, hata ingawa Yehova hahitaji kamwe kusamehewa, yeye husamehe “kabisa”! Kwa kweli, yeye ni Mungu mwenye fadhili nyingi za upendo. Tena, kwa kuwa Yehova ni mwenye rehema, yeye hufungua malango ya mbingu, na hivyo kufanya baraka nyingi zibubujike juu ya wale wanaomrudia kwa mioyo yao yote.—Malaki 3:10.

      Baraka Nyingi kwa Wale Wanaomrudia Yehova

      23. Yehova anatoa mfano gani kuonyesha kwamba hakika neno lake litatimizwa?

      23 Yehova anawaahidi watu wake hivi: “Kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.” (Isaya 55:10, 11) Kila jambo ambalo Yehova anasema litatimizwa hakika. Sawa na vile mvua na theluji hudondoka kutoka angani na kutimiza kusudi lake la kuinywesha maji ya kutosha ardhini na kutokeza matunda, ndivyo neno la Yehova litokalo katika kinywa chake linavyotegemeka kabisa. Yeye ataitimiza ahadi yake—kwa uhakika kabisa.—Hesabu 23:19.

      24, 25. Ni baraka zipi zinazowangoja wahamishwa Wayahudi wanaotenda kulingana na ujumbe wa Yehova kupitia Isaya?

      24 Basi, Wayahudi wakitii maneno yaliyotamkwa kwa faida yao kupitia Isaya, hakika wataupokea wokovu ambao Yehova ameahidi. Halafu watapata shangwe kubwa. Yehova anasema hivi: “Mtatoka kwa furaha, mtaongozwa kwa amani; mbele yenu milima na vilima vitatoa nyimbo; na miti yote ya kondeni itapiga makofi. Badala ya michongoma utamea msunobari, na badala ya mibigili [“upupu unaowasha ngozi,” “NW”], mhadesi; jambo hili litakuwa la kumpatia BWANA jina, litakuwa ishara ya milele isiyokatiliwa mbali.”—Isaya 55:12, 13.

      25 Katika mwaka wa 537 K.W.K., kweli wahamishwa Wayahudi wanatoka Babiloni kwenda zao wakishangilia. (Zaburi 126:1,2) Wanapofika Yerusalemu, wanakuta nchi imejaa michongoma, au vichaka vya miiba, na upupu unaowasha ngozi—kumbuka kwamba nchi hiyo imekaa ukiwa muda wa miongo mingi. Lakini sasa watu wa Mungu waliorudishwa kwao wanaweza kufanya mabadiliko ya kupendeza sana! Miti mirefu sana, kama vile mhadesi, inachukua mahali pa miiba na pupu zinazowasha ngozi. Baraka ya Yehova inaonekana wazi sana huku watu wake wakimtumikia ‘kwa nyimbo.’ Ni kana kwamba nchi yenyewe ndiyo inayoshangilia.

      26. Leo watu wa Mungu wanafurahia hali gani yenye baraka?

      26 Mwaka wa 1919 mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta walikombolewa katika utekwa wao wa kiroho. (Isaya 66:8) Wakiwa pamoja na umati mkubwa wa kondoo wengine, sasa wanamtumikia Mungu wakishangilia katika paradiso ya kiroho. Kwa kuwa hawana doa lolote la mavutano ya Kibabiloni, wanafurahia kuwa na hali inayokubalika, na hali hiyo ‘imempatia Yehova jina.’ Ufanisi wao wa kiroho unatukuza jina lake na kumkweza kwa kuonyesha kwamba yeye ndiye Mungu wa unabii wa kweli. Mambo ambayo Yehova amewatimizia yanaonyesha Uungu wake, na yanashuhudia kwamba yeye hutimiza ahadi yake kwa uaminifu na kwamba huwaonyesha rehema wale wanaotubu. Acheni wale wote wanaoendelea ‘kununua divai na maziwa, bila fedha na bila thamani’ washangilie kwa kumtumikia milele!

      [Maelezo ya Chini]

      a Majina mengi ya Kiyahudi yamepatikana katika maandishi ya kibiashara ya Babiloni ya kale.

      b Yesu anaendelea kusimamia kazi ya kufanya wanafunzi. (Ufunuo 14:14-16) Leo, wanaume na wanawake Wakristo humwona Yesu kuwa Kichwa cha kutaniko. (1 Wakorintho 11:3) Na katika wakati wa Mungu uliowekwa, Yesu atachukua hatua akiwa “kiongozi na jemadari” kwa njia nyingine, wakati atakapoongoza lile pigano la kukata maneno juu ya adui za Mungu kwenye vita ya Har-Magedoni.—Ufunuo 19:19-21.

      [Picha katika ukurasa wa 234]

      Wayahudi wenye kiu ya kiroho wanaalikwa ‘waje majini’ kisha ‘wanunue divai na maziwa’

      [Picha katika ukurasa wa 239]

      Yesu alijithibitisha kuwa “kiongozi na jemadari” kwa kabila za watu

      [Picha katika ukurasa wa 244, 245]

      “Mtu mbaya na aache njia yake”

  • Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya Sala
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Saba

      Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya Sala

      Isaya 56:1-12

      1, 2. Ni tangazo gani la kusisimua lililotolewa mwaka wa 1935, na tangazo hilo lilikuwa sehemu ya jambo gani?

      SIKU ya Ijumaa, Mei 31, 1935, Joseph F. Rutherford alihutubia umati katika mkusanyiko huko Washington, D.C. Alizungumzia jinsi “umati mkubwa” ambao mtume Yohana aliona katika njozi unavyoweza kutambuliwa. Kwenye kilele cha hotuba yake, Ndugu Rutherford alisema hivi: “Wote wale walio na tumaini la kuishi milele duniani wanaombwa wasimame.” Mmoja wa wale waliohudhuria alisema kwamba “zaidi ya nusu ya wasikilizaji walisimama.” Halafu msemaji akasema: “Tazameni! Umati mkubwa!” Mwingine aliyekuwako anakumbuka hivi: “Kwanza kukawa kimya, kisha nderemo, halafu kelele za kushangilia zikavuma kwa muda mrefu.”—Ufunuo 7:9.

      2 Hiyo ilikuwa hatua muhimu sana ya unabii uliokuwa ukiendelea kutimizwa. Unabii huo uliandikwa miaka 2,700 hivi mapema na unapatikana katika Isaya sura ya 56 katika Biblia zetu. Unabii huo una ahadi za kufariji na vilevile maonyo makali, sawasawa na unabii mwingine mwingi ulio katika Isaya. Unabii huo unatimizwa kwanza kuhusiana na watu wa agano la Mungu wa siku za Isaya mwenyewe, lakini unaendelea kutimizwa muda wa karne zote mpaka siku zetu.

      Matakwa ya Wokovu

      3. Ni lazima Wayahudi wafanye nini ikiwa wanatafuta wokovu kutoka kwa Mungu?

      3 Isaya sura ya 56 inaanza kwa kuwapa Wayahudi onyo la upole. Hata hivyo, waabudu wote wa kweli wanapaswa kusikiza yale ambayo nabii anaandika. Tunasoma hivi: “BWANA asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote.” (Isaya 56:1, 2) Ni lazima wakaaji wa Yuda wanaotafuta wokovu kutoka kwa Mungu waitii Sheria ya Kimusa, wakishika haki na kuishi maisha ya uadilifu. Kwa nini? Kwa sababu Yehova mwenyewe ni mwadilifu. Wale wanaofuatia uadilifu wanafurahi kwa sababu ya kukubaliwa na Yehova.—Zaburi 144:15b.

      4. Kwa nini kushika Sabato ni muhimu katika Israeli?

      4 Unabii huo unakazia kushika Sabato kwa sababu Sabato ni sehemu muhimu ya Sheria ya Kimusa. Kwa kweli, mojawapo ya sababu zinazofanya wakaaji wa Yuda wapelekwe uhamishoni hatimaye ni kwamba wanapuuza Sabato. (Mambo ya Walawi 26:34, 35; 2 Mambo ya Nyakati 36:20, 21) Sabato ni ishara ya uhusiano wa pekee kati ya Yehova na Wayahudi, na wale wanaoishika Sabato wanaonyesha kwamba wanauthamini uhusiano huo. (Kutoka 31:13) Zaidi ya hilo, kuishika Sabato kungewakumbusha watu wa siku za Isaya kwamba Yehova ndiye Muumba. Vilevile kungewakumbusha rehema anazowaonyesha. (Kutoka 20:8-11; Kumbukumbu la Torati 5:12-15) Mwishowe, kuishika Sabato kungeandaa mpangilio mzuri wa kumwabudu Yehova kwa ukawaida. Kwa sababu ya kupumzika mara moja kwa juma bila kufanya kazi yao ya kawaida, wakaaji wa Yuda wangepata nafasi ya kusali, kujifunza, na kutafakari.

      5. Kimsingi, Wakristo wanaweza kutumiaje lile shauri la kuishika Sabato?

      5 Namna gani Wakristo? Je, kile kitia-moyo cha kuishika Sabato kinawahusu wao pia? La, hakiwahusu moja kwa moja kwa kuwa Wakristo hawako chini ya ile Sheria, na hivyo hawajawekewa takwa la kuishika Sabato. (Wakolosai 2:16, 17) Ingawa hivyo, mtume Paulo alieleza kwamba kuna “pumziko la sabato” kwa ajili ya Wakristo waaminifu. Hilo “pumziko la sabato” linahusu pia kuwa na imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu ili kupata wokovu, na kuacha kutegemea matendo peke yake. (Waebrania 4:6-10) Kwa hiyo, maneno ya unabii wa Isaya kuhusu Sabato yanawakumbusha watumishi wa Yehova leo umuhimu wa kuwa na imani katika mpango wa Mungu wa wokovu. Vilevile maneno hayo ni kikumbusha kizuri sana kwamba kuna uhitaji wa kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova na kuwa wa kawaida katika ibada, bila kigeugeu.

      Faraja kwa Mgeni na Towashi

      6. Sasa fikira zinaelekezwa kwenye vikundi gani viwili?

      6 Sasa Yehova anahutubia vikundi viwili vinavyotaka kumtumikia, lakini vikundi hivyo vinahesabiwa kuwa havistahili kuingia katika kutaniko la Kiyahudi chini ya Sheria ya Kimusa. Tunasoma hivi: “Mgeni, aambatanaye na BWANA, asiseme hivi, Hakika yake BWANA atanitenga na watu wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu.” (Isaya 56:3) Hofu ya mgeni ni kwamba uhusiano wake na Israeli utakatiliwa mbali. Naye towashi ana wasiwasi kwamba hatapata kamwe watoto wa kuendeleza jina lake. Vikundi vyote viwili vinapaswa kuwa na moyo mkuu. Kabla hatujaona sababu, acheni tuchunguze vikundi hivyo vina msimamo gani chini ya Sheria kuhusiana na taifa la Israeli.

      7. Sheria inawawekea mipaka gani wageni walio katika Israeli?

      7 Wageni wasiotahiriwa hawakubaliwi kushiriki katika ibada pamoja na Israeli. Kwa mfano, hawaruhusiwi kushiriki kula sikukuu ya Kupitwa. (Kutoka 12:43) Wageni ambao hawavunji sheria za nchi kwa kuzipuuza wanafurahia kutendewa haki na kuonyeshwa ukaribishaji, lakini uhusiano wao na taifa hilo si wa kudumu. Ni kweli kwamba wengine wao wanaikubali Sheria kabisa, na wale ambao ni wanaume wanaonyesha hivyo kwa kutahiriwa. Ndipo sasa wanakuwa waongofu wenye pendeleo la kuabudu katika ua wa nyumba ya Yehova, na wanaonwa kuwa sehemu ya kutaniko la Israeli. (Mambo ya Walawi 17:10-14; 20:2; 24:22) Ingawa hivyo, hata waongofu si washiriki kamili katika agano la Yehova pamoja na Israeli, na hawapewi urithi wa ardhi katika Nchi ya Ahadi. Wageni wengine wanaweza kusali kwa kulielekea hekalu, na inaonekana kwamba wanaweza kutoa dhabihu kupitia makuhani, mradi tu dhabihu hizo zinapatana na Sheria. (Mambo ya Walawi 22:25; 1 Wafalme 8:41-43) Lakini Waisraeli hawapaswi kuwa na ushirika wa karibu pamoja na wageni hao.

      Matowashi Wanapokea Jina la Kudumu Milele

      8. (a) Matowashi walionwaje chini ya Sheria? (b) Matowashi walitumiwaje katika mataifa ya kipagani, na nyakati nyingine neno “towashi” linaweza kuwa na maana gani?

      8 Matowashi wanakatazwa kuwa washirika kamili wa taifa la Israeli, hata ikiwa wamezaliwa na wazazi Wayahudi.a (Kumbukumbu la Torati 23:1) Nyakati za Biblia, matowashi katika mataifa fulani ya kipagani walitumiwa kwa makusudi ya pekee. Kulikuwako desturi ya kukomesha nguvu za uzazi katika baadhi ya wana waliotekwa vitani. Matowashi waliwekwa kuwa maofisa katika maeneo ya mabaraza ya kifalme. Towashi angeweza kuwa ‘mlinzi wa wanawake,’ ‘mlinzi wa masuria,’ au mtumishi wa malkia. (Esta 2:3, 12-15; 4:4-6, 9) Hakuna ushuhuda wa kuonyesha kwamba Waisraeli walifuata mazoea hayo wala wa kuonyesha kwamba matowashi walitafutwa sana ili waandikwe kazi ya kuwatumikia wafalme Waisraeli.b

      9. Yehova anawaambia matowashi halisi maneno gani ya kutuliza moyo?

      9 Matowashi halisi katika Israeli wanawekewa mipaka ya kushiriki katika ibada ya yule Mungu wa kweli. Isitoshe, wanashushiwa sana heshima kwa sababu hawawezi kuzaa watoto wa kuendeleza jina la familia yao. Basi, maneno yafuatayo ya unabii huu yanafariji kweli kweli! Tunasoma hivi: “BWANA awaambia hivi matowashi, wanaozishika sabato zangu, na kuyachagua mambo yanipendezayo, na kulishika sana agano langu; Nitawapa hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina, lililo jema kuliko kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali.”—Isaya 56:4, 5.

      10. Hali ya matowashi ilibadilika lini, nao wamefunguliwa njia ya kupata pendeleo gani tangu wakati huo?

      10 Naam, wakati utafika kusiwe na kitu cha kumzuia towashi halisi kuwa mtumishi wa Yehova anayekubalika kabisa. Ikiwa matowashi watatii, watakuwa na “kumbukumbu,” au mahali, katika nyumba ya Yehova, tena wawe na jina lililo bora kuliko kuwa na wana na mabinti. Hiyo inatukia lini? Inatukia baada ya kifo cha Yesu Kristo. Wakati huo, mahali pa agano la kale la Sheria palichukuliwa na agano jipya, na mahali pa Israeli halisi pakachukuliwa na “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Tangu wakati huo, wote wale wanaodhihirisha imani wameweza kumtolea Mungu ibada inayokubalika. Sasa jambo la maana si tofauti za kimwili, wala si hali ya mwili wa mtu. Wale wanaovumilia kwa uaminifu, hata kama wana hali gani ya kimwili, ndio watakaopata “jina lidumulo milele, lisilokatiliwa mbali.” Yehova hatawasahau. Majina yao yataandikwa katika ‘kitabu chake cha ukumbusho,’ kisha watapokea uhai wa milele wakati wa Mungu ukifika.—Malaki 3:16; Mithali 22:1; 1 Yohana 2:17.

      Wageni Wanaabudu Pamoja na Watu wa Mungu

      11. Wageni wanatiwa moyo wafanye nini ili wazipokee baraka?

      11 Nayo hali ya wageni itakuwaje? Sasa unabii unaelekezwa kwao tena, naye Yehova ana maneno ya kuwafariji sana. Isaya anaandika hivi: “Wageni, walioandamana na BWANA ili wamhudumu, na kulipenda jina la BWANA, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.”—Isaya 56:6, 7.

      12. Unabii wa Yesu kuhusu “kondoo wengine” ulielewekaje wakati mmoja?

      12 Katika wakati wetu, “wageni” wamejitokeza hatua kwa hatua. Kabla ya vita ya ulimwengu ya kwanza, ilieleweka kwamba idadi ya wenye kupata wokovu ingekuwa kubwa kuliko ya wale wenye tumaini la kutawala pamoja na Yesu mbinguni, ambao leo tunawatambua kuwa Israeli wa Mungu. Wanafunzi wa Biblia waliyajua maneno ya Yesu yaliyoandikwa kwenye Yohana 10:16: “Nina kondoo wengine, ambao si wa zizi hili; hao pia lazima niwalete, nao watasikiliza sauti yangu, nao watakuwa kundi moja, mchungaji mmoja.” Ilieleweka kwamba hao “kondoo wengine” ni jamii ya kidunia. Lakini, wengi wa wanafunzi wa Biblia waliamini kwamba hao kondoo wengine wangetokea wakati wa Utawala wa Milenia ya Yesu Kristo.

      13. Kwa nini ilifikiriwa kwamba bila shaka kondoo wanaotajwa katika Mathayo sura ya 25 watatokea wakati wa siku za umalizio wa mfumo huu wa mambo?

      13 Mwishowe, andiko fulani linalohusiana na hilo ambalo linawataja kondoo, likaeleweka zaidi. Mathayo sura ya 25 ina mfano ambao Yesu alitoa wa kondoo na mbuzi. Kulingana na mfano huo, kondoo wanapokea uhai wa milele kwa sababu wanawaunga mkono ndugu za Yesu. Kwa hiyo, wao ni jamii iliyo kando na iliyo tofauti na ndugu za Kristo waliotiwa mafuta. Mwaka wa 1923, wakati wa mkusanyiko mmoja huko Los Angeles, California, Marekani, maelezo yalitolewa kuonyesha kwamba ni lazima kondoo hao watokee wakati wa siku za umalizio wa mfumo huu wa mambo, wala si wakati wa Utawala wa Milenia ya Yesu. Kwa nini? Kwa sababu Yesu alitoa mfano huo alipokuwa akijibu swali hili: “Ni wakati gani mambo haya yatakuwa, nayo itakuwa ni nini ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?”—Mathayo 24:3.

      14, 15. Maendeleo yalifanywaje kuhusu kuuelewa msimamo wa kondoo wengine katika wakati wa mwisho?

      14 Wakati wa miaka ya 1920, watu mmoja-mmoja walioshirikiana na Wanafunzi wa Biblia walikuja kuhisi kuwa roho ya Yehova haikuwa ikiwapa ushuhuda wa kwamba wana mwito wa kimbingu. Lakini walikuwa watumishi wenye bidii wa Mungu Aliye Juu Zaidi. Mwaka wa 1931, msimamo wao ulieleweka vema zaidi wakati kitabu Vindication kilipochapishwa. Kichapo hicho Vindication kilitoa maelezo juu ya njozi ya “mtu yule” mwenye kidau cha wino cha mwandishi. Maelezo hayo yalikuwa sehemu ya mazungumzo ya mstari kwa mstari kuhusu kitabu cha Ezekieli. (Ezekieli 9:1-11) “Mtu” huyo anaonekana akipita katika Yerusalemu na kutia alama katika paji za nyuso za wale wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yanayofanywa humo. “Mtu yule” anawakilisha ndugu za Yesu, wale mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta walio hai duniani wakati wa kuhukumiwa kwa Yerusalemu wa ufananisho, yaani Jumuiya ya Wakristo. Watu waliotiwa alama ni kondoo wengine wanaoishi wakati huo. Njozi inaonyesha kwamba watu hao hawaguswi wakati wafishaji wanaoelekezwa na Yehova wanapoleta kisasi juu ya jiji hilo lenye uasi-imani.

      15 Mwaka wa 1932, tamasha ya kiunabii inayohusu Mfalme Yehu wa Israeli pamoja na Yehonadabu, yaani yule mtu asiye Mwisraeli aliyemwunga Yehu mkono katika kuangamiza ibada ya Baali, ilieleweka zaidi. Ilionyeshwa ni jinsi gani kondoo wengine wanavyowaunga mkono ndugu watiwa-mafuta wa Kristo. Mwishowe, mwaka wa 1935 kondoo wengine wanaoishi wakati wa mwisho wa mfumo huu wa mambo wakatambuliwa kuwa ndio umati mkubwa ambao mtume Yohana aliona katika njozi. Jambo hilo lilielezwa kwanza kwenye ule mkusanyiko uliotajwa mapema kidogo, uliofanyika Washington, D.C., wakati ambapo Joseph F. Rutherford alinyoosha mkono akauelekeza kwa wale walio na tumaini la kidunia kuonyesha kwamba hao ndio ule “umati mkubwa.”

      16. “Wageni” wanafurahia mapendeleo na madaraka gani?

      16 Kwa njia hiyo ikazidi kuonekana hatua kwa hatua kwamba “wageni” hao wanahusika sana katika makusudi ya Yehova siku hizi za mwisho. Wanamjia Israeli wa Mungu ili kumwabudu Yehova. (Zekaria 8:23) Wanamtolea Mungu dhabihu zinazokubalika wakiwa pamoja na taifa hilo la kiroho, na wanaingia katika pumziko la sabato. (Waebrania 13:15, 16) Isitoshe, wao wanaabudu kwenye hekalu la Mungu la kiroho ambalo ni “nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote,” kama lile hekalu la Yerusalemu. (Marko 11:17) Wanadhihirisha imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo, ‘wakifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.’ Nao wanamtumikia Yehova daima, ‘wakimtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku.’—Ufunuo 7:14, 15.

      17. Wageni wa kisasa wanashika agano jipya jinsi gani?

      17 Wageni hawa wa kisasa wanashika agano jipya katika maana ya kwamba wanaposhirikiana na Israeli wa Mungu, wanafurahia faida na baraka nyingi zinazopatikana kupitia agano hilo. Ingawa wao si washiriki wa agano hilo, wanatii kwa moyo wote sheria zinazoshirikishwa nalo. Hivyo sheria ya Yehova imo katika mioyo yao, nao wanapata kujua kwamba Yehova ndiye Baba yao wa kimbingu na Mwenye Enzi Kuu anayewapita wote.—Yeremia 31:33, 34; Mathayo 6:9; Yohana 17:3.

      18. Ni kazi gani ya ukusanyaji inayotimizwa wakati wa mwisho?

      18 Unabii wa Isaya unaendelea kusema hivi: “Hili ni tamko langu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu ninayewakusanya Waisraeli waliotawanyika. Licha ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wajumuike nao.” (Isaya 56:8, “BHN”) Katika wakati wa mwisho, Yehova amewakusanya “Waisraeli waliotawanyika,” yaani mabaki watiwa-mafuta. Kwa kuongezea hilo, anawakusanya wengine, yaani umati mkubwa. Wakiwa pamoja wanaabudu kwa amani na upatano chini ya uangalizi wa Yehova na Mfalme aliyemtawaza, Kristo Yesu. Kwa sababu wao ni waaminifu-washikamanifu kwa serikali ya Yehova kupitia Kristo, Mchungaji Mwema amewafanya wawe kundi la kondoo wenye umoja na shangwe.

      Walinzi Vipofu, Mbwa Wasio na Sauti

      19. Hayawani wa kondeni na wa mwituni wanapewa mwaliko gani?

      19 Baada ya maneno hayo machangamfu yenye kujenga, kunatokea badiliko la kushangaza kabisa. Yehova yuko tayari kuwatendea rehema wageni na matowashi. Lakini wengi wanaodai kuwa washirika wa kutaniko la Mungu wanalaumiwa vikali na wanatazamia kuhukumiwa. Isitoshe, hata hawastahili mazishi ya heshima, bali kile tu wanachostahili ni kunyafuliwa na hayawani walafi. Hivyo, tunasoma hivi: “Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni.” (Isaya 56:9) Hayawani hawa watakula karamu gani? Unabii utaeleza. Na hiyo huenda ikatukumbusha msiba unaowangoja wale wanaompinga Mungu kwenye vita inayokuja ya Har-Magedoni. Maiti zao waliochinjwa zinaachiwa ndege wa mbinguni ili wazimeze-meze.—Ufunuo 19:17, 18.

      20, 21. Ni makosa gani yanayofanya viongozi wa kidini wawe viongozi bure wa kiroho?

      20 Unabii unaendelea kusema hivi: “Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi. Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. Husema, Njoni, nitaleta divai, na tunywe sana kileo; na kesho itakuwa kama leo, sikukuu kupita kiasi.”—Isaya 56:10-12.

      21 Viongozi wa kidini wa Yuda wanadai kuwa wanamwabudu Yehova. Wanadai kuwa wao ni “walinzi” wake. Lakini, wao ni vipofu kiroho, hawana sauti, wamelala usingizi. Ikiwa wanashindwa kuendelea kushika zamu ya ulinzi na kutangaza onyo la hatari, wana faida gani? Walinzi hao wa kidini hawaelewi mambo, hawafai kuwapa watu walio kama kondoo mwelekezo wa kiroho. Zaidi ya hilo, wao ni wafisadi. Tamaa zao ni za ubinafsi na haziwezi kutoshelezwa. Badala ya kufuata mwelekezo wa Yehova, wanatafuta njia yao wenyewe, wanakimbilia faida isiyo ya haki, wanakunywa mno kileo, na kuwatia wengine moyo wafanye hivyo hivyo. Kwa sababu wamezubaa sana hivi kwamba hawatambui kuwa hukumu ya Yehova inakaribia, wanawaambia watu hakuna wasiwasi, mambo ni shwari.

      22. Viongozi wa kidini wa siku za Yesu wanafananaje na wale wa Yuda ya kale?

      22 Pale mwanzoni mwa unabii wake, Isaya alitumia semi kama hizo za mfano kueleza tabia za viongozi wa kidini wa Yuda wasio waaminifu—walilewa, wakasinzia, na kukosa ufahamu kwa njia ya kiroho. Walitwika watu mzigo wa mapokeo ya wanadamu, wakasema uwongo mwingi wa kidini, wakatumainia Ashuru iwasaidie badala ya kumtegemea Mungu. (2 Wafalme 16:5-9; Isaya 29:1, 9-14) Ni wazi kwamba hawajajifunza somo lo lote. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba viongozi wa aina hiyo hiyo ndio waliokuwako karne ya kwanza. Badala ya kuzikubali habari njema walizoletewa na Yesu, Mwana wa Mungu mwenyewe, walimkataa wakatunga hila auawe. Yesu aliwaita “viongozi vipofu” bila kuwaficha, kisha akasema kwamba “ikiwa kipofu aongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.”—Mathayo 15:14.

      Walinzi wa Leo

      23. Ni unabii gani wa Petro ambao umetimizwa kuhusu viongozi wa kidini?

      23 Mtume Petro alionya kwamba walimu wa uwongo pia wangetokea ili kuwapoteza Wakristo. Aliandika hivi: “Kulikuja pia kuwa na manabii wasio wa kweli miongoni mwa watu [wa Israeli], kama pia kutakavyokuwa na walimu wasio wa kweli miongoni mwenu. Hawahawa wataleta ndani kimya-kimya mafarakano yenye kuangamiza na watakana hata mmiliki aliyewanunua, wakijiletea wenyewe uangamizo wa kasi.” (2 Petro 2:1) Matokeo yamekuwa nini kwa sababu ya walimu hao wa uwongo kuleta mafundisho ya uwongo na migawanyiko? Matokeo ni Jumuiya ya Wakristo, ambayo viongozi wake wa kidini leo husali ili Mungu abariki rafiki zao wa kisiasa, kisha wanawaahidi rafiki hao kwamba kuna matazamio mema wakati ujao. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wameonekana wazi kuwa ni vipofu, hawana sauti, tena wamelala usingizi wa kutojali mambo ya kiroho.

      24. Kuna umoja gani kati ya Israeli wa kiroho na wageni?

      24 Hata hivyo, Yehova analeta mamilioni ya wageni katika nyumba yake kuu ya kiroho ya kutolea sala, ili waabudu pamoja na mabaki wa mwisho wa Israeli wa Mungu. Ijapokuwa wageni hawa wametoka katika mataifa, makabila, na lugha nyingi, wana umoja kati yao wenyewe na pamoja na Israeli wa Mungu. Wanasadiki kwamba wokovu unaweza kuletwa na Yehova Mungu peke yake, kupitia Yesu Kristo. Kumpenda Yehova kunawachochea wajiunge na ndugu watiwa-mafuta wa Kristo kutoa sauti ya kutangaza imani yao waziwazi. Na wanafarijiwa sana na maneno ya mtume aliyepuliziwa ambaye aliandika hivi: “Ukitangaza hadharani lile ‘neno katika kinywa chako mwenyewe,’ kwamba Yesu ni Bwana, na kudhihirisha imani moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokolewa.”—Waroma 10:9.

      [Maelezo ya Chini]

      a Baadaye, neno “towashi” lilimaanisha pia kuhusu ofisa aliyetumika eneo la barazani, bila kumaanisha kukatwa kiungo cha uzazi. Bila shaka yule Mwethiopia aliyebatizwa na Filipo alikuwa towashi katika maana hiyo. Sababu ni kwamba, inaonekana towashi huyo alikuwa mwongofu kwa sababu alibatizwa kabla njia haijafunguliwa ya kuingia kwa watu wasiotahiriwa, wasio Wayahudi.—Matendo 8:27-39.

      b Ebed-meleki, ambaye alimwokoa Yeremia, na angeweza kwenda kwa Mfalme Sedekia bila kuzuiwa na mtu yeyote, anaitwa towashi. Inaonekana kwamba anatajwa kuwa towashi katika maana ya kuwa ofisa wa eneo la barazani, wala si katika maana ya kukatwa kiungo.—Yeremia 38:7-13.

      [Picha katika ukurasa wa 250]

      Sabato ingeandaa nafasi ya kusali, kujifunza, na kutafakari

      [Picha katika ukurasa wa 256]

      Msimamo wa kondoo wengine ulielezwa wazi mkusanyikoni Washington, D.C., mwaka wa 1935 (chini ni ubatizo, kulia ni programu)

      [Picha katika ukurasa wa 259]

      Hayawani wanaalikwa waje kula karamu

      [Picha katika ukurasa wa 261]

      Wageni na Israeli wa Mungu wana umoja kati yao wenyewe

  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Nane

      Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu

      Isaya 57:1-21

      1. Yehova alitoa uhakikisho gani, na maneno yake yanatokeza maswali gani?

      “YEYE aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua [“kuhuisha,” NW] roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.” (Isaya 57:15) Hivyo ndivyo alivyoandika nabii Isaya katika karne ya nane K.W.K. Ni nini kilichokuwa kikiendelea Yuda ambacho kilifanya ujumbe huo uwe wenye kutia moyo sana? Maneno haya yaliyopuliziwa yanawasaidiaje Wakristo leo? Mazungumzo ya Isaya sura ya 57 yatatusaidia kujibu maswali hayo.

      “Ninyi Karibuni Hapa”

      2. (a) Inaelekea kwamba maneno ya Isaya sura ya 57 yanatumika wakati gani? (b) Hali ya wenye haki ikoje siku za Isaya?

      2 Sehemu hii ya unabii wa Isaya inaonekana kuwa inatumika katika siku za Isaya mwenyewe. Fikiria jinsi ambavyo uovu umekolea sasa: “Mwenye haki hupotea, wala hakuna atiaye hayo moyoni; na watu watauwa huondolewa, wala hakuna afikiriye ya kuwa mwenye haki ameondolewa asipatikane na mabaya. Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake.” (Isaya 57:1, 2) Mtu mwenye haki akianguka, hakuna anayejali. Akifa mapema mno, watu hawajali. Yeye hupata amani kwa kulala usingizi wa kifo; hiyo humwondolea mateso aliyoletewa na wasiomhofu Mungu, na ni njia ya kumwepusha na mabaya. Taifa teule la Mungu limezorota likawa na hali ya kusikitisha sana. Lakini, bila shaka wale wanaobaki wakiwa waaminifu wanatiwa moyo kweli kweli kwa kujua kwamba, licha ya kuona yanayoendelea,Yehova atawategemeza pia!

      3. Yehova anatumia usemi wa namna gani anapoongea na kizazi kiovu cha Yuda, na kwa nini?

      3 Yehova anakiita kizazi kiovu cha Yuda kimjie, akisema hivi: “Lakini ninyi karibuni hapa, enyi wana wa mwanamke mchawi [“mwaguzi,” “NW”], uzao wa mzinzi na kahaba.” (Isaya 57:3) Wamestahili kuitwa majina ya aibu, yaani wana wa mwanamke mwaguzi na wazao wa mzinzi na wa kahaba. Ibada ya uwongo ambayo wamegeukia inahusisha matendo ya kuchukiza sana ya ibada ya sanamu na uwasiliani-roho, na vilevile mazoea ya ngono zisizo za adili. Kwa hiyo, Yehova anawauliza hivi watenda-dhambi hao: “Mnafanya dhihaka [“mnakula raha,” “NW”] yenu juu ya nani? Mmepanua vinywa vyenu, na kutoa ndimi zenu? je, ninyi si wana wa uasi, uzao wa uongo; ninyi mnaowasha tamaa zenu kati ya mialoni, chini ya kila mti wenye majani mabichi; ninyi mnaoua watoto mabondeni, chini ya mianya ya majabali?”—Isaya 57:4, 5.

      4. Waovu wa Yuda wana hatia ya jambo gani?

      4 Waovu wa Yuda wanafanya ibada ya upagani yenye kuchukiza sana hadharani, ‘wakila raha.’ Wanawacheka-cheka manabii wa Mungu ambao wametumwa kuwarekebisha, wakiwatolea ndimi zao kwa madharau, bila aibu. Ingawa wao ni watoto wa Abrahamu, njia zao za uasi zinawafanya wawe wana wa uasi na uzao wa uwongo. (Isaya 1:4; 30:9; Yohana 8:39, 44) Wakiwa kule nje mashambani, miongoni mwa miti mikubwa, wanachochea vishindo vingi vya kidini katika ibada ya sanamu. Nayo ni ibada ya ukatili we! Kwani, hata wanachinja watoto wao wenyewe kama yale mataifa yaliyofukuzwa na Yehova nchini kwa sababu ya machukizo yao makubwa!—1 Wafalme 14:23; 2 Wafalme 16:3, 4; Isaya 1:29.

      Kuyamwagia Mawe Toleo la Kinywaji

      5, 6. (a) Wakaaji wa Yuda wamechagua kufanya nini badala ya kumwabudu Yehova? (b) Ibada ya sanamu ya Yuda inafanywaje waziwazi bila kujali, na imeenea kiasi gani?

      5 Ebu ona jinsi ambavyo wakaaji wa Yuda wameingilia sana ibada ya sanamu: “Mnachagua mawe laini mabondeni, na kuyafanya kitovu cha maisha yenu. Mnayamiminia dhabihu ya kinywaji na kuyapelekea dhabihu ya nafaka! Je, mimi nitaridhishwa kwa vitu hivyo?” (Isaya 57:6, “BHN”) Wayahudi ni watu wa agano la Mungu, lakini badala ya kumwabudu yeye, wanaokota mawe chini ya mto na kuyafanya miungu. Daudi alitangaza kwamba Yehova ndiye fungu la maisha yake, lakini watenda-dhambi hawa wameamua kuabudu sanamu za mawe zisizo na uhai, na wanazimwagia matoleo ya vinywaji. (Zaburi 16:5; Habakuki 2:19) Yehova atawezaje kuridhika, na huku watu wanaoitwa kwa jina lake wanapotosha ibada jinsi hiyo?

      6 Kila mahali—chini ya miti mikubwa, katika mabonde ya mito, juu ya vilima, katika majiji yao—Yuda anaabudu sanamu. Lakini Yehova anaona yote, na anamtumia Isaya kufichua upotovu wa nchi hiyo: “Umeweka kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka sana; ukaenda huko ili kutoa dhabihu. Na nyuma ya milango na miimo umeweka kumbukumbu lako.” (Isaya 57:7-8a) Yuda anatandika kitanda chake chenye uchafu wa kiroho katika sehemu za juu, kisha anaitolea miungu ya kigeni dhabihu juu ya kitanda hicho.a Hata nyumba za watu binafsi zina sanamu nyuma ya milango na kwenye miimo ya milango.

      7. Yuda anaingilia ibada ya kukosa adili akiwa na roho gani?

      7 Huenda wengine wakashangaa wakijiuliza imekuwaje hata Yuda akahusika sana katika ibada chafu. Je, nguvu fulani yenye uwezo kumpita imemlazimisha kumwacha Yehova? La. Yeye anafanya hivyo kwa hiari, kwa hamu nyingi. Yehova anasema hivi: “Umejifunua nafsi yako kwa ajili ya mwingine, si kwa ajili yangu, ukakwea juu; umekipanua kitanda chako, nawe umefanya maagano na hao; ulikipenda kitanda chao hapo ulipokiona [“ulikiangalia kiungo cha mwanamume,” “NW”].” (Isaya 57:8b) Yuda amefanya agano pamoja na miungu ya uwongo, na anaupenda uhusiano wake haramu pamoja na miungu hiyo. Hasa anayapenda mazoea ya ngono zisizo za adili, ambayo inaelekea kuwa yanahusu kutumia vitu vinavyofananisha kiungo cha uzazi cha mwanamume. Na hilo ni jambo la kawaida katika ibada ya miungu hiyo!

      8. Ibada ya sanamu ilisitawi katika Yuda chini ya mfalme yupi hasa?

      8 Maelezo hayo kuhusu ibada ya sanamu yenye ukatili na ukosefu mwingi sana wa adili yanalingana na yale tunayojua kuhusu wafalme kadhaa waovu wa Yuda. Kwa mfano, Manase alijenga sehemu za juu, akamsimamishia Baali madhabahu nyingi, na kuweka madhahabu za dini ya uwongo ndani ya nyua mbili za hekalu. Alifanya wanawe wapite katika moto, akazoea mizungu ya uchawi, akatumia uaguzi, na kuendeleza mazoea ya uwasiliani-roho. Mfalme Manase pia aliweka ndani ya hekalu la Yehova mfano wa kuchongwa wa mti mtakatifu aliokuwa ameutengeneza.b Alitongoza Yuda “wafanye mabaya, kuliko mataifa BWANA aliowaharibu mbele za wana wa Israeli.” (2 Wafalme 21:2-9) Wengine huamini kwamba Manase ndiye aliyeagiza Isaya auawe, ingawa jina la Manase halionekani katika Isaya 1:1.

      ‘Uliendelea Kuwatuma Wajumbe Wako’

      9. Kwa nini Yuda anatuma wajumbe “mbali”?

      9 Kosa la Yuda halikuwa kutumikia miungu ya uwongo tu. Akimtumia Isaya kama msemaji wake, Yehova anasema hivi: “Ulimwendea mfalme [“Meleki,” “NW”] na mafuta ya marhamu, ukaongeza manukato yako, ukawatuma wajumbe wako waende mbali, ukajidhili sana hata kuzimu [“Sheoli,” “NW”].” (Isaya 57:9) Ufalme wa Yuda usio na uaminifu unateremka kumwendea “Meleki,” neno ambalo kwa Kiebrania linamaanisha “aliye mfalme,” ambaye yaelekea kuwa ni mfalme wa mamlaka ya kigeni. Walimtolea mfalme huyo zawadi za bei kubwa, tena za kuvutia, zinazofananishwa na mafuta ya marhamu na manukato. Yuda anatuma wajumbe sehemu za mbali. Kwa nini? Ili kushawishi mataifa yasiyo ya Kiyahudi kufanya mapatano ya kisiasa naye. Akiisha kumpa Yehova kisogo, anawatumainia wafalme wa kigeni.

      10. (a) Mfalme Ahazi anatafutaje njia ya kuungana na mfalme wa Ashuru? (b) Yuda ‘anajidhili sana hata Sheoli’ jinsi gani?

      10 Mfano mmoja wa jambo hilo unapatikana siku za Mfalme Ahazi. Mfalme huyo asiye mwaminifu wa Yuda anaona ametishwa na muungano wa Israeli na Shamu, kwa hiyo anatuma wajumbe kwa mfalme wa Ashuru, Tiglathi-pileseri wa Tatu, akisema hivi: “Mimi ni mtumishi, tena mwana wako; kwea, ukaniokoe mkononi mwa mfalme wa Shamu, na mkononi mwa mfalme wa Israeli, walioniinukia.” Ahazi anapeleka fedha na dhahabu ziwe rushwa kwa mfalme wa Ashuru, naye mfalme huyo anajibu kwa kushambulia Shamu vikali na kuiharibu. (2 Wafalme 16:7-9) Yuda anajiinamisha hadi kwenye “vilindi vya Sheoli” anapofanya shughuli zake na mataifa yasiyo ya Kiyahudi. (An American Translation) Kwa sababu ya shughuli hizo, atakufa, au akome kuwa taifa huru lenye mfalme.

      11. Yuda anahisi usalama gani wa uwongo?

      11 Yehova anaendelea kumwambia Yuda hivi: “Ulikuwa umechoka kwa ajili ya urefu wa njia yako; lakini hukusema, Hapana matumaini; ulipata kuhuishwa nguvu zako; kwa sababu hiyo hukuugua.” (Isaya 57:10) Naam, taifa hilo limechoka sana huku likifuata njia zake za uasi-imani, na linashindwa kuona kwamba jitihada zake hazina tumaini. Linajipumbaza kuamini kwamba linafanikiwa kwa nguvu zake lenyewe. Linajihisi kuwa lina nguvu na afya. Upumbavu we!

      12. Ni hali zipi katika Jumuiya ya Wakristo zinazolingana na zile za Yuda?

      12 Leo kuna tengenezo ambalo mwenendo wake ni kikumbusha cha mwenendo wa Yuda katika siku za Isaya. Jumuiya ya Wakristo hutumia jina la Yesu, lakini hufanya mapatano na mataifa na imeweka sanamu chungu nzima katika sehemu zake za ibada. Wafuasi wake hata huweka mifano ya ibada ya sanamu katika nyumba zao wenyewe. Jumuiya ya Wakristo imetoa vijana wawe dhabihu katika vita vya mataifa. Bila shaka jambo hili linamwudhi sana Mungu wa kweli, anayewaamuru Wakristo hivi: “Ikimbieni ibada ya sanamu”! (1 Wakorintho 10:14) Kwa kujihusisha katika siasa, Jumuiya ya Wakristo ‘imefanya uasherati na wafalme wa dunia.’ (Ufunuo 17:1, 2) Kwa kweli Jumuiya ya Wakristo ni mmoja wa wategemezaji wakuu wa Umoja wa Mataifa. Ni nini kinachomngoja kahaba huyu wa kidini? Ili tujue, tunapaswa kufahamu kile ambacho Yehova anaambia mfanani halisi wa kahaba huyo, yaani Yuda isiyo na uaminifu, ambayo inawakilishwa hasa na jiji lake kuu, Yerusalemu.

      “Na Wakuponye Hao Uliowakusanya”

      13. Yuda anaanza ‘kusema uwongo’ namna gani, na anatendaje kuhusu subira ya Yehova?

      13 “Ni nani uliyemwogopa na kumhofu, hata ukasema uongo?” Yehova anauliza. Swali safi! Hakika Yuda hamwonyeshi Yehova hofu ya kimungu inayofaa. Ama sivyo, hangekuwa taifa la waongo, waabudu wa miungu ya uwongo. Yehova anaendelea kusema hivi: “Hukunikumbuka mimi, wala kuweka hayo moyoni? je! mimi sikunyamaza tangu zamani, hata huniogopi?” (Isaya 57:11) Yehova amekaa kimya asiadhibu Yuda mara hiyo. Je, Yuda anashukuru? La. Badala yake, anauona uvumilivu wa Mungu kuwa ni kutokujali. Ameacha kabisa kumhofu Mungu.

      14, 15. Yehova anasema nini juu ya matendo ya Yuda na ‘hao aliowakusanya’?

      14 Hata hivyo, kipindi cha ustahimilivu wa Mungu kitafikia mwisho. Akiutazamia wakati huo, Yehova anatangaza hivi: “Mimi nitatangaza haki yako [“uadilifu wako,” “NW”] na matendo yako hayatakufaa. Utakapolia, na wakuponye hao uliowakusanya; lakini upepo utawachukua; uvuvio tu utawachukulia mbali.” (Isaya 57:12, 13a) Yehova atafichua kwamba uadilifu wa Yuda ni bandia. Matendo yake ya unafiki hayatakuwa na faida. ‘Hao aliowakusanya,’ maana yake sanamu zake nyingi, hawatamponya. Maafa yatakapotokea ghafula, miungu anayoitumaini itapeperushwa mbali kwa pumzi moja tu.

      15 Maneno ya Yehova yanatimizwa mwaka wa 607 K.W.K. wakati Mfalme Nebukadreza wa Babiloni anapoharibu Yerusalemu, anachoma hekalu kwa moto na kuteka idadi kubwa ya watu. “Hivyo Yuda wakachukuliwa utumwani kutoka nchi yao.”—2 Wafalme 25:1-21.

      16. Ni nini kinachoingoja Jumuiya ya Wakristo na sehemu nyinginezo za “Babiloni Mkubwa”?

      16 Vivyo hivyo, sanamu chungu nzima za Jumuiya ya Wakristo hazitamkomboa katika siku ya hasira ya Yehova. (Isaya 2:19-22; 2 Wathesalonike 1:6-10) Jumuiya ya Wakristo itaangamizwa kabisa pamoja na sehemu nyingine zote za “Babiloni Mkubwa,” ile milki ya ulimwengu ya dini za uwongo. Hayawani wa mfano mwenye rangi nyekundu nyangavu na pembe zake kumi ‘watamfanya Babiloni Mkubwa awe ukiwa na uchi, na watakula kabisa sehemu zake zenye nyama na watamchoma kabisa kwa moto.’ (Ufunuo 17:3, 16, 17) Sisi tunafurahi kama nini kwamba tumetii amri hii: “Tokeni kwake, watu wangu, ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake”! (Ufunuo 18:4, 5) Tusirudi kwake wala kwenye njia zake kamwe.

      ‘Atakayekimbilia Usalama Kwangu Ataimiliki Nchi’

      17. ‘Mwenye kukimbilia usalama kwa Yehova’ anapewa ahadi gani, na inatimizwa lini?

      17 Namna gani maneno yanayofuata ya unabii wa Isaya? “Watakaokimbilia usalama kwangu, wataimiliki nchi, mlima wangu mtakatifu utakuwa mali yao.” (Isaya 57:13b, “BHN”) Yehova anaongea na nani sasa? Anaeleza mambo yatakayotokea baada ya yale maafa makubwa yanayokuja, na anatabiri kwamba watu wake watakombolewa kutoka Babiloni kisha ibada safi irudishwe katika mlima wake mtakatifu, Yerusalemu. (Isaya 66:20; Danieli 9:16) Hiki ni kitia-moyo kweli kweli kwa Wayahudi wowote wanaobaki wakiwa waaminifu! Zaidi ya hilo, Yehova anasema hivi: “Naye atasema, Tutieni, tutieni, itengenezeni njia, kiondoeni kila kikwazacho katika njia ya watu wangu.” (Isaya 57:14) Wakati ufikapo wa Mungu kuwakomboa watu wake, njia itakuwa tayari, huku vipingamizi vyote vikiwa vimeondolewa.—2 Mambo ya Nyakati 36:22, 23.

      18. Kutukuka kwa Yehova kunaelezwaje, hata hivyo anaonyesha hangaiko gani lenye upendo?

      18 Hapo sasa ndipo nabii Isaya anapoyasimulia maneno yaliyonukuliwa pale mwanzoni: “Yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua [“kuhuisha,” “NW”] roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu [“wanaopondwa,” “NW”].” (Isaya 57:15) Kiti cha ufalme cha Yehova kiko katika mbingu za juu kabisa. Hakuna cheo kingine chochote kilicho juu wala kilichotukuka kuliko hicho. Inafariji kama nini kujua kwamba akiwa huko juu yeye huona kila kitu—si dhambi za waovu tu, bali hata matendo ya haki ya wale wanaojaribu kumtumikia! (Zaburi 102:19; 103:6) Tena, yeye anasikia sauti za kuugua za wale wanaoonewa, na anahuisha mioyo ya waliopondwa. Bila shaka maneno haya yaliigusa mioyo ya Wayahudi waliotubu nyakati za kale. Na hakika yanaigusa mioyo yetu sisi leo.

      19. Hasira ya Yehova hukoma wakati gani?

      19 Maneno ya Yehova yanayofuata ni yenye faraja pia: “Sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya.” (Isaya 57:16) Kama ghadhabu ya Yehova ingekuwa ya daima dawamu, hakuna kiumbe chochote cha Mungu ambacho kingeweza kubaki hai. Lakini ni jambo la kufurahisha kwamba hasira ya Mungu ni ya muda tu. Ghadhabu hiyo hukoma baada ya kutimiza kusudi lake. Ufahamu huo wa kina kirefu uliopuliziwa hutusaidia kuelewa sana kwamba Yehova anaupenda uumbaji wake.

      20. (a) Yehova hushughulikaje na mkosaji asiyetubu? (b) Yehova humfariji jinsi gani mtu mwenye majuto?

      20 Yehova anapoendelea kuongea, tunapata ufahamu wa kina kirefu zaidi. Kwanza anasema hivi: “Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake naliona hasira, nikampiga; nalificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe.” (Isaya 57:17) Hakuna shaka kwamba makosa yaliyofanywa kwa sababu ya pupa ndiyo yanayochochea ghadhabu ya Mungu. Maadamu mtu anabaki akiwa mkaidi moyoni, Yehova naye anabaki na hasira yake. Lakini namna gani mkaidi huyo akikubali nidhamu? Hapo ndipo Yehova huonyesha jinsi upendo na huruma zake humsukuma kutenda: “Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia.” (Isaya 57:18) Baada ya Yehova kutoa nidhamu, yeye humponya mtu mwenye majuto na kumfariji huyo na wale pia wanaoomboleza pamoja naye. Ndiyo sababu Wayahudi waliweza kurudi nyumbani mwaka wa 537 K.W.K. Ni kweli kwamba Yuda haikuweza tena kamwe kuwa ufalme wenye kujitawala chini ya mfalme wa ukoo wa Daudi. Hata hivyo, hekalu katika Yerusalemu lilijengwa upya, na ibada ya kweli ikarudishwa.

      21. (a) Yehova alihuishaje roho ya Wakristo watiwa-mafuta mwaka wa 1919? (b) Sisi mmoja-mmoja tunapaswa kusitawisha sifa gani?

      21 Yehova, “yeye aliye juu, aliyetukuka,” aliihangaikia pia hali njema ya mabaki watiwa-mafuta mwaka wa 1919. Kwa sababu ya roho yao ya majuto na unyenyekevu, huyo Mungu mkuu, Yehova, aliwafadhili kwa kuyaona mateso yao na kuwakomboa kutoka katika utekwa wa Kibabiloni. Aliondoa vikwazo vyote, akawapeleka mahali penye uhuru ili waweze kumtolea ibada safi. Hivyo maneno ya Yehova kupitia Isaya yakatimia wakati huo. Isitoshe, maneno hayo yana kanuni za milele zinazohusu kila mmoja wetu. Yehova hukubali ibada ya wale tu walio na akili ya unyenyekevu. Na mmoja wa watumishi wa Mungu akitenda dhambi, anapaswa kufanya haraka kukiri kosa lake, kukubali karipio, na kurekebisha njia zake. Sisi tusisahau kamwe kwamba Yehova huwaponya na kuwafariji wanyenyekevu, bali “huwapinga wenye kiburi.”—Yakobo 4:6.

      ‘Amani Kwao Walio Mbali na Walio Karibu’

      22. Yehova anatabiri wakati gani ujao kwa (a) wenye kutubu? (b) waovu?

      22 Akitofautisha wakati ujao wa wale wanaotubu na wakati ujao wa wale wanaoendelea tu kufuata njia zao za uovu, Yehova anatangaza hivi: “Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; . . . nami nitamponya. Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka. Hapana amani kwa wabaya.”—Isaya 57:19-21.

      23. Tunda la midomo ni nini, na Yehova ‘anaumbaje’ tunda hilo?

      23 Tunda la midomo ni ile dhabihu ya sifa ambayo hutolewa kuelekea Mungu—tangazo la peupe kuhusu jina lake. (Waebrania 13:15) Yehova ‘anaumbaje’ tangazo hilo la peupe? Ili kutoa toleo la dhabihu ya sifa, ni lazima kwanza mtu ajifunze juu ya Mungu kisha amwamini. Imani, ambayo ni tunda la roho ya Mungu, humchochea mtu huyo awaambie wengine mambo ambayo amesikia. Yaani, yeye hufanya tangazo la peupe. (Waroma 10:13-15; Wagalatia 5:22) Vilevile, na ikumbukwe kwamba Yehova ndiye hasa anayewapa watumishi wake utume wa kutangaza sifa yake. Tena Yehova ndiye anayewakomboa watu wake, na kufanya iwezekane kwao kutoa dhabihu hizo za sifa. (1 Petro 2:9) Kwa hiyo ni sawa kusema kwamba Yehova ndiye anayeumba tunda hilo la midomo.

      24. (a) Ni nani wanaopata kujua amani ya Mungu, na matokeo ni nini? (b) Ni nani ambao hawapati kujua amani, na wanapatwa na matokeo gani?

      24 Lo, Wayahudi wanatoa tunda la midomo lenye kusisimua kama nini wakati wanapoirudia nchi yao wakimwimbia Yehova sifa! Bila shaka wana shangwe ya kuijua amani ya Mungu, hata kama wako “mbali”—mwendo mrefu kutoka Yuda, wakiwa wangali wanangojea kurudi—au wakiwa “karibu,” yaani wakiwa tayari katika nchi yao. Lakini mambo ni tofauti kabisa kwa waovu! Waovu wowote wasioitikia nidhamu za Yehova, hata wawe akina nani, na hata wawe wapi, hawana amani hata kidogo. Wanachacha kama bahari iliyochafuka, wakiendelea kuzaa, si lile tunda la midomo, bali “tope na takataka” za baharini, uchafu wa kila aina.

      25. Watu wengi wa mbali na wa karibu huja kujua amani jinsi gani?

      25 Leo, pia, waabudu wa Yehova kila mahali wanatangaza habari njema za Ufalme wa Mungu. Wakristo wa mbali na karibu, katika nchi zaidi ya 230, wanatoa tunda la midomo yao, wakivumisha sifa za yule Mungu mmoja tu wa kweli. Sifa wanazoimba zinasikiwa “tokea mwisho wa dunia.” (Isaya 42:10-12) Wale wanaozisikia semi zao na kuziitikia wanaikubali kweli ya Neno la Mungu, Biblia. Watu wa jinsi hiyo huja kujua amani, inayopatikana kwa kumtumikia “Mungu apaye amani.”—Waroma 16:20.

      26. (a) Ni nini kinachowangojea waovu? (b) Watu wapole wanapewa ahadi gani bora, nasi tunapaswa kupiga moyo konde kufanya nini?

      26 Ni kweli kwamba waovu hawasikizi ujumbe wa Ufalme. Ingawa hivyo, hivi karibuni hawataruhusiwa kuivuruga amani ya wenye haki. “Bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo,” ndivyo Yehova anavyoahidi. Wale wanaomkimbilia Yehova watairithi nchi kwa njia nzuri ajabu. “Wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.” (Zaburi 37:10, 11, 29) Wakati huo dunia yetu itakuwa mahali pazuri wee! Sisi sote na tupige moyo konde tusipoteze kamwe amani ya Mungu, ili tuweze kuimba sifa ya Mungu milele hata milele.

      [Maelezo ya Chini]

      a Inaelekea kwamba neno “kitanda” linamaanisha madhabahu ama mahali pa ibada ya kipagani. Mahali hapo panaitwa kitanda ili neno hilo liwe kikumbusha cha kwamba ibada hiyo ni ukahaba wa kiroho.

      b Huenda ikawa kwamba miti mitakatifu iliwakilisha kiungo cha uke, na huenda ikawa nguzo takatifu zilifananisha kiungo cha uzazi cha mwanamume. Vitu hivyo viwili vilitumiwa na wakaaji wa Yuda wasio waaminifu.—2 Wafalme 18:4; 23:14.

      [Picha katika ukurasa wa 263]

      Yuda anafuata ibada isiyo na maadili chini ya kila mti wenye majani mabichi

      [Picha katika ukurasa wa 267]

      Yuda anajenga madhabahu kotekote nchini

      [Picha katika ukurasa wa 275]

      “Nayaumba matunda ya midomo”

  • Unafiki Wafichuliwa!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Kumi Na Tisa

      Unafiki Wafichuliwa!

      Isaya 58:1-14

      1. Yesu na Yehova wana maoni gani juu ya unafiki, na unafiki wa siku za Isaya unaonyeshwaje?

      YESU aliwaambia viongozi wa kidini wa siku zake hivi: “Mwaonekana kwa nje kuwa waadilifu kwa watu, lakini ndani mmejaa unafiki na uasi-sheria.” (Mathayo 23:28) Yesu anaposhutumu unafiki jinsi hiyo, inaonyesha kwamba hata Baba yake wa kimbingu anaushutumu hivyo hivyo. Unafiki ulioenea sana katika Yuda ndio hasa unaokaziwa fikira katika sura ya 58 ya unabii wa Isaya. Siku hizo zimejaa ugomvi, ukandamizaji, na fujo, na mwadhimisho wa Sabato umezorota ukawa desturi isiyo na maana. Watu wanamtolea Yehova utumishi mdogo tu kwa kufuata desturi tu na kujionyesha nje-nje eti wana kicho kwa Mungu kwa kufunga kula, lakini si kwa moyo mweupe. Si ajabu kwamba Yehova anawafichua wazi kabisa!

      ‘Uwahubiri Watu Dhambi Zao’

      2. Isaya anaonyesha roho gani anapoutangaza ujumbe wa Yehova, na ni nani leo walio kama yeye?

      2 Licha ya Yehova kuchukizwa sana na mwenendo wa Yuda, maneno Yake yanasihi sana taifa hilo litubu. Na bado, Yehova anataka karipio lake litolewe bila kuficha mambo. Kwa hiyo, anamwamuru Isaya hivi: “Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; uwahubiri watu wangu kosa lao, na nyumba ya Yakobo dhambi zao.” (Isaya 58:1) Isaya angeweza kuchukiwa na watu hao kwa sababu ya kutangaza maneno ya Yehova kwa ujasiri, lakini harudi nyuma kwa woga. Bado ana roho ile ile ya kujitoa aliyoonyesha aliposema: “Mimi hapa, nitume mimi.” (Isaya 6:8) Isaya ni mfano mzuri kama nini wa uvumilivu kwa Mashahidi wa Yehova wa kisasa, ambao pia wamepewa utume wa kuhubiri Neno la Mungu na kufichua unafiki wa kidini!—Zaburi 118:6; 2 Timotheo 4:1-5.

      3, 4. (a) Watu katika siku za Isaya wanajifanya wana hali gani? (b) Hali ya Yuda ikoje hasa?

      3 Watu wa siku za Isaya wanamtafuta Yehova kwa kujionyesha, huku wakisema eti wanapendezwa na hukumu zake za haki. Tunasoma maneno haya ya Yehova: “Wanitafuta kila siku; hupenda kujua njia zangu; kama vile taifa waliotenda haki, wasioacha sheria ya Mungu wao, hutaka kwangu amri za haki; hufurahi kumkaribia Mungu.” (Isaya 58:2) Je, wanasema kweli wanapodai kwamba wanapendezwa na njia za Yehova? La. Wao ni kama ‘taifa lililotenda haki,’ lakini wako hivyo kijuujuu tu. Kwa kweli, taifa hili ‘limeacha haki ya Mungu wao.’

      4 Hali hiyo inafanana sana na ile ambayo Ezekieli alifunuliwa baadaye. Yehova alimwambia Ezekieli kwamba Wayahudi walikuwa wakiambiana hivi: “Haya! twende tukasikie ni neno gani hilo litokalo kwa BWANA.” Lakini Mungu alimwonya Ezekieli kwamba hawakuwa na moyo mweupe: “Nao huja kwako . . . nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao. Na tazama, wewe umekuwa kwao kama wimbo mzuri sana, wa mtu mwenye sauti ipendezayo, awezaye kupiga kinanda vizuri; maana, wasikia maneno yako, lakini hawayatendi.” (Ezekieli 33:30-32) Watu wa siku za Isaya pia wanadai eti wanamtafuta Yehova daima, lakini hawatii maneno yake.

      Kufunga Kula kwa Njia ya Unafiki

      5. Wayahudi wanajaribu kukubaliwa na Mungu kwa kufanya nini, na Yehova anaitikiaje?

      5 Wayahudi wanajitahidi kukubaliwa na Mungu kwa kufuata desturi ya kufunga kula, lakini uchaji wao wa kusingizia unazidi tu kuwatenganisha na Yehova. Na inaonekana wanatatanika fikira, kwani wanauliza hivi: “Ya nini tufunge chakula usipoona? Ya nini tujitese usipoangalia?” Naye Yehova anawaambia hivi bila kuwaficha neno: “Siku za kufunga mwafanya biashara [“mlikuwa mkijifurahisha,” “NW”], na kuwalemea wote watendao kazi kwenu. Lakini, pale mfungapo, mwabishana na kugombana, na kumpiga ngumi maskini. Siyo mifungo kama hiyo ya leo itakayozifikisha sauti zenu huko juu. Je, huo ndio mfungo unaonipendeza, ndiyo siku mtu anapojikatalia? Kuinama kichwa kama tete, kujilaza juu ya gunia au majivu? Ndiyo hayo usemayo ni mfungo, ni siku ya kumpendeza Bwana?”—Isaya 58:3-5, “Verbum Bible,” chapa ya 1996.

      6. Ni vitendo gani vya Wayahudi vinavyoonyesha kwamba wanafunga kwa unafiki?

      6 Watu hao wanafunga kula, wanajifanya wenye haki, na hata wanaomba Yehova awafanyie hukumu za haki, huku wao wakifuatia raha kwa ubinafsi na kuendesha biashara zao. Wanagombana, wanakandamizana, na kufanya fujo. Wanajaribu kuficha mwenendo wao kwa kujifanya-fanya eti wanaomboleza—huku wakiinamisha vichwa kwa kunyong’onyea kama matete yaliyodhoofika, kisha wanakalia magunia na majivu—eti wametubu dhambi zao. Hayo yote ni ya faida gani ikiwa wanaendelea kuasi? Hawaonyeshi majonzi yoyote wala toba ya kimungu inayopasa kuambatana na mifungo ya moyo mweupe. Ingawa wanapiga mayowe makubwa, hayasikiki mbinguni.

      7. Wayahudi wa wakati wa Yesu walionyeshaje unafiki, na watu wengi leo huonyeshaje unafiki huo huo?

      7 Wayahudi wa siku za Yesu walikuwa na hali hiyo hiyo ya kujionyesha eti wanafuata desturi rasmi ya kufunga kula. Wengine wao hata walifanya hivyo mara mbili kwa juma! (Mathayo 6:16-18; Luka 18:11, 12) Vilevile, viongozi wengi wa kidini waliiga kizazi cha Isaya kwa kuwa wakali mno na kupiga ubwana. Kwa hiyo, Yesu aliwafichua wanafiki hao wa kidini kwa ushujaa, akawaambia kwamba njia yao ya kuabudu ilikuwa ya bure. (Mathayo 15:7-9) Leo, pia, mamilioni ya watu “hutangaza hadharani wamjua Mungu, lakini wao humkana yeye kwa kazi zao, kwa sababu ni wa kuchukiza na wasiotii na waliokataliwa kwa ajili ya kazi njema ya namna yoyote.” (Tito 1:16) Huenda watu wa jinsi hiyo wakatumainia kupata rehema ya Mungu, lakini mwenendo wao unaonyesha kwamba hawana moyo mweupe. Lakini Mashahidi wa Yehova ni tofauti, kwani wao huonyesha ujitoaji-kimungu wa kweli na upendo halisi wa kidugu.—Yohana 13:35.

      Yanayohusika Katika Toba ya Kweli

      8, 9. Ni vitendo gani vinavyofaa vinavyopaswa kuandamana na toba ya moyo mweupe?

      8 Licha ya Yehova kutaka watu wake wafunge kwa sababu ya dhambi zao, anataka watubu pia. Kisha watapata kibali chake. (Ezekieli 18:23, 32) Anaeleza kwamba kufunga kunaweza kuwa na maana ikiwa pia dhambi za wakati uliopita zitarekebishwa. Yafikirie maswali ya kupekua moyo ambayo Yehova anauliza: “Je! saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?”—Isaya 58:6.

      9 Vifungo na nira ni ishara zinazofaa sana za utumwa mkatili. Kwa hiyo, badala ya kufunga na huku wanawakandamiza waamini wenzao, watu hao wanapaswa kutii amri hii: “Umpende jirani yako kama nafsi yako.” (Mambo ya Walawi 19:18) Wanapaswa kuwafungua watu wote ambao wao wamewakandamiza na kuwatumikisha bila haki.a Vitendo vya kidini vya kujionyesha, kama vile kufunga kula, haviwezi kuchukua mahali pa ujitoaji halisi wa kimungu. Wala haviwezi kuchukua mahali pa vitendo vinavyoonyesha upendo wa kidugu. Nabii Mika, mtu aliyeishi wakati mmoja na Isaya, anaandika hivi: “BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!”—Mika 6:8.

      10, 11. (a) Ingekuwa afadhali Wayahudi wafanye nini kuliko kufunga kula? (b) Wakristo leo wanaweza kulitumiaje shauri ambalo Yehova aliwapa Wayahudi?

      10 Ili kutimiza haki, fadhili, na kiasi, inafaa kutendea wengine mema, na hiyo hasa ndiyo maana kuu ya Sheria ya Yehova. (Mathayo 7:12) Ingekuwa afadhali washiriki mali zao nyingi pamoja na wenye uhitaji, badala ya kufunga tu. Yehova anauliza hivi: “Je! [kufunga ninakochagua mimi] siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?” (Isaya 58:7) Naam, wale walio na uwezo wanapaswa kuwasaidia wakaaji wenzao wa Yuda, yaani watu wa damu moja nao, kwa kuwapa chakula, nguo, au makao, badala ya kujionyesha kuwa wanafunga.

      11 Kanuni hizo maridadi za upendo na huruma ya kidugu zilizotamkwa na Yehova hazihusu Wayahudi wa wakati wa Isaya tu. Zinawapa Wakristo pia mwongozo. Kwa hiyo, mtume Paulo aliandika hivi: “Basi, kwa kweli maadamu tuna wakati wenye kufaa kwa ajili ya hilo, acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote, lakini hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Wagalatia 6:10) Ni lazima kutaniko la Kikristo liwe makao salama yenye upendo na shauku ya kidugu, hasa kwa sababu nyakati zetu zinazidi kuwa za hatari.—2 Timotheo 3:1; Yakobo 1:27.

      Utii Huleta Baraka Nyingi

      12. Yehova atafanya nini watu wake wakimtii?

      12 Laiti watu wa Yehova wangekuwa na ufahamu wa kina kirefu waweze kusikiza karipio lake lenye upendo! Yehova anasema hivi: “Ndipo nuru yako itakapopambazuka [“mtang’ara kama pambazuko,” “BHN”] kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde. Ndipo utaita, na BWANA ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa.” (Isaya 58:8, 9a) Hayo ni maneno ya kuchangamsha na kuvutia kama nini! Yehova huwabariki na kuwalinda wale wanaopendezwa na fadhili za upendo na haki. Watu wa Yehova wakitubu matendo yao yenye ukali na unafiki, kisha wamtii, mambo yao yatang’ara zaidi. Yehova atawapa “afya,” yaani taifa hilo litapona kiroho na kimwili. Vilevile atawalinda kama vile alivyowalinda baba zao wa zamani walipokuwa wakiondoka Misri. Tena atajibu vilio vyao vya msaada bila kukawia.—Kutoka 14:19, 20, 31.

      13. Ni baraka zipi zinazowangoja Wayahudi ikiwa wataitikia himizo la Yehova?

      13 Sasa Yehova anaongeza jambo jingine kwenye himizo lake lililotangulia. Anasema hivi: “Kama ukiiondoa nira [ya utumwa mkali sana, wenye dhuluma]; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole [yawezekana kwa madharau au mashtaka ya uwongo], wala kunena maovu; na kama ukimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi yako, na kuishibisha nafsi iliyoteswa; ndipo nuru yako itakapopambazuka gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri.” (Isaya 58:9b, 10) Ubinafsi na ukali hauna faida yoyote na huleta ghadhabu ya Yehova. Hata hivyo, matendo ya fadhili na ukarimu hubarikiwa sana na Mungu, hasa iwapo wanaotendewa hayo ni wenye njaa na wenye kuteseka. Laiti Wayahudi wangezitia maanani kweli hizo! Ndipo uangavu na ufanisi wao wa kiroho ungeng’aa kama jua la adhuhuri na kufukuzia mbali giza lolote. Zaidi ya yote, Yehova, aliye Chanzo cha utukufu wao na baraka zao, angeheshimiwa na kusifiwa.—1 Wafalme 8:41-43.

      Taifa Larudishwa

      14. (a) Watu wa siku za Isaya wanaitikiaje maneno yake? (b) Yehova anaendelea kutoa nini?

      14 Kwa kusikitisha, taifa hilo linapuuza himizo la Yehova na kujibwaga ndani ya uovu mwingi zaidi. Hatimaye, wanafanya Yehova alazimike kuwapeleka uhamishoni, sawa na vile alivyowaonya. (Kumbukumbu la Torati 28:15, 36, 37, 64, 65) Na bado, maneno ambayo Yehova anasema baada ya hapo kupitia Isaya yanaendelea kutoa tumaini. Mungu anatabiri kwamba mabaki wenye majuto, waliotiwa nidhamu, watairudia nchi ya Yuda kwa shangwe hata ingawa imekaa hali ya ukiwa.

      15. Yehova anatabiri tukio gani la kurudishwa kwenye shangwe?

      15 Yehova anamtumia Isaya kusema yafuatayo kuonyesha kimbele tukio la kurudishwa kwa watu wake mwaka wa 537 K.W.K.: “BWANA atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.” (Isaya 58:11) Yehova atarudisha uzuri wa nchi ya Waisraeli iliyounguzwa na joto kali hata iwe na mazao ya kunawiri sana. Halafu we! atawabariki watu wake waliotubu, atie nguvu “mifupa” yao iache kukosa uhai wa kiroho, iimarike kabisa. (Ezekieli 37:1-14) Watu hao wenyewe watakuwa kama “bustani iliyotiwa maji,” yenye matunda tele ya kiroho.

      16. Nchi itarudishiwaje hali yake ya kwanza?

      16 Tukio hilo la kurudishwa litahusu pia kujenga upya majiji yaliyoharibiwa na wavamizi Wababiloni mwaka wa 607 K.W.K. “Watu wako watapajenga mahali palipokuwa ukiwa; utaiinua misingi ya vizazi vingi; nawe utaitwa, Mwenye kutengeneza mahali palipobomoka; na, Mwenye kurejeza njia za kukalia.” (Isaya 58:12) Semi hizo zinazolingana, yaani “mahali palipokuwa ukiwa” na “misingi ya vizazi vingi” (au, misingi ambayo imekuwa magofu muda wa vizazi vingi), zinaonyesha kwamba mabaki waliorudishwa watajenga upya majiji ya Yuda yaliyofanywa magofu, hasa Yerusalemu. (Nehemia 2:5; 12:27; Isaya 44:28) Watatengeneza “mahali palipobomoka,” maana yake sehemu zilizoharibika za kuta za Yerusalemu, na bila shaka za majiji mengine pia.—Yeremia 31:38-40; Amosi 9:14.

      Baraka Zinazotokana na Kuadhimisha Sabato kwa Uaminifu

      17. Yehova anawasihije watu wake wazitii sheria za Sabato?

      17 Sabato ilikuwa wonyesho wa jinsi ambavyo Mungu huhangaikia sana masilahi ya kimwili na ya kiroho ya watu wake. Yesu alisema hivi: “Sabato ilikuja kuwako kwa ajili ya binadamu.” (Marko 2:27) Siku hiyo iliyotakaswa na Yehova iliwapa Waisraeli nafasi ya pekee ya kuonyesha kwamba wanampenda Mungu. Kwa kuhuzunisha, kufikia wakati wa Isaya siku hiyo imekwisha zorota ikawa ya kufuata desturi tupu na kujihusisha katika tamaa za ubinafsi. Basi, kwa mara nyingine Yehova ana sababu nzuri ya kuwashutumu vikali watu wake. Na kwa mara nyingine tena, anajaribu kuifikia mioyo yao. Anasema hivi: “Kama ukigeuza mguu wako usihalifu sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya BWANA yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe; ndipo utakapojifurahisha katika BWANA; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha BWANA kimenena hayo.”—Isaya 58:13, 14.

      18. Kutakuwa na matokeo gani kwa sababu Yuda ameshindwa kuiheshimu Sabato?

      18 Sabato ni siku iliyowekwa ili watu watafakari mambo ya kiroho, wasali, na kuabudu pamoja wakiwa familia nzima. Yapasa kuwasaidia Wayahudi wafikiri juu ya matendo ya ajabu ambayo Yehova amewafanyia, na juu ya haki na upendo unaoonyeshwa wazi katika Sheria yake. Hivyo, watu hao wanapaswa kumkaribia Mungu zaidi kwa kuadhimisha siku hiyo takatifu kwa uaminifu. Badala ya kufanya hivyo, wanaipotosha Sabato, na kwa hiyo wamo katika hatari ya kutengwa mbali wasipokee baraka ya Yehova.—Mambo ya Walawi 26:34; 2 Mambo ya Nyakati 36:21.

      19. Ikiwa watu wa Mungu watageuka waanze kushika Sabato, watapata baraka zipi?

      19 Na bado, Wayahudi wakijifunza kutokana na nidhamu hiyo kisha wageuke na kuanza kuuheshimu mpango wa Sabato, watapata baraka nyingi. Matokeo mema ya kufuata ibada ya kweli na kuiheshimu Sabato yatafurika yaenee katika sehemu zote za maisha yao. (Kumbukumbu la Torati 28:1-13; Zaburi 19:7-11) Kwa mfano, Yehova atawafanya watu wake ‘wapande mahali pa nchi palipoinuka.’ Usemi huo unamaanisha kupata usalama na kuwashinda maadui. Yule anayefaulu kusimamia mahali palipoinuka, yaani vilima na milima, ndiye anayefaulu kuisimamia nchi. (Kumbukumbu la Torati 32:13; 33:29) Wakati mmoja Israeli walimtii Yehova, na taifa hilo lilifurahia ulinzi wake na kuheshimiwa, hata kuogopwa, na mataifa mengine. (Yoshua 2:9-11; 1 Wafalme 4:20, 21) Wakimgeukia Yehova tena kwa kumtii, watarudishiwa kiasi fulani cha utukufu huo wa zamani. Yehova atawapa watu wake sehemu kamili ya “urithi wa Yakobo,” yaani zile baraka zilizoahidiwa kupitia agano Lake na baba zao wa zamani, na hasa baraka ya kumiliki Nchi ya Ahadi bila wasiwasi wowote.—Zaburi 105:8-11.

      20. Wakristo wana ‘pumziko gani la sabato’?

      20 Je, Wakristo wanaweza kujifunza somo hapo? Yesu Kristo alipokufa, Sheria ya Kimusa iliondolewa mbali, pamoja na matakwa yake ya Sabato. (Wakolosai 2:16, 17) Hata hivyo, bado ni muhimu waabudu wa Yehova wawe na roho ile ambayo uadhimishaji wa Sabato ungalipaswa kuwahimiza watu wawe nayo, yaani roho ya kutanguliza masilahi ya kiroho na kumkaribia Yehova. (Mathayo 6:33; Yakobo 4:8) Zaidi ya hilo, Paulo anasema hivi katika barua yake kwa Waebrania: “Kumebaki pumziko la sabato kwa watu wa Mungu.” Wakristo huingia katika ‘pumziko hilo la sabato’ kwa kumtii Yehova na kufuatia uadilifu kwa kuonyesha imani katika damu iliyomwagwa ya Yesu Kristo. (Waebrania 3:12, 18, 19; 4:6, 9-11, 14-16) Aina hiyo ya mwadhimisho wa sabato hufanywa na Wakristo kila siku, wala si mara moja tu kwa juma.—Wakolosai 3:23, 24.

      Israeli wa Kiroho ‘Apanda Mahali pa Nchi Palipoinuka’

      21, 22. Yehova amefanyaje Israeli wa Mungu ‘apande mahali pa nchi palipoinuka’?

      21 Tangu wakati ambao Wakristo watiwa-mafuta walifunguliwa kutoka katika utekwa wa Kibabiloni mwaka wa 1919, wameadhimisha kwa uaminifu jambo ambalo Sabato ilikuwa kivuli chake. Tokeo ni kwamba, Yehova amewafanya ‘wapande mahali pa nchi palipoinuka.’ Katika maana gani? Kule nyuma mwaka wa 1513 K.W.K., Yehova alifanya agano na wazao wa Abrahamu kwamba, ikiwa wangetii, wangekuwa ufalme wa makuhani na taifa takatifu. (Kutoka 19:5, 6) Yehova aliwabeba wakiwa salama muda wote wa ile miaka 40 ya kuwa jangwani, kama vile tai anavyowabeba makinda wake. Yehova aliwabariki kwa kuwaandalia vitu vingi sana. (Kumbukumbu la Torati 32:10-12) Hata hivyo, taifa hilo halikuwa na imani, na mwishowe lilipoteza mapendeleo yote ambayo lingaliweza kuyapata. Ijapokuwa hivyo, Yehova ana ufalme wa makuhani leo. Ufalme huo ni Israeli wa kiroho wa Mungu.—Wagalatia 6:16; 1 Petro 2:9.

      22 Katika “wakati wa mwisho,” taifa hili la kiroho limefanya jambo lile ambalo Israeli wa kale walishindwa kufanya. Wamedumisha imani yao kwa Yehova. (Danieli 8:17) Wakati washirika wake wanafuata sana viwango vya Yehova vya hali ya juu na njia zake zilizotukuka, Yehova naye anawainua juu katika maana ya kiroho. (Mithali 4:4, 5, 8; Ufunuo 11:12) Kwa kuwa wanalindwa wasipatwe na uchafu unaowazunguka, wanafurahia maisha ya hali ya juu. Na badala ya kufuata njia zao wenyewe tu, wao ‘wanajifurahisha kwa Yehova’ na Neno lake. (Zaburi 37:4) Yehova amewatunza wakawa salama kiroho ijapokuwa wamepingwa vikali ulimwenguni pote. Tangu mwaka wa 1919, “nchi” yao ya kiroho haijaharibiwa hata kidogo. (Isaya 66:8) Wanaendelea kuwa taifa la watu wanaowakilisha jina lake tukufu, wakilitangaza kwa shangwe ulimwenguni kote. (Kumbukumbu la Torati 32:3; Matendo 15:14) Isitoshe, sasa idadi inayoongezeka ya watu watiifu kutoka mataifa yote inashirikiana nao katika pendeleo tukufu la kufundishwa njia za Yehova na kusaidiwa kutembea katika mapito yake.

      23. Ni jinsi gani Yehova ‘amewalisha urithi wa Yakobo’ watumishi wake watiwa-mafuta?

      23 Yehova ‘amewalisha urithi wa Yakobo’ watumishi wake watiwa-mafuta. Isaka alipombariki Yakobo badala ya Esau, maneno ya mzee huyo wa ukoo yalitabiri kwamba wale wote ambao wangedhihirisha imani katika Mbegu iliyoahidiwa ya Abrahamu wangepata baraka nyingi. (Mwanzo 27:27-29; Wagalatia 3:16, 17) Wakristo watiwa-mafuta na waandamani wao ni kama Yakobo, wala si kama Esau, kwani ‘wanathamini mambo matakatifu,’ na hasa chakula cha kiroho ambacho Mungu hugawa kwa wingi. (Waebrania 12:16, 17; Mathayo 4:4) Chakula hiki cha kiroho—kinachohusisha ujuzi wa mambo ambayo Yehova anatimiza kupitia Mbegu iliyoahidiwa, na pia kupitia washirika wa Mbegu hiyo—kinawaimarisha na kuwatia nguvu, tena ni muhimu kwa uhai wao wa kiroho. Basi, ni muhimu sana kwamba waendelee kutwaa lishe ya kiroho daima kwa kusoma Neno la Mungu na kulitafakari. (Zaburi 1:1-3) Ni lazima washirikiane na waamini wenzao kwenye mikutano ya Kikristo. Tena ni jambo la maana sana waunge mkono viwango vya juu vya ibada safi, huku wakiwagawia wengine lishe hiyo kwa shangwe.

      24. Wakristo wa kweli wanaenendaje leo?

      24 Wakristo wa kweli na waendelee kukataa katakata unafiki wa aina zote, huku wakingojea utimizo wa ahadi za Yehova kwa hamu. Wakati wanapolishwa ‘urithi wa Yakobo,’ na waendelee kufurahia usalama wa kiroho wakiwa katika ‘mahali pa nchi palipoinuka.’

      [Maelezo ya Chini]

      a Yehova aliwafanyia watu wake uandalizi wa kujiuza utumwani iwapo walitumbukia katika deni—wakawa hasa wafanya-kazi wa kuajiriwa—ili kulipia madeni yao. (Mambo ya Walawi 25:39-43) Hata hivyo, Sheria ilitaka kwamba watumwa watendewe fadhili. Wale waliotendwa ukatili walipaswa kuachiliwa huru.—Kutoka 21:2, 3, 26, 27; Kumbukumbu la Torati 15:12-15.

      [Picha katika ukurasa wa 278]

      Wayahudi walifunga na kuinamisha vichwa kwa toba ya kujifanya—lakini hawakubadili njia zao

      [Picha katika ukurasa wa 283]

      Walio na uwezo huwapa wenye uhitaji makao, nguo, au chakula

      [Picha katika ukurasa wa 286]

      Yuda akitubu, atajenga upya majiji yake yaliyofanywa ukiwa

  • Mkono wa Yehova Haujawa Mfupi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini

      Mkono wa Yehova Haujawa Mfupi

      Isaya 59:1-21

      1. Hali ikoje katika Yuda, na watu wengi wanashangaa wakijiulizaje?

      TAIFA la Yuda linadai eti lina uhusiano wa agano pamoja na Yehova. Hata hivyo, kila mahali ni matata tu. Haki ni haba. Uhalifu na ukandamizaji umeenea kila mahali. Na hali bora haziji kama ilivyotumainiwa. Kuna kasoro kubwa mahali fulani. Watu wengi wanashangaa wakijiuliza kama Yehova atarekebisha mambo. Hiyo ndiyo hali ya siku za Isaya. Lakini masimulizi ya Isaya kuhusu wakati huo si historia ya kale tu. Maneno yake yana maonyo ya kiunabii kwa watu wowote wanaodai eti wanamwabudu Mungu na kumbe wanapuuza sheria Zake. Na ule unabii ulioandikwa katika Isaya sura ya 59 unawapa kitia-moyo kichangamfu wale wote wanaojitahidi kumtumikia Yehova ijapokuwa wanaishi katika nyakati za magumu na hatari.

      Watenganishwa na Mungu wa Kweli

      2, 3. Kwa nini Yehova halindi Yuda?

      2 Ebu wazia—watu wa agano la Yehova wamerudi nyuma wakawa waasi-imani! Wamempa kisogo Mfanyi wao, wakajiondoa chini ya mkono wake wa ulinzi. Basi wanasononeka vikali. Je, labda wanamlaumu Yehova kwa magumu yanayowapata? Isaya anawaambia hivi: “Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka [“haujawa mfupi ,” “NW”], hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.”—Isaya 59:1, 2.

      3 Maneno hayo yamesemwa kinagaubaga, lakini ni ya kweli. Yehova angali Mungu wa wokovu. Kwa kuwa ndiye “Msikiaji wa sala,” Yeye husikiliza sala za watumishi wake waaminifu. (Zaburi 65:2, NW) Hata hivyo, hawabariki wakosaji. Watu hao wenyewe ndio wamefanya Yehova awatenganishe naye. Uovu wao wenyewe umemfanya afiche uso wake wasiuone.

      4. Yuda anashtakiwa mambo gani?

      4 Ukweli ni kwamba, matendo ya Yuda yamekuwa mabaya sana. Unabii wa Isaya unaorodhesha baadhi ya mashtaka yanayomkabili: “Mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.” (Isaya 59:3) Watu wanasema uwongo na mambo yasiyo ya haki. Usemi unaotaja ‘mikono iliyotiwa unajisi kwa damu’ unaonyesha kwamba wengine hata wameua. Loo, tendo hilo linamvunjia Mungu heshima kama nini, kwani, licha ya kukataza uuaji, yeye hukataza pia ‘kumchukia ndugu yako moyoni mwako’! (Mambo ya Walawi 19:17) Ile hali ya wakaaji wa Yuda ya kutenda dhambi bila kujizuia, na matokeo yasiyoepukika yanayowapata kwa sababu ya dhambi hiyo, inapasa kumkumbusha kila mmoja wetu leo kwamba tunahitaji kudhibiti mawazo na hisia zetu zenye dhambi. Ama sivyo, mwishowe tungeweza kufanya maovu ambayo yangetutenganisha na Mungu.—Waroma 12:9; Wagalatia 5:15; Yakobo 1:14, 15.

      5. Ufisadi wa Yuda umekuwa wa kadiri gani?

      5 Dhambi imeambukiza taifa zima kama ugonjwa. “Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.” (Isaya 59:4) Hakuna mtu anayesema mambo ya haki. Hata katika mahakama, ni nadra kupata mtu wa kutegemeka au aliye mwaminifu. Yuda amempa Yehova kisogo na kutumainia kupata msaada kwa kuungana na mataifa, hata anatumainia sanamu zisizo na uhai. Sanamu zote hizo ni “duni,” bure kabisa. (Isaya 40:17, 23; 41:29) Matokeo ni kwamba, wanapiga domo sana, wakisema upuuzi mtupu. Mipango inapangwa, lakini inapanguka na kuleta matata na madhara.

      6. Matendo ya Jumuiya ya Wakristo yanafananaje na yale ya Yuda?

      6 Ukosefu wa uadilifu na fujo zilizokuwa katika Yuda zina ulinganifu wa ajabu na zile zilizo katika Jumuiya ya Wakristo. (Ona “Jiji la Yerusalemu Lenye Uasi-Imani Linalingana na Jumuiya ya Wakristo,” katika ukurasa wa 294.) Vita viwili vikali vya ulimwengu vimepiganwa baina ya mataifa ambayo husemwa eti ni ya Kikristo. Hata sasa, ibada ya Jumuiya ya Wakristo imeshindwa kukomesha mauaji ya kufagilia mbali makabila fulani, na kuchinjana miongoni mwa washirika wake. (2 Timotheo 3:5) Ingawa Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuutumaini Ufalme wa Mungu, mataifa ya Jumuiya ya Wakristo yanaendelea kutegemea silaha nyingi za kijeshi zilizojazana akibani, na kufanya mapatano ya kisiasa. (Mathayo 6:10) Kwa kweli, wengi wa watengenezaji wakuu wa silaha ulimwenguni wanapatikana katika mataifa ya Jumuiya ya Wakristo! Naam, hata Jumuiya ya Wakristo inatumainia “ubatili” kwa kutumainia jitihada za wanadamu na mashirika ili kupata usalama wa wakati ujao.

      Kuvuna Matokeo Machungu

      7. Kwa nini mbinu za Yuda zinatokeza madhara matupu?

      7 Ibada ya sanamu na udanganyifu haziwezi kufanyiza jamii yenye hali njema. Sasa Wayahudi wasio waaminifu wanavuna matata ya mbegu walizopanda wenyewe kwa kutumainia jitihada za kibinadamu. Tunasoma hivi: “Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.” (Isaya 59:5) Tangu kutungwa hadi kutunguliwa, mbinu za Yuda hazifanikiwi kamwe. Kuwaza kwao kubaya kunaleta madhara matupu. Ni sawa na vile tu mayai ya nyoka mwenye sumu yanavyoangua nyoka wenye sumu. Basi taifa linateseka.

      8. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yuda ana kasoro katika kuwaza kwake?

      8 Wakaaji fulani wa Yuda wanaweza kufanya fujo ili wajilinde, lakini hawatafanikiwa. Kutumia mabavu hakuwezi kuwa bora kuliko kumtumainia Yehova na kufanya matendo ya uadilifu; ni kama vile tando za buibui zisivyoweza kuwa bora kuliko vazi la kujilinda na hali mbaya ya hewa. Isaya anatangaza hivi: “Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao. Miguu yao hukimbilia mayai [“ubaya,” “NW”], nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.” (Isaya 59:6, 7) Yuda ana kasoro katika kuwaza kwake. Kwa kufanya fujo eti ajaribu kutatua matatizo yake, anaonyesha mwelekeo wa kutomwogopa Mungu. Hata kama wengi wa wale wanaoumizwa na fujo zake ni watu wasio na hatia, na hata kama baadhi yao ni watumishi halisi wa Mungu, ni shauri lao, yeye hajali.

      9. Kwa nini amani ya kweli imewaponyoka kabisa viongozi wa Jumuiya ya Wakristo?

      9 Maneno haya yaliyopuliziwa yanatukumbusha jinsi ambavyo Jumuiya ya Wakristo imemwaga damu. Hakika, Yehova atamtoza hesabu kwa kuwakilisha Ukristo vibaya sana! Jumuiya ya Wakristo imefuatia mwendo ulio mpotovu kama wa Wayahudi wa siku za Isaya kwa sababu viongozi wake wanaamini kwamba huo tu ndio mwendo unaofaa. Huku wanasema amani, na huku wanatenda matendo yasiyo ya haki. Jamani, unafiki gani huo! Amani ya kweli itazidi tu kuwaponyoka kabisa viongozi wa Jumuiya ya Wakristo, maadamu wanaendelea kutumia mbinu hiyo. Ni kama vile unabii unavyoendelea kusema: “Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.”—Isaya 59:8.

      Kutanga-tanga Katika Giza la Kiroho

      10. Isaya anafanya ungamo gani kwa niaba ya Yuda?

      10 Yehova hawezi kuzibariki njia za Yuda zilizo kombokombo na zenye uharibifu. (Zaburi 11:5) Hivyo basi, akiongea kwa niaba ya taifa zima, Isaya anaungama hatia ya Yuda: “Hukumu ya haki i mbali nasi, wala haki haitufikilii; twatazamia nuru, na kumbe! latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu. Twapapasa-papasa kutafuta ukuta kama kipofu, naam, twapapasa kama watu wasio na macho; twajikwaa wakati wa adhuhuri, kana kwamba ni wakati wa ukungu wa alfajiri; kati yao waliowanda tumekuwa kama wafu. Sisi sote twanguruma [“tunaendelea kuguna,” “NW”] kama dubu; twaomboleza kama hua.” (Isaya 59:9-11a) Wayahudi hawajaacha Neno la Mungu liwe taa kwa miguu yao na mwanga kwa njia yao. (Zaburi 119:105) Matokeo ni kwamba, mambo yao yanaonekana kuwa yenye giza. Hata kukiwa kweupe kabisa wakati wa adhuhuri, wanapapasa-papasa kana kwamba ni usiku. Ni kana kwamba wao ni wafu. Wanatamani sana kitulizo, kwa hiyo wanaguna kwa sauti kubwa kama madubu wenye njaa au waliojeruhiwa. Wengine wao wanalia-lia kwa kuomboleza kama njiwa wapweke.

      11. Kwa nini matumaini ya Yuda ya kupata haki na wokovu ni ya bure?

      11 Isaya anajua vizuri sana kwamba shida za Yuda zimetokana na kumwasi Mungu. Anasema hivi: “Twatazamia hukumu ya haki, lakini hapana; na wokovu, lakini u mbali nasi. Maana makosa yetu yamezidi kuwa mengi mbele zako, na dhambi zetu zashuhudia juu yetu; maana makosa yetu tunayo pamoja nasi, na maovu yetu tumeyajua; katika kukosa na kumkana BWANA, na katika kugeuka tusimfuate Mungu wetu, tukinena jeuri na uasi, na kukusudia maneno ya uongo na kuyatoa moyoni.” (Isaya 59:11b-13) Kwa kuwa wakaaji wa Yuda hawajatubu, bado wanahesabiwa ubaya wa dhambi walizotenda. Haki imeondoka nchini kwa sababu watu wamemwacha Yehova. Wamekuwa waongo wa mwisho, hata huwakandamiza ndugu zao. Ni sawasawa kabisa na wale waliomo katika Jumuiya ya Wakristo leo! Si kwamba tu wengi wanapuuza haki, bali pia wanawanyanyasa Mashahidi waaminifu wa Yehova wanaojaribu kufanya mapenzi ya Mungu.

      Yehova Afanya Hukumu

      12. Wenye madaraka ya kusimamia kufikilizwa kwa haki katika Yuda wana mtazamo gani?

      12 Inaonekana hakuna haki, uadilifu, wala ukweli katika Yuda. “Hukumu imegeuka ikaenda nyuma, na haki inasimama mbali sana; maana kweli imeanguka katika njia kuu [“uwanja wa umma,” “NW”] na unyofu hauwezi kuingia.” (Isaya 59:14) Nyuma ya malango ya jiji katika Yuda, kuna viwanja vya umma ambapo wanaume wazee wanakutana kuzungumzia kesi. (Ruthu 4:1, 2, 11) Wanaume hao wanapaswa kuhukumu kwa uadilifu na kufuatia haki, wala si kukubali rushwa. (Kumbukumbu la Torati 16:18-20) Lakini wanahukumu kulingana na tamaa zao wenyewe zenye ubinafsi. Ubaya zaidi ni kwamba, wanaona ni rahisi kuwanasa watu wowote wanaojaribu kutenda mema kwa moyo mweupe. Tunasoma hivi: “Kweli imepunguka kabisa, na yeye auachaye uovu ajifanya kuwa mateka.”—Isaya 59:15a.

      13. Yehova atafanya nini kwa kuwa mahakimu wa Yuda wanafanya kazi yao kizembe?

      13 Wale wanaoshindwa kutoa sauti ya kupinga upotovu wa maadili wanasahau kwamba Mungu si kipofu, si mjinga, wala si mnyonge. Isaya anaandika hivi: “BWANA akaona hayo, akachukizwa kwa kuwa hapana hukumu ya haki. Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi; basi, mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu; na haki yake ndiyo iliyomsaidia.” (Isaya 59:15b, 16) Kwa kuwa mahakimu waliowekwa wanafanya kazi yao kizembe, Yehova ataingilia mambo. Wakati atakapofanya hivyo, atatenda kwa uadilifu na kwa uwezo.

      14. (a) Watu wengi leo wana mtazamo gani? (b) Yehova anajitayarishaje kuchukua hatua?

      14 Leo kuna hali inayofanana na hiyo. Tunaishi katika ulimwengu ambamo watu wengi ‘wamekwisha kuishiwa na hisia zote za adili.’ (Waefeso 4:19) Watu wengi hawaamini kwamba Yehova ataingilia mambo ili kukomesha uovu duniani. Lakini unabii wa Isaya unaonyesha kwamba Yehova hufuatilia kwa makini mambo ya kibinadamu. Yeye hufanya hukumu, naye huchukua hatua zinazolingana na hukumu zake katika wakati wake mwenyewe. Je, hukumu zake ni za haki? Isaya anaonyesha kwamba ni za haki. Anaandika hivi kuhusu taifa la Yuda: “[Yehova] akajivika haki kama deraya kifuani, na chapeo cha wokovu kichwani pake, akajivika mavazi ya kisasi yawe mavazi yake, naye alivikwa wivu kama joho.” (Isaya 59:17) Maneno haya ya kiunabii yanaonyesha Yehova akiwa shujaa anayejiandaa kwa ajili ya pigano. Ameazimia kabisa kuleta wokovu aliokusudia. Ana uhakika kwamba uadilifu wake mwenyewe ni kamili na hauwezi kushindwa. Na atafanya hukumu zake kwa bidii na bila woga. Hakuna shaka kwamba haki itashinda.

      15. (a) Wakristo wa kweli wataenendaje wakati Yehova afanyapo hukumu? (b) Ni nini linaloweza kusemwa juu ya hukumu za Yehova?

      15 Leo katika nchi fulani fulani, maadui wasiotaka ile kweli wanajaribu kuzuia kazi ya watumishi wa Yehova kwa kueneza propaganda za uwongo na zenye kuwaharibia jina. Wakristo wa kweli hawasiti-siti kuitetea kweli, lakini hawatafuti kamwe kujilipizia kisasi. (Waroma 12:19) Hata wakati Yehova atakapomaliza kisa chake na Jumuiya ya Wakristo yenye uasi-imani, waabudu wa Yehova duniani hawatashiriki kuharibu jumuiya hiyo. Wanajua kwamba Yehova amejiwekea haki ya kulipiza kisasi, na kwamba atachukua hatua ifaayo wakati ufikapo. Unabii unatuhakikishia hivi: “Kadiri ya matendo yao, kwa kadiri iyo hiyo atawalipa, ukali kwao wampingao, malipo kwa adui zake; naye atavirudishia visiwa malipo.” (Isaya 59:18) Hukumu za Mungu zitakuwa za haki, lakini pia zitakuwa kamili kama katika siku za Isaya. Hata zitafika ‘visiwani,’ sehemu za mbali. Hakuna mtu atakayekuwa mbali au kando sana asiweze kufikiwa na hukumu za Yehova.

      16. Ni nani watakaookoka hukumu za Yehova, na watajifunza nini kutokana na kuokoka kwao?

      16 Yehova anawahukumu kwa uadilifu wale wanaojitahidi kufanya yaliyo sawa. Isaya anatabiri kwamba kuanzia pembe moja ya nchi hadi pembe nyingine—kwenye mapana na marefu yote ya dunia—watu wa jinsi hiyo wataokoka. Halafu ulinzi watakaopewa na Yehova utaimarisha sana kicho na heshima wanayompa. (Malaki 1:11) Tunasoma hivi: “Wataliogopa jina la BWANA toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya BWANA.” (Isaya 59:19) Roho ya Yehova itaondoa vipingamizi vyote vinavyozuia kutimizwa kwa mapenzi yake, kama dhoruba yenye nguvu inayosukuma mafuriko makubwa ya maji ya uharibifu na kufagilia mbali vitu vyote vilivyo njiani. Roho ya Yehova ina nguvu nyingi kuliko nguvu yoyote ya mwanadamu. Atakapoitumia kufanya hukumu juu ya wanadamu na mataifa, atapata mafanikio yaliyo hakika na kamili.

      Tumaini na Baraka kwa Wenye Kutubu

      17. Mkombozi wa Sayuni ni nani, na anakomboa Sayuni lini?

      17 Chini ya Sheria ya Musa, Mwisraeli aliyejiuza utumwani angeweza kununuliwa na mkombozi ili atoke utumwani. Mapema katika kitabu cha unabii cha Isaya, Yehova ameonyeshwa kuwa Mkombozi wa watu mmoja-mmoja wanaotubu. (Isaya 48:17) Sasa anaelezwa tena kuwa Mkombozi wa watu wanaotubu. Isaya anaandika hivi kuhusu ahadi ya Yehova: “Mkombozi atakuja Sayuni, kwao waachao maasi yao katika Yakobo, asema BWANA.” (Isaya 59:20) Ahadi hiyo yenye kutuliza moyo inatimizwa mwaka wa 537 K.W.K. Lakini ina utimizo zaidi. Mtume Paulo alinukuu maneno hayo katika fasiri ya Septuagint, akayatumia kuwahusu Wakristo. Aliandika hivi: “Kwa namna hii Israeli wote wataokolewa. Kama vile imeandikwa: ‘Mkombozi atakuja kutoka Zayoni na kugeuzia mbali mazoea ya kutomwogopa Mungu yatoke kwa Yakobo. Na hili ndilo agano kwa upande wangu pamoja nao, niondoleapo mbali dhambi zao.” (Waroma 11:26, 27) Kwa kweli, unabii wa Isaya unatumika hadi wakati wetu na hata baada ya hapo. Jinsi gani?

      18. Yehova alitokeza “Israeli wa Mungu” wakati gani na jinsi gani?

      18 Katika karne ya kwanza, mabaki wachache wa taifa la Israeli walimkubali Yesu kuwa Mesiya. (Waroma 9:27; 11:5) Siku ya Pentekoste 33 W.K., Yehova alimimina roho yake takatifu juu ya waamini karibu 120 wa mabaki hao, akawaingiza katika agano lake jipya lililopatanishwa na Yesu Kristo. (Yeremia 31:31-33; Waebrania 9:15) Siku hiyo kulitokea “Israeli wa Mungu,” yaani taifa jipya ambalo washirika wake hawatambulishwi kwa ukoo wa kimwili wa Abrahamu, bali kwa kuzaliwa na roho ya Mungu. (Wagalatia 6:16) Watu wasiotahiriwa wa Mataifa yasiyo ya Kiyahudi walihusishwa pia katika taifa hilo jipya, wa kwanza kati yao akiwa ni Kornelio. (Matendo 10:24-48; Ufunuo 5:9, 10) Hivyo Yehova Mungu aliwafanya kuwa wana, wakawa watoto wake wa kiroho, warithi wenzi wa Yesu.—Waroma 8:16, 17.

      19. Yehova anafanya agano gani pamoja na Israeli wa Mungu?

      19 Sasa Yehova anafanya agano pamoja na Israeli wa Mungu. Tunasoma hivi: “Tena katika habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana [“wazao,” “NW”] wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.” (Isaya 59:21) Iwe maneno hayo yalitumika au hayakutumika kumhusu Isaya mwenyewe, hakika yalitimizwa katika Yesu, aliyehakikishiwa kwamba “ataona uzao wake.” (Isaya 53:10) Yesu alisema yale aliyokuwa amejifunza kutoka kwa Yehova, na roho ya Yehova ilikaa juu yake. (Yohana 1:18; 7:16) Basi ni vizuri kwamba hata ndugu zake na warithi wenzake, ambao ni washirika wa Israeli wa Mungu, wanapokea roho takatifu ya Yehova na kuhubiri ujumbe ambao wamejifunza kutoka kwa Baba yao wa kimbingu. Wote ‘wamefundishwa na Yehova.’ (Isaya 54:13; Luka 12:12; Matendo 2:38) Iwe ni kupitia Isaya au ni kupitia Yesu ambaye Isaya anamfananisha kiunabii, sasa Yehova anafanya agano kwamba hatabadilisha kamwe nafasi yao ichukuliwe na watu wengine, bali atawatumia milele wakiwa mashahidi wake. (Isaya 43:10) Hata hivyo, “wazao” wao ambao pia wanafaidika na agano hilo ni akina nani?

      20. Ahadi ya Yehova kwa Abrahamu ilitimizwaje katika karne ya kwanza?

      20 Nyakati za kale Yehova alimwahidi Abrahamu hivi: “Katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.” (Mwanzo 22:18) Kupatana na jambo hilo, mabaki wachache wa Waisraeli wa asili waliomkubali Mesiya waliingia katika mataifa mengi, wakahubiri habari njema juu ya Kristo. Kwa kuanza na Kornelio, watu wengi wasiotahiriwa wa Mataifa yasiyo ya Kiyahudi ‘walijibariki’ kupitia Yesu, Mbegu ya Abrahamu. Wakawa sehemu ya Israeli wa Mungu na sehemu ya pili ya ile mbegu ya Abrahamu. Wao ni sehemu ya “taifa takatifu” la Yehova, ambalo utume wake ni ‘kutangaza kotekote sifa bora kabisa za yeye aliyewaita wao kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’—1 Petro 2:9; Wagalatia 3:7-9, 14, 26-29.

      21. (a) Israeli wa Mungu wametokeza “wazao” gani nyakati za kisasa? (b) “Wazao” hao wanafarijiwaje na agano au mkataba ambao Yehova amefanya pamoja na Israeli wa Mungu?

      21 Leo inaonekana kwamba idadi kamili ya Israeli wa Mungu imekusanywa. Na bado, mataifa yanaendelea kubarikiwa—tena sana. Jinsi gani? Ni kwa vile Israeli wa Mungu wamekuwa na “wazao,” yaani wanafunzi wa Yesu walio na tumaini la kupata uhai wa milele katika dunia-paradiso. (Zaburi 37:11, 29) “Wazao” hao wanafundishwa na Yehova pia na kuagizwa katika njia zake. (Isaya 2:2-4) Ingawa hawabatizwi kwa roho takatifu wala hawaonwi kuwa washiriki katika agano jipya, wanaimarishwa na roho takatifu ya Yehova kushinda vipingamizi vyote ambavyo Shetani huwawekea wanapofanya kazi ya kuhubiri. (Isaya 40:28-31) Sasa idadi yao inafikia mamilioni na inaendelea kuongezeka, huku wakitokeza wazao wao wenyewe. Agano au mkataba ambao Yehova amefanya na watiwa-mafuta huhakikishia “wazao” hao kwamba Yehova ataendelea kuwatumia kuwa wasemaji wake hadi milele.—Ufunuo 21:3, 4, 7.

      22. Tunaweza kuwa na uhakika gani kuhusu Yehova, na hiyo inapaswa kuwa na matokeo gani kwetu?

      22 Basi, acheni sisi sote tuendelee kumwamini Yehova daima. Yeye ana nia na pia uwezo wa kuokoa! Hakuna wakati ambao mkono wake utakuwa mfupi; sikuzote yeye atawakomboa watu wake waaminifu. Wote wanaomtumainia wataendelea kuyabeba maneno yake mema vinywani mwao “tangu leo na hata milele.”

      [Sanduku katika ukurasa wa 294]

      Jiji la Yerusalemu Lenye Uasi-Imani Linalingana na Jumuiya ya Wakristo

      Yerusalemu, lile jiji kuu la taifa teule la Mungu, linafananisha tengenezo la Mungu la viumbe-roho wa kimbingu na pia jamii ya Wakristo watiwa-mafuta wanaofufuliwa mbinguni kuwa bibi-arusi wa Kristo. (Wagalatia 4:25, 26; Ufunuo 21:2) Hata hivyo, mara nyingi wakaaji wa Yerusalemu walikosa kuwa waaminifu kwa Yehova, na jiji hilo lilifafanuliwa kuwa kahaba na mwanamke mzinzi. (Ezekieli 16:3, 15, 30-42) Likiwa katika hali hiyo, jiji la Yerusalemu likawa mfano unaofaa kufananisha Jumuiya ya Wakristo yenye uasi-imani.

      Yesu aliliita jiji la Yerusalemu “muuaji wa manabii na mpigaji kwa mawe wa hao waliotumwa kwake.” (Luka 13:34; Mathayo 16:21) Kama Yerusalemu lisilo aminifu, Jumuiya ya Wakristo inadai eti inamtumikia Mungu wa kweli, na kumbe inaziacha sana njia zake za uadilifu. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atahukumu Jumuiya ya Wakristo kwa kutumia viwango vile vile vya uadilifu alivyovitumia kuhukumu Yerusalemu lenye uasi-imani.

      [Picha katika ukurasa wa 296]

      Hakimu anapaswa kuhukumu kwa uadilifu, atafute haki, na asikubali rushwa zozote

      [Picha katika ukurasa wa 298]

      Hukumu za Yehova zitakuwa kama mto uliofurika, zifagilie mbali vipingamizi vyote vinavyozuia mapenzi yake kufanyika

      [Picha katika ukurasa wa 302]

      Yehova anafanya agano kwamba watu wake hawatapoteza kamwe pendeleo la kuwa mashahidi wake

  • Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Moja

      Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote

      Isaya 60:1-22

      1. Isaya sura ya 60 ina ujumbe gani wa kutia moyo?

      SURA ya 60 ya Isaya imeandikwa kama drama yenye kuchochea kweli kweli. Katika mistari ya kwanza, fikira zetu zinanaswa na tamasha yenye kusisimua moyo. Matukio yanafuatana mbio-mbio, yakituongoza kwenye upeo wa kuvutia. Sura hiyo inatumia maneno maridadi kuhusu kurudishwa kwa ibada ya kweli katika Yerusalemu la kale na kupanuka kwa ibada ya kweli ulimwenguni pote leo. Tena, inaelekeza kwenye baraka za milele zinazowangoja wale wanaomwabudu Mungu kwa uaminifu-mshikamanifu. Kila mmoja wetu anaweza kushiriki katika utimizo wa sehemu hii ya kusisimua ya unabii wa Isaya. Basi acheni tuichunguze kwa uangalifu.

      Nuru Yang’aa Gizani

      2. Mwanamke fulani aliyelala gizani anapewa amri gani, na kwa nini anapaswa kutii haraka?

      2 Maneno ya kwanza ya sura hii ya Isaya yameelekezwa kwa mwanamke mwenye hali za huzuni. Ni wazi kwamba mwanamke huyo amelala kifudifudi gizani. Kwa ghafula, nuru yapenya ule weusi, huku Yehova akimtumia Isaya kupaaza sauti hivi: “Ondoka, [“inuka, Ee mwanamke,” “NW”] uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja; na utukufu wa BWANA umekuzukia.” (Isaya 60:1) Ndiyo, “mwanamke” huyo anapaswa kusimama ili yeye naye aangaze utukufu wa Mungu! Kwa nini afanye hivyo haraka? Unabii unaendelea kusema hivi: “Tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; bali BWANA atakuzukia wewe, na utukufu wake utaonekana juu yako.” (Isaya 60:2) Ni lazima “mwanamke” huyo ‘aangaze’ kwa faida ya wale wanaomzunguka, ambao wangali wanapapasa-papasa gizani. Kutakuwa na matokeo gani? “Mataifa wataijilia nuru yako, na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.” (Isaya 60:3) Maneno haya ya kwanza yanaandaa maana hasa ya kile kitakachoelezwa kwa urefu katika mistari inayofuata. Yaani, ni lazima ibada ya kweli ipanuke ulimwenguni pote!

      3. (a) “Mwanamke” huyo ni nani? (b) Kwa nini “mwanamke” huyo amekuwa akilala gizani?

      3 Ingawa Yehova anaongea juu ya matukio ya wakati ujao, anamwambia yule “mwanamke” kwamba nuru yake “imekuja.” Hiyo inakazia uhakika wa kwamba unabii huo utatimizwa. “Mwanamke” anayetajwa ni Sayuni, au Yerusalemu, jiji kuu la Yuda. (Isaya 52:1, 2; 60:14) Jiji hilo linawakilisha taifa zima. Wakati wa utimizo wa kwanza wa unabii huo, “mwanamke” huyo anapatikana amelala gizani, na amekuwa hapo tangu Yerusalemu lilipoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. Hata hivyo, mwaka wa 537 K.W.K., mabaki waaminifu kati ya Wayahudi waliohamishwa wanarudi Yerusalemu na kurudisha ibada safi. Mwishowe, Yehova anaangaza nuru juu ya “mwanamke” wake, na watu wake waliorudishwa wanakuwa chanzo cha kuangaza nuru miongoni mwa mataifa yaliyo katika giza la kiroho.

      Utimizo Mkubwa Zaidi

      4. Ni akina nani leo duniani wanaowakilisha yule “mwanamke,” na matumizi mapana ya unabii huo yanahusu nani?

      4 Licha ya kupendezwa na utimizo wa unabii huu kuhusiana na Yerusalemu la kale, tunapendezwa pia na utimizo wake wa baadaye. Leo “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova anawakilishwa duniani na “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Katika muda ambao taifa hili la kiroho limekuwako, tangu Pentekoste 33 W.K. mpaka sasa, limekuja kuwa na jumla ya washirika watiwa-mafuta 144,000, “ambao wamenunuliwa kutoka katika dunia” wakitazamia kutawala pamoja na Kristo mbinguni. (Ufunuo 14:1, 3) Utimizo wa kisasa wa Isaya sura ya 60 unawahusu hasa wale 144,000 walio hai duniani wakati wa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Unabii huu unawahusu pia waandamani wa Wakristo hao watiwa-mafuta, yaani “umati mkubwa” wa “kondoo wengine.”—Ufunuo 7:9; Yohana 10:11, 16.

      5. Washiriki waliobaki wa Israeli wa Mungu walijikuta wakiwa wamelala gizani lini, na nuru ya Yehova iliwaangazia lini?

      5 Kwa muda mfupi katika miaka ya mapema ya 1900, washirika wa Israeli wa Mungu ambao wangali duniani walikuwa wakisujudu gizani, kwa usemi wa mfano. Vita ya kwanza ya ulimwengu ilipokuwa ikikaribia kumalizika, walikuwa katika hali inayoelezwa kwa njia ya mfano katika kitabu cha Ufunuo, yaani, maiti zao zilikuwa zimelala “juu ya njia pana ya jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho laitwa Sodoma na Misri.” (Ufunuo 11:8) Hata hivyo, mwaka wa 1919 Yehova akawaangazia nuru yake. Nao wakaitikia kwa kusimama na kuangazia wengine nuru hiyo, wakitangaza habari njema za Ufalme wa Mungu bila hofu.—Mathayo 5:14-16; 24:14.

      6. Ulimwengu kwa ujumla umeitikiaje tangazo la kuwapo kwa Yesu akiwa mfalme, lakini ni nani ambao wamevutiwa na nuru ya Yehova?

      6 Wanadamu kwa ujumla wameshawishiwa na Shetani, mkuu wa “watawala wa ulimwengu wa giza hili,” kulikataa tangazo linalotolewa kuhusu kuwapo kwa Yesu Kristo, aliye “nuru ya ulimwengu.” Tangazo hilo linasema kwamba sasa Yesu ni mfalme. (Waefeso 6:12; Yohana 8:12; 2 Wakorintho 4:3, 4) Hata hivyo, mamilioni ya watu wamevutiwa na nuru ya Yehova. Watu hao ni kutia ndani “wafalme” (wale ambao wamekuwa warithi watiwa-mafuta wa Ufalme wa kimbingu) na “mataifa” (ule umati mkubwa wa kondoo wengine).

      Mpanuko Waleta Shangwe ya Moyoni

      7. Yule “mwanamke” anaona jambo gani la kuchangamsha moyo?

      7 Akiendeleza habari iliyotajwa katika Isaya 60:3, Yehova anampa yule “mwanamke” amri nyingine: “Inua macho yako, utazame pande zote”! “Mwanamke” huyo anapotii, anaona jambo la kuchangamsha moyo—loo, watoto wake ndio hawa wakija nyumbani! “Wote wanakusanyana; wanakujia wewe; wana wako watakuja kutoka mbali. Na binti zako watabebwa nyongani.” (Isaya 60:4) Matokeo ya kutangazwa kwa Ufalme katika mataifa yote kuanzia mwaka wa 1919 ni kwamba maelfu ya “wana” na “binti” watiwa-mafuta wanaunganishwa na Israeli wa Mungu. Kwa njia hiyo, Yehova alichukua hatua za kukamilisha idadi iliyotabiriwa ya wale 144,000, ambao watatawala pamoja na Kristo.—Ufunuo 5:9, 10.

      8. Israeli wa Mungu wamekuwa na sababu gani ya kufurahi tangu mwaka wa 1919?

      8 Ongezeko hilo lilileta shangwe. “Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, na moyo wako utatetemeka na kukunjuka; kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, utajiri wa mataifa utakuwasilia.” (Isaya 60:5) Israeli wa Mungu alifurahi sana kwa sababu ya kukusanywa kwa watiwa-mafuta miaka ya 1920 na ya 1930. Hata hivyo, wamekuwa na sababu nyingine ya shangwe. Hasa tangu miaka ya katikati ya 1930, watu ambao hapo kwanza walikuwa sehemu ya “bahari” ya wanadamu waliotenganishwa na Mungu wametoka katika mataifa yote ili kuabudu pamoja na Israeli wa Mungu. (Isaya 57:20; Hagai 2:7) Watu hawa hawaendi zao kumtumikia Mungu, kila mtu kivyake. Bali, wanamjia “mwanamke” wa Mungu na kuwa sehemu ya kundi la Mungu lenye umoja. Matokeo ni kwamba, watumishi wote wa Mungu wanashiriki kuipanua ibada ya kweli.

      Mataifa Yatoka Pande Zote Kuja Kukutanikia Yerusalemu

      9, 10. Ni nani wanaoonekana wakitoka pande mbalimbali kuja kukutanikia Yerusalemu, na Yehova anawapokeaje?

      9 Yehova anaeleza jinsi mpanuko utakavyofanyika, akitumia mifano inayofahamika na watu wa wakati wa Isaya. “Mwanamke” huyo anatazama akiwa pale alipo juu ya Mlima Sayuni na kuangaza-angaza macho yake kwenye upeo wa mashariki. Anaona nini? “Wingi wa ngamia utakufunika, ngamia vijana wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na uvumba; na kuzitangaza sifa za BWANA.” (Isaya 60:6) Misafara ya ngamia inayotumiwa na wafanya-biashara wa makabila mbalimbali inashika njia kwenda Yerusalemu ikipita katika barabara zinazoelekea huko. (Mwanzo 37:25, 28; Waamuzi 6:1, 5; 1 Wafalme 10:1, 2) Ngamia wako kila mahali, kama mafuriko yanayoifunika nchi! Misafara hiyo inaleta zawadi za thamani kubwa, kuonyesha kwamba wafanya-biashara hao wanakuja wakiwa na makusudio ya amani. Wanataka kumwabudu Yehova na kumpa kilicho bora.

      10 Si wafanya-biashara hawa tu walio mwendoni. “Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia.” Ndiyo, hata makabila yaliyo na desturi ya kuchunga mifugo yanasafiri kwenda Yerusalemu. Yanakuja na zawadi za mali zao zenye thamani kubwa zaidi, yaani makundi ya kondoo, kisha wanajitoa wawe wahudumu. Yehova atawapokeaje? Yeye anasema: “Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali, nami nitaitukuza nyumba ya utukufu wangu.” (Isaya 60:7) Yehova anazikubali zawadi zao, nazo zitatumiwa katika ibada safi.—Isaya 56:7; Yeremia 49:28, 29.

      11, 12. (a) Yule “mwanamke” anaona nini anapokaza macho magharibi? (b) Kwa nini watu wengi sana wanafanya haraka kwenda Yerusalemu?

      11 Sasa Yehova anamwagiza yule “mwanamke” atazame kwenye upeo wa magharibi. Halafu Yehova anauliza: “Ni nani hawa warukao kama wingu, na kama njiwa waendao madirishani kwao?” Yehova mwenyewe anajibu hivi: “Hakika yake visiwa vitaningojea, na merikebu za Tarshishi kwanza, ili kuleta wana wako kutoka mbali, na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao, kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wako, kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli, kwa kuwa amekutukuza wewe.”—Isaya 60:8, 9.

      12 Wazia kwamba umesimama pamoja na “mwanamke” huyo, ukikaza macho magharibi ng’ambo ya Bahari Kuu. Unaona nini? Wingu la mbali la madoa meupe yakielea juu ya maji. Wanaonekana kama ndege. Lakini wanapokaribia zaidi, unaona kwamba kumbe ni merikebu zenye matanga yaliyotwekwa. ‘Zimekuja kutoka mbali.’a (Isaya 49:12) Mashua zinazoenda kasi kuelekea Sayuni ni nyingi sana hivi kwamba zinaonekana kama kundi la njiwa wanaoelekea nyumbani. Haraka yote hiyo ya nini? Kikosi hicho kina hamu nyingi ya kuwafikisha pwani waabudu wa Yehova waliomo, ambao wametoka bandari za mbali. Kwa kweli, wote wale wanaowasili sasa hivi—Waisraeli na wageni pia, kutoka mashariki au magharibi na kutoka nchi za karibu au za mbali—wanafanya haraka kwenda Yerusalemu wakafanye vitu vyote walivyo navyo viwe wakfu kwa jina la Yehova, Mungu wao.—Isaya 55:5.

      13. Nyakati za kisasa, “wana” na “binti” ni akina nani, na “utajiri wa mataifa” ni akina nani?

      13 Lo, andiko la Isaya 60:4-9 linatoa ufafanuzi ulio wazi kama nini kuhusu mpanuko ambao umetukia ulimwenguni pote tangu “mwanamke” wa Yehova aanze kuangaza nuru katikati ya giza la ulimwengu huu! Kwanza wakafika “wana” na “binti” za Sayuni wa kimbingu, wale waliokuja kuwa Wakristo watiwa-mafuta. Mwaka wa 1931, walijitambulisha peupe kuwa Mashahidi wa Yehova. Halafu wingu la watu watiifu, ambao ndio “utajiri wa mataifa” na “wingi wa bahari,” likafanya haraka kujiunga na ndugu za Kristo waliobaki.b Leo watumishi wote hawa wa Yehova wanaotoka pembe nne za dunia na kutoka hali zote za maisha wanajiunga na Israeli wa Mungu kumsifu Bwana wao Mwenye Enzi Kuu, Yehova, na kukweza jina lake kuwa ndilo tukufu zaidi katika ulimwengu mzima.

      14. Wale wanaowasili sasa hivi ‘wanapandaje juu ya madhabahu ya Mungu’?

      14 Ingawa hivyo, inamaanisha nini kwamba watu hawa wanaowasili sasa hivi kutoka kwenye mataifa “watapanda juu ya madhabahu [ya Mungu]”? Dhabihu huwekwa juu ya madhabahu. Mtume Paulo alitumia usemi unaohusisha dhabihu alipoandika hivi: “Nawasihi sana nyinyi . . . mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri kuzuri.” (Waroma 12:1) Wakristo wa kweli wana moyo wa kujitoa. (Luka 9:23, 24) Wanatoa wakati wao, nguvu zao, na stadi zao kuendeleza ibada safi. (Waroma 6:13) Kwa kufanya hivyo, wanatoa dhabihu zinazokubalika za kumsifu Mungu. (Waebrania 13:15) Jambo la kwamba mamilioni ya waabudu wa Yehova leo, vijana kwa wazee, wameweka tamaa zao za kibinafsi nyuma ya masilahi ya Ufalme wa Mungu, linachangamsha moyo kama nini! Wanaonyesha roho ya kweli ya kujidhabihu.—Mathayo 6:33; 2 Wakorintho 5:15.

      Wale Wanaowasili Sasa Hivi Wanashiriki Katika Mpanuko

      15. (a) Nyakati za kale, rehema ya Yehova ilionyeshwaje kuhusiana na wageni? (b) Nyakati za kisasa, “wageni” wameshiriki jinsi gani kuijenga ibada ya kweli?

      15 Wale wanaowasili sasa hivi wanatoa mali zao na hata huduma zao binafsi kumtegemeza “mwanamke” wa Yehova. “Wageni watajenga kuta zako, na wafalme wao watakuhudumu; maana katika ghadhabu yangu nalikupiga, lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.” (Isaya 60:10) Rehema ya Yehova ilionyeshwa karne ya sita K.W.K. wakati wageni waliposaidia kazi ya ujenzi Yerusalemu. (Ezra 3:7; Nehemia 3:26) Katika utimizo mkubwa wa leo, “wageni,” yaani umati mkubwa, wanaunga mkono mabaki watiwa-mafuta kujenga ibada ya kweli. Wanasaidia kujenga sifa za Kikristo katika wanafunzi wao wa Biblia, na hivyo wanajenga makutaniko ya Kikristo na kuimarisha “kuta” za tengenezo la Yehova. (1 Wakorintho 3:10-15) Pia wanajenga kwa njia halisi, wakijibidiisha kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na majengo ya Betheli. Hivyo wanajiunga na ndugu zao watiwa-mafuta kutunza mahitaji ya tengenezo la Yehova linalopanuka.—Isaya 61:5.

      16, 17. (a) “Malango” ya tengenezo la Mungu yamewekwaje wazi? (b) “Wafalme” wamemhudumiaje Sayuni? (c) Itakuwaje kwa wale wanaojaribu kuyafunga “malango” ambayo Yehova anataka yaachwe wazi?

      16 Matokeo ya programu ya ujenzi wa kiroho ni kwamba, kila mwaka mamia ya maelfu ya “wageni” huanza kushirikiana na tengenezo la Yehova, na njia huwa wazi ili wengi hata zaidi waingie. Yehova anasema hivi: “Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; hayatafungwa mchana wala usiku; ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.” (Isaya 60:11) Ingawa hivyo, ni akina nani wale “wafalme” wanaoongoza kuuletea Sayuni utajiri wa mataifa? Nyakati za kale Yehova aligusa mioyo ya watawala fulani ili ‘kumhudumia’ Sayuni. Kwa mfano, Koreshi alichukua hatua ya kwanza ya kuwaagiza Wayahudi warudi Yerusalemu ili wakalijenge upya hekalu. Baadaye, Artashasta alichanga rasilmali na kumwagiza Nehemia ajenge upya kuta za Yerusalemu. (Ezra 1:2, 3; Nehemia 2:1-8) Kwa kweli “moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; kama mifereji ya maji.” (Mithali 21:1) Mungu wetu anaweza kugusa mioyo ya hata watawala walio na nguvu zaidi watende kupatana na mapenzi yake.

      17 Nyakati za kisasa “wafalme” au wenye mamlaka wengi wa kiserikali wamejaribu kufunga “malango” ya tengenezo la Yehova. Hata hivyo, wengine wametumikia Sayuni kwa kufanya maamuzi yaliyosaidia kuyaweka “malango” hayo yakiwa wazi. (Waroma 13:4) Mwaka wa 1919, wenye mamlaka wa kiserikali walimfungua Joseph F. Rutherford na waandamani wake kutoka gerezani walikokuwa wamefungwa bila haki. (Ufunuo 11:13) Serikali za kibinadamu ‘zilimeza kabisa’ mafuriko ya mnyanyaso yaliyomiminwa na Shetani kwa nguvu nyingi baada ya anguko lake kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:16) Serikali fulani zimeunga mkono maoni ya kuvumiliana na imani za kidini za watu, nyakati nyingine zikiwatetea Mashahidi wa Yehova hasa. Huduma ya aina hiyo imefanya iwe rahisi zaidi makundi ya watu watiifu yakubali kupita katika yale “malango” yaliyo wazi na kuingia katika tengenezo la Yehova. Namna gani wapinzani wanaojaribu kuyafunga “malango” hayo? Hawatafaulu kamwe. Yehova anasema hivi kuhusu watu hao: “Kila taifa na ufalme wa watu wasiotaka kukutumikia wataangamia; naam, mataifa hayo wataharibiwa kabisa.” (Isaya 60:12) Mtu ye yote au matengenezo mazima yanayopigana na “mwanamke” wa Mungu ataangamia katika vita ya Har-Magedoni, wala si baada ya hapo.—Ufunuo 16:14, 16.

      18. (a) Ahadi ya kwamba miti itasitawi katika Israeli inamaanisha nini? (b) Leo ‘mahali pa miguu ya Yehova’ ni wapi?

      18 Baada ya kutoa onyo hilo la hukumu, unabii unazirudia ahadi za utukuzo na ufanisi. Akiongea na “mwanamke” wake, Yehova anasema hivi: “Utukufu wa Lebanoni utakujia wewe, Mberoshi na mtidhari na mteashuri pamoja; ili kupapamba mahali pangu patakatifu, nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.” (Isaya 60:13) Miti inayositawi inafananisha urembo na uzaaji wa matunda. (Isaya 41:19; 55:13) Maneno “patakatifu” na “mahali pa miguu yangu” katika mstari huu yanamaanisha hekalu la Yerusalemu. (1 Mambo ya Nyakati 28:2; Zaburi 99:5) Hata hivyo, mtume Paulo alieleza kwamba hekalu la Yerusalemu lilikuwa kiwakilishi halisi kilichotangulia kuwa kivuli cha hekalu kubwa zaidi la kiroho ambalo lingetokea baadaye, yaani mpango wa kumkaribia Yehova katika ibada kwa msingi wa dhabihu ya Kristo. (Waebrania 8:1-5; 9:2-10, 23) Leo Yehova hupatukuza ‘mahali pa miguu yake,’ yaani nyua za kidunia za hekalu hilo kubwa la kiroho. Nyua hizo zinakuwa za kupendeza macho sana kiasi cha kwamba zinawavutia watu kutoka mataifa yote ili washiriki katika ibada ya kweli wakiwa hapo.—Isaya 2:1-4; Hagai 2:7.

      19. Wapinzani watalazimika kukubali nini, na watakubali hivyo kabla ya kumalizika kwa wakati gani?

      19 Sasa akielekeza fikira zake kwa wapinzani, Yehova anasema hivi: “Wana wa watu wale waliokutesa watakuja kwako na kukuinamia; nao wote waliokudharau watajiinamisha hata nyayo za miguu yako; nao watakuita, Mji wa BWANA, Sayuni wa Mtakatifu wa Israeli.” (Isaya 60:14) Ndiyo, wapinzani fulani watalazimika kuinama na kupaaza sauti wamwite yule “mwanamke” kwa kuona ongezeko hilo kubwa na njia bora ya maisha ambayo baraka ya Mungu inawaletea watu wake. Hiyo ni kusema kwamba, watu hao watalazimika kukubali kabla au wakati wa Har-Magedoni, wala si baada ya hapo, kwamba mabaki watiwa-mafuta na waandamani wao ndio wawakilishi wa kweli wa tengenezo la Mungu la kimbingu, ‘mji wa Yehova, Sayuni wa Mtakatifu wa Israeli.’

      Kutumia Mali Ambazo Zipo

      20. Hali za yule “mwanamke” zitabadilikaje sana?

      20 Lo, sasa hali za “mwanamke” wa Yehova zinabadilika kama nini! Yehova anasema hivi: “[Badala ya,” “NW”] kuwa umeachwa na kuchukiwa, hata ikawa hapana mtu aliyepita ndani yako, nitakufanya kuwa fahari ya milele, furaha ya vizazi vingi. Utanyonya maziwa ya mataifa, utanyonya matiti ya wafalme; nawe utajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako, na mkombozi wako, Mwenye enzi wa Yakobo.”—Isaya 60:15, 16.

      21. (a) Yerusalemu la kale linapataje “fahari”? (b) Watumishi watiwa-mafuta wa Yehova wamefurahia baraka zipi tangu mwaka wa 1919, na wamenyonyaje “maziwa ya mataifa”?

      21 Kwa muda wa miaka 70, Yerusalemu la kale ni kama limeondolewa kwenye ramani, kwani ‘hapana mtu anayepita ndani yake.’ Lakini kuanzia mwaka wa 537 K.W.K., Yehova anarudisha watu katika jiji hilo, akilipatia “fahari.” Vivyo hivyo, kuelekea mwisho wa vita ya kwanza ya ulimwengu, Israeli wa Mungu walipatwa na kipindi cha ukiwa ambamo walihisi ‘wameachwa.’ Lakini mwaka wa 1919, Yehova aliwakomboa watumishi wake watiwa-mafuta kutoka utekwani, na tangu wakati huo amewabariki kwa mpanuko na ufanisi wa kiroho ambao haujawahi kuonekana kabla ya hapo. Watu wake wamenyonya “maziwa ya mataifa,” wakitumia mali zinazotoka kwenye mataifa ili kuendeleza ibada ya kweli. Kwa mfano, kutumia ufundi wa kisasa kwa njia ya hekima kumefanya iwezekane kutafsiri na kuchapisha Biblia na vitabu vya Biblia katika mamia ya lugha. Matokeo ni kwamba, mamia ya maelfu ya watu hujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kila mwaka na kupata kujua kwamba Yehova ndiye Mwokozi na Mkombozi wao kupitia Kristo.—Matendo 5:31; 1 Yohana 4:14.

      Maendeleo ya Kitengenezo

      22. Yehova anaahidi maendeleo gani ya pekee?

      22 Ukuzi wa idadi ya watu wa Yehova unaambatana na maendeleo ya kitengenezo. Yehova anasema hivi: ‘Badala ya shaba nitaleta dhahabu, na badala ya chuma nitaleta fedha, na badala ya mti, shaba, na badala ya mawe, chuma; tena nitawafanya wasimamizi wako wawe amani, na hao wakutozao fedha kuwa haki.’ (Isaya 60:17) Kubadilisha fedha kwa dhahabu ni maendeleo, na hata kubadilishwa kwa vifaa vingine vilivyotajwa hapa ni maendeleo. Kupatana na hilo, watu wa Yehova wamekuwa wakipata maendeleo ya kitengenezo muda wote wa siku za mwisho.

      23, 24. Watu wa Yehova wamekuwa wakipata maendeleo gani ya kitengenezo tangu mwaka wa 1919?

      23 Kufikia mwaka wa 1919, makutaniko yalikuwa na wazee na mashemasi waliochaguliwa kidemokrasi. Kuanzia mwaka huo, mkurugenzi wa utumishi aliwekwa rasmi kitheokrasi ili asimamie utumishi mbalimbali wa shambani katika kutaniko, lakini kulikuwako visa fulani ambapo wazee waliochaguliwa kwa kupigiwa kura walimpinga mkurugenzi wa utumishi. Mwaka wa 1932, mambo yakabadilika. Kupitia Mnara wa Mlinzi, makutaniko yakaagizwa yaache uchaguzi wa kupigia wazee na mashemasi kura. Badala yake, wakawa sasa wakichagua halmashauri ya utumishi ifanye kazi kwa kushirikiana na mkurugenzi wa utumishi. Hayo yalikuwa maendeleo makubwa.

      24 Mwaka wa 1938, “dhahabu” zaidi ililetwa wakati ilipothibitishwa kwamba watumishi wote kutanikoni walipasa kuwekwa rasmi kitheokrasi. Usimamizi wa kutaniko ukaja kuwa mikononi mwa mtumishi wa kampuni (baadaye, mtumishi wa kutaniko) na watumishi mbalimbali waliomsaidia, wote hao wakiwa wamewekwa rasmi chini ya uangalizi wa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”c (Mathayo 24:45-47) Hata hivyo, mwaka wa 1972 ilionekana kwamba njia ya Kimaandiko ya uangalizi wa kutaniko ni kupitia baraza la wazee badala ya kupitia mwanamume mmoja. (Wafilipi 1:1) Mabadiliko mengine yalifanywa katika makutaniko na katika Baraza Linaloongoza. Mfano wa badiliko lililofanywa katika baraza hilo ulionekana siku ya Oktoba 7, 2000, ilipotangazwa kwamba washirika wa Baraza Linaloongoza waliokuwa wakitumikia wakiwa wakurugenzi wa shirika la Watch Tower Society of Pennsylvania na mashirika mengine yanayohusiana na hilo wameviacha vyeo vyao kwa hiari. Hivyo basi, Baraza Linaloongoza lenye kuwakilisha mtumwa mwaminifu na mwenye busara linaweza kuzingatia uangalizi wa kiroho wa kulitunza “kutaniko la Mungu” na washirika wake, wale kondoo wengine. (Matendo 20:28) Mipango yote hiyo imeleta maendeleo. Imelitia nguvu tengenezo la Yehova na kuwabariki waabudu wake.

      25. Ni nani ambaye amekuwa akisababisha maendeleo ya kitengenezo ya watu wa Yehova, na wamevuna manufaa gani?

      25 Ni nani ambaye amesababisha maendeleo hayo? Je, yametokana na watu wenye uwezo wa kusimamia mambo vizuri au akili bora za wanadamu fulani? Sivyo, kwa maana Yehova alisema hivi: “Nitaleta dhahabu.” Maendeleo yote haya ni matokeo ya mwongozo wa kimungu. Watu wa Yehova wanapojitiisha chini ya mwongozo wake na kufanya marekebisho, wanapata faida nyingi. Wao huwa na amani nyingi miongoni mwao, na kupenda uadilifu ndiko huwashurutisha kumtumikia.

      26. Ni alama gani inayowatambulisha Wakristo wa kweli ambayo hata wapinzani huiona?

      26 Amani inayotolewa na Mungu ina nguvu za kubadili mambo. Yehova anaahidi hivi: “Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako; bali utaziita kuta zako, Wokovu, na malango yako, Sifa.” (Isaya 60:18) Hiyo ni kweli kabisa! Hata wapinzani wanakubali kwamba hali ya amani ni alama ya wazi ya Wakristo wa kweli. (Mika 4:3) Kuwa na amani pamoja na Mungu na miongoni mwa Mashahidi wa Yehova wenyewe hufanya kila mahali pa mikutano ya Kikristo pawe kama sehemu ya kupata burudiko katika ulimwengu wenye jeuri. (1 Petro 2:17) Ni kionjo cha amani tele itakayokuwako wakati wakaaji wote wa dunia ‘watakapofundishwa na Yehova.’—Isaya 11:9; 54:13.

      Nuru Tukufu ya Ukubali wa Mungu

      27. “Mwanamke” wa Yehova huangaziwa nuru gani?

      27 Yehova anaeleza kwamba Yerusalemu ataangaziwa nuru nyingi sana, anaposema hivi: “Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana, wala mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake; bali BWANA atakuwa nuru ya milele kwako, na Mungu wako atakuwa utukufu wako. Jua lako halitashuka tena, wala mwezi wako hautajitenga; kwa kuwa BWANA mwenyewe atakuwa nuru yako ya milele; na siku za kuomboleza kwako zitakoma.” (Isaya 60:19, 20) Yehova ataendelea kuwa “nuru ya milele” kwa “mwanamke” wake. ‘Hatashuka’ kamwe kama jua la machweo, wala ‘kujitenga’ kama mwezi.d Nuru yake ya kibali cha daima inawaangazia Wakristo watiwa-mafuta, wawakilishi wa kibinadamu wa “mwanamke” wa Mungu. Wao, pamoja na umati mkubwa, wanafurahia nuru kubwa ajabu ya kiroho isiyoweza kuzimwa na giza lolote la kisiasa wala la kiuchumi. Kisha wana hakika ya kuupata wakati ujao mwangavu ambao Yehova ameweka mbele yao.—Waroma 2:7; Ufunuo 21:3-5.

      28. (a) Ni jambo gani ambalo limeahidiwa kuhusu wakaaji wa Yerusalemu wanaorudi? (b) Wakristo watiwa-mafuta walirithi nini mwaka wa 1919? (c) Waadilifu watairithi nchi kwa muda gani?

      28 Yehova anaendelea kusema hivi kwa habari ya wakaaji wa Yerusalemu: “Watu wako nao watakuwa wenye haki wote, nao watairithi nchi milele; chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe, kazi ya mikono yangu mwenyewe, ili mimi nitukuzwe.” (Isaya 60:21) Israeli wa asili waliporudi kutoka Babiloni, ‘walirithi nchi.’ Lakini wakati huo “milele” ikawa ni kufikia karne ya kwanza W.K. wakati majeshi ya Roma yalipoharibu Yerusalemu na taifa la Kiyahudi. Mwaka wa 1919 mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta walitoka katika utekwa wa kiroho wakamiliki nchi ya kiroho. (Isaya 66:8) Nchi hii, au makao ya utendaji, inatambulishwa na ufanisi wa paradiso ya kiroho ambao hautafifia. Israeli wa kiroho, wakiwa jamii nzima, hawataacha kuwa waaminifu kama vile Israeli wa kale walivyofanya. Zaidi ya hilo, unabii wa Isaya utatimizwa kihalisi pia wakati dunia itakapokuwa paradiso halisi yenye “wingi wa amani.” Wakati huo waadilifu walio na tumaini la kidunia watairithi nchi milele.—Zaburi 37:11, 29.

      29, 30. “Mdogo” amekuwaje “elfu”?

      29 Mwishoni mwa Isaya sura ya 60 mnaweza kupatikana ahadi nzito, ambayo Yehova anaitoa kwa kutumia jina lake mwenyewe kuhakikisha kabisa kwamba ataitimiza. Anasema hivi: “Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa hodari; mimi, BWANA, nitayahimiza hayo wakati wake.” (Isaya 60:22) Wakati watiwa-mafuta waliotawanywa waliporudishwa kwenye utendaji mwaka wa 1919, wao ndio waliokuwa yule “mdogo.”e Lakini idadi yao iliongezeka wakati Waisraeli wa kiroho waliobaki walipokuwa wakiletwa ndani. Kisha ongezeko hilo likawa kubwa sana wakati umati mkubwa ulipoanza kukusanywa.

      30 Muda si muda, amani na uadilifu uliomo miongoni mwa watu wa Mungu ukawavutia watu wengi sana wenye mioyo ya kupenda haki kiasi cha kwamba yule “mdogo” akaongezeka kuwa “taifa hodari” kihalisi. Kwa sasa taifa hilo lina watu wengi kuliko mataifa mengi ya ulimwengu yanayojitawala. Ni wazi kwamba Yehova, kupitia Yesu Kristo, ameelekeza kazi ya Ufalme na kuihimiza. Kuona ibada ya kweli ikipanuka ulimwenguni pote na kushiriki katika mpanuko huo kunasisimua kama nini! Ndiyo, ni shangwe kutambua kwamba ongezeko hili humletea Yehova utukufu, aliyetoa unabii wa mambo hayo zamani za kale.

      [Maelezo ya Chini]

      a Yaelekea kwamba Tarshishi ilikuwa mahali panapojulikana sasa kuwa Hispania. Hata hivyo, kulingana na vitabu fulani vya marejeo, usemi “merikebu za Tarshishi” unamaanisha aina ya merikebu zinazotumika, yaani “vyombo vya usafiri wa baharini vyenye milingoti mirefu” ambavyo “vilifaa kuenda-enda Tarshishi.” Maana yake, merikebu hizo zilionwa kuwa zinafaa kusafiri-safiri mwendo mrefu hadi bandari za mbali.—1 Wafalme 22:48.

      b Ingawa Wakristo fulani wenye bidii na wenye tumaini la kidunia walishirikiana na Israeli wa Mungu kabla ya mwaka wa 1930, idadi yao ilianza kuongezeka sana katika miaka ya 1930.

      c Siku hizo, makutaniko ya mahali popote pale yaliitwa kampuni.

      d Mtume Yohana anatumia usemi kama huo anapoeleza kuhusu “Yerusalemu jipya,” wale 144,000 wakiwa katika utukufu wa kimbingu. (Ufunuo 3:12; 21:10, 22-26) Hiyo inafaa, kwa maana “Yerusalemu jipya” linawakilisha washirika wote wa Israeli wa Mungu baada ya wao kupokea thawabu yao ya kimbingu, na hivyo kujumlika pamoja na Yesu Kristo kuwa sehemu ya jiji kuu la “mwanamke” wa Mungu, “Yerusalemu la juu.”—Wagalatia 4:26.

      e Mwaka wa 1918 idadi ya wastani ya wale walioshiriki kulihubiri neno kila mwezi ilikuwa ndogo kuliko 4,000.

      [Picha katika ukurasa wa 305]

      Yule “mwanamke” anaamriwa ‘ainuke’

      [Picha katika ukurasa wa 312, 313]

      “Merikebu za Tarshishi” zinabeba waabudu wa Yehova waliomo

  • Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Mbili

      Uadilifu Wachipuka Katika Sayuni

      Isaya 61:1-11

      1, 2. Israeli yuko karibu kupatwa na badiliko gani, na litaletwa na nani?

      UHURU na utangazwe! Yehova ameazimia kuwaweka huru watu wake na kuwarudisha kwenye nchi ya wazee wao wa kale. Ibada ya kweli itatokea tena, kama mbegu inayochipuka baada ya mvua kunyesha taratibu. Siku hiyo ifikapo, kutamauka kutakwisha, kuwe na sifa yenye shangwe. Na vichwa vilivyokuwa vimefunikwa kwa majivu ya kuomboleza vitavikwa taji la ukubali wa Mungu.

      2 Ni nani atakayeleta badiliko hilo zuri ajabu? Ni Yehova pekee anayeweza kufanya jambo kama hilo. (Zaburi 9:19, 20; Isaya 40:25) Nabii Sefania aliamuru hivi kiunabii: “Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli; furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu. BWANA ameziondoa hukumu zako, amemtupa nje adui yako; mfalme wa Israeli, naam, yeye BWANA, yu katikati yako; hutaogopa uovu tena.” (Sefania 3:14, 15) Huo utakuwa wakati wa shangwe iliyoje! Yehova atakapowakusanya mabaki waliorudishwa kutoka Babiloni mwaka wa 537 K.W.K., tukio hilo litakuwa kama utimizo wa ndoto iliyoonekana ngumu kutimia.—Zaburi 126:1.

      3. Maneno ya kiunabii ya Isaya sura ya 61 yanatimizwa kwa njia zipi?

      3 Kurudishwa huku kunatabiriwa katika Isaya sura ya 61. Hata hivyo, ingawa ni wazi kwamba unabii huo ulitimizwa mwaka wa 537 K.W.K., unatimizwa kwa njia kubwa zaidi baadaye. Utimizo ulio na mambo mengi zaidi unahusu Yesu na wafuasi wake katika karne ya kwanza na watu wa Yehova katika nyakati za kisasa. Basi, maneno hayo yaliyopuliziwa ni muhimu sana!

      “Mwaka wa Nia Njema”

      4. Katika utimizo wa kwanza wa Isaya 61:1, ni nani anayepewa utume wa kuhubiri habari njema, na ni nani anayepewa utume huo katika utimizo wa pili?

      4 Isaya anaandika hivi: “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.” (Isaya 61:1) Ni nani aliyepewa utume wa kuhubiri habari njema? Yaelekea kwamba katika kisa cha kwanza ni Isaya, anayepuliziwa na Mungu kuwaandikia habari njema mateka walioko Babiloni. Hata hivyo, Yesu alionyesha utimizo wa maana zaidi alipoyatumia maneno ya Isaya kujihusu yeye mwenyewe. (Luka 4:16-21) Ndiyo, Yesu alitumwa akawaeleze watu watiifu habari njema. Basi, wakati wa ubatizo wake alitiwa mafuta kwa roho takatifu ili atimize kusudi hilo.—Mathayo 3:16, 17.

      5. Ni nani ambao wamekuwa wakihubiri zile habari njema kwa muda wa miaka 2,000 hivi?

      5 Zaidi ya hilo, Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwa waeneza-injili, au wahubiri wa zile habari njema. Kwenye Pentekoste 33 W.K., karibu watu 120 kati ya wahubiri hao walitiwa mafuta kwa roho takatifu wakawa wana wa kiroho wa Mungu. (Matendo 2:1-4, 14-42; Waroma 8:14-16) Wao pia walipewa utume wa kuwaeleza watu watiifu na waliovunjika moyo kuhusu zile habari njema. Hao 120 walikuwa wa kwanza miongoni mwa watu 144,000 kutiwa mafuta kwa njia hiyo. Leo wale walio wa mwisho katika kikundi hiki wangali wakiendelea na utendaji wao duniani. Kwa hiyo, kwa karibu miaka 2,000, wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu wamekuwa wakitoa ushahidi “juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.”—Matendo 20:21.

      6. Ni nani waliopata kitulizo kwa kusikia habari njema zilizohubiriwa nyakati za kale, na namna gani leo?

      6 Ujumbe wa Isaya uliopuliziwa uliwaletea kitulizo Wayahudi wenye toba kule Babiloni. Siku za Yesu na wanafunzi wake, ujumbe huo uliwapa kitulizo Wayahudi waliokuwa wamevunjwa moyo na uovu uliokuwa katika Israeli na kunyong’onyea katika utekwa wa mapokeo ya uongo ya Dini ya Kiyahudi ya karne ya kwanza. (Mathayo 15:3-6) Leo, mamilioni walionaswa katika mtego wa desturi za kipagani za Jumuiya ya Wakristo na mapokeo yanayomvunjia Mungu heshima ‘wanaugua na kulia’ kwa sababu ya machukizo yanayofanywa katika mfumo huo wa kidini. (Ezekieli 9:4) Wale wanaoziitikia habari njema wanakombolewa watoke katika hali hiyo ya kusikitisha. (Mathayo 9:35-38) Macho yao ya ufahamu yanafunguliwa wazi wanapojifunza kumwabudu Yehova “kwa roho na kweli.”—Yohana 4:24.

      7, 8. (a) Kuna miaka gani miwili ‘ya nia njema’? (b) ‘Siku za kisasi’ cha Yehova ni zipi?

      7 Kuna wakati hususa uliowekwa ili habari njema zihubiriwe. Yesu na wafuasi wake walipewa utume wa “kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa [“mwaka wa nia njema,” “NW”], na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao.” (Isaya 61:2) Mwaka ni muda mrefu, lakini una mwanzo na mwisho. “Mwaka wa nia njema” wa Yehova ni kile kipindi ambacho yeye huwapa watu watiifu nafasi ya kuitikia anapowatangazia uhuru.

      8 Katika karne ya kwanza, mwaka wa nia njema kwa taifa la Kiyahudi ulianza mwaka wa 29 W.K. Yesu alipoanza huduma yake ya kidunia. Aliwaambia Wayahudi hivi: “Tubuni, nyinyi watu, kwa maana ufalme wa mbingu umekaribia.” (Mathayo 4:17) Mwaka huo wa nia njema uliendelea hadi “siku ya kisasi” cha Yehova, ambayo ilifikia upeo mwaka wa 70 W.K. Yehova aliporuhusu majeshi ya Roma yaharibu Yerusalemu na hekalu lake. (Mathayo 24:3-22) Sisi leo tunaishi katika mwaka mwingine wa nia njema, ulioanza wakati Ufalme wa Mungu uliposimamishwa katika mbingu mwaka wa 1914. Mwaka huu wa nia njema utamalizika na siku nyingine ya kisasi yenye kuenea sana, wakati Yehova atakapoleta uharibifu wa mfumo mzima wa mambo ya ulimwengu huu kwenye “dhiki kubwa.”—Mathayo 24:21.

      9. Ni nani leo wanaofaidika na mwaka wa Yehova wa nia njema?

      9 Ni nani leo wanaofaidika na mwaka wa Mungu wa nia njema? Ni wale wanaoukubali ujumbe, wanaotii, na kuunga mkono kwa bidii kazi ya kutangaza Ufalme wa Mungu katika “mataifa yote.” (Marko 13:10) Watu wa jinsi hiyo wanaona kuwa zile habari njema huleta faraja halisi. Hata hivyo, wale wanaoukataa ujumbe, na kukataa kuutumia vizuri mwaka wa nia njema ya Yehova maadamu ungali upo, watakabiliana na siku yake ya kisasi hivi karibuni.—2 Wathesalonike 1:6-9.

      Tunda la Kiroho Linalomtukuza Mungu

      10. Wayahudi wanaorudi kutoka Babiloni wanapatwa na hisia gani kutokana na tendo kubwa ambalo Yehova anawafanyia?

      10 Wayahudi wanaorudi kutoka Babiloni wanatambua kwamba Yehova amewafanyia tendo kubwa. Kuomboleza kwao wakiwa mateka kunageuka kuwa furaha nyingi na sifa kwa sababu hatimaye wamekuwa huru. Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.

      11. Ni nani katika karne ya kwanza waliokuwa na sababu nzuri ya kumsifu Yehova kuhusu tendo lake kubwa?

      11 Katika karne ya kwanza, hata Wayahudi waliokubali kufunguliwa watoke katika kifungo cha dini ya uwongo walimsifu Mungu kwa tendo kubwa alilowafanyia. Badala ya roho yao iliyoshuka, wakawa na “vazi la sifa” walipokombolewa kutoka katika taifa lililokufa kiroho. Badiliko hilo liliwapata kwanza wanafunzi wa Yesu walipoacha kuombolezea kifo chake wakaanza kushangilia wakati Bwana wao aliyefufuliwa alipowatia mafuta kwa roho takatifu. Upesi baada ya hapo, badiliko kama hilo lilipata kila mmoja wa watu watiifu 3,000 walioitikia na kubatizwa kwenye Pentekoste ya 33 W.K. baada ya kuhubiriwa na Wakristo hao waliotiwa mafuta karibuni. (Matendo 2:41) Ilikuwa vizuri kama nini kuwa na uhakika wa kupata baraka ya Yehova! Badala ya ‘kulilia Sayuni,’ walipokea roho takatifu wakaburudishwa na “mafuta ya furaha,” yanayofananisha furaha nyingi ya wale wanaobarikiwa sana na Yehova.—Waebrania 1:9.

      12, 13. (a) Ni akina nani waliokuwa ‘miti mikubwa ya haki’ miongoni mwa Wayahudi wenye kurudi mwaka wa 537 K.W.K.? (b) Ni akina nani ambao wamekuwa ‘miti mikubwa ya haki’ tangu Pentekoste ya 33 W.K.?

      12 Yehova anawabariki watu wake kwa kuwapa ‘miti mikubwa ya haki.’ Miti hiyo mikubwa ni akina nani? Katika miaka iliyofuata mwaka wa 537 K.W.K., miti hiyo ilikuwa watu mmoja-mmoja waliojifunza Neno la Mungu na kulitafakari, kisha wakasitawisha viwango vya Yehova vya uadilifu. (Zaburi 1:1-3; Isaya 44:2-4; Yeremia 17:7, 8) Wanaume kama vile Ezra, Hagai, Zekaria, na Kuhani Mkuu Yoshua walionekana hakika kwamba wao ni ‘miti mikubwa’ ya kutokeza—watu walio imara kuitetea kweli na kupinga uchafuzi wa kiroho katika taifa hilo.

      13 Kuanzia Pentekoste ya 33 W.K. na kuendelea, Mungu alipanda ‘miti mikubwa ya haki’ kama hiyo, yaani Wakristo watiwa-mafuta walio na moyo mkuu. Aliwapanda katika makao ya kiroho ya taifa lake jipya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Baada ya karne nyingi kupita, hatimaye idadi ya “miti” hiyo imekuwa 144,000, na inazaa matunda ya uadilifu ili kumrembesha, au kumtukuza, Yehova Mungu. (Ufunuo 14:3) Wale wa mwisho wa “miti” hiyo yenye fahari wamesitawi katika miaka ya tangu 1919, wakati Yehova alipowahuisha mabaki wa Israeli wa Mungu kutoka kwenye hali yao ya kutotenda kwa muda. Kwa kuwapa maji tele ya kiroho, inaweza kusemwa kwamba Yehova ametokeza msitu wa miti ya haki, yenye kuzaa matunda.—Isaya 27:6.

      14, 15. Waabudu wa Yehova waliofunguliwa walianza miradi gani kuanzia mwaka wa (a) 537 K.W.K.? (b) 33 W.K.? (c) 1919?

      14 Akikazia kazi ya “miti” hii, Isaya anaendelea kusema hivi: “Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.” (Isaya 61:4) Chini ya amri ya Mfalme Koreshi wa Uajemi, Wayahudi waaminifu waliorudi Babiloni walijenga upya Yerusalemu na hekalu lake lililokuwa limeachwa ukiwa muda mrefu sana. Pia, katika miaka iliyofuata mwaka wa 33 W.K. na mwaka wa 1919 kungetokea miradi ya kurudisha hali nzuri za kwanza.

      15 Mwaka wa 33 W.K., wanafunzi wa Yesu walihuzunika sana alipokamatwa, akajaribiwa, na kuuawa. (Mathayo 26:31) Hata hivyo, maoni yao yalibadilika alipowatokea baada ya kufufuliwa kwake. Kisha roho takatifu ilipomiminwa juu yao, walijishughulisha na kazi ya kuzihubiri habari njema, “katika Yerusalemu na pia katika Yudea yote na Samaria na hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8) Hivyo walianza kurudisha ibada safi. Vivyo hivyo, kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, Yesu Kristo alisababisha mabaki ya ndugu zake watiwa-mafuta wajenge upya “mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.” Kwa muda wa karne nyingi, makasisi wa Jumuiya ya Wakristo walikuwa wameshindwa kuwapa watu ujuzi wa Yehova, wakawapa mapokeo ya kibinadamu na mafundisho yasiyo ya Kimaandiko. Wakristo watiwa-mafuta walisafisha makutaniko yao kwa kuondoa mazoea yenye madoa ya dini ya uwongo ili kazi ya kurudisha ibada ya kweli isonge mbele. Halafu wakaanza shughuli ambayo ingekuja kuwa kubwa kuliko shughuli zote za kutoa ushahidi ulimwenguni.—Marko 13:10.

      16. Ni nani wamekuwa wakiwasaidia Wakristo watiwa-mafuta katika kazi yao ya kurudisha ibada safi, na wamekabidhiwa majukumu yapi?

      16 Huo ulikuwa utume mkubwa sana. Wale mabaki wa Israeli wa Mungu walio wachache kwa ulinganisho wangetimizaje jukumu hilo? Yehova alimpulizia Isaya kutangaza hivi: “Wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.” (Isaya 61:5) Kwa njia ya mfano, wageni hao na watu walio wa kabila nyingine wamekuwa “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu.a (Ufunuo 7:9; Yohana 10:11, 16) Wao hawatiwi mafuta kwa roho takatifu kupata urithi wa kimbingu. Bali, wana tumaini la kupata uhai wa milele katika dunia-paradiso. (Ufunuo 21:3, 4) Na bado, wanampenda Yehova na wamekabidhiwa wajibu wa kiroho wa kufanya uchungaji, ukulima, na utunzaji wa mizabibu. Utendaji huo si kazi za hali ya chini. Chini ya mwelekezo wa mabaki wa Israeli wa Mungu, wafanyakazi hawa husaidia kuchunga, kulea, na kuvuna watu.—Luka 10:2; Matendo 20:28; 1 Petro 5:2; Ufunuo 14:15, 16.

      17. (a) Washirika wa Israeli wa Mungu wataitwaje? (b) Ni dhabihu gani moja tu inayohitajiwa ili kuwe na msamaha wa dhambi?

      17 Namna gani juu ya Israeli wa Mungu? Yehova anawaambia hivi, kupitia Isaya: “Bali ninyi mtaitwa makuhani wa BWANA; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao.” (Isaya 61:6) Katika Israeli ya kale, Yehova alifanya uandalizi ili ukuhani wa Kilawi utoe dhabihu kwa niaba ya makuhani wenyewe na Waisraeli wenzao. Hata hivyo, mwaka wa 33 W.K., Yehova alikoma kutumia ukuhani wa Kilawi na kuanzisha mpango mzuri zaidi. Aliukubali uhai mkamilifu wa Yesu kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Tangu wakati huo, hakuna dhabihu nyingine yoyote ambayo imehitajiwa. Dhabihu ya Yesu ina nguvu za kutumika daima dawamu.—Yohana 14:6; Wakolosai 2:13, 14; Waebrania 9:11-14, 24.

      18. Israeli wa Mungu wanakuwa ukuhani wa aina gani, na wana utume gani?

      18 Basi, washirika wa Israeli wa Mungu ni ‘makuhani wa Yehova’ jinsi gani? Akiwaandikia Wakristo wenzake watiwa-mafuta, mtume Petro alisema hivi: “Nyinyi ni ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya miliki ya pekee, kwamba mpate kutangaza kotekote sifa bora kabisa’ za yeye aliyewaita nyinyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.” (1 Petro 2:9) Kwa hiyo, wakiwa kikundi, Wakristo watiwa-mafuta wanakuwa ukuhani wenye utume hususa: kuyaambia mataifa juu ya utukufu wa Yehova. Wanapaswa kuwa mashahidi wake. (Isaya 43:10-12) Muda wote wa siku za mwisho, Wakristo watiwa-mafuta wameutimiza utume huo muhimu kwa uaminifu. Matokeo ni kwamba, sasa mamilioni ya watu wanashirikiana nao katika kazi ya kutoa ushahidi juu ya Ufalme wa Yehova.

      19. Wakristo watiwa-mafuta watapendelewa kufanya utumishi gani?

      19 Zaidi ya hilo, washirika wa Israeli wa Mungu wana tazamio la kutumikia wakiwa makuhani kwa njia nyingine. Wakiisha kufa, wanafufuliwa mbinguni wakiwa roho wasioweza kufa. Licha ya kutumikia wakiwa watawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake huko, wanatumikia pia wakiwa makuhani wa Mungu. (Ufunuo 5:10; 20:6) Katika hali hiyo, watapendelewa kutumia faida za dhabihu ya fidia ya Yesu kuelekea wanadamu waaminifu duniani. Katika njozi ya mtume Yohana iliyoandikwa katika Ufunuo sura ya 22, wanatajwa tena kuwa “miti.” “Miti” yote 144,000 inaonwa ikiwa mbinguni, ikitokeza ‘mazao kumi na mawili ya matunda, ikitoa matunda yake kila mwezi. Na majani ya hiyo miti yalikuwa ya kuponya mataifa.’ (Ufunuo 22:1, 2) Lo, huo ni utumishi wa kikuhani ulio mzuri kama nini!

      Aibu na Fedheha, Kisha Furaha

      20. Ijapokuwa kuna upinzani, ni baraka gani ambayo ukuhani wa kifalme unaingojea?

      20 Tangu 1914, wakati mwaka wa Yehova wa nia njema ulipoanza, ule ukuhani wa kifalme umekuwa ukipingwa-pingwa tu na makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. (Ufunuo 12:17) Hata hivyo, hatimaye jitihada zote za kukomesha kuhubiriwa kwa habari njema zimeshindwa kabisa kufanikiwa. Unabii wa Isaya ulitabiri hilo, ukisema hivi: “Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele.”—Isaya 61:7.

      21. Wakristo watiwa-mafuta walikujaje kufurahia baraka maradufu?

      21 Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, mabaki watiwa-mafuta waliaibishwa na kutiwa fedheha na Jumuiya ya Wakristo yenye utukuzo wa taifa. Makasisi walikuwa miongoni mwa wale waliowashtaki ndugu wanane waaminifu wa makao makuu jijini Brookyln kwa kuwasingizia eti ni wachochezi waliopinga serikali. Ndugu hao walitiwa gerezani bila haki kwa muda wa miezi tisa. Mwishowe, katika Machi ya mwaka wa 1919, waliwekwa huru, na baadaye mashtaka yao yote yakaondolewa. Hivyo, njama ya wapinzani ya kukomesha kazi ya kuhubiri ikawarudia wao wenyewe. Badala ya kuwaacha waabudu wake waaibishwe daima, Yehova aliwakomboa, akawarudisha kwenye makao yao ya kiroho, yaani “nchi yao.” Wakiwa humo, walipokea baraka maradufu. Mateso yao yakawa si kitu kwa kulinganishwa na baraka tele za Yehova. Hakika walikuwa na sababu ya kupaaza sauti ya shangwe!

      22, 23. Wakristo watiwa-mafuta wamemwigaje Yehova, naye amewathawabishaje?

      22 Maneno ya Yehova yanayofuata yana sababu nyingine ya kuwafanya Wakristo leo washangilie: “Mimi, BWANA, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu; nami nitawalipa malipo katika kweli, nitaagana nao agano la milele.” (Isaya 61:8) Kupitia funzo lao la Biblia, mabaki watiwa-mafuta walijifunza kupenda haki na kuchukia uovu. (Mithali 6:12-19; 11:20) Walijifunza ‘kufua panga zao ziwe majembe,’ wakabaki bila kuwamo katika vita vya wanadamu na katika misukosuko ya kisiasa. (Isaya 2:4) Pia waliacha mazoea ya kumvunjia Mungu heshima, kama vile uchongezi, uzinzi, wivi, na ulevi.—Wagalatia 5:19-21.

      23 Kwa sababu Wakristo watiwa-mafuta wanapenda haki kama Muumba wao, Yehova amewapa ‘malipo yao katika kweli.’ Mojawapo ya “malipo” ya jinsi hiyo ni agano la kudumu kwa wakati usiojulikana—lile agano jipya—ambalo Yesu aliwatangazia wafuasi wake usiku uliotangulia kufa kwake. Agano hilo ndilo lililoweka msingi wa kuwa kwao taifa la kiroho, watu wa pekee wa Mungu. (Yeremia 31:31-34; Luka 22:20) Chini ya agano hilo, Yehova atatumia faida zote za dhabihu ya fidia ya Yesu, kutia na msamaha wa dhambi kwa ajili ya watiwa-mafuta na wanadamu wengine wote waaminifu.

      Kufurahia Sana Baraka za Yehova

      24. “Kizazi” kinachotoka katika mataifa na kubarikiwa ni akina nani, nao wamekuwaje “kizazi”?

      24 Wengine miongoni mwa mataifa wametambua kwamba baraka ya Yehova iko juu ya watu wake. Hiyo ilitabiriwa na ahadi hii ya Yehova: “Kizazi chao kitajulikana katika mataifa, na uzao wao katika kabila za watu; wote wawaonao watakiri ya kuwa wao ni kizazi kilichobarikiwa na BWANA.” (Isaya 61:9) Washirika wa Israeli wa Mungu, yaani Wakristo watiwa-mafuta, wamekuwa watendaji miongoni mwa mataifa wakati wa mwaka wa Yehova wa nia njema. Leo, mamilioni ya watu wameikubali huduma ya hao watiwa-mafuta. Kwa kushirikiana karibu-karibu na Israeli wa Mungu, wale wanaotoka katika mataifa wana pendeleo la kuwa ‘kizazi kilichobarikiwa na Yehova.’ Hali yao ya furaha inaonekana na wanadamu wote.

      25, 26. Wakristo wote wanaonyeshaje maoni yale yale yanayotajwa katika Isaya 61:10?

      25 Wakristo wote, watiwa-mafuta na kondoo wengine, wanatazamia kumsifu Yehova milele hata milele. Wanakubaliana kwa moyo wote na nabii Isaya, anayesema hivi kwa kupuliziwa: “Mimi nitachachawa katika Yehova bila kukosa. Nafsi yangu itakuwa na shangwe katika Mungu wangu. Kwa maana yeye amenivika mavazi ya wokovu; amenizungushia joho la uadilifu, kama bwana-arusi ambaye, kwa njia ya kikuhani, huvaa vazi la kichwani, na kama bibi-arusi anayejipamba kwa vitu vyenye mapambo.”—Isaya 61:10, “NW.”

      26 Wakiwa wamevaa “joho la uadilifu,” Wakristo watiwa-mafuta wamepiga moyo konde kubaki wakiwa wenye utakato na usafi machoni pa Yehova. (2 Wakorintho 11:1, 2) Wakiisha kutangazwa na Yehova kuwa waadilifu kwa kusudi la kurithi uhai wa kimbingu, hawatayarudia kamwe makao yenye ukiwa ya Babiloni Mkubwa, ambaye wamekombolewa kutoka kwake. (Waroma 5:9; 8:30) Kwao, yale mavazi ya wokovu ni ya thamani sana. Vivyo hivyo waandamani wao ambao ni kondoo wengine wamepiga moyo konde kufuata viwango vya juu vya ibada safi ya Yehova Mungu. Wakiisha ‘kufua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo,’ wanatangazwa kuwa waadilifu na wataiokoka “dhiki kubwa.” (Ufunuo 7:14; Yakobo 2:23, 25) Hadi wakati huo, wanawaiga waandamani wao watiwa-mafuta kwa kuepuka kuchafuliwa na Babiloni Mkubwa.

      27. (a) Ni ‘uoteshaji’ gani wenye kutazamisha utakaokuwako wakati wa Utawala wa Milenia? (b) Tayari haki inaoteshwaje miongoni mwa jamii ya wanadamu?

      27 Leo waabudu wa Yehova wanafurahia kuwa katika paradiso ya kiroho. Karibuni watafurahia Paradiso halisi pia. Kwa mioyo yetu yote, tunautazamia wakati huo unaoelezwa dhahiri katika maneno ya kumalizia ya Isaya sura ya 61: “Kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.” (Isaya 61:11) Wakati wa Milenia ya Kristo, dunia ‘itaoteshwa haki.’ Wanadamu watapaaza sauti kwa shangwe, na haki itapanuka hadi miisho ya dunia. (Isaya 26:9) Hata hivyo, si lazima tuingoje siku hiyo tukufu ndipo tutoe sifa mbele ya mataifa yote. Tayari haki inaoteshwa miongoni mwa mamilioni ya watu wanaompa utukufu Mungu wa mbinguni na kuzitangaza habari njema juu ya Ufalme wake. Hata sasa imani na tumaini letu zinatupa kila sababu ya kufurahia baraka za Mungu wetu.

      [Maelezo ya Chini]

      a Isaya 61:5 yaweza kuwa ilitimizwa nyakati za kale, kwa kuwa watu wasio Wayahudi waliambatana na Wayahudi wa asili wakati wa kurudi kwao Yerusalemu, na inaelekea walisaidia kuirudishia nchi hali yake ya kwanza. (Ezra 2:43-58) Hata hivyo, kuanzia mstari wa 6 unabii unaelekea kutumika kuhusu Israeli wa Mungu peke yake.

      [Picha katika ukurasa wa 323]

      Isaya ana habari njema za kuwatangazia mateka Wayahudi

      [Picha katika ukurasa wa 331]

      Kuanzia mwaka wa 33 W.K., Yehova amepanda ‘miti mikubwa ya haki’ 144,000

      [Picha katika ukurasa wa 334]

      Dunia itaoteshwa haki

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Tatu

      “Jina Jipya”

      Isaya 62:1-12

      1. Ni uhakikisho gani ambao umeandikwa katika Isaya sura ya 62?

      WAYAHUDI walioshuka moyo kule Babiloni wanahitaji hasa kupewa uhakikisho, faraja, na tumaini la kurudishwa. Miongo kadhaa imepita tangu Yerusalemu na hekalu lake ziharibiwe. Umbali wa kilometa 800 hivi kutoka Babiloni, nchi ya Yuda imekaa hali ya ukiwa, na inaonekana ni kama Wayahudi wamesahauliwa na Yehova. Ni nini kinachoweza kuleta maendeleo katika hali yao? Ni ahadi za kwamba Yehova atawarejesha nyumbani na kuwaruhusu warudishe ibada safi. Ndipo mitajo kama vile “Aliyeachwa” na “Ukiwa” zitaondolewa, na badala yake kuweko majina yanayoonyesha ukubali wa Mungu. (Isaya 62:4; Zekaria 2:12) Sura ya 62 ya Isaya imejaa ahadi hizo. Hata hivyo, kama vile unabii mwingine mbalimbali wa kurudishwa, sura hii inagusia masuala mengi sana, wala si kukombolewa tu kwa Wayahudi ili watoke utekwani kule Babiloni. Katika utimizo wake mkubwa, Isaya sura ya 62 inatuhakikishia kwamba wokovu wa taifa la kiroho la Yehova, yule “Israeli wa Mungu,” ni hakika.—Wagalatia 6:16.

      Yehova Hakai Kimya

      2. Kwa mara nyingine, Yehova anaonyeshaje kwamba anamkubali Sayuni?

      2 Babiloni yapinduliwa mwaka wa 539 K.W.K. Baada ya hapo, Mfalme Koreshi wa Uajemi anatoa amri inayowawezesha Wayahudi wanaomhofu Mungu warejee Yerusalemu wakairudishe ibada ya Yehova. (Ezra 1:2-4) Mwaka wa 537 K.W.K., Wayahudi wa kwanza kurudi wamekwisha fikia nchi yao. Kwa mara nyingine Yehova anaonyesha kwamba anamkubali Yerusalemu, kama vile inavyoonyeshwa kwa uchangamfu unaotumiwa kutoa tangazo lake la kiunabii: “Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia [“sitakaa kimya,” “NW”], hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo [“mwenge,” “VB”].”—Isaya 62:1.

      3. (a) Kwa nini Sayuni wa kidunia anakataliwa na Yehova mwishowe, na ni nani anayechukua mahali pake? (b) Ni ukengeufu gani unaotukia, unatukia wakati gani, nasi tunaishi katika kipindi gani leo?

      3 Mwaka wa 537 K.W.K., Yehova alitimiza ahadi yake kuelekea Sayuni, au Yerusalemu, iliyorudishwa. Wakaaji wake waliona akiwapa wokovu, na uadilifu wao ukang’aa sana. Ingawa hivyo, baadaye walipeperuka wakaiacha ibada safi. Mwishowe wakamkataa Mesiya, naye Yehova hatimaye akawaacha kabisa wasiwe taifa lake teule. (Mathayo 21:43; 23:38; Yohana 1:9-13) Yehova alisababisha taifa jipya, “Israeli wa Mungu,” lizaliwe. Taifa hili jipya likawa watu wake wa pekee, na katika karne ya kwanza, washirika wake wakazihubiri habari njema kwa bidii kotekote katika ulimwengu uliojulikana wakati huo. (Wagalatia 6:16; Wakolosai 1:23) Inahuzunisha kwamba baada ya mitume kufa kulitokea ukengeufu wa kuiacha dini ya kweli. Matokeo ni kwamba, Ukristo wa namna fulani ya uasi-imani ulisitawi, ule unaopatikana katika Jumuiya ya Wakristo leo. (Mathayo 13:24-30, 36-43; Matendo 20:29, 30) Kwa karne nyingi, Jumuiya ya Wakristo ikawa imeruhusiwa kuleta suto kubwa juu ya jina la Yehova. Hata hivyo, mwishowe “mwaka wa nia njema” wa Yehova ukaanza katika mwaka wa 1914, pamoja na utimizo mkubwa wa sehemu hii ya unabii wa Isaya.—Isaya 61:2, NW.

      4, 5. (a) Sayuni na watoto wake wanafananisha nani leo? (b) Yehova ametumiaje Sayuni ili kufanya ‘wokovu wake uwe kama taa iwakayo’?

      4 Leo ahadi ya Yehova ya kurudisha Sayuni imetimizwa kuhusiana na tengenezo lake la kimbingu, “Yerusalemu la juu,” kama vile linavyowakilishwa duniani na watoto wake, Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho. (Wagalatia 4:26) Tengenezo la Yehova la kimbingu ni msaidiaji mwenye moyo wa kujitoa—ni mlinzi aliye macho, mwenye upendo, na mwenye bidii. Mwaka wa 1914 ulikuwa pindi ya kusisimua kama nini wakati tengenezo hilo lilipozaa Ufalme wa Kimesiya! (Ufunuo 12:1-5) Kuanzia 1919 hasa, watoto wake wa kidunia wamehubiria mataifa kuhusu haki na wokovu wa tengenezo hilo. Kama vile Isaya alivyotabiri, watoto hawa wamelimulika giza kama mwenge, wakiacha nuru yao ing’ae.—Mathayo 5:15, 16; Wafilipi 2:15.

      5 Yehova anapendezwa sana na waabudu wake na hatapumzika, wala kukaa kimya, mpaka atimize ahadi zote alizomtolea Sayuni na watoto wake. Hata mabaki ya watiwa-mafuta pamoja na waandamani wao walio “kondoo wengine” wanakataa kukaa kimya. (Yohana 10:16) Wanatoa sauti kweli kweli wakiwaonyesha watu njia pekee ya kupata wokovu.—Waroma 10:10.

      Wapewa “Jina Jipya” na Yehova

      6. Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni?

      6 Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni, “mwanamke” wake wa kimbingu, aliyewakilishwa na Yerusalemu la kale? Anasema hivi: “Mataifa wataiona haki yako [“Ee mwanamke,” “NW”], na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.” (Isaya 62:2) Wakati Waisraeli wanapotenda uadilifu, mataifa yanalazimika kuangalia kwa makini. Hata wafalme wanalazimika kukubali kwamba Yehova anatumia Yerusalemu na kwamba utawala wowote walio nao si kitu ukilinganishwa na Ufalme wa Yehova.—Isaya 49:23.

      7. Jina jipya la Sayuni linamaanisha nini?

      7 Sasa Yehova anampa Sayuni jina jipya ili kuthibitisha kwamba hali yake imebadilika. Jina hilo jipya linamaanisha hali yenye baraka na cheo chenye heshima kinachofurahiwa na watoto wa kidunia wa Sayuni kuanzia mwaka wa 537 K.W.K.a Linaonyesha kwamba Yehova anamkubali Sayuni kuwa mali yake. Leo, Israeli wa Mungu wanasisimuka kuwa kipenzi cha Yehova kwa njia hiyo, na wale kondoo wengine wanashangilia pamoja nao.

      8. Yehova amemheshimu Sayuni kwa njia zipi?

      8 Akiisha kumpa Sayuni jina jipya, sasa Yehova anaahidi hivi: “Utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa BWANA, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.” (Isaya 62:3) Yehova anamwinua mke wake wa mfano, Sayuni wa kimbingu, atazamwe kwa mshangao kwa sababu anavutia. (Zaburi 48:2; 50:2) Taji la uzuri na “kilemba cha kifalme” zinaonyesha kwamba mke huyo amevikwa heshima na mamlaka. (Zekaria 9:16) Israeli wa Mungu, ambaye anawakilisha Sayuni wa kimbingu, au “Yerusalemu la juu,” ametokea kwa kufanyizwa vizuri ajabu na mkono wa Mungu, yaani nguvu zake zikiwa katika hali ya kutumika. (Wagalatia 4:26) Kwa msaada wa Yehova, taifa hilo la kiroho limeweka kumbukumbu zuri ajabu la uaminifu wa maadili na moyo wa kujitoa kwa muda mrefu. Mamilioni ya watu, kutia na watiwa-mafuta na kondoo wengine, wanaimarishwa kuonyesha imani na upendo wa kutokeza. Wakati wa Utawala wa Milenia ya Kristo, watiwa-mafuta, wakiisha kufikia thawabu yao tukufu ya kimbingu, watatumiwa kama vyombo mkononi mwa Yehova ili kuinua uumbaji unaougua ufikie kiwango cha uhai wa milele.—Waroma 8:21, 22; Ufunuo 22:2.

      ‘Yehova Amekufurahia’

      9. Eleza jinsi hali ya Sayuni inavyogeuzwa.

      9 Upaji wa jina jipya ni sehemu ya kumgeuza Sayuni wa kimbingu, anayewakilishwa na watoto wake wa kidunia, ili awe na hali ya kupendeza. Tunasoma hivi: “Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefsiba [Namfurahia]; na nchi yako Beula [Ameolewa]; kwa kuwa BWANA anakufurahia, na nchi yako itaolewa.” (Isaya 62:4) Sayuni wa kidunia amekuwa ukiwa tangu alipoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. Hata hivyo, maneno ya Yehova yanamhakikishia kwamba nchi yake itarudishiwa hali yake ya kwanza na kujazwa wakaaji tena. Sayuni aliyeteketezwa wakati mmoja hatakuwa tena mwanamke aliyeachwa pweke, wala nchi yake haitakuwa ukiwa tena. Kurudishwa kwa Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. kunamaanisha kwamba atapata hali mpya, inayotofautiana kabisa na hali yake ya kwanza ya kuwa magofu. Yehova anatangaza kwamba Sayuni ataitwa “Namfurahia,” na nchi yake itaitwa “Ameolewa.”—Isaya 54:1, 5, 6; 66:8; Yeremia 23:5-8; 30:17; Wagalatia 4:27-31.

      10. (a) Hali ya Israeli wa Mungu iligeuzwaje? (b) “Nchi” ya Israeli wa Mungu ni nini?

      10 Kuanzia mwaka wa 1919 badiliko kama hilo lilipata Israeli wa Mungu. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, Wakristo watiwa-mafuta walionekana ni kama wamekataliwa na Mungu. Lakini mwaka wa 1919 walirudishiwa hali ya kukubalika, na njia yao ya kuabudu ikatakaswa. Jambo hilo liligeuza mafundisho yao, tengenezo lao, na utendaji wao. Taifa la Israeli wa Mungu liliingia katika “nchi” yake, miliki yake ya kiroho, au makao ya utendaji.—Isaya 66:7, 8, 20-22.

      11. Wayahudi wanamwoaje mama yao?

      11 Yehova anazidi kukazia hali mpya ya kukubalika kwa watu wake, anapotangaza hivi: “Kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amafurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.” (Isaya 62:5) Wayahudi, wale “wana” wa Sayuni, wanawezaje kumwoa mama yao? Katika maana ya kwamba wana wa Sayuni wanaorudi baada ya kufunguliwa watoke uhamishoni Babiloni wanamiliki jiji lao kuu la zamani na kukaa humo tena. Inapokuwa hivyo, Sayuni si mkiwa tena, bali ana wana chungu nzima.—Yeremia 3:14.

      12. (a) Yehova amejulishaje wazi kwamba Wakristo watiwa-mafuta ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika ndoa? (b) Shughuli za Yehova pamoja na watu wake zinatoaje kielelezo cha ndoa ya hali ya juu leo? (Ona sanduku katika ukurasa wa 342.)

      12 Kwa njia ya ulinganifu, tangu mwaka wa 1919 watoto wa Sayuni wa kimbingu wamemiliki nchi yao, miliki yao ya kiroho, iliyo na jina la kiunabii “Ameolewa.” Utendaji wao wa Kikristo katika nchi hiyo umeonyesha wazi kwamba Wakristo hawa watiwa-mafuta ni “watu kwa ajili ya jina lake” Yehova. (Matendo 15:14) Kuzaa kwao matunda ya Ufalme na kutangaza jina la Yehova kumeonyesha wazi kwamba Yehova huwafurahia sana Wakristo hawa. Yeye ameonyesha wazi kwamba wao ni sehemu ya tengenezo ambalo limeungana naye katika umoja usiovunjika. Kwa kuwatia mafuta Wakristo hawa kwa roho takatifu, kuwakomboa watoke katika utekwa wa kiroho, na kuwatumia ili wahubirie jamii yote ya wanadamu tumaini la Ufalme, Yehova ameonyesha kwamba anawashangilia kwa shangwe ya bwana-arusi kumwelekea bibi-arusi.—Yeremia 32:41.

      “Msiwe na Kimya”

      13, 14. (a) Nyakati za kale, Yerusalemu linakuwaje jiji lenye usalama? (b) Nyakati za kisasa, Sayuni amekuwaje “sifa duniani”?

      13 Jina jipya la mfano ambalo Yehova amewapa watu wake huwafanya wahisi usalama. Wanajua kwamba yeye huwakubali na kwamba wao ni miliki yake. Sasa Yehova anatumia mfano tofauti na kuongea na watu wake kana kwamba anaongea na jiji lenye kuta: “Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha [“kumtaja,” “NW”] BWANA, msiwe na kimya; wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.” (Isaya 62:6, 7) Katika wakati wa Yehova, baada ya mabaki waaminifu kutoka Babiloni, Yerusalemu linakuwa “sifa duniani”—jiji lenye kuta za kuwapa wakaaji wake usalama. Mchana na usiku, walinzi katika kuta hizo wako macho kuhakikisha kwamba jiji lina usalama, na kuwapasha wakaaji wake habari za kuwaonya.—Nehemia 6:15; 7:3; Isaya 52:8.

      14 Nyakati za kisasa Yehova amewatumia walinzi wake watiwa-mafuta kuwaonyesha watu watiifu njia ya kupata uhuru kutoka kwenye utumwa wa dini ya uwongo. Watu hao wamealikwa waje ndani ya tengenezo lake, ambamo wanalindwa wasipatwe na uchafu wa kiroho, mavutano ya kutomhofu Mungu, na ili wasichukiwe na Yehova. (Yeremia 33:9; Sefania 3:19) Jamii ya mlinzi, yaani yule “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” inatimiza fungu muhimu sana la kutoa ulinzi huo, kwani inaandaa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao.’ (Mathayo 24:45-47) Kwa kufanya kazi na jamii ya mlinzi, ule “umati mkubwa” pia hushiriki sehemu ya maana katika kufanya Sayuni awe “sifa duniani.”—Ufunuo 7:9.

      15. Jamii ya mlinzi na waandamani wao wanamtumikiaje Yehova daima?

      15 Jamii ya mlinzi na waandamani wake inaendelea kutoa utumishi! Mtazamo wao wa kujitoa kwa nafsi yote unaonekana katika utendaji wenye bidii unaofanywa na mamilioni ya watu mmoja-mmoja walio waaminifu, huku wakiungwa mkono na waangalizi wanaosafiri na wake zao; watu waliojitolea katika makao mbalimbali ya Betheli na katika sehemu za uchapaji za Mashahidi wa Yehova; mishonari; na mapainia wa pekee, wa kawaida, na wasaidizi. Zaidi ya hilo, wanajibidiisha kujenga Majumba mapya ya Ufalme, kutembelea wagonjwa, kusaidia watu mmoja-mmoja wanaokabili hali ngumu za kitiba, na kuwapa msaada wa wakati wake wale wanaopatwa na majanga na misiba. Mara nyingi, wengi wa watu hawa wenye kujidhabihu hutumikia kihalisi “mchana na usiku”!—Ufunuo 7:14, 15.

      16. Ni jinsi gani watumishi wa Yehova ‘wasivyomwacha akae kimya’?

      16 Watumishi wa Yehova wanatiwa moyo kusali bila kukoma, kumwomba Mungu ‘mapenzi yake yatendeke, kama ilivyo katika mbingu, pia juu ya dunia.’ (Mathayo 6:9, 10; 1 Wathesalonike 5:17) Wanahimizwa hivi: “Msimwache [Yehova] akae kimya” mpaka awatimizie tamaa zenu na matumaini yanayohusiana na kurudishwa kwa ibada ya kweli. Yesu alikazia uhitaji wa kusali daima, akawahimiza wafuasi wake ‘kumpaazia Mungu kilio mchana na usiku.’—Luka 18:1-8.

      Kutumikia Mungu Kutathawabishwa

      17, 18. (a) Wakaaji wa Sayuni wanaweza kutazamiaje kufurahia matunda ya kazi yao? (b) Watu wa Yehova leo wanafurahiaje matunda ya kazi yao?

      17 Jina jipya ambalo Yehova anawapa watu wake linawahakikishia kwamba jitihada zao si za bure. “BWANA ameapa kwa mkono wake wa kuume, na kwa mkono wa nguvu zake, Hakika sitawapa adui zako nafaka yako tena kuwa chakula chao; wala wageni hawatakunywa divai yako, uliyoifanyia kazi. Lakini walioivuna, ndio watakaoila, na kumhimidi BWANA; na walioichuma, ndio watakaoinywa, ndani ya nyua za patakatifu pangu.” (Isaya 62:8, 9) Mkono wa kuume wa Yehova na mkono wa nguvu zake ni ishara za kuonyesha uwezo wake na nguvu zake. (Kumbukumbu la Torati 32:40; Ezekieli 20:5) Anapoapa kwa mkono wake wa kuume na kwa mkono wa nguvu zake, hiyo inaonyesha kwamba amepiga moyo konde kuibadili hali ya Sayuni. Mwaka wa 607 K.W.K., Yehova anaruhusu adui za Sayuni wamnyang’anye mali zake na kuzipora. (Kumbukumbu la Torati 28:33, 51) Lakini sasa, mali za Sayuni zitafurahiwa na wale tu walio na haki ya kuzigusa.—Kumbukumbu la Torati 14:22-27.

      18 Katika utimizo wa kisasa wa ahadi hiyo, watu wa Yehova waliorudishwa wanapata ufanisi mkubwa wa kiroho. Wanayafurahia kikamili matunda ya kazi yao, yaani idadi iliyoongezeka ya wanafunzi Wakristo na wingi wa chakula cha kiroho. (Isaya 55:1, 2; 65:14) Kwa sababu watu wake ni waaminifu, Yehova haachi adui zake wavuruge ufanisi wao wa kiroho wala wawanyang’anye matokeo ya utumishi wao wa nafsi yote. Hakuna kazi inayofanywa katika utumishi wa Yehova iliyo ya bure.—Malaki 3:10-12; Waebrania 6:10.

      19, 20. (a) Vikwazo vinaondolewaje njiani ili Wayahudi warudi Yerusalemu? (b) Katika nyakati za kisasa, vikwazo vimeondolewaje njiani ili watu watiifu waingie katika tengenezo la Yehova?

      19 Vilevile lile jina jipya linafanya tengenezo la Yehova liwavutie watu wenye mioyo ya kupenda haki. Makundi ya watu yanalimiminikia, na njia inaachwa wazi ili waendelee kuingia. Unabii wa Isaya unasema hivi: “Piteni, piteni, katika malango; itengenezeni njia ya watu; tutieni, tutieni barabara [“kuu,” “NW”]; toeni mawe yake; twekeni bendera kwa ajili ya kabila za watu.” (Isaya 62:10) Katika kisa cha kwanza, inaelekea kuwa mwito huu unamaanisha kupita na kutoka nje ya malango ya jiji ya Babilonia ili kurudi Yerusalemu. Hao wenye kurudi wanapaswa kuondoa mawe njiani ili kurahisisha safari na kuinua ishara ya kuonyesha njia ya kupitia.—Isaya 11:12.

      20 Tangu mwaka wa 1919, Wakristo watiwa-mafuta wamewekwa kando kwa ajili ya utumishi wa kimungu na wanasafiri katika ile “Njia ya utakatifu.” (Isaya 35:8) Walikuwa wa kwanza kutembea katika barabara kuu ya kiroho kutoka katika Babiloni Mkubwa. (Isaya 40:3; 48:20) Mungu aliwapa pendeleo la kuongoza katika kutangaza kazi zake hodari na kuwaonyesha wengine njia ya kuingia katika ile barabara kuu. Wao wenyewe ndio wangefaidika kwa kuondolea mbali mawe— kuondoa vikwazo njiani. (Isaya 57:14) Walihitaji kuyaona makusudi na mafundisho ya Mungu waziwazi. Imani za uwongo ni mawe ya kukwaza katika njia ya uhai, lakini Neno la Mungu ni “kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande.” Wakiwa nayo, Wakristo watiwa-mafuta walivunja-vunja mawe ya kukwaza ambayo yangeweza kuwatega wale waliotaka kumtumikia Yehova.—Yeremia 23:29.

      21, 22. Yehova amesimamisha ishara gani ili iwaongoze wale wanaotoka katika dini ya uwongo, nasi tunajuaje?

      21 Mwaka wa 537 K.W.K., jiji la Yerusalemu likawa ishara iliyowavutia mabaki Wayahudi ili warudi wakajenge hekalu upya. (Isaya 49:22) Mwaka wa 1919, mabaki watiwa-mafuta walipokombolewa kutoka kwenye utumwa wa dini ya uwongo, hawakutanga-tanga ovyo-ovyo. Walijua pa kwenda, kwa maana Yehova alikuwa amesimamisha ishara kwa ajili yao. Ishara gani? Ishara ile ile iliyotabiriwa kwenye Isaya 11:10, inayosema hivi: ‘Itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese litasimama kuwa ishara kwa kabila za watu.’ Mtume Paulo anatumia maneno hayo kumhusu Yesu. (Waroma 15:8, 12) Ndiyo, ile ishara ni Kristo Yesu, anayetawala akiwa Mfalme juu ya Mlima Sayuni wa kimbingu!—Waebrania 12:22; Ufunuo 14:1.

      22 Wakristo watiwa-mafuta na kondoo wengine pia wamekusanyika kumzunguka Yesu Kristo ili wajihusishe katika ibada ya Mungu Aliye Juu Zaidi inayounganisha watu. Utawala wake unasaidia kutetea enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu mzima na kubariki watu wa mataifa yote ya dunia ambao ni wanyofu moyoni. Je, hiyo si sababu ya kumfanya kila mmoja wetu ajiunge katika kumtukuza kwa kumpa sifa?

      “Wokovu Wako Unakuja”!

      23, 24. Wale walio na imani katika Mungu wanaletewaje wokovu?

      23 Jina jipya ambalo Yehova anapatia tengenezo lake lililo kama mke linahusiana na wokovu wa milele wa watoto wake. Isaya anaandika hivi: “Tazama, BWANA ametangaza habari mpaka mwisho wa dunia, Mwambieni binti Sayuni, Tazama, wokovu wako unakuja; tazama, thawabu yake i pamoja naye, na malipo yake yako mbele zake.” (Isaya 62:11) Wokovu uliwajia Wayahudi wakati Babiloni ilipoanguka, nao wakarudia nchi yao. Lakini maneno haya yanaelekeza kwenye jambo kubwa zaidi. Tangazo la Yehova linatokeza kikumbusha cha unabii huu wa Zekaria unaohusu Yerusalemu: “Furahi sana, Ee binti Sayuni; Piga kelele, Ee binti Yerusalemu; tazama, mfalme wako anakuja kwako; ni mwenye haki, naye ana wokovu; ni mnyenyekevu, amepanda punda, naam, mwana-punda, mtoto wa punda.”—Zekaria 9:9.

      24 Miaka mitatu na nusu baada ya Yesu kubatizwa katika maji na kutiwa mafuta kwa roho ya Mungu, alipanda punda akaingia Yerusalemu na kulisafisha hekalu la jiji hilo. (Mathayo 21:1-5; Yohana 12:14-16) Leo, Yesu Kristo ndiye anayewaletea wokovu wa Yehova wale wote wanaomwamini Mungu. Tangu atawazwe mwaka wa 1914, Yesu pia ndiye Hakimu na Mfishaji aliyewekwa na Yehova. Mwaka wa 1918, miaka mitatu na nusu baada ya yeye kutawazwa, alisafisha hekalu la kiroho la Yehova, kama linavyowakilishwa duniani na kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta. (Malaki 3:1-5) Alipoinuliwa awe ishara, hapo ndipo watu wa sehemu zote za dunia walipoanza kukusanywa ili kuunga mkono Ufalme wa Kimesiya. Kwa kufuata kielelezo cha kale, “wokovu” uliwajia Israeli wa Mungu walipofunguliwa kutoka Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919. Wafanyakazi wa mavuno wenye roho ya kujidhabihu wanapata “thawabu” au “malipo” ya uhai wa mbinguni usioweza kufa ama uhai wa milele duniani. Wote wale wanaobaki wakiwa waaminifu wanaweza kuwa na hakika kwamba ‘kazi yao ya jasho si bure kuhusiana na Bwana.’—1 Wakorintho 15:58.

      25. Watu wa Yehova wanahakikishiwa nini?

      25 Lo, kuna matazamio mazuri kama nini kwa ajili ya tengenezo la Yehova la kimbingu, kwa wawakilishi wake watiwa-mafuta hapa duniani, na kwa ajili ya kila mtu anayeshirikiana nao kwa bidii! (Kumbukumbu la Torati 26:19) Isaya alitoa unabii huu: “Nao watawaita, Watu watakatifu, waliokombolewa na BWANA; nawe utaitwa, Aliyetafutwa, Mji usioachwa.” (Isaya 62:12) Wakati mmoja “Yerusalemu la juu,” anayewakilishwa na Israeli wa Mungu, alihisi kuwa ameachwa. Hatahisi hivyo tena. Yehova atafurahi sana kuwalinda watu wake milele, huku wao pia wakifurahia kukubaliwa naye daima.

      [Maelezo ya Chini]

      a Katika unabii wa Biblia, “jina jipya” linaweza kumaanisha cheo kipya au pendeleo jipya.—Ufunuo 2:17; 3:12.

      [Sanduku katika ukurasa wa 342]

      Kielelezo cha Ndoa ya Hali ya Juu

      Watu wanapofunga ndoa, kila mmoja wao hutazamia mambo fulani katika muungano huo wa ndoa. Lakini Mungu ana matazamio gani? Ni yeye aliyeanzisha muungano wa ndoa. Alikusudia iwe namna gani?

      Jambo moja la kuonyesha maoni ya Mungu kuhusu ndoa linatokana na uhusiano wake na taifa la Israeli katika mambo mbalimbali. Isaya anauonyesha uhusiano huo kuwa kama ndoa. (Isaya 62:1-5) Angalia mambo ambayo Yehova Mungu akiwa kama “mume” anamfanyia “bibi-arusi” wake. Anamlinda na kumtakasa. (Isaya 62:6, 7, 12) Anamheshimu na kumthamini. (Isaya 62:3, 8, 9) Na anamfurahia sana huyo mke, kama vile inavyoonyeshwa na majina mapya anayompa.—Isaya 62:4, 5, 12.

      Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, Paulo anayarudia maelezo ya Isaya juu ya uhusiano ulio kati ya Yehova na Israeli wakati anapoulinganisha uhusiano wa mume na mke na ule wa Kristo na kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta.—Waefeso 5:21-27.

      Paulo aliwatia moyo Wakristo waige uhusiano ulio kati ya Yesu na kutaniko katika ndoa zao. Hakuwezi kuwako upendo mkubwa kuliko ule ulioonyeshwa na Yehova kuelekea Israeli na ule unaoonyeshwa na Kristo kuelekea kutaniko. Visa hivyo vya uhusiano wa kimfano vinaandaa kielelezo cha ndoa ya hali ya juu, yenye mafanikio na furaha kati ya Wakristo.—Waefeso 5:28-33.

      [Picha katika ukurasa wa 339]

      Yehova atamwita Sayuni wa kimbingu kwa jina jipya

      [Picha katika ukurasa wa 347]

      Nyakati za kisasa, jamii ya mlinzi wa Yehova haijakaa kimya

  • Yehova Ajifanyia Jina Maridadi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Nne

      Yehova Ajifanyia Jina Maridadi

      Isaya 63:1-14

      1, 2. (a) Wakristo wanapendezwaje kibinafsi na kuja kwa “siku ya Yehova”? (b) Ni suala gani la maana zaidi linalohusika katika kuja kwa siku ya Yehova?

      KWA karibu miaka elfu mbili, Wakristo wamekuwa ‘wakingojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova.’ (2 Petro 3:12; Tito 2:13) Inaeleweka ni kwa nini wanataka sana siku hiyo ifike. Ingawaje, hiyo ndiyo siku itakayokuwa mwanzo wa kitulizo cha kutopatwa tena na madhara  ya kutokamilika. (Waroma 8:22) Vilevile itawaondolea kabisa mikazo inayowapata katika hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.”—2 Timotheo 3:1.

      2 Hata hivyo, ingawa siku ya Yehova itawaletea waadilifu kitulizo, vilevile itawaletea uharibifu “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.” (2 Wathesalonike 1:7, 8) Hilo ni jambo linalostahili kufikiriwa kwa uzito. Je, kweli Mungu atawaharibu waovu ili tu awaokoe watu wake kutoka katika misononeko? Sura ya 63 ya Isaya inaonyesha kwamba suala fulani la maana zaidi linahusika, yaani, kutakaswa kwa jina la Mungu.

      Mwendo wa Shujaa Mshindi

      3, 4. (a) Unabii wa Isaya sura ya 63 unatolewa katika mazingira gani? (b) Isaya anaona nani akipiga mwendo kuelekea Yerusalemu, na wasomi fulani wamemtambulisha huyo kuwa nani?

      3 Katika Isaya sura ya 62, tunasoma juu ya kukombolewa kwa Wayahudi kutoka utekwani Babiloni na kurudishwa kwenye nchi yao. Basi inatazamiwa kwamba swali hili lingetokea: Je, mabaki ya Wayahudi waliorudishwa watahitaji kuhofu kwamba watafanywa ukiwa tena na mataifa mengine ya adui? Njozi ya Isaya inasaidia sana kutuliza hofu yao. Unabii unaanza kwa kusema hivi: “Ni nani huyu atokaye Edomu, mwenye mavazi ya kutiwa damu [“yenye rangi za kung’ara,” “NW”] kutoka Bosra? Huyu aliye na nguo za fahari, anayekwenda katika ukuu wa uweza wake?”—Isaya 63:1a.

      4 Isaya anaona shujaa akikaza mwendo kwa shangwe ya ushindi kuelekea Yerusalemu. Mavazi yake ya fahari yanaonyesha kwamba yeye ni mtu wa cheo cha juu kabisa. Anatoka upande wa jiji maarufu zaidi la Edomu, yaani Bosra, kudokeza kwamba amepata ushindi mkubwa juu ya nchi hiyo ya adui. Shujaa huyo aweza kuwa nani? Wasomi fulani humtambulisha kuwa Yesu Kristo. Wengine huamini kwamba ni Yuda Makabayo, yule kiongozi wa kijeshi Myahudi. Hata hivyo, shujaa huyo anajitambulisha mwenyewe anapojibu swali lililotangulia kwa kusema hivi: “Mimi nisemaye kwa haki, hodari wa kuokoa.”—Isaya 63:1b.

      5. Ni nani yule shujaa wa vita aliyeonwa na Isaya, na kwa nini unajibu hivyo?

      5 Hakuna shaka kwamba shujaa huyo ni Yehova Mungu mwenyewe. Mahali penginepo, anaelezwa kuwa mwenye “ukuu wa uweza” na kuwa ‘anasema haki.’ (Isaya 40:26; 45:19, 23) Mavazi yenye fahari nyingi ya shujaa huyo yanatukumbusha maneno haya ya mtunga zaburi: “Wewe, BWANA, Mungu wangu, umejifanya mkuu sana; umejivika heshima na adhama.” (Zaburi 104:1) Ingawa Yehova ndiye Mungu wa upendo, Biblia inaonyesha kwamba yeye huwa shujaa wa vita kunapokuwa na uhitaji.—Isaya 34:2; 1 Yohana 4:16.

      6. Kwa nini Yehova anarudi kutoka piganoni Edomu ?

      6 Ingawa hivyo, kwa nini Yehova anarudi kutoka piganoni Edomu? Waedomu, ambao ni waendelezaji wa kinyongo kilichoanza na baba yao wa zamani, Esau, ni maadui wa watu wa agano la Mungu tangu kale. (Mwanzo 25:24-34; Hesabu 20:14-21) Kina cha chuki ya Edomu kwa Yuda kilionekana wazi hasa wakati wa ukiwa wa Yerusalemu, Waedomu walipochochea fitina kwa kuwashangilia askari Wababiloni. (Zaburi 137:7) Yehova anauona uadui huo kuwa ni kumwudhi yeye binafsi. Si ajabu kwamba alipiga moyo konde kuvurumisha upanga wake wa kisasi juu ya Edomu!—Isaya 34:5-15; Yeremia 49:7-22.

      7. (a) Hapo kwanza unabii unaotabiri mabaya kuhusu Edomu ulitimizwaje? (b) Edomu anafananisha nini?

      7 Kwa hiyo njozi ya Isaya ina kitia-moyo kingi kwa Wayahudi wanaorudi kutoka Yerusalemu. Inawahakikishia kwamba watakaa salama katika makao yao mapya. Kwa kweli, kufikia siku za nabii Malaki, Mungu alifanya ‘milima yake Edomu kuwa ukiwa, na urithi wake akawapa mbweha wa nyikani.’ (Malaki 1:3) Basi je, hiyo inamaanisha kwamba unabii wa Isaya ulikuwa umetimizwa kabisa kufikia siku za Malaki? Sivyo, kwa maana ijapokuwa Edomu ilikuwa ukiwa, bado ilijikaza kujenga upya mahali pake mbalimbali palipoachwa ukiwa, na Malaki aliendelea kuita Edomu “mpaka wa uovu” na “watu ambao BWANA anawaghadhabikia milele.”a (Malaki 1:4, 5) Hata hivyo, kwa njia ya unabii Edomu inahusisha watu wengine pia wasio wazao wa Esau. Inafananisha mataifa yote yanayoonyesha wazi kwamba wao ni adui za waabudu wa Yehova. Mataifa ya Jumuiya ya Wakristo hasa ndiyo yamekuwa maarufu kwa kuonyesha uadui huo. Itakuwaje kwa Edomu huyu wa kisasa?

      Shinikizo la Divai

      8, 9. (a) Yule shujaa wa vita aliyeonekana na Isaya amekuwa akihusika katika utendaji gani? (b) Shinikizo la divai la mfano linakanyagwa-kanyagwa wakati gani na jinsi gani?

      8 Isaya anamwuliza hivi shujaa huyo anayerudi: “Kwani mavazi yako kuwa mekundu, na nguo zako kama za mtu akanyagaye zabibu?” Yehova anajibu hivi: “Nalikanyaga shinikizoni peke yangu; wala katika watu hakuwapo mtu pamoja nami; naam, naliwakanyaga kwa hasira yangu, naliwaponda kwa ghadhabu yangu; na mavazi yangu yametiwa madoa kwa damu yao, nami nimezichafua nguo zangu zote.”—Isaya 63:2, 3.

      9 Maneno hayo dhahiri sana yanaeleza kuhusu umwagikaji mwingi wa damu. Kwani, hata mavazi ya Mungu ya fahari yametiwa madoa, kama mavazi ya mtu anayekanyaga shinikizo la divai! Shinikizo la divai linafananisha vizuri hali ya kunaswa mtegoni, ambamo adui za Yehova Mungu wanajikuta wakati anapoondoka kwenda kuwaharibu. Shinikizo hili la divai la mfano litakanyagwa-kanyagwa lini? Unabii wa Yoeli na wa mtume Yohana unataja shinikizo la divai la mfano. Shinikizo la divai linalotajwa na unabii huo litakanyagwa-kanyagwa wakati Yehova atakapowakanyaga-kanyaga adui zake kwenye Har-Magedoni. (Yoeli 3:13; Ufunuo 14:18-20; 16:16) Shinikizo la mfano linalotajwa na Isaya linahusiana na wakati huo huo ulioko mbele.

      10. Kwa nini Yehova anasema kwamba alikanyaga-kanyaga shinikizo hilo la divai akiwa peke yake?

      10 Ingawa hivyo, ni kwa nini Yehova anasema kwamba alikanyaga-kanyaga shinikizo hilo la divai akiwa peke yake, bila kusaidiana na mtu yeyote wa kabila za watu? Kwani si Yesu Kristo atakayeshika usukani kwenda kulikanyaga-kanyaga shinikizo la divai, akiwa mwakilishi wa Mungu? (Ufunuo 19:11-16) Ndiyo, lakini Yehova anamaanisha wanadamu, wala si viumbe-roho. Anasema kwamba hakuna mwanadamu aliye hodari kiasi cha kuweza kuwang’oa wafuasi wa Shetani duniani. (Isaya 59:15, 16) Ni Mungu Mweza-Yote aliyeachiwa kazi ya kuendelea kuwakanyaga-kanyaga kwa hasira yake, mpaka wasagike tikitiki.

      11. (a) Kwa nini Yehova analeta “siku ya kisasi”? (b) Wale ‘waliokombolewa’ nyakati za kale ni akina nani, na leo hao ‘waliokombolewa’ ni akina nani?

      11 Yehova anaendelea kueleza ni kwa nini anafanya kazi hiyo yeye binafsi, akisema hivi: “Siku ya kisasi ilikuwamo moyoni mwangu, na mwaka wao niliowakomboa umewadia.” (Isaya 63:4)b Ni Yehova peke yake aliye na haki ya kulipiza kisasi juu ya wale wanaowadhuru watu wake. (Kumbukumbu la Torati 32:35) Wale ‘waliokombolewa’ nyakati za kale ni Wayahudi walioteswa na Wababiloni. (Isaya 35:10; 43:1; 48:20) Nyakati za kisasa, watu hao ni mabaki watiwa-mafuta. (Ufunuo 12:17) Wamekombolewa kutoka katika utekwa wa kidini, sawa na mabaki wenzao wa kale. Vilevile, watiwa-mafuta pamoja na waandamani wao walio “kondoo wengine” wamenyanyaswa na kupingwa kama Wayahudi hao. (Yohana 10:16) Hivyo unabii wa Isaya unawahakikishia Wakristo leo kwamba katika wakati wa Mungu uliowekwa rasmi, Yeye ataingilia mambo ili kuwasaidia.

      12, 13. (a) Ni kwa njia gani Yehova hana msaidiaji? (b) Mkono wa Yehova unaandaje wokovu, na ghadhabu yake inamtegemezaje?

      12 Yehova anaendelea kusema hivi: “Nikatazama, wala hakuna wa kusaidia; nikashangaa kwa kuwa hakuna mwenye kutegemeza; basi, mkono wangu mwenyewe uliniletea wokovu, ghadhabu yangu ndiyo iliyonitegemeza. Nikazikanyaga kabila za watu kwa hasira yangu, nikawalevya kwa ghadhabu yangu, nami nikaimwaga damu yao [“inayofoka-foka,” “NW”] chini.”—Isaya 63:5, 6.

      13 Hakuna msaidiaji wa kibinadamu anayeweza kudai sifa ya kuleta ile siku kuu ya kisasi cha Yehova. Wala Yehova hahitaji utegemezo wowote wa kibinadamu ili kutimiza mapenzi yake.c Mkono wake wenye nguvu unaiweza kazi iliyopo. (Zaburi 44:3; 98:1; Yeremia 27:5) Isitoshe, ghadhabu yake inamtegemeza. Kwa njia gani? Kwa maana ya kwamba ghadhabu ya Mungu si hisia-moyo isiyodhibitiwa, bali ni hasira ya haki. Kwa kuwa sikuzote Yehova huchukua hatua zinazotegemea kanuni za uadilifu, ghadhabu yake inamwunga mkono na kumchochea ‘kumwaga chini’ ile ‘damu inayofoka-foka’ ya adui zake, hata kuwashushia heshima na kuwashinda.—Zaburi 75:8; Isaya 25:10; 26:5.

      Fadhili za Upendo wa Mungu

      14. Sasa Isaya anatoa vikumbusha gani vinavyofaa?

      14 Nyakati zilizopita, Wayahudi waliacha upesi kuyathamini mambo ambayo Yehova aliwafanyia. Basi, inafaa kwamba Isaya anawakumbusha ni kwa nini Yehova alifanya mambo hayo. Isaya anatangaza hivi: “Nitautaja wema wa BWANA, sifa za BWANA kwa yote aliyotukirimia BWANA; na wingi wa wema wake kwa nyumba ya Israeli, aliowakirimia kwa rehema zake, na kwa wingi wa wema [“fadhili za upendo,” “NW”] wake. Maana alisema, Hakika ndio watu wangu hawa, wana wasio na hila; akawa Mwokozi wao. Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake [“mjumbe wake binafsi,” “NW”] akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale.”—Isaya 63:7-9.

      15. Yehova aliwaonyeshaje wazao wa Abrahamu fadhili za upendo kule Misri, na kwa nini alifanya hivyo?

      15 Yehova anaweka mfano wa kutokeza kama nini kwa kuonyesha fadhili za upendo, au upendo wenye uaminifu-mshikamanifu! (Zaburi 36:7; 62:12) Yehova alishikamana na Abrahamu kwa njia yenye upendo. (Mika 7:20) Alimwahidi mzee huyo wa ukoo kwamba mataifa yote ya dunia yangejibariki kupitia mbegu yake, au uzao wake. (Mwanzo 22:17, 18) Yehova alishikamana na ahadi hiyo, akaionyesha nyumba ya Israeli wema tele. Mojawapo la matendo yake ya uaminifu-mshikamanifu yenye kutokeza lilikuwa lile la kuwaokoa wazao wa Abrahamu kutoka utumwani Misri.—Kutoka 14:30.

      16. (a) Yehova alikuwa na maoni gani alipofanya agano lake na Israeli? (b) Mungu anashughulikaje na watu wake?

      16 Baada ya lile tukio la Kutoka, Yehova aliwaleta Israeli kwenye Mlima Sinai, akawapa ahadi hii: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu . . . nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6) Je, Yehova alikuwa mdanganyifu kwa kuahidi hivyo? Sivyo, kwa maana Isaya anafunua kwamba Yehova alijiambia hivi yeye mwenyewe: “Hakika ndio watu wangu hawa, wana wasio na hila.” Msomi mmoja anatoa maoni haya: “Neno hili ‘hakika’ halitumiwi kimamlaka ili kujionyesha kuwa na enzi kuu ya kujitawala wala kuonyesha uwezo wa kujua mambo kimbele: bali limetumiwa kuonyesha tumaini na uhakika wenye upendo.” Ndiyo, Yehova alifanya agano lake kwa nia safi, akiwa na tamaa ya moyo mweupe ya kuwasaidia watu wake wafanikiwe. Ingawa walikuwa na mapungufu ya wazi, yeye alionyesha kwamba anawaamini. Ni vizuri kama nini kuabudu Mungu anayewaamini waabudu wake! Leo, wazee wanapoonyesha kuwa hata wao wanaamini kwamba kwa msingi watu wa Mungu ni wema, hiyo husaidia sana kuwaimarisha wale waliowekwa chini ya uangalizi wao.—2 Wathesalonike 3:4; Waebrania 6:9, 10.

      17. (a) Yehova alithibitishaje kwamba aliwapenda Waisraeli? (b) Tunaweza kuwa na uhakika gani leo?

      17 Hata hivyo, mtunga zaburi anasema hivi kuhusu Waisraeli: “Wakamsahau Mungu, mwokozi wao, aliyetenda makuu katika Misri.” (Zaburi 106:21) Mtazamo wao wa kutokutii kwa shingo ngumu uliwaletea shida nyingi. (Kumbukumbu la Torati 9:6) Je, Yehova aliacha kuwaonyesha fadhili za upendo? Badala ya kufanya hivyo, Isaya anasimulia kwamba “katika mateso yao yote yeye aliteswa.” Lo, Yehova ana hisia-moyo zilizoje! Kama vile ilivyo kwa habari ya baba yeyote mwenye upendo, Mungu aliumia kuwaona watoto wake wakiteseka, hata walipoteseka kwa sababu ya upumbavu wao wenyewe. Kama vile ilivyotabiriwa, na pia ili kuthibitisha upendo wake, yeye alimtuma “mjumbe wake binafsi,” ambaye yaelekea alikuwa Yesu kabla hajaishi akiwa mwanadamu, ili awaongoze kuingia Nchi ya Ahadi. (Kutoka 23:20) Hivyo Yehova aliliinua taifa hilo akalibeba, “kama mtu amchukuavyo mwanawe.” (Kumbukumbu la Torati 1:31; Zaburi 106:10) Leo tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova anajua sana mateso yetu na kwamba anatuvumilia tunapokuwa katika matata makubwa. Tunaweza kuwa na uhakika wa ‘kutupa hangaiko letu lote juu yake, kwa sababu yeye hutujali.’—1 Petro 5:7.

      Mungu Anakuwa Adui

      18. Kwa nini Yehova akawa adui ya watu wake?

      18 Ingawa hivyo, tusithubutu kamwe kuchezea fadhili za upendo wa Mungu. Isaya anaendelea kusema hivi: “Walikuwa wakaidi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akawa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.” (Isaya 63:10, “BHN”) Yehova alionya kwamba ingawa yeye ni Mungu wa rehema na neema, “si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.” (Kutoka 34:6, 7) Waisraeli walijitia katika hali ya kustahili adhabu kwa kuzoea uasi. “Usisahau ulivyomtia BWANA, Mungu wako, kasirani jangwani,” Musa akawakumbusha. “Tangu siku uliyotoka nchi ya Misri hata mlipofika mahali hapa, mmekuwa na uasi juu ya BWANA.” (Kumbukumbu la Torati 9:7) Kwa kukinza matokeo mazuri ya roho ya Mungu, wameihuzunisha, au wakaitia kihoro. (Waefeso 4:30) Wamemlazimisha Yehova kuwa adui yao.—Mambo ya Walawi 26:17; Kumbukumbu la Torati 28:63.

      19, 20. Wayahudi wanakumbuka mambo gani, na kwa nini?

      19 Katikati ya mateso yao, Wayahudi fulani wanaguswa moyo kuufikiria wakati uliopita. Isaya anasema hivi: “Ndipo walipokumbuka siku za zamani, wakati wa Mose mtumishi wa Mwenyezi-Mungu. Wakauliza, ‘Yuko wapi sasa Mwenyezi-Mungu, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake baharini? Yuko wapi yule aliyeiweka roho yake takatifu kati yao, ambaye kwa mkono wake wenye nguvu [“maridadi,” “NW”] alifanya maajabu kwa njia ya Mose, akapasua bahari na kuwaongoza watu wake, na kujipatia jina la milele? Aliwaongoza katikati ya vilindi vya bahari, wakapita humo kama farasi bila kujikwaa. Kama ng’ombe wapelekwavyo malishoni bondeni, ndivyo roho ya Mungu ilivyowapumzisha watu wake.”—Isaya 63:11-14a, “BHN.”d

      20 Ndiyo, kwa kupatwa na matokeo ya kutokutii, Wayahudi wanatamani sana siku zile ambazo Yehova alikuwa Mkombozi wao wala si adui yao. Wanakumbuka jinsi “wachungaji” wao, Musa na Haruni, walivyowaongoza salama wakawavusha Bahari Nyekundu. (Zaburi 77:20; Isaya 51:10) Wanakumbuka wakati ambao, badala ya wao kuihuzunisha roho ya Mungu, roho hiyo iliwaongoza kupitia mwelekezo uliotolewa na Musa na wanaume wengine wazee waliowekwa rasmi kwa roho. (Hesabu 11:16, 17) Vilevile wanakumbuka ya kwamba waliona ‘mkono maridadi’ wa nguvu za Yehova ukitumiwa kwa niaba yao kupitia Musa! Baada ya muda, Mungu aliwaondoa katika lile jangwa kubwa la kuogofya, akawaongoza kuwaingiza nchi inayotiririka maziwa na asali—mahali pa pumziko. (Kumbukumbu la Torati 1:19; Yoshua 5:6; 22:4) Ingawa hivyo, sasa Waisraeli wanateseka kwa sababu wamepoteza uhusiano wao mzuri na Mungu!

      ‘Ajifanyia Jina Maridadi’

      21. (a) Israeli angaliweza kuwa na pendeleo gani kuu kuhusiana na jina la Mungu? (b) Ni sababu gani ya msingi iliyofanya Mungu awakomboe wazao wa Abrahamu kutoka Misri?

      21 Na bado, hasara ya vitu vya kimwili inayowapata Waisraeli ni kitu kidogo sana ikilinganishwa na hasara ya pendeleo ambalo wametupa, yaani, kushiriki kulitukuza jina la Mungu. Musa aliwaahidi Waisraeli hivi: “BWANA atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya BWANA, Mungu wako, na kutembea katika njia zake. Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la BWANA, nao watakuwa na hofu kwako.” (Kumbukumbu la Torati 28:9, 10) Wakati Yehova alipochukua hatua ya kuwalinda wazao wa Abrahamu, akiwaokoa utumwani Misri, hakuwa akifanya hivyo ili kurahisisha tu maisha yao au kuyafanya yawe ya kupendeza zaidi. Alikuwa akichukua hatua kwa ajili ya jambo la maana zaidi sana—jina lake. Naam, alitaka kuhakikisha kwamba jina lake ‘linatangazwa katika dunia yote.’ (Kutoka 9:15, 16) Na wakati Mungu alipoonyesha rehema baada ya ule uasi wa jangwani, hakufanya hivyo kwa msisimuko tu. Yehova mwenyewe alisema hivi: “Nalitenda kwa ajili ya jina langu, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa.”—Ezekieli 20:8-10.

      22. (a) Katika wakati ujao, kwa nini Mungu atawapigania watu wake tena? (b) Upendo wetu kwa jina la Mungu una matokeo gani juu ya vitendo vyetu?

      22 Kisha Isaya anaupa unabii huu umalizio wenye nguvu kama nini! Anasema hivi: “Ndivyo ulivyowaongoza watu wako, ili ujifanyie jina lenye utukufu [“lililo maridadi,” “NW”].” (Isaya 63:14b) Sasa inaweza kuonekana wazi ni kwa nini Yehova anapigania masilahi ya watu wake kwa nguvu nyingi sana. Kusudi lake ni kujifanyia jina lililo maridadi. Hivyo, unabii wa Isaya ni kikumbusha cha kwamba kubeba jina la Yehova ni pendeleo la kuogopesha sana na pia ni daraka kubwa. Wakristo wa kweli leo wanalipenda jina la Yehova kuliko uhai wao wenyewe. (Isaya 56:6; Waebrania 6:10) Wanachukia sana kufanya jambo lolote ambalo lingeweza kuliletea suto jina hilo takatifu. Wanauitikia upendo wa Mungu wenye uaminifu-mshikamanifu kwa kushikamana naye kwa uaminifu. Na kwa sababu wanalipenda jina maridadi la Yehova, wanatamani sana kuiona siku ambayo atawakanyaga-kanyaga adui zake katika shinikizo la divai la hasira yake—si kwa sababu wao tu watafaidika, bali kwa sababu jina la Mungu huyu wampendaye litatukuzwa.—Mathayo 6:9.

      [Maelezo ya Chini]

      a Maherode wa karne ya kwanza W.K. walikuwa Waedomu.

      b Usemi “mwaka wao niliowakomboa” huenda ukamaanisha kipindi kile kile kinachomaanishwa na mtajo “siku ya kisasi.” Angalia jinsi maneno yanayofanana na hayo yanavyotumiwa kwa ulinganifu kwenye Isaya 34:8.

      c Yehova anasema anastaajabu kwamba hakuna mtu aliyejitolea kumwunga mkono. Kweli ingeweza kustaajabisha kwamba karibu miaka 2,000 baada ya kifo cha Yesu, wenye mamlaka miongoni mwa wanadamu wangali wanapinga mapenzi ya Mungu.—Zaburi 2:2-12; Isaya 59:16.

      d Mstari huu ungeweza pia kuanza kwa kusema hivi: “Yeye akaanza kukumbuka.” (Isaya 63:11, kielezi-chini katika NW) Hata hivyo, si lazima hiyo imaanishe kwamba Yehova ndiye mwenye kukumbuka. Maneno yanayofuata yanaeleza hisia za watu wa Mungu wala si za Yehova mwenyewe. Hivyo, kichapo Soncino Books of the Bible kinayafasiri maneno hayo hivi: “Ndipo watu Wake wakazikumbuka siku za zamani.”

      [Picha katika ukurasa wa 359]

      Yehova alikuwa na matazamio makubwa kuhusiana na watu wake

  • Sala ya Toba
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Tano

      Sala ya Toba

      Isaya 63:15–64:12

      1, 2. (a) Kusudi la nidhamu ya kimungu ni nini? (b) Wayahudi watakabili uchaguzi gani baada ya kupokea nidhamu ya Yehova?

      UHARIBIFU wa Yerusalemu na hekalu lake mwaka wa 607 K.W.K. ulikuwa nidhamu kutoka kwa Yehova, dalili ya kwamba alikataa katakata kuwaonyesha kibali chake. Taifa hilo la Yuda lisilotii lilistahili adhabu hiyo kali. Hata hivyo, Yehova hakukusudia Wayahudi wamalizwe kabisa. Mtume Paulo aligusia kusudi la nidhamu ya Yehova aliposema hivi: “Kweli, hakuna nidhamu ionekanayo kwa wakati wa sasa kuwa yenye shangwe, bali yenye kihoro; lakini baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo hiyo hutoa tunda lenye kufanya amani, yaani, uadilifu.”—Waebrania 12:11.

      2 Wayahudi watayaitikiaje magumu yaliyowapata? Je, wataichukia nidhamu ya Yehova? (Zaburi 50:16, 17) Au wataikubali ili iwape mazoezi? Je, watatubu na kuponywa? (Isaya 57:18; Ezekieli 18:23) Unabii wa Isaya unadokeza kwamba angalau baadhi ya wakaaji wa zamani wa Yuda wataikubali nidhamu hiyo. Kuanzia mistari ya mwisho ya sura ya 63 na kuendelea hadi sura ya 64, taifa la Yuda linaonyeshwa kuwa watu wenye majuto wanaomfikia Yehova kwa dua yenye kuhisiwa moyoni. Nabii Isaya anatamka sala ya toba kwa niaba ya wananchi wenzake watakaokuwa uhamishoni wakati ujao. Anapofanya hivyo, anaongea juu ya matukio ya wakati ujao kana kwamba yanatukia mbele ya macho yake.

      Baba Mwenye Huruma

      3. (a) Sala ya Isaya ya kiunabii inamkwezaje Yehova? (b) Sala ya Danieli inaonyeshaje kwamba mawazo yanayotajwa katika sala ya kiunabii ya Isaya ndiyo mawazo ya Wayahudi wenye toba walioko Babiloni? (Ona sanduku katika ukurasa wa 362.)

      3 Isaya anasali hivi kwa Yehova: “Tazama toka mbinguni, ukaone toka makao ya utukufu wako na fahari yako.” Nabii anaongea juu ya mbingu za kiroho, makao ya Yehova na viumbe-roho wake wasioonekana. Akieleza mawazo ya Wayahudi uhamishoni, Isaya anaendelea kusema hivi: “Uko wapi wivu wako, na uweza wako? Shauku ya moyo wako, na huruma zako zimezuiliwa kwangu.” (Isaya 63:15) Yehova amezuilia nguvu zake na kudhibiti hisia zake za kina kirefu—“shauku ya moyo [wake], na huruma [zake]”—kuelekea watu wake. Hata hivyo, Yehova ndiye “Baba” wa taifa la Kiyahudi. Abrahamu na Israeli (Yakobo) walikuwa baba zao wa zamani wa kiasili, lakini kama wangerudishiwa uhai, huenda wakawa na mwelekeo wa kuwakataa watoto wao waasi-imani. Yehova ana huruma nyingi kuwapita. (Zaburi 27:10) Isaya anasema hivi akiwa mwenye shukrani: “Wewe, BWANA, ndiwe Baba yetu, mkombozi wetu tangu milele ndilo jina lako.”—Isaya 63:16.

      4, 5. (a) Yehova anawakoseshaje watu wake njia zake? (b) Yehova anataka ibada ya aina gani?

      4 Isaya anaendelea kwa kutaja hisia hii ya moyoni: “Ee BWANA,mbona umetukosesha njia zako,ukatufanyiza kuwa na mioyo migumu hata tusikuogope? Urudi kwa ajili ya watumishi wako, kabila za urithi wako.” (Isaya 63:17) Ndiyo, Isaya anasali Yehova ageuze fikira zake ziwaelekee tena watumishi wake. Ingawa hivyo, Yehova anawakoseshaje Wayahudi njia zake? Je, Yehova ndiye mwenye lawama kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao unaowafanya wasimhofu? Sivyo, lakini anawaruhusu wawe na ugumu huo, kisha wakati Wayahudi wanapokata tamaa, wanaomboleza wakisema eti ni Yehova aliyewapa uhuru wa kufanya walivyofanya. (Kutoka 4:21; Nehemia 9:16) Wanaona ingalikuwa vema kama Yehova angalichukua hatua ya kuwazuia wasifanye kosa walilolifanya.

      5 Bila shaka, Mungu hashughuliki na wanadamu jinsi hiyo. Sisi ni viumbe wenye hiari, na Yehova huturuhusu tujiamulie kama tutamtii au hatutamtii. (Kumbukumbu la Torati 30:15-19) Yehova anataka ibada inayotoka katika mioyo na akili zinazosukumwa na upendo wa kweli. Kwa hiyo, amewaacha Wayahudi waonyeshe wazi hiari yao, hata ingawa hiari hiyo imewaruhusu kumwasi. Hivyo ndivyo yeye ameifanya mioyo yao iwe migumu.—2 Mambo ya Nyakati 36:14-21.

      6, 7. (a) Wayahudi wanapoziacha njia za Yehova, matokeo yanakuwa nini? (b) Wayahudi wanajisumbua bure kwa kusema ni afadhali jambo gani lingetendeka, lakini hawana haki ya kutazamia nini?

      6 Matokeo ni nini? Isaya anasema hivi kiunabii: “Watu wako watakatifu waliumiliki kwa kitambo tu; adui zetu wamepakanyaga patakatifu pako. Tumekuwa kama watu usiowamiliki kamwe; kama watu wasioitwa kwa Jina lako.” (Isaya 63:18, 19) Watu wa Yehova walimiliki patakatifu pake kwa muda. Halafu Yehova akaruhusu paharibiwe, na taifa lake lipelekwe uhamishoni. Ilipokuwa hivyo, ni kana kwamba hakukuwa kumekuwa na agano lolote kati yake na uzao wa Abrahamu na kana kwamba walikuwa hawajaitwa kwa jina lake. Sasa wakiwa mateka Babiloni, Wayahudi wanalia kwa sauti kubwa kwa sababu ya kukosa tumaini: “Laiti ungepasua mbingu, na kushuka, ili milima iteteme mbele zako; kama vile moto uchomapo vichaka, na moto uchemshapo maji; ili kuwajulisha adui zako jina lako, mataifa wakatetemeke mbele zako!” (Isaya 64:1, 2) Kweli Yehova ana uwezo wa kuokoa. Hakika yeye angaliweza kushuka awapiganie watu wake, ararue-rarue mifumo ya serikali zilizo kama mbingu na kuvunja-vunja milki zilizo kama milima. Yehova angaliweza kulijulisha jina lake kwa kuonyesha bidii yake motomoto kwa niaba ya watu wake.

      7 Yehova alikuwa amefanya mambo ya jinsi hiyo zamani. Isaya anasimulia hivi: “Ulipofanya mambo ya kutisha tusiyoyatazamia, ulishuka, milima ikatetema mbele zako.” (Isaya 64:3) Matendo hayo makuu yanaonyesha uwezo wa Yehova na Uungu wake. Hata hivyo, Wayahudi wasio waaminifu wa wakati wa Isaya hawana haki ya kumtazamia Yehova atende hivyo kwa faida yao.

      Ni Yehova Peke Yake Awezaye Kuokoa

      8. (a) Yehova anatofautiana na miungu ya uwongo ya mataifa kwa njia gani moja? (b) Kwa nini Yehova hachukui hatua kuwaokoa ingawa ana uwezo wa kufanya hivyo? (c) Paulo ananukuu na kutumia Isaya 64:4 kwa njia gani? (Ona sanduku katika ukurasa wa 366.)

      8 Miungu ya uwongo haiwafanyii waabudu wake maajabu yoyote ya wokovu. Isaya anaandika hivi: “Tangu zamani za kale watu hawakusikia, wala kufahamu kwa masikio, wala jicho halikuona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake amngojaye. Wewe wamlaki yeye afurahiaye yaliyo haki na kuyatenda, watu wale wakukumbukao katika njia zako.” (Isaya 64:4, 5a) Ni Yehova peke yake aliye “mthawabishaji wa wale wanaomtafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Yeye huchukua hatua kuwalinda wale wanaotenda uadilifu na wale wanaomkumbuka. (Isaya 30:18) Je, Wayahudi wametenda hivyo? Sivyo. Isaya anamwambia Yehova hivi: “Tazama, ulikuwa na hasira, nasi tulitenda dhambi; tumekuwa katika mambo haya muda mwingi; nasi, je! tutaokolewa?” (Isaya 64:5b) Kwa sababu watu wa Mungu wamekuwa wakizidi tu kufanya dhambi kwa muda mrefu, hakuna msingi wa kumfanya Yehova asitesite kuleta ghadhabu yake ya haki na kuwaletea wokovu.

      9. Wayahudi wenye kutubu wanaweza kutumainia nini, nasi tunaweza kujifunza nini kutokana na jambo hili?

      9 Wayahudi hawawezi kufuta kasoro za wakati uliopita, lakini wakitubu na kurudia ibada safi, wanaweza kutumainia kupata msamaha na baraka za wakati ujao. Yehova atawathawabisha wenye kutubu kwa wakati wake kwa kuwafungua kutoka utekwa wa Babiloni. Lakini bado wanahitaji subira. Ingawa wana toba, Yehova hatabadili wakati aliouweka. Hata hivyo, wakiendelea kuwa macho na waitikie mapenzi ya Yehova, wanahakikishiwa kwamba hatimaye watakombolewa. Vivyo hivyo, Wakristo leo wanamtazamia Yehova kwa subira. (2 Petro 3:11, 12) Sisi tunayatia maanani maneno ya mtume Paulo, aliyesema hivi: “Tusife moyo katika kufanya lililo bora, kwa maana katika majira yapasayo tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.”—Wagalatia 6:9.

      10. Sala ya Isaya inaungama wazi kwamba ni jambo gani lisiloweza kufanyika?

      10 Sala ya Isaya ya kiunabii si ungamo la kidesturi tu kuhusu dhambi. Sala hiyo inaonyesha kwamba anatambua kwa moyo mweupe kuwa taifa lao haliwezi kujiokoa lenyewe. Nabii anasema hivi: “Sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi [“vazi la vipindi vya hedhi,” “NW”]; sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo.” (Isaya 64:6) Kufikia mwishoni mwa uhamisho, huenda ikawa Wayahudi wenye kutubu wameacha uasi-imani. Huenda ikawa wamemgeukia Yehova kwa kufanya matendo ya uadilifu. Lakini bado hawajakamilika. Ingawa mema waliyotenda yanastahili sifa, mema hayo ni sawa tu na mavazi yaliyotiwa unajisi, kwani hayawezi kufunika dhambi. Msamaha wa Yehova ni zawadi isiyostahiliwa, naye huitoa kwa sababu ya rehema yake. Msamaha huo si kitu kinachoweza kuchumwa kama mshahara.—Waroma 3:23, 24.

      11. (a) Wengi wa Wayahudi walioko uhamishoni wana hali gani mbaya ya kiroho, na huenda sababu ikawa ni nini? (b) Ni nani waliokuwa mifano bora ya imani wakati wa uhamisho?

      11 Isaya anaona nini anapotazama kule mbele? Nabii huyo anasali hivi: “Hapana aliitiaye jina lako, ajitahidiye akushike; kwa kuwa umetuficha uso wako, nawe umetukomesha kwa njia ya maovu yetu.” (Isaya 64:7) Hali ya kiroho ya taifa hilo imedidimia chini kabisa. Watu wamekuwa hawaiti jina la Mungu katika sala. Ingawa hawana tena hatia ya dhambi nzito ya kuabudu sanamu, ni wazi kwamba wanapuuza ibada yao, na hakuna ‘ajitahidiye kumshika Yehova.’ Ni wazi kwamba hawana uhusiano mzuri na Muumba wao. Labda wengine wanahisi kuwa hawastahili kusema na Yehova katika sala. Huenda wengine wakaendelea na shughuli zao za kila siku bila kumjali. Bila shaka, miongoni mwa wahamishwa mna watu mmoja-mmoja ambao ni mifano mizuri sana ya imani, kama vile Danieli, Hanania, Mishaeli, Azaria, na Ezekieli. (Waebrania 11:33, 34) Huku kile kipindi cha miaka 70 ya utekwa kikikaribia kumalizika, wanaume kama vile Hagai, Zekaria, Zerubabeli, na Kuhani Mkuu Yoshua wako tayari kuongoza kwa kuliitia jina la Yehova. Na bado, inaonekana kwamba sala ya Isaya ya kiunabii inaeleza jinsi hali ya wahamishwa wengi ilivyo.

      “Kutii Ni Bora Kuliko Dhabihu”

      12. Isaya anaonyeshaje kwamba Wayahudi wenye toba wana nia ya kubadili mwenendo wao?

      12 Wayahudi wenye toba wana nia ya kubadilika. Akiwawakilisha, Isaya anamtolea Yehova sala akisema hivi: “Sasa, Ee BWANA, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.” (Isaya 64:8) Maneno haya yanakiri tena kwamba Yehova ndiye mwenye mamlaka ya kuwa Baba, au Mpaji wa Uhai. (Ayubu 10:9) Wayahudi wanaotubu wanalinganishwa na udongo unaoweza kufinyangwa uwe na umbo lolote lile. Kwa njia ya mfano, wale wanaoitikia nidhamu ya Yehova wanaweza kupewa umbo au muundo unaopatana na viwango vya Mungu. Lakini inaweza kuwa hivyo iwapo tu Yehova, aliye Mfinyanzi, atawasamehe. Ndiyo maana Isaya anamsihi mara mbili akumbuke kwamba Wayahudi ni watu wake: “Ee BWANA, usione hasira nyingi, wala usiukumbuke uovu siku zote; tazama, angalia, twakusihi, sisi sote tu watu wako.”—Isaya 64:9.

      13. Watu wa Mungu wanapokuwa uhamishoni, nchi ya Israeli ina hali gani?

      13 Wakati wa uhamisho, Wayahudi wanavumilia mengi licha ya kuwa mateka tu katika nchi ya kipagani. Ukiwa wa Yerusalemu na hekalu lake unawaletea suto wao na Mungu wao. Sala ya toba ya Isaya inasimulia baadhi ya mambo yanayosababisha suto hilo: “Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa, Sayuni umekuwa jangwa, Yerusalemu umekuwa ukiwa. Nyumba yetu takatifu, nzuri, walimokusifu baba zetu, imeteketea moto; vitu vyetu vyote vyenye kupendeza vimeharibika.”—Isaya 64:10, 11.

      14. (a) Yehova alionyaje kuhusu hali iliyopo sasa? (b) Ingawa Yehova alilifurahia sana hekalu lake na dhabihu zilizotolewa humo, jambo la maana zaidi ni nini?

      14 Bila shaka Yehova anajua sana jinsi mambo yalivyo katika nchi ya babu za Wayahudi hawa. Karibu miaka 420 kabla ya uharibifu wa Yerusalemu, yeye aliwaonya watu wake kwamba wakiziacha amri zake na kutumikia miungu mingine, ‘angewakatilia mbali na uso wa nchi,’ kisha lile hekalu zuri ‘liwe marundo ya magofu.’ (1 Wafalme 9:6-9, NW) Ni kweli kwamba Yehova alifurahia nchi aliyokuwa amewapa watu wake, hekalu tukufu lililojengwa kwa heshima yake, na dhabihu zilizotolewa kwake. Lakini uaminifu-mshikamanifu na utii ni mambo ya maana kuliko vitu vya kimwili, hata kuliko dhabihu. Kwa kufaa, nabii Samweli alimwambia hivi Mfalme Sauli: “Je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia kuliko mafuta ya beberu.”—1 Samweli 15:22.

      15. (a) Isaya anamsihi Yehova jinsi gani kwa njia ya unabii, na anajibiwaje? (b) Ni matukio gani ambayo hatimaye yalifanya Yehova alikatae taifa zima la Israeli?

      15 Hata hivyo, je! kweli Mungu wa Israeli anaweza kuyatazama mabaya yanayowapata watu wake wenye toba bila kuguswa na huruma? Isaya anamalizia sala yake ya kiunabii kwa swali hilo. Anasihi hivi kwa niaba ya Wayahudi wahamishwa: “Utajizuia usiyaangalie mambo haya, Ee BWANA? utanyamaza, na kututesa sana?” (Isaya 64:12) Mwishowe, kwa kweli Yehova anawasamehe watu wake, na katika mwaka wa 537 K.W.K., anawarudisha kwenye nchi yao waweze kuanza tena ibada safi huko. (Yoeli 2:13) Hata hivyo, jiji la Yerusalemu na hekalu lake liliharibiwa tena karne nyingi baadaye, na hatimaye Mungu akalikataa taifa la agano lake. Kwa nini? Kwa sababu watu wa Yehova walikuwa wamepeperuka wakaziacha amri zake na kumkataa Mesiya. (Yohana 1:11; 3:19, 20) Hilo lilipotukia, Yehova alianzisha taifa jipya lichukue mahali pa Israeli. Hilo lilikuwa taifa la kiroho, yaani, “Israeli wa Mungu.”—Wagalatia 6:16; 1 Petro 2:9.

      Yehova, “Msikiaji wa Sala”

      16. Biblia inafundisha nini kuhusu msamaha wa Yehova?

      16 Kuna masomo muhimu ya kujifunza kutokana na yaliyopata Israeli. Tunaona kwamba Yehova ‘yu mwema na huwa tayari kusamehe.’ (Zaburi 86:5) Sisi hutegemea rehema na msamaha wake ili tuweze kupata wokovu, kwani sisi ni viumbe wasio wakamilifu. Hata tufanye nini, hatuwezi kupata baraka hizo kwa jitihada zetu wenyewe kana kwamba tunachuma mshahara. Ingawa hivyo, Yehova hatoi msamaha kiholela. Wale tu wanaotubu dhambi zao na kugeuka kabisa ndio wanaoweza kutazamia kupata msamaha wa Mungu.—Matendo 3:19.

      17, 18. (a) Tunajuaje kwamba Yehova anapendezwa na mawazo na hisia zetu kwa njia ya kweli? (b) Kwa nini Yehova anatumia subira kuelekea wanadamu wenye dhambi?

      17 Pia tunajifunza kwamba Yehova anapendezwa sana na mawazo na hisia zetu tunapozitaja katika sala. Yeye ndiye “Msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2, 3, NW ) Mtume Petro anatuhakikishia hivi: “Macho ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yaelekea dua zao.” (1 Petro 3:12) Zaidi ya hilo, tunajifunza kwamba sala ya toba ni lazima iwe pia na ungamo la dhambi lenye unyenyekevu. (Mithali 28:13) Lakini, hiyo haimaanishi kwamba tunaweza kuichezea rehema ya Mungu. Biblia inaonya Wakristo ‘wasiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi lake.’—2 Wakorintho 6:1.

      18 Mwisho, tunajifunza kusudi la subira ambayo Mungu aliwaonyesha watu wake wenye dhambi. Mtume Petro alieleza kwamba Yehova ni mwenye subira “kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Petro 3:9) Hata hivyo, wale wanaozidi kuitumia vibaya subira ya Mungu wataadhibiwa hatimaye. Tunasoma hivi kuhusu jambo hilo: “[Yehova] atamlipa kila mmoja kulingana na kazi zake: uhai udumuo milele kwa wale wanaotafuta sana utukufu na heshima na kutofisidika kwa kuvumilia katika kazi iliyo njema; hata hivyo, kwa wale wenye ugomvi na wale wasioitii kweli bali hutii ukosefu wa uadilifu kutakuwa na hasira ya kisasi na hasira.”—Waroma 2:6-8.

      19. Sikuzote Yehova ataonyesha sifa gani zisizobadilika?

      19 Hivyo ndivyo Mungu alivyoshughulika na Israeli wa kale. Uhusiano wetu na Yehova leo unasimamiwa na kanuni hizo hizo kwa sababu yeye si kigeugeu. Ingawa Yehova hasiti-siti kutoa adhabu inayostahiliwa, sikuzote atakuwa “BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi.”—Kutoka 34:6, 7.

      [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 362]

      Sala ya Danieli ya Toba

      Nabii Danieli aliishi Babiloni kipindi chote cha ile miaka 70 ya utekwa wa Wayahudi. Wakati fulani katika mwaka wa 68 wa uhamisho, Danieli alitambua kutokana na unabii wa Yeremia kwamba muda wa Israeli wa kukaa ugenini ulikuwa ukikaribia kwisha. (Yeremia 25:11; 29:10; Danieli 9:1, 2) Danieli alimgeukia Yehova katika sala—sala ya toba kwa niaba ya taifa zima la Kiyahudi. Danieli anasimulia hivi: “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama.”—Danieli 9:3, 4.

      Danieli alitamka sala yake miaka mia mbili hivi baada ya Isaya kuiandika sala ya kiunabii inayopatikana katika sura ya 63 na ya 64 ya kitabu chake. Bila shaka, Wayahudi wengi wenye moyo mweupe walimtolea Yehova sala wakati wa ile miaka migumu ya uhamisho. Hata hivyo, Biblia inaikazia fikira sala ya Danieli, ambayo inaonekana kuwa iliwakilisha hisia za Wayahudi wengi waaminifu. Hivyo, sala yake inaonyesha kwamba kwa kweli hisia zinazotajwa katika sala ya kiunabii ya Isaya ndizo zilizokuwa hisia za Wayahudi waaminifu katika Babiloni.

      Angalia mifanano fulani kati ya sala ya Danieli na ya Isaya.

      Isaya 63:16 Danieli 9:15

      Isaya 63:18 Danieli 9:17

      Isaya 64:1-3 Danieli 9:15

      Isaya 64:4-7 Danieli 9:4-7

      Isaya 64:6 Danieli 9:9, 10

      Isaya 64:10, 11 Danieli 9:16-18

      [Sanduku katika ukurasa wa 366]

      “Jicho Halijaona”

      Katika barua yake kwa Wakorintho, mtume Paulo alinukuu kitabu cha Isaya alipoandika hivi: “Kama vile imeandikwa: ‘Jicho halijaona na sikio halijasikia, wala hayajawaziwa katika moyo wa mwanadamu mambo ambayo Mungu amewatayarishia wampendao.’” (1 Wakorintho 2:9)a Taarifa hiyo ya Paulo wala maneno ya Isaya hazimaanishi mambo ambayo Yehova amewatayarishia watu wake katika urithi wa kimbingu au katika paradiso ya kidunia ya wakati ujao. Paulo anayatumia maneno ya Isaya kuhusu baraka zilizokuwa tayari zikifurahiwa na Wakristo katika karne ya kwanza. Baadhi ya baraka hizo ni kuyaelewa mambo ya Mungu ya kina kirefu zaidi na kupokea mwangaza wa elimu ya kiroho kutoka kwa Yehova.

      Tunaweza kuelewa mambo ya kiroho yenye kina kirefu iwapo tu wakati wa Yehova wa kuyafunua umefika—na hata hapo tutaweza kuyaelewa iwapo tu sisi ni watu wa kiroho wenye uhusiano wa karibu na Yehova. Maneno ya Paulo yanatumika kuwahusu wale ambao wamepungukiwa sana kiroho au hata hawana hali yoyote ya kiroho. Jicho lao haliwezi kuona au kutambua kweli za kiroho, wala sikio lao haliwezi kusikia au kuelewa mambo hayo. Ujuzi wa mambo ambayo Mungu amewatayarishia wanaompenda hata haupenyi ndani ya mioyo ya watu kama hao. Lakini Mungu ametumia roho yake kuwafunulia mambo hayo watu kama vile Paulo, ambao wamejiweka wakfu kwake.—1 Wakorintho 2:1-16.

      [Maelezo ya Chini]

      a Maneno ya Paulo hayapatikani katika Maandiko ya Kiebrania yakiwa sawasawa kabisa na vile alivyoyanukuu. Inaonekana kwamba anaunganisha mawazo ya Isaya 52:15; 64:4; na 65:17.

      [Picha katika ukurasa wa 367]

      Watu wa Mungu walimiliki Yerusalemu na hekalu lake “kwa kitambo tu”

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Sita

      ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’

      Isaya 65:1-25

      1. Ni maneno gani yenye kufariji yaliyoandikwa na mtume Petro, na ni swali gani linalotokea?

      JE, KUNA wakati ambapo dhuluma na mateso zitakwisha? Zaidi ya miaka 1,900 iliyopita, mtume Petro aliandika maneno haya yenye kufariji: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake [Mungu], na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13) Petro, pamoja na watumishi wengine wengi wa Mungu wa karne zote zilizopita, waliitazamia siku kuu ambapo uasi-sheria, ukandamizaji, na jeuri zingekoma kisha uadilifu uenee kila mahali. Je, tunaweza kuwa na hakika kwamba ahadi hiyo itatimizwa?

      2. Ni nabii yupi aliyekuwa ameongea juu ya “mbingu mpya na dunia mpya,” na unabii huo wa kale unatimizwa kwa njia zipi?

      2 Ndiyo, tunaweza! Petro alipoongea juu ya “mbingu mpya na dunia mpya,” hakuwa akianzisha wazo jipya. Karibu miaka 800 mapema, Yehova alimtumia nabii Isaya kutamka maneno kama hayo. Ahadi hiyo ya mapema ilitimizwa kwa njia ndogo mwaka wa 537 K.W.K. wakati Wayahudi walipofunguliwa kutoka utekwani Babiloni, na hivyo wakaweza kuirudia nchi yao. Lakini unabii wa Isaya unatimizwa kwa njia kubwa leo, na tunatazamia utimizo wa kusisimua hata zaidi katika ulimwengu mpya wa Mungu unaokuja. Kwa kweli, unabii wa kuchangamsha moyo uliotolewa kupitia Isaya ni kionjo tu cha baraka ambazo Mungu amewawekea wale wanaompenda.

      Yehova Anajitahidi Kuwavutia ‘Watu Wenye Vichwa Vigumu’

      3. Tunapewa jibu la swali gani katika Isaya sura ya 65?

      3 Kumbuka kwamba andiko la Isaya 63:15–64:12 lina sala ya Isaya ya kiunabii iliyotolewa kwa ajili ya wahamishwa Wayahudi walioko Babiloni. Kama vile maneno ya Isaya yanavyoonyesha wazi, Wayahudi wengi hawamwabudu Yehova kwa nafsi yote, lakini wengine wao wametubu na kumgeukia. Je, sasa Yehova atalirudishia taifa hali yake ya kwanza kwa ajili ya mabaki hao wenye majuto? Tunapata jibu la Yehova katika Isaya sura ya 65. Lakini kabla ya kutamka ahadi ya ukombozi kwa ajili ya waaminifu hao wachache, Yehova anaeleza hukumu inayowangoja wengi wasio na imani.

      4. (a) Kwa kutofautiana na watu wake waasi, ni nani atakayemtafuta Yehova? (b) Mtume Paulo aliyatumiaje maneno ya Isaya 65:1, 2?

      4 Yehova ameuvumilia uasi ambao watu wake wamezidi kuonyesha. Hata hivyo, wakati utafika awaachilie mikononi mwa adui zao, kisha awapokee wengine kwa fadhili na kuwaonyesha ukubali wake. Yehova anasema hivi kupitia Isaya: “Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu, Nitazameni, nitazameni.” (Isaya 65:1, 2a) Inasikitisha sana kwamba watu wa mataifa watamjia Yehova, lakini taifa la Yuda lenye kichwa kigumu litakataa kwa ujumla kufanya hivyo. Si nabii Isaya peke yake aliyetabiri kwamba hatimaye Mungu atachagua jamii ya watu wasiowahi kutambulikana hapo kwanza. (Hosea 1:10; 2:23) Mtume Paulo alinukuu Isaya 65:1, 2 kutoka kwenye Septuagint ili kuthibitisha kwamba watu wa mataifa wangepata “uadilifu utokanao na imani,” hata ingawa Wayahudi wa asili waliukataa.—Waroma 9:30; 10:20, 21.

      5, 6. (a) Yehova ameonyesha kwamba anatamani nini sana, lakini watu wake wameitikiaje? (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na njia za Yehova za kushughulika na Yuda?

      5 Yehova anaeleza ni kwa nini ataruhusu watu wake mwenyewe wapatwe na mabaya: “Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi [“wenye vichwa vigumu,” “NW”], watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe.” (Isaya 65:2b) Kunyoosha mikono kunamaanisha kualika watu au kuwasihi. Yehova amenyoosha mikono yake, si kwa muda mfupi tu, bali mchana kutwa. Moyo wake unatamani kwamba Yuda wamrudie. Lakini watu hawa wenye vichwa vigumu wamekataa kuitikia.

      6 Lo, maneno ya Yehova yanatufunza somo la kuchangamsha kama nini! Anataka tumkaribie kwa sababu yeye ni Mungu anayeweza kufikiwa. (Yakobo 4:8) Vilevile maneno hayo yanatuonyesha kwamba Yehova ni mnyenyekevu. (Zaburi 113:5, 6) Ingawaje, yeye huendelea kunyoosha mikono yake kwa njia ya mfano, akiwasihi sana watu wake warudi ijapokuwa vichwa vyao vigumu vimefanya ‘ahuzunike.’ (Zaburi 78:40, 41) Hatimaye anawaachilia mikononi mwa adui zao, baada tu ya kuwasihi kwa upole muda wa karne nyingi. Na bado hawafungii mlango watu mmoja-mmoja walio wanyenyekevu wanaotaka kurudi.

      7, 8. Watu wa Yehova walio na vichwa vigumu wamechocheaje hasira yake?

      7 Wayahudi wenye vichwa vigumu wamechochea hasira ya Yehova mara nyingi kwa mwenendo wao wa aibu. Yehova anaeleza hivi kuhusu matendo yao yenye kuudhi: “Watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali; waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao; watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.” (Isaya 65:3-5) Watu hawa ambao wanaonekana kama wenye kicho wanamwudhi Yehova ‘mbele za uso wake’—usemi unaoweza kumaanisha ujeuri na madharau. Hawajitahidi hata kidogo kuyaficha machukizo yao. Je, si kweli kwamba hatia ya dhambi zao inazidi kuwa kubwa kwa sababu wanazitenda pale pale mbele za Yule wanayepaswa kumheshimu na kumtii?

      8 Kwa kweli, watenda-dhambi hao wanaojiona kuwa waadilifu ni kama wanawaambia hivi Wayahudi wenzao: ‘Kaa mbali nami, kwa sababu mimi ni mtakatifu kukushinda.’ Unafiki gani huo! Watu hao wanaodai eti ni “wenye kicho” wanatoa dhabihu na kuiwashia uvumba miungu ya uwongo, jambo linalokatazwa na Sheria ya Mungu. (Kutoka 20:2-6) Wameketi kati ya makaburi,hiyo ikiwafanya wawe wachafu kulingana na Sheria.(Hesabu 19:14-16)Wanakula nyama ya nguruwe, chakula kichafu.a (Mambo ya Walawi 11:7) Hata hivyo, utendaji wao wa kidini unawafanya wajione kuwa watakatifu kuliko Wayahudi wengine, na wanataka wengine wakae mbali nao, eti watu hao wasitakasike au kuwa safi kwa sababu ya kushirikiana nao. Hata hivyo, jambo hilo halipatani hata kidogo na maoni ya yule Mungu ambaye hutaka apewe “ujitoaji wa pekee”!—Kumbukumbu la Torati 4:24, NW.

      9. Yehova anawaonaje watenda-dhambi hao wanaojiona kuwa waadilifu?

      9 Badala ya kuwaona kuwa watakatifu watu hawa wanaojiona kuwa waadilifu, Yehova anasema hivi: “Watu hao ni moshi puani mwangu.” Neno la Kiebrania la kutaja ‘pua’ au ‘tundu la pua’ hutumiwa mara nyingi kwa njia ya mfano kumaanisha hasira. Vilevile, moshi hushirikishwa na hasira ya Yehova inayowaka. (Kumbukumbu la Torati 29:20) Ibada ya sanamu yenye kuchukiza ambamo watu wake wametumbukia imechochea hasira kali ya Yehova.

      10. Yehova atawalipaje wale walio katika Yuda kwa sababu ya dhambi zao?

      10 Kwa kufuata haki yake, Yehova hawezi kuwaachilia watenda-dhambi hao wa kukusudia bila kuwapa adhabu. Isaya anaandika hivi: “Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao; maovu yenu na maovu ya baba zenu pamoja, asema BWANA, ninyi mliofukiza uvumba juu ya milima, na kunitukana juu ya vilima; basi, kwa ajili ya hayo nitawapimia kwanza kazi yao vifuani mwao.” (Isaya 65:6, 7) Kwa kujihusisha katika ibada ya uwongo, Wayahudi hawa wamemletea Yehova aibu. Wameifanya ibada ya Mungu wa kweli ionekane kuwa sawa tu na ibada ya mataifa yanayowazunguka. Yehova atawalipa “vifuani mwao” kwa ajili ya ‘maovu yao,’ ambayo ni kutia na ibada ya sanamu na uwasiliani-roho. Inaonekana kwamba usemi ‘kifua’ unamaanisha mkunjo uliotokea katika sehemu ya juu ya vazi, ukawa kama mfuko mdogo ambamo wauzaji wa bidhaa wangeweza kumwagilia mazao ya kipimo fulani. (Luka 6:38) Kinachomaanishwa kuhusu Wayahudi waasi-imani ni wazi—Yehova atawapimia “ujira” au adhabu yao. Mungu wa haki atadai malipo. (Zaburi 79:12; Yeremia 32:18) Vivyo hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba, kwa kuwa Yehova si kigeugeu, yeye ataupimia mfumo huu mwovu wa mambo kipimo cha adhabu katika wakati wake mwenyewe.—Malaki 3:6.

      “Kwa Ajili ya Watumishi Wangu”

      11. Yehova anaonyeshaje kwamba ataokoa mabaki waaminifu?

      11 Je, Yehova atawaonyesha rehema waaminifu walio miongoni mwa watu wake? Isaya anaeleza hivi: “BWANA asema hivi, Kama vile divai mpya ipatikanavyo katika kichala, na mtu mmoja husema, Usikiharibu kwa maana mna baraka ndani yake; ndivyo nitakavyotenda kwa ajili ya watumishi wangu, ili nisiwaharibu wote. Nami nitaleta uzao toka Yakobo, na mrithi wa milima yangu toka Yuda, na mteule wangu atairithi, na watumishi wangu watakaa huko.” (Isaya 65:8, 9) Akiwalinganisha watu wake na kichala cha zabibu, Yehova anatumia mfano wanaoweza kuuelewa kwa urahisi. Zabibu ni tele nchini, na divai inayotayarishwa kutokana na zabibu ni baraka kwa wanadamu. (Zaburi 104:15) Huenda ikawa kwamba wazo linalotolewa hapa ni lile la kichala ambacho kina zabibu kadhaa nzuri, na nyingine zisizo nzuri. Au huenda ikawa kwamba kichala kimoja ndicho kizuri, lakini vichala vile vingine havijaiva au vimeoza. Vyovyote vile, mtunza-mizabibu hataharibu zabibu nzuri. Hivyo Yehova anawahakikishia watu wake kwamba hataliharibu taifa hilo kabisa bali ataachilia mabaki waaminifu. Anasema kwamba mabaki hao wenye hali ya kukubaliwa watarithi “milima” yake, yaani Yerusalemu na nchi ya Yuda, nchi ya vilima-vilima ambayo Yehova aliitwaa iwe mali yake mwenyewe.

      12. Ni baraka zipi zinazowangoja mabaki waaminifu?

      12 Ni baraka zipi zinazowangoja mabaki hawa waaminifu? Yehova anaeleza hivi: “Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng’ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.” (Isaya 65:10) Makundi ya kondoo ni sehemu muhimu ya maisha ya Wayahudi wengi, na nchi kubwa ya malisho inasaidia kuleta ufanisi nyakati za amani. Yehova anataja maeneo mawili yaliyo kwenye miisho ya nchi ili kuonyesha hali ya amani na ufanisi. Upande wa magharibi kuna Uwanda wa Sharoni, unaojulikana sana kwa uzuri na rutuba yake, nao unaambaa na Pwani ya Mediterania kwa mwendo mrefu. Bonde la Akori ni sehemu ya mpaka wa nchi ulioko kaskazini-mashariki. (Yoshua 15:7) Maeneo haya, kutia na sehemu ile nyingine yote ya nchi, yatakaa hali ya ukiwa wakati wa uhamisho unaokuja. Hata hivyo, Yehova anaahidi kwamba baada ya uhamisho maeneo hayo yatakuwa malisho mazuri, yatumiwe na mabaki watakaorudi.—Isaya 35:2; Hosea 2:15.

      Kumtumaini “Mungu wa Bahati Nzuri”

      13, 14. Ni mazoea gani yanayoonyesha kwamba watu wa Mungu wamemwacha, nao watapatwa na jambo gani?

      13 Sasa unabii wa Isaya unaelekezwa tena kwa wale ambao wamemwacha Yehova na kudumu katika ibada ya sanamu. Unasema hivi: “Ninyi mmwachao BWANA, na kuusahau mlima wangu mtakatifu, na kuandika meza kwa ajili ya Bahati [“mungu wa Bahati Nzuri,” “NW”], na kuijazia Ajali [“mungu wa Ajali,” “NW”] vyombo vya divai iliyochanganyika.” (Isaya 65:11) Kwa kutandika meza ya chakula na kinywaji mbele ya “mungu wa Bahati Nzuri” na “mungu wa Ajali,” Wayahudi hawa wenye kurudi nyuma wametumbukia katika mazoea ya ibada ya sanamu ya mataifa ya kipagani.b Itakuwaje kwa wowote wanaoitumaini miungu hiyo kwa ujinga-ujinga?

      14 Yehova anawaonya wazi hivi: “Mimi nitawaandikia [“nitawajalia,” “NW”] kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia.” (Isaya 65:12) Kwa kutumia Kiebrania cha awali, Yehova anagonganisha maneno ‘jalia’ na “ajali” kusema kwamba wale wanaomwabudu mungu huyo wa uwongo ‘watajaliwa kuuawa kwa upanga,’ maana yake kupatwa na uharibifu. Mara nyingi Yehova amewatumia manabii wake kuwahimiza watu hao watubu, lakini wamempuuza wakaamua kwa vichwa vigumu kufanya yale wanayojua ni mabaya machoni pake. Lo, wanamwonyesha Mungu madharau yaliyoje! Onyo la Mungu litatimizwa wakati taifa hilo litakapopatwa na maangamizi makubwa mwaka wa 607 K.W.K. Huo ni wakati ambao Yehova atawaruhusu Wababiloni waharibu Yerusalemu na hekalu lake. Hapo “mungu wa Bahati Nzuri” atashindwa kuwalinda wafuasi wake wenye bidii walioko Yuda na Yerusalemu.—2 Mambo ya Nyakati 36:17.

      15. Wakristo wa kweli wanaliitikiaje onyo linalopatikana kwenye Isaya 65:11, 12?

      15 Leo Wakristo wa kweli wanatii onyo linalopatikana kwenye Isaya 65:11, 12. Wao hawaamini “Bahati Nzuri,” kana kwamba ina nguvu nyingi zinazopita zile za asili ya kibinadamu katika kuwafanyia mambo ya hisani. Wao hukataa kutapanya mali zao kwa kujaribu kumtuliza “mungu wa Bahati Nzuri,” na kwa hiyo wanaepuka namna zote za kucheza kamari. Wanasadiki kwamba wale wanaojitoa kufanya mapenzi ya mungu huyo watapoteza kila kitu hatimaye, kwani Yehova anawaambia hivi watu wa namna hiyo: ‘Nitawajalia kuuawa kwa upanga.’

      “Tazama, Watumishi Wangu Watafurahi”

      16. Yehova atawabariki watumishi wake waaminifu kwa njia zipi, lakini itakuwaje kwa wale ambao wamemwacha?

      16 Unabii unaeleza kwamba kuna thawabu tofauti-tofauti ambazo zinawangoja wale wanaomwabudu Mungu kwa moyo mweupe na wale wanaofanya hivyo kwa unafiki. Unafanya hivyo kwa kuwakaripia wale ambao wamemwacha Yehova: “Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika; tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha [“hali njema,” “NW”] ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.” (Isaya 65:13, 14) Yehova atawabariki watumishi wake waaminifu. Wakiwa na mioyo inayofurika shangwe, watabubujika kelele za furaha. Kula, kunywa, na kufurahi ni maneno yanayoonyesha kwamba Yehova atatosheleza mahitaji ya waabudu wake kwa vitu kemkemu. Tofauti na hivyo, wale ambao wamechagua kumwacha Yehova wataona njaa na kiu ya kiroho. Mahitaji yao hayatatoshelezwa. Watalia kwa sauti kubwa na kupiga makelele ya kuomboleza kwa uchungu na msononeko.

      17. Kwa nini watu wa Mungu leo wana sababu nzuri ya kuimba kwa furaha?

      17 Maneno ya Yehova yanaieleza vizuri hali ya kiroho ya watu ambao leo wanadai kwa maneno tu kwamba wanamtumikia Mungu. Hata ingawa mamilioni ya watu wa Jumuiya ya Wakristo wana uchungu wa roho, waabudu wa Yehova wanaimba kwa furaha. Nao wana sababu nzuri ya kushangilia. Wanalishwa vema kiroho. Yehova huwaandalia chakula kingi cha kiroho kupitia vichapo vya Kibiblia na makusanyiko ya Kikristo. Kwa hakika, zile kweli zenye kujenga na ahadi zenye faraja zilizo katika Neno la Mungu hutupatia ‘hali njema ya moyo’!

      18. Wale ambao wamemwacha Yehova watabaki na kitu gani, na kuapa kwa jina lao huenda kukawa kunadokeza nini?

      18 Yehova anaendelea kuongea na wale ambao wamemwacha: “Nanyi mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa wateule wangu. Na Bwana MUNGU atakuua; naye atawaita watumishi wake kwa jina lingine. Hata itakuwa yeye atakayejibariki duniani, atajibariki kwa Mungu wa kweli; naye atakayeapa duniani, ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za kwanza zimesahauliwa, na kwa kuwa zimefichwa machoni pangu.” (Isaya 65:15, 16) Wale ambao wamemwacha Yehova watabaki na jina lao tu, nalo litatumika katika kuapa tu, au kulaani. Huenda hiyo ikamaanisha kwamba wale wanaotaka kujifunga kwa kiapo kizito, watakuwa ni kama wanasema hivi: ‘Nisipotimiza ahadi hii, acha nipatwe na adhabu iliyowapata wale waasi-imani.’ Huenda hata ikamaanisha kwamba jina lao litatumiwa kwa njia ya mfano, kama Sodoma na Gomora, ili liwe mfano wa adhabu ya Mungu juu ya waovu.

      19. Watumishi wa Mungu wataitwaje jina jingine, na kwa nini watakuwa na uhakika wa kumwamini yule Mungu wa uaminifu? (Ona pia kielezi-chini.)

      19 Lakini hali ya watumishi wa Mungu itakuwa tofauti kama nini! Wataitwa jina jingine. Hiyo ni kuonyesha kwamba watabarikiwa na kuheshimiwa wakiisha kurudi katika nchi ya kwao. Hawatatafuta baraka kwa mungu yeyote wa uwongo wala hawataapa kwa jina la sanamu yoyote isiyo na uhai. Bali, wanapojibariki au kuapa, watafanya hivyo kwa jina la yule Mungu wa uaminifu. (Isaya 65:16, kielezi-chini katika tafsiri ya NW) Wakaaji wa nchi watakuwa na sababu ya kumwamini Mungu wakiwa na uhakika kabisa, kwani atakuwa amethibitisha kuwa yeye ni mtimizaji wa ahadi zake.c Wayahudi wakiisha kuwa salama nchini mwao, wataisahau upesi misononeko iliyowapata zamani.

      “Ninaumba Mbingu Mpya na Dunia Mpya”

      20. Ahadi ya Yehova ya “mbingu mpya na dunia mpya” ilitimizwaje mwaka wa 537 K.W.K.?

      20 Sasa Yehova anaieleza kwa mapana na marefu ahadi yake ya kuwarudishia hali nzuri wale mabaki wenye toba wakiisha kurejea kutoka uhamishoni Babiloni. Kupitia Isaya, Yehova anasema hivi: “Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya, na maneno ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17, “Zaire Swahili Bible”) Ni hakika kwamba ahadi ya Yehova ya kurudishwa kwa hali za kwanza itatimizwa, kwa hiyo yeye anaongea kana kwamba tukio hilo la wakati ujao la kurudishwa kwa hali za kwanza limekwisha anza. Unabii huu ulitimizwa mara ya kwanza mwaka wa 537 K.W.K. wakati mabaki Wayahudi waliporudishwa Yerusalemu. “Mbingu mpya” zilikuwa nini wakati huo? Zilikuwa ugavana wa Zerubabeli ulioungwa mkono na Kuhani wa Cheo cha Juu, Yoshua, mahali pakuu pa ugavana huo pakiwa ni Yerusalemu. Mabaki Wayahudi waliorudishwa ndio waliokuwa “dunia mpya,” yaani jamii iliyosafishwa, nao walijitiisha chini ya utawala huo na kusaidia kuanzisha upya ibada safi nchini. (Ezra 5:1, 2) Shangwe ya kurudishwa huko ilifunika mateso yote ya zamani; misononeko ya zamani hata haikukumbukwa.—Zaburi 126:1, 2.

      21. Ni mbingu mpya zipi zilizotokea mwaka wa 1914?

      21 Hata hivyo, kumbuka kwamba Petro alirudia maneno ya unabii wa Isaya akaonyesha kwamba ungetimizwa wakati ujao. Mtume huyo aliandika hivi: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13) Mwaka wa 1914 zile mbingu mpya zilizokuwa zimengojewa sana zilitokea. Ufalme wa Kimesiya uliozaliwa mwaka huo unatawala kutoka mbinguni kwenyewe, na Yehova ameupa ufalme huo mamlaka ya kuitawala dunia yote. (Zaburi 2:6-8) Serikali hiyo ya Ufalme, iliyo chini ya Kristo na watawala wenzake 144,000, ndio mbingu mpya.—Ufunuo 14:1.

      22. Dunia mpya itafanyizwa kwa watu gani, na watu wanatayarishwaje hata sasa ili wawe kiini cha mpango huo?

      22 Namna gani dunia mpya? Kwa kufuata kielelezo cha utimizo wa kale, dunia mpya itafanyizwa kwa watu wanaofurahia kujitiisha chini ya utawala wa serikali mpya ya kimbingu. Hata sasa, mamilioni ya watu mmoja-mmoja wenye mwelekeo unaofaa wananyenyekea chini ya serikali hiyo na kujitahidi kufuata sheria zake zilizo katika Biblia. Wanatoka katika taifa zote, lugha zote, na jamii zote, nao hushirikiana kumtumikia Mfalme Yesu Kristo anayetawala. (Mika 4:1-4) Mfumo mwovu wa mambo uliopo ukiisha kupita, kikundi hicho ndicho kitakachofanyizwa kuwa kiini cha dunia mpya na hatimaye kiwe jamii ya wanadamu wenye kumhofu Mungu watakaokuwa kila mahali ulimwenguni, wakiwa warithi wa makao ya kidunia ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 25:34.

      23. Ni habari zipi tunazozipata katika kitabu cha Ufunuo kuhusu “mbingu mpya na dunia mpya,” na unabii huo utatimizwaje?

      23 Kitabu cha Ufunuo kinaelezea njozi ambayo mtume Yohana aliona kuhusu siku ya Yehova inayokuja, wakati ambao mfumo huu wa mambo utaondolewa. Halafu Shetani atafungwa ndani ya abiso. (Ufunuo 19:11–20:3) Baada ya maelezo hayo, Yohana anayarudia maneno ya kiunabii ya Isaya, akiandika hivi: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya.” Mistari inayofuata ya masimulizi ya njozi hii tukufu inaeleza juu ya wakati ambao Yehova Mungu atabadili kabisa hali za dunia hii ziwe nzuri zaidi. (Ufunuo 21:1, 3-5) Ni wazi kwamba ahadi ya Isaya ya “mbingu mpya na dunia mpya” itatimizwa vizuri ajabu katika ulimwengu mpya wa Mungu! Jamii mpya ya kidunia itafurahia paradiso ya kiroho na hata ya kihalisi, ikiwa chini ya mbingu mpya za kiserikali. Ile ahadi ya kwamba “maneno ya kwanza [magonjwa, mateso, na ole mwingine mwingi unaopata wanadamu] hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni” inafariji kweli kweli. Ikiwa wakati huo tutakumbuka jambo lolote lile, halitatutia madhara wala maumivu yanayolemea mioyo ya wengi wakati wa sasa.

      24. Kwa nini Yehova atashangilia kurudishwa kwa Yerusalemu, na ni nini ambacho hakitasikiwa tena katika barabara za jiji?

      24 Unabii wa Isaya unaendelea kusema hivi: “Furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.” (Isaya 65:18, 19) Si Wayahudi peke yao watakaoshangilia kurudishwa kwenye nchi yao, bali Mungu mwenyewe atashangilia pia, kwa maana atarembesha jiji la Yerusalemu—ambalo kwa mara nyingine litakuwa limekuwa mahali pakuu pa ibada ya kweli duniani. Ile sauti ya kulia kwa sababu ya maafa, iliyosikiwa katika barabara za jiji miongo kadhaa mapema, haitasikiwa tena.

      25, 26. (a) Katika siku zetu, Yehova anafanyaje Yerusalemu liwe “shangwe”? (b) Yehova atatumia Yerusalemu Jipya kwa njia gani, na kwa nini sisi tunaweza kushangilia leo?

      25 Leo, pia, Yehova anafanya Yerusalemu liwe “shangwe.” Jinsi gani? Kama vile tumekwisha kuona, hatimaye zile mbingu mpya zilizotokea mwaka wa 1914 zitahusisha pia watawala wenzi 144,000, wenye kushiriki katika ile serikali ya kimbingu. Mbingu hizo zinatajwa kiunabii kuwa “Yerusalemu Jipya.” (Ufunuo 21:2) Yerusalemu Jipya ndilo linalomaanishwa wakati Mungu anaposema hivi: “Tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.” Yerusalemu Jipya litatumiwa na Mungu kuwamiminia wanadamu watiifu baraka zisizo na kifani. Haitasikiwa tena sauti ya kulia wala ya maombolezo, kwa maana Yehova atatosheleza “haja za moyo [wetu].”—Zaburi 37:3, 4.

      26 Kwa kweli, sisi leo tuna sababu kamili ya kufurahi sana! Karibuni Yehova atatakasa jina lake maarufu kwa kuwaharibu wapinzani wote. (Zaburi 83:17, 18) Kisha mbingu mpya peke yake zishike usukani kusimamia mambo yote. Lo, hizo ni sababu nzuri kama nini za kufurahi sana na kukishangilia milele kile kinachoumbwa na Mungu!

      Ahadi ya Wakati Ujao Wenye Usalama

      27. Isaya anaelezaje kuhusu usalama ambao wale wenye kurudi wataufurahia katika nchi yao?

      27 Katika utimizo wa kwanza, maisha yatakuwaje kwa Wayahudi wenye kurudi wakiwa chini ya mbingu mpya? Yehova anasema hivi: “Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.” (Isaya 65:20) Hiyo inaonyesha vizuri kama nini usalama ambao wahamishwa wenye kurudi watafurahia katika nchi yao iliyorudishwa! Kifo kisichotazamiwa hakitampata mzaliwa-juzi, maana yake kitoto cha siku chache tu. Wala kifo cha jinsi hiyo hakitammaliza mzee asiyetimiza maisha yake.d Maneno ya Isaya yanawafariji kweli kweli Wayahudi watakaorudi Yuda! Wakiisha kuwa salama nchini mwao, hawana tena haja ya kufanya wasiwasi eti adui zao watasomba watoto wao wachanga au kuchinja mashujaa wao.

      28. Tunajifunza nini kutokana na maneno ya Yehova juu ya maisha katika ulimwengu mpya chini ya Ufalme wake?

      28 Maneno ya Yehova yanatuambia nini juu ya maisha katika ulimwengu mpya unaokuja? Chini ya Ufalme wa Mungu, kila mtoto atakuwa na tarajio la kupata wakati ujao ulio salama. Kifo hakitaua tena mwanamume anayemhofu Mungu akiwa katika umri wake wa ufanisi mkubwa. Bali, wanadamu watiifu watakuwa salama salimini, na wataweza kufurahia maisha. Namna gani watu wowote wanaochagua kumwasi Mungu? Watapoteza pendeleo la uhai. Hata ikiwa mtenda-dhambi anayeasi ana “umri wa miaka mia,” atakufa. Hapo yeye atakuwa “mtoto wa siku chache” akilinganishwa na vile angaliweza kuwa—mtu mwenye maisha yasiyo na kikomo.

      29. (a) Watu wa Mungu walio watiifu watapata shangwe zipi katika nchi ya Yuda iliyorudishwa? (b) Kwa nini miti ni mfano unaofaa wa maisha marefu? (Ona kielezi-chini.)

      29 Yehova anaendelea kueleza juu ya hali zitakazokuwako katika nchi iliyorudishwa ya Yuda: “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22) Baada ya kuirudia nchi ya Yuda, ambayo bila shaka haikuwa na nyumba wala mizabibu, watu wa Mungu walio watiifu watakuwa na shangwe ya kuishi katika nyumba zao wenyewe na kula matunda kutoka mashamba yao wenyewe ya mizabibu. Mungu ataibariki kazi yao, na wataishi maisha marefu—marefu kama siku za mti—wafurahie matunda ya kazi zao.e

      30. Watumishi wa Yehova wanafurahia hali gani leo, na watafurahia nini katika ulimwengu mpya?

      30 Unabii huu umepata utimizo fulani katika siku zetu. Watu wa Yehova walitoka kwenye uhamisho wa kiroho mwaka wa 1919, wakaanza kurudisha hali za kwanza katika “nchi” au makao yao ya utendaji na ibada. Walijenga makutaniko na kusitawisha hali ya kuzaa matunda ya kiroho. Matokeo ni kwamba, hata sasa watu wa Yehova wanafurahia paradiso ya kiroho na amani waliyopewa na Mungu. Tunaweza kuwa na hakika kwamba amani hiyo itaendelea mpaka ndani ya ile Paradiso halisi. Hata haiwezekani kuwaza kwa usahihi ni maajabu gani ambayo Yehova atafanya katika ulimwengu mpya kwa kuitumia mioyo na mikono ya waabudu wake wenye nia ya kufanya kazi. Itakuwa shangwe iliyoje kujenga nyumba yako mwenyewe kisha kuishi ndani yake! Chini ya utawala wa Ufalme, hakutakuwako upungufu wa kazi ya kuridhisha. Utafurahi kama nini “kujiburudisha kwa mema” ya matunda ya kazi zako mwenyewe sikuzote! (Mhubiri 3:13) Je, tutapata wakati wa kutosha kuifurahia sana kazi ya mikono yetu? Kabisa! Maisha yasiyo na kikomo ya wanadamu waaminifu yatakuwa “kama siku za mti”—maelfu ya miaka, na hata zaidi!

      31, 32. (a) Wahamishwa wanaorudi watafurahia baraka zipi? (b) Wanadamu waaminifu watakuwa na tazamio gani katika ulimwengu mpya?

      31 Yehova anaeleza juu ya baraka zaidi zinazowangoja wahamishwa wanaorudi: “Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na BWANA, na watoto wao pamoja nao.” (Isaya 65:23) Wayahudi hao waliorudishwa watabarikiwa na Yehova, na kwa hiyo hawatafanya kazi ya bure. Wazazi hawatazaa watoto ili tu wapatwe na kifo cha mapema. Watu wale waliokuwa uhamishoni hawatafurahia baraka za kurudishwa wakiwa peke yao; wazao wao watakuwa pamoja nao. Mungu ana hamu nyingi ya kutimiza mahitaji ya watu wake kiasi cha kuahidi hivi: “Itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.”—Isaya 65:24.

      32 Yehova atatimizaje ahadi hizo katika ulimwengu mpya unaokuja? Tungoje tuone. Yehova hajaeleza jinsi kila kitu kitakavyokuwa, lakini tunaweza kuwa na hakika kwamba wanadamu waaminifu “hawatajitaabisha kwa kazi bure” tena. Umati mkubwa wa waokokaji wa Har-Magedoni na watoto wowote ambao huenda wakawazaa watakuwa na tazamio la maisha marefu ya kuridhisha—uhai wa milele! Hata wale watakaofufuliwa kisha wachague kuishi kupatana na viwango vya Mungu watapata shangwe ya kuwa katika ulimwengu mpya. Yehova atayasikia na kuyatimiza mahitaji yao, hata kuyatazamia. Kwa kweli, Yehova ataufungua mkono wake na kuridhisha “kila kilicho hai matakwa yake.”—Zaburi 145:16.

      33. Wayahudi watakapoirudia nchi yao, wanyama wataishije kwa amani?

      33 Amani na usalama ambazo zimeahidiwa zitakuwa za kiasi gani? Yehova anamalizia sehemu hii ya unabii kwa kusema hivi: “Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema BWANA.” (Isaya 65:25) Wakati mabaki ya Wayahudi waaminifu watakapoirudia nchi yao, watakuwa chini ya utunzaji wa Yehova. Itakuwa ni kama simba anakula majani kama ng’ombe, kwa maana simba hatawadhuru Wayahudi wala wanyama wao wa kufugwa. Ahadi hiyo ni hakika, kwa maana inamalizika kwa kusema, ‘asema Yehova.’ Na neno lake hutimia daima!—Isaya 55:10, 11.

      34. Maneno ya Yehova yana utimizo gani wenye kusisimua leo na katika ulimwengu mpya?

      34 Leo maneno ya Yehova yanatimizwa kwa njia ya kusisimua miongoni mwa waabudu wa kweli. Tangu mwaka wa 1919, Mungu ameibariki nchi ya kiroho ya watu wake, akaigeuza kuwa paradiso ya kiroho. Wale wanaoingia katika paradiso hii ya kiroho hufanya mabadiliko ya ajabu katika maisha yao. (Waefeso 4:22-24) Watu mmoja-mmoja ambao wakati mmoja walikuwa na nyutu za kinyama—ambao labda waliwatumia vibaya wanadamu wenzao au wakawadhulumu kwa njia nyinginezo—wanafanya maendeleo ya kuyamaliza makali ya tabia zisizopendeza kwa msaada wa roho ya Mungu. Matokeo ni kwamba, wanafurahia amani na umoja wa ibada pamoja na waamini wenzao. Baraka zinazofurahiwa sasa na watu wa Yehova katika paradiso yao ya kiroho zitaendelea mpaka ndani ya Paradiso halisi, ambamo amani itakuwamo miongoni mwa wanadamu, na hali kadhalika miongoni mwa wanyama. Tunaweza kuwa na hakika kwamba lile agizo ambalo Mungu aliwapa wanadamu hapo awali litatimizwa kabisa kwa njia inayofaa, yaani: ‘Kuitiisha nchi; kutawala samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.’—Mwanzo 1:28.

      35. Kwa nini tuna sababu nzuri sana ya ‘kushangilia daima’?

      35 Tunashukuru kama nini kwa ajili ya ahadi ya Yehova ya kuumba “mbingu mpya na dunia mpya”! Ahadi hiyo ilitimizwa mwaka wa 537 K.W.K., na inatimizwa zaidi leo. Utimizo huo wa mara mbili unaonyesha jinsi wanadamu watiifu wanavyoweza kupata wakati ujao ulio mtukufu. Yehova ametufadhili kwa kutupatia sisi, kupitia unabii wa Isaya, kionjo cha mambo ambayo amewawekea wale wanaompenda. Kwa kweli tuna sababu nzuri sana ya kuyatii maneno haya ya Yehova: “Mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo”!—Isaya 65:18.

      [Maelezo ya Chini]

      a Watu wengi wanafikiri kwamba watenda dhambi hawa walikuwa kati ya makaburi wakijaribu kuwasiliana na wafu. Kula kwao nyama ya nguruwe huenda kukawa kulihusiana na ibada ya sanamu.

      b Akitoa maelezo juu ya mstari huo, Jerome, mtafsiri wa Biblia (aliyezaliwa katika karne ya nne W.K.) anaeleza desturi fulani ya kale iliyofuatwa na waabudu-sanamu siku ya mwisho ya mwezi wa mwisho katika mwaka wao. Aliandika hivi: “Walikuwa wakitandika meza iliyojaa aina-aina za vyakula na kikombe kilichojazwa divai tamu ili kuhakikisha kwamba mazao waliyopata mwaka jana au yale watakayopata mwaka unaokuja yataleta bahati nzuri.”

      c Kulingana na Isaya 65:16 katika maandishi ya Kimasoreti ya Kiebrania, Yehova ndiye “Mungu wa Ameni.” “Ameni” humaanisha “na iwe hivyo,” au “ni hakika,” na hilo ni neno la kutoa uthibitisho au uhakikisho wa kwamba jambo fulani ni la kweli au ni sharti litimie. Kwa kutimiza ahadi zake zote, Yehova anaonyesha kwamba yale anayoyasema ni ya kweli.

      d Biblia iitwayo The Jerusalem Bible hufasiri Isaya 65:20 hivi: “Hakutapatikana tena kitoto kichanga chenye kuishi siku chache tu, wala mzee asiyeishi hadi mwisho wa siku zake.”

      e Miti ni mfano unaofaa wa maisha marefu kwa maana ina maisha marefu kuliko vitu vingine vyote vilivyo hai vinavyojulikana. Kwa mfano, mzeituni huzaa matunda kwa mamia ya miaka, na huenda ukaishi hata miaka elfu moja.

      [Picha katika ukurasa wa 389]

      Katika ulimwengu mpya wa Mungu, tutakuwa na wakati wa kutosha kuifurahia kazi ya mikono yetu

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Saba

      Yehova Hubariki Ibada Safi

      Isaya 66:1-14

      1. Ni vichwa gani vinavyokaziwa katika sura ya mwisho ya Isaya, na ni maswali gani yanayojibiwa?

      KATIKA sura ya mwisho ya Isaya, baadhi ya vichwa vikuu vya kitabu hiki cha kiunabii vinafikishwa kwenye upeo wenye mkazo mwingi, na maswali kadhaa muhimu yanajibiwa. Miongoni mwa vichwa vinavyokaziwa ni kutukuka kwa Yehova, chuki yake kuelekea unafiki, azimio lake la kuwaadhibu waovu, na upendo na hangaiko lake kuwaelekea waaminifu. Isitoshe, maswali yafuatayo yanajibiwa: Ni nini hutofautisha ibada ya kweli na ile ya uwongo? Tunaweza kuwaje na uhakika kwamba Yehova atawalipa wanafiki adhabu yao kwa sababu wanasingizia kuwa watakatifu huku wakiwakandamiza watu wa Mungu? Na Yehova atawabarikije wale wanaobaki wakiwa waaminifu kwake?

      Ufunguo wa Ibada Safi

      2. Yehova anatoa tamko gani kuhusu fahari yake, lakini tamko hilo halina maana gani?

      2 Kwanza, unabii unakazia fahari ya Yehova: “BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali [“kibago,” “NW”] pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?” (Isaya 66:1) Watu fulani wanaamini kwamba nabii anawavunja moyo Wayahudi wasimjengee Yehova hekalu tena wakati taifa litakaporudishwa kwenye nchi yao. Lakini si hivyo; Yehova mwenyewe atatoa amri hekalu lijengwe upya. (Ezra 1:1-6; Isaya 60:13; Hagai 1:7, 8) Basi je, kifungu hicho kina maana gani?

      3. Kwa nini inafaa kwamba dunia inaelezewa kuwa “kibago” cha Yehova?

      3 Kwanza, ingefaa tufikirie ni kwa nini dunia inatajwa kuwa “kibago” cha Yehova. Huo si usemi wa madharau. Kati ya yale mabilioni ya nyota na maumbo mengine yaliyo katika ulimwengu mzima, ni dunia tu inayopewa jina hilo la kipekee. Sayari yetu itabaki milele bila nyingine ya kufanana nayo, kwa maana hapa ndipo Mwana mzaliwa-pekee wa Yehova alipolipia ile fidia, na hapa ndipo Yehova atakapotetea ustahili wa enzi yake kuu kupitia Ufalme wake wa Kimesiya. Inafaa kama nini kwamba dunia inaitwa kibago cha Yehova! Huenda mfalme akatumia kibago kama kikanyagio cha kupanda kiti chake kilichoinuka, na baada ya hapo akitumie kupumzisha miguu juu yake.

      4. (a) Kwa nini haiwezekani jengo lolote duniani liwe mahali pa kupumzikia pa Yehova Mungu? (b) Maneno “vitu hivi vyote” yana maana gani, na ni lazima tukate kauli gani juu ya ibada ya Yehova?

      4 Bila shaka, mfalme hafanyi makao yake juu ya kibago chake, wala makao ya Yehova hayako katika dunia hii. Kwani, hata mbingu halisi zilizotandaa sana hazimtoshi! Sembuse jengo la kawaida tu hapa duniani kumtosha Yehova kiasi cha kuweza kuwa nyumba yake. (1 Wafalme 8:27) Kiti cha ufalme cha Yehova na mahali pake pa kupumzikia zimo katika makao ya roho, na hiyo ndiyo maana ya neno “mbingu” lililotumiwa kwenye Isaya 66:1. Mstari unaofuata unaeleza linalomaanishwa hasa: “Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA.” (Isaya 66:2a) Ebu wazia Yehova akinyoosha mkono kwa ishara ya mapana ili kuonyesha “vitu hivi vyote,” maana yake kila kitu mbinguni na duniani. (Isaya 40:26; Ufunuo 10:6) Kwa kuwa yeye ndiye Muumba Mkuu wa ulimwengu mzima, anastahili kufanyiwa mambo mengi kuliko kutoa jengo moja tu liwe lake. Anastahili mengi kuliko kuabudiwa kijuu-juu tu.

      5. Tunaonyeshaje kwamba sisi ni ‘wenye kuteseka na wenye roho iliyopondeka’?

      5 Ni ibada ya aina gani inayomfaa Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Mzima? Yeye mwenyewe anatuambia hivi: “Lakini, mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge [“mwenye kuteseka,” “NW”], mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.” (Isaya 66:2b) Ndiyo, ni muhimu mwabudu awe na mtazamo wa moyoni unaofaa ili ibada yake iweze kuwa safi. (Ufunuo 4:11) Mwabudu wa Yehova ni lazima ‘awe mwenye kuteseka na mwenye roho iliyopondeka.’ Je, inamaanisha kwamba Yehova anataka tukose furaha? La, yeye ndiye “Mungu mwenye furaha,” na anataka waabudu wake wawe na shangwe pia. (1 Timotheo 1:11; Wafilipi 4:4) Hata hivyo, sisi sote hutenda dhambi mara nyingi, na tusizione dhambi zetu kama mchezo tu. Tunapaswa ‘kuteswa’ nazo, kuhuzunika kwamba tumeikosa shabaha ya viwango vya Yehova vya uadilifu. (Zaburi 51:17) Tunahitaji kuonyesha kwamba ‘tuna roho iliyopondeka’ kwa kutubu, kupigana na maelekeo yetu yenye dhambi, na kumtolea Yehova sala ya kuomba msamaha.—Luka 11:4; 1 Yohana 1:8-10.

      6. Ni katika maana gani waabudu wa kweli wanapaswa ‘kutetemeka wasikiapo neno la Mungu’?

      6 Kwa kuongezea, Yehova huwatafuta wale ‘watetemekao wasikiapo neno lake.’ Je, hii inamaanisha kwamba anataka tutikisike kwa hofu kila tunaposikia matamko yake? Sivyo, bali anatutaka tuyaone maneno yake kwa kicho na staha nyingi. Tunatafuta shauri lake kwa moyo mweupe, tukilitumia ili litupe mwongozo katika shughuli zote za maisha. (Zaburi 119:105) Tunaweza pia ‘kutetemeka’ katika maana ya kuhofu tusije tukakosa kumtii Mungu, kuichafua kweli yake kwa mapokeo ya kibinadamu, au kuiona kama mchezo tu. Mtazamo huo wa unyenyekevu ni muhimu katika ibada safi—lakini inahuzunisha kwamba ni watu wachache walio na mtazamo huo katika ulimwengu wa leo.

      Yehova Anachukia Ibada ya Kiunafiki

      7, 8. Yehova anaionaje ibada ya kidesturi ya wanafiki wa kidini?

      7 Wakati Isaya anapotafakari juu ya watu walioishi wakati mmoja naye, anajua sana kwamba ni wachache wenye mwelekeo ambao Yehova huutafuta katika waabudu wake. Kwa sababu hiyo, Yerusalemu lenye uasi-imani linaistahili ile hukumu inayokaribia kulipata. Angalia jinsi Yehova anavyoiona ibada inayoendelea ndani ya jiji hilo: “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.”—Isaya 66:3.

      8 Maneno haya yanatukumbusha maneno ya Yehova yaliyoandikwa katika sura ya kwanza ya Isaya. Hapo Yehova aliwaambia watu wake wapotovu kwamba, licha ya yeye kutopendezwa na vitendo vyao vya kufuata desturi rasmi tu ya ibada, kwa kweli vitendo hivyo vilizidisha pia hasira yake ya uadilifu kwa sababu waabudu hao walikuwa wanafiki. (Isaya 1:11-17) Vivyo hivyo, sasa Yehova anafananisha matoleo yao na vitendo vya uhalifu mbaya sana. Hawawezi kuutuliza moyo wa Yehova kwa kumtolea dhabihu ya ng’ombe dume wa bei kubwa, kama vile tu wasivyoweza kuutuliza kwa kuua binadamu kimakusudi! Dhabihu nyingine zinafananishwa na kutoa toleo la mbwa au nguruwe, wanyama wachafu chini ya Sheria ya Kimusa, tena wasiofaa kamwe kutolewa kama dhabihu. (Mambo ya Walawi 11:7, 27) Je, Yehova anauachilia unafiki huo wa kidini bila kutoa adhabu?

      9. Wayahudi walio wengi wameitikiaje vikumbusha vya Yehova kupitia Isaya, na kutakuwa na matokeo gani yasiyoepukika?

      9 Sasa Yehova anasema hivi: “Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika;na niliponena,hawakusikia; bali walifanyayaliyo maovu machoni pangu, na kuyachagua nisiyoyafurahia.” (Isaya 66:4) Bila shaka Isaya anaweza kuyatamka maneno haya kwa usadikisho wa moyoni. Kwa muda wa miaka mingi amekuwa chombo cha Yehova, huku ‘akiita’ watu Wake na ‘kunena’ nao. Nabii anajua sana kwamba, kwa ujumla hakuna mtu amekuwa akisikiliza. Kwa sababu wameendelea kutenda mabaya, hawawezi kukosa adhabu. Kweli Yehova atachagua adhabu yao na kuwaletea watu wake waasi-imani matukio yenye kutisha.

      10. Shughuli za Yehova na Yuda zinatuonyesha kwamba yeye ana maoni gani kuhusu Jumuiya ya Wakristo?

      10 Vivyo hivyo, Jumuiya ya Wakristo ya kisasa imefanya mambo ambayo Yehova hayafurahii. Ibada ya sanamu inasitawi katika makanisa yake. Falsafa na mapokeo yasiyo ya Kimaandiko yanatukuzwa kwenye vijukwaa vya makanisa. Na jumuiya hiyo imeng’ang’ania kupata mamlaka ya kisiasa, na kwa njia hiyo ikadidimia hata zaidi katika uhusiano wa kuzini na mataifa ya ulimwengu. (Marko 7:13; Ufunuo 18:4, 5, 9) Kama vile ilivyokuwa kwa habari ya Yerusalemu la kale, Jumuiya ya Wakristo itapatwa na kitu cha kutia “hofu,” yaani malipo ya adhabu yaliyo haki yake, ipende isipende. Mojawapo ya sababu zitakazofanya ipate adhabu hakika ni jinsi imewatendea watu wa Mungu.

      11. (a) Ni nini kinachoongezea dhambi ya waasi-imani katika siku za Isaya? (b) Watu wanaoishi wakati mmoja na Isaya wanawatupaje waaminifu ‘kwa ajili ya jina la Mungu’?

      11 Isaya anaendelea kusema hivi: “Lisikilizeni neno la BWANA, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe BWANA, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.” (Isaya 66:5) “Ndugu” za Isaya, ambao ni wananchi wenzake hasa, ndio wanaopaswa kubeba daraka walilopewa na Mungu la kumwakilisha Yehova Mungu na kutii enzi yake kuu. Wameshindwa kufanya hivyo wakawa na dhambi nzito kweli kweli. Lakini kinachoongezea dhambi yao ni kwamba wanawachukia wanaume walio waaminifu na wanyenyekevu, kama vile Isaya. Waasi-imani hao wanawachukia waaminifu na kuwatupa kwa sababu wanamwakilisha Yehova Mungu kwa njia ya kweli. Ni katika maana hiyo kwamba waaminifu hao wanatupwa ‘kwa ajili ya jina la Mungu.’ Wakati huo huo, watumishi hawa wa Yehova wasio wa kweli wanadai kumwakilisha, wakijifanya eti wanamcha Mungu sana kwa kutumia maneno yanayosikika kama ya kidini, kama vile ‘Yehova na atukuzwe!’a

      12. Ni baadhi ya mifano gani inayoonyesha jinsi wanafiki wa kidini wanavyonyanyasa watumishi waaminifu wa Yehova?

      12 Chuki ambayo dini ya uwongo inayo kuelekea wale wanaoshikamana na ibada safi haikuanza sasa hivi. Chuki hiyo inazidi tu kutimiza unabii ulio kwenye Mwanzo 3:15, uliotabiri uadui wa muda mrefu kati ya mbegu ya Shetani na Mbegu ya mwanamke wa Mungu. Yesu aliwaambia wafuasi wake watiwa-mafuta katika karne ya kwanza kwamba wao pia wangeteseka mikononi mwa wananchi wenzao—watupwe nje ya masinagogi na kunyanyaswa hadi kifo. (Yohana 16:2) Namna gani nyakati za kisasa? “Siku za mwisho” zilipokuwa zikianza, watu wa Mungu waliona kwamba mnyanyaso kama huo ungetokea siku za usoni. (2 Timotheo 3:1) Huko nyuma mwaka wa 1914, gazeti Mnara wa Mlinzi lilinukuu Isaya 66:5, likisema hivi: “Karibu minyanyaso yote ambayo imewapata watu wa Mungu imetoka kwa watu wanaodai eti ni Wakristo.” Makala hiyo hiyo ilisema hivi: “Hatujui watafika wapi na mambo hayo, kwani huenda hata wakaruka mipaka katika siku zetu—kutuangamiza katika mambo ya kijamii, kutuangamiza kidini, na labda hata kutuangamiza kimwili.” Maneno hayo yalikuwa kweli kama nini! Muda mfupi baada ya maneno hayo kuchapishwa, mnyanyaso wenye kuchochewa na makasisi uliwaka kweli kweli wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Lakini Jumuiya ya Wakristo ikaaibishwa, kama ilivyotabiriwa. Jinsi gani?

      Kurudishwa Upesi Sana na kwa Ghafula

      13. “Sauti ya fujo” ni nini katika utimizo wa kwanza?

      13 Isaya anatoa unabii hivi: “Sauti ya fujo itokayo mjini! Sauti itokayo hekaluni! Sauti ya BWANA awalipaye adui zake adhabu!” (Isaya 66:6) Katika utimizo wa kwanza wa maneno hayo, ‘mji’ ni Yerusalemu, ambamo mna hekalu la Yehova. “Sauti ya fujo” inaleta wazo la msukosuko wa vita, unaosikiwa katika jiji wakati majeshi ya Babiloni yanapovamia mji huo na kuushambulia mwaka wa 607 K.W.K. Namna gani utimizo wa kisasa?

      14. (a) Malaki alitabiri nini kuhusu kuja kwa Yehova kwenye hekalu Lake? (b) Kulingana na unabii wa Ezekieli, matokeo yalikuwa nini Yehova alipokuja kwenye hekalu lake? (c) Yehova na Yesu walilichunguza hekalu la kiroho wakati gani, na matokeo yakawa nini kwa wenye kudai eti wanawakilisha ibada safi?

      14 Maneno haya katika Isaya yanapatana na matamko mengine mawili ya kiunabii. Tamko moja ni lile lililoandikwa kwenye Ezekieli 43:4, 6-9 na lile jingine liko kwenye Malaki 3:1-5. Ezekieli na hata Malaki wanautabiri wakati ambao Yehova Mungu anakuja kwenye hekalu lake. Unabii wa Malaki unaonyesha kwamba Yehova anakuja kuchunguza nyumba yake ya ibada safi na kutenda kama Mtakasaji, akiwakataa wale wanaomwakilisha vibaya. Njozi ya Ezekieli inaonyesha Yehova akiingia katika hekalu na kudai kwamba alama zote za ukosefu wa adili na za ibada ya sanamu ziondolewe.b Katika utimizo wa kisasa wa unabii huo mbalimbali, jambo muhimu la kiroho lilitokea mwaka wa 1918 kuhusiana na ibada ya Yehova. Ushuhuda unaonyesha kwamba Yehova na Yesu waliwachunguza wale wote wale waliodai kuwakilisha ibada safi. Matokeo ya uchunguzi huo ni kwamba, mwishowe Jumuiya ya Wakristo yenye ufisadi ilitupiliwa mbali. Uchunguzi huo ulitokeza kipindi kifupi cha kuwatakasa watiwa-mafuta wa Kristo, kisha wakarudishiwa upesi sana hali nzuri ya kiroho mwaka wa 1919.—1 Petro 4:17.

      15. Ni uzazi gani unaotabiriwa, na unatimizwaje mwaka wa 537 K.W.K.?

      15 Hali hiyo ya kurudishwa inaonyeshwa kwa kufaa sana katika mistari ifuatayo ya Isaya: “Kabla hajaona utungu alizaa; kabla maumivu yake hayajampata, alizaa mtoto mwanamume. Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipoona utungu, alizaa watoto wake.” (Isaya 66:7, 8) Maneno haya yanatimizwa mara ya kwanza kwa njia ya kusisimua kuhusiana na Wayahudi wahamishwa walioko Babiloni. Sayuni, au Yerusalemu, anaonyeshwa tena kuwa mwanamke anayezaa. Lakini huo ni uzazi wa kushangaza kama nini! Unafanyika upesi sana, ghafula sana, hata kabla ya utungu kuanza! Maelezo ya tukio hilo yanafaa sana. Kuzaliwa kwa watu wa Mungu mwaka wa 537 K.W.K. wakiwa taifa la kipekee kunatukia upesi sana, ghafula sana, hivi kwamba kunaonekana kama mwujiza. Kwani, muda unaopita kuanzia wakati ambao Koreshi anawaweka huru Wayahudi watoke utekwani hadi wakati ambao mabaki waaminifu wanakuwa wamerudia nchi yao, ni miezi michache tu! Hali hiyo inatofautiana kama nini na matukio yaliyotangulia kuzaliwa kwa taifa la Israeli mara ya kwanza! Mwaka wa 537 K.W.K., hakuna haja ya kumwomba mtawala mpinzani atoe uhuru wa kuondoka, hakuna haja ya kukimbia jeshi lenye uadui, hakuna haja ya kukaa-kaa jangwani muda wa miaka 40.

      16. Katika utimizo wa kisasa wa Isaya 66:7, 8, Sayuni inafananisha nini, na wazao wake wamezaliwaje upya?

      16 Katika utimizo wa kisasa, Sayuni inawakilisha “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova, yaani tengenezo lake la kimbingu la viumbe-roho. Mwaka wa 1919 “mwanamke” huyu alishangilia kuona kuzaliwa kwa wana wake watiwa-mafuta duniani ili wawe watu waliopangwa kitengenezo, maana yake “taifa.” Tukio hilo la kuzaliwa upya lilifanyika upesi sana, tena kwa ghafula.c Katika muda wa miezi michache tu, watiwa-mafuta wakiwa kikundi walitoka katika hali ya kutotenda iliyo kama kifo, wakaanza maisha ya utendaji wa kujibidiisha sana katika “nchi” yao, yale makao yao ya utendaji wa kiroho waliyopewa na Mungu. (Ufunuo 11:8-12) Kufikia miezi ya mwishoni mwa mwaka wa 1919, hata walitangaza kuchapishwa kwa gazeti jipya la kukamilishana na Mnara wa Mlinzi. Kichapo hicho kipya kiliitwa The Golden Age (sasa Amkeni!), na kilikuwa ushuhuda wa kwamba watu wa Mungu wametiwa nguvu mpya, wakiwa wamepangwa tena kuwa tengenezo kwa ajili ya utumishi.

      17. Yehova anawahakikishiaje watu wake kwamba hakuna cha kumzuia asitimize kusudi lake kuhusiana na Israeli wa kiroho?

      17 Katika ulimwengu mzima hakuna nguvu yoyote ambayo ingeweza kuzuia uzaliwa huo mpya. Mstari unaofuata unasema lilo hilo: “Je! mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? asema BWANA; mimi nizalishaye, je! nilifunge tumbo? asema Mungu wako.” (Isaya 66:9) Sawa na vile hatua za kuzaa mtoto zisivyoweza kuepukwa zikiisha kuanza, ndivyo kuzaliwa upya kwa Israeli wa kiroho hakungeweza kuzuiliwa baada ya kuanza. Ni kweli kwamba upinzani ulikuwako, na yaelekea kwamba kutakuwako upinzani zaidi wakati ujao. Lakini ni Yehova peke yake aliye na uwezo wa kukomesha kitu anachokianzisha. Hata hivyo, yeye hafanyi hivyo kamwe! Ingawa hivyo, Yehova anawatendeaje watu wake waliotiwa nguvu mpya?

      Utunzaji Mwororo wa Yehova

      18, 19. (a) Yehova anatumia mfano gani wenye kugusa moyo, nao unatumikaje kuwahusu watu wake walio uhamishoni? (b) Leo mabaki watiwa-mafuta wamefaidikaje na lishe na utunzaji wenye upendo?

      18 Mistari minne inayofuata inaufafanua utunzaji mwororo wa Yehova kwa njia ya kuvutia. Kwanza, Isaya anasema hivi: “Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake.” (Isaya 66:10, 11) Hapa Yehova anatumia mfano wa mwanamke anayenyonyesha kitoto chake kichanga. Mtoto mchanga anapoumwa na njaa, kazi yake ni kulia-lia tu. Lakini anapoletwa karibu na matiti ya mama yake anyonye, sasa yeye huacha kihoro chake na kutosheka akiwa na furaha kamili. Vivyo hivyo, mabaki ya Wayahudi waaminifu walioko Babiloni watatolewa haraka haraka katika hali ya kuomboleza waingie katika hali ya furaha na uradhi ufikapo wakati wao wa kukombolewa na kurudishwa. Watakuwa na shangwe. Yerusalemu litapewa utukufu tena, huku likijengwa upya na kukaliwa upya. Na utukufu wa jiji hilo utaenea uangaze juu ya wakaaji wake wote waaminifu. Kwa mara nyingine, watalishwa kiroho kupitia ukuhani wenye utendaji wa bidii.—Ezekieli 44:15, 23.

      19 Israeli wa kiroho pia alibarikiwa kwa lishe tele baada ya kurudishwa mwaka wa 1919. Tangu wakati huo, chakula cha kiroho kinachotolewa kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kimekuwa kikitiririka kwa ukawaida. (Mathayo 24:45-47) Kweli huu umekuwa wakati wa faraja na shangwe kwa mabaki watiwa-mafuta. Lakini kumekuwako na baraka nyingine nyingi.

      20. Yerusalemu limebarikiwaje kwa “kijito kifurikacho,” nyakati za kale na za kisasa pia?

      20 Unabii unaendelea kusema hivi: “BWANA asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa [“ubavuni,” “NW”]; na juu ya magoti mtabembelezwa.” (Isaya 66:12) Hapa mfano wa kunyonyesha umeunganishwa na wazo la mtiririko wa baraka nyingi, yaani “mto” na “kijito kifurikacho.” Licha ya kubarikiwa kwa amani tele kutoka kwa Yehova, Yerusalemu litabarikiwa pia kwa “utukufu wa mataifa,” unaowatiririkia watu wa Mungu na kuwabariki. Hii inamaanisha kwamba watu wa mataifa watafurika kuwaendea watu wa Yehova. (Hagai 2:7) Katika utimizo wa kale, ni kweli kwamba watu kadhaa wa mataifa mbalimbali walijiunga na Israeli wakawa waongofu Wayahudi. Hata hivyo, utimizo mkubwa zaidi umetukia wakati wetu wenyewe ambapo “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha”—ambao kwa kweli ni miminiko kubwa sana la wanadamu—wamejiunga na mabaki ya Wayahudi wa kiroho.—Ufunuo 7:9; Zekaria 8:23.

      21. Ni faraja ya aina gani inayotabiriwa kwa maneno ya ufananisho yenye kuvutia?

      21 Andiko la Isaya 66:12 pia linataja semi zitumiwazo na mama-mzazi kuonyesha upendo. Semi hizo zinahusu kubembeleza mtoto kwa kumpakata magotini na kumbeba kwa kumweka ubavuni. Katika mstari unaofuata, wazo la namna hiyo linaelezwa kwa maoni tofauti yanayostahili kufikiriwa. “Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu.” (Isaya 66:13) Sasa mtoto huyo ni “mtu,” mtu mzima. Lakini mama yake hajaacha kutamani kumfariji wakati wa msononeko.

      22. Yehova anaonyeshaje wororo na uthabiti wa upendo wake?

      22 Kwa njia hiyo ya kuvutia, Yehova anaonyesha jinsi anavyowapenda watu wake kwa uthabiti na wororo mwingi. Hata upendo imara kabisa wa mama-mzazi unakuwa kitu kidogo sana unapolinganishwa na upendo wa kina kirefu ambao Yehova huwaonyesha watu wake waaminifu. (Isaya 49:15) Ni muhimu kama nini Wakristo wote waonyeshe sifa hiyo ya Baba yao wa kimbingu! Mtume Paulo aliionyesha, na hivyo akawaachia wazee wa kutaniko la Kikristo mfano mzuri. (1 Wathesalonike 2:7) Yesu alisema kwamba upendo wa kidugu ndio ungekuwa alama kuu ya kutambulisha wafuasi wake.—Yohana 13:34, 35.

      23. Simulia hali yenye furaha ya watu wa Yehova waliorudishwa.

      23 Yehova huonyesha upendo wake kwa matendo. Hivyo, yeye anaendelea kusema hivi: “Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa BWANA utajulikana, uwaelekeao watumishi wake, naye atawaonea adui zake ghadhabu.” (Isaya 66:14) Mtaalamu fulani wa sarufi ya Kiebrania anadokeza kwamba usemi “nanyi mtaona” una wazo la kwamba popote pale ambapo wahamishwa wanaorudi wanatazama katika nchi yao iliyorudishwa, “sasa macho yao yanaona shangwe tupu.” Watashangilia vilivyo, wasisimuke hata midomo ibaki wazi kwa kuona kwamba wamerudishwa kwenye nchi yao kipenzi. Watahisi kurudishiwa nguvu za ujana, kana kwamba mifupa yao imeanza kuimarika tena, wapate nguvu mpya kama nyasi wakati wa masika. Watu wote watajua kwamba hali hii yenye baraka haikutokea kwa jitihada ya mwanadamu yeyote, bali kwamba imesababishwa na ‘mkono wa Yehova.’

      24. (a) Wewe unakata kauli gani unapoyafikiria matukio yanayowahusu watu wa Yehova leo? (b) Tunapaswa kufanya azimio gani?

      24 Je, wewe unatambua wakati mkono wa Yehova unapofanya kazi miongoni mwa watu wake leo? Hakuna mwanadamu yeyote yule ambaye angaliweza kuirudisha ibada safi. Hakuna mwanadamu angaliweza hata kidogo kusababisha mamilioni ya watu wa thamani kubwa wamiminike kutoka katika mataifa yote kujiunga na mabaki waaminifu katika nchi yao ya kiroho. Ni Yehova Mungu peke yake awezaye kufanya hayo. Maonyesho hayo ya upendo wa Yehova yanatupa sisi sababu ya kuwa na shangwe nyingi sana. Tusithubutu kamwe kuuchezea-chezea upendo wa Yehova. Na tuendelee ‘kutetemeka tusikiapo neno lake.’ Na tuazimie kuishi kwa kufuata kanuni za Biblia na kufurahia kumtumikia Yehova.

      [Maelezo ya Chini]

      a Leo watu wengi katika Jumuiya ya Wakristo wanakataa kulitumia jina la Mungu la kibinafsi, na hata wanaliondoa katika tafsiri nyingi sana za Biblia. Wengine huwadhihaki vikali watu wa Mungu kwa sababu wanatumia jina lake la kibinafsi. Na bado, watu mmoja-mmoja kati yao hujionyesha kuwa wanadini wanaomcha Mungu kwa kutumia neno “Haleluya,” maana yake “Sifuni Yah.”

      b Usemi “mizoga ya wafalme wao,” uliotumiwa kwenye Ezekieli 43:7, 9, humaanisha sanamu. Viongozi na watu wa Yerusalemu walio waasi walikuwa wamelichafua hekalu la Mungu kwa sanamu na, kwa njia hiyo wakazifanya kuwa wafalme.

      c Uzaliwa unaotajwa hapa kwa njia ya unabii sio ule ule unaoelezwa kwenye Ufunuo 12:1, 2, 5. Katika sura hiyo ya Ufunuo, “mwana, wa kiume,” anafananisha Ufalme wa Kimesiya, ulioanza kazi mwaka wa 1914. Hata hivyo, “mwanamke” wa unabii anayetajwa katika maandiko hayo mawili ni yule yule.

      [Picha katika ukurasa wa 395]

      “Mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote”

      [Picha katika ukurasa wa 402]

      Yehova ataelekezea Sayuni “utukufu wa mataifa”

  • Nuru kwa Mataifa
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sura Ya Ishirini Na Nane

      Nuru kwa Mataifa

      Isaya 66:15-24

      1, 2. Kwa nini nuru ni muhimu, na leo ni giza la namna gani linaloifunika dunia?

      YEHOVA ndiye Chanzo cha nuru, yule “awapaye watu jua, ili kuwa nuru wakati wa mchana, na amri za mwezi na nyota, ili kuwa nuru wakati wa usiku.” (Yeremia 31:35) Sababu hiyo peke yake inatosha kufanya Yehova astahili kutambuliwa kuwa ndiye Chanzo cha uhai, kwani hakuna uhai bila nuru. Kama dunia haingepashwa joto na nuru ya jua daima, haingewezekana tuendelee kuwa hai. Sayari yetu dunia ingekuwa isiyokalika.

      2 Kwa hiyo, inatupasa tuhangaishwe sana na wazo la kwamba, Yehova alipotazama mbele kwenye siku zetu, alitabiri wakati wa giza wala si wa nuru. Isaya alipuliziwa kuandika hivi: “Tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu.” (Isaya 60:2) Bila shaka, maneno hayo yalihusiana na giza la kiroho, wala si giza halisi, lakini yana uzito usiopasa kupuuzwa. Hatimaye, inakuwa haiwezekani kwa wale wasio na nuru ya kiroho kuendelea kuwa hai, sawa na vile inavyokuwa kwa wale wasioweza kupata nuru ya jua.

      3. Tunaweza kupata nuru wapi nyakati hizi za giza?

      3 Nyakati hizi za giza, tusithubutu kamwe kuipuuza nuru ya kiroho ambayo Yehova ametupatia leo. Ni muhimu tutegemee Neno la Mungu ili lituangazie njia yetu, tukiisoma Biblia kila siku ikiwezekana. (Zaburi 119:105) Mikutano ya Kikristo inatuandalia nafasi za kutiana moyo ili tubaki katika “njia ya wenye haki.” (Mithali 4:18; Waebrania 10:23-25) Nguvu tunazopata kwa kujifunza Biblia na kutokana na ushirika mzuri wa Kikristo hutusaidia tuepuke kupotelea ndani ya giza la hizi “siku za mwisho,” ambalo litafikia upeo katika ‘siku ya hasira ya Yehova.’ (2 Timotheo 3:1; Sefania 2:3) Siku hiyo inakuja mbio-mbio! Hakika itakuja, sawasawa na vile siku nyingine kama hiyo ilivyowajilia wakaaji wa Yerusalemu la kale.

      Yehova ‘Ateta’

      4, 5. (a) Yehova anavamia Yerusalemu jinsi gani? (b) Kwa nini tunaweza kukata kauli kwamba ni idadi ndogo tu kwa kulinganishwa ambayo itauokoka uharibifu wa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K.? (Ona kielezi-chini.)

      4 Katika mistari ile inayoumalizia unabii wa Isaya wenye kusisimua, Yehova anatoa maelezo dhahiri sana kuhusu matukio yatakayoelekeza kwenye siku ya hasira yake. Tunasoma hivi: “BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto. Kwa maana BWANA atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na BWANA watakuwa wengi.”—Isaya 66:15, 16.

      5 Maneno hayo yanapasa kuwasaidia watu wa siku za Isaya wautambue uzito wa hali yao. Wakati unakaribia ambapo Wababiloni wenye kuleta hukumu ya Yehova watavamia Yerusalemu, huku magari yao ya kivita yakitifua vumbi kwa fujo kana kwamba ni upepo wa kisulisuli. Hicho kitakuwa kivumbi cha kutisha wee! Yehova atatumia wavamizi hao kutimiza hukumu zake mwenyewe zilizo motomoto juu ya Wayahudi “wote wenye mwili” wasio waaminifu. Itakuwa kana kwamba Yehova mwenyewe anapigana na watu wake. “Ghadhabu” yake haitarudi nyuma. Wayahudi wengi wataanguka wakiwa ‘wameuawa na Yehova.’ Mwaka wa 607 K.W.K., unabii huo unatimizwa.a

      6. Ni mazoea gani yenye hatia yanayotukia katika Yuda?

      6 Je, Yehova ana haki ya ‘kuteta’ kwa kuwapinga watu wake? Tena sana! Katika mazungumzo yetu ya kitabu cha Isaya, tumeona mara nyingi kwamba Wayahudi wameingilia sana ibada ya uwongo, huku ikidhaniwa kwamba eti wamejiweka wakfu kwa Yehova. Na Yehova hajawa kipofu muda huo, asiweze kuyaona matendo yao. Tunaona hivyo tena katika maneno yafuatayo ya unabii: “Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA.” (Isaya 66:17) Je, Wayahudi hao ‘wanajitakasa na kujisafisha’ ili wajitayarishe kwa ajili ya ibada safi? La, hasha. Badala ya hivyo, wanajihusisha katika desturi za utakaso wa kipagani katika bustani za pekee. Kisha wanakula kwa pupa nyama ya nguruwe na viumbe wengine walioonwa kuwa wachafu chini ya Sheria ya Kimusa.—Mambo ya Walawi 11:7, 21-23.

      7. Jumuiya ya Wakristo inafananaje na Yuda yenye kuabudu sanamu?

      7 Ni chukizo kama nini kwamba jambo hilo linatendwa na taifa lililo katika uhusiano wa agano pamoja na yule Mungu wa pekee wa kweli! Lakini ebu fikiri: Leo kuna hali ya kuchukiza jinsi hiyo katika dini za Jumuiya ya Wakristo. Dini hizo pia hudai kwamba zinamtumikia Mungu, na wengi wa viongozi wake hujifanya eti wanamcha Mungu sana. Hata hivyo, wanajitia unajisi kwa mafundisho na mapokeo ya kipagani, jambo linalothibitisha kuwa wamo katika giza la kiroho. Giza tititi!—Mathayo 6:23; Yohana 3:19, 20.

      “Watauona Utukufu Wangu”

      8. (a) Yuda na hata Jumuiya ya Wakristo zitapatwa na jambo gani? (b) Mataifa ‘yatauona utukufu wa Yehova’ jinsi gani?

      8 Je, Yehova anaziona hatia za Jumuiya ya Wakristo na mafundisho yake ya uwongo? Ebu yasome maneno ya Yehova yafuatayo, kama yalivyoandikwa na Isaya, uone utakata kauli gani: “Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu.” (Isaya 66:18) Licha ya kujua na kuwa tayari kuhukumu matendo ya wale wanaodai kuwa watumishi wake, anayajua hata mawazo yao na atayahukumu hayo pia. Yuda anadai kuwa anamwamini Yehova, lakini matendo yake ya kuabudu sanamu na mazoea ya kipagani yanakanusha dai lake. Raia zake ‘wanajitakasa’ bure kulingana na desturi za kipagani. Taifa hilo litafyekwa, tena peupe mbele ya jirani zake wanaoabudu sanamu. Majirani hao ‘watauona utukufu wa Yehova’ kwa maana ya kwamba watashuhudia matukio hayo kwa macho yao wenyewe na kulazimika kukubali kwamba neno la Yehova limetimia. Yote hayo yanatumikaje kuhusu Jumuiya ya Wakristo? Wakati jumuiya hiyo itakapofikia mwisho wake, wengi wa wale waliokuwa rafiki zake na waliofanya biashara pamoja naye watalazimika kusimama kando tu na kutazama wakiwa hoi wakati neno la Yehova linapotimizwa.—Yeremia 25:31-33; Ufunuo 17:15-18; 18:9-19.

      9. Yehova anatangaza habari njema zipi?

      9 Je, kuharibiwa kwa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K. kunamaanisha kwamba Yehova hatakuwa tena na mashahidi duniani? Sivyo. Watu walio na uaminifu-maadili wenye kutokeza, kama vile Danieli na waandamani wake watatu, wataendelea kumtumikia Yehova hata wakiwa wahamishwa Babiloni. (Danieli 1:6, 7) Naam, ule mfuatano wa mashahidi wengi waaminifu wa Yehova utabaki hivyo hivyo, na mwishoni mwa miaka 70, wanaume na wanawake waaminifu wataondoka Babiloni kurudi Yuda ili kuirudisha ibada safi huko. Hilo ndilo jambo ambalo sasa Yehova anagusia: “Nami nitaweka ishara kati yao, nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na Yavani, visiwa vilivyo mbali; watu wasioisikia habari yangu, wala kuuona utukufu wangu; nao watahubiri utukufu wangu katika mataifa.”—Isaya 66:19.

      10. (a) Wayahudi waaminifu waliokombolewa Babiloni watakuwaje ishara? (b) Ni nani leo wanaokuwa ishara?

      10 Kundi la wanaume na wanawake waaminifu wanaorudi Yerusalemu mwaka wa 537 K.W.K. litatumika likiwa ishara ya kugutusha, ushuhuda wa kwamba Yehova amewakomboa watu wake. Ni nani angaliwaza kwamba siku moja Wayahudi mateka wangekuwa huru ili kufuatia ibada safi kwenye hekalu la Yehova? Hali kadhalika, katika karne ya kwanza Wakristo watiwa-mafuta ndio waliokuwa “ishara na ajabu,” nao walimiminikiwa na watu watiifu waliotaka kumtumikia Yehova. (Isaya 8:18; Waebrania 2:13) Leo Wakristo watiwa-mafuta, wanaopata ufanisi katika nchi yao iliyorudishiwa hali nzuri, wanakuwa kama ishara ya kugutusha duniani. (Isaya 66:8) Wao ni ushuhuda halisi wa kuonyesha kwamba roho ya Yehova ina nguvu za kuvuta watu watiifu wanaosukumwa na mioyo yao kumtumikia Yehova.

      11. (a) Baada ya kurudishwa, itakuwaje kwamba watu wa mataifa watakuja kujifunza habari za Yehova? (b) Andiko la Zekaria 8:23 lilitimizwaje mara ya kwanza?

      11 Lakini, baada ya kurudishwa mwaka wa 537 K.W.K., watu wa mataifa ambao hawajawahi kuisikia habari za Yehova watamjuaje? Si Wayahudi wote waaminifu watakaorudi Yerusalemu mwishoni mwa utekwa wa Kibabiloni. Wengine, kama vile Danieli, watabaki Babiloni. Na wengine zaidi watatawanyika hadi pembe nne za dunia. Kufikia karne ya tano K.W.K., sehemu zote za Milki ya Uajemi zilikuwa na Wayahudi. (Esta 1:1; 3:8) Bila shaka wengine wao waliwaeleza majirani zao wapagani habari za Yehova, kwa maana wengi kutoka mataifa hayo walikuja kuwa waongofu Wayahudi. Inaonekana hata yule towashi Mwethiopia aliyehubiriwa na Filipo mwanafunzi Mkristo katika karne ya kwanza alikuwa mwongofu. (Matendo 8:26-40) Yote hayo yalitukia yakiwa utimizo wa kwanza wa maneno ya nabii Zekaria: “Siku hizo watu kumi, wa lugha zote za mataifa, wataushika upindo wa nguo yake yeye aliye Myahudi; naam, wataushika wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.” (Zekaria 8:23) Kwa kweli, Yehova aliyapelekea mataifa nuru!—Zaburi 43:3.

      ‘Kumletea Yehova Zawadi’

      12, 13. Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K., “ndugu” wataletwa Yerusalemu kwa njia gani?

      12 Baada ya Yerusalemu kujengwa upya, Wayahudi waliotawanyika mbali sana na nchi yao wataelekeza fikira na mtazamo wao kwenye jiji hilo pamoja na ukuhani wake uliorudishwa likiwa kituo cha ibada safi. Wengi wao watasafiri mbali kuhudhuria sherehe za kila mwaka huko. Isaya anaandika hivi kwa kupuliziwa: “Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka [“zawadi,” “NW”] kwa BWANA, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema BWANA; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka [“zawadi,” “NW”] yao nyumbani kwa BWANA katika chombo safi. Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi.”—Isaya 66:20, 21.

      13 Wengine wa hao ‘ndugu kutoka mataifa yote’ walikuwako siku ya Pentekoste wakati roho takatifu ilipomiminwa juu ya wanafunzi wa Yesu. Masimulizi hayo yanasema hivi: “Kulikuwa na Wayahudi wakikaa katika Yerusalemu, wanaume wenye kumhofu Mungu, kutoka kila taifa la yale yaliyo chini ya mbingu.” (Matendo 2:5) Walikuja Yerusalemu kuabudu kulingana na desturi ya Kiyahudi, lakini walipozisikia habari njema juu ya Yesu Kristo, wengi walionyesha wazi kwamba wanamwamini kisha wakabatizwa.

      14, 15. (a) Wakristo watiwa-mafuta waliwakusanyaje wengi wa “ndugu” zao wa kiroho baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, nao waliletwaje kwa Yehova wakiwa ‘zawadi katika chombo safi’? (b) Yehova ‘alitwaa baadhi ya hao kuwa makuhani’ jinsi gani? (c) Ni akina nani waliokuwa baadhi ya Wakristo watiwa-mafuta waliohusika katika kukusanya ndugu zao wa kiroho? (Ona sanduku katika ukurasa huu.)

      14 Je, unabii huu una utimizo wa kisasa? Tena sana. Baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, watumishi watiwa-mafuta wa Yehova walitambua kutokana na Maandiko kwamba Ufalme wa Mungu ulikuwa umeanzishwa mbinguni mwaka wa 1914. Kupitia funzo la uangalifu la Biblia, walijifunza kwamba warithi wa ziada wa Ufalme, au akina “ndugu,” walipasa kukusanywa. Wahudumu hodari walisafiri “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia,” wakitumia usafiri wa kila namna ili kuwatafuta wale waliotazamiwa kuwa washirika wa mabaki-watiwa mafuta, wengi wao wakitoka kwenye makanisa ya Jumuiya ya Wakristo. Walipopatikana, waliletwa wawe zawadi kwa Yehova.—Matendo 1:8.

      15 Watiwa-mafuta waliokusanywa miaka ya mapema hawakumtazamia Yehova awakubali wakiwa na hali waliyokuwa nayo kabla ya kuujua ukweli wa Biblia. Walichukua hatua za kujisafisha uchafu wa kiroho na wa kiadili ili waweze kutolewa wawe ‘zawadi katika chombo safi,’ au kama ilivyotajwa na mtume Paulo, wawe “bikira safi kiadili kwa Kristo.” (2 Wakorintho 11:2) Zaidi ya kukataa kosa la kimafundisho, watiwa-mafuta walilazimika kujifunza jinsi ya kudumisha msimamo wa kutokuwamo kabisa katika mambo ya kisiasa ya ulimwengu huu. Mwaka wa 1931, watumishi wake walipokuwa wamesafishwa kwa kiasi kinachofaa, Yehova aliwaonyesha neema kwa kuwapa pendeleo la kubeba jina lake wakiwa Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10-12) Ingawa hivyo, Yehova ‘aliwatwaa baadhi yao kuwa makuhani’ jinsi gani? Wakiwa kikundi, watiwa-mafuta hawa wanakuwa sehemu ya “ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,” wakimtolea Mungu dhabihu za sifa.—1 Petro 2:9; Isaya 54:1; Waebrania 13:15.

      Ukusanyaji Waendelea

      16, 17. Ni nani wale wanaoitwa “uzao wenu” baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu?

      16 Idadi kamili ya huo “ukuhani wa kifalme” ni 144,000, na baada ya muda, kazi ya kuwakusanya ilimalizika. (Ufunuo 7:1-8; 14:1) Je, huo ulikuwa mwisho wa kazi ya kukusanya? Sivyo. Unabii wa Isaya unaendelea kusema hivi: “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema BWANA, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.” (Isaya 66:22) Katika utimizo wa kwanza wa maneno hayo, Wayahudi wanaorudi kutoka kwenye utekwa wa Babiloni wataanza kulea watoto. Kwa njia hiyo, mabaki ya Wayahudi waliorudishwa, yaani ile “dunia mpya,” wakiwa chini ya usimamizi mpya wa Kiyahudi, yaani “mbingu mpya,” wataimarika sana. Hata hivyo, unabii huo umekuwa na utimizo wenye kutokeza sana katika siku zetu.

      17 “Uzao” ambao taifa la ndugu za kiroho wanautokeza ni “umati mkubwa,” walio na tumaini la uhai wa milele duniani. Wao ‘hutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha,’ na husimama “mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” “Wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 7:9-14; 22:17) Leo wale walio “umati mkubwa” wanaepuka giza la kiroho na kuja kwenye nuru ambayo Yehova huandaa. Wanaonyesha imani katika Yesu Kristo, na wanajitahidi kubaki wakiwa safi kiroho na kiadili kama ndugu na dada zao watiwa-mafuta. Wakiwa kikundi, wanaendelea kutumikia chini ya mwelekezo wa Kristo na ‘watakaa’ milele!—Zaburi 37:11, 29.

      18. (a) Washirika wa umati mkubwa wameenenda kama ndugu zao watiwa-mafuta jinsi gani? (b) Watiwa-mafuta na waandamani wao humwabudu Yehova “mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato” jinsi gani?

      18 Wanaume na wanawake hawa wenye bidii walio na tumaini la kidunia wanajua kwamba ingawa ni muhimu kubaki safi kiadili na kiroho, mengi zaidi yanahusika ili kumfurahisha Yehova. Kazi ya ukusanyaji inavuma, nao wanataka kuishiriki. Kitabu cha Ufunuo kinatoa unabii huu kuwahusu: “Wako mbele ya hicho kiti cha ufalme cha Mungu; nao wanamtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.” (Ufunuo 7:15) Maneno hayo yanatukumbusha mstari wa pili kutoka mwisho wa unabii wa Isaya: “Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema BWANA.” (Isaya 66:23) Jambo hilo linatendeka leo. “Mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato,” yaani, kwa ukawaida, kila juma la kila mwezi, Wakristo watiwa-mafuta na waandamani wao, yaani ule umati mkubwa, hukutanika kumwabudu Yehova. Njia mojawapo ambayo wanafanya hivyo ni kuhudhuria mikutano ya Kikristo na kushiriki katika huduma ya peupe. Je, wewe ni mmoja wa wale ‘wanaokuja kuabudu mbele za Yehova’? Watu wa Yehova wanapata shangwe kubwa wanapofanya hivyo, na wale wa umati mkubwa wanautazamia wakati ambao “wanadamu wote,” watamtumikia Yehova “mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato” kwa umilele wote.

      Mwisho Kamili wa Adui za Mungu

      19, 20. Gehena ilitumika kwa kusudi gani nyakati za Biblia, na inafananisha nini?

      19 Mstari mmoja unabaki katika funzo letu la unabii wa Isaya. Kitabu kinafikia mwisho kwa kusema hivi: “Watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.” (Isaya 66:24) Inaelekea kwamba Yesu Kristo alikuwa akiufikiria unabii huu alipowahimiza wanafunzi wake kurahisisha maisha yao na kuweka masilahi ya Ufalme kwanza. Alisema hivi: “Ikiwa jicho lako lakufanya ukwazike, litupilie mbali; ni bora zaidi kwako kuingia katika ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa ndani ya Gehena ukiwa na macho mawili, mahali ambapo funza wao hafi na ule moto hauzimwi.”—Marko 9:47, 48; Mathayo 5:29, 30; 6:33.

      20 Ni mahali gani hapa panapoitwa Gehena? Karne nyingi zilizopita, msomi Myahudi David Kimhi aliandika hivi: “Hapo ni mahali . . . ambapo pamepakana na Yerusalemu, tena ni mahali pa kuchukiza sana, na watu hutupa humo vitu vichafu na mizoga. Vilevile, humo mlikuwa na moto ulioendelea kuwaka ili kuchoma vitu vichafu na mifupa ya mizoga. Kwa hiyo, hukumu ya waovu huitwa Gehinnom kwa njia ya mfano.” Ikiwa, kama vile msomi huyu Myahudi anavyodokeza, Gehena ilitumiwa kama mahali pa kutupia takataka na mizoga ya wale walioonwa hawastahili kuzikwa, basi moto ungekuwa kitu kinachofaa cha kumaliza takataka hizo. Kisichoteketezwa na moto, kingeliwa na funza. Hiyo inaonyesha vizuri kama nini mwisho kamili utakaowapata adui za Mungu!b

      21. Kitabu cha Isaya kinafikia mwisho mzuri kuhusiana na akina nani, na kwa nini?

      21 Kwa sababu ya kutaja maiti, moto, na funza, je, si kweli kwamba unabii wenye kusisimua wa Isaya unamalizika kwa njia ya kutisha? Hakuna shaka kwamba maadui sugu wa Mungu watafikiri hivyo. Lakini uharibifu wa milele wa waovu ni kitia-moyo kweli kweli kwa marafiki wa Mungu. Watu wa Yehova wanahitaji uhakikisho huo kwamba sasa adui zao hawatawaweza tena. Maadui hao, ambao wamewatesa sana watu wa Mungu na kuliletea jina lake suto kubwa, wataharibiwa milele. Halafu, “mateso hayatainuka mara ya pili.”—Nahumu 1:9.

      22, 23. (a) Eleza baadhi ya njia ambazo umefaidika kwa kujifunza kitabu cha Isaya. (b) Baada ya kujifunza kitabu cha Isaya, umeazimia kufanya nini, na unatumainia nini?

      22 Tunapomalizia funzo letu la kitabu cha Isaya, hakika tunafahamu kwamba kitabu hiki cha Biblia si historia ya kale tu. Bali, kina ujumbe wa maana kwa ajili yetu leo. Tunapozifikiria nyakati zisizo na matazamio mazuri ambamo Isaya aliishi, tunaweza kuona mifanano kati ya kipindi hicho na siku zetu. Wakati wa Isaya kulikuwa na msukosuko wa kisiasa, unafiki wa kidini, ufisadi katika utekelezaji wa sheria, na ukandamizaji wa waaminifu na maskini, na wakati wetu pia una mambo hayo. Bila shaka Wayahudi waaminifu katika karne ya sita K.W.K. walishukuru kwa kuweza kuwa na unabii wa Isaya, nasi leo tunafarijiwa tunapojifunza unabii huo.

      23 Nyakati hizi za hatari ambapo giza linafunika dunia, na giza zito kufunika mataifa, sisi sote tunashukuru sana kwamba Yehova amemtumia Isaya kuwaandalia wanadamu wote nuru! Nuru hiyo ya kiroho itawaletea uhai ulio wa milele na milele wale wote wanaoikubali kwa moyo wote, hata wawe ni wa taifa au kabila gani. (Matendo 10:34, 35) Basi, na tuendelee kutembea katika nuru ya Neno la Mungu, kulisoma kila siku, kulitafakari, na kuthamini sana ujumbe wake. Hiyo itatuletea baraka za milele na kuliletea sifa lile jina takatifu la Yehova!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki