-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Moabu Yanyamazishwa
9. Ufunuo unaofuata unatolewa dhidi ya nani, na watu hao wamethibitikaje kuwa adui za watu wa Mungu?
9 Mashariki mwa Bahari ya Chumvi, kuna jirani mwingine wa Israeli—Moabu. Tofauti na Wafilisti, Wamoabi wanahusiana kiukoo na Israeli, kwa kuwa wao ni wazao wa Loti, mpwa wa Abrahamu. (Mwanzo 19:37) Licha ya uhusiano huo, Moabu ni adui wa muda mrefu wa Israeli. Kwa kielelezo, huko nyuma katika siku za Musa, mfalme wa Moabu alimkodi nabii Balaamu, akitumaini kwamba nabii huyo angewalaani Waisraeli. Mbinu hiyo iliposhindwa, Moabu ilitumia ukosefu wa adili na ibada ya Baali ili kunasa Israeli. (Hesabu 22:4-6; 25:1-5) Basi haishangazi kwamba Yehova sasa ampulizia Isaya kurekodi “ufunuo juu ya Moabu”!—Isaya 15:1a.
10, 11. Ni nini kitakachotukia kwa Moabu?
10 Unabii wa Isaya wahusu majiji na sehemu mbalimbali katika nchi ya Moabu, kutia ndani Ari, Kiri (au Kir-haresethi), na Diboni. (Isaya 15:1b, 2a)
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Eglath-shelishiya, ambao labda jina lake lamaanisha “Ndama wa Miaka Mitatu,” utakuwa kama ng’ombe jike mchanga anayepaza sauti zenye huzuni kwa kukata tamaa. (Isaya 15:5, “BHN”) Majani ya nchi yatakauka huku “maji ya Dimoni” yakijaa damu kwa sababu ya machinjo ya Wamoabi. “Maji ya Nimrimu” yatakuwa “mahali palipoharibika,” kitamathali au kihalisi—yaelekea kwa sababu majeshi ya adui yazuia vijito vyao.—Isaya 15:6-9.
11 Wamoabi watavaa nguo za gunia, mavazi ya maombolezo. Watanyoa vichwa vyao upaa ili kuonyesha aibu na maombolezo. Ndevu zao ‘zitanyolewa,’ kuonyesha huzuni kali na kutwezwa. (Isaya 15:2b-4)
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Moabu” ya Siku ya Kisasa Yaangamia
13. Ni tengenezo gani leo liwezalo kulinganishwa na Moabu?
13 Leo, kuna tengenezo la ulimwenguni kote linalofanana na Moabu ya kale. Tengenezo hilo ni Jumuiya ya Wakristo, sehemu kuu ya “Babiloni Mkubwa.” (Ufunuo 17:5) Moabu na Israeli zilitokana na baba ya Abrahamu, Tera. Vivyo hivyo, Jumuiya ya Wakristo, kama vile kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, hudai kwamba mwanzo wake uko katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza. (Wagalatia 6:16) Hata hivyo, Jumuiya ya Wakristo—sawa na Moabu—ni fisadi, nayo yaendeleza ibada ya miungu tofauti na Mungu mmoja wa kweli, Yehova. (Yakobo 4:4; 1 Yohana 5:21) Viongozi wa Jumuiya ya Wakristo, wakiwa kikundi, hupinga wale wanaohubiri habari njema ya Ufalme.—Mathayo 24:9, 14.
14. Licha ya shauri la Yehova dhidi ya “Moabu” ya leo, kuna tumaini gani kwa washiriki mmoja-mmoja wa tengenezo hilo?
14 Hatimaye Moabu ilinyamazishwa. Jambo hilohilo litakumba Jumuiya ya Wakristo. Yehova, huku akitumia mfano wa kisasa wa Ashuru, atamfanya ukiwa. (Ufunuo 17:16, 17)
-