-
Nabii wa Kale Mwenye Ujumbe wa KisasaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Amozi, baba ya Isaya, siye yule Amosi aliyetoa unabii mwanzoni mwa utawala wa Uzia na ambaye aliandika kitabu cha Biblia chenye jina lake.
-
-
Nabii wa Kale Mwenye Ujumbe wa KisasaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Mtu Mwadilifu Katika Nyakati Zenye Ghasia
4. Isaya alikuwa nani, naye alitumikia lini akiwa nabii wa Yehova?
4 Katika mstari wa kwanza wa kitabu chake, Isaya ajitambulisha kuwa “mwana wa Amozi,”a naye atuambia kuwa alitumikia akiwa nabii wa Mungu katika “siku za Uzia na Yothamu na Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.” (Isaya 1:1) Hii ingemaanisha kwamba Isaya aliendelea kutumikia akiwa nabii wa Mungu kwa taifa la Yuda kwa angalau miaka 46, labda kuanzia mwishoni mwa utawala wa Uzia—wapata mwaka wa 778 K.W.K.
5, 6. Ni jambo gani ambalo lazima lilikuwa kweli kuhusu maisha ya familia ya Isaya, na kwa nini?
5 Tukilinganisha yale tujuayo kuhusu manabii wengine, twajua machache juu ya maisha ya kibinafsi ya Isaya. Twajua kuwa alikuwa mwanamume aliyeoa na kwamba alimwita mkewe “nabii mke.” (Isaya 8:3) Kwa mujibu wa kichapo Cyclopedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature cha McClintock na Strong, jina hilo huonyesha kuwa maisha ya ndoa ya Isaya “yalipatana na kazi yake, na kushikamana nayo vilevile.” Yawezekana kwamba mke wa Isaya, kama vile wanawake wengine wenye kumhofu Mungu katika Israeli ya kale, alikuwa na mgawo wake mwenyewe akiwa nabii mke.—Waamuzi 4:4; 2 Wafalme 22:14.
6 Isaya na mkewe walikuwa na angalau wana wawili, kila mmoja alipewa jina lenye maana ya unabii. Mzaliwa wa kwanza, Shear-yashubu, aliandamana na Isaya alipowasilisha ujumbe mbalimbali wa Mungu kwa Mfalme Ahazi mwovu. (Isaya 7:3) Ni wazi kwamba Isaya na mkewe waliifanya ibada ya Mungu kuwa jambo muhimu katika familia—kielelezo chema kwa wenzi wa ndoa leo!
-
-
Nabii wa Kale Mwenye Ujumbe wa KisasaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 7]
Isaya Alikuwa Nani?
MAANA YA JINA: “Wokovu wa Yehova”
FAMILIA: Mtu aliyeoa, mwenye angalau wana wawili
MAKAO: Yerusalemu
MIAKA YA UTUMISHI: Angalau miaka 46, kuanzia karibu mwaka wa 778 K.W.K. hadi wakati fulani baada ya mwaka wa 732 K.W.K.
WAFALME WA YUDA WALIOKUWAPO SIKU ZAKE: Uzia, Yothamu, Ahazi, Hezekia
MANABII WALIOKUWAPO SIKU ZAKE: Mika, Hosea, Odedi
-