-
Wenye Furaha Ni Yule Ambaye Mungu Wake Ni YehovaMnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 1
-
-
Nilishangaa kuona kwamba ukweli ulikuwa umefikia eneo la Far North. Pindi moja, mimi na Walter Lewkowicz tulitembelea kibanda kilichokuwa karibu na kijiji cha Lower Post, British Columbia, kando ya Barabara Kuu ya Alaska, karibu na mpaka wa Yukon Territory. Tulijua kwamba kuna mtu aliyeishi kwenye kibanda hicho kwa sababu tuliona mwangaza mdogo kupitia dirisha dogo. Ilikuwa karibu saa tatu usiku tulipogonga mlango huo. Tulisikia sauti ya mwanamume ikitukaribisha, kwa hiyo tukaingia ndani. Tulishangaa kama nini kumwona mwanamume mzee amejilaza kwenye kitanda chake cha ghorofa akisoma gazeti la Mnara wa Mlinzi! Lo! alikuwa na gazeti la karibuni zaidi kuliko lile tulilokuwa tunaonyesha watu! Alitueleza kwamba yeye hupokea magazeti yake kwa ndege. Kufikia wakati huu, hatukuwa na magazeti ya karibuni zaidi kwa kuwa hatukuwa tumehudhuria mikutano kwa siku nane. Mtu huyo alituambia kwamba anaitwa Fred Berg, na ingawa alikuwa ameandikisha magazeti kwa miaka kadhaa, hii ndiyo iliyokuwa mara ya kwanza kutembelewa na Mashahidi wa Yehova. Fred alitukaribisha tulale kwake usiku huo. Tulimweleza kweli nyingi za Kimaandiko na tukapanga Mashahidi wengine waliokuwa wakipitia eneo hilo kwa ukawaida, wamtembelee.
-
-
Wenye Furaha Ni Yule Ambaye Mungu Wake Ni YehovaMnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 1
-
-
Nilifurahi kujua kwamba katika maeneo ya mbali, sawa na kwingineko, Yehova huonyesha watu wote fadhili zenye upendo na kwamba roho yake huchochea akili na mioyo ya wale walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uhai wa milele. Mtu mmoja mwenye mwelekeo huo alikuwa Henry Lepine kutoka Dawson City, Yukon, jiji ambalo sasa linaitwa Dawson. Henry aliishi katika eneo lililojitenga. Alikuwa hajawahi kuondoka kwenye eneo la migodi ya dhahabu kwa zaidi ya miaka 60. Hata hivyo, roho ya Yehova ilimchochea mzee huyo mwenye umri wa miaka 84 kusafiri umbali wa zaidi ya kilometa 1,600 hadi Anchorage kuhudhuria kusanyiko la mzunguko, hata ingawa hakuwa amewahi kuhudhuria mkutano wa kutaniko hata mmoja. Alifurahia sana programu na ushirika huo. Aliporudi Dawson City, Henry aliendelea kuwa mwaminifu hadi kifo chake. Wengi waliomjua Henry walishangaa ni nini kilichomchochea mzee huyo kufunga safari hiyo ndefu. Kisa hicho kiliwachochea wazee wengine kukubali ukweli. Kwa hiyo, Henry alitoa ushahidi mzuri kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
-