Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Tanzania

      Wakati wa kampeni ya kuhubiri maeneo ya mbali mnamo Oktoba 2005, ndugu tisa kutoka Kutaniko la Iringa walienda eneo la Pawaga, lililo umbali wa kilomita 75 hivi. Walikuwa wamepata habari kwamba kulikuwa na mhubiri aliyeishi sehemu hiyo ya mbali, na hivyo wakaenda kumtafuta. Baada ya kuuliza watu kadhaa, walimpata ndugu huyo ambaye alisema kwamba amekuwa akiishi katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka 20 akidhani kwamba kazi ya Ufalme ilikuwa bado imepigwa marufuku nchini Tanzania. Kwa muda huo wote alikuwa akiwahubiria watu na alisema kwamba baadhi yao walipendezwa kikweli na ujumbe wa Biblia. Kila walipotembelea Pawaga, ndugu wa Kutaniko la Iringa walijitolea kukaa kwa muda wa majuma mawili ili kufuatilia upendezi. Mnamo 2006, mapainia wa kawaida wawili walihamia eneo hilo lenye upendezi mwingi. Ndugu aliyeishi mahali hapo alisaidiwa kiroho, na kikundi hicho sasa kina wahubiri tisa. Kwa sasa wanafanya mikutano chini ya mti, lakini kuna mipango ya kujenga mahali padogo pa kukutania wakitumia vifaa vinavyopatikana katika eneo hilo.

  • Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 46]

      Kujifunza kitabu “Biblia Inafundisha” pamoja na kikundi cha watu huko Pawaga, Tanzania

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki