-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Zaidi ya hayo, kwa kuwashawishi wanadamu wawili wa kwanza wasimtii Mungu, Shetani pia alitilia shaka ushikamanifu wa viumbe wote wenye akili. Kama ilivyoonyeshwa katika kisa cha Ayubu, ambaye alikuwa mshikamanifu kwa enzi kuu ya Yehova, Shetani alidai kwamba anaweza kuwashawishi wanadamu wote wamwasi Mungu.—Ayu. 2:1-5.
10. Kwa kuruhusu muda upite kabla ya kutetea enzi yake kuu, Mungu ameruhusu nini?
10 Kwa kuruhusu muda upite kabla ya kutetea enzi yake kuu, Yehova amempa Shetani wakati wa kuthibitisha dai lake. Pia, Mungu amewapa wanadamu nafasi ya kuonyesha ushikamanifu wao kwa enzi yake.
-
-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
11. Wanadamu wengi wamefanya nini kuhusiana na enzi kuu ya Yehova?
11 Wanadamu wengi wameonyesha imani na kudumisha utimilifu wao kwa enzi kuu ya Yehova na kutakaswa kwa jina lake. Wanadamu hao wanatia ndani Abeli, Enoko, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Ruthu, Daudi, Yesu, wanafunzi wa mapema wa Kristo, na mamilioni ya watu wanaoshika utimilifu leo. Watu kama hao ambao wanaunga mkono enzi kuu ya Mungu wanashiriki katika kuthibitisha kwamba Shetani ni mwongo na katika kuondoa suto ambayo Ibilisi ameleta juu ya jina la Yehova kwa kujigamba kwamba anaweza kuwashawishi wanadamu wote wamwasi Mungu.—Met. 27:11.
-