Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Ingawa Mashahidi katika Italia walikuwa na idadi ipatayo mia moja tu katika 1946, miaka mitatu baadaye kulikuwa makutaniko 64—madogo lakini yenye kufanya kazi kwa bidii. Makasisi walikuwa na wasiwasi. Wakishindwa kupinga kweli za Biblia walizohubiri Mashahidi wa Yehova, makasisi Wakatoliki walikaza wenye mamlaka wa serikali wajaribu kuwaondolea mbali. Hivyo, katika 1949, wamishonari walio Mashahidi waliamriwa waondoke nchini.

      Kwa kurudiarudia makasisi wa Roma Katoliki walijaribu kukatiza au kuzuia makusanyiko ya Mashahidi katika Italia. Walitumia watu wenye kusumbua ili kukatiza kusanyiko katika Sulmona katika 1948. Katika Milan walimkaza mkuu wa polisi afute ruhusa ya kufanya mkusanyiko katika Teatro dell’Arte katika 1950. Tena, katika 1951, walitumia uvutano juu ya polisi wakafuta ruhusa ya kufanya kusanyiko katika Cerignola. Lakini katika 1957, wakati polisi walipoamuru mkusanyiko wa Mashahidi katika Milan ukomeshwe, vyombo vya habari vya Italia vilipinga, na maswali yalizushwa bungeni. Gazeti la habari la kila juma la Roma Il Mondo, la Julai 30, 1957, halikusita kutaarifu kwamba tendo hilo lilichukuliwa ili “kumridhisha askofu mkuu,” Giovanni Battista Montini, aliyepata baadaye kuwa Papa Paul wa 6.

  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 493]

      Ujapokuwa upinzani wa makasisi, maelfu walimiminika kwenye mikusanyiko ya Mashahidi katika Italia (Roma, 1969)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki