-
Kutembelea Majiji Yenye Kuvutia ya Milan na TurinAmkeni!—2001 | Julai 22
-
-
Historia ya Milan inahusiana sana na Kanisa Katoliki, kama vile historia ya sehemu nyingine za Italia. Basi, si ajabu kwamba kanisa kuu la Milan, au duomo, ni kanisa la tatu kwa ukubwa huko Ulaya, nalo ni mojawapo ya makanisa makubwa ulimwenguni ya aina ya Gothic. Kanisa hilo lina urefu wa meta 150 hivi, na lina vijimnara vingi sana na sanamu na nguzo zaidi ya 3,000 zenye maumbo ya ajabu. Ujenzi ulianza katika mwaka wa 1385 na ilichukua miaka 500 kumaliza kujenga kanisa hilo. Siku hizi, Waitalia wanapotaja kazi inayochukua muda mrefu mno kumaliza, wanasema ni kama “kujenga lile kanisa kuu.”
Wasomaji wa Biblia watapendezwa kuona jina la Mungu, ambalo limeandikwa kwa muundo wa “Jahve,” huko juu katika dirisha kwenye ukuta wa mbele wa kanisa hilo. Ukuta wa mbele umepambwa kwa michoro kadhaa ya matukio yanayosimuliwa katika Biblia.
-
-
Kutembelea Majiji Yenye Kuvutia ya Milan na TurinAmkeni!—2001 | Julai 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 24]
Kanisa kuu la Milan
-