Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nafurahia Sehemu Yangu ya Kufundisha Biblia Duniani Kote
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Julai 1
    • Natumwa Nchi Nyingine na Kujifunza Lugha Nyingine

      Baada ya muda, watu wa familia yetu huko Ugiriki walianza kuathiriwa na uzee na afya mbaya. Lakini hawakuniomba niache utumishi wa wakati wote na kurudia yale yanayoonwa kuwa maisha ya kawaida ili niweze kuwasaidia. Hata hivyo, baada ya kutafakari na kusali sana, niliona inafaa nitumike karibu na familia yetu. Kwa upendo, ndugu kwenye ofisi ya tawi walikubaliana na maoni yangu, nao wakanituma Italia. Familia yetu ilijitolea kulipia gharama za kuhama. Kwa kweli, kulikuwa na uhitaji mkubwa wa waeneza-injili nchini Italia.

      Kwa mara nyingine, ilinibidi kujifunza lugha mpya, yaani, Kiitaliano. Mwanzoni nilitumwa katika jiji la Foggia na baadaye nikatumwa Naples, ambako kulikuwa na uhitaji mkubwa zaidi. Nilipaswa kuhubiri katika eneo linaloitwa Posilipo, mojawapo ya maeneo yenye kuvutia zaidi huko Naples. Ingawa eneo hilo lilikuwa kubwa sana, kulikuwa na mhubiri mmoja tu wa Ufalme. Nilifurahia sana kuhubiri, naye Yehova alinisaidia kuanzisha mafunzo mengi ya Biblia. Baada ya muda, kulikuwa na kutaniko kubwa katika eneo hilo.

      Watu wa kwanza kabisa ambao nilijifunza Biblia pamoja nao huko Posilipo ni mama mmoja na watoto wake wanne. Mama huyo na binti zake wawili bado ni Mashahidi wa Yehova. Pia, nilijifunza na mume na mke ambao walikuwa na msichana mdogo. Wote walifanya maendeleo ya kiroho na kuonyesha wakfu wao kwa Yehova kwa kubatizwa katika maji. Sasa binti yao ameolewa na mtumishi mwaminifu wa Yehova, na wote wawili wanamtumikia Mungu kwa bidii. Nilipokuwa nikijifunza Biblia na familia moja kubwa, nilivutiwa sana na nguvu za Neno la Mungu. Tuliposoma maandiko kadhaa yanayoonyesha kwamba Mungu hakubali kuabudiwa kupitia sanamu, mama hata hakungoja tumalize kujifunza. Aliharibu papo hapo sanamu zote zilizokuwa nyumbani kwake!

      Katika Hatari za Baharini

      Sikuzote nilisafiri kwa meli kati ya Italia na Ugiriki. Kwa kawaida nilifurahia safari hizo. Lakini mwaka wa 1971, mambo yalikuwa tofauti. Nilikuwa nikirudi Italia kwa meli iliyoitwa Heleanna. Asubuhi na mapema Agosti 28, moto ulizuka kwenye jiko la meli hiyo. Moto huo ulienea, nao abiria wakawa na wasiwasi. Wanawake walianza kupoteza fahamu, watoto walikuwa wakilia, nao wanaume walikuwa wakiteta vikali na kutoa vitisho. Watu walikimbilia mashua za kuokolea maisha zilizokuwa kwenye sitaha. Lakini jaketi za kujiokolea zilikuwa chache sana, nao mtambo wa kushusha mashua za kuokolea maisha haukufanya kazi vizuri. Sikuwa na jaketi ya kujiokolea, nao moto ulikuwa unazidi kuwa mkubwa, kwa hiyo nikaona jambo la busara kufanya ni kujitosa baharini.

      Punde baada ya kujitosa baharini, nilimwona mwanamke ambaye alikuwa amevaa jaketi ya kujiokolea akielea karibu nami. Ilionekana kama hawezi kuogelea, kwa hiyo nikamshika mkono ili kumburuta kutoka kwenye meli iliyokuwa ikizama. Kwa kuwa mawimbi yalizidi kuwa makali, nilipambana nayo ili nisizame, nami nikachoka sana. Sikuwa na matumaini yoyote kamwe, lakini niliendelea kumwomba Yehova anipe ujasiri, na jambo hilo likanitia nguvu. Hali hiyo ilinikumbusha wakati Paulo alipoharibikiwa na meli.—Matendo, sura ya 27.

      Huku nikiwa nimemshika yule mwanamke, niliendelea kupambana na mawimbi kwa muda wa saa nne, huku nikiogelea tu nilipokuwa na nguvu za kufanya hivyo na kumwomba Yehova anisaidie. Mwishowe niliona mashua ndogo ikitukaribia. Niliokolewa lakini mwenzangu alikuwa tayari amekufa. Tulipofika mjini Bari, Italia, nilipelekwa hospitalini, ambako nilipewa huduma ya kwanza. Nililazwa hospitalini kwa muda wa siku kadhaa. Mashahidi wengi walinitembelea na kwa fadhili wakashughulikia mahitaji yangu yote. Upendo wa Kikristo walioonyesha uliwavutia sana wagonjwa wengine waliokuwa wamelazwa pia.b

      Baada ya kupona kabisa, nilitumwa Roma. Niliombwa nihubiri kwenye eneo la biashara la katikati mwa jiji, na kwa msaada wa Yehova nilihubiri kwa miaka mitano. Nilifurahia utumishi nchini Italia kwa miaka 20, na niliwapenda Waitaliano sana.

      Narudi Athens

      Afya ya Ariadne na mume wake ilidhoofika sana. Niliona kwamba nikikaa karibu nao, ninaweza kulipia kwa kadiri fulani mema ambayo walinitendea kwa upendo. Nilihuzunika sana kuondoka Italia.

  • Nafurahia Sehemu Yangu ya Kufundisha Biblia Duniani Kote
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Julai 1
    • [Picha katika ukurasa wa 11]

      Nikiwa Italia, mapema katika miaka ya 1970

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki