-
Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Baada ya Yehoshafati kusali, hapo “katikati ya kutaniko,” roho ya Yehova ilimchochea Yahazieli, Mlawi, kusema maneno yenye kufariji ambayo yaliwapa watu tumaini.—Soma 2 Mambo ya Nyakati 20:14-17.
10. (a) Yehoshafati na Yuda walipata mwongozo jinsi gani? (b) Tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tunathamini mwongozo tunaopata kutoka kwa Yehova leo?
10 Ndiyo, wakati huo, Yehoshafati na ufalme wa Yuda walipata mwongozo kutoka kwa Yehova kupitia kwa Yahazieli. Leo, tunapata faraja na mwongozo kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Bila shaka, sikuzote tunapaswa kuwaheshimu na kushirikiana na wazee waliowekwa rasmi, ambao wanafanya kazi ya uchungaji kwa bidii na kuhakikisha kwamba miongozo ya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” inafuatwa.—Mt. 24:45; 1 The. 5:12, 13.
-
-
Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
12 Yehoshafati na watu wake walifuata mwongozo uliotolewa na Mungu kupitia Yahazieli. Walipata matokeo gani? Walishinda vita na wakarudi Yerusalemu ‘wakishangilia’ huku wakipiga “vinubi na tarumbeta, kwenye nyumba ya Yehova.” (2 Nya. 20:27, 28) Sisi pia tunaheshimu mwongozo unaotolewa na Yehova kupitia tengenezo lake na tunajiunga na wengine katika kumsifu.
-