Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
    • 12. Yehova hutusaidiaje kufahamu jinsi alivyo kwa kutumia usemi tunaoweza kuelewa?

      12 Yehova, ambaye ni roho, amefanya mengi zaidi ili kutusaidia kumjua. Tukiwa wanadamu, uwezo wetu wa kuona una mipaka na hivyo hatuwezi kuona makao ya roho. Kama Mungu angetueleza utu wake kwa kutumia usemi wa roho ingekuwa ni kama kujaribu kumweleza mtu aliyezaliwa kipofu kila jambo kuhusu sura yako, kama vile rangi ya macho yako au madoa uliyo nayo ngozini. Badala yake, Yehova hutusaidia kwa fadhili kufahamu jinsi alivyo kwa kutumia usemi tunaoweza kuelewa. Nyakati nyingine, yeye huongea kwa kutumia semi za mlinganisho na mifano, akijifananisha na vitu tunavyojua. Hata anajieleza kuwa na viungo fulani vya kibinadamu.b

      13. Andiko la Isaya 40:11 linaleta picha gani akilini, nalo linakufanya uhisije?

      13 Hebu tazama jinsi Yehova anavyofafanuliwa katika Isaya 40:11: “Atalilisha kundi lake kama mchungaji, atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; na kuwachukua kifuani mwake.” Hapa Yehova analinganishwa na mchungaji ambaye hubeba wana-kondoo “mikononi mwake.” Hilo laonyesha uwezo wa Mungu wa kuwalinda na kuwategemeza watu wake, hata wale walio dhaifu. Tunaweza kuhisi tukiwa salama katika mikono yake yenye nguvu, kwa sababu hatatuacha kamwe tukiwa waaminifu kwake. (Waroma 8:38, 39) Mchungaji Mkuu huwachukua wana-kondoo “kifuani mwake”—usemi huo unarejezea mapindo mapana ya vazi la juu, ambamo nyakati nyingine mchungaji alibebea mwana-kondoo aliyetoka kuzaliwa. Kwa hiyo, tunahakikishiwa kwamba Yehova anatupenda sana naye anatutunza kwa upendo. Ni jambo la kawaida kutaka kuwa karibu naye.

  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
    • b Kwa mfano, Biblia husema juu ya uso, macho, masikio, pua, kinywa, mikono, na miguu ya Mungu. (Zaburi 18:15; 27:8; 44:3; Isaya 60:13; Mathayo 4:4; 1 Petro 3:12) Semi hizo za mfano hazipasi kuchukuliwa kihalisi, kama tusivyoelewa kihalisi semi kama vile Yehova ni “Mwamba” au “ngao.”—Kumbukumbu la Torati 32:4; Zaburi 84:11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki