-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Msaada kwa Watafsiri
Chakula cha kiroho kinachoandaliwa na jamii ya msimamizi-nyumba mwaminifu kinapatikana sasa katika angalau lugha 390. (Luka 12:42) Kwa hiyo, kazi ya kutafsiri ni mojawapo ya kazi muhimu ya tengenezo la Yehova, nayo inaongezeka daima.
Tafsiri sahihi si tafsiri ya neno kwa neno. Bali inamaanisha kutafsiri kwa usahihi maana ya habari. Kwa hiyo ni lazima watafsiri waelewe habari vizuri kabla ya kuanza kutafsiri. Nyakati nyingine, hilo linaweza kuwa jambo gumu.
Ili kutatua tatizo hilo, Baraza Linaloongoza lilielekeza kwamba ndugu kadhaa walioteuliwa wazoezwe kufundisha Mtaala wa Kuongeza Ujuzi wa Lugha ya Kiingereza. Baada ya kuhudhuria mtaala kwenye Kituo cha Elimu cha Watchtower huko Patterson, New York, ndugu hao waliwafundisha watafsiri kotekote duniani katika mwaka wa utumishi wa 2002 na 2003. Walitumia miezi mitatu hivi kufundisha kila kikundi cha watafsiri mtaala huo na kuwapa mawaidha kuhusiana na kazi yao. Mtaala huo umewasaidia watafsiri kuelewa vizuri zaidi habari za Kiingereza wanazotafsiri.
Kikundi kimoja cha watafsiri kilisema hivi: “Kwa fadhili, Yehova alitusaidia kufanya kazi yetu kwa ustadi zaidi. Sasa tuna uhakika zaidi. Tunatarajia kuona matokeo mazuri, Yehova akiendelea kutubariki.” Msimamizi mmoja wa Idara ya Kutafsiri alisema hivi: “Zamani, wengi wetu tuling’ang’ana kwa saa nyingi kuelewa maneno au sentensi fulani za Kiingereza. Jambo hilo lilichelewesha kazi yetu. Kwa hiyo, tunathamini sana mtaala huo. Tulionyeshwa jinsi ya kuchanganua maana ya habari za Kiingereza hatua kwa hatua, na tulifundishwa njia nzuri sana za kushughulikia habari tata. Kwa hiyo, sasa hatuna wasiwasi mwingi, na tunaweza kutafsiri kwa usahihi na haraka zaidi.”
Watafsiri wengine waliandika hivi: “Mtaala huo ulikuwa mzuri kuliko mtaala unaotolewa chuoni, kwa kuwa ulilenga hasa matatizo tunayokabili katika kazi yetu. Tunaamini kwamba masomo hayo yatawasaidia watafsiri ulimwenguni pote, na kuwawezesha watu wenye mfano wa kondoo ‘kuelewa maana’ ya kweli za Biblia kwa urahisi zaidi.”—Mt. 13:23.
Kufikia leo, watafsiri 1,660 hivi ambao wanatafsiri katika zaidi ya lugha 150 wamefaidika na mtaala huo. Isitoshe, mpango huo umewasaidia pia watafsiri wa lugha ya ishara na wale wanaotafsiri kutoka Kihispania hadi lugha mbalimbali za kienyeji za Amerika ya Kati na Kusini.
-
-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
[Picha katika ukurasa wa 14]
Walimu wa Mtaala wa Kuongeza Ujuzi wa Lugha ya Kiingereza, na wake zao
-