-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Baadhi ya kazi zilifanywa na wanakandarasi ambao si Mashahidi. Mwanakandarasi mmoja alisema: “Watu wangu hawawezi kufanya kazi kama ninyi hata nikiwapa pesa nyingi kadiri gani. Mnafanya kazi kwa moyo.” Naye msimamizi fulani wa mradi wa ujenzi, akasema, “Nimeelewa na kujifunza mambo mengi kuhusu kazi yangu katika miezi michache ambayo nimefanya kazi mahali hapa kuliko yale niliyojifunza kwa miaka mitano shuleni!” Wawakilishi wa shirika lililowauzia akina ndugu mashine yenye ukanda wa kusafirishia mizigo alisema: “Asanteni enyi watu, hii ndiyo mara yetu ya kwanza kuunganisha mashine haraka hivi. Kila mtu hapa ana furaha, na jambo hilo lanifurahisha! Mahali hapa panapendeza.”
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Akina ndugu walitoa ushahidi mzuri walipokuwa wakijenga. “Ninyi mnaishi paradisoni,” mwanakandarasi fulani alisema.
“Unazungumzia paradiso halisi au ya kiroho?” ndugu wakauliza.
“Zote mbili!” mwanakandarasi huyo akajibu.
-