Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • “NA IANGAMIE ILE SIKU NILIYOZALIWA”

      (Ayubu 1:1–3:26)

      Siku moja Shetani alitilia shaka utimilifu wa Ayubu mbele za Mungu. Yehova alikubali madai hayo naye akamruhusu Shetani alete mfululizo wa misiba juu ya Ayubu. Hata hivyo, Ayubu alikataa ‘kumlaani Mungu.’—Ayubu 2:9.

      Marafiki watatu wa Ayubu walikuja “kumsikitikia.” (Ayubu 2:11) Walikaa pamoja naye bila kusema neno lolote hadi Ayubu alipokatiza kimya hicho kwa kusema: “Na iangamie ile siku niliyozaliwa.” (Ayubu 3:3) Alitamani kuwa “kama watoto ambao hawajaona nuru,” au kama watoto ambao hufa kabla ya kuzaliwa.—Ayubu 3:11, 16.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • “SITAJIONDOLEA UTIMILIFU WANGU!”

      (Ayubu 4:1–31:40)

      Marafiki watatu wa Ayubu walidai kwamba Ayubu alipokea adhabu hiyo kali kutoka kwa Mungu kwa sababu huenda alikuwa amefanya jambo fulani baya sana. Elifazi ndiye aliyeongoza mazungumzo, na Bildadi akafuata kwa kutumia maneno ya dhihaka zaidi. Sofari ndiye aliyekuwa mwenye dharau hata zaidi.

      Ayubu hakukubaliana na mawazo yenye kupotoka ya marafiki wake. Kwa kuwa hakuelewa kwa nini Mungu aliruhusu ateseke, Ayubu alitaka kujitetea tu. Hata hivyo, Ayubu alimpenda Mungu naye akasema: “Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu wangu!”—Ayubu 27:5.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • “NINATUBU KATIKA MAVUMBI NA MAJIVU”

      (Ayubu 32:1–42:17)

      Kijana mmoja mtazamaji aliyeitwa Elihu alikuwa akisikiliza kwa subira mjadala huo. Kisha akaanza kuzungumza kwa ujasiri. Alimkosoa Ayubu na watesi wake watatu.

      Punde tu baada ya Elihu kumaliza, Yehova alijibu kupitia dhoruba ya upepo. Hakueleza kwa nini Ayubu anateseka. Hata hivyo, kwa kuuliza mfululizo wa maswali, Mweza-Yote alimjulisha Ayubu kuhusu nguvu Zake zenye kutia hofu na hekima Yake nyingi. Ayubu alikubali kwamba alisema bila kuelewa, naye akasema hivi: “Ninayatangua niliyosema, nami ninatubu katika mavumbi na majivu.” (Ayubu 42:6) Jaribu la Ayubu lilipokoma, alipata thawabu kwa sababu ya utimilifu wake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki