Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Mambo yaliyompata Ayubu yanaelezwa vizuri sana katika kitabu cha Ayubu hivi kwamba masimulizi hayo yanatajwa kuwa uandishi bora. Hata hivyo, zaidi ya yote simulizi hilo linajibu maswali haya: Kwa nini watu wema huteseka? Kwa nini Yehova anaruhusu uovu? Je, wanadamu wasio wakamilifu wanaweza kudumisha utimilifu wao kwa Mungu? Ujumbe wa kitabu cha Ayubu ni sehemu ya Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho na uko hai na una nguvu hata leo.—Waebrania 4:12.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Mambo Tunayojifunza:

      1:8-11; 2:3-5. Kama inavyoonyeshwa katika kisa cha Ayubu, mbali na matendo na usemi unaofaa, ili mtu awe mtimilifu anahitaji kumtumikia Yehova akiwa na nia nzuri.

      1:21, 22. Tukiwa washikamanifu kwa Yehova wakati wa hali nzuri na hali mbaya pia, tunaweza kumthibitisha Shetani kuwa mwongo.—Methali 27:11.

      2:9, 10. Kama Ayubu, tunapaswa kuendelea kuwa imara katika imani hata ikiwa watu wa familia hawathamini mambo ya kiroho au wanafanya yote wawezayo ili tubadili msimamo wetu au tuache imani yetu.

      2:13. Marafiki wa Ayubu hawakusema jambo lolote lenye kufariji kuhusu Mungu na ahadi zake kwa sababu hawakuwa na maoni kama ya Mungu.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Mambo Tunayojifunza:

      4:7, 8; 8:5, 6; 11:13-15. Hatupaswi kukata kauli haraka kwamba mtu fulani aliye katika hali ya kufadhaika anavuna kile alichopanda na kwamba hana kibali cha Mungu.

      4:18, 19; 22:2, 3. Mashauri yetu yanapaswa kutegemea Neno la Mungu, wala si maoni yetu wenyewe.—2 Timotheo 3:16.

      10:1. Kuudhika kulimpofusha Ayubu hivi kwamba hakufikiria sababu nyingine ambazo zilisababisha mateso yake. Hatupaswi kuudhika tunapoteseka, hasa kwa kuwa tunaelewa vizuri masuala yanayohusika.

      14:7, 13-15; 19:25; 33:24. Tumaini la ufufuo linaweza kututegemeza wakati wa jaribu lolote lile ambalo Shetani anaweza kutuletea.

      16:5; 19:2. Maneno yetu yanapaswa kuwatia wengine moyo na kuwaimarisha, wala si kuwakasirisha.—Methali 18:21.

      22:5-7. Shauri linalotolewa kwa msingi wa shutuma zisizo na uthibitisho halina maana na ni lenye madhara.

      27:2; 30:20, 21. Hatuhitaji kuwa wakamilifu ili kudumisha utimilifu. Ayubu alimlaumu Mungu isivyo haki.

      27:5. Ni Ayubu mwenyewe tu ambaye angeweza kujiondolea utimilifu wake kwa sababu utimilifu unategemea upendo wa mtu kwa Mungu. Kwa hiyo, tunapaswa kumpenda Yehova sana ili tudumishe utimilifu wetu.

      28:1-28. Mwanadamu anajua mahali hazina za dunia hupatikana. Anapozitafuta, ustadi wake humwongoza kwenye vijia vilivyochimbwa chini ya ardhi ambavyo haviwezi kuonekana na ndege yeyote mwenye kuwinda aliye na uwezo wa kuona mbali. Hata hivyo, hekima ya Mungu, hupatikana kwa kumwogopa Yehova.

      29:12-15. Tunapaswa kuwa tayari kuonyesha fadhili zenye upendo kwa wale walio katika uhitaji.

      31:1, 9-28. Ayubu alituwekea kielelezo kizuri kwa kuwa aliepuka kuwachezea wengine kimapenzi. Pia, aliepuka uzinzi, ukosefu wa haki, kuwatendea wengine bila huruma, kupenda vitu vya kimwili, na ibada ya sanamu.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Mambo Tunayojifunza:

      32:8, 9. Mtu hawi na hekima kwa sababu tu ana umri mkubwa. Hekima inatokana na uelewaji wa Neno la Mungu na mwongozo wa roho yake.

      34:36. Utimilifu wetu huonekana “tunapojaribiwa mpaka ukomo.”

      35:2. Elihu alisikiliza kwa makini na kutambua tatizo hususa kabla ya kusema. (Ayubu 10:7; 16:7; 34:5) Kabla ya kutoa shauri, wazee Wakristo wanapaswa kusikiliza kwa makini, kuwa na uthibitisho, na kuelewa waziwazi mambo yote yanayohusika.—Methali 18:13.

      37:14; 38:1–39:30. Kutafakari juu ya kazi za ajabu za Yehova, yaani, mambo yanayoonyesha nguvu zake na hekima, hutunyenyekeza na kutusaidia tutambue kwamba kutetewa kwa enzi yake kuu ndilo jambo muhimu zaidi kuliko mapendezi yetu.—Mathayo 6:9, 10.

      40:1-4. Tunapohisi kwamba tunataka kumlaumu Mweza-Yote, tunapaswa ‘kuuweka mkono wetu juu ya kinywa chetu.’

      40:15–41:34. Behemothi (kiboko) na Lewiathani (mamba) wana nguvu nyingi sana! Ili kuvumilia katika utumishi wa Mungu, sisi pia tunahitaji nguvu kutoka kwa Muumba wa wanyama hao wenye nguvu nyingi, anayetutia nguvu.—Wafilipi 4:13.

      42:1-6. Kusikiliza neno la Yehova na kukumbushwa kuhusu mambo yanayoonyesha nguvu zake kulimsaidia Ayubu ‘kumwona Mungu,’ au kuona ukweli kumhusu. (Ayubu 19:26) Hilo lilirekebisha namna yake ya kufikiri. Tunapopata rekebisho kutoka katika Biblia, tunapaswa kutambua kwa haraka kosa letu na kufanya marekebisho.

      Kusitawisha “Uvumilivu wa Ayubu”

      Kitabu cha Ayubu kinaonyesha waziwazi kwamba si Mungu anayewatesa wanadamu. Shetani ndiye anayewatesa. Kwa kuruhusu uovu duniani, Mungu hutupa nafasi ya kuonyesha tunaunga mkono upande gani katika suala la enzi kuu ya Yehova na la utimilifu wetu.

      Kama Ayubu, wote wanaompenda Yehova watajaribiwa. Simulizi kuhusu Ayubu hutupa uhakika wa kwamba tunaweza kuvumilia. Linatukumbusha kwamba matatizo yetu hayatadumu milele. Andiko la Yakobo 5:11 linasema hivi: “Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu nanyi mmeona matokeo ambayo Yehova alileta.” Yehova alimpa Ayubu thawabu kwa kuwa alidumisha utimilifu wake. (Ayubu 42:10-17) Mbele yetu tuna tumaini zuri sana, yaani, uzima wa milele katika Paradiso duniani! Kama Ayubu, acheni tuazimie kudumisha utimilifu wetu.—Waebrania 11:6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki