Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • BARUA tatu za mtume Yohana ambazo inaelekea ziliandikwa mwaka wa 98 W.K. huko Efeso, ni kati ya vitabu vya mwisho vya Maandiko yaliyoongozwa na roho takatifu. Barua mbili za kwanza zinawatia moyo Wakristo waendelee kutembea katika nuru na kupinga uasi-imani.

  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • ENDELEA KUTEMBEA KATIKA NURU NA UPENDO NA KWA IMANI

      (1 Yohana 1:1–5:21)

      Barua ya kwanza ya Yohana iliandikwa kwa ajili ya wote walio katika ushirika na Kristo, na ina mashauri mazuri ya kuwasaidia Wakristo kupinga uasi-imani na kubaki imara kwa ajili ya kweli na uadilifu. Anakazia uhitaji wa kuendelea kutembea katika nuru na upendo na kwa imani.

      Yohana anaandika hivi: “Ikiwa tunatembea katika nuru kama yeye [Mungu] mwenyewe alivyo katika nuru, tuna ushirika sisi kwa sisi.” Na kwa kuwa Mungu ndiye Chanzo cha upendo, mtume huyo anasema: “Acheni tuendelee kupendana.” Ingawa “kumpenda Mungu” kunatuchochea ‘kuzishika amri zake,’ tunaushinda ulimwengu kupitia “imani yetu” katika Yehova Mungu, Neno lake, na Mwana wake.—1 Yoh. 1:7; 4:7; 5:3, 4.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      2:2; 4:10—Yesu ni “dhabihu ya upatanisho” kwa njia gani? Kupatanisha kunamaanisha “kutuliza,” au “kuridhisha.” Yesu alitoa uhai wake kuwa dhabihu ya upatanisho kwa njia ya kwamba aliridhisha au kutosheleza matakwa ya haki kamilifu. Kwa msingi wa dhabihu hiyo, Mungu anaweza kuonyesha rehema na kusamehe dhambi za wale walio na imani katika Yesu.—Yoh. 3:16; Rom. 6:23.

      2:7, 8—Ni amri gani ambayo Yohana anasema ni “ya zamani” na pia ni “mpya”? Yohana anazungumzia amri inayohusu upendo wa kindugu wa kujidhabihu. (Yoh. 13:34) Anasema kwamba ni “ya zamani” kwa sababu Yesu aliitoa miaka zaidi ya 60 kabla ya Yohana kuandika barua yake ya kwanza ambayo iliongozwa na roho. Kwa hiyo, waamini wamekuwa nayo “tangu mwanzo” wa maisha yao wakiwa Wakristo. Amri hiyo pia ni “mpya” kwa sababu inahusisha mengi zaidi ya ‘kumpenda mwenzako kama wewe mwenyewe’ na inatia ndani upendo wa kujidhabihu.—Law. 19:18; Yoh. 15:12, 13.

      3:2—Ni nini ambacho ‘hakijafunuliwa’ kwa Wakristo watiwa-mafuta, na ni nani ambaye watamwona “kama vile yeye alivyo”? Kile ambacho hakijafunuliwa kwao ni jinsi watakavyokuwa watakapofufuliwa na kwenda mbinguni wakiwa na miili ya roho. (Flp. 3:20, 21) Hata hivyo, wanajua kwamba “wakati wowote [Mungu] atakapofunuliwa [watakuwa] kama yeye, kwa sababu [watamwona] kama vile yeye alivyo,” yaani, “Roho.”—2 Kor. 3:17, 18.

      5:5-8—Maji, damu, na roho ilitoa ushahidi jinsi gani na kuthibitisha kwamba “Yesu ndiye Mwana wa Mungu”? Maji yalitoa ushahidi kwa sababu Yesu alipobatizwa katika maji, Yehova mwenyewe alisema kwamba anamkubali akiwa Mwana Wake. (Mt. 3:17) Damu ya Yesu, au uhai wake, uliotolewa kuwa “fidia inayolingana kwa ajili ya wote,” ulionyesha pia kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu. (1 Tim. 2:5, 6) Nayo roho takatifu ilitoa ushahidi wa kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu iliposhuka juu yake wakati alipobatizwa, na kumwezesha ‘kupita katika nchi akitenda mema na kuwaponya wote waliokandamizwa na Ibilisi.’—Yoh. 1:29-34; Mdo. 10:38.

      Mambo Tunayojifunza:

      2:9-11; 3:15. Mkristo akiruhusu kitu chochote au mtu yeyote aharibu upendo wake wa kindugu, anatembea katika giza la kiroho, hajui anakoenda.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki