-
Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya YudaMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
Barua mbili za kwanza zinawatia moyo Wakristo waendelee kutembea katika nuru na kupinga uasi-imani.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya YudaMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
ENDELEA KUTEMBEA KATIKA NURU NA UPENDO NA KWA IMANI
Barua ya kwanza ya Yohana iliandikwa kwa ajili ya wote walio katika ushirika na Kristo, na ina mashauri mazuri ya kuwasaidia Wakristo kupinga uasi-imani na kubaki imara kwa ajili ya kweli na uadilifu. Anakazia uhitaji wa kuendelea kutembea katika nuru na upendo na kwa imani.
Yohana anaandika hivi: “Ikiwa tunatembea katika nuru kama yeye [Mungu] mwenyewe alivyo katika nuru, tuna ushirika sisi kwa sisi.” Na kwa kuwa Mungu ndiye Chanzo cha upendo, mtume huyo anasema: “Acheni tuendelee kupendana.” Ingawa “kumpenda Mungu” kunatuchochea ‘kuzishika amri zake,’ tunaushinda ulimwengu kupitia “imani yetu” katika Yehova Mungu, Neno lake, na Mwana wake.—1 Yoh. 1:7; 4:7; 5:3, 4.
-