-
Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya YudaMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
BARUA tatu za mtume Yohana ambazo inaelekea ziliandikwa mwaka wa 98 W.K. huko Efeso, ni kati ya vitabu vya mwisho vya Maandiko yaliyoongozwa na roho takatifu. Barua mbili za kwanza zinawatia moyo Wakristo waendelee kutembea katika nuru na kupinga uasi-imani.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya YudaMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
ENDELEA ‘KUTEMBEA KATIKA KWELI’
Yohana anaanza barua yake ya pili kwa kusema hivi: “Mwanamume mzee, kwa bibi aliyechaguliwa, na kwa watoto wake.” Anashangilia kwa sababu amekuta “baadhi ya watoto [wake] wanatembea katika kweli.”—2 Yoh. 1, 4.
Baada ya kuwatia moyo wasitawishe upendo, Yohana anaandika hivi: “Upendo unamaanisha hivi, kwamba tuendelee kutembea kulingana na amri zake.” Pia, Yohana anaonya kuhusu “yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.”—2 Yoh. 5-7.
Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:
1, 13—Yule “bibi aliyechaguliwa” ni nani? Huenda Yohana anazungumza kuhusu mwanamke fulani ambaye anamwita Kyria, neno la Kigiriki linalomaanisha “bibi.” Au huenda anatumia usemi wa mfano kuhusu kutaniko fulani ili watesaji wasijue. Ikiwa anazungumza kuhusu kutaniko fulani, basi washiriki wa kutaniko hilo ni watoto wake, nao “watoto wa dada [yake]” ni washiriki wa kutaniko lingine.
7—Ni ‘kuja’ gani kwa Yesu ambako Yohana anazungumzia hapa, na ni jinsi gani wadanganyifu ‘hawakiri’ hilo? Si ‘kuja’ kwa baadaye kwa Yesu kusikoonekana. Badala yake ni kuja kwake katika mwili na kutiwa mafuta ili awe Kristo. (1 Yoh. 4:2) Wadanganyifu hawakiri kuja huko katika mwili. Labda wanapinga kwamba Yesu alikuwapo au wanakataa kwamba alitiwa mafuta na roho takatifu.
Mambo Tunayojifunza:
2, 4. Ili tupate wokovu ni lazima tujue “kweli,” yaani, mafundisho yote ya Kikristo ambayo ni sehemu ya Biblia, na kushikamana nayo.—3 Yoh. 3, 4.
8-11. Ikiwa hatutaki kupoteza ‘fadhili zisizostahiliwa, rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Yesu Kristo,’ na pia ushirika wetu wenye upendo pamoja na waamini wenzetu, tunapaswa ‘kujihadhari’ kiroho na kuwakataa kabisa wale ambao ‘hawakai katika fundisho la Kristo.’—2 Yoh. 3.
-