Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • BARUA tatu za mtume Yohana ambazo inaelekea ziliandikwa mwaka wa 98 W.K. huko Efeso, ni kati ya vitabu vya mwisho vya Maandiko yaliyoongozwa na roho takatifu.

  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • Katika barua ya tatu, Yohana anazungumza kuhusu kutembea katika kweli na pia anawatia moyo Wakristo washirikiane.

  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • IWENI “WAFANYAKAZI WENZI KATIKA KWELI”

      (3 Yohana 1-14)

      Yohana anaandika barua yake ya tatu kwa rafiki yake Gayo. Anaandika hivi: “Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba niwe nikisikia watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.”—3 Yoh. 4.

      Yohana anampongeza Gayo kwa sababu ya ‘kufanya kazi ya uaminifu’ ya kuwasaidia ndugu wageni. Mtume huyo anasema hivi: “Sisi tuna wajibu wa kuwakaribisha watu wa namna hiyo, ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.”—3 Yoh. 5-8.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      11—Kwa nini watu fulani wanatenda mabaya? Hawathamini mambo ya kiroho, na hawamwoni Mungu kwa macho yao ya ufahamu. Kwa kuwa hawawezi kumwona Mungu kihalisi, wanatenda kana kwamba Mungu hawaoni.—Eze. 9:9.

      14—“Rafiki” wanaotajwa hapo ni nani? Neno “rafiki” katika andiko hilo linatia ndani wengine zaidi ya watu walio na uhusiano wa karibu kati yao. Yohana anatumia neno hilo kuwahusu waamini wenzake kwa ujumla.

      Mambo Tunayojifunza:

      4. Watu wakomavu kiroho katika kutaniko wanapata shangwe kubwa wanapoona washiriki wachanga wa kutaniko ‘wakiendelea kutembea katika kweli.’ Na wazazi wanapata shangwe kubwa kama nini wanapofaulu kuwasaidia watoto wao kuwa watumishi wa Yehova!

      5-8. Waangalizi wanaosafiri, wamishonari, wale wanaotumika katika Betheli au ofisi za tawi na wale walio katika utumishi wa upainia ni kati ya wale ambao wanafanya kazi kwa bidii kwa ajili ya ndugu zao kwa sababu wanawapenda na wanampenda Yehova. Imani yao inastahili kuigwa, na tunapaswa kuwategemeza kwa upendo.

      9-12. Tunapaswa kuiga mfano wa Demetrio ambaye alikuwa mwaminifu, bali si yule mpiga-porojo Diotrefe, aliyekuwa mchongezi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki