-
Alijifunza Kutokana na Makosa YakeMnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
Lakini ngoja kidogo! Aliona kitu kikisonga karibu naye, kitu kikubwa, cheusi, kilicho hai. Kilizidi kumkaribia. Mdomo mkubwa ulifunguka na kummeza!
Huu ndio mwisho. Hata hivyo, Yona alishangazwa na jambo moja. Bado alikuwa hai! Hakuwa amevunjwa-vunjwa, wala kumeng’enywa, wala kusongwa pumzi. Ingawa ni kana kwamba alikuwa katika kaburi lake, bado alikuwa hai. Pole kwa pole, Yona alijawa na woga wenye heshima. Bila shaka, ni Mungu wake, Yehova, ‘aliyemweka samaki mkubwa ammeze Yona.’c—Yona 1:17.
Dakika zilizidi kupita. Akiwa humo, katika giza kubwa zaidi ambalo amewahi kuona, Yona alipata nafasi ya kutafakari na kusali kwa Yehova Mungu. Sala yake, ambayo yote imerekodiwa katika sura ya pili ya Yona, inafunua mambo mengi. Inaonyesha kwamba Yona alikuwa na ujuzi mwingi wa Maandiko, kwa sababu inarejelea Zaburi mara nyingi. Pia, inaonyesha sifa fulani nzuri ya Yona: alikuwa mwenye shukrani. Yona alimalizia sala yake hivi: “Lakini mimi, kwa sauti ya kutoa shukrani nitakutolea dhabihu. Nilichoweka nadhiri, nitakitimiza. Wokovu ni wa Yehova.”—Yona 2:9.
Yona alijifunza kwamba Yehova anaweza kumwokoa mtu yeyote, mahali popote, wakati wowote. Hata humo, “ndani ya tumbo la samaki huyo,” Yehova alimpata na kumwokoa mtumishi wake aliyekuwa taabani. (Yona 1:17) Ni Yehova peke yake ambaye angeweza kumhifadhi mtu hai kwa siku tatu mchana na usiku ndani ya tumbo la samaki mkubwa. Leo, tunafaa kukumbuka kwamba ‘pumzi yetu imo mkononi mwa’ Yehova Mungu. (Danieli 5:23) Tuko hai kwa sababu ya mapenzi yake. Je, tunaonyesha kwamba tunashukuru? Basi, je, hatupaswi kumtii Yehova?
Namna gani Yona? Je, alijifunza kumwonyesha Yehova shukrani kwa kumtii? Ndiyo. Baada ya kukaa siku tatu mchana na usiku, samaki huyo alimpeleka Yona hadi ufuoni na “akamtapika Yona kwenye nchi kavu.” (Yona 2:10) Hebu fikiria—baada ya kupitia mambo hayo yote, Yona hakuhitaji hata kuogelea!
-
-
Alijifunza Kutokana na Makosa YakeMnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
c Neno la Kiebrania “samaki,” lilitafsiriwa katika Kigiriki kuwa “mnyama mkubwa wa baharini,” au “samaki mkubwa.” Ingawa hakuna njia ya kuthibitisha ni kiumbe gani wa baharini anayetajwa, imegunduliwa kwamba katika Bahari ya Mediterania kuna papa wakubwa wanaoweza kummeza mtu mzima. Kuna papa wakubwa zaidi katika maeneo mengine. Kwa mfano, papa-nyangumi anaweza kukua kufikia urefu wa mita 15 au zaidi!
-