Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • Waninawi walisikiliza ujumbe wa Yona. Huenda alifikiri kwamba watu wangekuwa wajeuri na wenye uhasama. Badala yake, jambo la ajabu lilitendeka. Watu walisikiliza na kutii ujumbe wake! Maneno yake yalienea kama umeme. Baada ya muda, jiji lote lilikuwa likizungumzia unabii wa hukumu wa Yona. Simulizi la Yona linatuambia: “Watu wa Ninawi wakaanza kumwamini Mungu, ndipo wakatangaza kufunga na kuvaa nguo za magunia, kutoka aliye mkubwa zaidi kati yao mpaka aliye mdogo zaidi.” (Yona 3:5) Watu wote walikuwa na mtazamo uleule wa kutubu, matajiri kwa maskini, wenye nguvu kwa wadhaifu, na wadogo kwa wakubwa. Muda si muda, mfalme alisikia kwamba watu walikuwa wakitubu.

      Mfalme pia alianza kumwogopa Mungu. Aliinuka kutoka kiti chake cha ufalme, akavua nguo zake za kifahari, akavaa nguo za magunia ambazo watu wake walikuwa wamevaa, na hata ‘akaketi katika majivu.’ Ingawa tayari watu wenyewe walikuwa wameanza kufunga, sasa mfalme pamoja na “wakubwa,” au watu wenye vyeo, alitoa agizo la kisheria kwamba watu wote wanapaswa kufunga. Aliamuru kwamba watu wote na pia wanyama wa kufugwa wavae nguo za magunia.c Alikiri kwa unyenyekevu kwamba watu wake walikuwa na hatia ya kutenda mabaya na jeuri. Pia alitumaini kwamba Mungu wa kweli angewaonyesha rehema alipoona kuwa wametubu. Mfalme huyo alisema: ‘Huenda Mungu wa kweli atageuka na kuacha hasira yake inayowaka, tusije tukaangamia.’—Yona 3:6-9.

      Wachambuzi fulani wanafikiri kwamba Waninawi hawangeweza kubadili mtazamo wao haraka hivyo. Hata hivyo, wasomi wa Biblia wanasema kwamba nyakati za kale mara nyingi watu wenye ushirikina katika tamaduni kama hizo walibadili maoni haraka. Vyovyote vile, Yesu Kristo mwenyewe alitaja kutubu kwa Waninawi baadaye. (Mathayo 12:41) Alijua ukweli wa mambo kwa sababu alikuwa hai mbinguni na alijionea mambo hayo yalipotukia. (Yohana 8:57, 58)

  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • c Huenda jambo hilo likashangaza, lakini lilitukia katika siku za kale. Mwanahistoria Mgiriki Herodoto alisema kwamba Waajemi wa kale waliomboleza kifo cha jenerali maarufu kwa kuhusisha wanyama wa kufugwa katika desturi za kuomboleza.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki