Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuijua “Akili ya Kristo”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 15
    • 12. Ni nini kinachoonyesha kwamba yaelekea Yosefu alikufa kabla ya Yesu, na jambo hilo lingemaanisha nini kwa Yesu?

      12 Akiwa mtoto wa kwanza, yaelekea Yesu alisaidia kutunza familia, hasa kwa sababu inaonekana Yosefu alikufa kabla ya Yesu.b Gazeti Zion’s Watch Tower la Januari 1, 1900, lilisema: “Mapokeo yanaonyesha kwamba Yosefu alikufa Yesu akiwa angali mchanga, na kwamba [Yesu] alianza useremala ili kuiruzuku familia. Jambo hilo laungwa mkono na ushuhuda wa Kimaandiko mahali ambapo Yesu mwenyewe anaitwa seremala, na mamake na ndugu zake wanatajwa, lakini Yosefu hatajwi. (Marko 6:3) . . . Basi inawezekana kwamba kile kipindi kirefu cha miaka kumi na minane ya maisha ya Bwana wetu, tokea wakati wa lile tukio [linalotajwa kwenye Luka 2:41-49] hadi wakati alipobatizwa, alikitumia kufanya mambo ya kawaida maishani.” Yaelekea Maria na watoto wake, kutia ndani Yesu, walihuzunishwa na kifo cha mume na baba mpendwa.

  • Kuijua “Akili ya Kristo”
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 15
    • b Mara ya mwisho ambapo Yosefu anatajwa moja kwa moja ni wakati Yesu mwenye umri wa miaka 12 alipopatikana hekaluni. Yosefu hatajwi kuwapo kwenye sherehe ya arusi kule Kana, mwanzoni mwa huduma ya Yesu. (Yohana 2:1-3) Mwaka wa 33 W.K., Yesu aliyetundikwa mtini alimkabidhi Maria kwa mtume mpendwa Yohana ili amtunze. Yaelekea Yesu hangalifanya hivyo kama Yosefu angalikuwa bado hai.—Yohana 19:26, 27.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki