Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mipango ya Mahali pa Ibada
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • pa kuketi, kuandika hudhurio la mikutano, na kuhakikisha kwamba mifumo ya kupitisha hewa inafanya kazi vizuri. Inapohitajika, wakaribishaji wanapaswa kuwakumbusha wazazi wawaangalie watoto wao wasikimbie-kimbie ndani ya jumba kabla na baada ya mikutano au kucheza jukwaani. Kwa fadhili na busara, mkaribishaji anaweza kumwomba mzazi mwenye mtoto mtundu amtoe nje, ili wasikilizaji wasikengeushwe. Kazi inayofanywa na wakaribishaji huwawezesha wote kufurahia mikutano. Inafaa wazee na watumishi wa huduma watumiwe kuwa wakaribishaji.

      UJENZI WA MAJUMBA YA UFALME

      15 Katika karne ya kwanza, Wakristo fulani walikuwa na mali kuliko wengine, ndiyo sababu mtume Paulo aliandika hivi: “Kupitia usawazisho, ziada yenu kwa sasa ijazie uhitaji wao, ili ziada yao pia ijazie upungufu wenu, ili kuwe na usawazisho.” (2 Kor. 8:14) Leo, kuna “usawazisho” kama huo. Michango inayokusanywa katika makutaniko ulimwenguni pote huunganishwa ili kutoa msaada wa kifedha wa kujenga na kukarabati Majumba ya Ufalme. Ukarimu huo wa akina ndugu ulimwenguni pote unathaminiwa sana na tengenezo na makutaniko yanayonufaishwa na michango hiyo.

      16 Ikitegemea mpango na ukubwa wa eneo, ofisi ya tawi hupanga makutaniko kadhaa yatumie Majumba fulani ya Ufalme. Pia, ofisi ya tawi huamua wakati na mahali pa kujenga Majumba mapya ya Ufalme na yale yaliyopo kufanyiwa ukarabati. Majanga yanapotokea, mipango inayohitajiwa hufanywa ili kurekebisha Majumba ya Ufalme yaliyoharibika, na nyakati nyingine, kurekebisha nyumba za akina ndugu.

      17 Ofisi ya tawi huratibu jinsi wajitoleaji watakavyosaidia kupata uwanja, vibali, kusanifu, kudumisha, na kujenga Jumba la Ufalme. Kwa sababu kuna uhitaji mkubwa wa Majumba ya Ufalme katika nchi nyingi, wajitoleaji wengi wanahitajiwa. Wahubiri wote waliobatizwa wanaostahili na wangependa kusaidia, wanatiwa moyo kujaza fomu na kuwapa wazee walio katika Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko lao. Hata wahubiri ambao hawajabatizwa wanaweza kusaidia kujenga au kukarabati Jumba lao la Ufalme.

      MAJUMBA YA KUSANYIKO

      18 Kwa kawaida, Wakristo wa karne ya kwanza walikutana katika vikundi vidogo. Hata hivyo, nyakati nyingine “umati mkubwa” ulikusanyika. (Mdo. 11:26) Vivyo hivyo, watu wa Yehova leo hufanya mikutano mikubwa kama vile makusanyiko ya mzunguko na makusanyiko ya eneo. Mara nyingi, wao hukodi sehemu za kufanyia makusanyiko hayo, hata hivyo isipowezekana, wanajenga mahali pa ibada panapoitwa Jumba la Kusanyiko.

      19 Nyakati nyingine, wao hununua jengo, hulirekebisha, na kulitumia kama Jumba la Kusanyiko. Hata hivyo, mara nyingi uwanja hununuliwa na jumba jipya kujengwa. Ukubwa wa Majumba ya Kusanyiko hutofautiana ikitegemea mahitaji ya eneo. Uamuzi wa kununua au kujenga hufanywa na ofisi ya tawi baada ya kuchanganua kwa uangalifu gharama na jinsi jumba hilo litakavyotumika.

      20 Ofisi ya tawi huwaweka rasmi ndugu wasimamie uendeshaji na udumishaji wa Jumba la Kusanyiko. Mipango hufanywa katika mizunguko ili jumba hilo lisafishwe kwa ukawaida, usafi mkubwa ufanywe mara mbili kwa mwaka, na ukarabati ufanyike ili kulidumisha. Ingefaa wahubiri wajitolee kufanya kazi hiyo. Kwa hiyo, makutaniko yanahimizwa kuunga mkono mipango hiyo kwa moyo wote.—Zab. 110:3; Mal. 1:10.

      21 Nyakati nyingine, Jumba la Kusanyiko linaweza pia kutumiwa kwa ajili ya shughuli nyingine za kitheokrasi, kama vile Shule za Biblia na mikutano ya pekee ya waangalizi wa mzunguko. Jumba la Kusanyiko ni mahali pa ibada palipowekwa wakfu sawa na Jumba la Ufalme. Tunapokutana katika Jumba la Kusanyiko, mwenendo, mavazi, na mapambo yetu yanapaswa kuwa ya heshima, kama tu tunapohudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya ibada.

      22 Mwishoni mwa siku hizi za mwisho, watu wengi wapya wanafanya haraka kuwa sehemu ya tengenezo la Mungu. Huo ni uthibitisho wa baraka za Yehova. (Isa. 60:8, 10, 11, 22) Kwa hiyo, tunapenda kuunga mkono mipango ya kupata na kudumisha mahali safi na pazuri pa ibada. Tunapofanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunathamini umuhimu wa mahali pa ibada katika kutusaidia kutiana moyo kadiri tunavyoona siku ya Yehova ikikaribia.

  • Kutegemeza Kazi ya Ufalme Kwenu na Ulimwenguni Pote
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 12

      Kutegemeza Kazi ya Ufalme Kwenu na Ulimwenguni Pote

      MASHAHIDI WA YEHOVA wanatimiza unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho kwa kuhubiri habari njema “mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8; Mt. 24:14) Ili kufanya hivyo, wametumia wakati na nguvu zao nyingi katika kuwajulisha wengine mambo ya kiroho. Kwa kuwa wanamtegemea Yehova awaandalie mahitaji yao wakiwa wafanyakazi wenzake, wanaendelea kuutanguliza Ufalme wa Mungu maishani mwao. (Mt. 6:25-34; 1 Kor. 3:5-9) Matokeo yanaonyesha wazi kwamba wana kibali na baraka za Yehova.

      KUSHUGHULIKIA FAIDA ZA UFALME ULIMWENGUNI POTE

      2 Wanapoona jinsi tunavyohubiri habari njema na kutambua kwamba Biblia na machapisho yetu yanayotegemea Biblia hutolewa bila malipo, baadhi ya watu hujiuliza hivi: “Inawezekanaje?” Ni kweli kwamba pesa zinahitajiwa ili kuchapisha Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia. Pia, pesa zinahitajiwa ili kulipia gharama nyingine za ujenzi na udumishaji wa Betheli kwa ajili ya wahudumu wanaoendesha mashine za kuchapisha, kusimamia kazi ya kuhubiri, na utumishi mwingine wa kueneza habari njema. Isitoshe, waangalizi wa mzunguko, wamishonari, mapainia wa pekee, na wengine ambao wako katika utumishi wa pekee wa wakati wote hupewa pesa kidogo ili kuwasaidia waendelee

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki