-
Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na WanadamuMnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
-
-
Katika nchi nyingi, serikali humpa mhudumu wa Mashahidi wa Yehova mamlaka ya kuandikisha ndoa. Ikiwa ndivyo ilivyo, yaelekea kwamba atafanya hivyo katika Jumba la Ufalme ambapo hotuba ya arusi itatolewa. Jumba la Ufalme ni mahali pa ibada ya kweli na panafaa kwa ajili ya hotuba inayohusu mpango huo ambao ulianzishwa na Yehova Mungu.
-
-
Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na WanadamuMnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
-
-
Wale wanaotaka kufunga ndoa ya kiserikali na baada ya hapo wawe na hotuba ya arusi kwenye Jumba la Ufalme, wanapaswa kuomba ruhusa ya wazee wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Mbali na kuhakikisha kwamba watu hao wana sifa nzuri, waangalizi hao watahakikisha kwamba arusi haivurugi saa za mikutano ya kawaida na mipango mingine kwenye jumba. (1 Wakorintho 14:33, 40) Pia, watachunguza matayarisho yoyote ambayo huenda wenzi hao wakaomba yafanywe kwenye jumba na kuamua ikiwa tangazo litatolewa kuhusu matumizi ya jumba.
-