-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndugu mmoja aliyejifunza Kihispania anasema hivi: “Tamaa yetu imetimizwa. Kwa miaka mingi mimi na mke wangu tulitamani kuwa wamishonari, lakini tulikuwa na watoto wawili. Sasa watoto wetu ni watu wazima nami nimestaafu. Kwa hiyo, miezi mitatu iliyopita, mimi na mke wangu tulijiunga na kutaniko la Kihispania, na tayari tumepewa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Pia, tuna marudio mengi na huenda tukaweza kuripoti mafunzo matano ya Biblia. Sisi tuna umri wa miaka 67 na 64, na tumetambua kwamba hakuna aliye mzee sana asiweze kujifunza lugha ya kigeni.”
-
-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Paula aliye na miaka 82 alianza kujifunza lugha ya Vietnam naye husafiri kilomita 150 hivi ili ahudhurie mikutano. Anasema hivi: “Mimi sina kipawa cha kujifunza lugha, lakini ninamshukuru Yehova kwa kunipa shangwe kubwa sana.” Paula alijifunza na familia moja kutoka Vietnam. Mume ndiye aliyependezwa na kweli kwanza kisha mke wake. Sasa wote wawili wamebatizwa.
Baada ya kubatizwa, mume huyo na mke wake pamoja na binti yao, walifanikiwa kutimiza tamaa yao ya kumtumikia Yehova nchini kwao. Walijenga nyumba iliyo na nafasi ya kutosha ya kufanyia mikutano ya kutaniko. Mume ni mzee wa kutaniko na painia-msaidizi. Mke wake ni painia wa kawaida. Paula alifurahi sana alipopokea barua kutoka kwa familia hiyo iliyoeleza kwamba baba alimbatiza binti yake. Binti huyo alimwandikia Paula hivi: “‘Nyanya’ Mpendwa. Ninatamani kukuona. Ninakufikiria mara nyingi. Wewe ni nyanya yangu wa kiroho milele. Ninakupenda.” Wazia jinsi jambo hilo lilivyomtia moyo dada yetu mpendwa aliyejifunza lugha ngumu akiwa mzee!
-