-
Fahari Iliyosahaulika ya Milki ya ByzantiumAmkeni!—2001 | Oktoba 8
-
-
Matokeo Yenye Kudumu
Amini usiamini, serikali ya Byzantium, sheria, mafundisho yake ya kidini, na sherehe zake za kifahari zingali zinaathiri mabilioni ya watu leo. Kwa mfano, kanuni mashuhuri za kisheria za Justinian zilizoitwa Corpus Juris Civilis (Mkusanyo wa Sheria za Kiraia) zilikuja kuwa msingi wa sheria za Roma katika bara la Ulaya leo. Mfumo wa Sheria wa Napoléon ulisambaza sheria za Byzantium huko Amerika Kusini na katika nchi nyingine, ambako zingali zinatumika.
-
-
Fahari Iliyosahaulika ya Milki ya ByzantiumAmkeni!—2001 | Oktoba 8
-
-
Sheria na Utaratibu
Sera nyingi za kiserikali zinazovutia za Milki ya Byzantium zingalipo leo. Kwa mfano, watu maskini waliajiriwa madukani na katika makampuni ya serikali ya kuoka mikate. “Uzembe husababisha uhalifu,” ndivyo alivyoamini Mfalme Leo wa Tatu (karibu 675-741 W.K.). Mabaa yalifungwa saa 2 usiku kwa sababu ilidhaniwa kwamba ulevi ulitokeza vurugu na uchochezi. Gazeti la National Geographic Magazine linasema kwamba “mtu aliyehusika na ngono ya maharimu, uuaji, kutengeneza au kuuza kisiri mavazi ya zambarau (yaliyotumiwa na wafalme peke yao) au kuwafundisha maadui kutengeneza meli angeweza kukatwa kichwa, kutundikwa mtini au kuzamishwa majini akiwa katika gunia lenye nguruwe, jogoo, nyoka wa kipiri, na nyani. Mwuza-mboga aliyewaibia wateja alikatwa mkono. Wale walioteketeza mali ya wengine kimakusudi walichomwa moto.”
Inapendeza kwamba Milki ya Byzantium iliandaa huduma za jamii kuanzia utotoni hadi uzeeni kama ilivyo katika nchi zinazoandaa huduma za jamii leo. Wafalme na raia matajiri walijitoa mhanga kuchanga pesa za kudumisha hospitali, makao ya kuwatunza maskini na mayatima. Kulikuwa na makao ya wanawake walioacha ukahaba—baadhi yao wakaja kuwa “watakatifu.” Hata kulikuwa na makao ya kuwasaidia wanawake wenye shida wa jamii ya kifalme.
-