Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jifunze Kutokana na ‘Ile Picha ya Kweli’
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Januari 15
    • Jifunze Kutokana na ‘Ile Picha ya Kweli’

      “[Una] picha ya ujuzi na ya ile kweli katika Sheria.” ​—ROM. 2:20.

  • Jifunze Kutokana na ‘Ile Picha ya Kweli’
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Januari 15
    • 1. Kwa nini tunapaswa kujitahidi kuelewa umuhimu wa Sheria ya Musa?

      KAMA hatungekuwa na maandishi ya mtume Paulo yaliyoongozwa na roho takatifu, ingekuwa vigumu kwetu kuelewa maana ya mambo mengi katika Sheria ya Musa. Kwa mfano, katika barua yake kwa Waebrania, anaeleza jinsi ambavyo Yesu akiwa ‘kuhani mkuu mwaminifu’ angeweza kutoa “dhabihu ya upatanisho” mara moja kwa wakati wote na hivyo kuwawezesha wale ambao wanaonyesha imani katika dhabihu hiyo kupata “ukombozi wa milele.” (Ebr. 2:17; 9:11, 12) Paulo alieleza kwamba maskani yalikuwa tu “kivuli cha vitu vya mbinguni” na kwamba Yesu alikuwa Mpatanishi wa “agano bora” kuliko lile ambalo Musa alikuwa mpatanishi wake. (Ebr. 7:22; 8:1-5) Katika siku za Paulo, maelezo kama hayo kuhusu Sheria yalikuwa muhimu sana kwa Wakristo, na bado ni muhimu leo. Yanatusaidia kuelewa kikamili zaidi thamani ya maandalizi ambayo Mungu ametupatia.

      2. Wakristo Wayahudi walikuwa na pendeleo gani ambalo watu wa Mataifa hawakuwa nalo?

      2 Paulo alipowaandikia Wakristo huko Roma, alielekeza baadhi ya maelezo yake kwa washiriki wa kutaniko ambao walikuwa wa asili ya Kiyahudi na ambao walikuwa wamefundishwa Sheria ya Musa. Alikiri kwamba kwa sababu ya kuifahamu Sheria hiyo ya Mungu, watu hao walikuwa na pendeleo la kuwa na “picha ya ujuzi na ya ile kweli” kumhusu Yehova na kanuni zake za uadilifu. Kuelewa ‘picha hiyo ya kweli’ na kuiheshimu kutoka moyoni kuliwawezesha Wayahudi Wakristo, kama Wayahudi waaminifu waliowatangulia, kuweza kuongoza, kufundisha, na kuwaelimisha wale ambao hawakujua Sheria ambayo Yehova alikuwa amewapa watu wake.​—Soma Waroma 2:17-20.

      MAMBO YALIYOKUWA KIVULI CHA DHABIHU YA YESU

      3. Tunafaidika jinsi gani kwa kujifunza kuhusu dhabihu ambazo Wayahudi walitoa zamani?

      3 Picha ya ile kweli ambayo Paulo alirejelea bado ni muhimu kwetu ili tuelewe makusudi ya Yehova. Kanuni zinazotokana na Sheria ya Musa hazijapoteza umuhimu au thamani yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki