Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Pumziko la Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
    • Wakristo Wengine Hawakuingia Katika Pumziko la Mungu

      13, 14. Kulikuwa na uhusiano gani kati ya kufuata Sheria ya Musa na kuingia katika pumziko la Mungu (a) katika siku za Musa? (b) katika karne ya kwanza?

      13 Paulo aliwaandikia Wakristo Waebrania kwa sababu wengine wao walikuwa wakitenda kinyume na kusudi la Mungu. (Soma Waebrania 4:1.) Katika maana gani? Jambo la kushangaza ni kwamba bado walikuwa wakifuata Sheria ya Musa. Ni kweli kwamba kwa miaka 1,500 hivi, Mwisraeli yeyote ambaye alitaka kuishi kulingana na kusudi la Mungu alipaswa kufuata Sheria ya Musa. Hata hivyo, baada ya kifo cha Yesu, Sheria hiyo iliondolewa. Wakristo fulani walikosa kutambua jambo hilo, na walisisitiza kuendelea kufuata mambo fulani katika Sheria ya Musa.b

      14 Paulo aliwaeleza Wakristo waliokuwa na mwelekeo wa kufuata Sheria ya Musa kwamba ukuhani mkuu wa Yesu, agano jipya, na hekalu la kiroho, vyote hivyo vilikuwa bora zaidi kuliko agano la Mungu pamoja na Waisraeli. (Ebr. 7:26-28; 8:7-10; 9:11, 12) Kwa hiyo, inaelekea kwamba akifikiria wale walioshika Sabato ya kila juma chini ya Sheria, Paulo aliandika kuhusu pendeleo la kuingia katika siku ya pumziko la Yehova: “Bado limebaki pumziko la sabato kwa ajili ya watu wa Mungu. Kwa maana mtu ambaye ameingia katika pumziko la Mungu yeye mwenyewe pia amepumzika kutokana na kazi zake mwenyewe, kama Mungu alivyopumzika kutokana na kazi zake mwenyewe.” (Ebr. 4:8-10) Wakristo hao Waebrania walipaswa kuacha kufikiri kwamba wangeweza kukubaliwa na Yehova kwa kufuata matendo yaliyotegemea Sheria ya Musa. Tangu Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K., ni wale tu ambao wanamwamini Yesu Kristo ndio wanaopata kwa rehema kibali cha Mungu.

      15. Kwa nini kutii ni jambo la maana ikiwa tunataka kuingia katika pumziko la Mungu?

      15 Ni nini kilichowazuia Waisraeli wa siku za Musa kuingia katika ile Nchi ya Ahadi? Ni kutotii. Ni nini kilichokuwa kikiwazuia Wakristo fulani katika siku za Paulo kuingia katika pumziko la Mungu? Ni jambo lilelile, kutotii. Walishindwa kutambua kwamba Sheria ilitimiza kusudi lake na kwamba Yehova alikuwa akiwaongoza watu wake katika njia tofauti.

  • Pumziko la Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
    • b Hatujui ikiwa Mkristo yeyote Myahudi alitoa dhabihu Siku ya Upatanisho baada ya siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. Bila shaka, Mkristo ambaye angefanya hivyo angeonyesha kwamba haheshimu dhabihu ya Yesu. Lakini, Wakristo fulani Wayahudi walishikilia mapokeo mengine yaliyohusiana na Sheria.—Gal. 4:9-11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki