-
Je, Mungu Alikubali Biashara ya Watumwa?Amkeni!—2001 | Septemba 8
-
-
Sheria ya Mungu ilisema kwamba adhabu ya kumteka na kumuuza mtu ilikuwa kifo. Isitoshe, Yehova alitoa mwongozo ili kuwalinda watumwa. Kwa mfano, mtumwa aliyelemazwa na bwana wake angeachiliwa huru. Ikiwa mtumwa angekufa kwa sababu alipigwa na bwana wake, huyo bwana aliweza kuadhibiwa hukumu ya kifo. Wanawake watekwa walifanywa kuwa watumwa, au waliolewa na mabwana wao. Lakini haikuruhusiwa watumiwe vibaya ili kutosheleza tamaa ya ngono. Bila shaka, Sheria iliwaongoza Waisraeli wanyoofu wawatendee watumwa kwa heshima na fadhili, kana kwamba walikuwa wafanyakazi walioajiriwa.—Kutoka 20:10; 21:12, 16, 26, 27; Mambo ya Walawi 22:10, 11; Kumbukumbu la Torati 21:10-14.
Baadhi ya Wayahudi walikubali kwa hiari kuwa watumwa kwa Wayahudi wenzao ili walipe deni. Desturi hiyo ililinda watu wasione njaa na kuwasaidia watoke katika hali ya umaskini. Isitoshe, watumwa waliotaka uhuru walipaswa kuachiliwa katika pindi fulani kulingana na kalenda ya Wayahudi.a (Kutoka 21:2; Mambo ya Walawi 25:10; Kumbukumbu la Torati 15:12) Msomi Myahudi, Moses Mielziner, alisema hivi kuhusu sheria hizo zilizohusu watumwa: “Mtumwa alitendewa sikuzote kama mwanadamu, alionwa kuwa mtu mwenye haki fulani za asili ambazo hata bwana wake hangeweza kuziondoa bila kuadhibiwa.” Jambo hilo ni tofauti jinsi gani na mifumo mbalimbali ya utumwa yenye kukandamiza ambayo imekuwapo tangu zamani!
-
-
Je, Mungu Alikubali Biashara ya Watumwa?Amkeni!—2001 | Septemba 8
-
-
a Mpango wa Sheria ulioruhusu baadhi ya watumwa kubaki kwa bwana wao unaonyesha wazi kwamba watumwa hawakukandamizwa huko Israeli.
-