-
Wale Wafalme Wawili WabadilikaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
11. ‘Mkuu wa maagano alivunjwaje’?
11 “Mkuu wa maagano” ambayo Yehova Mungu alikuwa amefanya na Abrahamu ili kubariki familia zote duniani ‘alivunjwa’ pia. Yesu Kristo alikuwa Mbegu ya Abrahamu iliyoahidiwa katika agano hilo. (Mwanzo 22:18; Wagalatia 3:16) Nisani 14, 33 W.K., Yesu alisimama mbele ya Pontio Pilato katika jumba la gavana wa Roma huko Yerusalemu. Makuhani Wayahudi walikuwa wamemshtaki Yesu kuwa mhaini dhidi ya maliki. Lakini Yesu alimwambia Pilato hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. . . . Ufalme wangu si kutoka chanzo hiki.” Kwa kuwa Wayahudi hawakutaka gavana Mroma amwachilie Yesu asiye na hatia, walipaaza sauti, wakisema: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. Kila mtu anayejifanya mwenyewe mfalme asema vibaya dhidi ya Kaisari.” Baada ya kuagiza Yesu auawe, walisema hivi: “Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.” Kulingana na sheria ya ‘uhaini,’ ambayo Tiberio alikuwa ameipanua itie ndani kumtukana Kaisari kwa njia yoyote, Pilato akamtoa Yesu ‘avunjwe,’ au atundikwe kwenye mti wa mateso.—Yohana 18:36; 19:12-16; Marko 15:14-20.
-
-
Wale Wafalme Wawili WabadilikaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 237]
Kama ilivyotabiriwa, Yesu ‘alivunjwa’ kwenye kifo
-